nipe moyo wako - gospel truth · kanisa la mungu. ————————— the gospel truth, po...

8
NIPE MOYO WAKO moyo, akasimama polepole huku moyoni akiwa amejaa masumbuko makubwa. Alipatwa na majonzi mengi kwa sababu alitaka sana kumfuata Bwana, lakini alikuwa na utajiri mwingi na basi hakuwa tayari kuuza mali yake. Basi huzuni kubwa ikionekana hata kwenye macho yake kijana huyu alingiza kichwa chake na kuondoka kwa mwendo wa tarabu. Nayo macho ya Yesu yakaonekana kujaa machozi alipomtaza kijana huyo akiondoka. Hata ingawa Yesu alijua sifa nzuri za mwanaume huyo Yeye alitambua kwamba sifa hizo hazingemwezesha kijana huyo kuingia Mbinguni. Kuingia mbinguni kungemgharimu kijana huyo kutoa moyo wake na kumpenda Mungu kuliko kingine chote maishani mwake. Mungu alitaka kuwa mtawala wa shauku zote za kijana huyo. Naye Yesu alijua kwamba waka utakuja ambapo upendo wa kijana huyo kwa mambo ya dunia kungevurugana na shauku lake la kumfuata Bwana. Basi Yesu alishughulikia msingi na maana ya kumfuata Yeye. Mtu kuwa na tabia nzuri na kudumisha nidhamu sio mambo yatoshayo kumfanya mtu kupata uzima wa milele; pia mtu kuwa na na shauku ya mambo ya Mungu silo jambo ambalo linatosha. Inambidi mtu kujitoa mhanga kwa upendo wa kumfuata Bwana (Endelea kwa ukurasa 2) huyu wa kuvua alikuwa amejinyenyekeza, na alikuwa na shauku ya kumpendeza Mungu. Ndipo (huku sau yake ikiwa imejaa upendo) akamwambia, Umepungukiwa na neno moja. Enenda, ukauze ulivyo navyo vyote, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.Uso wa kijana huyo ukakunjamana kwa maana maneno ya Yesu yalimfanya kufa Mtu kuwa na tabia nzuri na kudumisha nidhamu sio mambo yatoshayo kumfanya kupata uzima wa milele.BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MISSION FIELD WORLDWIDE. Toleo 3 (Marko 10:17-23; Luka 18:18-24) Jua lilikuwa limewaka sana kaka sehemu hiyo ya mlima ambako kulijaa mawe waka Yesu alikuwa akitembea kwenye barabara hizo zilizojaa vumbi. Siku hiyo ilikuwa ndefu na wanafunzi hawa walikuwa wamechoka sana kutokana na kushughulikia makusanyiko ya watu ambao kila waka waliwaandama. Lakini kwa ghafla bwana mmoja ambaye alikuwa amevaa nguo za kitajiri akatokea huku akikimbia kwenye barabara hiyo kuwaelekea. Na hapo akipunga pumzi kwa nguvu alisujudu mbele yake Yesu na kwa sau ambayo ilijaa matarajio akamuuliza Yesu, Mwalimu mwema, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa milele?Yesu akasimama na kumtazama bwana huyu kwa huruma nyingi na akamjibu: Wazijua amri, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Usidanganye, Waheshimu baba yako na mama yako.Lakini huku moyo wake ukiwa umejaa ukweli kijana huyu akamwambia Yesu, Haya yote nimeyashika tangu utoto wangu.Yesu naye akageuza uso wake upande akiwa amejaa mawazo na kutafakari kuhusu mwanaume huyo ambaye alikuwa mbele zake. Alijua kwamba huyu alikuwa kiongozi, na kwamba alikuwa na utajiri mkubwa. Basi akaguzwa sana moyoni kuona kwamba kijana Tahariri 3 Kujifunza Biblia: Uhusiano Unaoongozwa wa Upendo 4 Shauka kubwa ya Mungu 5 Je, Wajua? Sio kwa Ufasaha wa Maneno 8 Swali na Jibu 7 MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE

Upload: others

Post on 31-Jan-2021

8 views

Category:

Documents


1 download

TRANSCRIPT

  • NIPE MOYO WAKO

    moyo, akasimama polepole huku moyoni

    akiwa amejaa masumbuko makubwa.

    Alipatwa na majonzi mengi kwa sababu

    alitaka sana kumfuata Bwana, lakini alikuwa

    na utajiri mwingi na basi hakuwa tayari kuuza

    mali yake. Basi huzuni kubwa ikionekana hata

    kwenye macho yake kijana huyu alitingiza

    kichwa chake na kuondoka kwa mwendo wa

    taratibu. Nayo macho ya Yesu yakaonekana

    kujaa machozi alipomtaza kijana huyo

    akiondoka.

    Hata ingawa Yesu alijua sifa nzuri za

    mwanaume huyo Yeye alitambua kwamba

    sifa hizo hazingemwezesha kijana huyo

    kuingia Mbinguni. Kuingia mbinguni

    kungemgharimu kijana huyo kutoa moyo

    wake na kumpenda Mungu kuliko kingine

    chote maishani mwake. Mungu alitaka kuwa

    mtawala wa shauku zote za kijana huyo. Naye

    Yesu alijua kwamba wakati utakuja ambapo

    upendo wa kijana huyo kwa mambo ya dunia

    kungevurugana na shauku lake la kumfuata

    Bwana. Basi Yesu alishughulikia msingi na

    maana ya kumfuata Yeye.

    Mtu kuwa na tabia nzuri na kudumisha

    nidhamu sio mambo yatoshayo kumfanya

    mtu kupata uzima wa milele; pia mtu kuwa

    na na shauku ya mambo ya Mungu silo jambo

    ambalo linatosha. Inambidi mtu kujitoa

    mhanga kwa upendo wa kumfuata Bwana

    (Endelea kwa ukurasa 2)

    huyu wa kuvutia alikuwa amejinyenyekeza,

    na alikuwa na shauku ya kumpendeza

    Mungu. Ndipo (huku sauti yake ikiwa imejaa

    upendo) akamwambia, “Umepungukiwa na

    neno moja. Enenda, ukauze ulivyo navyo

    vyote, uwape maskini, nawe utakuwa na

    hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.”

    Uso wa kijana huyo ukakunjamana kwa

    maana maneno ya Yesu yalimfanya kufa

    “Mtu kuwa na tabia nzuri

    na kudumisha nidhamu

    sio mambo yatoshayo

    kumfanya kupata uzima

    wa milele.”

    BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE

    MISSION FIELD WORLDWIDE.

    Toleo 3

    (Marko 10:17-23; Luka 18:18-24)

    Jua lilikuwa limewaka sana katika sehemu

    hiyo ya mlima ambako kulijaa mawe wakati

    Yesu alikuwa akitembea kwenye barabara

    hizo zilizojaa vumbi. Siku hiyo ilikuwa ndefu

    na wanafunzi hawa walikuwa wamechoka

    sana kutokana na kushughulikia makusanyiko

    ya watu ambao kila wakati waliwaandama.

    Lakini kwa ghafla bwana mmoja ambaye

    alikuwa amevaa nguo za kitajiri akatokea

    huku akikimbia kwenye barabara hiyo

    kuwaelekea. Na hapo akipunga pumzi kwa

    nguvu alisujudu mbele yake Yesu na kwa

    sauti ambayo ilijaa matarajio akamuuliza

    Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili

    nipate kuurithi uzima wa milele?”

    Yesu akasimama na kumtazama bwana huyu

    kwa huruma nyingi na akamjibu: “Wazijua

    amri, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie

    uongo, Usidanganye, Waheshimu baba yako

    na mama yako.” Lakini huku moyo wake

    ukiwa umejaa ukweli kijana huyu

    akamwambia Yesu, “Haya yote nimeyashika

    tangu utoto wangu.”

    Yesu naye akageuza uso wake upande akiwa

    amejaa mawazo na kutafakari kuhusu

    mwanaume huyo ambaye alikuwa mbele

    zake. Alijua kwamba huyu alikuwa kiongozi,

    na kwamba alikuwa na utajiri mkubwa. Basi

    akaguzwa sana moyoni kuona kwamba kijana

    Tahariri

    3

    Kujifunza Biblia:

    Uhusiano Unaoongozwa

    wa Upendo

    4

    Shauka kubwa ya Mungu

    5

    Je, Wajua?

    Sio kwa Ufasaha wa

    Maneno

    8

    Swali na Jibu

    7

    MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA

    KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE

  • Inafundisha Kuhusu...

    BIBLIA

    Ukurasa wa 2

    Yesu ili yeye aweze kurithi Mbingu. Tunaweza kuwa na shauku kwa Mungu, tunaweza

    pia kuwa na kiwango fulani cha upendo, tunaweza pia kuwa wake au waume wazuri

    (kwa watu ambao tulioa), hata tunaweza kuwa wananchi wazuri, na pia kuwa majirani

    bora; lakini tunahitaji kuwa zaidi ya hayo.

    Mungu anataka kwanza kabisa awe mtawala wa shauku zetu: “Mwanangu, nipe moyo

    wako; Macho yako yapendezwe na njia zangu” (Mithali 23:26). Maneno hayo yangali

    ndio kilio chake Mungu kwa mwanadamu— “Nipe moyo wako.” Shauku zetu zote

    zinapokuwa kwake Mungu ndipo ambapo tunaweza kumpenda kwa mioyo yetu yote,

    nafsi zetu, mawazo yetu na nguvu zetu zote. Ni wakati ambapo Mungu amepata

    mioyo yetu ndipo anapata shauku zetu, wakati wetu, pesa zetu, ndoto zetu na hata

    mipango yetu. Wakati huo ndipo anakuwa nambari moja katika kila fani ya maisha

    yetu.

    Watu wengi katika siku zetu huja kanisani huku wakitaka kujua kuhusu Mbingu kama

    ambavyo kiongozi huyo tajiri alifanya. Lakini wengine wao huondoka kwa sababu

    hawako tayari kumpa Mungu shauku zao zote. Wengine nao washirika wa kanisa—

    huku wakiimba, wakiomba, wakifunza biblia na hata wakati mwingine wakihubiri;

    lakini wao huwa hawampatii Mungu “kitu hicho kimoja” ambacho hunabaki kuwa

    kizuizi cha upendo wao kwa Mungu.

    Je, upendo wako uko wapi leo? Je, umebakisha kitu kimoja? Je, umejitolea mhanga

    kwa Mungu? Hebu mpe moyo wako. Chochote ambacho utahitaji kuachilia basi

    kiachilie ili umfuate Bwana Yesu nawe utalipiwa kwa zawadi kuu katika maisha haya

    na hata katika siku zijazo.

    —mws

    (Endelea kutoka ukurasa 1)

    Neno la Mungu

    2 Tim. 3:6, 2 Pet. 1:20-21, Mt. 24:35

    Uhusiano wa Upendo

    Mt. 22:37-40, Yn. 14:21-23, 1 Yoh. 4:7-21

    Toba

    Mdo. 3:19, 17:30, 2 Kor. 7:10

    Uzao Mpya

    Yn. 3:3-7, 2 Kor. 5:17, Rum. 6:1-4, Efe. 2:1, 5-6

    Uhuru Kutokana na Dhambi

    1 Yoh. 5:18, Mt. 1:21, Yn. 8:11

    Ujazo wa Roho Mtakatifu

    Mdo. 19:2, 15:8-9, 1:8

    Utakatifu

    Lk. 1:73-75, Ebr. 12:14, 1 Pet. 1:15-16,

    Tit. 2:11-12, Rum. 6:22

    Ufalme wa Mungu

    Lk. 17:20-21, Rum. 14:17, Yn. 18:36

    Kanisa

    Mdo. 2:47, Efe. 4:4-6, 1 Kor. 12:12-13,

    Kol. 1:18

    Umoja

    Yn. 17:20-23, Gal. 3:28, Ufu. 18:2-4

    Kanuni za Kanisa

    Mt. 28:19-20, 26:26-30, I Kor. 11:23-27,

    Yn. 13:14-17

    Uponyaji wa Kiungu

    Lk. 4:18, Isa. 53:4-5, Yak. 5:13-16

    Utakatifu wa Ndoa

    Mt. 19:5-6, Lk. 16:18, Rum. 7:2-3,

    I Kor. 7:10-11

    Urembo wa Nje

    I Tim. 2:9-10, I Kor. 11:14-15, Kum. 22:5

    Mwisho wa Nyakati

    2 Pet. 3:7-12, Yn 5:28-29, 2 Kor. 5:10, Mt.

    25:31-46

    Kupenda Amani

    Lk. 6:27-29, 18:20

    Ibada

    Yn. 4:23-24, Efe. 5:19, 2 Kor. 3:17

    Wajibu Mkuu

    Mk. 16:15

    Gazeti a Ukweli wa injili linachapishwa katika mataifa mbalimbali ili kusambazwa katika maeneo hayo. Kazi hii na zingine za kimishenari ambazo sisi hufanya huwezekana kupitia kwa matoleo ya kujitolea yanayotolewa kwa jina la

    Kanisa la Mungu.

    —————————

    The Gospel Truth, PO Box 2042, Nixa, MO 65714 USA

    [email protected]

    Gazeti la ‘Ukweli wa Injili’ huchapishwa kwa jina la Bwana kwa matumizi ya watu wa mataifa yote

    kwa kusudi la kuimarisha na kuwahimiza watu wote katika ukweli wa neno la Mungu. Gazeti hili hufundisha na kueneza ukweli wa Biblia ambao umethibitishwa tangu nyakati za Yesu Kristo na

    mitume.

    Neno la Mungu ndio mwongozo halisi na wa kipekee wa imani. Linafundisha wokovu na ukom-bozi kutokana na dhambi unaoletwa na utakaso wa Yesu Kristo; ambao hufuatiwa na ujazo wa

    Roho Mtakatifu anayemwongoza mhudumu, kumwonyesha njia, na kumpatia nguvu; pia unam-letea mtu utakatifu halisi katika kila fani ya maisha yake; na pia kuleta umoja na utangamano wa watu wa Mungu. Huduma inayokubalika na Mungu inatokana na mtu kuwa na uhusiano wa kibin-

    afsi na wa upendo ambao msingi wake ni ukweli.

    Waandishi: Michael na René Smith

    Ukweli wa Injili ni gazeti la kieletroniki linalochapishwa kila robo ya mwaka kwa jinsi Mungu

    anavyotuongoza. Tutembelee katika tovuti yetu ya www.thegospeltruth.org ili uagize jalida hili kupitia kwa orodha yetu ya anwani pepe na upokee toleo lako la wakati huu. Hebu jisikie huru kututumia orodha ya majina na anwani pepe za watu wengine ambao wangependa kupokea toleo

    hili kutoka kwa mwandishi wa jalida la Ukweli wa Injili.

    UKWELI WA INJILI

    UAGIZAJI

    WASILIANA NASI

  • Tutembelee katika

    www.thegospeltruth.org

    ili uagize na uweze

    kupata toleo za

    hapo mbeleni.

    Tahariri

    Ukurasa wa 3

    Haleluya. Nampenda BWANA kwa kuwa anaisikiliza Sauti yangu na dua zangu. Kwa

    maana amenitegea sikio lake, Kwa hiyo nitamwita siku zangu zote —Zaburi 116:1-2

    Nikiwa mtoto mdogo niliutoa moyo wangu kwa Mungu na kujisalimisha kwa utunzi

    wake. Mimi ninakumbuka sana jinsi nilivyodondokwa na machozi kwa vile ambavyo

    Roho Mtakatifu alifanya kazi yake ya kunihakikishia moyoni mwangu. Hapo katika

    chumba cha nyuma katika Shule ya Jumapili mama yangu aliomba nami ili Yesu aingie moyoni mwangu.

    Hata ingawa sikuwa nimejiingiza sana dhambini nilihitaji neema ile ya wokovu wa Mungu ambayo

    humwokoa mwanadamu iingie katika maisha yangu kama jinsi ambavyo mshiriki wa madawa ya kulevya

    hata mlevi wa pombe anahitaji. Na nilipokuwa nikikua na kukomaa mimi nilipitia na “uchungu wa kukua

    kiroho” hata wakati mwingine nikakosa kufikia malengo ya maisha ya Kikristo—kama ambavyo hutokea

    kwa watu wengi ambao wanaokoka wakiwa wangali wadogo. Lakini kamwe sikuwahi kupoteza shauku

    langu la kumtumikia Mungu, hata ingawa nilifanya safari nyingi madhabahuni ili kuombewa kuokoka

    tena. Hadi leo mimi ninamshukuru Mungu kwa ajili ya uaminifu wa Roho wake. Kama wimbo

    unavyosema, “Roho ndiye aliyeniongoza hadi mahali nilipo sasa.” Mimi nilikuwa (na ningali) na shauku

    kubwa sana ya kuwepo na uwepo wa Mungu maishani maishani mwangu kila siku, kwa maana nikifuata

    njia zangu mwenyewe nitapotea.

    Mimi nampenda Bwana na ninatilia umuhimu swala la uwepo wake maishani mwangu hata kuliko uhai

    wangu mwenyewe. Mungu amekuwa mwaminifu kusikia sauti yangu na kujibu maombi yangu. Yeye

    ameponya mwili wangu na akaniokoa kutoka mautini, na pia amenipatia familia ya ajabu, na kukutana

    na mahitaji yangu ya kila siki; zaidi ya yote Yeye aliniokoa kutokana na minyororo na utumwa wa

    dhambi. Amenipatia amani yake na uwepo wa Roho wake Mtakatifu. Kwa kweli ninayo mengi ya

    kumshukuru Mungu. Hata ingawa wewe unakumbana na majaribu na masumbufu ya aina nyingi kama

    unampenda Bwana maishani mwako una hazina kuu zaidi kuliko ingine ulimwenguni mote. Tolea hili la

    Ukweli wa Injili linatilia umuhimu amri ambayo ni kuu zaidi na mafundisho ambayo ni makuu zaidi

    katika Biblia, maanake—Upendo.

    Unapokazana na mwaka huu mpya uwe na uhakika kwamba Mungu ataendelea kuwa mwaminifu

    kwako. Kama jinsi ambavyo amekutana na mahitaji yako hapo mbeleni na kukuwezesha kupitia

    mabonde na hata motoni ndivyo ambavyo atakuwa nawe mwaka huu. Ewe msafiri pamoja na Yesu,

    endelea kuwa mwaminifu na uendelee kumtumaini Bwana wako. Ushindi mpya wakungoja na

    ukiendelea kushikamana naye Yesu siku moja utatembea naye Mbinguni.

    Ombi langu ni kwamba toleo la jalida la Ukweli wa Injili litaendelea kuwa na himizo na msaada mkuu

    kwa kila msomi hapa kwetu nyumbani na hata katika nchi za kigeni. Kama gazeti hili limekuwa la

    msaada kwako sisi tutapata kujengwa katika kazi hii ikiwa utaweza kutuandikia kuhusiana na swala hilo.

    Basi jisikie huru kuniandikia kwa njia ya moja kwa moja kupitia kwa barua pepe:

    [email protected].

    Basi ni ombi letu kwamba Mungu atakubariki na kukupatia mwaka wa ajabu kupitia kwa uwepo wake.

    Ninaomba kwamba tutembee katika mwanga na utakatifu wa Neno lake Mungu ili tuweze kudumu

    katika amani.

    —Michael W. Smith

    Januari 2013.

    mailto:[email protected]

  • MAFUNZO YA BIBLIA

    Somo la Biblia: Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo

    Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo,

    naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu,

    na Mungu hukaa ndani yake. Katika hili pendo

    limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika

    siku ya hukumu; kwa kuwa, kama yeye alivyo,

    ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu.

    – 1 Yohana 4:16-70

    Maana ya upendo: Kuvutiwa na mtu, kumtakia

    mema, kumfanyia mema, kushikamana na mtu.

    Tendo la mtu analochagua kufanya.

    I. Mawazo ya Mungu kwa Mwanadamu

    A. Yeremia 31:3 Kuvutiwa na fadhili zake.

    B. Yeremia 29:11-13 Mawazo ya amani.

    II. Shauku la Mungu la Kuwa na Uhusiano na

    Mwanadamu

    A. Mwanzo 3:8-9 Mungu alikuwa na shauku la

    ushirika.

    B. Ufunuo 3:20 Tazama nasimama mlangoni.

    C. 2 Wakorintho 5:17-18 Kupatanishwa na

    Mungu.

    III. Mungu Anapenda Nani?

    A. Yohana 3:16 Ulimwengu.

    B. Warumi 5:8 Watu wenye dhambi.

    C. Waefeso 5:25 Kanisa.

    IV. Dhihirisho la Upendo wa Mungu

    A. 1 Yohana 4:9-10 Mungu alimtuma Mwanawe

    wa pekee.

    B. 1 Yohana 3:1,16 Tazameni ni pendo la

    namna gani.

    V. Upendo Ndio Amri Kuu Zaidi

    A. Kumbukumbu 10:12 Upendo umeamriwa.

    B. Mathayo 22:36-38 Mpende Bwana wako.

    C. 1 Wakorintho 13:1-3 Bila upendo.

    VI. Upendo ni Kipawa cha Mungu

    A. 1 Yohana 4:7-8 Upendo unatokana na

    Mungu.

    B. Warumi 5:5 Upendo unatolewa na Roho

    Mtakatifu.

    JINSI YA KUTILIA

    NGUVU UPENDO WAKO

    KWA MUNGU

    TUBU

    Kubali kwamba umekuwa mlegevu na

    kwamba umepoteza ari yako na bidii kwa

    Mungu. Tubu na umwombe Mungu

    msamaha na kwamba akurudishe mahali

    ambapo ulikuwa hapo mbeleni kwa

    mambo yako ya kiroho.

    MTAFUTE MUNGU Anza kujifunza maandiko tena kwa bidii.

    Mwombe Mungu akurudishie shauku ya

    kuupenda ukweli na haki.

    KUWA MTIIFU Jitenge kutokana na mambo ambayo

    yatakuvuta mbali na Mungu na

    kukupeleka mbali na makusudio yake

    maishani mwako. Utiifu ni jambo ambalo

    hutokana na mtu kufanya uchaguzi wa

    wazi wa kumpenda Mungu zaidi ya

    mambo mengine yote.

    USIPUUZE USHIRIKA Usiache kutilia maanani swala la

    kuhudhuria ibada. Andaa moyo wako na

    uweke kando kila jambo ambalo

    linakusumbua wakati ambapo umeingia

    nyumbani mwake Mungu.

    WATUMIKIE WENGINE Usiuruhusu ubinafsi ufanye uwe na uvivu

    wa kiroho. Mwombe Mungu akuonyeshe

    jinsi utakavyomtumikia kwa kuwatumikia

    wale ambao wako karibu nawe.

    KUWA NA FURAHA YA WOKOVU Dumu ukiwa na moyo ambao una

    shukrani kwa ajili ya baraka zake Mungu.

    Kila siku mwonyeshe Mungu upendo

    wako (kwake) kwa mambo yote

    unayofanya.

    Ukurasa wa 4

    Somo: Uhusiano Unaoongozwa na

    VII. Upendo Ni kwa Matendo

    A. 1 Yohana 3:18 Tupendane kwa matendo

    na kweli.

    B. Mathayo 15:8 Wengine huniheshimu kwa

    mdomo.

    VIII. Jinsi Upendo Wetu kwa Mungu

    Unavyojidhihirisha

    A. Yohana 14:15, 23-24 Atadumisha maneno

    yangu.

    B. 1 Yohana 5:3 Atadumisha amri zake.

    C. 1 Yohana 4:20-21Twawapenda ndugu.

    IX. Haiwezekani Kumpenda Mungu na

    Ulimwengu

    A. Mathayo 6:24 Huwezi kutumikia mabwana

    wawili.

    B. 1 Yohana 2:15-17 Usiupende ulimwengu.

    C. Kumbukumbu 13:3 Bwana hujaribu

    upendo wetu.

    X. Sifa za Upendo wa Kweli

    A. 2 Wakorintho 6:6 Hauna unafiki.

    B. 2 Wakorintho 8:8 Wenye unyoofu.

    C. 1 Timotheo 1:5 Unaotokana na moyo safi.

    XI. Ukamilifu Unaotokana na Upendo

    A. Waefeso 3:17-19 Utimilifu wa Mungu.

    B. Yohana 15:10-11 Ili furaha yenu itimizwe.

    XII. Nguvu za Upendo

    A. 1 Yohana 4:18 Upendo ulio kamili hutupa

    hofu nje.

    B. 2 Wakorintho 5:14-15 Upendo hubidisha.

    XIII. Ni Nini Hutenganisha Mwanadamu na

    Upendo wa Mungu?

    A. Warumi 8:35 Ni nani atatutenganisha?

    B. Yohana 14:23-24 Kutofuata amri.

    XIV. Kupoteza Upendo

    A. Mathayo 24:12 Upendo utakuwa baridi.

    B. Ufunuo 2:4 Kuacha upendo wa kwanza.

    C. Ufunuo 3:15-17 Si moto si baridi.

    XV. Kipawa kwa Wale Wampendao Mungu

    A. Yakobo 2:5 Warithi wa ufalme.

    B. 2 Timotheo 4:7-8 Taji la haki.

  • Ukurasa wa 5

    What is Truth?

    SHAUKU KUBWA YA MUNGU Nakala ya kuandamana na Mafunzo ya Biblia

    MUNGU AMTAFUTA MWANADAMU Tangu kuumbwa kwa ulimwengu Mungu amekuwa na

    shauku ya kuwa na uhusiana na mwanadamu. Tunasoma

    jinsi Mungu alitembea katika Shamba la Edeni wakati wa

    kupunga hewa ya mchana huku akiwa na shauku la kuwa na

    ushirika na Adamu na Hawa (Mwanzo 3:8-9). Ingawa Biblia

    ni historia na kitabu cha thiolojia kusema kweli biblia ni

    nakala ya shauku la Mungu na juhudi zake za kutafuta

    uhusiano wa upendo na wanadamu.

    DHAMBI YAVUNJA UHUSIANO NA MUNGU Mungu aliumba wanadamu na shauku lake kuu ni kuwa na

    uhusiano na viumbe wake—sio kwa njia

    ya kushurutishwa bali kwa upendo.

    Adamu na Hawa walikosa kumtii

    Mungu na dhambi yao ikawatenganisha

    na uhusiano wa karibu ambao

    walikuwa nao na Mungu hapo mbeleni.

    Daima dhambi huvunja uhusiano kati ya

    mwanadamu na Mungu. Lakini Mungu hakurusu utengano

    ulioletwa na dhambi, ukosefu wa utakatifu, na hukumu ya

    kifo iliyokuwa juu yetu kuendelea kututenganisha naye.

    MUNGU ALIMTUMA MWANAWE ILI

    TUPATANISHWE NAYE

    Mungu alitupenda sana hata akamtuma Mwanawe wa

    pekee duniani ili tuweze kuokolewa (Yohana 3:16).

    Msukumo ambao Mungu alikuwa nao ulikuwa ni wa

    upendo na upendo huo ungaliko hawa wakati wa sasa:

    “Bwana alinitokea zamani, akisema, Naam nimekupenda

    kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa

    fadhili zangu” (Yeremia 31:3).

    MATENDO YOTE YA MUNGU HUTOKANA NA

    UPENDO

    “Mungu ni upendo”(1 Yohana 4:8) na hiyo ndio nguzo ya

    mahusiano yake na wanadamu. Wengine humwona Mungu

    kama Mungu wa kufanyisha watu kazi ya sulubu—ambaye

    ana matakwa mengi na ambaye ni vigumu kumpendeza.

    Lakini picha hii inamwakilisha Shetani, haimwakilishi

    Mungu. Mungu ni Mungu wa upendo ambaye hujali kuhusu

    mambo yote ambayo huadhiri maisha yetu. Yeye anajaribu

    kumfikia kila mwanadamu kwa upendo haijalishi hali yake.

    Kamwe sisi hatustahili upendo wa Mungu na hakuna

    chochote ambacho tumefanya cha kustahili upendo huo.

    “Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu

    sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa

    tungali wenye dhambi” (Warumi 5:8).

    UPENDO UKIPATANA NA UPENDO HUWA

    UPENDO ULIOKAMILIKA Kama upendo haupewi upendo huwa basi haujakamiika.

    Mungu anatupenda lakini upendo huo haukamiliki hadi

    hapo tunapompenda bila kujibakishia

    chochote na kwa moyo wetu wote.

    Mwanasheria mmoja alimuuliza Yesu,

    “Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo

    kuu? Akamwambia, Mpende Bwana

    Mungu wako kwa moyo wako wote, na

    kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.

    Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.

    Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu? Akamwambia,

    Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa

    roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo

    kuu, tena ni ya kwanza.” Mafundisho mengine yote huwa

    bure iwapo msingi wake sio sheria hii ya kwanza na iliyo kuu

    zaidi. Watu wengi humtumikia Mungu kutokana na woga au

    kwa kujitolea kwa kanisa au kwa thiolojia fulani. Lakini

    uhusiano wa upendo huwa wenye kina zaidi na utajiri

    mkubwa. Uhusiano wa upendo huleta utoshelevu wa kweli

    kwa maana sasa uhusiano huwa umekamilika. Hii ndiyo

    chanzo cha amani ya kweli na furaha ya kumtumikia

    Mungu.

    UPENDO WA KWELI HAUPATIKANI KWA NJIA

    YA MABAVU

    Kulikuwa na jamaa mmoja ambaye angemfungia mkewe

    kwa nyororo jikoni mwao kila siku alipokuwa akitoka

    kwenda kazini. Yeye alikuwa na hofu kwamba mkewe

    angemwacha na asirudi. Uhusiano wao ulikuwa wa uongo

    na utumwa. Ingekuwa afadhali zaidi kama mume

    (Endelea kwa ukurasa 6)

  • Ukurasa wa 6

    angeondoka kwenda kazini huku akifahamu kwamba mkewe

    angekuwa tu hapo nyumbani atakaporudi kwa sababu mke

    huyo alimpenda. Huu ndio uhusiano ambao Mungu

    anatamani—uhusiano ambao mtu hashurutishwi kuishi kwa

    utakatifu lakini ambao mtu anaishi kwa utakatifu kutokana na

    moyo wake wa upendo. Nguvu za upendo ndizo husukuma

    watoto wa kweli wa Mungu kuishi maisha matakatifu

    (2 Wakorintho 5:14).

    USHAHIDI WA UPENDO WETU NI UTIIFU WETU

    Watu wengi humkaribia Mungu kwa vinywa vyao na

    kumtukuza kwa midomo yao huku mioyo yao ikiwa mbali naye

    (Mathayo 15:8). Lakini upendo wa kweli haudhihiriki kwa

    maneno tunayonena bali kwa tabia za maisha yetu. “Yesu

    akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno

    langu” (Yohana 14:23). Huu ndio ushahidi wa kweli wa upendo

    katika ulimwengu ambao wengi humkiri Kristo lakini ni

    wachache ambao hutii Neno la Mungu. Mahali ambako hamna

    utiifu hapana upendo. Hakuna chochote ambacho kinaweza

    kututenganisha na upendo wa Mungu (Warumi 8:35)

    isipokuwa kutokutii kwetu (Yohana 14:23-24).

    HAKUNA UPENDO MWINGINE ISIPOKUWA

    “UPENDO WA KWANZA” “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili” (Mathayo

    6:24). Hakuna nafasi katika uhusiano na Mungu wa mtu

    kufuata ulimwengu wenye dhambi na wakati huo huo

    kumfuata Mungu. Mtu akipenda ulimwengu upendo wa Baba

    haumo ndani yake (1 Yohana 2:15-17).

    UPENDO HUFANYA MTU KUJITOA MHANGA

    Wakati watu wawili wanapendana kwa kweli wao huwa tayari

    kujinyima wakati na uwezo wao ili wawe pamoja. Shauku yao

    kubwa huwa ni mmoja kumpendeza mwingine. Jambo hili

    huwa la kweli hata kwa upendo wa kweli kwa Mungu utokao

    moyoni mwa mtu. Upendo humfanya mtu kumwabudu Mungu

    kwa hiari yake mwenyewe na kumtumikia. Basi utiifu unakuwa

    si kazi ngumu ya sulubu bali huwa ni dhihirisho la upendo.

    Upendo huleta furaha, kutoshereka, na nguvu katika utumishi

    kwa Bwana.

    APENDAYE MUNGU HUPENDA NDUGU YAKE

    Watu wanapopata ujuzi wa upendo wa Mungu upendo wak

    humwagwa mioyoni mwao kupitia kwa Roho Mtakatifu

    (Warumi 5:5). Uhusiano huo huonekana sio tu kupitia kwa mtu

    kuwa mtiifu kwa Mungu bali pia kwa upendo ambao mtu

    huonyesha ndugu zake kanisani. Kwa maana mtu asipopenda

    ndugu yake basi upendo wa Mungu haumo ndani yake

    (1 Yohana 4:20-21).

    UPENDO MKAMILIFU HUTUHAKIKISHIA UZIMA

    WA MILELE

    Sio tu kwamba uhusiana wa upendo na Mungu hutuletea

    amani na uhusiano wa karibu na Mungu bali pia

    unatuhakikishia uzima wa milele. “Baada ya hayo nimewekewa

    taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa

    siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda

    kufunuliwa kwake (1 Timotheo 4:8).

    SHAUKU KUU LA MUNGU NI KUWA NA UHUSIANO

    NAWE Shauku kuu la Mungu ni wewe kuwa na uhusiana na urafiki wa

    karibu naye. Mungu angetaka kuwa sehemu ya maisha yako.

    Yeye ana shauku kwamba utatumia wakati wako na Yeye na

    pia kwamba utawasiliana na Yeye. Kuna ushirikia wa karibu na

    wa ajabu ambao unapatikana katika uhusiano kama huo.

    Uhusiano na Mungu ambao msingi wake ni upendo utapatia

    maisha yako maana na kusudi la kuishi.

    —mws.

    (Endelea kutoka ukurasa 5)

  • Ukurasa wa 7

    Kikristo yenye uchovu mwingi ya kuwa na msimamo dhabiti kwa mafundisho ya Kikristo lakini bila upendo wa kupatia maisha hayo uhai. Uhusiano huchukuwa wakati wa mtu. Pia unahitaji kulindwa dhidi ya mambo ambayo yanaweza kuingilia kati.

    “Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa” (Mathayo 24:12). Wengi wamepoteza upendo wao wa kwanza kwa maana wametoa upendo wao kwa mambo ya ulimwengu huu huku wakidumisha msimamo ambao kimsingi unaambatana na mafundisho ya Kikristo. Mungu basi anakuwa na wa kiwango cha pili kwa upendo wao au hata anakuwa ni wa kiwango cha chini zaidi. Wakati wao, uwezo wao, umakini wao, na mvuto wa upendo wao unakuwa kwa mambo mengine.

    Jambo hili huleta uvivu kwa maisha ya mtu kumwishia Mungu na kunakuwa na ukosefu wa bidii ya kueneza injili. Kunakuwa tu na aina ya utauwa. Basi ni jambo muhimu kwetu kuchunguza tena maisha yetu ili kuhakikisha kwamba maisha yetu na bidii yetu ili kuhakikisha kwamba hatupotezi upendo wa kwanza.

    Kama ambavyo mke na mume wanahitaji kuwasiliana na kutumia wakati pamoja ili kudumisha upendo wao ukiwa wenye nguvu ndivyo hivyo ilivyo kwa Mungu. Ni jambo muhimu kwetu ni kufanya bidii kudumisha “upendo wa kwanza” kwa kusoma Neno la Mungu, kuomba, kudumisha mahusiano, na kumweka Mungu mwanzo katika maamuzi yote tunayofanya. Zaidi ya yote tunahitaji kuufanya upendo kuwa ndio msukumo wa huduma yetu na sababu yetu ya kufanya mambo yafaayo.

    Ni katika ujuzi huo wa upendo wa kwanza ndipo utakapopata bidii ya kushiriki injili na upako wa maisha ya kila siku. Upendo huo hufanya mafundisho ya Kikristo kuwa hai na kutoa sababu na furaha ya maisha.

    —mws

    upendo wao huwa limetokomea. Na mambo pia huwa hivyo kwa watu wengi katika uhusiano wao na Mungu. Waokovu wapya huwa na wakati mzuri wakiwa katika hali hiyo ya kujihisi wamesamehewa dhambi zao na wako kwenye maisha yaliyojaa amani na neema. Lakini ikiwa uhusiano huo haudumishwi mtu huyo anaweza aidha kuirudia dhambi ama kuendelea kufanya mambo “ya haki” lakini bila ukakamavu wa upendo huo wa kwanza.

    Wale ambao wamepoteza upendo wa kwanza wameamuriwa kutubu. Kunao watu wengi na makusanyiko mengi ambayo wamesimama wima dhidi ya

    uovu lakini wamepoteza moto wa upendo ambao ulikuwa ukiwaka hapo mbeleni. Wao wamepoteza kile kitu ambacho Mungu alitaka wawe nacho toka mwanzo—uhusiano wa upendo.

    Upendo mkuu kwa Mungu ndio huleta joto katika huduma ambayo mtu anamfanyia Mungu. Basi tusianguke kwenye mtego wa kuwa na maisha ya

    SWALI: Je, ni nini maana ya mtu kupoteza upendo wa kwanza?

    JIBU: Swahili hili linaambatana na andiko la Ufunuo 2:4 ambalo linasema: “Lakini nina neno juu yako, ya kwamba umeuacha upendo wako wa kwanza.” Roho wa Mungu alikuwa akizungumza kuhusu kusanyiko la Efeso.

    Zingatia kwamba kusanyiko hili lilikuwa limesimama wima dhidi ya uovu na walikuwa wakifanya mambo mengi yaliyokuwa mazuri na ya haki. Ingawa walikuwa watiifu kwa mambo ya thiolojia na mafunzo ya kanisa Waefeso walikuwa wamepoteza uhusiano wa upendo uliowaambatanisha na Mungu ambao walikuwa nao hapo mbeleni. Nakala ya mafafanuzi cha JFB inasema: “Joto lao la upendo lilikuwa limeondoka na badala yake wakapatwa na maisha ya kushikilia mafundisho ya Kikristo kwa nguvu na ambayo hayakuwa na uhai.”

    Wakati mwingi Maandiko hulinganisha uhusiano kati ya mwanadamu na Kristo kuwa kama ule wa kati ya bwana na mkewe. Hebu fikiria kuhusu wapenzi ambao walioa majuzi na ambao wanapendana sana na kujitolea mmoja kwa mwingine kwa uhusiano ulio hai. Wao hutaka kutumia wakati mwingi pamoja na kujinyima mambo mengi mmoja kwa ajili ya yule mwingine. Ndoa yao huwa na moto sana na pia uhai mwingi.

    Lakini kama inavyokuwa wakati mwingi kwenye ulimwengu huu wenye dhambi wapendanao hupoteza ule upendo wao wa mmoja kwa mwingine na ndoa yao inakosa uhai. Wao huanza kuishi tu kwenye nyumba moja lakini joto la

    “Wengi wamepoteza

    upendo wao wa kwanza . . .

    Wakati wao, uwezo wao,

    umakini wao,

    na mvuto wa upendo wao unaku-

    wa kwa mambo mengine . . .

    Mungu basi anakuwa na wa

    kiwango cha pili kwa upendo

    wao au hata anakuwa ni wa

    kiwango cha chini zaidi.”

    MASWALI

    MAJIBU na

  • The Gospel Truth

    P.O. Box 2042

    Nixa, MO 65714

    USA

    Email:

    [email protected]

    Anwani

    Basi, ndugu zangu, mimi nilipokuja kwenu, sikuja niwahubiri siri ya Mungu kwa ufasaha wa

    maneno, wala kwa hekima. Maana naliazimu nisijue neno lo lote kwenu ila Yesu Kristo,

    naye amesulibiwa. Nami nalikuwako kwenu katika hali ya udhaifu na hofu na matetemeko

    mengi. Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye

    kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu, ili imani yenu isiwe katika

    hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu. —1 Wakorintho 2:1-5

    Jumapili moja mhubiri Charles Haddon Spurgeon ambaye

    anajulikana kama “mhubiri wa wahubiri” alijihisi kwamba

    amehubiri kwa njia dhaifu sana hivi kwamba akajionea aibu.

    Alipokuwa akiondoka kutoka mle kanisana mwake lililokuwa

    katika mji wa London na ambalo lilijulikana kama Metropolitan

    Tabernacle yeye aliduwazwa na swali kama kwamba kutakuwa

    na jambo lolote nzuri ambalo lingetokana na ujumbe kama huo

    wake. Alipofika nyumbani akapiga magoti na kuomba, “Ewe

    Bwana Mungu, waweza kufanya kitu bila kuwa na chochote.

    Naomba ukaubariki ujumbe huo wangu ambao ni hafifu sana.”

    Kwa muda wa miezi kadhaa iliyofuata watu 41 wakasema waliamua kumwamini Kristo

    kama mwokozi kutokana na ujumbe huo “dhaifu.” Katika Jumapili iliyofuata na ili kufuta

    “makosa” yake Spurgen aliandaa ujumbe “kemkem” lakini ng’o hakuna mtu aliyeokoka.

    Ujuzi ambao Spurgeon alipata unatilia mkazo masomo mawili muhimu kwa watu wote

    wamtumikiao Bwana. Kwanza kabisa tunahitaji baraka za Mungu kwa juhudi zetu zote.

    Sulemani alisema katika Zaburi 127:1, “BWANA asipoijenga nyumba waijengao wanafanya

    kazi bure.” Pili, udhaifu wetu huwa nafasi kwa Mungu kudhihirisha nguvu zake. Mtume

    Paulo akasema, “Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na matusi, na matatizo, na adha, na

    shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu”

    (2 Wakorintho 12:10).

    Mkate Wetu wa Kila Siku, Mei 18, 1992.

    Utakatifu kwa Bwana

    Sio kwa Ufasaha wa Maneno

    Ukurasa wa 8

    • Yehova (Yahweh – Kiebrania) ni jina la kibinafsi la Mungu katika Maandiko. Mungu yule

    ambaye ana uhai wake wa kibinafsi, asiyebadilika, wa milele, muumbaji na Bwana wa yote.

    • Yesu ni jina lenye maana ya “Mwokozi.”

    • Imanueli ni jina lenye maana ya “Mungu pamoja nasi.”

    • Masihi nalo linatokana na Kiebrania na maana yake ni “kupakwa mafuta.”

    • Kristo ni neno la Kiyunani lenye maana ya “aliyepakwa mafua.” Jina hili lina

    maana moja na Masihi.

    • Alfa na Omega ni herufi za kwanza na za mwisho za alfabeti ya Kiyunani. Maana yake ni kumwakilisha Yesu

    kama “mwanzo na mwisho, maana yake ni wa kwanza na wa mwisho.”

    Je, Wajua?

    Neno Katika

    Majira Yake