nacopha swahili newsletter 005 final low res
TRANSCRIPT
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
WALK THE TALK TOLEO NO. 005 JUNI - SEPT 2020
Mwitikio wa NACOPHA dhidiya COVID 19Meneja wa kanda ya Dar es Salaam Victoriah Huburyaakigawa vifaa kinga dhidi ya COVID 19 kwa konga yaChamanzi, Mbagala Dar es SalaamUk 6-7
Ziara ya ukaguzi wa vikundiwezeshi mkoani Lindi na MtwaraWashiriki wa uchaguzi mkuu wa konga H/WilayaNachingwea katika picha ya pamoja Mara baada yauchaguzi mkuu uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauriya Nachingwea tar 9/06/2020. Uk 9
Mwenyekiti NACOPHA atembeleavikundi wezeshi
HEBU
TUFIKIE 95-95-95
Katika kipindi cha miaka mitano ijayo, NACOPHA itakuwa inatekeleza mradi mpyaunaofadhiliwa na USAID unaojulikana kwa jina la HEBU TUYAJENGE. HEBU TUYAJENGE ni maneno ya kiswahili yanayo maanisha mazungumzo kati yamakundi mbalimbali ya watu (marafiki, familia, watunga sera n.k) yakiwa na lengo lakufikia makubaliano au maamuzi yenye kuleta tija kuhusu jambo fulani. Katika mtazamowa mradi HEBU TUYAJENGE ni mazungumzo yanayohusu masuala ya UKIMWI Tanzaniakatika kufikia 95-95-95 mwaka 2030.
www.nacopha.or.tzNACOPHA Tanzania NACOPHA Tanzania nacophatz NACOPHA
3 ZE
ROS
Uk 6-7
Uk 6-8
Ushirikishwaji kamiliwa WAVIU
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
NYP+ wakutana na Waziri wa Nchi Ofisiya Waziri mkuu Mhe. Jenista Mhagama
Ziara ya viongozi wa NACOPHA ofisi yaWaziri Mkuu - Dodoma
Mwenyekiti wa NACOPHA Bi. Leticia Mourice alitembeleashughuli za kiuchumi za kikundi cha WAVIU cha Jitumemkoani Morogoro. Uk 4-5
HEBU
TUFI
KIE
95-9
5-95
KANDA YA DAR ES SALAAM
1. Ilala H/Manispaa
2. Temeke H/Manispaa
3. Masasi H/Wilaya
4. Masasi H/Mji
5. Mtwara H/Manispaa
6. Newala H/Wilaya
7. Newala H/Mji
8. Lindi H/Wilaya
9. Lindi H/Manispaa
10. Nachingwea H/Wilaya
11. Ruangwa H/Wilaya
12. Tanga H/Jiji
13. Moshi H/Wilaya
14. Moshi H/Manispaa
15. Chalinze H/Wilaya
KANDA YA MWANZA
1. Nyamagana H/Manispaa
2. Musoma H/Manispaa
3. Shinyanga H/Manispaa
4. Igunga H/Wilaya
5. Nzega H/Wilaya
6. Nzega H/Mji
7. Sikonge H/Wilaya
8. Tabora H/Manispaa
9. Urambo H/Wilaya
10. Uyui H/Wilaya
11. Bukoba H/Manispaa
12. Kigoma Ujiji H/Manispaa
KANDA YA DODOMA1. Bahi H/Wilaya2. Chemba H/Wilaya3. Dodoma H/Manispaa 4. Kondoa H/Wilaya5. Kondoa H/Mji 6. Kongwa H/Wilaya7. Gairo H/Wilaya8. Ifakara H/Mji9. Kilombero H/Wilaya10. Kilosa H/Wilaya11. Malinyi H/Wilaya12. Morogoro H/Manispaa13. Ulanga H/Wilaya14. Ikungi H/Wilaya15. Iramba H/Wilaya16. Manyoni H/Wilaya17. Mkalama H/Wilaya18. Singida H/Wilaya19. Babati H/Mji 20. Simanjiro H/Wilaya21. Arusha H/Jiji22. Arusha H/Wilaya23. Ngorongoro H/Wilaya
Konga za utekelezaji
KANDA YA MBEYA
1. Mbeya H/jiji
2. Rungwe H/Wilaya
3. Ludewa H/Wilaya
4. Makambako H/mji
5. Makete H/Wilaya
6. Njombe H/Wilaya
7. Njombe H/Mji
8. Wanging'ombe H/Wilaya
9. Iringa H/Wilaya
10. Iringa H/Manispaa
11. Kilolo H/Wilaya
12. Mafinga H/Mji
13. Mufindi H/Wilaya
14. Sumbawanga H/Manispaa
15. Songea H/Manispaa
KAGERAMARA
ARUSHA
SINGIDADODOMA
MANYARA
TANGA
KILIMANJARO
PWANI
DAR ES SALAAM
LINDI
MTWARA
RUVUMA
IRINGAMOROGORO
MBEYARUKWA
MWANZASIMIYU
GEITA
SONGWE
KATAVI
SHINYANGA
TABORA
KIGOMA
Shinyanga MC
Kigoma Ujiji MC
Nzega DC
Nzega TC
Igunga DC
Uyui DCUrambo DC
Tabora MC
Sikonge DC
Chemba DC
Kondoa TC
Dodoma MCKongwa DC
Kilosa DC
Ifakara TC
Kilombero DC
Morogoro MC
Gairo DC
Ulanga DC
Malinyi DC
Manyoni DC
Ikungi DC
Iramba DC
MkalamaDC
Singida DC
Babati TC
Ngorongoro DC
Arusha CC
Arusha DC
Simanjiro DC
Rungwe DC
Ludewa
Makambako
Iringa MC
Njombe TC
Kilolo DC
Mbeya CC Sumbawanga MC
Wanging'ombe DC
Songea MC
Mufindi DC
Mafinga TC
Makete DC
Masasi DC
Mtwara MC
Newala
Lindi DC
Lindi MC
Masasi TC
Nachingwea
Ruangwa DC
Tanga CC
Moshi DC
Moshi MC
Chalinze DC
Temeke MCIlala MC
Njombe DC
Bahi DC
KENYA
UGANDA
MOZAMBIQUE
MALAWI
ZAMBIA
NJOM
BE
Bukoba MCMusoma MC
Nyamagana MC
Mradi wa Hebu Tuyajenge – Konga za utekelezaji
Mikoa ambayo haifikiwi na mradi
Ufunguo:
ENEO LA UTEKELEZAJI WA MRADI WA HEBU TUYAJENGE
Konga za utekelezaji Halmashauri 65 zilizopo katika mikoa 22 ya Tanzania bara
DISEMBA 10, 2019 – DISEMBA 9, 2024
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Mwenyekiti NACOPHA atembeleashughuli za kiuchumi za WAVIUmkoani Morogoro na Arusha
Katika toleo hili
Bodi ya wahariri
Uk.
2 - 3
Mafunzo ya Wakiri tiba
4 - 5
6 - 7Unyanyapaa ni kikwazo kufikia95-95-95
8
Ziara ya ukaguzi wa vikundiwezeshi mkoani Lindi
9
10
12 - 13
Simulizi za mafanikio 14 - 15
NYP+ wakutana na Mhe. JenisterMhagama Waziri wa Nchi Ofisi yaWaziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira,Kazi na wenye Ulemavu
11
Lulu Kansary | Pantaleon ShokiRose Olotu | Last Mlaki
Msanifu ubunifuRobert Salala
MwandishiGrace Mollel
MshauriDeogratius Rutatwa
1
3 ZE
ROS
Bi. Leticia Mourice
Deogratius Rutatwa
Ujumbe kutoka kwaMwenyekiti wa Barazala watu wanaoishi naVirusi vya UKIMWITanzania (NACOPHA)
Ujumbe kutokakwa MkurugenziMkuu Mtendaji
Baraza la Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI Tanzania (NACOPHA) tunaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara yaAfya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa juhudi na mikakati mbalimbali dhidi ya mwitikio wa UKIMWI nchini. Tumekuwa tukishirikiana na Wizara ya Afya katika kuhakikisha huduma ya VVU na UKIMWI inawafikia wananchi kuanzia ngazi ya jamii sambamba na utolewaji wa elimu ya UKIMWI ili kuwa na Taifa imara. Pia tunaishukuru Serikali ya Watu wa Marekani kupitia Shirika la Maendeleo la Watu wa Marekani (USAID) kwa kuendelea kutufadhili kupitia mradi HEBU TUYAJENGE (HT) katika kufikia malengo ya kitaifa na kimataifa ya 95 95 95 ifikapo 2030.
HT ni moja ya miradi tunayoitekeleza ikiwa moja ya malengo ni kulifikia kundi la wasichana balehe, wanawake wa umri wa kati pamoja na WAVIU ambao kiujumla ndio wamekuwa walengwa wakuu ambapo tukiangalia takwimu za Wizara ya Afya za mwaka 2016/2017 zinaonyesha maambukizi mapya ni vijana wa kati ya miaka 15 -24 ambapo ni 40% (wanawake 80% na wanaume 20%). Tuna imani kupitia mradi wa HT tutachangia kuzifikia 95-95-95 ili vijana wetu na jamii kwa ujumla waweze kufikia ndoto zao na kutengeneza kizazi salama.
HEBU TUYAJENGE ni moja ya miradi inayote-kelezwa na NACOPHA kwa kipindi cha miaka mitano kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Watu wa Marekani USAID. Mradi huu unalenga kufikia malengo ya juhudi za kitaifa ya 95 95 95 na utatekelezwa kwenye kata 325 katika Halmashauri 65 Tanzania bara, utahamasisha katika kuongeza huduma za upimaji, tiba na matunzo, uzazi wa mpango, pamoja na utetezi na uraghibishi kwa watu wanaoishi na VVU.
Kimsingi, mradi huu unafanywa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za mitaa, Kamati za Bunge, Wizara ya Fedha, Mamlaka ya serikali za mitaa, Tume ya Taifa ya kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) pamoja na kamati za uangalizi wa konga za WAVIU, mashirika mbalimbali yanayotekeleza afua za UKIMWI kama vile, FHI 360, AGPAHI, BMF, PACT Tanzania, JSI, JHPIEGO na EGPAF.
Mradi huu unatekelezwa katika mikoa 22 ambayo ni Dar es salaam, Mtwara,Tanga, Lindi, Kilimanjaro, Pwani, Dodoma, Morogoro, Singida, Manyara, Arusha, Shinyanga, Mwanza, Mara, Kagera, Tabora, Kigoma, Mbeya, Njombe, Iringa, Rukwa na Ruvuma.
Napenda kuwakumbusha kwamba, tunapaswa kuendelea kujikinga na ugonjwa wa COVID-19 kwa kufuata elimu na miongozo inayotolewa na Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ili tuweze kuendelea kuchapa kazi na kukuza uchumi wa nchi yetu.
Barabara ya Whitesand 86, Mtaa wa Keni Close/Kilongawima,Nyumba Na KUN/KIL/83. SLP 55811, Dar es Salaam, Tanzania.Simu: +255 22 2618518, Barua Pepe: [email protected]: nacopha.or.tz
Mwitikio wa NACOPHA dhidi yaCOVID-19
Serikali mkoani Tabora yaviwezeshavikundi vya WAVIU
Ziara ya viongozi wa NACOPHAOfisi ya Waziri Mkuu - Dodoma
2
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Kwa kuitikia wito wa kuonana na Mhe. Waziri Mkuu Mtandao wa Vijana
Wanaoishi na Maambukizi ya virusi vya UKIMWI (NYP+) kupitia Baraza la
Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (NACOPHA) walipata fursa ya
kuonana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira na
watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Joackim Mhagama na kuwasilisha
maombi yao katika Ofisi ya Waziri Mkuu Mkoani Dodoma.
Nafasi hiyo waliipata Katika mkutano wa maazimio ya viongozi wa dini
katika kuondoa unyanyapaa na ubaguzi dhidi ya Watu wanaoishi na virusi
vya UKIMWI ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu Mhe. Kassimu
Majaliwa na ulihudhuriwa na NACOPHA, Mhe. Job Dungai Spika wa Bunge,
Wabunge, Viongozi wa Kitaifa wa dini na wadau mbalimbali.
Vijana walipata nafasi ya kuwasilisha maombi yao kwa Mh. Mhagama
kupitia kwa Mwenyekiti wao Pundensia Bwiliza ambapo aliwasilisha
maombi matatu. Moja ya Maombi hayo ni kuhusu mpango endelevu wa
uwezeshwaji kiuchumi, kiujuzi (stadi) na kiuzalishaji mali kwa Vijana
wanaoishi na VVU, kujadili uwezekano wa suala la UKIMWI kupewa nguvu
ya kipaumbele cha upekee ili iwe ni agenda inayojitegemea katika mipango
ya maendeleo ya nchi yetu tunapoelekea 2025 na 2030 ili kuutokomeza
mapema UKIMWI.
Pia waliwasilisha ombi la kumuomba Waziri Mkuu awe mlezi wa Vijana kwa
Ofisi ya Waziri Mkuu, Dodoma
kutambua heshima na mafanikio aliyonayo Kitaifa ya kuwa ni Balozi wa
kampeni ya “Furaha Yangu” inayohamasisha wanaume kupima VVU.
Mheshimiwa Mhagama alipokea maombi ya vijana hao na aliahidi kuyafanyia
kazi yale yaliyo ndani ya uwezo wake na mengine kuyawasilisha kwa
Waziri Mkuu.” Naomba niwahakikishie sitawaangusha yatakuwa kati ya
mambo muhimu ya kupewa kipaumbele na nitayafanyia kazi nawaahidi”
Mhe. Muhagama alinukuliwa akisema “Maombi yenu mengine ambayo
mmeyaomba yako kisera na mmeomba sehemu sahihi maana hii ndio ofisi
inayoratibu masuala yote ya UKIMWI, na leo sikujua tu ilikua ni siku muhimu
ambapo tulikua na uzinduzi wa mfuko ambao unawezesha vijana wa aina
zote ila kwa kuwa tuko pamoja tutaangalia ni jinsi gani tutazitatua
changamoto za vijana kwa kuwajengea uwezo kiuchumi”.
Kutokana na changamoto wanazozipitia vijana WAVIU suala hili kuna haja
ya kulitazama kwa jicho la kipekee, “mimi ndiye nashughulikia Sera na
Uwezeshaji Kiuchumi, na pia ndiye Waziri anayeshughulikia mifuko yote ya
uwezeshaji upande wa Elimu, Ajira na Uwezeshaji. Naomba kuwahakikishia
kuwa suala la uwezeshwaji liko ndani ya uwezo wangu”.
Katika programu aliyozindua Mhe. Waziri ambayo aliyepewa jukumu la
kuratibu na kusimamia ni SIDO na VETA , aliomba watu wote hasa vijana
kuitumia fursa hii kwa kuzingatia masharti yaliyopo ili kupata mkopo. Aidha
aliwapongeza vijana kwa moyo wa ushupavu na jitihada walizonazo kwani
wao ni mfano wa kuigwa katika jamii zetu. Alizidi kuwatia moyo kutokata
tamaa kwani Serikali iko bega kwa bega na inatambua uwepo wao.
NYP+ wakutana na Waziri wa Nchi Ofisi yaWaziri Mkuu Mhe. Jenista Mhagama
Mhe. Mhagama alisema, imefika wakati tujue sisi hatuishi kisiwani na hii
inapelekea tufanye kazi kwa kushirikiana na wadau wote wanaotekeleza
Afua za UKIMWI ili kuleta matokeo chanya.
Kwa mujibu wa takwimu za Kitaifa za viashiria vya UKIMWI 2016/2017,
asilimia 40% ya maambukizi mapya ya VVU nchini Tanzania yako kwa
vijana, asilimia 80% ya maambukizi haya yako kwa vijana wa kike. Mhe.
Mhagama alisema” Tumejiunga na harakati za kidunia, kikanda katika
kupambana na kuangalia ustawi wa suala hili kwa undani na tuna chombo
makini katika kuyatekeleza haya kupitia Tume ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi
TACAIDS na tume hii kwakweli imefanya kazi nzuri na imesaidia kwa kiasi
kikubwa kupambana na ugonjwa huu na kuwaondolea watu hofu.”
Mhe. Jenister Mhagama, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi na wenye Ulemavu akifungua mkutano na baadhi ya wawakilishi wa Jukwaa la vijana wanaoishi na VVU Tanzania
Picha ya Pamoja; waliokaa Mhe. Jenista Mhagama, Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuuu Sera, Bunge, Ajira Kazi na wenye ulemavu wa tatu kutoka kulia akiwa katika picha ya Pamoja na Mkurugenzi mtendaji wa TACAIDS Dk. Leornard Maboko wa tatu kutoka kushoto, Mwenyekiti wa NACOPHA Bi. Leticia Mourice wakwanza kulia, Mkurugenzi Mtendaji wa NACOPHA Deogratius Rutatwa wa kwanza kushoto na Mwenyekiti wa
Jukwaa la Vijana wanaoishi na VVU Pudensiana Bwiliza. Waliosimama ni baadhi ya wawakilishi wa jukwaa la vijana wanaoishi na VVU kutoka mikoa mbalimbali Tanzania.
3
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Kwa kuitikia wito wa kuonana na Mhe. Waziri Mkuu Mtandao wa Vijana
Wanaoishi na Maambukizi ya virusi vya UKIMWI (NYP+) kupitia Baraza la
Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (NACOPHA) walipata fursa ya
kuonana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira na
watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Joackim Mhagama na kuwasilisha
maombi yao katika Ofisi ya Waziri Mkuu Mkoani Dodoma.
Nafasi hiyo waliipata Katika mkutano wa maazimio ya viongozi wa dini
katika kuondoa unyanyapaa na ubaguzi dhidi ya Watu wanaoishi na virusi
vya UKIMWI ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu Mhe. Kassimu
Majaliwa na ulihudhuriwa na NACOPHA, Mhe. Job Dungai Spika wa Bunge,
Wabunge, Viongozi wa Kitaifa wa dini na wadau mbalimbali.
Vijana walipata nafasi ya kuwasilisha maombi yao kwa Mh. Mhagama
kupitia kwa Mwenyekiti wao Pundensia Bwiliza ambapo aliwasilisha
maombi matatu. Moja ya Maombi hayo ni kuhusu mpango endelevu wa
uwezeshwaji kiuchumi, kiujuzi (stadi) na kiuzalishaji mali kwa Vijana
wanaoishi na VVU, kujadili uwezekano wa suala la UKIMWI kupewa nguvu
ya kipaumbele cha upekee ili iwe ni agenda inayojitegemea katika mipango
ya maendeleo ya nchi yetu tunapoelekea 2025 na 2030 ili kuutokomeza
mapema UKIMWI.
Pia waliwasilisha ombi la kumuomba Waziri Mkuu awe mlezi wa Vijana kwa
kutambua heshima na mafanikio aliyonayo Kitaifa ya kuwa ni Balozi wa
kampeni ya “Furaha Yangu” inayohamasisha wanaume kupima VVU.
Mheshimiwa Mhagama alipokea maombi ya vijana hao na aliahidi kuyafanyia
kazi yale yaliyo ndani ya uwezo wake na mengine kuyawasilisha kwa
Waziri Mkuu.” Naomba niwahakikishie sitawaangusha yatakuwa kati ya
mambo muhimu ya kupewa kipaumbele na nitayafanyia kazi nawaahidi”
Mhe. Muhagama alinukuliwa akisema “Maombi yenu mengine ambayo
mmeyaomba yako kisera na mmeomba sehemu sahihi maana hii ndio ofisi
inayoratibu masuala yote ya UKIMWI, na leo sikujua tu ilikua ni siku muhimu
ambapo tulikua na uzinduzi wa mfuko ambao unawezesha vijana wa aina
zote ila kwa kuwa tuko pamoja tutaangalia ni jinsi gani tutazitatua
changamoto za vijana kwa kuwajengea uwezo kiuchumi”.
Kutokana na changamoto wanazozipitia vijana WAVIU suala hili kuna haja
ya kulitazama kwa jicho la kipekee, “mimi ndiye nashughulikia Sera na
Uwezeshaji Kiuchumi, na pia ndiye Waziri anayeshughulikia mifuko yote ya
uwezeshaji upande wa Elimu, Ajira na Uwezeshaji. Naomba kuwahakikishia
kuwa suala la uwezeshwaji liko ndani ya uwezo wangu”.
Katika programu aliyozindua Mhe. Waziri ambayo aliyepewa jukumu la
kuratibu na kusimamia ni SIDO na VETA , aliomba watu wote hasa vijana
kuitumia fursa hii kwa kuzingatia masharti yaliyopo ili kupata mkopo. Aidha
aliwapongeza vijana kwa moyo wa ushupavu na jitihada walizonazo kwani
wao ni mfano wa kuigwa katika jamii zetu. Alizidi kuwatia moyo kutokata
tamaa kwani Serikali iko bega kwa bega na inatambua uwepo wao.
Picha ya pamoja kutoka kulia Mwenyekiti wa NACOPHA Bi Leticia Mourice, Mkurugenzi wa TACAIDS Dk. Leonard Maboko, Pudensia Bwiliza, Mwenyekiti wa Mtandao wa vijana wanaoishi
na Virusi vya UKIMWI na Afisa Mtendaji Mkuu wa NACOPHA Bw. Deogratius Rutatwa.
Mhe. Mhagama alisema, imefika wakati tujue sisi hatuishi kisiwani na hii
inapelekea tufanye kazi kwa kushirikiana na wadau wote wanaotekeleza
Afua za UKIMWI ili kuleta matokeo chanya.
Kwa mujibu wa takwimu za Kitaifa za viashiria vya UKIMWI 2016/2017,
asilimia 40% ya maambukizi mapya ya VVU nchini Tanzania yako kwa
vijana, asilimia 80% ya maambukizi haya yako kwa vijana wa kike. Mhe.
Mhagama alisema” Tumejiunga na harakati za kidunia, kikanda katika
kupambana na kuangalia ustawi wa suala hili kwa undani na tuna chombo
makini katika kuyatekeleza haya kupitia Tume ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi
TACAIDS na tume hii kwakweli imefanya kazi nzuri na imesaidia kwa kiasi
kikubwa kupambana na ugonjwa huu na kuwaondolea watu hofu.”
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi na wenye Ulemavu Mhe. Jenister Mhagama, akifurahia jambo na washiriki wa mkutano wa mtandao wa vijana wanaoishina Virusi vya UKIMWI wakati wa mkutano uliofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dodoma
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
4
Mwenyekiti wa Baraza la watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI Tanzania
(NACOPHA), Bi Leticia Mourice alifanya ziara ya kutembelea vikundi wezeshi
vya watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU) Ikiwa ni ziara maalum ya
kuratibu na ufuatiliaji wa maendeleo ya vikundi hivyo, ziara hiyo ilifanyika
mwaka huu 2020 katika mkoa wa Morogoro.
Aidha katika ziara hiyo mkoani Morogoro aliweza kutembelea Konga ya
Morogoro MC, Kilombero DC na Gairo DC ambapo katika ziara hiyo aliambata-
na na viongozi kutoka Halmashauri za Serikali CHAC/DAC ambapo alifanikiwa
kuona shughuli mbali mbali zinazofanywa na vikundi hivyo pamoja na
changamoto wanazokabiliana nazo katika shughuli zao.
Wanavikundi hao wameweza kuanzisha miradi mbalimbali ya ujasiriamali ili
kujikimu kiuchumi na kuendesha maisha yao. Hii ni hatua mojawapo kubwa
kwa WAVIU kwani hapo mwanzo vikundi hivi vilitambulika kama vikundi vya
misaada na sasa hivi vinatambulika kama vikundi wezeshi.Wanavikundi
wamekuwa wakijiendesha wenyewe kupitia viongozi wao wa Konga ambapo
katika ziara hiyo Mwenyekiti wa Konga ya manispaa ya Morogoro Kareen
Mpesa aliwasilisha ripoti kwa Mwenyekiti wa Baraza Bi Leticia Mourice
ambapo alishukuru kwa motisha ya kazi wanayoipata na mchango wao
kutambulika kwa Serikali kupitia ngazi ya Halmashauri kwani wamekuwa
wakifanya kazi karibu na CHAC/DACC. Aidha alishukuru kwa Mwenyekiti wa
Baraza kuwatembelea na kuwatia moyo katika shughuli zao.
Katika Konga ya manispaa ya Mororogo kuna Vikundi wezeshi 20
ambapo katika vikundi hiyo jumla ya wanachama ni 591 (291
wanawake na 300 wanaume). Vikundi hivyo vimekuwa vikijishughulisha
na kuuza batiki na vito vya asili kama shanga. Mwenyekiti wa Konga ya
manispaa ya Morogoro alisema wameweza kuendesha maisha yao
kupitia vikundi wezeshi na kuweza kuzingatia suala zima la utumiaji wa
dawa, kufuatilia/kupima kinga za mwili, uhamasishaji na kurudisha
walioacha kutumia dawa. Aidha alizungumzia suala zima la Ugonjwa wa
COVID-19 ambalo ni hatari kwa WAVIU na kusisitiza kufuata kanuni na
taratibu za Wizara husika ili kujikinga.
Katika Konga ya halmashauri ya wilaya ya Kilombero kuna vikundi
wezeshi 42 ambavyo vinaongozwa na viongozi wa konga. Mwenyekiti
wa Konga Bi Halida Kumba alielezea kwa undani jinsi vikundi vinavyo-
endesha shughuli zao na changamoto wanazokabiliana nazo. Shughuli
kubwa wanazojishughulisha nazo ni kilimo na ufugaji ambavyo vimeku-
wa vikiwasaidia kuendesha maisha yao ya kila siku aidha alisema
changamoto kubwa wanayokutana nayo ni katika suala zima la uchuku-
aji wa dawa na ufuatiliaji. Alibainisha ya kuwa kipindi cha mavuno eneo
hilo limekuwa likipata wageni wengi na kusababisha huduma za Afya
kuzorota. Alizungumzia pia suala la wanaume kutojiunga na vikundi
wezeshi kutokana na suala zima la kujinyanyapaa.
Katika Konga ya Gairo kuna kata 18 na vikundi wezeshi 20. Mwenyekiti
wa Konga Abeli Bigambo alimshukuru Mwenyekiti wa Baraza la Watu
Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (NACOPHA) kwakuwa sehemu ya ufuatiliaji
katika vikundi wezeshi vya Gairo. Aidha alizungumzia suala la unyanyapaa
ambalo wameweza kukabiliana nalo ambapo alibainisha kikwazo
kikubwa kimekuwa ni ushirikina ambao umekuwa ukikwamisha
shughuli za maendeleo katika eneo hilo.
Aidha katika ziara hiyo alifanikiwa kutembelea Kikundi cha CHICHI
ambacho kipo katika kata ya Chamwino mkoani Dodoma ambapo jina la
kikundi CHICHI lina maana kwa lugha ya kigogo “Chipimile chimanyile”
ambayo kwa lugha ya Kiswahili ina maana NIMEPIMA NA NINAJUA AFYA
YANGU. Kikundi hiki ni kati ya vikundi vinavyofanya vizuri katika Konga ya
halmashauri ya wilaya ya Dodoma.
Kikundi hicho wameweza kujiendesha chenyewe na kuweza kujipatia
mahitaji muhimu ya kila siku ikiwa ni pamoja na suala zima la ufatiliaji wa
afya zao. Katika ziara hiyo Mwenyekiti aliwasihi kuacha dhana ya
kujinyanyapaa na badala yake kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo
ya 95 95 95
Mwenyekiti wa NACOPHA atembeleashughuli za kiuchumi za WAVIUMorogoro na Arusha
Timu ya usimamizi wakijadili namna bora ya uendeshaji vikundi wezeshi wakati wa ziara ya mwenyekiti waNACOPHA alipotembelea vikundi wezeshi mkoani Morogoro
Mwenyekiti wa NACOPHA akiangalia bidhaa za batiki zilizotengenezwa na kikundi chaJitambue cha H/Manispaa Morogoro
5
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Mwenyekiti wa Baraza la watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI Tanzania
(NACOPHA), Bi Leticia Mourice alifanya ziara ya kutembelea vikundi wezeshi
vya watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU) Ikiwa ni ziara maalum ya
kuratibu na ufuatiliaji wa maendeleo ya vikundi hivyo, ziara hiyo ilifanyika
mwaka huu 2020 katika mkoa wa Morogoro.
Aidha katika ziara hiyo mkoani Morogoro aliweza kutembelea Konga ya
Morogoro MC, Kilombero DC na Gairo DC ambapo katika ziara hiyo aliambata-
na na viongozi kutoka Halmashauri za Serikali CHAC/DAC ambapo alifanikiwa
kuona shughuli mbali mbali zinazofanywa na vikundi hivyo pamoja na
changamoto wanazokabiliana nazo katika shughuli zao.
Wanavikundi hao wameweza kuanzisha miradi mbalimbali ya ujasiriamali ili
kujikimu kiuchumi na kuendesha maisha yao. Hii ni hatua mojawapo kubwa
kwa WAVIU kwani hapo mwanzo vikundi hivi vilitambulika kama vikundi vya
misaada na sasa hivi vinatambulika kama vikundi wezeshi.Wanavikundi
wamekuwa wakijiendesha wenyewe kupitia viongozi wao wa Konga ambapo
katika ziara hiyo Mwenyekiti wa Konga ya manispaa ya Morogoro Kareen
Mpesa aliwasilisha ripoti kwa Mwenyekiti wa Baraza Bi Leticia Mourice
ambapo alishukuru kwa motisha ya kazi wanayoipata na mchango wao
kutambulika kwa Serikali kupitia ngazi ya Halmashauri kwani wamekuwa
wakifanya kazi karibu na CHAC/DACC. Aidha alishukuru kwa Mwenyekiti wa
Baraza kuwatembelea na kuwatia moyo katika shughuli zao.
Katika Konga ya manispaa ya Mororogo kuna Vikundi wezeshi 20
ambapo katika vikundi hiyo jumla ya wanachama ni 591 (291
wanawake na 300 wanaume). Vikundi hivyo vimekuwa vikijishughulisha
na kuuza batiki na vito vya asili kama shanga. Mwenyekiti wa Konga ya
manispaa ya Morogoro alisema wameweza kuendesha maisha yao
kupitia vikundi wezeshi na kuweza kuzingatia suala zima la utumiaji wa
dawa, kufuatilia/kupima kinga za mwili, uhamasishaji na kurudisha
walioacha kutumia dawa. Aidha alizungumzia suala zima la Ugonjwa wa
COVID-19 ambalo ni hatari kwa WAVIU na kusisitiza kufuata kanuni na
taratibu za Wizara husika ili kujikinga.
Katika Konga ya halmashauri ya wilaya ya Kilombero kuna vikundi
wezeshi 42 ambavyo vinaongozwa na viongozi wa konga. Mwenyekiti
wa Konga Bi Halida Kumba alielezea kwa undani jinsi vikundi vinavyo-
endesha shughuli zao na changamoto wanazokabiliana nazo. Shughuli
kubwa wanazojishughulisha nazo ni kilimo na ufugaji ambavyo vimeku-
wa vikiwasaidia kuendesha maisha yao ya kila siku aidha alisema
changamoto kubwa wanayokutana nayo ni katika suala zima la uchuku-
aji wa dawa na ufuatiliaji. Alibainisha ya kuwa kipindi cha mavuno eneo
hilo limekuwa likipata wageni wengi na kusababisha huduma za Afya
kuzorota. Alizungumzia pia suala la wanaume kutojiunga na vikundi
wezeshi kutokana na suala zima la kujinyanyapaa.
Katika Konga ya Gairo kuna kata 18 na vikundi wezeshi 20. Mwenyekiti
wa Konga Abeli Bigambo alimshukuru Mwenyekiti wa Baraza la Watu
Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (NACOPHA) kwakuwa sehemu ya ufuatiliaji
katika vikundi wezeshi vya Gairo. Aidha alizungumzia suala la unyanyapaa
ambalo wameweza kukabiliana nalo ambapo alibainisha kikwazo
kikubwa kimekuwa ni ushirikina ambao umekuwa ukikwamisha
shughuli za maendeleo katika eneo hilo.
Aidha katika ziara hiyo alifanikiwa kutembelea Kikundi cha CHICHI
ambacho kipo katika kata ya Chamwino mkoani Dodoma ambapo jina la
kikundi CHICHI lina maana kwa lugha ya kigogo “Chipimile chimanyile”
ambayo kwa lugha ya Kiswahili ina maana NIMEPIMA NA NINAJUA AFYA
YANGU. Kikundi hiki ni kati ya vikundi vinavyofanya vizuri katika Konga ya
halmashauri ya wilaya ya Dodoma.
Kikundi hicho wameweza kujiendesha chenyewe na kuweza kujipatia
mahitaji muhimu ya kila siku ikiwa ni pamoja na suala zima la ufatiliaji wa
afya zao. Katika ziara hiyo Mwenyekiti aliwasihi kuacha dhana ya
kujinyanyapaa na badala yake kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo
ya 95 95 95
Mwenyekiti wa NACOPHA Bi. Leticia Mourice akifurahia na kupongeza shughuli za kilimo cha mpungazinazofanywa na kikundi cha WAVIU cha Jitume kilichopo kata ya Malimba mkoani Morogoro alipotembelea
kujionea shughuli mbalimbali za kiuchumi zinazofanywa na WAVIU
Mwenyekiti wa Baraza la watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI NACOPHA Bi. Leticia Mourice alifanikiwa kutembelea Kikundi cha wanaume Wanaoishi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI (KIWAWARU) kilichopo Halmashauri ya wilaya ya Arusha, mkoani Arusha lengo likiwa kuwawezesha wanakikundi pamoja na kuwahamasisha wanaume kujiunga na huduma za UKIMWI.
Katika ziara hiyo ambayo ilikuwa na jumla ya wanachama 40, ilihudhuriwa na viongozi wa Serikali Mratibu wa Ukimwi wa Halmashauri (CHAC) na Afisa Mtendaji wa Kata (WEO). Mwenyekiti wa Konga Bw.Francis Temu alielezea changamoto na mafanikio ya kikundi akisema jumla ya wanaume wanachama ilikuwa 165 ambao waliacha mahudhurio ila tuliwarudisha kupitia ushauri nasaha na huduma za kiafya. Pia tuliweza kuwahamasisha na kuwaunganisha vijana na huduma za upimaji na waliobainika wana maambukizi kuanza huduma stahiki za tiba na dawa.
Mwenyekiti atembelea kikundi chawanaume WAVIU - KIWAWARU, Arusha
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
6
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Meneja wa Kanda ya Dar es Salaam Victoriah Huburya akigawa vifaa kinga dhidi yaCOVID 19 kwenye Konga ya WAVIU Chamanzi Mbagala
Dk. Martha Macha - DACC Temeke na Heriet Kamara - CHACC Temeke wakikabidhi vifaa kinga dhidi ya COVID 19 kwa mwenyekiti wa Konga ya Chamanzi , Mbagala, Dar es Salaam
COVID-19 iliripotiwa kwa mara ya kwanza Tanzania Machi 17 mwaka
huu 2020 na Aprili 9 iliripotiwa wagonjwa 12, ambapo Serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ilichukua hatua za haraka ikiwa ni pamoja na
kufunga shule zote kuanzia ngazi ya chini mpaka vyuo vikuu. Ugonjwa
huu ni wa kuambukiza unaosababishwa na virusi vya Corona. Virusi vya
corona havikuwa vikifahamika kabla ya sayansi ya tiba, na vilianzia
Wuhan, Hubei China January 2020 ambapo Shirika la Afya DunianI
(WHO) lilithibitisha kuwepo kwa ugonjwa huo.
Dalili kubwa za COVID-19 ni pamoja na homa kali, mwili kuchoka,
kikohozi, kubanwa mbavu, kupumua kwa shida, vidonda kooni na
kuumwa kichwa. Kutokana na tafiti za Shirika la Afya Duniani (WHO)
linadai watu wenye athari kubwa zaidi ya kupata maambukizi ni wazee
na watu wenye magonjwa ya kudumu kama shinikizo la damu, Figo,
kisukari pamoja na watu wanaoishi na VVU ambao kwa takwimu za
Tanzania kwa mwaka 2019 idadi ya WAVIU imefikia milioni 1.6.
Serikali kupitia Wizara husika, katika kudhibiti maambukizi ilianzisha
utaratibu maalum kwa WAVIU katika suala zima la uchukuaji wa dawa
pamoja na huduma nyingine za afya. Baadhi ya taratibu hizo ni pamoja
na utolewaji wa dawa za muda mrefu ambapo vituo vya kutolea dawa
(CTC) walihakikisha wanakuwa na mawasiliano na mpokea huduma ili
kama ikitokea tatizo kabla ya tarehe ya kurudi kuna utaratibu wa kufuat-
wa, kuhudumiwa kwa kufuata taratibu zilizowekwa na wizara husika
ikiwa ni pamoja na kuepuka msongamano wakati wa kusubiri huduma,
kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni, kutumia vitakasa mikono
mara kwa mara pamoja na uvaaji wa barakoa zenye viwango
vilivyodhibitiwa. Hata hivyo mpaka sasa ugonjwa huu hauna chanjo wala
tiba ya moja kwa moja, hivyo kama yalivyo magonjwa mengine yanayos-
ababishwa na virusi, matibabu hufanyika kwa kuzingatia dalili zilizopo na
ufuatiliaji wa karibu.
NACOPHA kupitia mradi wa HEBU TUYAJENGE unaofadhiliwa na Shirika la
Maendeleo la watu wa Marekani USAID limekuwa bega kwa bega katika
kuunga mkono jitihada za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mwitikio wa NACOPHA dhidiya COVID-19
7
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Baadhi ya washiriki kutoka konga ya Temeke jijini Dar es Salaam wakionyesha vifaa kinga walivyopokea dhidi ya COVID -19
katika kupambana na ugonjwa wa COVID 19 ikiwa ni pamoja na kutoa
vifaa kinga pamoja na elimu ya kujikinga katika mabaraza ya watu
wanaoishi na virusi vya UKIMWI ngazi ya jamii.
Utaratibu wa utoaji wa vifaa kinga pamoja na elimu ya kujikinga dhidi ya
COVID 19 ulitolewa kwa kufuata kanuni na taratibu zilizowekwa na
Wizara husika ili kuhakikisha zinawafikia walengwa, ambapo nia na
madhumuni ni kufikia Halmashauri 65 zilizoko katika mikoa 22 nchi
nzima kwenye ngazi ya jamii. Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na barakoa,
sabuni, ndoo, vitakasa mikono pamoja na elimu ya jinsi ya kutumia vifaa
hivi ili kukabiliana na ugonjwa wa COVID-19.
Kanda ya Dar es salaam ugawaji wa vifaa kinga dhidi ya COVID-19
ulifanyika katika Konga ya Ilala na Temeke ambapo zaidi ya WAVIU 900
tuliwafikia. Katika Konga ya Ilala jumla ya vikundi vilivyopokea 44 mbele
ya Mratibu msaidizi wa kudhibiti UKIMWI kutoka Manispaa ya Ilala Bi.
Anna Kagya na Mwenyekiti wa Konga ya Ilala Bw. Emanuel Msinga
pamoja na Katibu wa Konga Zawadi Bahenge ambao waliongoza zoezi
zima la ugawaji wa vifaa hivyo kwa kuhakikisha kila MVIU anapata na
kupatiwa elimu ya jinsi ya kujikinga, ambapo afisa ufuatialiaji na tathmini
wa NACOPHA Bi. Victoria Huburya pamoja na Meneja wa Kanda ya Dar
es saam Bw. Maligo Raphaeli wakiwa mstari wa mbele kuhakikisha
zoezi linaenda kama lilivyopangwa.
Katika Konga ya Temeke jumla ya vikundi vilivyopokea ni vikundi 8
ambapo zoezi hilo liliendeshwa mbele ya Mratibu wa UKIMWI wa
Halmashauri ya wilaya ya Temeke Bi, Martha Macha pamoja na mratibu
msaidizi upande wa jamii Bi.Herieth Kamara wa Manispaa ya Temeke.
Aidha Kanda ya Mwanza sehemu tulizoweza kuzifikia ni kata 60,
Halmashauri 12 ambapo ni katika mikoa ya Mwanza, Mara, Shinyanga,
Kagera,Tabora na Kigoma, ambapo tulipata ushirikiano kutoka kwa
Viongozi wa Serikali akiwema Mkuu wa mkoa wa Kigoma Bw. Samson
Anga, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw. Aggrey Mwanri pamoja na viongozi
kutoka manispaa na viongozi wa Konga.
Mwenyekiti wa Baraza la watu Wanaoishi na virusi vya UKIMWI Bi. Leticia Mourice amezungumzia suala la unyanyapaa kama kikwazo kwa watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI (WAVIU) katika malengo ya kitaifa na kimataifa kufikia 95 95 95. Aliyasema hayo Mwezi Juni Mwaka huu 2020, katika mjadala na waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi za NACOPHA jijini Dar es salaam.
Unyanyapaa unaohusishwa na Virusi ya UKIMWI unaweza kuelezewa kama ni mchakato wa kupunguza thamani ya mtu anayeishi na virusi vya UKIMWI, takwimu za mwaka 2012 zinaonyesha ya kuwa kiwango cha unyanyapaa nchini ni kwa asilimia 49.7 ambapo katika utafiti huo ulionyesha unyanyapaa umeathiri kwa kiwango kikubwa kwa watu kupata huduma za upimaji, tiba na matunzo na hata kubaki kwenye tiba kwa usahihi, katika jitihada za kupinga unyanyapaa kila mwezi Machi 01, kila mwaka jamiiinaazimisha siku hiyo.
Aidha katika mjadala huo Bi. Leticia alizungumzia suala la unyanyapaa kama kikwazo na tatizo kubwa kwa Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU) ambapo aliomba jamii kuondokana na dhana potofu ya unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na VVU. Alielezea unyanyapaa uliopo katika jamii yetu ni wa aina mbili, aina ya kwanza ni unyanyapaa binafsi na aina ya pili ni ule wa mtu kunyanyapaliwa na mtu, kikundi au jamii kwa ujumla.
Bi Leticia alieleza ya kuwa unyanyapaa binafsi ni ile hali ya mtu kujinyanyapaa mwenyewe pale anapojihisi hana thamani na kujihisi watu watanionaje. Aina ya pili ni ile hali ya Jamii kumnyanyapaa mtu, kushindwa kuthamini utu kwasababu anaishi na VVU wakati yapo magojwa mengine ambayo yanapelekea hata mtu kukatwa viungo vya mwili mfano Kisukari
Hata hivyo katika suala zima la unyanyapaa vijana wameku-wa wahanga ambapo asilimia kubwa ya vijana wanajin-yanyapaa wenyewe hali inayopelekea wengi wao kuacha kutumia dawa kwa kuhofia kuonekana katika sehemu za kuchukulia dawa (CTC) na hivyo kusaba-bisha madhara kama kupoteza kizazi kijacho.
Katika utekelezaji wa Mradi wa HEBU TUYAJENGE, vijana ikiwa ni sehemu ya walengwa wakuu katika kuwahimiza utumiaji sahihi wa huduma za UKIMWI, pamoja na kuwajengea uwezo wa kujitambua na kusimama kwa kujiamini ili kuweza kutimiza ndoto zao.
Hata hivyo, Bi Leticia alishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanza-nia kupitia Wizara ya Afya Maendelo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto kwa mchango mkubwa katika mwitikio wa UKIMWI nchini, ikiwa ni pamoja na kushusha umri wa vijana kupima kutambua afya zao kwa ridhaa yao kutoka miaka 18 iliyokuwa awali na sasa imekuwa miaka 15, hii itamsaid-ia kijana kujua afya yake mapema na kama ana maambukizi aanze tiba mapema ili aweze kutimiza ndoto zake na kutengeneza Taifa la kesho.
Mwe
nyek
iti wa
Bar
aza
la wa
tu W
anao
ishi n
a vir
usi v
ya U
kimwi
Tanz
ania
Bi. L
etici
a M
ouric
e
Unyanyapaa ni kikwazo kufikia95-95-95
8
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
9
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Afisa Mtendaji Mkuu wa Baraza la Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI
(NACOPHA) Bw. Deogratius Rutatwa pamoja na wajumbe wa bodi walifanya
ziara ya ukaguzi wa vikundi vya Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI
(WAVIU) pamoja na shughuli mbali mbali katika utekelezaji wa mradi wa
HEBU TUYAJENGE unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Watu wa
Marekani USAID katika mikoa ya Lindi na Mtwara. Ziara hii ilifanyika kwa
siku tano kuanzia mnamo mwezi Juni 2020.
Lengo la ziara ilikuwa kukagua shughuli zinazoendeshwa na vikundi vya
WAVIU na shughuli zinazoendelea katika Konga hususani uimarishaji na
uundwaji wa Vikundi. Katika ziara hii wajumbe waliweza kutembelea
Konga za Manispaa ya Mtwara Mikindani na Halmashauri ya Wilaya ya
Newala ambapo waliweza kukutana na wawakilishi wa Vikundi 14 vya
WAVIU Mkoani Mtwara. Mkoani Lindi Konga ya Nachingwea ilitembelewa
na wajumbe waliweza kuhudhuria mkutano mkuu wa Uchaguzi wa
Konga uliofanyika mapema Tarehe 09/06/2020.
Aidha wajumbe walitembelea Ofisi za Makatibu tawala mikoa ya Lindi na
Mtwara kwa ajili ya kutambulisha mradi katika ngazi ya Mkoa. Katika utambulisho huu wajumbe walionana na Makatibu tawala pamoja na maafisa maendeleo ya jamii wa mkoa.
Ziara hii imekuwa jukwaa muhimu la kuleta chachu ya mabadiliko kwa
kuwataka WAVIU mmoja mmoja na katika vikundi kuondokana na dhana
ya kuwa watu au vikundi vya misaada na badala yake wawe na mtizamo
Ziara ya ukaguzi wa vikundi wezeshimkoani Lindi na Mtwara
wa kujiamini, kujengana na kujasirishana Katika ngazi ya Konga,
Mtendaji mkuu wa Baraza aliwaagiza viongozi wa Konga
kufanya juhudi za makusudi za kuunda vikundi vya WAVIU pamoja
na Konga kata kwenye kila kata.
Ofisi ya Kanda ya Dar es Salaam ambayo ndio inaratibu Mikoa ya
Lindi na Mtwara tunatoa shukrani za dhati kwa Afisa Mtendaji Mkuu
pamoja na wajumbe wa bodi kwa jitihada za kutembelea Konga na
vikundi vyetu. Ziara hii imeleta mwamko mkubwa wa kujiamini na
kujijenga miongoni mwa WAVIU.
Afisa mtendaji mkuu (NACOPHA) Deogratius Rutatwa akielezea mradi wa Hebu Tuyajenge kwa WAVIU konga ya Newala vijijini alipokuwa katika ziara ya kukagua shughuli za vikundi wezezeshi mkoani
Mtwara 8/6/2020.
Afisa mtendaji mkuu wa NACOPHA na wajumbe wa bodi ya Baraza pamoja na wawakilishi wa vikundi vya WAVIU katika picha ya pamoja alipowatembelea wanavikundi hao kwenye ofisi yaHalmashauri ya wilaya ya Newala Vijijini tarehe 8/06/2020
10
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Serikali mkoani Tabora yaviwezesha vikundi vya WAVIU
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akiongea na wanakikundi chaFaraja pamoja na wananchi katika kata ya Nkinga Wilayani Igunga katika ziara ya kuhamasisha
kufikia malengo ya 95-95-95 pamoja na uanzishwaji wa Vikundi wezeshi vya WAVIU.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora ametoa milioni 12 kwa vikundi vya watu
wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU) katika ziara yake alipotembelea
katika vikundi wezeshi kuona shughuli zinazofanywa na Konga kupitia
vikundi vya WAVIU ikiwa ni sehemu ya uhamasishaji na utekelezaji wa
Mradi wa Hebu Tuyajenge unaotekelezwa na NACOPHA na kufadhiliwa na
Shirika la Maendeleo la Watu wa Marekani (USAID) ambapo ziara hiyo
ilifanyika kwa siku saba June 22/06/2020 mpaka 28/06/2020 mkoani
Tabora.
Aidha amevutiwa na jitihada zinazofanywa na WAVIU katika vikundi vyao
na kuahidi kutoa kiasi cha Shilingi milioni moja katika kila kikundi ambapo
kiasi cha milioni 12 zilitolewa kwa vikundi kumi na mbili alipotembelea
katika vikundi mbali mbali ikiwemo Halmashauri ya Sikonge, Urambo,
Igunga, nzega mji, pamoja na Nzega Wilaya, ikiwa ni zoezi endelevu katika
utekelezaji wa mradi ambalo limeanza katika kanda ya Mwanza na
kujumuisha washiriki 42, wanawake 22 na wanaume 20.
Mkuu wa mkoa amesema fedha hizo zitaingizwa katika akaunti za vikundi
moja kwa moja kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao ili kujikwamua
kiuchumi. Hata hivyo Mwanri amewataka wakurugenzi wa halmashauri
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akipokea zawadi ya Kuku na Mafuta kutoka katika kikundi cha Upendo kilichopo Wilayani Sikonge wakati alipofanya ziara ya kutembelea vikundi wezeshi
zote za mkoa wa Tabora kutoa kipaumbele kwa vikundi vya watu Wanaoishi
na Virusi vya UKIMWI katika fedha za mikopo zinazotolewa na Halmashauri kwa makundi maalum.
Bwana Zakaria Matope, mjumbe wa Konga ya Nzega na Bi. Neema Samweli mjumbe wa Konga ya Igunga wamepongeza jitihada zinazofanywa na NACOPHA kupitia USAID kwa kuwapa kipaumbele katika miradi ya kuhakikisha inatokomeza maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi, pia wameshukuru NACOPHA kwa kuwaunganisha na Serikali na jitihada zinazofanywa na mkuu wa mkoa kwa kuwathamini ikiwa ni pamoja na kuwatembelea na kuwapa moyo katika shughuli mbalimbali wanazojishughulisha nazo kama sehemu ya kujipatia kipato.
11
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Mafunzo ya Wakiri tiba ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa HEBU TUYAJENGE( HT), ambayo hutolewa kwa kuzingatia utaratibu maalum ili kufikia walengwa na kuleta matokeo chanya. Utolewaji wa mafunzo haya umefanyika katika Kanda nne za mradi, Kanda ya Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza na Mbeya ambapo kabla ya utolewaji wa mafunzo kulikuwa na mafunzo ya Timu ya Uratibu wa Konga (CCT) ambayo walijengewa uwezo katika suala zima la kusimamia na kuendesha shughuli za mafunzo kwa wakati kwa kuzingatia taratibu zilizopo ili kuhakikisha ujumbe unafika kwa jamii ipasavyo.
Katika kanda Kanda ya Dar es Salaam, mafunzo yalifanyika kwa kipindi tofauti katika konga 15 ambapo jumla ya wakiri tiba 150 walipatiwa mafunzo hayo ambayo yanalenga namna ya utekelezaji wa shughuli za mradi katika kutoa huduma za UKIMWI ngazi ya jamii, ambayo yalikuwa yanatolewa kwa nyakati tofauti kwa kila konga na yalifanyika takriban siku sita na yalihusisha WAVIU na wawakilishi kutoka Halmashauri husika kama, Mratibu wa Ukimwi wa Wilaya(CHACC), Mratibu wa Afya (DACC) na Mratibu wa huduma za Afya majumbani (CBHSCO).
Aidha mafunzo haya yalitolewa na Wataalamu kwa kutumia mifano stahiki na kulikuwa na wasaa wa maswali na majibu ili kuhakikisha upokeaji wa taarifa unawafikia walengwa na kupata matokeo chanya ili kuweza kuzifikia 95 95 95 ifikapo 2030. Kanda ya Dar es Salaam Konga zilizoshiriki katika mafunzo ni H/wilaya Ilala, H/wilaya Temeke, H/wilaya Masasi, H/mji
Mafunzo ya wakiri tiba katikautekelezaji wa mradi
Timu za uratibu wa mradi wa Hebu Tuyajenge (HT) wakiwa katika mafunzo elekezi ya utekelezaji wa mradi yaliyofanyika katika kanda ya Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza na Mbeya
Masasi, H/wilaya Mtwara, Newala H/wilaya, Newala H/wilaya, H/wilaya Lindi, H/mji Lindi, H/wilaya Nachingwea, H/wilaya Ruangwa, H/mji Tanga, H/manispaa Moshi, H/wilaya Moshi na H/wilaya Chalinze.
Aidha katika Kanda ya Mbeya, mafunzo ya wakiri tiba yalitolewa katika konga 15 ambayo yalihudhuriwa na wawakilishi kutoka Manispaa (CHACC na DACC) ambapo utaratibu wa utolewaji wa mafunzo uliendeshwa na wataalamu kwa ufanisi na kwa kutumia njia mbali mbali ili kuhakikisha ujumbe unafika kwa jamii ipasavyo.
Konga zilizoshiriki katika mafunzo hayo ni Konga ya Makambako halmashauri ya Mji, Makete h/wilaya, Mafinga h/mji, Ludewa h/wilaya, Iringa h/wilaya, Songea h/manispaa, Sumbawanga h/manispaa, Rungwe h/wilaya, Mbeya h/jiji, Njombe h/mji, Kilolo h/wilaya, Iringa h/manispaa, Wanging’ombe h/wilaya Mufindi h/wilaya, na Njombe h/wilaya.
Kanda ya Dodoma jumla ya Konga zilizopatiwa mafunzo ni konga 23 ambayo yalihudhuriwa na wawakilishi kutoka Serikalini CHACC na DACC ambapo mafunzo hayo yalitolewa kwa ufanisi wa hali ya juu na kwa kutumia njia mbali mbali ili kujenga uelewa na kupata matokeo ya stahiki.Hali kadhalika kanda ya Mwanza mafunzo yaliendeshwa na wataalamu na waliendesha mafunzo hayo kwa awamu tofauti na kwa kuzingatia utolewaji wa mafunzo wa kiwango cha juu ambapo jumla ya Konga 15 zilishiriki katika mafunzo ambayo yalilenga kuwajengea uwezo wa kuwa mabalozi wazuri katika Konga zao.
Timu za uratibu zikiwa kwenye mafunzo elekezi ya utekelezaji wa mradi kanda ya Dar es Salaam yaliyofanyika katika ukumbi wa Upland Changanyikeni
12
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Ziara ya viongozi wa NACOPHAOfisi ya Waziri Mkuu - Dodoma
Baraza la watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI Tanzania (NACOPHA)
mwezi wa Agosti mwaka huu 2020 waliweza kuwasilisha taarifa ya
utendaji wa shughuli za Baraza kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu,
Sera, Uratibu na Uwekezaji Bi. Doroth Mwaluko katika Mkutano uliofanyika
Ofisi ya Waziri Mkuu, mkoani Dodoma.
Katika mkutano huo ambao mgeni rasmi alikuwa Bi. Doroth Mwaluko,
pia ulihudhuriwa na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI
(TACAIDS) Dr. Leornard Maboko, Pundensia Mbwiliza, Mwenyekiti wa
Mtandao wa Vijana wanaoishi na maambukizi ya UKIMWI (NYP+), Ms.
Leticia Mourice Mwenyekiti NACOPHA, Bw. Deogratius Rutatwa Afisa
Mtendaji Mkuu NACOPHA, pamoja na wawakilishi wengine kutoka Ofisi
ya Waziri Mkuu.
Aidha Mwenyekiti wa NACOPHA Bi. Mourice alishukuru Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Tawala za mikoa na serikali
za mitaa (TAMISEMI), Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee
na Watoto (MoHDGEC) kwa kazi nzuri ambayo wanaendelea kuifanya
na hasa kuhakikisha watu wanoishi na VVU wanapata huduma stahiki.
Pia alishukuru Serikali kwa kuendelea kuitambua NACOPHA na
kufanya nayo kazi kwa ukaribu sana, hali kadhalika aliishukuru Serikali
ya Watu wa Marekani kupitia Shirika la Maendeleo la watu wa
Marekani USAID kwa kuendelea kuwezesha NACOPHA dhidi ya
mwitikio wa VVU NA UKIMWI na kuunganisha sauti za WAVIU nchini. Bi.
Leticia alielezea kuwa “NACOPHA inafanya kazi kwa kuzingatia sheria
na miongozo ya nchi kwa kuanzia ngazi ya jamii kupitia vikundi
wezeshi, konga kata na konga wilaya”. Bw. Rutatwa alielezea historia
ya NACOPHA kuwa ilianzishwa na Tume wakati wa NMSF II kwa lengo
na kuratibu WAVIU nchini, hivyo mwaka 2003 NACOPHA iliundwa na
kupata usajili rasmi mwaka 2005. Alielezea dira, dhima na lengo kuu la
NACOPHA, na alitaja tunu za NACOPHA kuwa ni uwajibikaji, utamaduni
bora, uadilifu, usawa wa kijinsia, kujitoa na kuheshimu utu na misingi
ya utawala bora.
Aidha, Bw. Rutatwa pia alibainisha kuwa hadi sasa NACOPHA ina jumla
ya konga 175 kati ya 185 za Tanzania Bara, pia ina wanachama
640,483 (406,838 wanawake na 233,645 wanaume) ambao ni 43%
ya WAVIU wote nchini. Vile vile aliwataja wanufaika wakuu wa
NACOPHA kuwa ni WAVIU kupitia ushiriki wao katika ngazi ya jamii
kutoka kwenye vikundi na konga za WAVIU.
Wakati wa wasilisho pia alipata wasaa wa kuelezea maeneo makuu ya
kimkakati ambayo ni:- Ushirikishwaji jamii na Uwezeshaji wa WAVIU;
Kuhamasisha uhitaji na utumiaji wa huduma za VVU; Utetezi na ushaw-
ishi wa kisera; Taarifa za kimkakati, Utafiti na mawasiliano; Kujengea
uwezo taasisi, vikundi na konga za WAVIU. Vile vile alielezea miradi
mbalimbali inayotekelezwa na NACOPHA ambayo ni pamoja na mradi
wa HEBU TUYAJENGE unaofadhiliwa na USAID, Mradi wa COMPASS
Africa unaofadhiliwa na AIDS Vaccine Advocacy Coalition (AVAC),
Pamoja na mradi wa Ushirikishwaji wa makundi maalum na WAVIU
katika ushawishi wa huduma mbadala zinazoshirikisha WAVIU
kikamilifu unaofadhiliwa na Global Network of People Living with HIV
and AIDS (GNP+)
Kwa kumalizia wasilisho lake Afisa Mtendaji mkuu wa NACOPHA
alielezea fursa mbalimbali kwa ajili ya maboresho ya baadaye ambazo
ni:- Upungufu wa rasilimali kwa ajili ya kuboresha uratibu na msaada
wa kitaalamu kwa Konga za WAVIU, Kuendeleza juhudi za kutokomeza
unyanyapaa na ubaguzi ili kuchagiza utumiaji wa huduma za upimaji
wa hiari, kujiweka wazi, utambuzi wa watoto na Wanaume dhidi ya
kinga ya maambukizi ya VVU, Mwitikio mdogo wa Wanaume, vijana na
Watoto, Uhamasishaji mkubwa wa utumiaji huduma usioendana na
huduma zilizopo katika baadhi ya vituo vya huduma za UKIMWI, Ukweli
ni kwamba lipo kundi kubwa linalohitaji kukingwa/ kujikinga na
maambukizi ya VVU.
Katibu mkuu alieleza ya kuwa, Watu wanoishi na virusi vya UKIMWI ni
wengi tu lakini hawajaamua kuwa wazi, hivyo alipongeza viongozi wa
NACOPHA kwa kuweza kupata ujasiri wa kuwa huru na kusema kuwa
wanaishi na maambukizi ya VVU. Aidha alielekeza kuwa ifike mahala
neno unyanyapaa wadau wote ikiwemo NACOPHA waachane nalo
kwani kadri linavyotamkwa ndivyo linavyokomaa, hivyo fikra zetu
zikiondokana na hili neno na mambo mengine yatakaa sawa.
Alihitimisha kwa kusema kuwa amefurahishwa kuona NACOPHA
inawajibika ipasavyo, lakini pia aliahidi kutafuta nafasi ya kutembelea
Ofisi za NACOPHA ili kujionea shughuli za WAVIU na kuendelea
kushirikiana, na pia alisisitiza kuwa NACOPHA ndiyo chachu kubwa ya
kuhakikisha kuwa mipango iliyopangwa inatekelezeka ili kuweza
kufikia malengo ya kitaifa.
Afisa Mtendaji Mkuu wa NACOPHA Deogratius Rutatwa akiwasilisha utekelezaji wa shughuli za barazakwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Uwekezaji Mhe. Dorothy Mwaluko
Mkurugenzi wa TACAIDS, Dk. Leonard Maboko akifurahia jambo wakati wa mkutano wa wasilisho la utekelezaji wa shughuli za Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWII (NACOPHA) kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Uwekezaji Mhe. Dorothy Mwaluko, katika
ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Dodoma
13
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Baraza la watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI Tanzania (NACOPHA)
mwezi wa Agosti mwaka huu 2020 waliweza kuwasilisha taarifa ya
utendaji wa shughuli za Baraza kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu,
Sera, Uratibu na Uwekezaji Bi. Doroth Mwaluko katika Mkutano uliofanyika
Ofisi ya Waziri Mkuu, mkoani Dodoma.
Katika mkutano huo ambao mgeni rasmi alikuwa Bi. Doroth Mwaluko,
pia ulihudhuriwa na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI
(TACAIDS) Dr. Leornard Maboko, Pundensia Mbwiliza, Mwenyekiti wa
Mtandao wa Vijana wanaoishi na maambukizi ya UKIMWI (NYP+), Ms.
Leticia Mourice Mwenyekiti NACOPHA, Bw. Deogratius Rutatwa Afisa
Mtendaji Mkuu NACOPHA, pamoja na wawakilishi wengine kutoka Ofisi
ya Waziri Mkuu.
Aidha Mwenyekiti wa NACOPHA Bi. Mourice alishukuru Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Tawala za mikoa na serikali
za mitaa (TAMISEMI), Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee
na Watoto (MoHDGEC) kwa kazi nzuri ambayo wanaendelea kuifanya
na hasa kuhakikisha watu wanoishi na VVU wanapata huduma stahiki.
Pia alishukuru Serikali kwa kuendelea kuitambua NACOPHA na
kufanya nayo kazi kwa ukaribu sana, hali kadhalika aliishukuru Serikali
ya Watu wa Marekani kupitia Shirika la Maendeleo la watu wa
Marekani USAID kwa kuendelea kuwezesha NACOPHA dhidi ya
mwitikio wa VVU NA UKIMWI na kuunganisha sauti za WAVIU nchini. Bi.
Leticia alielezea kuwa “NACOPHA inafanya kazi kwa kuzingatia sheria
na miongozo ya nchi kwa kuanzia ngazi ya jamii kupitia vikundi
wezeshi, konga kata na konga wilaya”. Bw. Rutatwa alielezea historia
ya NACOPHA kuwa ilianzishwa na Tume wakati wa NMSF II kwa lengo
na kuratibu WAVIU nchini, hivyo mwaka 2003 NACOPHA iliundwa na
kupata usajili rasmi mwaka 2005. Alielezea dira, dhima na lengo kuu la
NACOPHA, na alitaja tunu za NACOPHA kuwa ni uwajibikaji, utamaduni
bora, uadilifu, usawa wa kijinsia, kujitoa na kuheshimu utu na misingi
ya utawala bora.
Aidha, Bw. Rutatwa pia alibainisha kuwa hadi sasa NACOPHA ina jumla
ya konga 175 kati ya 185 za Tanzania Bara, pia ina wanachama
640,483 (406,838 wanawake na 233,645 wanaume) ambao ni 43%
ya WAVIU wote nchini. Vile vile aliwataja wanufaika wakuu wa
NACOPHA kuwa ni WAVIU kupitia ushiriki wao katika ngazi ya jamii
kutoka kwenye vikundi na konga za WAVIU.
Wakati wa wasilisho pia alipata wasaa wa kuelezea maeneo makuu ya
kimkakati ambayo ni:- Ushirikishwaji jamii na Uwezeshaji wa WAVIU;
Kuhamasisha uhitaji na utumiaji wa huduma za VVU; Utetezi na ushaw-
ishi wa kisera; Taarifa za kimkakati, Utafiti na mawasiliano; Kujengea
uwezo taasisi, vikundi na konga za WAVIU. Vile vile alielezea miradi
mbalimbali inayotekelezwa na NACOPHA ambayo ni pamoja na mradi
wa HEBU TUYAJENGE unaofadhiliwa na USAID, Mradi wa COMPASS
Africa unaofadhiliwa na AIDS Vaccine Advocacy Coalition (AVAC),
Pamoja na mradi wa Ushirikishwaji wa makundi maalum na WAVIU
katika ushawishi wa huduma mbadala zinazoshirikisha WAVIU
kikamilifu unaofadhiliwa na Global Network of People Living with HIV
and AIDS (GNP+)
Kwa kumalizia wasilisho lake Afisa Mtendaji mkuu wa NACOPHA
alielezea fursa mbalimbali kwa ajili ya maboresho ya baadaye ambazo
ni:- Upungufu wa rasilimali kwa ajili ya kuboresha uratibu na msaada
wa kitaalamu kwa Konga za WAVIU, Kuendeleza juhudi za kutokomeza
unyanyapaa na ubaguzi ili kuchagiza utumiaji wa huduma za upimaji
wa hiari, kujiweka wazi, utambuzi wa watoto na Wanaume dhidi ya
kinga ya maambukizi ya VVU, Mwitikio mdogo wa Wanaume, vijana na
Watoto, Uhamasishaji mkubwa wa utumiaji huduma usioendana na
huduma zilizopo katika baadhi ya vituo vya huduma za UKIMWI, Ukweli
ni kwamba lipo kundi kubwa linalohitaji kukingwa/ kujikinga na
maambukizi ya VVU.
Katibu mkuu alieleza ya kuwa, Watu wanoishi na virusi vya UKIMWI ni
wengi tu lakini hawajaamua kuwa wazi, hivyo alipongeza viongozi wa
NACOPHA kwa kuweza kupata ujasiri wa kuwa huru na kusema kuwa
wanaishi na maambukizi ya VVU. Aidha alielekeza kuwa ifike mahala
neno unyanyapaa wadau wote ikiwemo NACOPHA waachane nalo
kwani kadri linavyotamkwa ndivyo linavyokomaa, hivyo fikra zetu
zikiondokana na hili neno na mambo mengine yatakaa sawa.
Alihitimisha kwa kusema kuwa amefurahishwa kuona NACOPHA
inawajibika ipasavyo, lakini pia aliahidi kutafuta nafasi ya kutembelea
Ofisi za NACOPHA ili kujionea shughuli za WAVIU na kuendelea
kushirikiana, na pia alisisitiza kuwa NACOPHA ndiyo chachu kubwa ya
kuhakikisha kuwa mipango iliyopangwa inatekelezeka ili kuweza
kufikia malengo ya kitaifa.
Picha ya pamoja ya washiriki wa mkutano wa wasilisho la utekelezaji wa shughuli za NACOPHA wakiwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Uwezeshaji Mhe. Dorothy Mwaluko aliyekaa katikati
Makamu Mwenyekiti wa NACOPHA Yusufu Marere aliyekaa katikati akiwa na wajumbe wa Bodi ya NACOPHA kulia; Pudensiana Mbwiliza na kushoto; Eliasi Charles wakati wa mkutano wa wasilisho la utekelezaji wa shughuli za Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWII (NACOPHA) kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Uwekezaji Mhe. Dorothy Mwaluko, Dodoma
14
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
SIMULIZI ZA MAFANIKIO
Kurudiana kwa wanandoaambao mmoja anaishi na VVU
Bi. Kanisia Kadege aliachwa na mumewe Bw. Fisto Kisakali baada ya kufahamu anaishi na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI. Bw. Kisakali aliamua kuitelekeza familia yake na kuhamia sehemu nyingine na kumtuhumu mkewe kwa kutokuwa muaminifu katika ndoa yao.
Hali hiyo ilibainika katika kipindi cha ujauzito wa pili wa Kanisia ambapo mumewe alitaka waende katika kituo cha afya kwa ajili ya kujua hali ya afya yake ndipo alipogundulika anaishi na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI lakini hakuwa muwazi kwa mumewe ambaye hanamaambukizi.
Bi. Kadege ana umri wa miaka 42 na ni Mwanachama wa Konga ya Njombe anayeishi katika Kijiji cha Iyendela, katika kata ya Matembwe Mkoani Njombe. Anaishi na maambukizi toka mwaka 2014 na anafata taratibu za utumiaji wa dawa katika vituo vya utoaji wa huduma CTC.
Aliolewa na Bw. Kisakali kama mke wa pili na walifanikiwa kupata Watoto wawili. Mtoto wa kwanza ana miaka minne na wa pili ana mwaka mmoja ambapo watoto wote hawana maambukizi kutokana na mama kufuata taratibu za utumiaji wa dawa za kinga dhidi ya mama na mtoto (PMCT)
Mwezi wa tano mwaka huu 2020, Bw. Christopher Gwivaha na Bi. Evarista Hongoli wa kata ya Matembwe walihudhuria mafunzo ya
wakiritiba kupitia mradi wa HEBU TUYAJENGE na kujifunza jinsi ya kuwarudisha waliotoroka katika dawa, huduma za upimaji, upimaji wa wenza (index testing) na upimaji wa wingi wa virusi. Kupitia mafunzo ya wakiritiba waliamua kuwatembelea Bi Kanisia na Bw.Kisakali kila mtu katika makazi yake na walipata muda wa kuongea nao kuhusi-ana na mgogoro wao. Waliwashauri waende kupima katika kata ya Matembwe na baada ya matokeo wakiritiba walikaa nao na kuanza kutoa ushauri wa jinsi ya kuishi pamoja na kukubaliana na hali hiyo na walimueleza kwakuwa mkewe anafuata huduma za tiba (ART) hawezi kumuambukiza na pia walimsisitiza Bw. Kisakali kurejea nyumbani.
Baada ya jitihada hizo kikao kilifanyika Julai 07, 2020 ambapo Bw.
Kisakali alikubali kurudi nyumbani kwake na kumuomba mkewe
msamaha pamoja na wote waliohusika katika upatanishi. Hata hivyo
ili kuhakikisha amani na upendo unazidi kujengeka na kuleta furaha
baina yao, wawakilishi wetu katika sehemu husika wako karibu na
familia hii ili kujenga Taifa Imara.
Ni muhimu kwa jamii kutambua ya kuwa, kuishi na maambukizi ya
UKIMWI haiondoi haki ya kuolewa, kwani kuna asilimia kubwa ya
Watu wanaoishi na Maambukizi ya VVU na wameoa/kuolewa na watu
wasio na maambukizi na kuzaa Watoto wasio na maambukizi.
NinamshukuruBw. Christopher Gwivaha na Bi. Evarista, sasa hivi tuna furaha na tunatambua jinsi ya kuishi ikiwa mmoja ana maambukizi na mwingine hana na tunaahidi tutakuwa mabalozi wazuri na kusaidia wengine Said Fisto
Bi, Kanisia Kadege na mumewe Bw. Fisto
Kisakali pamoja na Watoto wao Chesco na Editoni Kisakaliwakiwa nyumbani kwao
baada ya kupatana
15
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Konga ya Halmashauri ya Manispaa Sumbawanga wamekuwa na uhaba
wa ofisi kwa muda mrefu na kufikia maamuzi ya kupanga ofisi toka
mwaka 2018. Konga hii ni miongoni mwa konga zinazotekeleza mradi wa
HEBU TUYAJENGE kanda ya Mbeya ambao unatekelezwa na NACOPHA
kwa ufadhili wa USAID.
Kumekuwa na ushirikiano mzuri kati ya Konga na Halmashauri ya
Manispaa Sumbawanga kwa muda mrefu, tunathamini mchango na
ushirikiano mzuri kutoka kwa Serikali.
Mnamo tarehe 15/07/2020 jumla ya konga 18 za Halmashauri ya
Manispaa Sumbawanga zilitumwa kwa wawakilishi kushiriki katika
mafunzo ya Wakiri tiba yaliofanyika katika ukumbi wa Sambala katika
Halmashauri ya Manispaa Iringa, Pia walihudhuria wawakilishi kutoka
Halmashauri za wilaya (CHAC/DACC),Mwenyekiti wa Konga, Makamu
mwenyekiti, Katibu, Karani na mwakilishi wa Vijana, ni kati ya watu
walioshiriki katika mafunzo hayo pamoja na Wakiritiba kutoka katika kata
tano Mazwi, Majengo, Chanji, Pito and Ntendo.
Malengo ya mafunzo haya nikuwaunganisha WAVIU na huduma za
upimaji, upimaji wa wenza, Ufuatiliaji wa wingi wa virusi kwenye damu,
kuwarudisha katika dawa na kuwaunganisha na vikundi wezeshi.
Baada ya mafunzo Viongozi wa Konga kwa kushirikiana na mratibu wa
Ukimwi wa Wilaya na Mratibu wa Afya wa Wilaya wa Halmashauri ya
Manispaa ya Sumbawanga waliutambulisha mradi wa HEBU TUYAJENGE
malengo na sehemu zinazofikiwa na mradi na pia waliwatambulisha
wakiritiba waliopata mafunzo kwa Afisa Maendeleo ya Jamii wa
wilaya(DCDO) na Afisa Tawala wa Wilaya (DED) ili kupata ruhusa ya
kuwatambulisha katika kata na sehemu za utolewaji wa huduma za Afya
(CTC) kwa ajili ya shughuli za utekelezaji wa mradi. Hata hivyo Viongozi
wa Konga wana nafasi ya kuainisha changamoto wanazokabiliana nazo
katika utendaji.
Afisa Tawala wa wilaya anatambua juhudi zinazofanywa na Konga katika
utekelezaji wa mwitikio wa Ukimwi. Hivyobasi katika kuunga mkono
juhudi na utekelezaji yakinifu dhidi ya UKIMWI Afisa tawala wa wilaya
ametoa kiwanja chenye ukubwa wa mita za mraba 900 katika Kijiji cha
Masufa street kilichopo kilomita saba kutoka mjini na ameagiza Afisa
Serikali bega kwa bega na konga H/ManispaaSumbawanga katika mwitikio wa UKIMWI
mipango miji wa Halmashauri kuhakikisha nyaraka zote ikiwepo Hati za
viwanja zimekamilika ili ujenzi wa Ofisi za Konga uanze pamoja na ufanyaji
wa shughuli nyingine za kiuchumi.
Pia aliahidi kutoa usafiri katika shughuli za utekelezaji wa mradi ili kusaidia
suala zima la kupambana na ugonjwa wa UKIMWI kwa wakazi wa eneo
husika.
“Kwa niaba ya NACOPHA Konga ya Halmashauri ya Manispaa ya
Sumbawanga, Ningependa kutoa shukrani kwa uongozi wa NACOPHA kwa
kutushirikisha katika mradi wa HEBU TUYAJENGE katika Halmashauri zetu.
Katika konga yetu huu ni mradi wa kwanza ambao tutautekeleza katika
Halmashauri yetu.Tunawashukuru uongozi wa Halmashauri ya Manispaa
ya Sumbawanga kwa msaada tulioupokea na msaada tunaoendelea
kupokea katika shughuli za utekelezaji wa UKIMWI na tunaahidi kuongeza
juhudi kwa lengo la kuokoa kizazi na maambukizi mapya,kuondoa
unyanyapaa katika jamii na kuhakikisha WAVIU wanapata huduma za tiba
na matunzo (ART). Ni matumaini kipindi cha utekelezaji wa shughuli za
mradi, unyanyapaa katika jamii utapungua na tutarudisha waliotoroka
katika dawa na kuwaunganisha WAVIU katika huduma za tiba na matunzo”
alisema mwenyekiti wa Halmashauri Manispaa ya Sumbawanga Bi.
Christina Mulisa.
Nimatumaini ya kwamba,kipindi cha utekelezaji wa shughuli za mradi
katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga,WAVIU wapya watapati-
kana,watoro wa dawa watarudishwa,Utolewaji wa huduma za afya katika
jamii, kuwaunganisha WAVIU na vikundi wezeshi pamoja na huduma za
ufuatiliaji wa wingi wa virusi katika damu.
Viongozi wa Konga ya Halmashauri ya Manispaa Sumbawanga pamoja na Wakiri tiba katika ofisi za Afisa Tawala wa Wilaya wakati wa utambulisho wa mradi wa HEBU TUYAJENGE.
SIMULIZI ZA MAFANIKIO
3 ZE
ROS
BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA
Baraza la Taifa la watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI Tanzania (NACOPHA)Barabara ya Whitesand 86, Mtaa wa Keni Close/Kilongawima, Nyumba Na. KUN/KIL/83 S. L. P 55811. Dar es Salaam, Tanzania. Simu: +255-22-2618518,
Barua pepe: [email protected], Tovuti: www.nacopha.or.tz