juni 15, 2013 34567 - download.jw.orgdownload.jw.org/files/media_magazines/ad/w_sw_20130615.pdf ·...

Download JUNI 15, 2013 34567 - download.jw.orgdownload.jw.org/files/media_magazines/ad/w_SW_20130615.pdf · HILO ni mojawapo ya mambo ya zamani zaidi ninayokumbu-ka kumhusu baba yangu, mwanamume

If you can't read please download the document

Upload: lethu

Post on 06-Mar-2018

826 views

Category:

Documents


101 download

TRANSCRIPT

  • MAKALA ZA FUNZO

    AGOSTI 5-11

    Thamini KikamiliSifa za YehovaUKURASA WA 7 NYIMBO: 69, 89

    AGOSTI 12-18

    Thamini Ukarimuna Usawazikowa YehovaUKURASA WA 12 NYIMBO: 22, 110

    AGOSTI 19-25

    ThaminiUshikamanifuna Msamahawa YehovaUKURASA WA 17 NYIMBO: 63, 77

    AGOSTI 26SEPTEMBA 1

    Acha Nidhamuya YehovaIkufinyangeUKURASA WA 24 NYIMBO: 120, 64

    34567JUNI 15, 2013

  • Gazeti hili haliuzwi. Ni sehemu ya kazi ya elimu ya Bib-

    lia ya ulimwenguni pote inayotegemezwa kwa michango

    ya hiari. Isipokuwa iwe imeonyeshwa vingine, Maandiko

    yamenukuliwa kutoka katika Biblia TakatifuTafsiri ya

    Ulimwengu Mpya.

    The Watchtower (ISSN 0043-1087) is published

    semimonthly by Watchtower Bible and Tract Society of

    New York, Inc.; L. Weaver, Jr., President; G. F. Simonis,

    Secretary-Treasurer; 25 Columbia Heights, Brooklyn,

    NY 11201-2483, and by Watch Tower Bible and Tract

    Society of South Africa NPC, 1 Robert Broom Drive

    East, Rangeview, Krugersdorp, 1739. 2013 WatchTower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Haki

    zote zimehifadhiwa. Printed in South Africa.

    34567 June 15, 2013Vol. 134, No. 12 Semimonthly SWAHILI

    MAKALA ZA FUNZO

    Thamini Kikamili Sifa za Yehova

    Thamini Ukarimu na Usawaziko wa Yehova

    Thamini Ushikamanifu na Msamahawa Yehova

    Wakristo wengi hufikiri kwamba Yehova ana sifa nne kuu pekee.

    Lakini makala hizi tatu zitatusaidia kuthamini zaidi sifa kadhaa za

    Yehova ambazo watu hawajifunzi mara nyingi. Kuhusu kila sifa, tu-

    tajibu maswali haya: Inamaanisha nini? Yehova anaionyeshaje?

    Na tunawezaje kumwiga Yehova katika kuonyesha sifa hiyo?

    Acha Nidhamu ya Yehova Ikufinyange

    Maandiko yanapoeleza kwa njia ya mfano kuhusu mamlaka ya Ye-

    hova juu ya wanadamu akiwa mwenye enzi kuu, yanamwita Yehova

    Mfinyanzi wetu. (Isa. 64:8) Makala hii inaonyesha mambo tuna-

    yoweza kujifunza kumhusu huyo Mfinyanzi Mkuu kutokana na jinsi

    alivyowafinyanga watu mmoja-mmoja na mataifa nyakati za kale.

    Inazungumzia pia jinsi tunavyoweza kunufaika anapotufinyanga

    leo.

    PIA KATIKA TOLEO HILI

    3 Kumtii Yehova Kumeniletea Baraka Nyingi

    22 Maswali Kutoka kwa Wasomaji

    29 WazeeJe, Mtaiburudisha Nafsi Iliyochoka?

    32 Je, Unakumbuka?

    UJERUMANI

    JALADA: Kuhubiri barabarani katika eneola umma huko Frankfurt, Ujerumani

    IDADI YA WATU

    81,751,600MASHAHIDI

    162,705MAFUNZO YA BIBLIA

    74,466HUDHURIO LA UKUMBUSHO MWAKA WA 2012

    265,407

    MAMILIONI YA VITABU AMBAVYOVIMECHAPISHWA NA OFISI YA TAWI YAUJERUMANI KATIKA MUDA WA MIAKA 25

    M20

    M15

    M10

    M5

    02010

    20

    05

    20

    00

    19

    95

    19

    90

    19

    85

  • HILO ni mojawapo ya mambo ya zamani zaidi ninayokumbu-ka kumhusu baba yangu, mwanamume mnyenyekevu namwenye bidii ya kazi. Alipenda sana haki, kwa hiyo alivutiwamara moja na ujumbe wa Biblia alipousikia katika mwaka wa1953. Tangu wakati huo na kuendelea, alifanya yote aliyowe-za ili kutufundisha tukiwa watoto mambo aliyokuwa akijifu-nza. Mwanzoni mama yangu alisita kuacha desturi za dini yaKatoliki. Hata hivyo, baada ya muda yeye pia akaanza kutha-mini mafundisho ya Biblia.

    Ilikuwa vigumu kwa wazazi wetu kutufundisha Biblia kwakuwa Mama hakujua kusoma wala kuandika vizuri, naye Babaalifanya kazi ngumu kwa saa nyingi shambani. Pindi nyinginealichoka sana hivi kwamba alisinzia wakati wa funzo. Hata hi-vyo, jitihada zake hazikuwa za bure. Nilikuwa mtoto wa kwa-nza katika familia yetu, hivyo, niliwasaidia wazazi wangu ku-mfundisha dada yangu na ndugu zangu wawili. Hilo lilitiandani jambo fulani alilotaja Baba mara nyingi, yaani, upendowa Noa kwa familia yake, aliouonyesha kwa kumtii Mungu.Nilipenda sana simulizi hilo la Biblia! Baada ya muda mfupi,sote tulikuwa tukihudhuria mikutano katika Jumba la Ufalmehuko Roseto degli Abruzzi, mji ulio kwenye pwani ya Adriati-ki nchini Italia.

    Nilikuwa na umri wa miaka 11 tu katika mwaka 1955 nili-povuka na mama yangu milima iliyo magharibi mwa nchi ilikuhudhuria kusanyiko letu la kwanza la wilaya huko Rome.Tangu wakati huo, nimeyaona makusanyiko hayo makubwakuwa mojawapo ya sehemu zinazopendeza zaidi za maisha yaMkristo.

    Mwaka uliofuata nilibatizwa, na baada ya muda mfupi ni-kaanza utumishi wa wakati wote. Nilipokuwa na umri wa mia-ka 17, niliwekwa rasmi kuwa painia wa pekee katika jiji la Lati-na, upande wa kusini wa jiji la Rome, kilomita 300 hivi kutokanyumbani. Lilikuwa jiji jipya, hivyo hakuna yeyote aliyehofusana maoni ya jirani zake. Mimi na painia mwenzangu tulifu-rahia sana kuwaachia watu machapisho mengi ya Biblia, hatahivyo, kwa kuwa nilikuwa na umri mdogo, nilitamani sana ku-rudi nyumbani! Lakini, niliazimia kutii agizo nililopewa.

    SIMULIZI LA MAISHA

    KumtiiYehovaKumenileteaBarakaNyingiLIMESIMULIWA NA

    ELISA PICCIOLI

    Tunajifunza somo zuri kama nini kutoka kwaNoa! akasema baba yangu. Noa alimtii Yehovana kuipenda familia yake, na wote waliokokaGharika kwa sababu familia yote iliingia ndaniya safina.

    JUNI 15, 2013 3

  • 4 MNARA WA MLINZI

    Baadaye nilipewa mgawo wa kusaidia kufanya ma-tayarisho ya Kusanyiko la Kimataifa la mwaka 1963lenye kichwa Habari Njema za Milele, lililofanywakatika jiji la Milan. Katika kusanyiko hilo, nilifanyakazi nikiwa mjitoleaji pamoja na wengine wengi, ku-tia ndani Paolo Piccioli, ndugu kijana kutoka Flor-ence. Siku ya pili ya kusanyiko, alitoa hotuba yenyekuchochea sana kuhusu useja. Ninakumbuka niki-waza hivi, Bila shaka ndugu huyu hataoa kamwe.Hata hivyo, tulianza kuandikiana barua na baada yamuda ikawa wazi kwamba mapendezi yetu mengi ya-lifanana, yaani, tulikuwa na miradi ileile, sote tuli-mpenda Yehova, na tulitaka sana kumtii. Nilifungandoa na Paolo mwaka wa 1965.

    KUPAMBANA NA MAKASISI

    Nilitumikia kwa miaka kumi nikiwa painia wa ka-waida katika jiji la Florence. Lilikuwa jambo lenyekusisimua kuona ongezeko katika makutaniko nahasa kuona vijana wakifanya maendeleo. Mimi naPaolo tulifurahia kutumia wakati wetu pamoja naokuzungumzia mambo ya kiroho na kufurahia tafrija,na katika pindi hizo Paolo alicheza mpira wa miguu.Ni kweli kwamba nilithamini kutumia wakati pamo-ja na mume wangu, lakini niliona wazi kwamba vija-na hao na familia katika kutaniko zilihitaji na zili-faidika Paolo alipotumia wakati wake kuwa nao nakupendezwa nao kwa fadhili.

    Bado mimi hupata shangwe ninapokumbuka mafu-nzo mengi ya Biblia tuliyoongoza. Nilijifunza na Adria-na, aliyezungumza na familia mbili kuhusu mamboaliyokuwa akijifunza. Familia hizo zikapanga tuwe namkutano na kasisi ili kuzungumzia mafundisho ya ka-nisa kama vile Utatu na kutokufa kwa nafsi. Makasisiwatatu walifika katika mkutano huo. Maelezo yao ku-husu mafundisho hayo hayakueleweka na yalipinga-na, jambo lililogunduliwa kwa urahisi na wanafunziwetu wa Biblia walipolinganisha maelezo hayo na ma-fundisho ya Biblia yaliyo wazi. Kwa kweli, mkutanohuo ulileta mabadiliko makubwa. Baada ya muda, wa-shiriki 15 hivi wa familia hizo wakawa Mashahidi.

    Ni kweli kwamba siku hizi tunatumia njia tofau-ti kabisa za kuhubiri. Wakati huo, Paolo alikuwamtaalamu wa kupambana na makasisi, naye alipa-mbana nao mara kadhaa. Ninakumbuka mkutanommoja uliofanywa mbele ya wasikilizaji wasio Ma-shahidi. Yaonekana kwamba wapinzani walipangamapema wasikilizaji fulani waulize maswali ya ubi-shi. Hata hivyo, mambo hayakuwa hivyo. Mtu mmo-ja aliuliza ikiwa ni jambo linalofaa kwa kanisa kuji-husisha na siasa kama lilivyofanya kwa karne nyingi.Wakati huo, ilikuwa wazi kwamba makasisi waliku-wa mashakani. Kwa ghafla, taa zikazima na mkutanoukavunjwa. Miaka mingi baadaye tukajua kwambamakasisi ndio waliopanga kuzima taa ikiwa mazu-ngumzo hayangeenda kama walivyopanga.

    Siku yetu ya harusi Tulifurahia sana kutumia wakati wetu pamoja na vijana,na katika pindi hizo Paolo alicheza mpira wa miguu

  • MAPENDELEO MAPYA YA UTUMISHI

    Miaka kumi baada ya kufunga ndoa na Paolo, tuli-pewa mgawo wa kuzungukia makutaniko. Paolo ali-kuwa na kazi nzuri hivyo haikuwa rahisi kukubalimgawo huo. Hata hivyo, baada ya kutafakari na ku-sali kuhusu jambo hilo, tulikubali mgawo huo mpyawa utumishi. Tulifurahia kukaa pamoja na familia zi-lizotukaribisha. Mara nyingi tulijifunza jioni tukiwakikundi, kisha Paolo aliwasaidia watoto kufanya kaziza shule hasa hesabu. Zaidi ya hayo, Paolo alikuwamsomaji mwenye bidii na aliwaambia wengine kwamsisimko mambo yenye kuvutia na yenye kujengaaliyosoma. Mara nyingi tulienda kuhubiri katika mijiisiyo na Mashahidi kila Jumatatu, tukiwaalika watuili waje kusikiliza hotuba jioni.

    Baada ya miaka miwili tu katika kazi ya mzungu-ko, tulialikwa kutumikia Betheli katika jiji la Rome.Paolo alipewa mgawo katika idara ya sheria, na miminilipewa mgawo katika Idara ya Magazeti. Badilikohilo halikuwa rahisi, lakini tuliazimia kuwa watiifu.Ilisisimua kuona upanuzi wa hatua kwa hatua wa ofi-si ya tawi na ongezeko kubwa la ndugu zetu nchiniItalia. Wakati huo ndipo Mashahidi wa Yehova wali-potambuliwa kisheria nchini Italia. Bila shaka, tulifu-rahia utumishi huo.

    Tulipokuwa tukitumikia Betheli, msimamo wetuunaotegemea Biblia kuhusu damu ulijaribiwa Italia.Mwanzoni mwa miaka ya 1980, kulikuwa na kesi

    kuhusu suala hilo iliyosababisha upinzani mkubwasana. Wenzi fulani wa ndoa waliokuwa Mashahi-di, walishtakiwa kwa uwongo kwamba walisababi-sha kifo cha binti yao, ingawa alikufa kutokana naugonjwa fulani mbaya wa damu unaorithiwa na watuwengi wanaoishi katika eneo la Mediterania. Nduguna dada wa familia ya Betheli waliwasaidia mawaki-li waliowatetea wazazi hao Wakristo. Trakti na toleomaalumu la Amkeni! liliwasaidia watu kujua ukweliwa mambo na kuelewa kwa usahihi maoni ya Nenola Mungu kuhusu damu. Katika miezi hiyo, mara nyi-ngi Paolo alifanya kazi kwa saa 16 hivi kwa siku bilakupumzika. Nilifanya yote niwezayo kuunga mkonojitihada zake muhimu.

    BADILIKO LINGINE MAISHANI

    Tulikuwa tumeoana kwa miaka 20 wakati mamboyalipobadilika kwa ghafla. Nilikuwa na umri wa mia-ka 41 naye Paolo alikuwa na miaka 49 nilipomwa-mbia ninahisi kwamba nina mimba. Aliandika hivikatika kitabu chake cha kumbukumbu siku niliyo-mwambia kuhusu hali yangu: Sala: Ikiwa ni kweli,tusaidie tubaki katika utumishi wa wakati wote, tusi-punguze bidii yetu ya kiroho, na tuwe wazazi wazurikupitia mfano wetu. Zaidi ya yote, nisaidie nitendeangalau asilimia 1 ya yote niliyosema jukwaani kati-ka kipindi cha miaka 30 hivi iliyopita. Ninapoanga-lia maisha yetu, ni wazi kwamba Yehova alijibu salayake na yangu.

    Paolo alipenda kazi yake BetheliMara nyingi Ilaria alisema, Baba ndiye rafiki yangu bora zaidi

  • Maisha yetu yalibadilika sana baada ya kumzaaIlaria. Kwa kweli, pindi nyingine tulivunjika moyokama Methali 24:10 inavyosema: Je, umejionyeshakuwa umevunjika moyo siku ya taabu? Nguvu zakozitakuwa chache. Hata hivyo tulitegemezana hukutukikumbuka umuhimu wa kutiana moyo.

    Ilaria husema bila kusita jinsi anavyofurahi kuwana wazazi wawili Mashahidi waliokuwa na mengi yakufanya katika utumishi wa wakati wote. Hajawa-hi kamwe kuhisi kwamba anapuuzwa, badala yakealikua katika familia yenye hali za kawaida kabi-sa. Nilikaa naye wakati wa mchana. Paolo aliporudinyumbani jioni, mara nyingi alihitaji kumalizia kazifulani; hata hivyo, alitumia wakati wake pamoja naIlaria, akicheza naye na kumsaidia kazi za shule. Ali-fanya hivyo hata kama ingemaanisha kwamba ange-hitaji kuendelea na kazi yake hadi saa nane au saatisa usiku. Mara nyingi Ilaria alisema, Baba ndiye ra-fiki yangu bora zaidi.

    Kama ujuavyo, tulihitaji kuwa na msimamo thabi-ti ili kumsaidia Ilaria kubaki katika njia ya Kikristo.Nakumbuka pindi moja alitenda isivyofaa alipokuwaakicheza na rafiki yake. Tulitumia Biblia kumwelezakwa nini hapaswi kutenda hivyo. Pia tukamwambiaamwombe msamaha rafiki yake mbele yetu.

    Ilaria husema wazi jinsi anavyothamini sana upe-ndo ambao wazazi wake walionyesha kwa ajili ya hu-duma. Kwa kuwa sasa ameolewa, anaelewa vizuri

    hata zaidi umuhimu wa kutii na kufuata mwongozowa Yehova.

    TULITII HATA NYAKATI ZA HUZUNI

    Mwaka wa 2008, Paolo alijua kwamba ana ugo-njwa wa kansa. Mwanzoni ilionekana kwamba ange-pona ugonjwa huo, naye alinitia moyo sana. Mba-li na kutafuta matibabu bora zaidi, mimi na Ilariatulitoa sala nyingi ndefu kwa Yehova, tukimwombaatusaidie kukabiliana na hali hiyo. Hata hivyo, nili-shuhudia mwanamume huyo ambaye wakati mmojaalikuwa mwenye nguvu na afya njema, akidhoofikapolepole. Kifo chake katika mwaka wa 2010 kiliku-wa pigo kubwa sana. Hata hivyo, ninafarijiwa sanana tuliyotimiza kwa miaka 45 tuliyokuwa pamoja. Tu-limpa Yehova kilicho bora kabisa. Ninajua kwambakazi yetu ina thamani ya kudumu. Nina hamu ku-bwa ya kumwona Paolo akifufuliwa kama alivyosemaYesu katika Yohana 5:28, 29.

    Moyoni, mimi bado ni yule msichana mdogo ana-yependa sana simulizi la Noa. Azimio langu halija-badilika. Ninataka kumtii Yehova katika kila jambo.Nina uhakika kwamba vikwazo, kujidhabihu, au mi-siba ya aina yoyote ni mambo madogo sana yanapo-linganishwa na baraka nzuri ajabu tunazopewa naMungu wetu mwenye upendo. Mimi binafsi nimejio-nea jambo hilo na ninakuhakikishia kwamba ni mu-himu kuwa na uhakika huo.

    Moyoni, mimi bado ni

    yule msichana mdogo

    anayependa sana

    simulizi la Noa. Azimio

    langu halijabadilika

  • UNAPOFIKIRIA utu wa Yehova, ni sifa gani unazoku-mbuka? Wengi wetu hukumbuka sifa ya upendo, haki,hekima, na nguvu. Hata hivyo, tunajua kwamba Yehovaana sifa nyingi zinazovutia. Kwa kweli, tunaweza kuo-rodhesha sifa zaidi ya 40 za Yehova, na kila sifa imezu-ngumziwa katika machapisho yetu. Hebu wazia hazinaya kweli zenye kuvutia sana kuhusu utu wa Yehova tu-nazoweza kupata kupitia funzo letu la kibinafsi au iba-da ya familia! Tunaweza kunufaika katika njia zipi kwakujifunza sifa hizo? Kufanya hivyo kunaweza kutusai-dia kumthamini zaidi Baba yetu wa mbinguni. Kadiritunavyomthamini Yehova zaidi, ndivyo tamaa yetu yakutaka kumkaribia na kumwiga inavyozidi kuongeze-ka.Yos. 23:8; Zab. 73:28.

    2 Hata hivyo, kuthamini kitu fulani kunamaanishanini? Tutatumia neno hilo katika makala hii kumaani-sha kutambua thamani halisi ya kitu. Uthamini unawe-za kuongezeka hatua kwa hatua. Kwa mfano: Huendauthamini wetu kuelekea chakula ambacho hatujawahikula ukaongezeka tunaposikia harufu yake nzuri, tuna-pokila, na mwishowe tunapokipika wenyewe. Vivyo hi-vyo, tunazidi kuithamini zaidi sifa fulani ya Yehova kwakuijua, kuitafakari, na kuiga sifa hiyo maishani mwe-tu. (Efe. 5:1) Makala hii na makala mbili zinazofuata,zinakusudiwa kutusaidia kuthamini zaidi sifa za Mu-ngu ambazo huenda hatuzikazii sana fikira kama tuna-vyokazia sifa zake kuu. Tutajibu maswali haya tunapo-chunguza kila moja ya sifa hizo: Sifa hiyo inamaanishanini? Yehova anaionyeshaje? Na tunawezaje kumwigaYehova katika kuonyesha sifa hiyo hususa?

    1. (a) Ni sifa gani za Yehova ambazo huenda Mkristo akafikiria?(b) Tutanufaikaje kwa kuchunguza sifa za Mungu?2. (a) Toa mfano unaoonyesha jinsi tunavyoweza kuthamini zai-di sifa za Yehova. (b) Tutachunguza nini?

    THAMINI KIKAMILISIFA ZA YEHOVA

    Iweni waigaji waMungu, kama watotowapendwa.EFE. 5:1.

    UNGEJIBUJE?

    Tunawezaje kuthamini zaidi sifa

    za Yehova?

    Mtu anawezaje kuwa mwenye

    urafiki au mwenye kufikika?

    Tunaweza kuigaje sifa ya Yehova

    ya kutokuwa na ubaguzi?

    7

  • 8 MNARA WA MLINZI

    YEHOVA NI MWENYE URAFIKI

    3 Acheni kwanza tuchunguze sifa yakuwa mwenye urafiki au mwenye kufiki-ka. Ungesema mtu mwenye urafiki ni mtuwa aina gani? Huenda ukasema, Ni mwe-nye fadhili, anayepatikana kwa urahisi, naambaye ni rahisi kuzungumza naye. Maranyingi unaweza kutambua ikiwa mtu nimwenye urafiki au la kwa kusikiliza ana-chosema na kutazama ishara zake za mwilikama vile ishara za mikono, uso, na nyingi-nezo.

    4 Yehova anaonyeshaje kwamba ni mwe-nye urafiki? Ingawa yeye ni Muumba mwe-za-yote wa ulimwengu wote mzima, Yeho-va anatuhakikishia kwamba yuko tayari naanatamani sana kusikiliza na kujibu salazetu. (Soma Zaburi 145:18; Isaya 30:18, 19.)Tunaweza kuongea na Mungu kwa mudamrefu pindi yoyote na mahali popote. Tuna-weza kumfikia kwa uhuru tukijua kwambahatatushutumu kamwe tukifanya hivyo.

    3, 4. (a) Ungesema mtu mwenye urafiki ni mtu waaina gani? (b) Yehova anatuhakikishiaje kwamba nimwenye urafiki au mwenye kufikika?

    (Zab. 65:2; Yak. 1:5) Neno la Mungu li-napoeleza kumhusu Yehova linatumia ma-neno ambayo wanadamu wanaelewa kuo-nyesha kwamba anataka wamkaribie. Kwamfano, mtunga-zaburi Daudi aliandikakwamba macho ya Yehova yanatuelekeana kwamba mkono wake wa kuume una-tushika sana. (Zab. 34:15; 63:8) Nabii Isa-ya alimfananisha Yehova na mchungaji kwakusema hivi: Atawakusanya pamoja wana-kondoo kwa mkono wake; naye atawabe-ba katika kifua chake. (Isa. 40:11) Hebuwazia! Yehova anataka tuwe karibu nayekama mwana-kondoo aliyebebwa kwenyekifua cha mchungaji anayejali. Tuna Babamwenye urafiki kama nini! Tunawezaje ku-mwiga Yehova katika kuonyesha sifa hiyo?

    SIFA YENYE THAMANI SANA

    5 Hivi karibuni, Mashahidi wenye bidiiwanaoishi katika nchi mbalimbali waliuli-zwa hivi: Ni sifa gani unayothamini sanamzee akiwa nayo? Wengi walijibu, Mwe-

    5. Kwa nini ni muhimu wazee wawe wenye ura-fiki?

    Yehova yuko karibu nawote wanaomwitia.Zab. 145:18(Tazama fungu la 9)

    Yehova Mungu wenu hamtendeiyeyote kwa upendeleo.Kum. 10:17(Tazama fungu la 17)

  • JUNI 15, 2013 9

    nye urafiki. Ni kweli kwamba kila Mkri-sto anahitaji kusitawisha sifa hiyo kikamili,hata hivyo ni muhimu hata zaidi kwa wazeekuwa wenye urafiki. (Isa. 32:1, 2) Akielezakwa nini anahisi kwamba sifa hiyo ni mu-himu sana, dada mmoja alisema hivi: Iki-wa mzee ni mwenye urafiki, ndipo tu tu-napoweza kunufaika na sifa nyingine nzuriambazo huenda anazo. Je, unaona umuhi-mu wa maoni hayo? Lakini ni nini kinacho-mfanya mtu kuwa mwenye urafiki?

    6 Siri ya kuwa mwenye urafiki ni kupe-ndezwa kikweli na wengine. Ikiwa mzeeanawajali wengine naye anajitolea kwa hia-ri kuwatumikia, inaelekea kwamba nduguna dada zake, kutia ndani watoto, watao-na mtazamo huo. (Marko 10:13-16) Carlosmwenye umri wa miaka 12 anasema hivi:Mimi huwatazama wazee wa kutaniko ka-tika Jumba la Ufalme wakitabasamu na wa-kiwa wenye fadhili, na jambo hilo linanivu-tia sana. Bila shaka, haitoshi kwa mzee wakutaniko kusema tu kwamba yeye ni mwe-nye urafiki; anapaswa kuonyesha sifa hiyo.(1 Yoh. 3:18) Anawezaje kufanya hivyo?

    7 Fikiria mfano huu. Hivi karibuni, ndu-gu mmoja alikuwa bado amevaa beji yakeya kusanyiko ndani ya ndege alipokuwaakisafiri kurudi nyumbani baada ya kuhu-dhuria kusanyiko katika nchi fulani. Mhu-dumu wa ndege alipoiona beji hiyo iliyo-kuwa na maneno Ufalme wa Mungu naUje! alimwambia hivi ndugu huyo, Ndi-yo, na uje, tunahitaji kuzungumza zaidi ku-husu hilo. Baadaye, walizungumza, namhudumu huyo akakubali papo hapo ma-gazeti yetu. Wengi wetu tumewahi kupatahali kama hiyo. Lakini, kwa nini mara nyi-ngi beji ya kusanyiko huanzisha mazungu-mzo? Kwa sababu kwa njia fulani inawaa-mbia watu: Jihisi huru kunifikia. Niulize

    6. Ni nini siri ya kuwa mwenye urafiki?7. Kwa nini mara nyingi kuvaa beji ya kusanyi-ko huanzisha mazungumzo, na tunajifunza somogani?

    ninaenda wapi. Beji ni ishara inayooneka-na inayowaambia watu kwamba tuko tayarikuzungumza nao kuhusu imani yetu. Vivyohivyo, wazee Wakristo wanapaswa kuonye-sha ishara zinazowaambia hivi waaminiwenzao: Jihisi huru kunifikia. Ni zipi baa-dhi ya ishara hizo?

    8 Huenda desturi zikatofautiana katikanchi mbalimbali, hata hivyo, kwa kawaidatunapotabasamu kwa uchangamfu, tuna-powasalimu kwa shauku na utulivu nduguna dada zetu, tunatoa ishara zinazoonye-sha kwamba tunapendezwa nao kikweli. Ninani anayepaswa kuchukua hatua ya kwa-nza? Fikiria mfano wa Yesu. Mathayo ana-sema kwamba katika mkutano ambao Yesualifanya pamoja na wanafunzi wake, Yesuakakaribia na kuwaambia. (Mt. 28:18)Leo pia wazee huchukua hatua ya kwa-nza kuwafikia na kuongea na waamini we-nzao. Hilo linaweza kuwa na matokeo ganikwa kutaniko? Dada painia mwenye umriwa miaka 88 anasema hivi: Mimi hugu-swa moyo sana na tabasamu changamfu namaneno yenye kutia moyo ninayoambiwana wazee ninapoingia katika Jumba la Ufal-me. Dada mwingine mwaminifu alionge-za hivi: Linaweza kuonekana kuwa jambodogo, lakini mzee anaponikaribisha katikamkutano akitabasamu, ninathamini sanajambo hilo.

    MWENYE URAFIKI NA ANAYEPATIKANA9 Ni wazi kwamba hatuwezi kuwa we-

    nye urafiki ikiwa hatupatikani. Yehova ana-tuwekea mfano bora sana kuhusiana najambo hilo. Hayuko mbali sana na kilammoja wetu. (Mdo.17:27) Njia moja amba-yo wazee wanafanya iwe rahisi kwa wengi-ne kuwafikia ni kutenga wakati kabla na

    8. Wazee huonyeshaje kwamba wanapendezwa ki-kweli na wengine, na hilo lina matokeo gani kwakutaniko?9, 10. (a) Yehova anatuwekea mfano gani bora?(b) Wazee wanawezaje kufanya iwe rahisi kwa we-ngine kuwafikia?

  • 10 MNARA WA MLINZI

    baada ya mikutano ya Kikristo ili kuongeana ndugu na dada zao, vijana kwa wazee.Ndugu mmoja painia alisema hivi: Mzeeanaponiuliza hali yangu na kisha kunisiki-liza kwa subira, ninahisi kwamba ninatha-miniwa. Dada ambaye amekuwa akimtu-mikia Yehova kwa miaka karibu 50 alisemahivi: Wazee wanaotumia muda fulani ku-zungumza nami baada ya mkutano hunifa-nya nihisi ninathaminiwa.

    10 Ni kweli kwamba wachungaji Wakri-sto wanahitaji pia kutimiza majukumu me-ngine. Hata hivyo, lengo lao katika mikuta-no linapaswa kuwa kukazia kwanza fikirakondoo.

    YEHOVA HANA UBAGUZI

    11 Kutokuwa na ubaguzi ni sifa nyingi-ne ya Yehova inayovutia sana. Kutokuwa naubaguzi kunamaanisha nini? Kunatia ndanikutenda kwa haki, kutokuwa au kutoonye-

    11, 12. (a) Kutokuwa na ubaguzi kunatia ndaninini? (b) Yehova anatuwekea mfano gani katika ku-tokuwa na ubaguzi?

    sha ubaguzi au upendeleo. Mtu anawezakuonyesha kikweli kwamba hana ubaguzikwa njia mbili: kupitia mtazamo na mate-ndo yake. Kwa nini yote mawili yanahita-jika? Kwa sababu ikiwa mtu hana ubaguzikatika mtazamo wake atachochewa kuwa-tendea wote bila ubaguzi. Katika Maandikoya Kigiriki ya Kikristo, neno kutobagua,kihalisi linamaanisha kutoangalia nyuso,yaani, kutopendelea uso wa mtu mmoja ku-liko wa mwingine. (Mdo. 10:34; Kingdom In-terlinear) Hivyo, mtu asiye na ubaguzi haka-zii fikira tu sura ya nje ya mtu au hali zake,bali sifa za mtu huyo.

    12 Yehova ndiye mfano bora zaidi katikakutokuwa na ubaguzi. Neno lake linasemakwamba hana ubaguzi naye hamtendeiyeyote kwa upendeleo. (Soma Matendo 10:34, 35; Kumbukumbu la Torati 10:17.) Kisafulani kilichotokea katika siku za Musa ki-naonyesha jambo hilo.

    13 Muda mfupi kabla ya Waisraeli kui-ngia katika Nchi ya Ahadi, dada watanowaseja hawakujua la kufanya. Kwa nini?Walijua kwamba kama familia nyingi-ne za Waisraeli, familia yao pia ingepewaardhi aliyogawiwa baba yao. (Hes. 26:52-55)Hata hivyo, baba yao, Selofehadi wa kabi-la la Manase, alikuwa amekufa. Kulinganana desturi, wana wa Selofehadi ndio walio-paswa kurithi ardhi, hata hivyo, alikuwa namabinti tu. (Hes. 26:33) Kwa sababu fami-lia yao haikuwa na mwana wa kurithi ardhihiyo, je, watu wa ukoo ndio waliopaswa ku-pewa ardhi hiyo na mabinti kuachwa bilaurithi wowote wa familia?

    14 Dada hao watano walimfikia Musa nakumuuliza hivi: Kwa nini jina la baba yetuliondolewe kutoka katikati ya familia yakekwa sababu hakuwa na mwana? Nao wa-kamsihi hivi: Tupe miliki katikati ya ndu-gu za baba yetu. Je, Musa aliwajibu kwa

    13, 14. (a) Binti watano wa Selofehadi walikabi-li hali gani? (b) Yehova alionyeshaje kwamba hanaubaguzi?

    Binti za Selofehadi walithamini sifa yaMungu ya kutokuwa na ubaguzi

    (Tazama fungu la 13 na 14)

  • kusema Sheria hiyo haiwezi kamwe kuba-dilika? Hapana, badala yake aliiwe-ka kesi yao mbele za Yehova. (Hes. 27:2-5) Matokeo yakawa nini? Yehova alimwa-mbia Musa hivi: Binti za Selofehadi wa-nasema jambo lililo sawa. Wape miliki yaurithi katikati ya ndugu za baba yao, naweutaupitisha urithi wa baba yao kwao. Ye-hova alifanya mengi zaidi. Aliongeza jambohilo katika sheria kwa kumwambia Musahivi: Ikiwa mtu yeyote atakufa bila kuwana mwana, mtaupitisha urithi wake kwa bi-nti yake. (Hes. 27:6-8; Yos. 17:1-6) Tanguwakati huo na kuendelea, sheria hiyo inge-walinda wanawake wote Waisraeli walioka-bili tatizo hilo.

    15 Kwa kweli, huo ulikuwa uamuzi we-nye fadhili na usio na ubaguzi kama nini!Yehova aliwatendea kwa heshima wanawa-ke hao waliokuwa na uhitaji kama tu alivyo-watendea Waisraeli wengine waliokuwa nahali nzuri zaidi. (Zab. 68:5) Hilo ni simuli-zi moja tu kati ya masimulizi mengi kati-ka Biblia yanayoonyesha ukweli huu wenyekuchangamsha moyo: Yehova anawatendeabila ubaguzi watumishi wake wote.1 Sam.16:1-13; Mdo. 10:30-35, 44-48.

    TUNAWEZA KUMWIGA YEHOVA

    16 Tunawezaje kuiga sifa ya Yehova ya ku-tokuwa na ubaguzi? Kumbuka kwamba ku-tokuwa na ubaguzi kunatia ndani mambomawili. Tunaweza tu kuwatendea wenginebila ubaguzi ikiwa hatuna ubaguzi. Ni kwe-li kwamba sote hufikiri kuwa tunakubalimaoni ya wengine na hatuna ubaguzi. Hatahivyo, inaelekea utakubali kwamba si ra-hisi sikuzote kuchanganua hisia zetu kwaunyoofu. Basi, tunaweza kufanya nini ili ku-jua ikiwa wengine wanatuona kuwa watu

    15. (a) Yehova anawatendeaje watu wake, hasawenye uhitaji? (b) Ni masimulizi gani mengine yaBiblia yanayoonyesha kwamba Yehova hana uba-guzi?16. Tunawezaje kusitawisha na kuimarisha sifa yakutokuwa na ubaguzi?

    wasio na ubaguzi? Yesu alipotaka kujuamaoni ya watu kumhusu, aliwauliza hivirafiki zake aliowaamini: Watu wanasemaMwana wa binadamu ni nani? (Mt. 16:13, 14) Kwa nini usifuate mfano wa Yesu?Unaweza kumuuliza rafiki unayemwaminiakueleze kwa unyoofu ikiwa una mwelekeowa kutokuwa na ubaguzi. Ufanye nini aki-kuambia kwamba una dalili fulani za uba-guzi wa rangi, jamii, au kiuchumi? Sali kwaYehova kwa bidii kuhusu hisia zako, uki-mwomba akusaidie kurekebisha mtazamowako ili uige kikamili zaidi sifa yake ya ku-tokuwa na ubaguzi.Mt. 7:7; Kol. 3:10, 11.

    17 Katika kutaniko la Kikristo, tunaonye-sha kwamba tunatamani kuiga sifa ya Ye-hova ya kutokuwa na ubaguzi kwa kuwate-ndea kwa heshima na fadhili zenye upendondugu na dada zetu wote. Kwa mfano, ina-pohusu kuonyesha ukarimu, tunapaswakuwaalika waabudu wenzetu wa aina zote,kutia ndani wale wenye malezi tofauti nayetu, maskini, mayatima, au wajane. (SomaWagalatia 2:10; Yakobo 1:27.) Zaidi ya hilo,katika kazi yetu ya kuhubiri kuhusu Ufal-me, tunawatangazia habari njema bila uba-guzi watu wenye malezi mbalimbali, kutiandani wale wanaotoka nchi nyingine. Tuna-furahi sana kwamba tunaweza kupata ma-chapisho ya Biblia katika lugha 600 hivi.Huo ni ushahidi ulio wazi wa sifa ya kuto-kuwa na ubaguzi!

    18 Kwa kweli, kadiri tunavyotumia waka-ti kutafakari sifa ya Yehova ya kuwa mwe-nye urafiki na kutokuwa na ubaguzi, ndivyotunavyozidi kumthamini. Uthamini huowenye kina unapaswa kutuchochea kuigakikamili sifa za Yehova, na kuonyesha sifahizo tunaposhughulika na waamini wenze-tu na wale tunaowahubiria.

    17. Tunaweza kuwatendea wengine bila ubaguzikatika njia zipi?18. Wewe binafsi utaonyeshaje kwamba unatha-mini sifa ya Yehova ya kuwa mwenye urafiki na ku-tokuwa na ubaguzi?

    JUNI 15, 2013 11

  • 12 MNARA WA MLINZI

    MIAKA 35 hivi imepita tangu niolewe, anasema Mkri-sto anayeitwa Monika. Mimi na mume wangu tunajua-na vizuri sana. Hata hivyo, ingawa tumeishi pamoja mia-ka hiyo yote, kila mmoja wetu angali anajifunza mambomapya kuhusu mwenzake, mambo ambayo hatukuya-jua kamwe! Bila shaka, ndivyo mambo yalivyo katikandoa nyingi na kati ya marafiki wengi.

    2 Tunafurahia kuwajua vizuri wale tunaowapenda.Hata hivyo, hakuna urafiki wowote tunaoweza kusitawi-sha ulio muhimu zaidi ya urafiki wetu pamoja na Yeho-va. Hatutawahi kamwe kujua kila kitu kumhusu. (Rom.11:33) Kwa umilele wote, tutakuwa na fursa na shangweya kuthamini hata zaidi sifa za Yehova.Mhu. 3:11.

    3 Makala iliyotangulia ilitusaidia kuthamini zaidi sifaya Yehova ya kuwa mwenye urafiki na kutokuwa na uba-guzi. Acheni sasa tuchunguze sifa nyingine mbili za Ye-hova zenye kuvutia, yaani, ukarimu na usawaziko wake.Tukifanya hivyo, tutaelewa kikamili zaidi kwamba Ye-hova ni mwema kwa wote, na rehema zake ziko juu yakazi zake zote.Zab. 145:9.

    YEHOVA NI MKARIMU

    4 Ni nini maana ya kuwa mkarimu? Yesu alijibu swa-li hilo katika andiko la Matendo 20:35: Kuna furaha zai-di katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea. Kwa ma-neno hayo rahisi, Yesu alifafanua vizuri maana halisi yaukarimu wa kweli. Mtu mkarimu hutumia kwa hiari wa-kati, nguvu, na mali zake kwa faida ya wengine, akifa-nya hivyo kwa shangwe. Kwa kweli, ukarimu haupimwina ukubwa wa zawadi inayotolewa, bali nia ya mtoaji.

    1, 2. Marafiki wa Yehova wana fursa gani?3. Tutachunguza nini katika makala hii?4. Ni nini maana halisi ya ukarimu wa kweli?

    THAMINI UKARIMUNA USAWAZIKOWA YEHOVA

    Yehova ni mwema kwawote, na rehema zakeziko juu ya kazizake zote.ZAB. 145:9.

    UNGESEMA NINI?

    Ni sifa gani mbili za Yehova tuna-

    zoweza kuthamini zaidi?

    Tunaweza kuiga jinsi gani ukari-

    mu wa Yehova?

    Tunaweza kuiga usawaziko wa

    Yehova kwa njia zipi?

  • (Soma 2 Wakorintho 9:7.) Hakuna mtumkarimu zaidi ya Mungu wetu mwenye fu-raha, Yehova.1 Tim. 1:11.

    5 Yehova huonyeshaje ukarimu? Yeye hu-wapa wanadamu wote mahitaji yao, ku-tia ndani wale ambao hawajaanza kumwa-budu. Kwa kweli, Yehova ni mwema kwawote. Yeye hulichomoza jua lake juuya watu waovu na wema na hunyesha mvuajuu ya watu waadilifu na wasio waadilifu.(Mt. 5:45) Ndiyo sababu mtume Paulo alipo-kuwa akiongea na watu wasio waamini ali-waambia kwamba Yehova alitenda mema,akiwapa mvua kutoka mbinguni na majirayenye kuzaa matunda, akijaza mioyo yao ki-kamili kwa chakula na uchangamfu. (Mdo.14:17) Ni wazi kwamba Yehova ni mkari-mu kuwaelekea wanadamu wote.Luka6:35.

    6 Yehova hufurahia hasa kuwaandaliawaabudu wake waaminifu mahitaji yao.Mfalme Daudi alisema hivi: Nilikuwa kija-na, pia nimezeeka, na bado sijamwona mtuyeyote mwadilifu akiwa ameachwa kabi-sa, wala uzao wake ukitafuta mkate. (Zab.37:25) Wakristo wengi waaminifu wamejio-nea uthibitisho wa kwamba Yehova huwatu-nza watu wake. Fikiria mfano ufuatao.

    7 Miaka kadhaa iliyopita, mtumishimmoja wa wakati wote anayeitwa Nancyalijikuta katika hali ngumu. Nancy anaku-mbuka hivi: Nilihitaji dola 66 za Mareka-ni ili nilipe kodi yangu ya nyumba siku ili-yofuata. Sikujua ningepata wapi pesa hizo.Nilisali kuhusu tatizo hilo, kisha nikae-nda kazini ambako nilikuwa mhudumu wamkahawa. Sikutarajia kupata bakshishi nyi-ngi jioni hiyo kwa sababu kwa kawaida wa-teja si wengi siku hiyo. Jambo la kushangazani kwamba jioni hiyo wateja wengi walikuja

    5. Yehova huonyesha ukarimu katika njia zipi?6, 7. (a) Yehova hufurahia kuwaandalia nani hasamahitaji yao? (b) Toa mfano unaoonyesha jinsi Ye-hova anavyowaandalia mahitaji waabudu wakewaaminifu.

    kwenye mkahawa huo. Nilipomaliza zamuyangu na kuhesabu bakshishi nilizopata, ni-likuwa na jumla ya dola 66. Nancy anasadi-ki kwamba Yehova alimwandalia kwa uka-rimu kile alichohitaji hasa.Mt. 6:33.

    8 Kila mtu anaweza kufaidika kutokanana zawadi kubwa zaidi inayoonyesha ukari-mu wa Yehova. Ni zawadi gani hiyo? Dha-bihu ya fidia ya Mwana wake. Yesu alise-ma hivi: Mungu aliupenda ulimwengusana hivi kwamba akamtoa Mwana wakemzaliwa-pekee, ili kila mtu anayemwaminiasiangamizwe bali awe na uzima wa milele.(Yoh. 3:16) Katika muktadha huo, neno uli-mwengu linarejelea wanadamu. Naam, ye-yote anayekubali zawadi hiyo kubwa zaidiinayoonyesha ukarimu wa Yehova anawezakufaidika kutokana nayo. Wale wanaodhi-hirisha imani katika Yesu watapata uzimakwa wingi, naam, uzima wa milele! (Yoh.10:10) Kwa kweli, huo ni uthibitisho wa ku-tosha kwamba Yehova ni mkarimu, sivyo?

    8. Ni zawadi gani kubwa zaidi inayoonyesha ukari-mu wa Yehova?

    Waisraeli walitiwa moyo kuiga ukarimu wa Yehova(Tazama fungu la 9)

    JUNI 15, 2013 13

  • 14 MNARA WA MLINZI

    IGA UKARIMU WA YEHOVA

    9 Tunaweza kuiga jinsi gani ukarimu waYehova? Yehova hutupa sisi vitu vyote kwawingi ili tuvifurahie; kwa hiyo, tunapaswakuwa tayari kushiriki pamoja na wengine,na hivyo kuchangia shangwe yao. (1 Tim. 6:17-19) Kwa furaha, tunatumia mali zetu ku-wapa zawadi wapendwa wetu na kuwasai-dia wale walio na uhitaji. (Soma Kumbuku-mbu la Torati 15:7.) Ni nini kinachowezakutusaidia kukumbuka kuwa wakarimu?Wakristo fulani huchukua hatua hii inayo-faa: Kila mara wanapopewa zawadi, wanata-futa fursa ya kumpa mtu mwingine zawa-di. Kutaniko la Kikristo limebarikiwa kwakuwa na ndugu na dada wengi wanaositawi-sha roho ya ukarimu.

    10 Njia moja bora zaidi ya kuonyesha uka-rimu ni kujitoa kuwasaidia wengine kwa

    9. Tunawezaje kuiga ukarimu wa Yehova?10. Tunaweza kuonyesha ukarimu katika njia ganibora zaidi?

    maneno na matendo. Tunawezaje kufanyahivyo? Kwa kutumia wakati na nguvu zetukuwasaidia na kuwatia moyo wengine. (Gal.6:10) Ili kujua ikiwa tunatimiza jambo hilo,tunaweza kujiuliza hivi: Je, wengine wa-nahisi kwamba niko tayari kujitoa na kusi-kiliza mahangaiko yao? Mtu anaponiombanimsaidie kufanya kazi fulani, je, mimi hu-kubali inapowezekana? Ni lini mara ya mwi-sho nilipompongeza kwa unyoofu mshirikiwa familia yangu au mwamini mwenza-ngu? Tukiwa na mazoea ya kuwapa watu,tuna hakika kwamba tutamkaribia zaidi Ye-hova na rafiki zetu.Luka 6:38; Met. 19:17.

    11 Tunaweza pia kumwonyesha Yehovaukarimu. Maandiko yanatuhimiza hivi:Mheshimuni Yehova kwa vitu vyenu vye-nye thamani. (Met. 3:9) Vitu hivyo vye-nye thamani vinatia ndani wakati, ngu-vu, na mali zetu tunazoweza kutumia kwa

    11. Tunaweza kumwonyesha Yehova ukarimu kwanjia gani?

    Mheshimu Yehova kwa vitu vyakovyenye thamani.Met. 3 :9(Tazama fungu la 11)

    Lolote mnalofanya, lifanyeni kwanafsi yote.Kol. 3:23(Tazama fungu la 17)

  • JUNI 15, 2013 15

    hiari tunapomtumikia. Hata watoto wadogowanaweza kujifunza kumwonyesha Yehovaukarimu. Familia yetu inapotoa michangokatika Jumba la Ufalme, tunawapa watotopesa hizo ili wazitumbukize katika sandukula michango, asema baba yao anayeitwa Ja-son. Wanafurahia jambo hilo kwa sababuwanapofanya hivyo, wanampa Yehova kitufulani. Inaelekea kwamba watoto wanao-pata shangwe kwa kumpa Yehova kitu fula-ni wakiwa wachanga wataendelea kumwo-nyesha ukarimu hata watakapokuwa watuwazima.Met. 22:6.

    YEHOVA NI MWENYE USAWAZIKO

    12 Usawaziko ni sifa nyingine ya Yeho-va yenye kuvutia sana. Inamaanisha ninikuwa na usawaziko? Neno la lugha ya awaliambalo kwa kawaida hutafsiriwa kuwa usa-waziko katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya,kihalisi linamaanisha kukubali maoni yawengine. (Tito 3:1, 2) Mtu mwenye usawazi-ko hasisitizi daima kufuata mambo madogo-madogo ya sheria, wala si mkali kupindukia,mgumu, au asiye na huruma. Badala yake,anajitahidi sana kuwatendea wengine kwawororo, akijali hali zao. Yuko tayari kuwasi-kiliza wengine, na inapofaa, hukubali maoniyao na kubadili matakwa yake.

    13 Yehova huonyeshaje usawaziko? Kwafadhili, yeye hujali hisia za watumishi wake,na mara nyingi anakubali maombi yao. Kwamfano, fikiria jinsi Yehova alivyoshughulikana Loti, yule mwanamume mwadilifu. Yeho-va alipoazimia kuyaangamiza majiji ya So-doma na Gomora, alimpa Loti maagizo yawazi kwamba akimbilie milimani. Hata hi-vyo, kwa sababu fulani Loti alimsihi Yehovaamruhusu akimbilie eneo lingine. Hebu fiki-riakwa kweli Loti alimwomba Yehova aba-dili maagizo Yake!Soma Mwanzo 19:17-20.

    12. Inamaanisha nini kuwa na usawaziko?13, 14. (a) Yehova huonyeshaje usawaziko? (b) Tu-najifunza nini kuhusu usawaziko kutokana na jinsiYehova alivyoshughulika na Loti?

    14 Huenda ikawa rahisi kusema kwambaLoti alikuwa na imani dhaifu au hakuwamtiifu. Kwa vyovyote vile, bila shaka Yeho-va angemwokoa Loti popote pale, kwa hiyoLoti hakuwa na sababu ya kuhofu. Hatahivyo, alihofuhivyo ndivyo Loti alivyohi-si, na Yehova alijali maoni yake. Alimruhu-su Loti kukimbilia katika jiji ambalo Yeho-va alikusudia kuangamiza. (Soma Mwanzo19:21, 22.) Ni wazi kwamba Yehova si mka-li kupindukia wala hashikilii sana maoniyake. Yeye hukubali maoni ya wengine na nimwenye usawaziko.

    15 Fikiria mfano mwingine katika Sheriaya Musa unaoonyesha usawaziko wa Yeho-va. Ikiwa Mwisraeli alikuwa maskini sanahivi kwamba hangeweza kutoa dhabihu yamwana-kondoo au mbuzi, angeweza kutoanjiwa-tetere wawili au hua wawili. Lakininamna gani ikiwa Mwisraeli alikuwa maski-ni sana hivi kwamba hangeweza kupata huawawili? Katika hali hiyo, Yehova alimruhu-su Mwisraeli huyo maskini kutoa kiasi kido-go cha unga. Hata hivyo, kumbuka jambohili muhimu: Ulipaswa kuwa unga anao-weza kuwatayarishia wageni waheshimiwa,yaani, unga laini, wala si unga wowote tu.(Mwa. 18:6) Kwa nini hilo ni jambo muhi-mu?Soma Mambo ya Walawi 5:7, 11.

    16 Hebu jiwazie ukiwa Mwisraeli maski-ni sana. Unapofika kwenye maskani ukiwana kiasi kidogo cha unga ili kutoa dhabihu,unawaona Waisraeli matajiri wakileta mifu-go. Huenda ukaaibika kwa sababu ya dhabi-hu yako ya unga inayoonekana kuwa hainathamani. Kisha, unakumbuka kwamba ma-choni pa Yehova, dhabihu yako ina thamanisana. Kwa nini? Kwa sababu Yehova aliagizakwamba unga huo ulipaswa kuwa bora ka-bisa. Ni kana kwamba Yehova alikuwa aki-waambia hivi Waisraeli maskini: Ninaele-wa kwamba huwezi kutoa kama wengine,

    15, 16. Sheria ya Musa ilionyeshaje usawaziko waYehova? (Tazama picha kwenye ukurasa wa 12.)

  • 16 MNARA WA MLINZI

    lakini ninajua pia kwamba unanipa kilichobora zaidi. Kwa kweli, Yehova anaonyeshausawaziko kwa kutilia maanani upungufuwa watumishi wake na anaelewa hali zao.Zab. 103:14.

    17 Tunaweza kufarijiwa tunapojua kwa-mba Yehova hukubali utumishi wetu wanafsi yote kwa sababu ya sifa yake ya usa-waziko. (Kol. 3:23) Dada mmoja Mwitalianoaliyezeeka aitwaye Constance alisema hivi:Hakuna jambo ninalopenda zaidi kulikokuzungumza na wengine kuhusu Muumbawangu. Ndiyo sababu ninaendelea kuhubi-ri na kuongoza mafunzo ya Biblia. Nyakatinyingine ninasikitika kwamba siwezi kufa-nya mengi zaidi kwa sababu ya afya yangu.Lakini ninatambua kwamba Yehova anajuaupungufu wangu na ananipenda na kutha-mini kile ninachotimiza.

    IGA USAWAZIKO WA YEHOVA

    18 Tunawezaje kuiga usawaziko wa Yeho-va? Fikiria tena jinsi Yehova alivyoshughu-lika na Loti. Yehova ndiye aliyekuwa namamlaka; hata hivyo, alimsikiliza Loti kwafadhili alipokuwa akieleza jinsi anavyohi-si. Na Mungu alikubali ombi la Loti. Ikiwawewe ni mzazi, je, unaweza kuiga mfanowa Yehova? Je, unaweza kusikiliza maombiya watoto wako, na inapofaa, kukubali mao-mbi yao? Kuhusiana na hilo, gazeti la Mnarawa Mlinzi la Septemba 1, 2007, lilitaja kwa-mba huenda wazazi fulani wakazungumzana watoto wao wanapoweka sheria za nyu-mbani. Kwa mfano, wazazi huamua kuwe-ka wakati hususa wa kurudi nyumbani, nakwa kweli wana haki ya kuchagua saa hu-susa wanayotaka watoto wafike nyumbani.Hata hivyo, huenda wazazi Wakristo waka-sikiliza maoni ya watoto wao kuhusu saa ili-yowekwa. Katika visa fulani, wazazi wana-

    17. Unaweza kuwa na hakika kwamba Yehova ana-kubali utumishi wa aina gani?18. Wazazi wanaweza kuiga mfano wa Yehova ka-tika njia gani?

    weza kuamua kubadili saa waliyowawekeawatoto wao ikiwa kufanya hivyo hakuvunjikanuni za Biblia. Wazazi wanaweza kugu-ndua kwamba wanapotilia maanani maoniya watoto wao wanapoweka sheria za nyu-mbani, watoto wataelewa sheria hizo na ku-zitii kwa utayari zaidi.

    19 Wazee wa kutaniko hujitahidi kuigausawaziko wa Yehova kwa kutilia maananihali za waamini wenzao. Kumbuka kwambaYehova alithamini pia dhabihu zilizotolewana Waisraeli maskini. Vivyo hivyo, baadhiya ndugu na dada hawawezi kufanya mengikatika utumishi, labda kwa sababu ya mata-tizo ya kiafya au kuzeeka. Namna gani ikiwawapendwa hao wanavunjika moyo kwa sa-babu hawawezi kufanya mengi katika hudu-ma? Wazee wanaweza kuwahakikishia kwafadhili kwamba Yehova anawapenda kwasababu wanampa kilicho bora.Marko 12:41-44.

    20 Bila shaka, hatupaswi kamwe kufiki-ri kimakosa kwamba tunaonyesha usawa-ziko kwa kutomtumikia Mungu kwa moyowote kwa sababu tu tunataka kujitendeakwa fadhili. (Mt. 16:22) Hatutaki kufanyamachache tu na kisha kutetea mtazamo huotukisema kwamba tuna usawaziko. Badalayake, sote tunahitaji kujitahidi sana kuu-nga mkono kazi ya Ufalme. (Luka 13:24)Kwa kweli, tunajitahidi kusawazisha kanu-ni mbili. Kwa upande mmoja, tunajitahidisana kutofanya machache katika utumishiwetu. Kwa upande mwingine, tunakumbu-ka kwamba Yehova hatazamii tutimize me-ngi zaidi ya uwezo wetu. Tunapompa kilichobora, tuna hakika kwamba anafurahi. Je, ha-tufurahi kumtumikia Bwana huyo mwenyeuthamini na usawaziko? Katika makala ina-yofuata, tutachunguza sifa nyingine mbilizinazovutia za utu wa Yehova.Zab. 73:28.

    19. Wazee wanawezaje kujitahidi kuiga usawazikowa Yehova?20. Je, kuwa na usawaziko kunamaanisha kuto-mtumikia Mungu kwa moyo wote? Eleza.

  • UNGESEMA rafiki wa kweli ni rafiki wa aina gani?Dada Mkristo anayeitwa Ashley anasema hivi: Kwamaoni yangu, rafiki wa kweli ni yule aliye tayari sikuzo-te kukusaidia na anayekusamehe unapomkosea. Sisisote tunathamini marafiki washikamanifu na wanaosa-mehe. Wanatusaidia kuhisi kwamba tuko salama na tu-napendwa.Met. 17:17.

    2 Yehova ndiye Rafiki mwenye kusamehe na mshika-manifu zaidi tunayeweza kupata. Ni kama mtunga-zaburialivyosema: Wewe, Ee Yehova, ni mwema na uko ta-yari kusamehe; na fadhili zenye upendo [au, upendomshikamanifu] ni nyingi kwa wale wote wanaokuitia.(Zab. 86:5) Inamaanisha nini kuwa mshikamanifu namwenye kusamehe? Yehova huonyeshaje sifa hizo zi-nazovutia? Na tunaweza kuiga jinsi gani mfano wake?Majibu ya maswali hayo yatatusaidia kumpenda zaidiRafiki yetu mkubwa zaidi, Yehova. Yatatusaidia pia kui-marisha urafiki pamoja na waamini wenzetu.1 Yoh.4:7, 8.

    YEHOVA NI MSHIKAMANIFU

    3 Ushikamanifu ni sifa yenye kuvutia inayotia nda-ni ujitoaji, uaminifu, na utii usioyumba-yumba. Mtumshikamanifu hana kigeugeu. Badala yake, anashika-mana kabisa kwa upendo na mtu (au kitu fulani), hatachini ya hali ngumu. Naam, Yehova ni Mshikamanifukwa njia isiyo na kifani.Ufu. 16:5.

    4 Yehova huonyeshaje ushikamanifu? Hawaachi ka-mwe waabudu wake waaminifu. Mmoja wa waabu-du hao, Mfalme Daudi, alishuhudia ushikamanifu wa

    1, 2. (a) Kwa nini tunawathamini marafiki walio washikamani-fu na wanaosamehe? (b) Tutajibu maswali gani?3. Inamaanisha nini kuwa mshikamanifu?4, 5. (a) Yehova huonyeshaje ushikamanifu? (b) Kutafakari ma-tendo ya Mungu ya ushikamanifu kutatuimarishaje?

    THAMINIUSHIKAMANIFUNA MSAMAHAWA YEHOVA

    Wewe, Ee Yehova, nimwema na uko tayarikusamehe; na fadhilizenye upendo ni nyi-ngi kwa wale wotewanaokuitia.ZAB. 86:5.

    JE, UNAWEZA KUELEZA?

    Tunaweza kuiga ushikamanifu

    wa Yehova katika njia zipi?

    Tunawezaje kumwiga Yehova

    katika kuwasamehe wengine?

    Kwa nini unataka kuendelea

    kuthamini hata zaidi sifa za

    Yehova?

    17

  • 18 MNARA WA MLINZI

    Yehova. (Soma 2 Samweli 22:26.) Daudialipokabili majaribu, Yehova alimwongo-za, akamlinda, na kumkomboa kwa ushi-kamanifu. (2 Sam. 22:1) Daudi alijuakwamba Yehova haonyeshi ushikamani-fu kwa maneno peke yake. Kwa nini Ye-hova alimtendea Daudi kwa ushikamani-fu? Kwa sababu Daudi mwenyewe alikuwamtu mshikamanifu. Yehova huthami-ni sana ushikamanifu wa waabudu wake,naye huwatendea kwa ushikamanifu.Met. 2:6-8.

    5 Tunaweza kuimarishwa kwa kutafaka-ri matendo ya Yehova ya ushikamanifu.Ndugu mwaminifu anayeitwa Reed anase-ma hivi: Kusoma masimulizi yanayoonye-sha jinsi Yehova alivyoshughulika na Dau-di nyakati za taabu hunisaidia sana. HataDaudi alipokimbia na kuishi katika ma-pango, Yehova alimtegemeza sikuzote.Hilo ni jambo linalonitia moyo sana! Li-nanikumbusha kwamba katika hali yo-yote ile, hata inayoonekana kuwa ngu-mu kadiri gani, Yehova atanitegemezamaadamu ninabaki mshikamanifu kwa-ke. Bila shaka, unahisi vivyo hivyo.Rom.8:38, 39.

    6 Yehova huonyesha ushikamanifu kati-ka njia zipi nyingine? Yeye hushikamanana viwango vyake. Anatuhakikishia hivi:Hata uzeeni mwa mtu mimi ni yuleyule.(Isa. 46:4) Sikuzote yeye hufanya maamu-zi akitegemea viwango vyake visivyobadili-ka vya mema na mabaya. (Mal. 3:6) Zaidiya hayo, Yehova huonyesha ushikamani-fu kwa kutimiza ahadi zake kwa uamini-fu. (Isa. 55:11) Hivyo, ushikamanifu wa Ye-hova huwanufaisha waabudu wake wotewaaminifu. Jinsi gani? Tunapojitahidi kadi-ri tuwezavyo kushikamana na viwango vyaYehova, tuna hakika kwamba atatubarikikama alivyoahidi.Isa. 48:17, 18.

    6. Yehova huonyesha ushikamanifu katika njiazipi nyingine, na waabudu wake hunufaikaje?

    IGA USHIKAMANIFU WA YEHOVA

    7 Tunaweza kuiga jinsi gani ushikama-nifu wa Yehova? Njia moja ni kuwasaidiawale wanaokabili hali ngumu. (Met. 3:27)Kwa mfano, je, unajua mwamini mwenza-ko yeyote ambaye amevunjika moyo, lab-da kwa sababu ya matatizo ya kiafya, upi-nzani kutoka kwa familia yake, au udhaifuwake? Kwa nini usichukue hatua ya ku-msaidia mtu huyo kwa kumwambia ma-neno mema, maneno yenye kufariji. (Zek.1:13) Unapofanya hivyo, unaonyesha wazikwamba wewe ni mshikamanifu na rafi-ki wa kweli, anayeshikamana na mtu kwaukaribu zaidi kuliko ndugu.Met. 18:24.

    8 Tunaweza pia kuiga ushikamanifu waYehova kwa kuendelea kuwa waaminifukwa wale tunaowapenda. Kwa mfano, ikiwatumefunga ndoa, tunajua kwamba ni lazi-ma tubaki waaminifu kwa mwenzi wetu wandoa. (Met. 5:15-18) Kwa hiyo, hatuthubutukufanya jambo lolote linaloweza kutuongo-za kufanya uzinzi. (Mt. 5:28) Zaidi ya hayo,tunaonyesha ushikamanifu kwa waaminiwenzetu kwa kuepuka uchongezi au porojozenye kudhuru, kutoeneza au hata kutosiki-liza habari hizo zisizofaa.Met. 12:18.

    9 Zaidi ya yote, tunataka kubaki washika-manifu kwa Yehova. Tutafanyaje hivyo? Kwakujitahidi kabisa kuona mambo kama ana-vyoyaona, yaani, kupenda mambo anayope-nda na kuchukia anayochukia, na kisha ku-jiendesha ifaavyo. (Soma Zaburi 97:10.) Unaweza kupata mapendekezo mazuri katika maka-

    la yenye kichwa Je, Umetia Moyo Yeyote Karibuni? ka-tika toleo la Mnara wa Mlinzi la Januari 15, 1995, na maka-la Kuchochea Kwenye Upendo na Kazi Zilizo BoraJinsiGani? katika toleo la Aprili 1, 1995.

    7. Tunaweza kuiga ushikamanifu wa Mungu kwanjia gani moja?8. Tunawezaje kuiga ushikamanifu wa Yehova,kwa mfano katika ndoa?9, 10. (a) Tunapaswa kubaki washikamanifu kwanani hasa? (b) Kwa nini si rahisi sikuzote kutii amriza Yehova?

  • JUNI 15, 2013 19

    Kadiri tunavyojifunza kufikiri na kuwa nahisia kama za Yehova, ndivyo inavyokuwarahisi zaidi kutii amri zake.Zab. 119:104.

    10 Ukweli ni kwamba si rahisi siku-zote kutii amri za Yehova. Huenda tu-kahitaji kupambana ili kubaki washi-kamanifu. Kwa mfano, Wakristo fulaniwaseja wangependa kufunga ndoa, la-kini bado hawajapata mwenzi anayefaakati ya waabudu wa Yehova. (1 Kor. 7:39) Huenda dada mseja akagunduakwamba wafanyakazi wenzake wasiowaamini wanajaribu daima kumtafutiamwenzi wa ndoa. Labda dada huyo ana-pambana na hisia za upweke. Hata hi-vyo, anajitahidi sana kudumisha utimi-lifu wake kwa Yehova. Je, hatuthaminimifano bora kama hiyo ya ushikamani-fu? Bila shaka, Yehova atawathawabishawote wanaobaki waaminifu kwake lichaya hali ngumu.Ebr. 11:6.

    YEHOVA HUSAMEHE

    11 Miongoni mwa sifa za Yehova zina-

    11. Kusamehe kunamaanisha nini?

    zovutia ni utayari wake wa kusamehe.Kusamehe kunamaanisha nini? Kuna-tia ndani hasa kumsamehe mkosaji ku-napokuwa na msingi halali wa kufanyahivyo. Hilo halimaanishi kwamba mtualiye tayari kusamehe anapuuza tu ma-kosa au kukataa kwamba alikosewa. Ba-dala yake, anaamua kutokuwa na kinyo-ngo. Maandiko yanafundisha kwambaYehova yuko tayari kuwasamehe walewanaotubu kikweli.Zab. 86:5.

    12 Yehova husamehe jinsi gani? Yeho-va anaposamehe, anasamehe kwa njiakubwa; anasamehe kabisa na milele.(Isa. 55:7) Tunajuaje kwamba Yehova hu-samehe kabisa? Fikiria uhakikisho uliokatika Matendo 3:19. (Soma.) MtumePetro aliwahimiza watu waliomsikilizawatubu na kugeuka. Mtenda-dhambianapotubu kikweli, anajuta kabisa kwasababu ya mwenendo wake wa dhambi.Anaazimia pia kutorudia dhambi hiyo.(2 Kor. 7:10, 11) Isitoshe, toba ya kweli

    12. (a) Yehova husamehe jinsi gani? (b) Yeho-va hufuta dhambi za mtu katika maana gani?

    Yuko rafiki anayeshikamana na mtukwa ukaribu zaidi kuliko ndugu.Met. 18:24(Tazama fungu la 7)

    Msameheane kwa hiari.Efe. 4:32(Tazama fungu la 16)

  • 20 MNARA WA MLINZI

    humchochea mtenda-dhambi kugeuka nakuacha mwenendo wake wa dhambi na ku-fuatilia mwenendo unaompendeza Mungu.Matokeo yangekuwa nini ikiwa watu walio-msikiliza Petro wangeonyesha toba hiyo yakweli? Petro alisema kwamba dhambi zaozingefutwa. Neno hilo linatokana na nenola Kigiriki linalomaanisha kufuta kabisa,kupangusa. Kwa hiyo, Yehova anaposame-he, anafuta kabisa dhambi. Anasamehe ka-bisa.Ebr. 10:22; 1 Yoh. 1:7.

    13 Tunajuaje kwamba Yehova husamehemilele? Fikiria unabii wa Yeremia kuhusuagano jipya alilofanya Yehova pamoja naWakristo watiwa-mafuta, linalowawezeshawale wanaoonyesha imani katika fidia ku-pata msamaha wa kweli. (Soma Yeremia31:34.) Yehova anasema hivi: Nitalisame-he kosa lao, na dhambi yao sitaikumbukatena. Kwa hiyo, Yehova anatuhakikishiakwamba baada ya kutusamehe, hatatua-dhibu kamwe wakati ujao kwa sababuya dhambi hizo. Hakumbuki dhambi zetuili atuhukumu au kutuadhibu tena na tena.Badala yake, Yehova hutusamehe dhambihizo na kuzisahaumilele.Rom. 4:7, 8.

    14 Tunaweza kufarijiwa kwa kutafakarikuhusu msamaha wa Yehova. Fikiria mfa-no mmoja. Miaka mingi iliyopita, dada tu-takayemwita Elaine alitengwa na ushirika.Miaka kadhaa baadaye alirudishwa kuta-nikoni. Elaine anakiri hivi: Ingawa ni-lijiambia na kuwaambia wengine kwambaniliamini kuwa Yehova amenisamehe, siku-zote nilihisi kwamba kwa kiasi fulani ali-kuwa mbali nami au wengine walikuwa nauhusiano wa karibu zaidi naye na alikuwahalisi zaidi kwao. Hata hivyo, Elaine ali-pata faraja aliposoma na kutafakari baadhiya mifano inayotumiwa katika Biblia kuo-

    13. Maneno dhambi yao sitaikumbuka tena ya-natuhakikishia nini?14. Tunawezaje kupata faraja kwa kutafakari ku-husu msamaha wa Yehova? Toa mfano.

    nyesha jinsi Yehova anavyosamehe. Elaineanaongeza hivi: Nilihisi upendo na wororowa Yehova katika njia ambayo sijawahi ka-mwe kuhisi. Aliguswa moyo hasa na wazohili: Yehova anapotusamehe dhambi zetu,hatupaswi kuhisi kwamba tutabeba hatiaya dhambi hizo maisha yetu yote. Elaineanasema: Niligundua kuwa sikuaminikwamba Yehova angeweza kunisamehe ka-bisa, na nilifikiri nitabeba mzigo huo mai-sha yangu yote. Ninajua itachukua muda,lakini nimeanza kuhisi kwamba ninawezakwa kweli kumkaribia Yehova zaidi, na ni-nahisi mzigo niliokuwa nao umeondolewa.Kwa kweli tunamtumikia Mungu anayesa-mehe na mwenye upendo kama nini!Zab.103:9.

    MWIGE YEHOVA

    UNAPOWASAMEHE WENGINE

    15 Tunaweza kumwiga Yehova kwa kuwatayari kusameheana tunapokuwa na msi-ngi wa kufanya hivyo. (Soma Luka 17:3, 4.) Kumbuka kwamba Yehova anaposa-mehe, anasahau dhambi zetu katika maa-na ya kwamba hatatuhukumu baadaye kwasababu ya dhambi hizo. Tunapowasame-he wengine, sisi pia tunaweza kusahau kwakuachilia mbali na kutozungumzia tenamakosa hayo wakati ujao.

    16 Kuwasamehe wengine hakumaanishikwamba tunaachilia makosa au kuwaruhu-su wengine watukandamize. Hapana, kwakweli kunamaanisha tumeamua kutokuwana kinyongo. Hata hivyo, jambo muhimuni kwamba ili tusamehewe na Yehova, ni la-zima tuige njia yake ya kusamehe tunapo-

    Tazama fungu la 10 katika sura ya 26 ya kitabu Mka-ribie Yehova.

    15. Tunawezaje kumwiga Yehova tunapowasame-he wengine?16. (a) Je, kuwa mwenye kusamehe kunamaani-sha kwamba tunaachilia makosa au kuwaruhusuwengine watukandamize? Eleza. (b) Ni lazima tufa-nye nini ili Mungu atusamehe?

  • shughulika na wengine. (Mt. 6:14, 15) Kwakweli, hisia-mwenzi humchochea Yehovakukumbuka kwamba sisi ni mavumbi.(Zab. 103:14) Hivyo basi, wengine wanapo-tukosea, je, hatupaswi kuchochewa na hi-sia-mwenzi kuwasamehe kwa hiari kutokamoyoni?Efe. 4:32; Kol. 3:13.

    17 Bila shaka, nyakati nyingine si rahi-si kuwasamehe wengine. Inaonekana kwa-mba haikuwa rahisi hata kwa baadhi yaWakristo watiwa-mafuta katika karne yakwanza kusameheana. (Flp. 4:2) Ni nini ki-nachoweza kutusaidia ikiwa tumekosewana mwamini mwenzetu? Mfikirie Ayubu.

    17. Ni nini kinachoweza kutusaidia ikiwa tumeko-sewa na mwamini mwenzetu?

    Aliumia sana wakati marafiki wake, yaa-ni, Elifazi, Bildadi, na Sofari, walipotoa ma-shtaka ya uwongo kumhusu. (Ayu. 10:1;19:2) Hatimaye, Yehova aliwakaripia wa-shtaki hao wa uwongo. Mungu aliwaagizawaende kwa Ayubu na kutoa dhabihu kwaajili ya dhambi zao. (Ayu. 42:7-9) Lakini Ye-hova alitaka pia Ayubu afanye jambo fula-ni. Jambo gani? Yehova alimwambia Ayu-bu atoe sala kwa ajili ya washtaki hao.Ayubu alifanya kama Yehova alivyomwagi-za, na Yehova akambariki kwa sababu yaroho yake ya kusamehe. (Soma Ayubu 42:10, 12, 16, 17.) Tunajifunza nini? Kusali kwaunyoofu kwa ajili ya mtu aliyetukosea ku-naweza kutusaidia kuondoa kinyongo.

    ENDELEA KUTHAMINI KIKAMILI

    SIFA ZA YEHOVA

    18 Bila shaka tumeburudishwa sana ku-chunguza sifa mbalimbali za utu wa Yeho-va wenye upendo. Tumeona kwamba yeyeni mwenye urafiki, hana ubaguzi, ni mkari-mu, ni mwenye usawaziko, mshikamanifu,na anasamehe. Ukweli ni kwamba tume-chunguza sifa hizo kijuujuu tu. Tunawe-za kupata shangwe ya kujifunza mengi ku-mhusu Yehova kwa umilele wote. (Mhu. 3:11) Tunakubaliana na mtume Paulo aliyea-ndika hivi: Lo! Jinsi kilivyo kina cha utaji-ri wa Mungu na hekima na ujuzi mbali naupendo na sifa sita ambazo tumechunguza.Rom. 11:33.

    19 Sote na tuendelee kuthamini hata zai-di utu wa Yehova unaovutia. Tunaweza ku-fanya hivyo kwa kuzielewa sifa zake, ku-zitafakari, na kisha kuziiga katika maishayetu wenyewe. (Efe. 5:1) Tunapofanya hi-vyo, bila shaka tutakubaliana hata zai-di na mtunga-zaburi aliyeimba hivi: Lakinimimi, kumkaribia Mungu ni kwema kwa-ngu.Zab. 73:28.

    18, 19. Tunaweza kuendeleaje kuthamini hata zai-di utu wa Yehova unaovutia?

    Sala zetu za kuomba msamaha na zitoke moyoni(Tazama fungu la 17)

    JUNI 15, 2013 21

  • Uthibitisho unaonyesha kwamba maneno hayo ya-narejelea wana wa roho wa Mungu. Uthibitisho gani?

    Mstari wa pili unasomeka hivi: Wana wa Munguwa kweli wakaanza kuwaona mabinti wa wanadamu,kwamba ni wenye sura ya kupendeza; nao wakajichu-kulia wake, yaani, wote waliowachagua.Mwa. 6:2.

    Katika Maandiko ya Kiebrania, maneno wana waMungu wa kweli na wana wa Mungu yanapatikanakatika Mwanzo 6:2, 4; Ayubu 1:6; 2:1; 38:7; na Zaburi89:6. Maandiko hayo yanaonyesha nini kuhusu wana[hao] wa Mungu?

    Ni wazi kwamba wana wa Mungu wa kweli tu-naosoma kuwahusu katika Ayubu 1:6 walikuwa viu-mbe wa roho waliokusanyika mbele za Mungu. She-tani aliyetoka kuzurura huku na huku duniani,alikuwa miongoni mwa viumbe hao wa roho. (Ayu.1:7; 2:1, 2) Vivyo hivyo, katika Ayubu 38:4-7, tunaso-ma kuhusu wana wa Mungu waliopaaza sauti kwakushangilia Mungu alipoweka jiwe la pembeni la du-

    nia. Kwa sababu wanadamu hawakuwa wameumbwa,ni lazima wana hao walikuwa wana wa kimalaika waMungu. Wana wa Mungu wanaotajwa katika Zabu-ri 89:6 lazima wawe ni viumbe wa kimbingu walio pa-moja na Mungu, wala si wanadamu.

    Basi, wana wa Mungu wa kweli wanaotajwa kati-ka Mwanzo 6:2 na 4 ni nani? Kulingana na ushahidiwa Biblia tuliozungumzia, ni jambo linalopatana naakili kusema kwamba simulizi hilo linarejelea wanawa roho wa Mungu waliokuja duniani.

    Ni vigumu kwa wengine kukubali kwamba malai-ka wanaweza kutamani kuwa na mahusiano ya kingo-no. Maneno ya Yesu katika Mathayo 22:30 yanaonye-sha kwamba mbinguni hakuna ndoa wala mahusianoya kingono. Hata hivyo, katika pindi fulani malaikawalivaa miili ya kibinadamu, na hata kula na kunywapamoja na wanadamu. (Mwa.18:1-8; 19:1-3) Hivyo, nijambo linalopatana na akili kufikia mkataa kwambawakiwa wamejivika miili ya kibinadamu, wangewezakufanya ngono na wanawake.

    Kuna sababu zinazotegemea Biblia za kuamini kwa-mba malaika fulani walifanya hivyo. Andiko laYuda 6, 7 linalinganisha dhambi ya watu wa Sodoma,waliofuatilia mwili kwa ajili ya matumizi yasiyo ya asi-li, na dhambi ya malaika ambao hawakubaki maha-li pao pa kwanza bali waliyaacha makao yao wenye-we yanayofaa. Malaika hao walikuwa kama watu waSodoma kwa sababu walifanya uasherati kwa kuzidimno na kwenda kufuatilia mwili kwa ajili ya matumi-zi yasiyo ya asili. Andiko la 1 Petro 3:19, 20 linalozu-ngumzia habari hiyo linahusianisha malaika hao wa-siotii na siku za Noa. (2 Pet. 2:4, 5) Hivyo, mwelekeowa kutotii walioonyesha malaika katika siku za Noaunaweza kulinganishwa na dhambi ya Sodoma na Go-mora.

    Mkataa huo unapatana na akili hasa tunapotambuakwamba wana wa Mungu wa kweli wanaotajwa ka-tika Mwanzo 6:2 na 4 ni malaika waliojivika miili yakibinadamu na kufanya uasherati na wanawake.

    MASWALI KUTOKA KWA WASOMAJI

    Wana wa Mungu wa kweli wanaotajwa katikaMwanzo 6:2 na 4 walioishi kabla ya Gharika ni nani?

    MNARA WA MLINZI

  • Mtume Petro anasema kwamba roho hao ni wale ambao wa-kati fulani hawakuwa watiifu wakati subira ya Mungu ilipoku-wa ikingoja katika siku za Noa. (1 Pet. 3:20) Ni wazi kwambaPetro alikuwa akirejelea viumbe wa roho waliochagua kuungamkono uasi wa Shetani. Yuda anataja malaika ambao hawa-kubaki mahali pao pa kwanza bali wakayaacha makao yao we-nyewe yanayofaa, akisema kwamba Mungu amewaweka aki-ba wakiwa na vifungo vya milele chini ya giza zito kwa ajili yahukumu ya ile siku kuu.Yuda 6.

    Viumbe wa roho walikosa kutii katika siku za Noa kwanjia gani? Kabla ya Gharika, roho hao waovu walijivika mii-li ya kibinadamujambo ambalo Mungu hakuwa amekusu-dia malaika wafanye. (Mwa. 6:2, 4) Isitoshe, malaika haowaliofanya ngono na wanawake walikuwa wakifanya jambo li-silo la asili. Mungu hakuwaumba viumbe wa roho wafanyengono na wanawake.(Mwa. 5:2) Mungu atawaharibu malaikahao waovu na wasiotii wakati wake utakapofika. Kwa sasa,kama Yuda anavyosema, ni kama wako chini ya giza zito,yaani, gereza la kiroho la mfano.

    Yesu aliwahubiria lini na jinsi gani roho walio gerezani?Petro anaandika kwamba jambo hilo lilitukia baada ya Yesukufanywa kuwa hai katika roho. (1 Pet. 3:18, 19) Ona piakwamba Petro anasema kuwa Yesu aliwahubiria. Petro ana-tumia neno linaloonyesha tendo la wakati uliopita kudoke-za kwamba Yesu aliwahubiria roho hao kabla Petro hajaandikabarua yake ya kwanza. Hivyo basi, inaonekana kwamba mudafulani baada ya kufufuliwa, Yesu aliwatangazia roho hao wao-vu habari kuhusu hukumu waliyostahili kabisa ambayo wata-pata. Hayakuwa mahubiri yaliyowapa tumaini lolote. Yalikuwamahubiri ya kihukumu. (Yona 1:1, 2) Mara tu Yesu alipokuwaamedhihirisha imani na ushikamanifu wake hadi kifo na ku-fufuliwa na hivyo kuthibitisha wazi kwamba Ibilisi hakuwa nauwezo juu yake, Yesu alikuwa na msingi wa kutangaza ujumbehuo wa kihukumu.Yoh. 14:30; 16:8-11.

    Wakati ujao, Yesu atamfunga Shetani pamoja na malaikahao na kuwatupa ndani ya abiso. (Luka 8:30, 31; Ufu. 20:1-3)Kabla ya wakati huo, roho hao wasiotii wako katika hali ya gizazito la kiroho, na bila shaka wataharibiwa kabisa hatimaye.Ufu. 20:7-10.

    Biblia inasema kwamba Yesu aliwahubiria roho waliogerezani. (1 Pet. 3:19) Hilo linamaanisha nini?

    JUNI 15, 2013 23

  • 24 MNARA WA MLINZI

    KUMKARIBIA Mungu ni kwema kwangu. Nimewekakimbilio langu katika Bwana Mwenye Enzi Kuu Ye-hova. (Zab. 73:28) Katika andiko hilo, mtunga-zaburialieleza uhakika wake katika Mungu. Ni hali gani zili-zomwongoza kufikia mkataa huo muhimu? Alipoonaamani ya watu waovu, mwanzoni mtunga-zaburi aliu-mia sana moyoni. Alilalamika hivi: Nimeusafishamoyo wangu bure na kuiosha mikono yangu katikakutokuwa na hatia. (Zab. 73:2, 3, 13, 21) Hata hi-vyo, alipoingia patakatifu pakuu pa Mungu, aliku-wa katika mazingira yaliyomsaidia kubadili fikira zakena kuendelea kuwa na uhusiano wa karibu pamo-ja na Mungu. (Zab. 73:16-18) Jambo hilo lilimfundishasomo muhimu sana mwanamume huyo aliyemwogo-pa Mungu: Ili kuwa na uhusiano wa karibu pamo-ja na Yehova, ni muhimu tuwe miongoni mwa watuwa Mungu, tukubali, na kutumia mashauri yake.Zab.73:24.

    2 Sisi pia tunatamani kuwa na uhusiano wa karibusana pamoja na Mungu wa kweli aliye hai. Ili kutimizalengo hilo, ni muhimu turuhusu mashauri au nidha-mu yake itufinyange, ili tuwe watu wanaompendeza.Nyakati za kale, Mungu aliwapa kwa rehema watu namataifa mbalimbali nafasi za kukubali nidhamu yake.Masimulizi yanayoonyesha jinsi walivyoitikia nidhamuyake yameandikwa katika Biblia ili kutufundisha sisina kuwa onyo kwetu sisi ambao tumefikiwa na mii-sho ya mifumo ya mambo. (Rom. 15:4; 1 Kor. 10:11)Kuchunguza masimulizi hayo kwa undani kutatusaidiakuelewa zaidi utu wa Yehova na kutuonyesha jinsi tu-navyoweza kunufaika tukikubali atufinyange.

    1, 2. (a) Ni muhimu tufanye nini ili tuwe na uhusiano mzuri pa-moja na Yehova? (b) Tutanufaikaje tukichunguza masimulizi yaKimaandiko yanayoonyesha jinsi watu walivyoitikia nidhamu yaMungu?

    ACHA NIDHAMUYA YEHOVAIKUFINYANGE

    Utaniongoza kwashauri lako, nabaadaye utanipelekakwenye utukufu.ZAB. 73:24.

    UNGEJIBUJE?

    Ni nini kinachoonyesha kwamba

    yule Mfinyanzi Mkuu hawafinya-

    ngi watu kwa lazima au kuonye-

    sha upendeleo anapotoa

    nidhamu?

    Kwa nini tunafurahi kwamba Mfi-

    nyanzi wetu anaweza kujuta?

    Tunapaswa kuitikiaje mashauri

    au nidhamu ya Yehova?

  • JUNI 15, 2013 25

    JINSI MFINYANZI

    ANAVYOTUMIA MAMLAKA YAKE

    3 Andiko la Isaya 64:8 linasema hivi kwanjia ya mfano kuhusu mamlaka ambayo Ye-hova anayo juu ya mtu mmoja-mmoja najuu ya mataifa: Ee Yehova, wewe ni Babayetu. Sisi ni udongo, nawe ni Mfinyanziwetu; nasi sote ni kazi ya mkono wako.Mfinyanzi ana mamlaka kamili ya kuufi-nyanga udongo na kutengeneza chomboanachotaka. Udongo hauna mamlaka yo-yote katika jambo hilo. Ndivyo ilivyo katiya mwanadamu na Mungu. Mwanadamuhana haki ya kubishana na Mungu kamavile tu udongo usivyoweza kubishana namfinyanzi anayeufinyanga kwa mikonoyake.Soma Yeremia 18:1-6.

    4 Yehova aliposhughulika na taifa la kalela Israeli, alionyesha uwezo wake wa kuwa-finyanga kama mfinyanzi anavyoufinyangaudongo. Hata hivyo, Yehova ni tofauti kwanjia fulani kubwa. Mfinyanzi anaweza kufi-nyanga chombo cha aina yoyote kutokanana udongo. Je, Yehova huwafinyanga kwalazima watu au mataifa, akiwafanya wengi-ne kuwa wema na wengine wabaya? Jibula Biblia ni hapana. Yehova amewapa wa-nadamu zawadi yenye thamani sana, yaa-ni, zawadi ya uhuru wa kuchagua. Akiwamwenye enzi kuu, hatumii mamlaka yakekwa njia inayowazuia wanadamu kutu-mia zawadi hiyo. Ni lazima wanadamu wa-kubali kufinyangwa na Muumba, Yehova.Soma Yeremia 18:7-10.

    5 Vipi wanadamu wakikataa kwa ukai-di kufinyangwa na yule Mfinyanzi Mkuu?Anatumiaje mamlaka yake akiwa Mungu?Fikiria inavyokuwa kwa udongo usiofaa

    3. Andiko la Isaya 64:8 na Yeremia 18:1-6 yanao-nyesha nini kuhusu mamlaka ya Yehova juu yawatu? (Tazama picha iliyo kwenye ukurasa wa 24.)4. Je, Mungu huwafinyanga watu au mataifa kwalazima? Eleza.5. Wanadamu wanapokataa kufinyangwa na Yeho-va, anatumiaje mamlaka yake juu yao?

    kutumiwa kwa kusudi fulani hususa. Mfi-nyanzi anaweza kuutumia udongo huo ku-finyanga chombo kingine au kuutupa! Hatahivyo, kwa kawaida udongo usipofaa, nikosa la mfinyanzi. Lakini Mfinyanzi wetuhawezi kamwe kukosea. (Kum. 32:4) Mtuasipokubali kufinyangwa na Yehova, nikosa la mtu huyo. Yehova hutumia mamla-ka yake kama ya mfinyanzi kuwafinya-nga wanadamu ikitegemea jinsi wanavyoi-tikia jitihada zake za kuwafinyanga. Walewanaoitikia ifaavyo wanafinyangwa kwanjia yenye manufaa. Kwa mfano, Wakri-sto watiwa-mafuta ni vyombo vya rehemaambavyo vimefinyangwa na kuwa vyombokwa matumizi yenye kuheshimika. Kwaupande mwingine, wale wanaompinga Mu-ngu kwa ukaidi wanakuwa vyombo vyaghadhabu vilivyofanywa kuwa vyenye ku-faa kwa ajili ya uharibifu.Rom. 9:19-23.

    6 Njia moja anayotumia Yehova kuwafi-nyanga watu ni kupitia mashauri au ni-dhamu. Tukichunguza wafalme wawili wakwanza wa Israeli, yaani, Sauli na Daudi,tunaweza kuona jinsi anavyotumia mamla-ka yake juu ya wale anaowafinyanga. Mfal-me Daudi alipofanya uzinzi na Bath-sheba,matendo yake yalimwathiri sana yeye nawengine. Hata ingawa Daudi alikuwa mfal-me, Yehova hakusita kumtia nidhamu kali.Mungu alimtuma Nathani, nabii wake, ku-mpa Daudi ujumbe mkali. (2 Sam. 12:1-12)Daudi aliitikiaje? Alichomwa sana moyoninaye akatubu. Daudi alionyeshwa rehemana Mungu.Soma 2 Samweli 12:13.

    7 Kinyume chake, Mfalme Sauli aliyeta-wala kabla ya Daudi, hakuitikia vyema ali-poshauriwa. Yehova alimpa Sauli amri yamoja kwa moja kupitia nabii Samweli: Waa-ngamize Waamaleki wote na mifugo yao.Sauli hakutii amri hiyo ya Mungu. Haku-mwangamiza Mfalme Agagi na mifugo yao

    6, 7. Mfalme Daudi na Mfalme Sauli waliitikia ma-shauri ya Yehova kwa njia gani tofauti?

  • 26 MNARA WA MLINZI

    bora zaidi. Kwa nini? Sababu moja ni kwa-mba alitaka aheshimiwe. (1 Sam. 15:1-3,7-9, 12) Aliposhauriwa, Sauli hakupaswakuufanya moyo wake uwe mgumu, alipa-swa kukubali kufinyangwa na yule Mfinya-nzi Mkuu. Hata hivyo, Sauli alikataa kufi-nyangwa. Aliutetea mwenendo wake. Alitoakisingizio kwamba jambo alilofanya liliku-balika kwa sababu mifugo ingetolewa dha-bihu, na hivyo akapunguza uzito wa shaurila Samweli. Yehova alikataa Sauli asiende-lee kuwa mfalme, naye Sauli hakuwa tenana uhusiano mzuri pamoja na Mungu wakweli.Soma 1 Samweli 15:13-15, 20-23.

    MUNGU HANA UPENDELEO

    8 Yehova humpa mtu mmoja-mmojana pia mataifa mbalimbali nafasi ya ku-

    8. Tunajifunza somo gani kutokana na jinsi taifa laIsraeli lilivyoitikia lilipofinyangwa na Yehova?

    kubali awafinyange. Katika mwaka wa1513 K.W.K., wana wa Israeli waliwekwahuru kutoka katika utumwa huko Misri nakufanya agano pamoja na Mungu. Waisrae-li walikuwa taifa lake alilolichagua na wa-likuwa na pendeleo la kufinyangwa naye,kana kwamba juu ya gurudumu la yule Mfi-nyanzi Mkuu. Hata hivyo, watu hao wali-zidi kufanya mabaya machoni pa Yehova,hata wakaanza kuabudu miungu ya ma-taifa yaliyowazunguka. Yehova aliwatumamanabii tena na tena ili wawachochee ku-tubu, lakini Waisraeli hawakusikiliza. (Yer.35:12-15) Waisraeli walitiwa nidhamu kalikwa sababu ya kujiendesha kwa ukaidi.Kama chombo kinachostahili kuharibiwa,ufalme wa kaskazini wa makabila kumi uli-shindwa na Waashuru na ufalme wa kusiniwa makabila mawili ulishindwa na Waba-biloni. Jambo hilo linapaswa kutufundisha

    Sauli alikataa nakupunguza uzito wa

    shauri. Alikataakufinyangwa!

    (Tazama fungu la 7)

    Daudi alichomwamoyoni naye akakubalishauri. Alikubali Munguamfinyange. Je, wewehukubali?(Tazama fungu la 6)

  • JUNI 15, 2013 27

    somo muhimu kama nini! Yehova anawezakutufinyanga na kutusaidia ikiwa tu tutaiti-kia ifaavyo.

    9 Pia, Yehova aliwapa watu wa Ninawi,mji mkuu wa Ashuru, nafasi ya kutii onyolake. Neno lake lilimjia Yona, na kusema:Ondoka, uende Ninawi lile jiji kubwa,ukalitangazie kwamba ubaya wao umefikambele zangu. Ninawi lilionwa kuwa lina-stahili uharibifu.Yona 1:1, 2; 3:1-4.

    10 Hata hivyo, Yona alipotangaza uju-mbe wa maangamizi, watu wa Ninawi wa-kaanza kumwamini Mungu, ndipo wakata-ngaza kufunga na kuvaa nguo za magunia,kutoka aliye mkubwa zaidi kati yao mpakaaliye mdogo zaidi. Mfalme wao akasima-ma kutoka kwenye kiti chake cha ufalme,akavua vazi lake rasmi na kujifunika nguoza magunia na kuketi katika majivu. Wa-ninawi walikubali kufinyangwa na Yehovanao wakatubu. Kwa hiyo, Yehova hakuletamsiba.Yona 3:5-10.

    11 Yehova hakukosa kuwatia nidhamuWaisraeli hata ingawa walikuwa taifa ali-lolichagua. Kwa upande mwingine, Wani-nawi hawakuwa wamefanya agano pamojana Mungu. Hata hivyo, Yehova aliagiza wa-tangaziwe ujumbe wake wa hukumu nayealiwaonyesha rehema walipobadilika nakuwa kama udongo laini mikononi mwake.Mifano hiyo miwili inaonyesha waziwazikwamba Yehova Mungu wetu hamtendeiyeyote kwa upendeleo.Kum. 10:17.

    YEHOVA NI MWENYE USAWAZIKO

    NAYE HUNYUMBULIKA

    12 Utayari wa Mungu wa kutufinyangaunaonyesha kwamba ana usawaziko na

    9, 10. Waninawi waliitikiaje onyo la Mungu?11. Yehova alionyesha wazi sifa gani aliposhughu-lika na Waisraeli na Waninawi?12, 13. (a) Kwa nini Mungu hubadili uamuziwake watu wanapokubali awafinyange? (b) Kujutakwa Yehova kulimaanisha nini kuhusiana na Sauli?Na kuhusiana na Ninawi?

    ananyumbulika. Hilo linathibitishwa nahali zinazomfanya Yehova aamue kuwa-chukulia watu hatua ikitegemea hukumuyake ya haki, kisha anabadili uamuzi huokwa sababu ya itikio lao. Kuhusu mfal-me wa kwanza wa Israeli, Maandiko yana-sema kwamba Yehova alijuta kwamba ali-mfanya Sauli kuwa mfalme. (1 Sam. 15:11)Watu wa Ninawi walipotubu, walipogeu-ka, na kuacha njia zao mbaya, Biblia inase-ma: Mungu wa kweli akajuta juu ya msibaambao alikuwa amesema ataleta juu yao;naye hakuuleta.Yona 3:10.

    13 Kwa kweli, neno la Kiebrania lililo-tafsiriwa akajuta linamaanisha kubadilimtazamo au nia. Ingawa Yehova alimcha-gua Sauli kuwa mfalme, alibadili mtaza-mo Wake na kumkataa. Yehova hakubadilimtazamo wake eti kwa sababu alikosea ku-mchagua Sauli, aliubadili kwa sababu Saulialitenda bila imani naye hakumtii. Munguwa kweli alijuta aliposhughulika na Wani-nawi; yaani, alibadili nia yake kuwaelekea.Inafariji kama nini kujua kwamba Yeho-va, Mfinyanzi wetu, ni mwenye usawaziko,ananyumbulika, ni mwenye neema na re-hema, na yuko tayari kubadili uamuzi wakeikiwa wakosaji wanafanya mabadiliko ya-faayo!

    TUSIKATAE

    NIDHAMU YA YEHOVA

    14 Leo, Yehova hutufinyanga akitumiahasa Neno lake, Biblia, na tengenezo lake.(2 Tim. 3:16, 17) Je, hatupaswi kukubalishauri au nidhamu yoyote tunayopokea ku-pitia njia hizo? Hata kama muda mrefu ka-diri gani umepita tangu tubatizwe au tunamapendeleo mengi kadiri gani, tunapaswakuendelea kukubali mashauri ya Yehova,na kuyaruhusu yatufinyange ili tuwe vyo-mbo vya matumizi yenye kuheshimika.

    14. (a) Yehova hutufinyanga jinsi gani leo? (b) Tu-napaswa kuitikiaje tunapofinyangwa na Mungu?

  • 28 MNARA WA MLINZI

    15 Huenda tukatiwa nidhamu kwa ku-rekebishwa au kufundishwa. Hata hivyo,huenda nyakati nyingine tukahitaji kuti-wa nidhamu tusipofanya jambo linalofaa.Nidhamu hiyo inaweza kuhusisha kupote-za mapendeleo. Fikiria mfano wa Dennisaliyekuwa akitumikia akiwa mzee. Alite-nda dhambi kwa sababu ya kufanya uamu-zi usiofaa katika masuala ya kibiashara,na hivyo akakaripiwa faraghani. Dennisalihisije usiku ambao kutaniko lilitangazi-wa kwamba hatumikii tena akiwa mzee?Anasema hivi: Nilihisi kwamba sifai hatakidogo. Kwa miaka 30 nilikuwa na ma-pendeleo mengi. Nilikuwa painia wa ka-waida, nilitumikia Betheli, niliwekwa ras-mi kuwa mtumishi wa huduma na kishamzee. Nilikuwa pia nimetoa tu hotuba ya-ngu ya kwanza katika kusanyiko la wi-laya. Kwa ghafla, nilipoteza mapendeleoyote. Licha ya kwamba niliaibika na kuo-na haya, nilihisi sistahili tena kuwa katikatengenezo.

    16 Dennis alihitaji kubadili mwenendowake na kuacha makosa yaliyofanya ati-we nidhamu. Lakini ni nini kilichomsai-dia kukabiliana na hisia zisizofaa? Anae-leza hivi: Niliazimia kudumisha mazoeamazuri ya kiroho. Nilisaidiwa vilevile nautegemezo niliopata kutoka kwa unduguwetu wa Kikristo na kitia-moyo kutoka ka-tika machapisho yetu. Makala yenye ki-chwa Umewahi Kuwa na Mapendeleo yaUtumishi? Je, Unaweza Kutumikia Tena?katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Ago-sti 15, 2009, ilikuwa kama barua ya kibi-nafsi iliyojibu sala zangu. Nilithaminizaidi shauri hili: Kwa kuwa sasa huna ma-

    Majina yamebadilishwa.

    15, 16. (a) Mtu anaweza kuwa na hisia gani zisi-zofaa anapotiwa nidhamu inayohusisha kupotezamapendeleo? Toa mfano. (b) Ni nini kinachowezakutusaidia kukabiliana na hisia zisizofaa zinazoto-kana na kutiwa nidhamu?

    daraka mengi katika kutaniko, jitahidi ku-boresha hali yako ya kiroho. Nidhamuimemnufaishaje Dennis? Baada ya miakakadhaa, anasema hivi: Yehova ameniba-riki tena kwa kunipa pendeleo la kutumi-kia nikiwa mtumishi wa huduma.

    17 Kutenga na ushirika ni aina nyingi-ne ya nidhamu kutoka kwa Yehova. Hatuahiyo inalilinda kutaniko kutokana na uvu-tano mbaya na inaweza kumsaidia mte-nda-dhambi kutubu. (1 Kor. 5:6, 7, 11)Robert alitengwa na ushirika kwa miakakaribu 16. Wakati huo, wazazi wake nandugu zake walifuata kwa ushikamanifumwongozo wa Neno la Mungu wa kutoshi-rikiana na hata kutowasalimu wakosaji.Miaka kadhaa imepita tangu Robert alipo-rudishwa kutanikoni, na sasa anaendeleavizuri kiroho. Alipoulizwa kilichomcho-chea amrudie Yehova na watu Wake baa-da ya kukaa nje kwa muda mrefu hivyo,alisema kwamba alichochewa na msima-mo wa familia yake. Kama familia yanguingeshirikiana nami hata kidogo, labdakwa kunijulia hali, ningetosheka na ushi-rika huo mdogo na inaelekea kwamba si-ngechochewa kumrudia Mungu kwa saba-bu ya kutamani ushirika wao.

    18 Huenda tusihitaji nidhamu ya ainahiyo, lakini tutakuwa udongo wa aina ganimikononi mwa yule Mfinyanzi Mkuu? Tu-taitikiaje tukitiwa nidhamu? Je, tutaku-wa kama Daudi au kama Sauli? YuleMfinyanzi Mkuu ni Baba yetu. Usisa-hau kamwe kwamba yeye ambaye Ye-hova anampenda, humkaripia, kama vilebaba anavyomkaripia mwana anayemfura-hia. Kwa hiyo, usikatae nidhamu ya Ye-hova; wala usichukie karipio lake.Met.3:11, 12.

    17. Kutenga na ushirika kunaweza kumsaidiajemtenda-dhambi kutubu? Toa mfano.18. Tunapaswa kuwa udongo wa aina gani miko-noni mwa yule Mfinyanzi Mkuu?

  • Angela, dada mseja mwenye umri wamiaka 30 hivi, ana wasiwasi. Anawasubiri

    wazee. Watamwambia nini? Ni kweli kwa-

    mba amekosa kuhudhuria mikutano ka-

    dhaa, lakini amechoka baada ya kuwahu-

    dumia kwa siku nzima watu waliozeeka.

    Mbali na mahangaiko yake ya kila siku,

    anahangaishwa sana na hali ya afya ya

    mama yake.

    Ikiwa ungemtembelea Angela, ungeitia-

    je moyo nafsi hiyo iliyochoka? (Yer. 31:25)

    Kwanza kabisa, ungejitayarishaje kufanya

    ziara ya uchungaji inayoburudisha?

    FIKIRIA HALI ZA NDUGU ZAKO

    Nyakati nyingine, sisi sote huchoka sana

    kwa sababu ya kazi yetu ya kimwili au ma-

    jukumu ya kitheokrasi. Kwa mfano, nabii

    Majina yamebadilishwa.

    Danieli alichoka kabisa alipopata mao-

    no ambayo hakuelewa. (Dan. 8:27) Ma-

    laika Gabrieli alikuja kumsaidia. Mjumbe

    wa Mungu alimfanya Danieli aelewe mao-

    no hayo na kumhakikishia kwamba Yeho-

    va amesikia sala zake, kisha akamwambia

    kwamba bado alikuwa mtu mwenye kuta-

    manika sana. (Dan. 9:21-23) Pindi fula-

    ni baadaye, maneno yaliyochaguliwa vizuri

    yaliyosemwa na malaika mwingine yali-

    mwimarisha nabii huyo aliyechoka sana.

    Dan. 10:19.

    Vivyo hivyo, kabla ya kumtembelea

    mwamini mwenzako ambaye huenda ame-

    choka au kuvunjika moyo, fikiria kwanza

    hali zake. Anakabili matatizo gani? Hue-

    nda matatizo hayo yanamdhoofisha kwa

    njia gani? Anaonyesha sifa gani nzuri?

    Mimi hukazia fikira sifa nzuri za ndugu

    WAZEE Je, MtaiburudishaNafsi Iliyochoka?

    Kabla ya kufanyaziara ya uchungaji,fikirieni hali zamwamini mwenzenu

  • 30 MNARA WA MLINZI

    zangu, anasema Richard, ambaye ame-

    kuwa mzee wa kutaniko kwa miaka zaidi

    ya 20. Anaongezea hivi: Kwa kufikiria kwa

    makini hali zao kabla ya kuwatembelea,

    inakuwa rahisi zaidi kupata njia za kuwatia

    moyo kulingana na mahitaji yao hususa.

    Ikiwa mzee mwingine ataenda nawe kati-

    ka ziara hiyo, kwa nini msizungumzie hali

    ya ndugu yenu mkiwa pamoja?

    WAFANYE NDUGU ZAKO WASTAREHE

    Huenda ukakubali kwamba ni jambo li-

    naloaibisha kueleza jinsi unavyohisi. Kwa

    mfano: Ndugu yako anaweza kuogopa ku-

    waeleza wazee jinsi anavyohisi wanapo-

    mtembelea. Kwa hiyo, unawezaje kumfa-

    nya ahisi huru kujieleza? Tabasamu yako

    changamfu na maneno ya kumtia moyo

    yanaweza kuwa na matokeo mazuri. Mi-

    chael, ambaye amekuwa mzee kwa zai-

    di ya miaka 40, mara nyingi huanza ziara

    zake kwa kusema hivi: Unajua, mojawa-

    po ya mapendeleo mazuri zaidi ya kuwa

    mzee ni kuwatembelea ndugu nyumbani

    kwao na kuwajua vizuri zaidi. Kwa hiyo, ni-

    mekuwa nikiitazamia kwa hamu sana zia-

    ra ya leo.

    Mwanzoni mwa ziara hiyo, mnaweza

    kuamua kutoa sala inayotoka moyoni. Ka-

    tika sala zake, mtume Paulo alikazia kwa

    kufaa imani, upendo, na uvumilivu wa ndu-

    gu zake. (1 The. 1:2, 3) Unapoeleza ji-

    nsi unavyohisi kuhusu sifa nzuri za ndugu

    yako, kwa kweli unautayarisha moyo wako

    na wake kwa ajili ya mazungumzo yenye

    kujenga. Maneno yako yanaweza pia ku-

    mtuliza. Nyakati nyingine, sote husahau

    mambo mazuri tunayotimiza, anasema

    Ray, mzee mwenye uzoefu. Kwa hiyo mtu

    fulani anapotukumbusha mambo hayo,

    nafsi yetu inaburudishwa.

    WAPE ZAWADI YA KIROHO

    Sawa na Paulo, unaweza kuwapa zawa-

    di ya kiroho kwa kuzungumza nao wazo la

    Kimaandiko, hata kama ni mstari mmoja

    tu. (Rom. 1:11) Kwa mfano, ndugu aliye-

    shuka moyo anaweza kuhisi hafai, sawa tu

    Kwa kawaida,waaminiwenzetuhufurahiakutoa maelezokuhusu Biblia

  • na mtunga-zaburi aliyejilinganisha na kiri-

    ba katika moshi kilichosinyaa. (Zab. 119:

    83, 176) Baada ya kueleza kwa ufupi maa-

    na ya maneno hayo, unaweza kumwambia

    ndugu yako una hakika kwamba hajazisa-

    hau amri za Mungu.

    Je, mfano wa sarafu ya drakma iliyopo-

    tea unaweza kugusa hisia za dada aliyepe-

    peruka kutoka kutanikoni au aliyepunguza

    bidii yake? (Luka 15:8-10) Huenda sara-

    fu iliyopotea ilikuwa sehemu ya mkufu we-

    nye thamani uliokuwa na sarafu nyingi za

    fedha. Ukizungumzia mfano huo, unawe-

    za kumsaidia dada huyo kuona kwamba

    yeye ni sehemu yenye thamani sana ya ku-

    taniko la Kikristo. Baada ya kuzungumzia

    jambo hilo, unaweza kukazia jinsi Yehova

    anavyomjali sana akiwa mmoja wa kondoo

    zake wadogo.

    Kwa kawaida, waamini wenzetu hufu-

    rahia kutoa maelezo kuhusu Biblia. Kwa

    hiyo, usizungumze sana! Baada ya kuso-

    ma andiko linalohusiana na hali yao, una-

    weza kutaja jambo au wazo kuu, na ki-

    sha uwaombe watoe maelezo. Kwa mfano,

    baada ya kusoma andiko la 2 Wakori-

    ntho 4:16, mzee anaweza kuuliza hivi: Je,

    wewe binafsi umeona jinsi Yehova anavyo-

    kufanya upya? Kutumia njia hiyo kunawe-

    za kwa kweli kuongoza kwenye ubadili-

    shanaji wa kitia-moyo.Rom. 1:12.

    Unaweza pia kumburudisha mwamini

    mwenzako kwa kuzungumza juu ya mtu fu-

    lani anayetajwa katika Biblia aliyekabili

    hali kama yake. Huenda mtu aliyekata ta-

    maa akawakumbuka watu kama vile Hana

    au Epafrodito, ambao pindi fulani walishuka

    moyo lakini bado walikuwa wenye thamani

    machoni pa Mungu. (1 Sam. 1:9-11, 20; Flp.

    2:25-30) Kwa nini msizungumzie mifano mi-

    zuri iliyo katika Biblia hali inaporuhusu?

    HAKIKISHA UNAFUATILIA HALI YAO

    Unaweza kuonyesha kwamba unawaha-

    ngaikia kikweli ndugu na dada zako kwa

    kuendelea kupendezwa na hali zao baada

    ya ziara. (Mdo. 15:36) Mnapomalizia ziara

    hiyo, mnaweza kupanga kushiriki pamoja

    na ndugu au dada huyo katika huduma.

    Bernard, mzee mwenye uzoefu anapokuta-

    na tena na ndugu au dada aliyemtembe-

    lea karibuni, anaweza kuuliza hivi kwa bu-

    sara kuhusu shauri lolote alilotoa, Hebu

    niambie, je, limefanya kazi? Kwa kuonye-

    sha upendezi huo wa kibinafsi, utajua iki-

    wa msaada zaidi unahitajiwa.

    Kuliko wakati mwingine wowote, ndu-

    gu na dada zetu wanahitaji kuhakikishiwa

    sasa kwamba mtu fulani anawajali, anae-

    lewa hali zao, na anawapenda. (1 The. 5:

    11) Kwa hiyo, kabla ya kufanya ziara ya

    uchungaji, tafakarini kwanza hali ya ndugu

    yenu. Salini kuhusu jambo hilo. Chagueni

    maandiko yanayofaa. Mkifanya hivyo, mta-

    pata maneno yanayofaa yatakayoweza kui-

    burudisha nafsi iliyochoka!

    Endeleakupendezwakikweli nawengine

  • Bibliomancy ni nini, na Wakristowanapaswa kuonaje zoea hilo?

    Bibliomancy ni zoea la kufungua

    Biblia bila kufikiri na kusoma andiko

    ambalo mtu analiona kwanza, akia-

    mini kwamba maneno hayo yata-

    mpa msaada anaohitaji. Wakristo

    wa kweli hawatafuti ishara za baha-

    ti. Badala yake, wanajifunza Biblia ili

    kupata ujuzi sahihi na mwongozo

    wa Mungu.12/15, ukurasa wa 3.

    Ni ulimwengu gani utakaopiti-lia mbali?

    Ulimwengu utakaopitilia mbali ni

    wanadamu ambao hawaishi kupata-

    na na mapenzi ya Mungu. (1 Yoh. 2:

    17) Dunia na wanadamu waaminifu

    wataokoka.1/1, ukurasa wa 5-7.

    Ijapokuwa Abeli alikufa, ni ka-tika maana gani bado anasemanasi? (Ebr. 11:4)

    Anafanya hivyo kupitia imani. Tu-

    naweza kuiga imani yake na kujitahi-

    di kuifuata. Mfano wake unaende-

    lea kuishi nao ni kiwango imara

    tunachoweza kuiga.1/1, ukurasa

    wa 12.

    Hatupaswi kuruhusu chochote ki-tutenganishe na Mungu katikasehemu gani?

    Baadhi ya sehemu hizo ni: kazi

    yetu ya kimwili, tafrija na burudani

    tunazochagua, jinsi tunavyoshughu-

    lika na mshiriki wa familia aliyete-

    ngwa na ushirika, matumizi ya vifaa

    vya kielektroniki, kuhangaikia afya

    yetu, maoni yasiyofaa kuhusu pesa,

    na kufikiri kwamba mapendeleo au

    maoni yetu ni yenye thamani sana.

    1/15, ukurasa wa 12-21.

    Tunaweza kujifunza nini kutoka-na na unyenyekevu wa Musa?

    Musa hakujivuna alipopata mamla-

    ka, naye alimtegemea Mungu bada-

    la ya kujitegemea mwenyewe. Hatu-

    paswi kuruhusu uwezo, mamlaka,

    wala vipawa vyetu vifanye tuwe na

    kiburi; badala yake tunapaswa ku-

    mtegemea Yehova. (Met. 3:5, 6)

    2/1, ukurasa wa 5.

    Wale watakaofufuliwa wataishiwapi?

    Hesabu ndogo, yaani, 144,000, wa-

    taishi mbinguni. Hata hivyo, wengi

    watafufuliwa na kuishi duniani, wa-

    kifurahia uzima wa milele duniani.

    3/1, ukurasa wa 6.

    Waisraeli hawakutahiriwamoyoni katika maana gani?(Yer. 9:26)

    Walikuwa na mioyo migumu na ye-

    nye kuasi, nao walihitaji kuondolea

    mbali mambo yaliyofanya mioyo yao

    iwe migumu, yaani, mawazo, nia, au

    mapendezi yaliyopingana na ya Mu-

    ngu. (Yer. 5:23, 24)3/15, ukurasa

    wa 9-10.

    Yesu aliwekaje mfano katikakuwa na maisha yenye kusudi?

    Alikuwa na kusudi maishani, yaani,

    kufanya mapenzi ya Mungu. Alimpe-

    nda sana Baba yake, na watu pia.

    Pia, Yesu alijua kwamba alipendwa

    na kukubaliwa na Baba yake. Hayo ni

    mambo muhimu ili kuwa na maisha

    yenye kusudi.4/1, ukurasa wa 4-5.

    Sehemu ya kidunia ya tengenezola Mungu inatia ndani nini?

    Inatia ndani Baraza Linaloongoza,

    halmashauri za tawi, waangalizi wa-

    naosafiri, mabaraza ya wazee, ma-

    kutaniko, na Shahidi mmoja-mmoja.

    4/15, ukurasa wa 29.

    Kwa nini tunaweza kusema kwa-mba Mungu hakuwa mkatili ali-potekeleza hukumu zake?

    Yehova hafurahii kifo cha mwovu.

    (Eze. 33:11) Matendo yake ya zama-

    ni yanaonyesha kwamba kwa upe-

    ndo Mungu huwaonya watu kabla ya

    kutekeleza hukumu. Jambo hilo lina-

    tupa tumaini la kuokoka hukumu

    zake za wakati ujao.5/1, ukurasa

    wa 5-6.

    Je, Waisraeli waliwaua wahalifukwa kuwatundika juu ya miti?

    Hapana. Mataifa mengine katika

    nyakati za kale yalifanya hivyo, laki-

    ni Waisraeli hawakufanya hivyo. Ka-

    tika Maandiko ya Kiebrania, wate-

    nda maovu waliuawa kwanza, labda

    kwa kupigwa kwa mawe. (Law. 20:2,

    27) Kisha, huenda maiti hiyo ilitundi-

    kwa juu ya mti ili kuwa onyo kwa we-

    ngine.5/15, ukurasa wa 13.

    Kwa nini wanadamu wameshi-ndwa kuleta amani duniani?

    Ingawa wanadamu wametimiza ma-

    mbo mengi, hawana uwezo wa kuo-

    ngoza hatua zao wenyewe. (Yer.

    10:23) Kwa kuwa Shetani anatawa-

    la ulimwengu, wanadamu hawata-

    weza kuleta amani. (1 Yoh. 5:19)

    6/1, ukurasa wa 16.

    JE, UNAKUMBUKA?

    Je, umesoma kwa makini makala za hivi karibuni za Mnara wa Mlinzi?Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:

    sUnaweza kupakua

    gazeti hili na machapisho

    mengine bila malipo

    kwenye www.jw.org/sw

    Unaweza pia kusoma

    Biblia ya Tafsiri ya

    Ulimwengu Mpya

    kwenye Intaneti

    Tumia alama hii

    kufungua gazeti

    kwenye Intaneti au

    tumia anwani ya

    www.jw.org/sw

    no

    p

    w1

    30

    6/1

    5-S

    W

    http://www.jw.org/http://www.jw.org/swhttp://www.jw.org/sw