the standard: enock maregesi

28
ENOCK MAREGESI MSHINDI WA PILI WA TUZO YA KISWAHILI YA MABATI- CORNELL YA FASIHI YA KIAFRIKA 2015 MWANDISHI WA KOLONIA SANTITA MAHOJIANO

Upload: enock-maregesi

Post on 12-Apr-2017

136 views

Category:

Career


5 download

TRANSCRIPT

Page 1: The Standard: Enock Maregesi

ENOCK MAREGESI MSHINDI WA PILI WA TUZO YA

KISWAHILI YA MABATI-CORNELL YA FASIHI YA KIAFRIKA 2015

MWANDISHI WA KOLONIA SANTITA

MAHOJIANO

Page 2: The Standard: Enock Maregesi

Ulianzaje kuandika?Nilianza kuandika kwa kujijengea

utamaduni. Utamaduni wa kuandika. Popote pale nilipoona kitu ambacho nilidhani kilifaa kuandikwa mahali,

nilikiandika bila kusita au kuchelewa kwa namna yoyote ile. Nilianza kwa kuandika

insha na kitu chochote kile kama vile barua kwa rafiki yangu wa kike wa kipindi kile, marafiki na kwa familia

yangu pia. Hicho ndicho kilichoniingiza katika biashara hii ya uandishi wa vitabu.

Page 3: The Standard: Enock Maregesi

Hadithi yangu ya kwanza kabisa kuandika iliitwa Magaidi wa Namba

One – Namba One likiwa jina la sehemu – hadithi fupi ya kijasusi

iliyohusu genge la kijambazi, lililokuwa na maskani yake mjini

Dodoma. Magaidi wa Namba One ilikuwa na urefu wa kurasa 15.

Niliiandika nikiwa na umri wa miaka 15 au 16 hivi, katika Shule ya

Sekondari ya Bihawana ya mkoani Dodoma.

Page 4: The Standard: Enock Maregesi

Hadithi hii ilihusu kikundi cha kigaidi kilichoitwa Namba One.

Kikundi hiki kilikuwa na makao yake makuu nje ya Dodoma, katika pori

la Namba One, kama unaelekea Iringa. Lilifanya shughuli zake ndani na nje ya Dodoma hadi siku moja mkubwa wake alipokamatwa; na

baadaye kupata adhabu ya kifungo cha maisha jela kilichoambatana na

kazi ngumu, katika gereza lenye ulinzi mkali la mkoani Shinyanga.

Page 5: The Standard: Enock Maregesi

Baada ya hapo, viongozi wote wakubwa wa kikundi hicho walikamatwa na kukabidhiwa vifungo kulingana na

makosa waliyoyafanya.

Page 6: The Standard: Enock Maregesi

Nini kilikusukuma kuwa mwandishi wa vitabu?Nilihamasishwa na watu wengi na

matukio mengi kuwa mwandishi wa vitabu: Ngugi wa Thiong’o, Ben Mtobwa,

Euphrase Kezilahabi, Penina Mlama, Shafi Adam Shafi, sinema za mapigano kama vile The Big Boss ya Bruce Lee na

Missing in Action ya Chuck Norris, hadithi kutoka kwa wazee na watu wengine wakubwa, na kadhalika.

Page 7: The Standard: Enock Maregesi

Hata hivyo, hamasa kubwa zaidi kushinda zote ilitoka kwa Shaaban

Robert – mzalendo wa kweli wa Tanzania na kinara wa lugha ya

Kiswahili – ambaye vitabu vyake vilinipa nguvu (na tumaini) kuandika riwaya yangu ya kwanza ya Kolonia Santita,

ambayo awali iliitwa Salina Cruz.

Page 8: The Standard: Enock Maregesi

Salina Cruz ni mji wa mwambao wa kusini-magharibi mwa Meksiko, katika jimbo la Oaxaca, kateli ya Kolonia Santita ilipoanzishwa.

Page 9: The Standard: Enock Maregesi

Nilipomaliza masomo yangu ya sekondari mwaka 1992 nilianza kuandika

Kolonia Santita. Kipindi hicho nilikuwa nikisubiri majibu ya mtihani wa taifa wa

kidato cha nne. Siku moja (nilipoanza rasmi kuandika, miaka 23 iliyopita) niliijiwa ghafla na ndoto ya mchana

nikiwa katika bustani ya nyumbani kwetu Kijitonyama, Dar es Salaam. Vita kubwa ya mawazo iliendelea kichwani mwangu kwa muda mrefu bila kukoma, kuhusiana

na dhana fulani ambayo nilikuwa bado sijaielewa sawasawa.

Page 10: The Standard: Enock Maregesi

Ndoto hiyo ikawa msingi wa taaluma yangu ya uandishi wa vitabu na msingi

wa utetezi wangu wa lugha ya Kiswahili. Ikanikumbusha uzuri wa kipaji na uwezo

wa talanta nilivyopewa na Mungu na jinsi gani nivitumie, na ikanikumbusha jinsi gani nilivyoweza kuwa na uwezo mkubwa kuburudisha na kuelimisha

watu kwa nguvu ya neno.

Page 11: The Standard: Enock Maregesi

Ujasiri wa kujaribu au jeuri ya kufanya kitu na kujiamini na tumaini, ulinipa

msingi wa kufikiri vyema na kuandika kwenye karatasi dhana mbalimbali na

mawazo kadha wa kadha kutoka katika dunia niliyoigundua. Nilikuwa na

uwezo, nilidhani, wa kuwa mojawapo kati ya watoa burudani bora na

waandishi bora wa vitabu Tanzania.

Page 12: The Standard: Enock Maregesi

Bustanini nilitamani sana kuchapisha kitabu changu nje ya Tanzania na Afrika,

mathalani Uingereza au Marekani, ambapo uchapishaji wa vitabu ni wa

kimataifa na wa daraja la kwanza. Kichwa changu kilifikiria riwaya ambayo

ingesimulia mandhari ya miji zaidi ya minne ulimwenguni kote, ambayo baadaye ingekuwa ya kwanza kwa

mauzo hapa Afrika ya Mashariki na Kati.

Page 13: The Standard: Enock Maregesi

Nilitamani hadithi yangu ichapishwe nje kupata ubora wa kitabu, na ubora wa huduma za

uchapishaji wa vitabu.

Page 14: The Standard: Enock Maregesi

Hadithi ya Kolonia Santita niliiandika kwa miezi mitatu mfululizo hadi

nilipokamilisha rasimu ya kwanza kabisa ya muswada wenyewe. (Nilikuwa na

umri wa miaka 20 nilipofanya hivyo). Kila nilipodhani muswada umekamilika ili

niupeleke kwa wachapishaji, niligundua bado ulihitaji marekebisho.

Page 15: The Standard: Enock Maregesi

Mwaka 1999 hata hivyo nilidhani umekamilika, na niliupeleka Popular

Publications Ltd (PPL) kwa ajili ya mkataba wa uchapishaji wa vitabu.

Lakini PPL waliukataa muswada huo. Waliukataa kutokana na ripoti iliyokuwa na mchango mkubwa kwangu ya Hayati Saifu D. Kiango, ambaye kipindi hicho

alikuwa mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Tanzania (BAKITA).

Page 16: The Standard: Enock Maregesi

Kiango alishauri katika ripoti yake masahihisho mengi katika muswada

wangu, ambayo yote nilikubaliana nayo, kabla sijaurudisha kwa wachapishaji

lakini nikashindwa kufanya hivyo. Nilishindwa kuurudisha kwa

wachapishaji.

Page 17: The Standard: Enock Maregesi

PPL walipoteza baadhi ya sura za muswada wa Kolonia Santita (sura ya 7,

8 na 9) na sikufurahishwa na majibu niliyopewa na Ndg. Mhando (nimesahau

majina yake mengine) kwamba yeye/ofisi hawakujua hizo sura

zilipokwenda na kwamba yeye/ofisi walipeleka muswada BAKITA ukiwa

umekamilika kabisa. Mhando alikuwa mhariri mwandamizi wa PPL.

Page 18: The Standard: Enock Maregesi

Kwa sababu hiyo niliuondoa muswada wangu PPL na kuweka nadhiri ya kusahihisha kila kosa

aliloliona Kiango na kushauri nilisahihishe, na nadhiri ya

kuchapisha kitabu hicho mimi mwenyewe nje ya Afrika kama

ningepata nafasi.

Page 19: The Standard: Enock Maregesi

Mnamo mwaka 1992 hadi 1999 nilipata nafasi ya kuandika miswada mingine mitano. Miwili kati ya miswada hiyo ilikuwa imekamilika. Mitatu ilikuwa

bado. Mitatu ni ya kipelelezi. Miwili ni ya kimapenzi. Septemba 2004 nilihamia

London nchini Uingereza. Huko nilipata nafasi nzuri zaidi ya kufanya utafiti

yakinifu, wa miswada yangu yote sita, kwa kiwango nilichokitaka.

Page 20: The Standard: Enock Maregesi

Katika maisha yangu yote nilitamani sana kuwa mtetezi wa lugha na

utamaduni wa Kiswahili. Nadhani tunahitaji wote kuwa watetezi wa

lugha hii na lugha zingine za Kiafrika kwani hizi ndiyo utambulisho wa

bara letu.

Page 21: The Standard: Enock Maregesi

Kutokana na hamu hiyo, mwaka 1995 niliweka nadhiri ya kupigania

lugha ya Kiswahili maisha yangu yote yaliyobakia. Lakini nilijua hilo

lisingewezekana bila kwanza kufanikisha elimu.

Page 22: The Standard: Enock Maregesi

Mwaka 2010 nilijiunga na chuo cha ubunifu wa kifasihi cha Manchester (The

Writers Bureau) nchini Uingereza, kwa lengo la kutimiza ndoto zangu na kupata

taaluma ya uandishi wa vitabu. The Writers Bureau walinipa moyo wa

kujiamini. Nilikuwa nikiishi shimoni, gizani. Hata hivyo, baada ya kupitia

vitabu vichache vya kozi niliona nuru upande wa pili wa tobwe.

Page 23: The Standard: Enock Maregesi

Nilijua, kutokea kipindi hicho kwamba, endapo ningesoma kwa bidii ningepata uzoefu na utaalamu na mwongozo hasa

niliyoutaka. Nilitamani kuwa mwandishi bora wa vitabu na

nilitamani kuwaelimisha watu na kuwaburudisha pia. Nilitamani kuwa

mojawapo ya waandishi bora wa vitabu na wauzaji bora wa vitabu nchini

Tanzania, na nje ya hapo.

Page 24: The Standard: Enock Maregesi

Ulishindaje?

Habari ya Tuzo ya Kiswahili ya Mabati-Cornell ya Fasihi ya Kiafrika niliipata kwa mshangao

mkubwa. Kwanza, niliipata kutoka kwa Mkurugenzi wa CDEA (Culture for Development

East Africa) Ayeta Anne Wangusa mwezi wa tatu 2015 ofisini kwake Dar es Salaam. Kisha

nikaandaa muswada wangu vizuri na kuutuma kupitia tovuti ya tuzo kwa waamuzi wa tuzo,

kwa ajili ya mashindano.

Page 25: The Standard: Enock Maregesi

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Tuzo ya Kiswahili ya Mabati-Cornell ya

Fasihi ya Kiafrika Profesa Abdillatif Abdalla aliponipigia simu kunijulisha kwamba muswada wangu ulishinda

nafasi ya pili nilifurahi sana. Nilifurahi sana kiasi kwamba nilijifungia chumbani kwangu hotelini na kucheza muziki kwa masaa matatu mfululizo, na nimekuwa

na furaha kuanzia kipindi hicho na kuendelea.

Page 26: The Standard: Enock Maregesi

Sababu kubwa ya muswada wangu kushinda ni kujitahidi kwa kadiri ya uwezo wangu WOTE. Ni uvumilivu,

uchapakazi na nidhamu.

Page 27: The Standard: Enock Maregesi

Nini ushauri wako kwa waandishi chipukizi?

Ushauri wangu pekee ninaoweza kutoa kwa waandishi chipukizi ni elimu! Hutaweza kufikia malengo

yako kikamilifu bila msaada wa wataalamu – Hata kama una kipaji

au ujuzi kiasi gani.

Page 28: The Standard: Enock Maregesi

Ukiwa na kipaji nenda shule kurekebisha kipaji chako, ukiwa na ujuzi nenda shule

kurekebisha ujuzi wako.