wildaftanzania.org · web viewhotuba ya mheshimiwa kassim m. majaliwa (mb), waziri mkuu wa jamhuri...

28
HOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA KATIKA VIWANJA VYA JAMHURI DODOMA, TAREHE 25 NOVEMBA 2018 SALAMU Mhe. Ummy Mwalimu (Mb), Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto; Mhe. Binilith Mahenge, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma; Dkt. John Jingu, Katibu Mkuu anayeshughulikia Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto; Bw. Alvaro Rodriguez, Mratibu Mkaazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania; Ndugu Hodan Addou, Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Wanawake (UN-Women); Ndugu Ann Theresa Ndong Jatta, Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO); 1

Upload: others

Post on 26-Jan-2020

0 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

HOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA KATIKA VIWANJA VYA JAMHURI DODOMA, TAREHE 25 NOVEMBA 2018

SALAMU

Mhe. Ummy Mwalimu (Mb), Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto;

Mhe. Binilith Mahenge, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma;

Dkt. John Jingu, Katibu Mkuu anayeshughulikia Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto;

Bw. Alvaro Rodriguez, Mratibu Mkaazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania;

Ndugu Hodan Addou, Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Wanawake (UN-Women);

Ndugu Ann Theresa Ndong Jatta, Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO);

Mhe. Paul Sherlock, Balozi wa Ireland nchini;

Mhe. Sarah Cooke, Balozi wa Uingereza nchini;

Viongozi na Watendaji Wakuu wa Serikali mliopo hapa;1

Page 2: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

Ndugu Anna Meela Kulaya, Mratibu wa Kitaifa wa Shirika la Wanawake Katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WiLDAF);

Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la WiLDAF;

Ndugu Kees Groenendijk, Mkurugenzi wa Taasisi ya Huduma za Sheria (LSF);

Ndugu Francis Odokorach, Mkurugenzi wa Shirika la Oxfam;

Wawakilishi kutoka Balozi na Mashirika ya Kimataifa nchini;

ACP Mary Nzuki, Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto kutoka Jeshi la Polisi Tanzania;

Wawakilishi wa Taasisi za Utafiti na Elimu ya Juu mliopo;

Wawakilishi wa Wafanyakazi na Watendaji kutoka Serikalini;

Wawakilishi kutoka Taasisi na Asasi za Kiraia na Binafsi mliopo;

Waandishi wa Habari;

Walimu na Wanafunzi wa Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo mbalimbali mliopo hapa;

Wageni Waalikwa;

Mabibi na Mabwana.2

Page 3: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

Habari za Mchana.

UTANGULIZI

Ndugu Wananchi;

Awali ya yote, namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa

rehema kwa kutujaalia afya na uzima na kutuwezesha

kuhudhuria uzinduzi huu wa Kampeni ya Siku 16 za Kupinga

Ukatili wa Kijinsia 2018.

Pili, napenda kutumia fursa hii kutoa shukrani zangu za dhati

kwa heshima kubwa ambayo mmenipatia kwa kunialika kuwa

Mgeni Rasmi kwenye Uzinduzi wa kampeni hii.

Tatu, kipekee nitoe pongezi za dhati kwa Uongozi wa Mkoa

wa Dodoma kwa kuwa mwenyeji wa uzinduzi wa Kampeni hii

Kitaifa. Hongereni sana kwa maandalizi mazuri!

Nne, nitakuwa mchoyo wa fadhila nisipowafikishia salamu

zenu kutoka kwa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph

3

Page 4: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na

Makamu wa Rais, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ambao

kwa pamoja wanawatakia kampeni salama, ya amani na

yenye mafanikio yaliyokusudiwa.

UKATILI WA KIJINSIA

Ndugu Wananchi,

Ukatili wa Kijinsia ni kutenda vitendo viovu, vinavyodhalilisha,

vinavyotesa, vinavyonyanyasa, vinavyokandamiza, visivyojali

haki za kuishi kwa binadamu anaweza kuwa wa kiume au

kike.

Ukatili wa kijinsia huja katika taswira nyingi. Aidha, kwa

uchache tunapozungumzia ukatili wa kijinsia tunamaanisha

vitendo kama vile, vipigo, ubakaji, ukeketaji, ulawiti, matusi,

lugha na vitendo vya udhalilishaji pamoja na kunyimwa fursa

za kushiriki katika shughuli za kiuchumi.

4

Page 5: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

Hivyo, ukatili wa kijinsia ni unyanyasaji wowote unaofanywa

na mtu dhidi ya mtu mwingine bila kujali umri, maumbile,

kabila, rangi, dini au mtazamo wa kisiasa.

Unyanyasaji huu unahusisha mambo mengi yakiwemo;

kumpiga mwanamke au mwanamme, kumnyima mtoto elimu,

kumlawiti mtoto wa kike au kiume, kumbagua mtu katika

mahitaji ya msingi au kuwanyima urithi warithi wanaohusika.

Mambo mengine yenye kuhusisha ukatili wa kijinsia ni mimba

na ndoa za utotoni na vitendo vingine vinavyofanana na

hivyo ambavyo vinafanyika mahali pa kazi, shuleni, mitaani,

majumbani na mitandaoni ambavyo kwa sehemu kubwa

huwaathiri zaidi wanawake na watoto.

Tafiti zinaonesha kuwa ukatili wa kijinsia ni tatizo kubwa

ambalo linaikabili Dunia na hutokea katika Nchi mbalimbali.

Kwa mfano, takwimu zilizotolewa na Shirika la Afya Duniani

mwaka 2013 zinaonesha kuwa takriban asilimia 35 ya

wanawake Duniani wamefanyiwa ukatili wa kijinsia wa

kupigwa au kubakwa katika kipindi cha maisha yao. 5

Page 6: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

Aidha, taarifa kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la

Kuwahudumia Watoto (UNICEF) za mwaka 2017 zinaonesha

kuwa wanawake na wasichana wapatao milioni 750 Duniani

waliolewa wakiwa chini ya miaka 18. Halikadhalika, taarifa

hiyo inakadiria kuwa wasichana milioni 120 (yaani mmoja kati

ya wasichana 10) Duniani wamekumbana na vitendo vya

kulazimishwa kufanya ngono bila ridhaa yao.

Kwa upande mwingine, wanawake na wasichana milioni 200

walifanyiwa vitendo vya ukeketaji katika Nchi 30 Duniani.

Vilevile, wasichana na wavulana wapatao milioni 246

wamefanyiwa ukatili wa kijinsia wakiwa shuleni.

Ndugu Wananchi,

Kama zilivyo Nchi nyingine Duniani, Tanzania ni miongoni mwa

Nchi ambazo zinakabiliwa na tatizo la ukatili wa kijinsia.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Ofisi ya Taifa

ya Takwimu mwaka 2015/2016 kupitia Taarifa ya Idadi ya

Watu na Afya inakadiriwa kuwa asilimia 40 ya wanawake wenye

6

Page 7: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

umri kati ya miaka 15 - 49 wamefanyiwa ukatili wa kupigwa au

kingono katika kipindi cha maisha yao.

Kadhalika, asilimia 22 ya wanawake wenye umri kati ya miaka 15

- 49 walifanyiwa vitendo vya kingono kinyume na matakwa yao.

Kwa ujumla taarifa hiyo, inaonesha hakuna tofauti kubwa ya

mabadiliko katika jamii zetu kuhusu mitazamo na matendo ya

jamii zetu kuhusiana na Ukatili wa Kijinsia. Ni dhahiri kuwa bado

tuna kazi kubwa ya kuhamasisha jamii zetu kubadili fikra na

mitazamo inayochochea vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia.

JUHUDI ZA SERIKALI KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA

Ndugu Wananchi,

Nimefahamishwa kuwa Kaulimbiu ya Kampeni ya Siku 16 za

Kupinga Ukatili wa Kijinsia kwa mwaka huu ni “FUNGUKA!

USALAMA WAKE: WAJIBU WANGU”. Kaulimbiu hii inatupa

jukumu sisi sote la kuhakikisha kuwa kila mtu katika nafasi yake

anapaza sauti na kuchukua hatua ya kuzuia na kutokomeza

7

Page 8: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

ukatili wa kijinsia hususan dhidi ya wanawake na watoto katika

maeneo mbalimbali ikiwemo katika nyumba tunazoishi, mahali pa

kazi, shuleni na mahali pengine katika jamii zetu.

Ndugu Wananchi,

Katika kukabiliana na ukatili wa kijinsia hapa nchini, Serikali ya

Awamu ya Tano chini ya uongozi mahiri wa Mheshimiwa

Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania, imechukua hatua mbalimbali za kuzuia

na kutokomeza ukatili.

Hatua hizo ni pamoja na kuandaa Mpango wa Taifa wa

Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (2017/2018 -

2021/2022) ambao utekelezaji wake unaendelea. Mpango huo,

unalenga kupunguza kiwango cha ukatili dhidi ya wanawake na

watoto katika jamii yetu kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2022.

Mpango huo, ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya

Wanawake na Jinsia (2000); Mkakati wa Taifa wa Maendeleo ya

Jinsia (2005); Sera ya Maendeleo ya Mtoto (2008); Sheria ya

8

Page 9: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

Makosa ya Kujamiiana – SOSPA (1998) ambayo imehuishwa

kwenye Sheria ya Kanuni za Adhabu Sura ya 16 kwa lengo la

kuhakikisha kuwa utu wa wanawake na watoto unalindwa pamoja

na Sheria ya Mtoto (2009) inayolinda haki za mtoto.

Aidha, utekelezaji wa Mpango huo utachangia katika utekelezaji

wa mipango na Mikataba ya Kikanda na Kimataifa kuhusu usawa

wa kijinsia, uwezeshaji wanawake na wasichana pamoja na haki

na ustawi wa mtoto.

Ndugu Wananchi,

Mpango huo jumuishi, unatekelezwa na wadau mbalimbali nchini

ikiwemo Wizara, Idara, na Wakala mbalimbali za Serikali,

Sekretarieti za Mikoa, Serikali za Mitaa, Asasi za Kiraia, Sekta

Binafsi na wanajamii mmoja mmoja au katika vikundi. Serikali

inaamini kuwa mpango huo utasaidia sana wadau mbalimbali

kuchukua hatua stahiki zitakazopunguza au kuondoa kabisa

vitendo vya Ukatili wa Kijinsia hapa nchini.

9

Page 10: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

Aidha, natoa wito kwa kila mwananchi na watekelezaji wengine

wa Mpango huo kutimiza wajibu wenu ipasavyo katika

kuhakikisha ukatili wa kijinsia unatokomezwa hapa nchini. Ni

imani yangu kuwa kila mmoja akitimiza wajibu wake ipasavyo,

ukatili wa kijinsia utabaki kuwa historia hapa nchini.

Ndugu Wananchi,

Juhudi nyingine ambazo zimefanywa na Serikali kwa kushirikiana

na wadau mbalimbali ni kama zifuatazo:

Mosi: Kuanzisha Madawati ya Jinsia na Watoto katika Vituo vya

Polisi ambapo hadi sasa madawati 417 yameanzishwa na

yanafanya kazi kwa lengo la kuwezesha huduma stahiki

katika vituo vya Polisi na kutenda haki. Huduma hii

imewezesha wahanga 58,059 kuripoti aina mbalimbali za

matukio ya ukatili wa kijinsia kwa watu wazima na watoto,

ikiwemo ubakaji, ulawiti, vipigo na ukeketaji. Madawati

haya yameongeza mwamko wa wananchi katika kujiamini

10

Page 11: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

na kutoa taarifa za ukatili unapotokea kwenye maeneo

yao.

Kwa kuzingatia ukweli kuwa watu wenye ulemavu wana

mahitaji maalumu na kwamba ni wahanga wa ukatili wa

kijinsia naelekeza Jeshi la Polisi kuboresha Dawati hili ili

liweze kushughulikia kikamilifu masuala ya ukatili wa

kijinsia dhidi ya watu wenye ulemavu. Hivyo, kuanzia sasa

Dawati hilo liitwe Dawati la Polisi la Jinsia, Watoto na

Watu wenye Ulemavu.

Pili: Vituo vya Mkono kwa Mkono vya Kutoa huduma kwa

Wahanga wa Ukatili wa Kijinsia (One Stop Centres)

vimeanzishwa katika Mikoa sita ya Tanzania Bara. Mikoa

hiyo ni pamoja na Dar es Salaam, Pwani, Mwanza, Mbeya,

Iringa na Shinyanga. Vituo hivi vinawezesha utoaji wa

huduma rafiki na za haraka kwa waathirika wa vitendo vya

ukatili na vinahusisha wataalamu mbalimbali ikiwemo

Maafisa wa Jeshi la Polisi, Wataalamu wa Ustawi wa

Jamii, Wanasheria na Madaktari kwa ajili ya utoaji wa

11

Page 12: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

huduma za matibabu, unasihi, kipolisi na msaada wa

kisheria.

Tatu: Kuanzishwa kwa huduma ya simu bila malipo kwa watoto

wanaofanyiwa vitendo vya Ukatili na unyanyasaji (Child

Helpline) ili kutoa taarifa kwa haraka. Watoto ambao

hufanyiwa vitendo hivi huunganishwa na huduma

mbalimbali za kijamii kama Polisi, Hospitali, Ustawi wa

Jamii na Mahakama. Kwa kupitia huduma hii kwa mwaka

2017 jumla ya watoto 17,443 walipiga simu na

kuunganishwa na huduma stahiki mbalimbali.

Nne: Kupitia Serikali ya Awamu ya Tano, tumeanzisha na

kutekeleza Sera ya Elimumsingi Bila Malipo ili kusaidia

kuleta usawa wa fursa za kielimu kwa watoto wote wa kike

na wa kiume bila kujali uwezo wa kiuchumi wa familia.

Serikali ya Awamu ya Tano inatarajia kuwa utekelezaji wa

Sera hii siyo tu utapunguza mimba na ndoa za utotoni bali

pia utaondoa pengo la kijinsia katika elimu baina ya watoto

wetu wa kike na wa kiume.

12

Page 13: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

Tano: Sambamba na utoaji wa elimu pasipo malipo kwa ngazi

husika, Serikali imewezesha Marekebisho ya Sheria ya

Elimu na kulifanya kosa la kumpa mimba mwanafunzi;

kuoa mwanafunzi au kuolewa na mwanafunzi wa shule za

msingi na sekondari kuwa kosa la jinai na pale

inapothibitika adhabu yake ni kifungo cha miaka 30.

Sita: Serikali imewezesha kutungwa kwa Sheria ya Msaada wa

Kisheria ya mwaka 2017 kwa ajili ya kuwawezesha watu

wote wakiwemo wanawake na watoto kupata haki zao za

kisheria kupitia vyombo vya usimamizi wa Sheria

sambamba na kushughulikia makosa ya ukatili wa kijinsia.

Saba: Serikali imeifanyia marekebisho Sheria ya Fedha za

Mamlaka za Serikali za Mitaa mwaka 2018 kwa lengo la

kuufanya uchangiaji wa asilimia 10 wa pato la ndani la

Halmashauri kwa ajili ya wanawake (asilimia 4), vijana

(asilimia 4) na watu wenye ulemavu (asilimia 2). Aidha,

marekebisho hayo yameondoa riba kwenye mikopo

inayotokana na fedha hizo.

13

Page 14: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

Ndugu Wananchi,

Hatua zilizochukuliwa na Serikali ni nyingi na sitaweza kuzitaja

zote hapa. Lengo la juhudi hizi ni kuhakikisha kuwa wanawake,

wanaume, wasichana, wavulana na watu wenye ulemavu

wanakuwa na mazingira mazuri ya kujikwamua na kuondokana

na vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia.

Hata hivyo, juhudi hizi za Serikali hazitaweza kuzaa matunda

mazuri iwapo hazitaungwa mkono na wananchi wenyewe pamoja

na wadau mbalimbali. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kuna

changamoto ambazo Serikali peke yake haitaweza kuzimaliza

pasipo ushiriki wa wananchi. Changamoto hizo ni pamoja na

kuendelea kuwepo kwa mila na desturi zenye kuleta madhara

kama vile ukeketaji, mimba na ndoa za utotoni.

Changamoto nyingine ni umaskini miongoni mwa jamii;

mmomonyoko wa maadili; mapungufu katika malezi ya vijana na

watoto wetu kuhusu maisha yao hususan katika zama hizi za

sayansi, teknolojia na utandawazi pamoja na upungufu wa

14

Page 15: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

makazi ya muda kwa wahanga wa vitendo vya ukatili wa kijinsia

(yaani safe house).

ATHARI ZA UKATILI WA KIJINSIA

Ndugu Wananchi,

Napenda niwafahamishe kuwa, ukatili wa kijinsia hususan dhidi

ya wanawake na watoto unarudisha nyuma juhudi za Serikali za

kuhakikisha kuwa mapinduzi ya viwanda na kilimo yanafikiwa.

Hatuwezi kuwa na Taifa linalozalisha na kufikia malengo ya kuwa

Nchi ya uchumi wa kati iwapo muda mwingi unatumika kuamua

migogoro na kuhudumia wahanga wa ukatili wa kijinsia badala ya

kushiriki katika shughuli za uzalishaji.

Aidha, Serikali inatumia gharama nyingi katika kushughulikia

wahanga wa ukatili ambapo fedha hizo zingeweza kutumika

katika kutoa huduma nyingine za jamii. Kimsingi, Serikali ya

Awamu ya Tano haiwezi kuvumilia vitendo hivi kwa kuwa

vinaathiri maendeleo yetu na kusababisha uvunjifu wa amani.

15

Page 16: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

Natumia fursa hii kuwaagiza Wakuu wa Mikoa wote kuhakikisha

wanasimamia uanzishwaji wa Kamati za Ulinzi wa Wanawake

na Watoto za ngazi za Mikoa, Halmashauri, Kata na Vijiji kama

inavyoelekezwa katika Mwongozo wa uratibu wa Mpango wa

Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto.

Vilevile, nawaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini

kuanzisha Programu za Kijamii za kutokomeza ukatili wa

kijinsia katika Halmashauri husika zitakazozingatia hali halisi na

kuzitengea bajeti programu hizo kama inavyoelekezwa kwenye

Mpango Kazi wa Kitaifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya

Wanawake na Watoto.

MATARAJIO

Ndugu Wananchi,

Nimeelezwa kuwa, huu ni mwaka wa 27 wa maadhimisho ya Siku

16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia hapa Tanzania. Aidha,

maadhimisho haya yanafanyika Kitaifa kwa mara ya kwanza hapa

Dodoma ambapo ndio Makao Makuu ya Nchi. Hivyo, ni

16

Page 17: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

matumaini yangu kuwa kupitia Kampeni za aina hii kila mmoja

wetu na kila Taasisi itakuwa Balozi wa kuzuia na kutokomeza

ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake, wanaume, wasichana na

wavulana hapa nchini.

Ndugu Wananchi,

Nawapongeza ninyi wananchi wote kwa kuona umuhimu wa

Kampeni hii na kushiriki kikamilifu katika uzinduzi wa Kampeni hii.

Ni matarajio yangu kwamba kampeni hii ya Siku 16 za Kupinga

Ukatili wa Kijinsia – Kitaifa, italeta mabadiliko makubwa kupitia

jumbe mbalimbali zilizoandaliwa kupitia machapisho, nyimbo,

shuhuda na semina zitakazokuwa zinaendelea kutolewa kwenye

majukwaa mbalimbali katika kipindi chote cha kampeni.

Natoa wito kwa wadau wote kutumia kampeni hii kama jamvi la

kupata elimu na uelewa kuhusu namna ya kuzuia na kutokomeza

ukatili wa kijinsia kwa kuwa na sauti ya pamoja katika kukabiliana

na vitendo hivyo.

Ndugu Wananchi,

17

Page 18: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

Kwa mara nyingine nawahakikishia kuwa Serikali itaendelea

kuboresha na kuweka mazingira salama kwa wananchi wote kwa

kutekeleza Sera, Sheria, Mikakati, Mipango na Miongozo

mbalimbali ili kutokomeza ukatili wa kijinsia hapa nchini.

Pia, nirudie tena kuwasisitiza na kuwataka wadau wote kuendelea

kutekeleza Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya

Wanawake na Watoto (2017/2018 – 2021/2022). Ni matumaini

yangu kuwa kwa nguvu ya pamoja kati ya Serikali, Wadau wa

Maendeleo, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na Sekta Binafsi

tunaweza kupunguza na kuondoa kabisa vitendo vya ukatili wa

kijinsia katika jamii yetu.

HITIMISHO

Ndugu Wananchi,

Mwisho, natoa pongezi zangu za dhati kwa Wizara yenye

dhamana na jinsia, Shirika la Wanawake katika Sheria na

Maendeleo Afrika (WiLDAF) Tawi la Tanzania, Mtandao wa

Mashirika yanayopambana na Ukatili wa Kijinsia (MKUKI) na

18

Page 19: wildaftanzania.org · Web viewHOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

wadau wengine kwa kuandaa na kuratibu ufunguzi wa Kampeni

hii kwa mafanikio makubwa.

Halikadhalika, nawashukuru Wadau wa Maendeleo waliounga

mkono na kuweza kufanikisha Kampeni hii. Kwa hakika sitaweza

kumtaja kila mmoja lakini naomba niwataje wafuatao: Shirika la

Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Wanawake (UN-Women);

Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Elimu, Sayansi, na

Utamaduni (UNESCO); Shirika la Misaada la Uingereza (UKAID);

Ubalozi wa Ireland; Taasisi ya Huduma za Sheria (LSF); Shirika

la Oxfam na wengine wote waliofanikisha Kampeni hii.

Ndugu Wananchi

Baada ya kusema hayo, sasa natamka kwamba Kampeni ya

Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia kwa mwaka 2018

imezinduliwa rasmi leo tarehe 25 Novemba, 2018 kwenye

Viwanja hivi vya Jamhuri, jijini Dodoma.

ASANTENI KWA KUNISIKILIZA

19