kuhusu afrodad - afrodad.files.wordpress.com · mchakato wa mkataba wa mkopo ilifanyika kulingana...
TRANSCRIPT
KUHUSU AFRODAD
Dira ya AFRODAD
AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa
maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.
Dhamira ya AFRODAD
Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni
ya Afrika kulingana na thamani ya mfumo wa haki za
binadamu.
Malengo ya AFRODAD ni pamoja na yafuatayo:
1. Kuongeza ufanisi na usimamizi wenye tija na matumizi
ya rasilimali ya serikali za Afrika;
2. Kupata/kuleta mabadiliko katika dhana ya kimataifa ya
kijamii na kiuchumi na mpangilio wa kidunia wa kisiasa
kwenye mchakato wa maendeleo unaotambulisha
mahitaji na matakwa ya watu wengi duniani;
3. Kuwezesha mazungumzo kati ya vyama vya kiraia na
serikali kwenye masuala yanayohusiana na Madeni na
maendeleo Afrika au sehemu nyingine.
MKATABA WA KUKOPAKanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi
za AfrikaToleo Lililorekebishwa
Hatimiliki © 2013 AFRODAD Haki zote zimehifadhiwa
ISBN 978-0-7974-4509-3EAN 9780797445093
YALIYOMO
DIBAJI 6
1. UZINGATIAJI WA BUSARA NA DESTURI ZA
UKOPAJI NA USIMIMIAJI WA MADENI YA UMMA 8
2. UWEPO WA SHERIA NA KANUNI
ZINAZOTABIRIKA 11
3. MIUNDO NA WAJIBU ZINAZORATIBIKA NA
MADHUBUTI 13
4. UWEPO WA OFISI HURU YA USIMAMIZI WA
MADENI 18
5. USHIRIKI WA UMMA, UJUMUISHWAJI NA
KUWEKA TAARIFA HADHARANI 20
6. KUHESHIMU UBINADAMU NA HAKI ZA
WATU ZA KIIKOLOJIA 23
7. KUHESHIMIANA NA USAWA KATIKA UBIA NA
WAKOPESHAJI NA WAFADHILI WA KIMATAIFA 25
MAREJEO NA USOMAJI WA ZIADA 27
MKATABA WA KUKOPA
6
DIBAJI
Nchi za Kusini mwa jangwa la Sahara zinakabiliwa na
changamoto kubwa katika michakato ya kuingia mikataba
ya madeni na usimamizi wa madeni ya umma. Changamoto
hizo zinatokana na vyanzo vya fedha za maendeleo,
michakato ya kuidhinisha mikopo, hali na masharti ya
mikopo, uchumi mkuu na sera za udhibiti, uwezo wa
kitaasisi kwa ujumla, na uwezo wa nchi kukopesheka.
Majeraha ya Migogoro ya madeni ya miaka ya 1970,
1980 na 1990 yanatokana na udhaifu wa michakato ya
uingiaji wa mikataba ya mikopo na usimamizi wa madeni
ya umma. Migogoro hii ya madeni ilichangia kwa kiasi
kikubwa matatizo ya kiuchumi na kijamii katika nchi za
Kusini mwa jangwa la Sahara kwa kuathiri uimara wa
uchumi na uwezo wa kukopesheka kimataifa. Madeni ya
muda mrefu yalidumaza uwekezaji, ukuaji wa uchumi na
biashara. Kulipia madeni kuliyasonga matumizi ya serikali
katika elimu, afya na mahitaji mengine ya kijamii katika
nchi nyingi zilizokuwa zinadaiwa.
7
KAnUni nA MiOngOzO yA UKOPAji hURU WA FeDhA KWA nchi zA AFRiKA
Mkataba huu wa Kukopa una Kanuni na Miongozo ya
Ukopaji huru wa fedha. Unataka kutoa mwongozo na
kujulisha ukopaji huru kwa lengo la kuchangia uboreshaji
wa utawala dhaifu wa sasa, michakato ya kitaasisi na
kisheria ya mikataba ya mikopo na usimamizi wa deni
la umma. Kwahiyo, AFRODAD inazihimiza nchi zote
zinazokopa hasa zile zilizopo Kusini mwa jangwa la Sahara
kufuata kanuni na miongozo, ili kuhakikisha ufanisi na
utumiaji wenye tija wa rasilimali madeni na vifaa, kuzuia
kujirudia kwa migogoro ya madeni na kuzifanya serikali
kuwajibika kwa wananchi wao.
Mkataba huu una kanuni na miongozo saba pana
zifuatazo:
1. Uzingatiaji wa busara na desturi za ukopaji na
usimimiaji wa madeni ya umma
2. Uwepo wa sheria na kanuni zinazotabirika
3. Miundo na wajibu zinazoratibika na madhubuti
4. Uwepowaofisihuruyausimamiziwamadeni
5. Ushiriki wa umma, ujumuishwaji na kuweka taarifa
hadharani
6. Kuheshimu ubinadamu na haki za watu za kiikolojia
7. Kuheshimiana na usawa katika ubia na wakopeshaji
na wafadhili wa kimataifa
MKATABA WA KUKOPA
8
1 UZINGATIAJI WA BUSARA NA DESTURI ZA UKOPAJI NA USIMIMIAJI WA MADENI YA UMMA
1.1 Msaada wa Kisiasa: Serikali za Kitaifa zinahitaji
kutumia busara na kuupatia msaada umuhimu wa
kisiasa ukopaji na usimamizi wa madeni ya umma ili
kuhakikisha uendelevu wa madeni.
1.2 Mazingira imara ya Kiuchumi: Serikali za Kitaifa lazima:-
1.2.1 Zihakikishe kuwa mkakati wa madeni ya
Umma unaendana na sera kuu ya uchumi kwa
kuhakikisha kwamba kiwango cha ukuaji wa thamani
ya sasa ya deni jipya linalotolewa ni sawa au ni pungufu
ya kiwango cha ukuaji wa mauzo ya nje ya nchi, kwa
ajili ya uendelevu wa deni la nje.
1.2.2 Angalia kama mkopo mpya wa mradi
unaendana na sera ya maendeleo ya uchumi kwa
ujumla kabla ya kuidhinishwa.
9
KAnUni nA MiOngOzO yA UKOPAji hURU WA FeDhA KWA nchi zA AFRiKA
1.2.3 Kuhakikisha kuwa mkopo ni kwa ajili ya sekta
zilizo kipaumbele na lazima kuimarisha uwezo wa
sekta ya Umma hasa katika usimamizi wa uwekezaji
wa umma ili kuongeza thamani ya fedha kwenye
miradi inayofadhiliwa na mkopo.
1.2.4 Kuhakikisha uthabiti wa uchumi mkuu,
uendelevu wa fedha, viwango vya chini vya riba, na
usimamiaji wa viwango vya athari za ukopeshaji taasisi
huru.
1.3 Vifungu vya Katiba: Serikali lazima zianzishe
mifumo sahihi na yenye nguvu kisheria na miundo
itakayowajibika kuratibu na kusimamia madeni ya
Umma.
1.4 Ridhaa ya Umma na Uwazi: Serikali lazima zichukue
hatua za Kisheria kuhakikisha kwamba ukopaji wote
wa Umma na usimamizi wa madeni unapata idhini ya
Bunge na Umma kwa ujumla.
1.5 Kujenga Uwezo: Serikali ni lazima zihakikishe kuwa
nchi zao zina uwezo wa kina, endelevu na wa muda
mrefu wa kusimamia madeni. Hii ni pamoja na:
MKATABA WA KUKOPA
10
1.5.1 Kuwa na fungu la zana za usimamizi wa madeni:
Kumbukumbu sahihi na rekodi za kisasa za madeni
yote na madeni yote ya nje yaliyohakikiwa wazi wazi,
ratiba ya majukumu ya malipo ya madeni ikiwa ni
pamoja na masuala ya dharura; uwezo wa kukadiria
athari za maamuzi ya kukopa ya taasisi nyingi za ndani
kwenye wasifu mzima wa deni la nchi; bajeti ya Taifa
na uwiano wa malipo.
1.5.2 Kuhakikisha kwamba wafanyakazi wote wa
Umma wanaoshughulika na kuingia mikataba ya
mikopo na usimamizi wa deni la Umma wanalenga
katika ufanisi wa kazi na majukumu yao:
1.5.2.1 Hakikisha mafunzo zaidi kwa walioshika
ofisi zinazohusika kwenye mikataba ya mikopo na
usimamizi wa deni la Umma – wakaguzi wa hesabu,
wahasibu, wachumi na wanasheria.
1.5.2.2 Hakikisha kwamba wafanyakazi wenye uzoefu
na motisha wanabakia na kupatiwa msaada wa
miundombinu muhimu, teknolojia na rasilimali fedha.
1.5.2.3 Hamasisha ushirikishaji wa wataalamu wa
nje ili kujenga ujuzi wa rasilimali watu waliopo
inavyotakiwa au hitajika.
1.5.2.4 Hamasisha kaguzi za pamoja na Taasisi
nyingine kubwa za Ukaguzi zilizoendelea.
11
KAnUni nA MiOngOzO yA UKOPAji hURU WA FeDhA KWA nchi zA AFRiKA
2 UWEPO WA SHERIA NA KANUNI ZINAZOTABIRIKA
2.1 Mfumo wa Sheria: Mikataba yote ya mikopo ya
Umma na sheria na kanuni za usimamizi wa madeni
lazima zifungamane na vifungu vya katiba na sehemu
nyingine halisi za sheria zinazofafanua jinsi gani mikopo
ya Umma ipatikane, itumike na kulipwa.
2.1.1 Mfumo wa Sheria lazima pia utoe muda
maalum ambamo maombi ya mkopo yatafanyika na
kuidhinishwa ili kuepuka kupunguza kasi ya michakato
ya uidhinishaji ili kuhakikisha utekelezaji kwa wakati
na ufuatiliaji wenye ufanisi.
2.1.2 Mikataba mipya ya mikopo itakuwa ndani ya
muktadha wa mkakati mzima wa deni la serikali na
kulingana na programu/mipango ya maendeleo ya
Taifa. Mipango ya kukopa ya serikali inabidi kuendana
na uendelezaji wa muda mrefu wa deni.
2.2 Mamlaka ya Kukopa: Mfumo wa Kisheria lazima
uweke wazi ni nani mwenye mamlaka ya kukopa kwa
niaba ya serikali.
MKATABA WA KUKOPA
12
2.2.1 Kuna haja ya kuwa na miongozo iliyowazi
ya kisheria/kikatiba kuhusu majukumu na uwajibikaji
kati ya wakala wa serikali wanaohusika kwenye
usimamizi wa madeni, hasa kwa upande wa Wizara
ya Fedha, Benki Kuu na wakala tofauti au yeyote wa
usimamizi wa madeni na majukumu ya wafanyakazi
yaliyoainishwa vizuri ikiwa ni pamoja na sera bayana
za udhibiti na ufuatiliaji na mipangilio ya utoaji taarifa.
2.3Kiwango cha juu cha Kukopa: Inabidi ziwepo sheria,
kanuni na sera ambazo zitaainisha mipaka ya ukopaji
wa madeni ya Umma ya nje. Hii lazima ilandane na
uchambuzi endelevu wa deni la nchi.
2.4 idhini ya Kukopa: Muhimili wa kutunga sheria wa
serikali – Bunge litaidhinisha mikopo kabla mikataba
haijasainiwa. Hii itawezesha na kuhakikisha kwamba
mchakato wa mkataba wa mkopo ilifanyika kulingana
na miongozo na sheria zilizowekwa, na inaweza
kulipwa katika bajeti ya Taifa.
2.5 Mchakato wa Kuidhinisha: Sera ya Kukopa ambayo
inaainisha taratibu za kuidhinisha, muundo wa kamati
ya majadiliano na maandalizi ya majadiliano lazima
zianzishwe.
13
KAnUni nA MiOngOzO yA UKOPAji hURU WA FeDhA KWA nchi zA AFRiKA
3 MIUNDO NA WAJIBU ZINAZORATIBIKA NA MADHUBUTI
3.1 Muundo wa Taasisi, Uratibu na Mawasiliano: Serikali
zitaanzisha Ofisi ya Usimamizi wa Madeni yaTaifa
(OUMT) kuhakisha uratibu na mawasiliano mazuri
kati ya wadau mbalimbali kwenye kuingia mikataba ya
mikopo na taratibu za usimamizi wa madeni.
3.2 Wizara ya Fedha: Wizara husika (mf. Wizara ya
Fedha) itawasilisha mahitaji ya serikali kukopa kwa
ajili ya idhini bungeni ili kupitishwa kama inavyotakiwa
kwa mujibu wa sheria na kanuni za nchi.
3.2.1 Wizara ya Fedha: Itasimamia fedha za nchi
ili kuhakikisha kuwa uwajibikaji kamili unafanyika
kwa Bunge na kwamba udhibiti wake wa fedha
unaimarishwa.
3.2.2 Wizara husika: Wizara husika zita:
3.2.2.1 Toa taarifa za mara kwa mara za maendeleo
ya programu zote zinazofadhiliwa na mikopo ya nje/
miradi kwa Wizara ya Fedha.
MKATABA WA KUKOPA
14
3.2.2.2 Shiriki katika majadiliano na mashauriano yote ya mikataba yote ya mkopo kwa ajili ya miradi na programu chini ya mamlaka yao.
3.2.2.3 Tekeleza, fuatilia na tathmini miradi na programu zote kwenye mamlaka yao kwa kushirikiana kwa karibu na wafadhili, Wizara ya Fedha, asasi za kiraia na walengwa.
3.3 Uangalizi wa Bunge: Bunge litasimamia jukumu muhimu la kuhakikisha uwajibkaji katika kuingia mikataba na michakato ya usimamizi wa madeni.
3.3.1 Bunge madhubuti na linalowajibika hukabiliana na athari za ukopaji uliokithiri kwa kushinikiza mifumo ya uwajibikaji wa serikali na uchunguzi wa kisheria, na kuishinikiza serikali kuboresha utendaji wa kifedha na
kibajeti. 3.3.2 Mwanasheria Mkuu: Mwanasheria Mkuu wa
Serikali atatoa ushauri wa kisheria wakati mchakato wa mkataba wa mkopo ili kuhakikisha kwamba unaenda sambamba na sheria za nchi.
3.4 Ukopaji wa Makampuni ya Umma: Serikali lazima ianzishe utaratibu na vigezo kwa ajili ya kutoa dhamana kwa makampuni ya Umma. Hii ni muhimu kwasababu endapo makampuni ya Umma yatashindwa kulipa riba
na gharama za madeni, serikali itatakiwa kulipa.
15
KAnUni nA MiOngOzO yA UKOPAji hURU WA FeDhA KWA nchi zA AFRiKA
3.5 jukumu la Benki Kuu: Benki Kuu itapaswa kufanya kazi
kama mshauri wa kifedha wa serikali kwenye masuala
ya mikataba ya mikopo na kusimamia madeni.
3.5.1 Sheria ya nchi inatakiwa ionyeshe wazi
madaraka ya Benki Kuu, uhusiano wake na Wizara
ya Fedha, uhuru wake, uwajibikaji wake kwa Bunge
na Taifa, tahadhari lazima ichukuliwe ili kuepuka
udhalimu/matumizi mabaya ya madaraka kama hayo.
3.5.2 Benki Kuu inatakiwa kudumisha mfumo
salama na madhubuti wa malipo na ulipaji.
3.5.3 Benki Kuu itapaswa kupata maelezo yote ya
mali fedha za serikali na taasisis zake kutoka kwenye
taasisi za fedha na kuziwasilisha kwenye Ofisi ya
Madeni na Wizara ya Fedha.
3.5.4 Benki Kuu itapaswa kuwezesha ulipaji wa
madeni kwa kufuata ushauriwaOfisi yaUsimamizi
wa Madeni.
3.6 Mkaguzi Mkuu wa hesabu:OfisiyaMkaguziMkuuwa hesabu itawajibika kukagua taarifa za madeni ya
umma zilizowekwa wazi kwenye taarifa za fedha za
serikali au nyaraka nyingine ambazo kiasi cha deni
la Umma limeonyeshwa na kuhakikisha kuwa kiasi
kimeonyeshwa/wakilishwa katika misingi sahihi.
MKATABA WA KUKOPA
16
3.6.1 Mkaguzi Mkuu wa Hesabu lazima awezeshwe
vizuri na aripoti kwa wakati kuhusu akaunti ya umma
ya nchi.
3.6.2 Mkaguzi Mkuu wa Hesabu atafanya uchambuzi
huru na kuhakikisha kwamba taarifa zinawekwa
bayana kwa umma na bodi muhimu au makundi ili
kuwezesha usimamizi wa madeni ulioboreshwa na
uelewa wa athari za kujifunga kifedha za sasa na za
baadaye. Mkaguzi Mkuu wa Hesabu lazima afanye
kaguzi kuhakikisha ufuatiliaji wa vigezo vya biashara za
kifedha vilivyowekwa kwenye usimamizi wa madeni.
3.7 Mhasibu Mkuu: Ofisi ya Mhasibu Mkuu itatoamiongozo na taratibu kwa ajili ya usimamizi wa fedha
za umma.Ofisi yaMhasibuMkuu inapaswa kuweka
mfumo wa jumla wa udhibiti na utumiaji wa rasilimali
za umma.
3.8 Taasisi za Fedha za Kimataifa/wakopeshaji: Taasisi
za fedha za Kimataifa kwa kutumia Miongozo ya
Usimamiaji wa Madeni ya Umma ya Kundi la IMF/
Benki ya Dunia lazima ziwezeshe ushauri wa kitaalamu
kwa nchi, mara kwa mara kusisitiza haja ya madeni
endelevu na kuwezesha utekelezaji wenye ufanisi wa
mipango ya uchumi.
17
KAnUni nA MiOngOzO yA UKOPAji hURU WA FeDhA KWA nchi zA AFRiKA
3.8.1 Uwezo wa ufadhili wa ndani: Taasisi za Fedha
za Kimataifa zisaidie katika kujenga na kuimarisha
uwezo wa ndani wa kufanya tafiti ambazo zitaarifu
mchakato wa kutengeneza sera.
MKATABA WA KUKOPA
18
4 UWEPO WA OFISI HURU YA USIMAMIZI WA MADENI
4.1 Mfumo wa Usimamizi wa Madeni: Kwa madhumuni ya kuwa na mfumo mzuri wa uratibu wa mikataba ya mikopo na usimamizi wa madeni serikali inabidi ianzisheOfisi yaUsimamiziwaMadeni. Shughuli zaUsimamiziwaMadenilazimaziwekwechiniyaOfisimoja ya Usimamizi wa Madeni yenye majukumu ya nyuma, kati na ya mbele ya kiofisi.Wakati ofisiya mbele itashughulika na sera za madeni, sera za kukopa, taratibu na mbinu za kujadiliana, uelewa wa kitaaluma, ofisi ya kati itajikita kwenye kitengo chauchambuzi/upembuzi na athari, umuhimu wa mkopo uliopendekezwawakatiofisiyanyumaitajishughulishana utunzaji wa takwimu, ukuaji wa mikopo, uthibitishaji wa taarifa za madeni, misaada na masharti.
4.2 Uratibu wa Madeni yote: Ofisi ya Usimamizi waMadeni inaiwezesha nchi kuunganisha, kupanga na kuimarisha shughuli zote za usimamizi wa madeni kwenye chombo kimoja maalumu kilicho huru. Hii inaruhusu mpangilio mzuri wa udhibiti na inaondoa mwingiliano na kujirudia kunakohusiana na ushirikishwaji wa mawakala wengi, na ambapo usambaaji wa habari ni dhaifu na unaratibiwa vibaya.
19
KAnUni nA MiOngOzO yA UKOPAji hURU WA FeDhA KWA nchi zA AFRiKA
4.3 Mfumo wa Taarifa za Usimamizi wa Madeni: ShughulinajukumulaOfisiyaUsimamiziwaMadenivinapaswa kuwa vimeandikwa vizuri na kuwekwa kwenye nyaraka, ikiwa na kitabu cha muongozo, ikiwa ni pamoja na program muhimu za usimamizi za komputa.
4.4 Uwepo wa huduma za Kitaalamu: Ofisi huru yaUsimamizi wa madeni ya umma (DMOs) itoe faida za kipekee za kiutawala na utumishi na ubadilikaji ambao siowa kawaida kwaofisi/vitengo vya usimamiziwamadeni ambavyo ‘vimeingizwa’ kwenye wizara za fedha na/Benki Kuu.
4.5AinayaOfisiyaUsimamiziwaMadeni: Jukumu la Ofisi yaMadeni linategemeana na shughuli zake zausimamizi wa madeni, kama majukumu inayopangiwa na sheria na taratibu, kwenye mkakati inayochagua kuufuata na kwenye njia ilizowekewa kuyafikiamalengo yake. Ili kuhakikisha kwamba michakato ya usimamizi wa madeni, kama vile ulipaji wa madeni inafanyika kwa ufanisi zaidi; wajibu na majukumu lazima yawe wazi na taarifa za madeni lazima ziwe zimeimarishwa.
MKATABA WA KUKOPA
20
5 USHIRIKI WA UMMA, UJUMUISHWAJI NA KUWEKA TAARIFA HADHARANI
5.1 Umiliki na Uwajibikaji: Umiliki wa Kitaifa ni muhimu
kwa mafanikio ya miradi yote ya maendeleo
inayofadhiliwa kwa mikopo na ruzuku. Watu, ambao
wanapaswa kuwa walengwa wa mwisho wa mikopo
iliyochukuliwa kwa jina lao, lazima wawe na haki ya
kushiriki katika mchakato wa kufanya maamuzi ya
yanayohusu kukopa kwa umma. Hili lifanyike kupitia
uwakilishi wa bunge, ushiriki wa raia wa moja kwa
moja au ushiriki wa raia kupitia asasi za kiraia au
uwakilishaji. Asasi za kiraia, hasa waangalizi na makundi
yenye maslahi, yanapaswa kutambuliwa kama njia za
kuimarisha umiliki wa fedha za umma na uwajibikaji.
5.2 Uwazi na ushirikishaji wa wananchi kikamilifu: Mchakato wa mkataba wa mkopo lazima uwe wa
uwazi na shirikishi, ukiwashirikisha wananchi na
jamii zinazoathirika kwa kuwapa taarifa na muda wa
kutosha kujadili uchukuaji wa mkopo, ikiwa ni pamoja
na kusudi na masharti ya mkopo kwa mujibu wa
katiba ya nchi.
21
KAnUni nA MiOngOzO yA UKOPAji hURU WA FeDhA KWA nchi zA AFRiKA
5.3 Kutambuliwa asasi za Kiraia Kisheria na Kitaasisi: Serikali zilizokubaliana na Mkataba huu zianzishe
mabaraza na taratibu ambazo wananchi kwa kupitia
hayo mabaraza na hizo taratibu wanaweza kujadili
na kushawishi mapendekezo ya sera za kiuchumi
kuimarisha umiliki wa umma wa mikakati ya uchumi
na madeni. Sheria za serikali lazima zionyeshe wazi
kwamba hii asasi ya kiraia ita:
5.3.1 Kuwa na jukumu la kushauri katika mchakato
wa mkataba wa mkopo na usimamizi wa madeni
ikifanya kama wataalamu ikifanya kazi kwa karibu na
wanaoongoza majadiliano na serikali kwa kushawishi
maamuzi ya kisera, kwa kutoa ushauri wa kisheria,
kitaalamu au kiufundi.
5.3.2 Fanya tafiti na uhamasishaji wakati wa
kutengeneza mapendekezo ya mradi/programu
na kwenye hatua za majadiliano ya makubaliano ya
mkopo.
5.3.3 Fuatilia miradi na mipango ya maendeleo,
ikiwa ni pamoja na namna inavyofadhiliwa. Hii
inaruhusu asasi za kiraia kufuatilia matokeo ya miradi
na programu zinazofadhiliwa na mikopo, pamoja na
fedha zilizotolewa kama matokeo ya mipango ya
msamaha wa madeni.
MKATABA WA KUKOPA
22
5.3.4 Hamasisha umma na ongeza ufahamu juu ya
masuala ya mikopo, ruzuku na masuala ya fedha za
maendeleo.
5.4 Utoaji wa taarifa kwa umma: Sheria ya Serikali ya
Fedha za Umma na uwajibikaji ieleze bayana kuwa
taarifa za matumizi ya fedha za mikopo ziwekwe
wazi kwa umma, hasa makundi ya kiraia, yenye nia
ya kufuatilia mikopo na ruzuku za serikali. Mkataba
wa mkopo uwekwe wazi kwa umma na usambazwe
kwa wadau mbalimbali kwa kutumia njia sahihi za
mawasiliano na zinazopatikana chini. Hii inaweza kuwa
kupitia kwa wabunge, matangazo kwa njia ya tovuti,
vyombo vya habari vya taifa, radio na/au televisheni.
5.5 Lugha: Mkataba upatikane kwa lugha kuu za Taifa
(ikiwa ni pamoja na lugha za jumuiya zilizoathirika).
Matoleo yote mawili toleo kuu na lililotafsiriwa yawe
na uhalali sawa mahakamani.
23
KAnUni nA MiOngOzO yA UKOPAji hURU WA FeDhA KWA nchi zA AFRiKA
6 KUHESHIMU BINADAMU NA HAKI ZA WATU ZA KIIKOLOJIA
6.1 haki ya Umma ya Maendeleo endelevu: Sambamba
na mkataba wa Afrika Haki za Binadamu serikali
zihakikishe kuwa wananchi wanayo haki ya kupata
kikamilifu haki yao ya maendeleo endelevu kutoka
kwenye rasilimali madeni. Haki ya maendeleo na
uchumi zisitengwe na haki za kijamii, kisiasa na
kitamaduni.
6.2 Kukabili madhara ya Kukopa: Serikali ihakikishe
kwamba madhara ya kukopa na athari zozote za
utekelezaji wa miradi ya maendeleo vinapunguzwa
mpaka kiwango cha chini kwa watu wa kawaida hasa
makundi maalumu kama vile wanawake na watoto.
Miradi inayofadhiliwa kwa madeni lazima isikiuke haki
za binadamu na wala isichangie ukiukwaji wa haki za
binadamu. Haki hizi zimebainishwa kwenye Mikataba
na makubaliano yanayotambulika kimataifa ya Haki
za Binadamu ambayo wakopaji au wakopeshaji
wamesaini.
MKATABA WA KUKOPA
24
6.3 Uhamishaji: Miradi mikubwa ya maendeleo kwa hali
yoyote ile lazima iepuke kuwa chanzo cha uhamishaji
wa wazawa, masikini wa vijijini na wale wa kwenye
makazi duni mijini kwenye ardhi yao, chanzo cha
kipato na jamii. Iwapo miradi ya maendeleo kwa
sababu yoyote itasababisha uhamishaji wa watu
kutokakwenyemakaziyaofidiastahiliitatolewakwa
jamii zilizoathiriwa.
6.4 Uharibifu wa Mazingira: Ukopaji wowote wa Umma
ni lazima usikubali miradi inayokiuka viwango vya
chini vinavyokubalika kimataifa vya utunzaji/ulinzi wa
jamii, kazi na mazingira.
25
KAnUni nA MiOngOzO yA UKOPAji hURU WA FeDhA KWA nchi zA AFRiKA
7 KUHESHIMIANA NA USAWA KATIKA UBIA NA WAKOPESHAJI NA WAFADHILI WA KIMATAIFA
7.1 Kuheshimiana: Serikali zitahakikisha kuwa uingiaji
wa mikataba ya mikopo na masuala ya usimamizi wa
madeni na wakopeshaji yanafanyika kwa kuheshimiana
na utu. Kanuni za msingi za Ufanisi wa Msaada
kwenye Azimio la Paris ya mwaka 2005, Ajenda ya
Accra ya mwaka 2008 na Ushirikiano wa Busan kwa
Ushirikiano Madhubuti wa Maendeleo ya mwaka 2011
lazima zitumike kuhakikisha usawa katika ushirikiano
kati ya wafadhili na mataifa yanayokopa.
7.2 Kukataa Masharti: Nchi wanachama wa Mkataba huu
lazima wakatae utumiaji wa masharti wa wafadhili na
taasisi za fedha za kimataifa wanapokopa fedha. Hii
huwasababishia kuwajibika kwa wakopeshaji na sio
kwa wananchi wao.
MKATABA WA KUKOPA
26
7.3 Kuheshimu na Kuwezesha Taasisi za ndani: Wafadhili
na Wakopeshaji wote wanapaswa kuvipatia vyombo
vya uangalizi vya serikali na mabunge msaada wa
kifedha na kitaalamu kuviwezesha kushiriki kikamilifu
katika kujadili na kufuatilia mikopo ya nje.
7.4 Usuluhishi wa haki na Uwazi: Mkataba wa mkopo
lazima uwe na kifungu kwa ajili ya utaratibu wa
usuluhishi huru na wazi iwapo kutakuwa na ugumu
katika ulipaji au mgogoro (kwa ombi la mkopaji au
mkopeshaji). Kutakuwa na usubirishaji wa ulipaji
wa deni wakati majadiliano yakiendelea. Mkopaji
asifunguliwe kesi mahakamani wakati majadiliano
yanaendelea. Wakopaji na Wakopeshaji lazima
wakubaliane na uamuzi wa msuluhishi huru na kuna
haki ya kukata rufaa.
27
KAnUni nA MiOngOzO yA UKOPAji hURU WA FeDhA KWA nchi zA AFRiKA
MAREJEO NA USOMAJI NA ZIADA
1. AFRODAD (2007) “The Loan Contraction Process in Africa: Making
Loans Work for the Poor: The Case of DRC,” Study Report
2. AFRODAD (2007) “The Loan Contraction Process in Africa: Making
Loans Work for the Poor: The Case of Malawi,” Study Report
3. AFRODAD (2007) “The Loan Contraction Process in Africa: Making
Loans Work for the Poor: The Case of Tanzania,” Study Report
4. AFRODAD (2007) “The Loan Contraction Process in Africa: Making
Loans Work for the Poor: The Case of Mozambique,” Study Report
5. Borresen P and Pascal E.C (2001); “Role and organization of a debt
office”,Proceedingsofthesecondinter-regionaldebtmanagement
conference, United Nations Conference on Trade and Development,
pp33-53.
6. Chadambuka. Z.T. (2009) A Critical Review of the Legal Framework
of the Public Loan Contraction and Debt Management System in
Zimbabwe. ZIMCODD, Harare.
7. Mutasa, C. (2007) ‘Operationalizing debt sustainability’ in UNCTAD
(2007) Proceedings of the Fifth Inter-regional Debt Management
Conference, UN, Geneva.
MKATABA WA KUKOPA
28
8. De Renzio, P and Krafchik,W. (2007) “Lessons from the field:
The impact of Civil Society Budget Analysis and Advocacy in Six
Countries”, A Practitioners’ Guide, International Budget Project,
Washington D.C. International Budget Project.
9. Fyson, S (2009) “Sending in the Consultants: development agencies,
theprivatesectorandthereformofpublicfinanceinlow-income
countries,” International Journal of Public Policy, Vol.4 n. ½.
10. Krafchik, W (2003) “What role can Civil Society and Parliament
Play in Strengthening the External Auditing Function?” International
Budget Project, Washington D.C. International Budget Project.
11. Maruping. A.M. (2003) ‘ Public Debt Sustainability and the
development of domestic markets’ in UNCTAD (2003) Proceedings
of the Fifth Inter-regional Debt Management Conference and
WADMO conference, UN, Geneva.
12. MEFMI (2004) Towards an Effective national debt management
strategy in Tanzania, Workshop on Debt Management, Dar es Salaam,
United Republic of Tanzania.
13. MEFMI (2005) MEFMI, Public Debt Management Procedures Manual
vol 1. Sable Press (PVT) Ltd, Harare.
14. Meja,V.(2008)ThePublicLoanContractionProcess-AkeytoDebt
Management and Economic Governance, AFRODAD. Harare.
15. OverseasDevelopmentInstitute(2007)“Reformingpublicfinancial
management when the politics aren’t right: A proposal,” Opinion
Paper 89, London.
29
KAnUni nA MiOngOzO yA UKOPAji hURU WA FeDhA KWA nchi zA AFRiKA
16. UNCTAD (2007) Proceedings of the Fifth Inter-regional Debt
Management Conference, UN, Geneva.
17. UNCTAD (2003) Proceedings of the Fifth Inter-regional Debt
Management Conference and WADMO conference, UN, Geneva.
18. United Republic of Tanzania (2004) Governments Loans, Guarantees
and Grants Act, 1974 and Amendments 2004
19. UNITAR (2002) Institutional Framework for Public Sector
Borrowing, UNITAR Training Programmes in the Legal Aspects and
Financial Management, Document No.17. Geneva.
MKATABA WA KUKOPA
30
KWA TAARiFA zAiDi WASiLiAnA nAAfrican Forum and Network on Debt and
Development (AFRODAD)
31 Atkinson Drive, Hillside
S.L.P. CY1517, Causeway
Harare, Zimbabwe
Simu: +263 4 778531/6
Nukushi: +263 4 747878
Tovuti: www.afrodad.org
Barua pepe: [email protected]