jamhuri ya muungano wa tanzania wizara ya uchukuzi€¦ · kampuni ya ndege tanzania (atcl). dira...

98
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI TAARIFA YA MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA BARA (1961 - 2011) DESEMBA, 2011.

Upload: others

Post on 29-Oct-2020

32 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA UCHUKUZI

TAARIFA YA MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA BARA (1961 - 2011)

DESEMBA, 2011.

Page 2: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

ii

YALIYOMO

1.0 MAELEZO YA UTANGULIZI KUTOKA KWA WAZIRI WA UCHUKUZI . 1

2.0 UJUMBE WA KATIBU MKUU - WIZARA YA UCHUKUZI ...................... …4

3.0 UTANGULIZI ...................................................................................................... 7

4.0 HISTORIA FUPI YA WIZARA YA UCHUKUZI ............................................. 7

5.0 DIRA NA DHAMIRA YA WIZARA ................................................................... 7

5.1 Dira........................................................................................................................ 7

5.2 Dhamira ................................................................................................................ 8

6.0 MUUNDO WA WIZARA YA UCHUKUZI ........................................................ 8

6.1 Taasisi zilizo chini ya Wizara ............................................................................... 8

6.1.1 Wakala .................................................................................................................. 8

6.1.2 Mamlaka za Udhibiti ............................................................................................ 8

6.1.3 Mabaraza .............................................................................................................. 8

6.1.4 Mashirika na Makampuni .................................................................................... 8

7.0 MAJUKUMU YA WIZARA YA UCHUKUZI ................................................... 9

8.0 MALENGO YA WIZARA YA UCHUKUZI ...................................................... 9

9.0 UONGOZI NA UTAWALA KUANZIA MWAKA 1961 – 2011 ....................... 10

10.0 SERA NA SHERIA............................................................................................. 22

11.0 SEKTA NDOGO ZILIZO CHINI YA WIZARA YA UCHUKUZI ........................ 23

9.1 USAFIRI WA NCHI KAVU.................................................................................. 23

9.1.1 Shirika la Reli Tanzania ......................................................................................... 23

9.1.2 Kuanzishwa kwa Kampuni Miliki ya Rasilimali za Reli (RAHCO) ................. 26

9.1.3 Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) ..................................... 28

9.2 USAFIRI/UCHUKUZI WA MAJINI ................................................................ 32

9.2.1 Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) .............................................................. 32

9.2.2 Kampuni ya Meli ya SINOTASHIP ................................................................... 43

9.2.3 Kampuni ya Huduma za Meli – MSCL ............................................................. 46

9.2.4 Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA)........ 53

9.3 USAFIRI WA ANGA ......................................................................................... 57

9.3.1 Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) .............................................................. 57

9.3.2 Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) ............................................................ 62

Page 3: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

iii

9.3.3 Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) .............................................................. 72

9.3.4 Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) ............................................................... 74

9.4 VYUO VYA MAFUNZO CHINI YA WIZARA ............................................... 76

9.4.1 Chuo Cha Bahari Dar Es Salaam (DMI) ........................................................... 76

9.4.2 Chuo Cha Usafirishaji (NIT) .............................................................................. 84

9.5 HUDUMA ZA HALI YA HEWA NCHINI ....................................................... 87

Page 4: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

1

1.0 MAELEZO YA UTANGULIZI KUTOKA KWA WAZIRI WA UCHUKUZI

Kipindi hiki tunapoadhimisha miaka 50 tangu tupate uhuru mwaka 1961, Taifa

linashuhudia mabadiliko makubwa ya kisera na kimuundo katika Sekta ya Uchukuzi na Hali ya

Hewa. Miundombinu mbalimbali na huduma za uchukuzi zimeboreka kwa kiasi kikubwa.

Mara baada ya kupata uhuru, Serikali ilifanya mabadiliko makubwa ya kiuchumi kwa

kuanzisha programu na mikakati mbalimbali yenye lengo la kufufua uchumi. Programu hizo ni

pamoja na programu ya kufufua uchumi (Economic Recovery Programme) na marekebisho ya

kimuundo na kimenejimenti (Structural Adjustment Programme). Kufuatia juhudi hizo, mwaka

1987, Serikali ilizindua Programu ya kufufua sekta ya uchukuzi (Transport Sector Recovery

Programme) ili iwe chachu katika juhudi za kufufua uchumi. Mabadiliko katika sekta ya

uchukuzi yalilenga kuboresha miundombinu na huduma za uchukuzi ili kusaidia utendaji wa

sekta nyingine za kiuchumi na kijamii.

Baadhi ya Programu zilizoanzishwa kwa lengo la kuboresha sekta ya uchukuzi ni

pamoja na;

Programu ya kuboresha miundombinu na huduma za bandari (Port Modernization

Programme -1985),

Programu ya uboreshaji wa sekta ya uchukuzi (Transport Sector Recovery Proggramme

- 1987),

Programu ya kuboresha miundombinu na huduma za Reli (Railway Restructuring

Programme -1991), na

Programu ya kuboresha miundombinu na huduma za barabara (Integrated Roads

Programme - 1991).

Aidha, katika mwaka 1992, Serikali iliruhusu sekta binafsi kushiriki katika utoaji wa

huduma za ndani za uchukuzi kwa njia ya anga.

Juhudi nyingine zilizochukuliwa ni kubadili mfumo wa uendeshaji na uongozi wa Idara

na mashirika mbalimbali yenye majukumu ya kuendeleza Sekta za Uchukuzi na Hali ya Hewa

nchini. Kutokana na hatua hizi, ziliundwa taasisi mbalimbali za Umma ambazo zilisaidia

kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi. Taasisi hizo ni pamoja na Mamlaka ya Udhibiti

wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA),

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mamlaka ya Reli Tanzania na Zambia

Page 5: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

2

(TAZARA). Taasisi nyingine ni Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Mamlaka ya Hali ya

Hewa (TMA) na Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA),

Vile vile jitihada za kuboresha usafirishaji na uchukuzi nazo zilifanywa kwa kuanzisha;

Kampuni Miliki ya Mali za Reli iliyokuwa TRC (RAHCO),

Kampuni ya Reli Tanzania (TRL),

Kampuni ya uendelezaji wa uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KADCO) na

Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL).

Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na

Hali ya Hewa zenye ubora, salama, gharama nafuu na endelevu zinazochochea maendeleo ya

jamii kwa kuzingatia dira ya taifa ifikapo mwaka 2025.

Kutokana na dira ya wizara na ile ya taifa ya mwaka 2025, hali ya miundombinu na

huduma za uchukuzi bado hazijafikia viwango vya kukidhi mahitaji ya kiuchumi na kijamii. Ili

kuimarisha na kuboresha miundombinu na huduma za uchukuzi, Wizara ya Uchukuzi

imepanga kutekeleza yafuatayo;

Kuongeza uwekezaji katika miundombinu ya uchukuzi.

Kushirikisha Sekta binafsi katika uwekezaji kupitia utaratibu wa ubia kati ya Sekta ya

Umma na binafsi (PPP). Hatua hii itahusu kutafuta wawekezaji kwenye miundombinu

ya reli, viwanja vya ndege na bandari.

Kuboresha Rasilimali watu kwa kuimarisha vyuo vya mafunzo katika nyanja za Reli,

Anga, Majini na hali ya hewa.

Kuimarisha usalama wa abiria na mizigo katika vyombo vya uchukuzi.

Kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika sekta ya uchukuzi. Hii ni pamoja na

utekelezaji wa Mpango Kamambe wa Sekta ya Reli, huduma za pamoja za utafutaji na

uokoaji, ushirikiano katika kupambana na matukio ya uharamia na uimarishaji wa

usalama wa usafiri wa Anga.

Kuimarisha huduma za reli ya Dar es Salaam - Tabora hadi Kigoma na Mwanza

pamoja na matawi yake,

Kujenga upya Reli ya Kati na matawi yake yote na kujenga reli mpya kutoka Isaka hadi

Kigali (Rwanda) na Musongati (Burundi) kwa kiwango cha kimataifa (Stndard Gauge),

Kukarabati na kuimarisha huduma za reli ya Tanga hadi Arusha,

Kuboresha reli ya Tanga hadi Arusha na kujenga reli mpya ya Arusha hadi Musoma

kwa kiwango cha kimataifa (Standard Gauge)

Kuimarisha huduma za bandari za Dar es Salaam, Mtwara na Tanga,

Kujenga bandari mpya za Mbegani (Bagamoyo) na Mwambani (Tanga), na

Kujenga na kuboresha miundombinu ya viwanja vya ndege

Page 6: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

3

Katika kipindi cha miaka 50 ijayo, Serikali itahakikisha kuwa miundombinu na huduma za

uchukuzi zinaboreshwa ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka siku hadi siku. Lengo ni

kuhakikisha kuwa mifumo yote ya uchukuzi (Reli, Barabara, Anga, bandari na hali ya hewa)

inafanya kazi kwa kutegemeana na inakuwa na mtandao wa reli na usafiri wa anga

unaoiunganisha nchi nzima. Katika kufanya hayo, Sekta binafsi itashirikishwa kikamifu.

Kutokana na juhudi zilizofanyika na zinazoendelea kufanyika katika kuboresha

miundombinu na huduma za uchukuzi tangu tupate uhuru, Sekta ya uchukuzi tunasema

TUMETHUBUTU, TUMEWEZA, TUNAZIDI KUSONGA MBELE. Kwa pamoja,

tutafanikiwa.

Omari Rashid Nundu (Mb),

WAZIRI WA UCHUKUZI

Desemba, 2011

Page 7: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

4

2.0 UJUMBE W AKA TIBU MKUU - WIZARA YA UCHUKUZI

Mwezi Desemba, 2011 nchi yetu inasherehekea miaka 50 ya

Uhuru wa Tanzania Bara. Sherehe hizo zinaambatana na kuainisha tulikotoka; mafanikio

yaliyopatikana na tuendako katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa. Mafanikio

yaliyopatikana ni pamoja na kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka shilingi bilioni 7.2 mwaka

1961 hadi kufikia shilingi trilioni 16.83 mwaka 2010. Ongezeko hili linachangiwanasektaya

Uchukuzi pamoja na sekta nyingine za kuichumi na kijamii.

Mchango wa sekta ya Uchukuzi katika pato la Taifa kwa mwaka 2010 pekee ni shilingi bilioni

853.53 sawa na asilimia 5.4 ya pato la Taifa. Kati ya mwaka 2005 na 2010 sekta ya Uchukuzi

imekua kwa wastani wa asilimia 6.4 na hivyo kuwa miongoni mwa sekta muhimu katika

kukuza uchumi wa Taifa letu.

Wakati wa Uhuru wa Tanzania Bara mwaka 1961, majukumu ya sekta ya uchukuzi yalikuwa

chini ya iliyokuwa Wizara ya Mawasiliano, Umeme na Ujenzi. Kwa nyakati tofauti, majukumu

yasekta ya uchukuzi yamekuwa yakijumuishwa pamoja na sekta nyingine chini ya Wizara za

Usafirishaji, Kazi na Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mawasiliano na Ujenzi na

Miundombinu.

Baada ya Serikali ya Awamu ya Nne kuingia madarakani katika kipindi chake cha pili,

Desemba, 2011, Wizara ya Miundombinu iligawanywa na kuundwa Wizara mpya za Uchukuzi

na ile yaUjenzi. Wizara ya Uchukuzi ina jukumu la kusimamia huduma na miundombinu ya

sekta ya Uchukuzi katika maeneo ya usafiri wa reli, usafiri wa majini, usafiri wa anga na

huduma za hali ya hewa

Majukumu ya Wizara ya Uchukuzi ni pamoja na kutunga sera zinazohusu sekta katika

masuala ya uchukuzi na hali ya hewa na kusimamia utekelezaji wake. Aidha, huratibu na

kusimamia shughuli za utoaji wa leseni na usalama wa usafiri wa anga. Pia Wizara inaendeleza

Page 8: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

5

na inasimamia ujenzi wa miundombinu ya reli, viwanja vya ndege, bandari na hali ya hewa.

Wizara ya Uchukuzi inasimamia masuala ya ulinzi na usalama katika Sekta ya Uchukuzi;

kuendeleza rasilimali watu pamoja na kusimamia Idara za Serikali, Taasisi, Mashirika ya

Umma, Programu na Miradi.

Katika kipindi cha miaka 50 iliyopita Wizara ya Uchukuzi imekuwa ikitekeleza

majukumu yake kwa kuzingatia Sera na Sheria za nchi, mipango na mikakati mbalimbali

ikiwemo MKUKUTA na Dira ya Taifa ya mwaka 2025.

Jitihada na mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya uchukuzi kwa miaka 50 iliyopita

ni pamoja na:

(i) Ujenzi wa Reli mpya kwenye maeneo ya:

Stesheni ya Ruvu - Mruazi (Kilometa 188) mwaka 1963,

Kilosa - Mikumi - Kidatu (kilometa 108) mwaka 1960-1965,

Kahe - Taveta (kilometa 18) mwaka 1984,

Manyoni - Singida (kilometa 115) mwaka 1985-1997.

(ii) Ujenzi wa reli ya Uhuru - TAZARA (kilometa 1,860; kwa upande wa Tanzania ni

km.975) mwaka 1970 - 1975. Reli hii inaanzia Dar es Salaam hadi New Kapiri

Mposhi, Zambia.

(iii) Ukarabati wa reli kati ya stesheni za Gulwe na Kilosa baada ya mafuriko,

(iv) Uimarishaji wa uwezo wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini ili kutoa utabiri wa hali ya

hewa wa uhakika.

(v) Uanzishwaji wa vyuo vya mafunzo katika Sekta ya Uchukuzi. Vyuo hivyo ni Chuo cha

Bahari Dar es Salaam (DMI), Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Chuo cha Hali ya

Hewa Kigoma, Chuo cha Reli Tabora, Chuo cha Usafiri wa Anga Dar es Salaam na

Chuo cha Bandari.

(vi) Ujenzi na upanuaji wa bandari za mwambao. Hii ni pamoja na kuongezeka kwa magati

kutoka 3 hadi 14 katika bandari ya Dar es Salaam; kuanzisha vituo 8 vya kuhifadhi

makasha nje ya bandari (ICDs).

(vii) Kuongezeka kwa shehena kupitia Bandari zetu kutoka tani milioni 1.2 mwaka 1961

hadi kufikia tani rnilioni 10.2 mwaka 2010.

(viii) Kuandaa na kuanza kutekeleza Mpango wa Uwekezaji katika Sekta ya Uchukuzi(TSIP)

(ix) Kuongezeka kwa Viwanja vya Ndege vya Kimataifa nchini kutoka kimoja mwaka 1961

hadi vitatu mwaka 2011. Mwaka 1961 kulikuwa na Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa

cha Dar es Salaam (hivi sasa Julius Nyerere International Airport - JNIA), Kiwanja cha

Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (Kilimanjaro International Airport - KIA)

kilichojengwa mwaka 1971 na Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Songwe

ambacho kinatarajiwa kukamilika Desemba, 2011.

Page 9: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

6

Pamoja na mafanikio mengi yaliyopatikana tangu Uhuru, Wizara ya Uchukuzi

imeendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali katika utekelezaji wa majukumu yake.

Changamoto hizo ni pamoja na uwezo mdogo wa kifedha kulinganisha na mahitaji halisi ya

miradi ya maendeleo, ajali mbalimbali ambazo zimepoteza maisha ya watu na mali, uchakavu

wa miundombinu ya reli na Bandari.

Katika kulinda na kuendeleza mafanikio yaliyopatikana baada ya miaka 50 ya Uhuru,

Wizara imejiwekea malengo ya muda rnrefu kwa ajili ya kuendeleza sekta ya uchukuzi.

Baadhi ya malengo hayo ni pamoja na kuendelea kutekeleza Mpango wa Uwekezaji wa Sekta

ya Uchukuzi (TSIP) ili kuboresha miundombinu ya reli, bandari na viwanja vya ndege. Lengo

la Mpango huu ni kupunguza umaskini na kuleta maendeleo; kuimarisha bandari za mwambao

na zile za maziwa makuu; kuimarisha huduma za uchukuzi wa anga na hali ya hewa nchini;

kuweka mazingira mazuri ya kuvutia sekta binafsi kuwekeza katika sekta ya uchukuzi;

uendelezaji wa matumizi ya TEHAMA katika utekelezaji wa majukumu ya Serikali na

kuendeleza rasilimali watu ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi katika sekta.

Ni matarajio yangu kwamba katika kipindi cha miaka 50 ijayo Wizara ya Uchukuzi

itakuwa na miundombinu ya Uchukuzi ya kisasa inayoendeshwa kwa kutumia teknolojia ya

kisasa. Aidha, ni matumaini yangu pia kwamba watumishi wa Wizara ya Uchukuzi na

Watanzania kwa ujumla tutawajibika zaidi katika miaka 50 ijayo kwa nia ya kuijenga nchi kwa

manufaa yetu na vizazi vijavyo.

Tumethubutu, Tumeweza Tunazidi kusonga mbele

Mhandisi Omar A. Chambo

KATIBU MKUU

Desemba, 2011

Page 10: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

7

2.0 UTANGULIZI

Tanzania Bara ilipata uhuru mwaka 1961. Mwaka 2011 Serikali imeazimia kusherehekea

miaka 50 ya Uhuru. Azma hiyo ya kusherehekea miaka 50 ya Uhuru ilitangazwa kwa

mara ya kwanza na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.

Jakaya Mrisho Kikwete wakati akitoa salamu za mwaka mpya 2011.

Taifa linasherehekea miaka 50 ya Uhuru wake huku likishuhudia mafanikio ya

maendeleo katika nyanja mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kisiasa. Maendeleo haya ya

jumla yamechangiwa na michango ya sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na Sekta ya

Uchukuzi.

Nafasi ya Sekta ya Uchukuzi katika maendeleo ya nchi inaweza kufananishwa na damu

katika mwili wa binadamu. Sekta ya Uchukuzi huwezesha ukuaji wa shughuli za

kiuchumi na kijamii. Kwa mfano wakulima wanategemea mchango wa sekta ya uchukuzi

katika kusafirisha pembejeo katika maeneo yao ya kilimo na kusafirisha mazao ya kilimo

kutoka kwenye maeneo ya uzalishaji kwenda kwenye masoko; wafanyabiashara na

viwanda huhitaji kusafirisha bidhaa zao kutoka maeneo ya uzalishaji kwenda kwa

watumiaji katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi; watalii huhitaji usafiri kuja

nchini na kwenda kwenye maeneo mbalimbali yenye vivutio vya kitalii nchini, usafiri

unahitajika kuwawezesha wananchi kupata huduma za kijamii kama elimu, afya, nk.

3.0 HISTORIA FUPI YA WIZARA YA UCHUKUZI

Wakati wa Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961, shughuli za Sekta ya Uchukuzi zilikuwa chini ya

iliyokuwa Wizara ya Mawasiliano, Umeme na Ujenzi. Kwa nyakati tofauti, shughuli za Sekta ya

Uchukuzi zimekuwa zikijumuishwa pamoja na Sekta nyingine kama inavyoonekana katika

Jedwali Na. 5.1.

Mnamo Disemba 2010 baada ya Serikali ya Awamu ya Nne kuingia madarakani kwa kipindi chake

cha pili, Wizara ya Uchukuzi iliundwa. Wizara hii inahusika na usimamizi wa sekta za Uchukuzi na

Hali ya Hewa.

4.0 DIRA NA DHAMIRA YA WIZARA

4.1 Dira

Dira ya Wizara ya Uchukuzi ni kuwa na Miundombinu na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

zenye ubora, salama, gharama nafuu na endelevu zinazochochea maendeleo ya jamii kwa

kuzingatia dira ya Taifa ifikapo mwaka 2025.

Page 11: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

8

4.2 Dhamira

Dhamira ya Wizara ni kuwa na huduma na Miundombinu ya Uchukuzi, ambazo ni salama;

zinazotegemewa; zilizo na uwiano na ambazo zinakidhi mahitaji ya usafiri na uchukuzi katika

kiwango bora kwa bei nafuu na zinazoendana na mikakati ya Serikali ya maendeleo ya kiuchumi na

kijamii wakati huo huo zikiwa endelevu kiuchumi na kimazingira.

5.0 MUUNDO WA WIZARA YA UCHUKUZI

Wizara ya Uchukuzi ina Idara tano ambazo ni Idara za Utawala na Rasilimali Watu, Miundombinu

ya Uchukuzi, Huduma za Uchukuzi, Sera na Mipango, na Usalama na Mazingira. Aidha, Wizara

ina Vitengo sita ambavyo ni Uhasibu, Habari, Ununuzi, Ukaguzi wa Ndani, Sheria na TEHAMA.

5.1 Taasisi zilizo chini ya Wizara

5.1.1 Wakala

Wakala za Serikali ambazo zipo chini ya Wizara ni pamoja na Wakala wa Hali ya Hewa

(TMA), Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), na Wakala wa Viwanja vya Ndege

(TAA).

5.1.2 Mamlaka za Udhibiti

Ili kuhakikisha kuwa huduma za Uchukuzi zinatolewa kwa viwango na kwa kuzingatia

usalama, Serikali iliunda Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) na Mamlaka ya Usafiri

wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA).

5.1.3 Mabaraza

i. Baraza la Watumiaji wa Huduma za Usafiri wa Nchi kavu na Majini

ii. Baraza la Watumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga

5.1.4 Mashirika na Makampuni

Wizara ina Taasisi na Makampuni ambayo yanahusika na utekelezaji wa majukumu ya

Sekta. Taasisi na Makampuni hayo ni kama ifuatavyo:-

i. Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA)

ii. Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL)

iii. Kampuni Miliki ya Raslimali za Reli (RAHCO)

iv. Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA)

v. Kampuni ya Reli Tanzania (TRL)

Page 12: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

9

vi. Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL)

vii. Kampuni ya Meli ya pamoja kati ya Serikali ya China na Tanzania

(SINOTASHIP)

viii. Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT)

ix. Chuo cha Bahari Dar Es Salaam (DMI)

x. Chuo cha Hali ya Hewa (Kigoma)

xi. Kampuni ya Uendelezaji wa Kiwanja cha ndege cha Kilimanjaro (KADCO)

6.0 MAJUKUMU YA WIZARA YA UCHUKUZI

Kulingana na Hati (Instrument) iliyotolewa na Mhe. Rais kwa mujibu wa Katiba ya Nchi,

Wizara ya Uchukuzi imepewa majukumu ya kusimamia masuala yafuatayo:

i. Kutunga Sera zinazohusu Sekta katika masuala ya Uchukuzi na Hali ya Hewa na

kusimamia Utekelezaji wake.

ii. Kuratibu na kusimamia shughuli za Utoaji wa Leseni za usafirishaji.

iii. Kusimamia masuala ya Usalama wa usafiri wa Anga.

iv. Kusimamia masuala ya Usafiri na Uchukuzi wa Anga

v. Kuendeleza na kusimamia Viwanja vya Ndege (vikubwa na vidogo) na huduma

zake.

vi. Kuendeleza na kusimamia Miundombinu ya Reli na Huduma zake.

vii. Kuendeleza na kusimamia miundombinu ya Bandari na Huduma zake.

viii. Kusimamia masuala ya Ulinzi na Usalama katika Sekta ya Uchukuzi.

ix. Kuendeleza na kusimamia miundombinu ya Hali ya Hewa na Huduma zake.

x. Kuongeza tija (Utendaji kazi) na kuendeleza Rasilimali watu.

xi. Kusimamia Idara za Serikali, Taasisi, Mashirika ya Umma, Programu na Miradi

iliyo chini ya Wizara.

7.0 MALENGO YA WIZARA YA UCHUKUZI

Katika kufanikisha utekelezaji wa majukumu yake, Wizara ilijiwekea malengo ya muda mrefu

kama ifuatavyo:

i. Kutayarisha na kutekeleza mpango wa muda mrefu wa maendeleo ya Sekta ya

Uchukuzi ili kuboresha miundombinu ya reli, bandari na viwanja vya ndege kwa

lengo la kupunguza umasikini na kuleta maendeleo,

ii. Kuimarisha reli ili kuongeza uwezo wa uchukuzi wa shehena nchini na zile za nchi

jirani,

iii. Kuimarisha bandari za mwambao na zile za maziwa makuu

Page 13: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

10

iv. Kutekeleza Mpango Kabambe wa Uendelezaji Bandari (Ports Masterplan) katika

maeneo muhimu ya kipaumbele katika uendelezaji wa bandari nchini.

v. Kuimarisha huduma za uchukuzi wa anga hasa viwanja vya ndege.

vi. Kuendelea kuweka mazingira mazuri ya kuvutia sekta binafsi kuwekeza katika

sekta.

vii. Kuendelea kushirikiana na taasisi husika katika kushughulikia masuala mtambuka

kama vile kampeni za kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI, uhifadhi

wa mazingira, masuala ya jinsia pamoja uendelezaji wa matumizi ya Teknolojia ya

Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika utekelezaji wa shughuli za Serikali.

viii. Kuendeleza na kuimarisha huduma za hali ya hewa nchini.

ix. Kuendeleza rasilimali watu ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi.

8.0 UONGOZI NA UTAWALA KUANZIA MWAKA 1961 – 2011

Mawaziri mbalimbali walipata fursa ya kuongoza Wizara hii tangu tupate uhuru mwaka

1961. Waziri wa kwanza wa Wizara ya Mawasiliano, Umeme na Ujenzi ambayo ilikuwa

na dhamana ya kusimamia shughuli za uchukuzi, alikuwa marehemu Amir Habib Jamal.

Mawaziri wengine ambao waliopata fursa ya kuiongoza Wizara hii wameoneshwa katika

Jedwali Na. 7.1. Aidha, Manaibu Waziri, Makatibu Wakuu na Manaibu Makatibu Wakuu

waliowahi kuwa katika wizara hii wameoneshwa kuanzia Jedwali Na. 7.2 hadi 7.4.

Jedwali Na.7.1: Wizara ya Uchukuzi ilivyokuwa inajulikana na Mawaziri waliowahi

kuiongoza Wizara tangu mwaka 1961 hadi 2011

S/N JINA JINA LA WIZARA KIPINDI

1. Amir Habib Jamal Mawasiliano, Umeme na Ujenzi 1959 - 1963

2. Job M. Lusinde Mawasiliano, Umeme na Ujenzi 1963 - 1965

3. Job M. Lusinde Usafirishaji, Kazi na Ujenzi 1965 - 1972

4. Alfred C. Tandau Mawasiliano na Uchukuzi 1972 - 1973

5. Job M. Lusinde Mawasiliano na Ujenzi 1973 - 1976

6. Amir H. Jamal Mawasiliano na Uchukuzi 1977 - 1979

7. Guntram A. M. Itatiro Mawasiliano na Ujenzi 1980 - 1981

Page 14: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

11

8. Ibrahim Kaduma Mawasiliano na Uchukuzi 1981

9. Agustin Mwingira Mawasiliano na Uchukuzi 1982

9. Guntram A. M. Itatiro Mawasiliano na Uchukuzi 1981 - 1984

10. John. S. Malecela Mawasiliano na Uchukuzi 1984 - 1985

11. Steven Kibona Mawasiliano na Ujenzi 1986 - 1989

12. Mustafa Nyang‟anyi Mawasiliano na Ujenzi 1989 – 1990

13. Pius Ngw‟andu Uchukuzi 1990

14. Jackson Makweta Mawasiliano na Uchukuzi 1991 – 1992

15. Prof. Philemon Sarungi Mawasiliano na Uchukuzi 1993 - 1994

16. Nalaila Kiula Mawasiliano na Uchukuzi 1994 - 1995

17. William J. Kusila Mawasiliano na Uchukuzi 1995 - 1997

18. Ernest Nyanda Mawasiliano na Uchukuzi 1997 - 2000

19. Prof. Mark Mwandosya Mawasiliano na Uchukuzi 2000 - 2006

20. Basil P. Mramba Miundombinu 2006 - 2007

21. Andrew Chenge Miundombinu 2007 - 2008

22. Dkt.Shukuru J. Kawambwa Miundombinu 2008 - 2010

23. Omari R. Nundu Uchukuzi 2010 - hadi sasa

Jedwali Na.7.2: Manaibu Waziri waliopata fursa ya kuongoza Wizara 1961 – 2011

S/N JINA JINA LA WIZARA KIPINDI

1. Chifu E. A. Mang‟enya Mawasiliano, Umeme na Ujenzi 1963

2. John. A. Mhaville Mawasiliano na Ujenzi 1964

3. F.V. Mponji na

Alhaji Omari Muhaji Mawasiliano, Kazi na Ujenzi 1965 - 1967

4. F.V. Mponji na

Edward M. Sokoine Usafirishaji, Kazi na Ujenzi 1967 - 1968

Page 15: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

12

5. Richard. S. Wambura Mawasiliano, Uchukuzi na Kazi 1969

6. Robert Ng‟itu Mawasiliano na Ujenzi 1973

7. Mustafa Nyang‟anyi Mawasiliano na Ujenzi 1974

8. Samwel J. Sitta Mawasiliano na Uchukuzi 1977

9. Edgar M. Majogo Mawasiliano na Uchukuzi 1978 -1979

10. Arcado D. Ntagazwa Mawasiliano na Ujenzi 1985 – 1987

11. Simai Pandu Makame Mawasiliano na Uchukuzi 1991- 1992

12. Capt.Ditopile Mzuzuri Mawasiliano na Uchukuzi 1993

13. Edgar M. Majogo Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi 1993 - 1995

14. Dkt. Maua Daftari Mawasiliano na Uchukuzi 1995 – 2005

15. Dkt. Maua Daftari na

Dkt.Makongoro Mahanga Miundombinu 2006 - 2008

16. Hezekiel N. Chibulunje Miundombinu 2008 - 2010

17. Athuman R. Mfutakamba Uchukuzi 2010 hadi sasa

Jedwali Na.7.3: Makatibu wakuu waliopata fursa ya kuongoza Wizara 1961 – 2011

S/N JINA JINA LA WIZARA KIPINDI

1. F. K. Burengelo Mawasiliano, Uchukuzi na Kazi 1962

2. Balozi Juma Maggidi Mawasiliano, Umeme na Ujenzi 1962 – 1965

3. Ainamansa E. Mbuya Usafirishaji, Kazi na Ujenzi 1965 - 1968

4. J. Sepeku Mawasiliano na Uchukuzi 1970

5. Daniel N. M. Mloka Mawasiliano na Ujenzi 1978 – 1979

6. Odira Ongara Mawasiliano na Uchukuzi 1979 – 1980

7. Richard Shenkunde Juma Mawasiliano na Uchukuzi 1980 –1983

8. Paul Justine Mkanga Mawasiliano na Uchukuzi 1983 - 1984

Page 16: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

13

9. Odira Ongara Mawasiliano na Ujenzi 1984 – 1987

10. Paul Justine Mkanga Mawasiliano na Ujenzi 1987 – 1989

11. Dkt Felician Mujuni Mawasiliano na Ujenzi 1989 – 1990

12. Balozi Richard Maliki Mawasiliano na Uchukuzi 1990 – 1993

13. Dkt George Mlingwa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi 1993 – 1995

14. Salim M. Msoma Mawasiliano na Uchukuzi 1995 – 2005

15. John Kijazi Miundombinu 2005 – 2006

16. Dkt.Enos Bukuku Miundombinu 2006 – 2008

17. Mhandisi Omar A. Chambo Miundombinu 2008 - 2010

18. Mhandisi Omar A. Chambo Uchukuzi 2010 hadi sasa

Jedwali Na.7.4: Manaibu Makatibu wakuu waliopata fursa ya kuongoza Wizara

1. Mhandisi Omar A. Chambo Miundombinu 2006 - 2008

2. Ndg. Joyce Mapunjo Miundombinu 2008 - 2009

3. Balozi Harbert Mrango Miundombinu 2010

4. Ndg. John T. Mngodo Uchukuzi 2011 hadi sasa

Page 17: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

14

Kielelezo 1: PICHA ZA VIONGOZI WA SASA WA WIZARA

Mhe. Omari R. Nundu (Mb.)

Waziri wa Uchukuzi

Mhe. Dkt. Athuman R. Mfutakamba (Mb.)

Naibu Waziri wa Uchukuzi

Mhandisi Omar A. Chambo Ndg. John T. Mngodo

Katibu Mkuu Naibu Katibu Mkuu

Page 18: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

15

Kielelezo 2: PICHA ZA MAWAZIRI WALIOWAHI KUONGOZA WIZARA

Amir H. Jamal

Job M. Lusinde

Wizara ya Mawasiliano, Umeme na Ujenzi

Wizara ya Mawasiliano, Umeme na Ujenzi

1959 - 1963

1963 - 1972

Alfred C. Tandau

Job M. Lusinde

Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi

Wizara ya Mawasiliano na Ujenzi

1972 - 1973

1973 - 1976

Amir H. Jamal

Guntram A.M Mtatiro

Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi

Wizara ya Mawasiliano na Ujenzi

1977 - 1979

1980 - 1981

Page 19: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

16

Ibrahim Kaduma

Augustin Mwingira

Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi

Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi

1981

1982

Guntram A.M Mtatiro

John S. Malecela

Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi

Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi

1982- 1984

1984 - 1985

Steven Kibona

Mustafa Nyang'anyi

Wizara ya Mawasiliano na Ujenzi

Wizara ya Mawasiliano na Ujenzi

1985 - 1989

1989 - 1990

Page 20: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

17

Pius Ngw'andu

Jackson Makweta

Wizara ya Uchukuzi

Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi

1990

1991 - 1992

Prof. Philemon Sarungi

Nalaila Kiula

Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi

Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi

1993 - 1994

1994- 1995

William J. Kusila

Ernest Nyanda

Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi

Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi

1995- 1997

1997- 2000

Page 21: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

18

Prof. Mark Mwandosya

Basil Mramba

Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi

Wizara ya Miundombinu

2000- 2006

2006 - 2007

Andrew Chenge

Dkt. Shukuru J. Kawambwa

Wizara ya Miundombinu

Wizara ya Miundombinu

2007 - 2008

2008- 2010

Page 22: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

19

Kielelezo 3: PICHA ZA MANAIBU MAWAZIRI WALIOWAHI KUONGOZA

WIZARA

Chifu E. A Mang'enya John A. Mhavile

Wizara ya Mawasiliano,

Umeme na Ujenzi

Wizara ya Mawasiliano na

Ujenzi

1963 1964

F.V Mponji Alhaji Omari Muhaji

Wizara ya Mawasiliano, Kazi

na Ujenzi

Wizara ya Mawasiliano, Kazi

na Ujenzi

1965 - 1968 1965 - 1968

Edward M. Sokoine Richard S. Wambura

Wizara ya Usafirishaji, Kazi

na Ujenzi

Wizara ya Mawasiliano,

Uchukuzi na Kazi

1967 - 1968 1969

Page 23: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

20

Robert Ng'itu Mustafa Nyang'anyi

Wizara ya Mawasiliano na

Ujenzi

Wizara ya Mawasiliano na

Ujenzi

1973 1974

Samwel J. Sitta Edgar M. Majogo

Wizara ya Mawasiliano na

Uchukuzi

Wizara ya Mawasiliano na

Uchukuzi

1977 1978 - 1979

Arcado D. Ntagazwa Edgar M. Majogo

Wizara ya Mawasiliano na

Ujenzi

Wizara ya Ujenzi,

Mawasiliano na Uchukuzi

1985 – 1987

1993 - 1995

Page 24: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

21

Kapt. Ditopile U. Mzuzuri Dkt. Maua Daftari

Wizara ya Mawasiliano na

Uchukuzi

Wizara ya Mawasiliano na

Uchukuzi

1993 1995 - 2005

Dkt. Maua Daftari Dkt. Makongoro Mahanga

Wizara ya Miundombinu Wizara ya Miundombinu

2006 - 2008 2006 - 2008

Hezekiel N. Chibulunje

Wizara ya Miundombinu

2008 - 2010

Page 25: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

22

9.0 SERA NA SHERIA

Tangu uhuru Serikali imeendelea kuandaa sera na sheria mbalimbali kwa lengo la kuboresha

huduma katika sekta hii ya uchukuzi. Sera na sheria hizo ni pamoja na;

i. Airports Service Charges (1962)

ii. The Transport Licensing Act (1973) ambayo ilifanyiwa marekebisho mwaka 1978,

1979, 1994, 1996, 1999, 2001, 2005 na 2009 ikiwa inatekelezwa na Central Traffic

Licensing na Regional Licensing Authorities.

iii. The Aerodromes (Licensing and Control) Act No. 1 of 1974

iv. Tanzania Railways Corporation Act No. 11 of 1977

v. Civil Aviation Act No. 13 of 1977 ambayo ilifanyiwa marekebisho mwaka 2002 na

2003.

vi. Meteorology Act 1978

vii. Sheria ya Bunge Na. 30 ya 1997 kuhusu uundwaji wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege

viii. Sheria ya Bunge Na. 30 ya 1997 kuhusu uundwaji wa Mamlaka ya hali ya Hewa

Tanzania

ix. Sheria ya ya Bunge Na. 212 ya mwaka 1997 inayohusu uanzishwaji wa makampuni

iliyoanzisha MSC

x. Sheria ya Bunge Na. 9 ya mwaka 2001 iliyoanzisha Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri

wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA)

xi. Sheria ya Bunge Na. 4 ya Mwaka 2002 (Railway Act No. 4 of 2002) kuhusu uanzishaji

wa Reli Assets Holding Company – (RAHCO)

xii. Sera ya Taifa ya Uchukuzi (2003)

xiii. Mamlaka ya Usafiri wa Usafiri wa Anga (TCAA) ilianzishwa upya kwa Sheria Na. 10

ya mwaka 2003 (Civil Aviation Authority Act 2003)

xiv. Sera ya Taifa ya Teknohama 2003

xv. Sheria ya Bunge Na. 17 ya mwaka 2004 kuhusu uanzishaji wa Mamlaka ya Usimamizi

wa Bandari Tanzania (TPA)

xvi. Sera ya Taifa ya Usalama Barabarani 2010

Page 26: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

23

xvii. Sheria ya Bunge Na 4 ya mwaka 1975 kuhusu uanzishwaji wa TAZARA

10.0 SEKTA NDOGO ZILIZO CHINI YA WIZARA YA UCHUKUZI

10.1 USAFIRI WA NCHI KAVU

10.1.1 Shirika la Reli Tanzania

Uendelezaji wa Reli nchini ulianzishwa kwa mara ya kwanza wakati wa enzi za Utawala wa Kijerumani

mnamo miaka ya 1880, wakati reli ya kwanza ilipojengwa kutoka Tanga na kufika Mombo mwaka 1904.

Ujenzi wa reli hiyo uliendelea na kufika Moshi mwaka 1911, na baadaye Arusha katika mwaka 1929.

Ujenzi wa reli ya kati ulianzia Dar es salaam mnamo mwaka 1905 na kufika Morogoro mwaka 1907, na

baadaye kufika Mwanza mwaka 1926. Reli ya kutoka Tabora hadi Kigoma ilijengwa kati ya mwaka 1912

-1914. Mtandao wote wa reli kwa wakati huo uliendelea kumilikiwa na kuendeshwa na Serikali za

Kikoloni, hadi ilipofika Mwaka 1961, Tanganyika ilipojitawala.

Kama ilivyo katika nchi nyingi duniani, usafiri wa reli umeendelea kuwa nguzo muhimu ya kuwezesha na

kuchochea ukuaji wa uchumi na biashara. Hii inatokana na ukweli kwamba usafiri wa reli ni wa gharama

nafuu sana ikilinganishwa na aina nyingine za usafiri, hususan kwa kusafirisha mizigo mikubwa kwa

umbali mrefu kuanzia kilometa 400 na zaidi.

Wakati wa Utawala wa Kijerumani, ujenzi wa reli ulifanywa kwa lengo kubwa la kusafirisha mali ghafi

kama katani, kahawa, pamba, madini na mbao ngumu n.k kwa ajili ya Soko la Ulaya. Malighafi hizi kwa

ujumla zilisafirishwa kutoka bara kuelekea pwani kwa ajili ya kusafirisha nje ya nchi. Kwa Upande

mwingine usafiri wa reli ulitumika kama njia rahisi ya kusafirisha bidhaa mbalimbali za viwandani kutoka

nje ya nchi, kwa ajili ya soko la hapa nchini.

Mwaka 1948 Reli ya Tanganyika (Tanganyika Railways) na huduma za Bandari ( Port services)

ziliungana na makampuni ya reli ya Kenya na Uganda na bandari kuwa “ East African Railways and

Harbours – (EAR& H)” . Wakati Tanzania, Kenya na Uganda zilipoanzisha Jumuiya ya Afrika

Mashariki (EAC) mwaka 1967, Shirika la reli la Afrika Mashariki (EARC) liliundwa kama nguzo

mojawapo ya msingi wa kiuchumi wa Jumuiya ya Afrika mashariki. Katika miaka ya sabini (70s), Shirika

la reli la Afrika Mashariki lilianza kufifia polepole kutokana na mahusiano kudorora na kila nchi ikawa

inajitegemea zaidi yenyewe nje ya Jumuiya. Sehemu ya reli ya Tanzania wakati mwingine ilikuwa

ikijulikana kama EAR (T) ilianza kutafuta vitendea kazi vyake na kujitegemea. Mwaka 1977, baada ya

kuvunjika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Tanzania ilianzisha Shirika la Reli Tanzania ( Tanzania

Railways Corporation – TRC) kwa sheria ya Bunge Na. 11 ya mwaka 1977.

Mtandao wa Reli ya Kati uliopo hivi sasa una umbali wa jumla ya kilometa 2,707, kama unavyoanishwa

hapa chini.

Njia Kuu (Main Lines);-

Dar es Salaam –Tabora 840km

Tabora – Kigoma 411km

Page 27: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

24

Tabora – Mwanza 379km

Tanga - Moshi - Arusha 438km

Ruvu Junction – Mruazi Junction 188km

Matawi (Branch Lines);-

Kilosa – Kidatu 108 km

Kaliua - Mpanda 210 km

Manyoni – Singida 115 km

Kahe –Taveta (Mpakani na Kenya) 18 km

Mtandao wa TRC uliopo unahudumia nchi nne zisizopakana na bahari. Nchi hizo ni Burundi, Rwanda,

Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Vile vile mtandao huu unaungana na ule wa Kenya

kupitia tawi la reli lenye urefu wa Kilometa 18 kutoka Kahe hadi Taveta.

Katika kipindi cha miaka hamsini (1961 – 2011) baada ya uhuru mafanikio kadhaa yameweza kupatikana

katika Sekta ya Reli kama yanavyoainishwa katika aya zifuatazo.

Ujenzi wa Reli mpya

i. Kujengwa kwa reli (kilometa 188) kutoka Stesheni ya Ruvu hadi Mruazi iliyoko katika njia ya

reli ya Tanga – Arusha, mwaka 1963.

ii. Kukamilika kwa ujenzi wa reli kati ya Kilosa - Mikumi – Kidatu (kilometa 108) mwaka 1960-

1965.

iii. Kukamilika kwa ujenzi wa reli (kilometa 18) kati ya Kahe – Taveta mwaka 1984.

iv. Ujenzi wa reli (kilometa 115) kati ya Manyoni – Singida mwaka 1985-1997.

Kuanzishwa kwa Shirika la Reli la Afrika Mashariki

Moja ya mafanikio makubwa ilikuwa ni kuanzishwa kwa Shirika la Reli la Afrika Mashariki, lililodumu

kwa miaka kumi (1967 – 1977), ambapo zilizokuwa nchi za Afrika Mashariki (Kenya, Uganda na

Tanzania) ziliweza kuendesha shughuli za reli katika mtandao mmoja wa reli, wenye upana wa mita moja

(meter gauge). Shirika hili lilivunjika mwaka 1977 kutokana na kutoelewana miongoni mwa nchi

wanachama.

Usafirishaji wa Mizigo na Abiria

Sekta ya reli iliendelea kuwa njia muhimu katika usafirishaji wa mizigo na abiria hapa nchini. Mfano

mwaka 1984 kati abiria 4,100,000 waliosafirishwa kwa njia zote za usafiri abiria 3,040,000 walisafirishwa

kwa reli, hii ikiwa ni sawa na asilimia 74. Katika mwaka huo pia, kati ya tani 1,030,000 za mizigo yote

iliyosafirishwa nchini, tani 910,000 zilisafirishwa kwa njia ya reli, hii ikiwa ni sawa na asilimia 89.

Katika mwaka 2002, Shirika la Reli (TRC) lilivunja rekodi kwa kusafirisha jumla ya tani 1,446,000 za

mizigo, kiwango ambacho hakijawahi kufikiwa tangu mwaka 1977 Shirika lilipoanzishwa. Jedwali 9.1(a)

na Jedwali 9.1(b) yafuatayo yanabainisha jinsi ambavyo sekta ya reli iliweza kuchangia, kuwezesha na

kuchochea shughuli za kiuchumi, kijamii na kimaendeleo.

Page 28: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

25

Jedwali Na 9.1 (a): Usafirishaji wa abiria TRC (Miaka ya 1970, 1980, 1990 na

2000)

Mwaka Idadi ya abiria wote Idadi ya abiria

waliosafirishwa kwa Treni

Asilimia

1976 (1970‟s) 2,660,333 2,197,912 83

1987(1980‟s) 2,154,000 1,485,000 69

1990(1990‟s) 2,486,142 1,714,000 69

2007(2000‟s) 585,310

Jedwali Na 9.1 (b): Usafirishaji wa mizigo TRC (Miaka ya 1970, 1980, 1990 na

2000)

Mwaka Kiasi cha mizigo yote

iliyosafirishwa nchini

(Tani)

Kiasi cha mizigo

iliyosafirishwa kwa

Treni (Tani)

Asilimia

1976 (1970‟s) 712,030 698,206 98

1987(1980‟s) 1,000,000 902,000 90

1990(1990‟s) 1,011,580 898,810 89

2007(2000‟s) 545,241

Ubinafsishaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC)

Kama sehemu ya Mpango wa Taifa wa kubinafsisha Mashirika ya Umma, Shirika la Reli

Tanzania (TRC) lilibinafsishwa rasmi mnamo mwezi Septemba mwaka 2007, baada ya Serikali

ya Tanzania kuingia ubia na Kampuni ya RITES ya India, iliyokuwa imeshinda zabuni ya

kuendesha reli ya kati kwa kipindi cha miaka 25.

Ubinafsishaji huu ulisababisha kuundwa kwa Kampuni ya Reli Tanzania (Tanzania Railways

Ltd). Tanzania Railways Limited (TRL) ni Kampuni iliyoundwa na kumilikiwa kwa pamoja

kati ya Serikali ya Tanzania iliyomiliki asilimia 49 ya hisa na RITES iliyomiliki asilimia 51 ya

hisa. Kampuni ilianza kazi rasmi ya kuendesha reli ya kati mwezi Oktoba 2007, chini ya

menejimenti ya RITES.

Page 29: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

26

Pamoja na Serikali kuingia ubia na Kampuni ya RITES kwa lengo la kuboresha usafiri wa reli

ya kati, TRL ilishindwa kabisa kufikia na kutimiza malengo yaliyowekwa na kutegemewa.

Hivyo, baada ya majadiliano ya muda mrefu kati ya Serikali na RITES, na baada ya

kukubaliana, Serikali iliamua kununua hisa asilimia 51 za RITES. Ili kuinusuru Kampuni ya

Reli (TRL), pamoja na huduma ya reli nchini, Serikali iliamua kuteua menejimenti ya mpito

kuendesha Kampuni, wakati utaratibu wa kumpata mwekezaji ukiendelea. Bodi ya

Wakurugenzi ya RITES ilijiuzulu tarehe 22 Julai, 2011 na kufuatia kujiuzulu huko shughuli za

TRL zilikabidhiwa rasmi kwa Menejimenti ya mpito tarehe 26 Julai, 2011.

10.1.2 Kuanzishwa kwa Kampuni Miliki ya Rasilimali za Reli (RAHCO)

Kwa kupitia Sheria ya Reli Namba 4 ya mwaka 2002 na kama sehemu ya mchakato wa

ubinafsishaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Serikali iliamua kuanzisha Kampuni ya

Kusimamia na Kuendeleza Miundombinu na Rasilimali za Reli (RAHCO). Majukumu na kazi

za RAHCO ni pamoja na:

Kurithi majukumu ya iliyokuwa TRC ya utoaji wa huduma ya usafiri wa reli, ikiwa ni

pamoja na kurithi mali, haki na madeni ya TRC;

Kwa niaba ya Serikali Kusimamia, Kukuza na Kuendeleza Miundombinu ya Reli

Kuingia mikataba na makampuni mengine kwa njia za ukodishaji (concession), ubia,

ushirikishaji wa sekta binafsi n.k. katika kutoa huduma ya usafiri wa reli.

Kutafuta maeneo mapya ya ardhi (Estates) kwa ajili ya kuendeleza shughuli za reli

kama kujenga ICDs, maghala n.k.

Kuboresha miundombinu iliyopo ya reli ya kati ili kuhakikisha inapitika kwa kipindi

chote cha mwaka.

Kwa ujumla RAHCO ni mmiliki (Landlord) wa miundombinu ya Reli iliyokuwa inamilikiwa

na TRC na pia muendelezaji wa miundombinu ya Reli nchini wakati TRL ni muendeshaji

(Operator) wa huduma za reli.

Katika kutekeleza majumu yake baadhi ya kazi ambazo RAHCO imeendelea kutekeleza na

kufanikisha ni pamoja na:

Kuendelea na mchakato wa uendelezaji na ujenzi wa reli mpya kutoka Dar es Salaam -

Isaka – Kigali / Keza-Gitega-Musongati kwa kiwango cha kimataifa “Standard

Gauge”.

Kufanya matengenezo ya awali (restoration works) na kuendelea na matengenezo ya

kudumu (protection works) ya miundombinu ya reli iliyokuwa imeharibiwa vibaya na

mvua kati ya Stesheni za Kilosa na Gulwe mnamo miezi ya Disemba 2009 na Januari

2010. Baadhi ya kazi zinazoendelea kufanyika, ni pamoja na Kurekebisha mwelekeo

wa mto Mkondoa (River Training) kwa kutumia matuta, Kuimarisha kingo za tuta la

Page 30: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

27

reli katika sehemu hatarishi kwa kutumia “gabioni”, Kuimarisha / kujenga madaraja

katika sehemu ya reli, Kuhamisha njia ya reli (diversion of route) ili ipite sehemu

salama n.k.

Kufidia wananchi wanaoishi katika maeneo yaliyoainishwa kwa ajili ya kujenga

miundombinu ya reli ili kugeuzia mabehewa (Marshalling yard) katika maeneo

yanayotegemewa kujengwa bandari ya Mwambani (Tanga) na Mbegani (Bagamoyo).

Kufanya upembuzi yakinifu kwa ajili ya miradi mipya ya ujenzi wa reli kama mradi wa

reli ya kutoka Mwambani (Tanga) kupitia Arusha mpaka Musoma.

Eneo No. 3 km 289+575 kabla ya kutengenezwa Jan-2010

Eneo No. 3 km 289+575 Baada matengenezo Novemba -2010

Changamoto zinazoikabili Reli ya Kati:

Page 31: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

28

Uchakavu wa miundombinu ya reli kwa nchi nzima. Mtandao wa reli ya kati uliopo

ulijengwa miaka mingi iliyopita, takribani miaka 100. Mtandao huu kwa sasa unahitaji

kuboreshwa, ikiwa ni pamoja na utandikaji wa reli nzito zaidi ili kuweza kuhimili na

kukidhi mahitaji ya sasa.

Uchakavu wa Injini, mabehewa na mitambo mbalimbali (Rolling stock).

Ufinyu wa bajeti kwa ajili ya ujenzi na Uboreshaji wa miundombinu ya reli unaohitaji

fedha nyingi (capital intensive).

Idadi ndogo na kushuka kwa ubora wa injini za treni kwa sababu ya uchakavu.

Mipango ya RAHCO katika uboreshaji wa Miundombinu ya Reli katika miaka 50 ijayo

Mipango muhimu ya uboreshaji na uendelezaji wa huduma ya usafiri wa reli inayotegemewa

kutekelezwa katika kipindi cha miaka hamsini ijayo ni kama ifuatavyo:

i. Kuboresha kilometa 982 za njia ya reli kutoka Dar es salaam – Isaka ili kufikia kiwango

cha kimataifa (standard gauge) itakayokuwa na kiwango cha upana wa mm 1435 na

uzito wa ratili 120 kwa yadi,

ii. Kujenga kilometa 690 ya njia ya reli mpya kutoka Isaka – Kigali (Rwanda)/Keza-

Gitega-Musongati (Burundi) kwa kiwango cha upana wa mm 1435 na uzito wa ratili

120 kwa yadi kwa kushirikiana na Serikali za Rwanda na Burundi.

iii. Kuboresha reli kutoka Isaka – Mwanza, Tabora- Kigoma na matawi ya Kidatu, Singida

na Mpanda kwa kiwango cha kimataifa (standard gauge) itakayokuwa na upana wa

mm 1435 na uzito wa ratili 120 kwa yadi (Jumla ya kilometa 1,105)

iv. Kuboresha na kujenga reli ya kutoka Tanga (Mwambani) – Arusha – Musoma

(kilometa 938) kwa kiwango cha upana wa mm 1435 na uzito wa ratili 120 kwa yadi.

Hii itajumuisha pia kujenga matawi ya njia kwenda sehemu za Minjingu katika kiwanda

cha mbolea na Wosiwosi – Lake Natron panapotarajiwa kujengwa kiwanda cha

kuzalisha magadi.

v. Kujenga reli ya kutoka Mtwara – Songea mpaka Mbamba Bay na kuunganisha na

maeneo ya Liganga na Mchuchuma kunapotarajiwa kujengwa Migodi ya chuma na

makaa ya mawe.

vi. Kujenga reli kutoka eneo la Kidomole katika njia ya reli (Ruvu – Mruazi) kwenda eneo

la Bandari mpya ya Mbegani – Bagamoyo.

vii. Kuboresha na kujenga mtandao mzuri wa reli ndani ya Jiji la Dar es salaam kwa ajili ya

treni za abiria ili kupunguza msongamano.

10.1.3 Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA)

TAZARA imeanzishwa kwa mujibu wa sheria ya TAZARA namba 23 ya mwaka 1975

iliyorekebishwa kwa sheria ya TAZARA namba 4 ya mwaka 1995 na inamilikiwa kwa uwiano

wa hisa hamsini kwa hamsini 50:50 baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na

Serikali ya Jamhuri ya Zambia.

Page 32: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

29

TAZARA ilijengwa katika mwaka 1970 hadi mwaka 1975 na kuanza rasmi biashara ya

usafirishaji kwa treni za abiria na mizigo katika mwezi Julai, 1976. Serikali ya Jamhuri ya watu

wa China (PRC) ilifadhili ujenzi wa reli hii.

Mamlaka ya reli TAZARA huanzia katika jiji la Dar es Salaam nchini Tanzania na huishia

katika mji wa New Kapiri Mposhi nchini Zambia ikiwa ni urefu wa umbali wa jumla ya km

1,860; upande wa Tanzania kuna umbali wa km 975 na kwa upande wa Zambia kuna umbali

wa km 885. TAZARA inasafirisha mizigo kati ya nchi ya Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya

Congo (DRC), Malawi na Bandari ya Dar es Salaam. Reli hii pia husafirisha mizigo ya ndani

ya nchi ya Tanzania, kati ya mikoa ya ukanda wa kusini na Dar es Salaam. TAZARA pia

hufanya biashara ya usafirishaji wa abiria wa ndani na wa kimataifa kwa treni zake za abiria

zinazofanya kazi kati ya Dar es Salaam na New Kapiri Mposhi. TAZARA imekuwa ikitoa

huduma ya treni maalum kwenda na kurudi kwenye mbuga za wanyama za „Sealous National

Park‟ kwa kadri ya mahitaji.

Usafirishaji wa abiria na mizigo – TAZARA

Takwimu za mafanikio katika usafirishaji wa mizigo na abiria kuanzia mwaka 1976/77 hadi

mwaka 2009/10 zimeoneshwa katika Jedwali Na.9.2 ambapo jumla ya tani za mizigo

26,998,477 zilizosafirishwa na jumla ya abiria 43,671,888 waliosafirishwa.

Jedwali Na 9.2: Tani za mizigo na idadi ya abiria waliosafirishwa kwa miaka ya 1976/77

hadi 2009/10

Mwa

ka

wa

fedha

Jumla

ya Tani

za

mizigo

zilizosaf

i rishwa

(tani)

Kati ya hizo

Mizigo

iliyosafir

ishwa ya

nchi

nyingine

Jumla ya

idadi ya

abiria

waliosafi

rishwa

(Watu)

Kwenda

nje ya

Zambia

Kuingi

a

ndani

ya

Zambi

a

Mizigo

ya

ndani

mkoa

wa

Zambia

Kwend

a nje

ya

Tanzan

ia

Kuingi

a

ndani

ya

Tanza

nia

Mizigo

ya

ndani

mkoa

wa

Tanzan

ia

(tani)

76/77 1134000 511000 418000 37000 - - 168000 - 826000

77/78 1273000 596000 425000 16000 - - 236000 - 1134000

78/79 924000 393000 271000 9000 - - 251000 - 1313000

79/80 790000 228000 204000 33000 - - 325000 - 1397000

80/81 752000 312000 235000 20000 - - 185000 - 1025000

81/82 797000 328000 263000 42000 - - 174000 - 987000

Page 33: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

30

82/83 825000 392000 239000 42000 - - 152000 - 564000

83/84 973000 431000 492000 58000 - - 192000 - 1198000

84/85 1102000 491000 289000 55000 - - 267000 - 1080000

85/86 984000 402000 168000 61000 - - 306000 47000 1220000

86/87 1228000 483000 323000 57000 - - 310000 55000 1335000

87/88 1173000 419000 351000 52000 - - 291000 60000 1575000

88/89 1075000 370000 365000 55000 - - 245000 40000 1652000

89/90 996000 343000 261000 56000 - - 310000 26000 1681000

90/91 927000 349000 187000 62000 - - 285000 44000 1551000

91/92 963000 345000 165000 39000 - 91000 228000 95000 1888000

92/93 1079000 282000 399000 21000 37000 69000 96000 175000 2180000

93/94 647000 239000 85000 7000 21000 68000 88000 139000 1789000

94/95 641000 236000 124000 28000 34000 34000 96000 89000 1762000

95/96 663000 227000 64000 29000 100000 11000 144000 88000 1475000

96/97 555235 198291 61481 7334 26195 19144 137149 105641 1225487

97/98 631751 180890 88495 7708 26667 25918 220570 81503 1535814

98/99 616073 162256 27857 22050 38952 51412 229643 83903 1422138

99/00 633832 163559 65784 22599 26980 19476 226974 108460 1543297

00/01 608528 156082 45728 20092 15638 14731 228624 127633 1540682

01/02 577207 164682 79663 36345 10408 6203 155820 124086 1068287

02/03 613693 175975 107591 68313 15173 19675 108615 118351 1050612

03/04 610280 196567 55829 16168 26698 18277 183151 113590 929138

04/05 632478 166819 90631 14422 39093 45284 161180 115049 933439

05/06 601229 164209 97145 13727 43669 17124 136298 129057 889740

06/07 538530 153501 83740 8087 29066 8866 123188 132082 1090359

07/08 527620 170211 118984 11075 45307 16856 73393 91794 1047281

Page 34: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

31

08/09 383055 112907 157932 2325 27033 5978 25861 53019 996548

09/10 522966 179032 114123 986 27287 8196 87997 105345 767066

Juml

a

2699847

7

972198

1

652298

3

1030231 590166 550140 644746

3

2347513 43671888

Chanzo: Vitabu vya Takwimu za TAZARA

Hali ya sasa ya Reli ya TAZARA

Reli ya TAZARA ina jumla ya Stesheni 93 ambapo 56 zipo upande wa Tanzania na 37 upande

wa Zambia.

Kwa upande wa matanuli (tunnels), reli ya TAZARA ina jumla ya matanuli 23 ambapo 12

yapo upande wa Tanzania na 1 lipo mpakani mwa Tanzania na Zambia. Tanuli refu kabisa lina

urefu wa km 1.8 na lipo kati ya Mrimba na Makambako. Aidha, katika eneo hili, ndani ya km

30 kuna jumla ya matanuli 9.

Reli ya TAZARA ina jumla ya madaraha 322 ambapo 274 yapo upande wa Tanzania na 48

upande wa Zambia. Daraja kunbwa kabisa lipo kati ya Mrimba na Makambako na lina urefu

wa mita 800 na kina cha mita 50.

Changamoto zinazoikabili Reli ya TAZARA

Sekta ya Reli imekuwa ikikabiliwa na changamoto zifuatazo:

Uchakavu wa miundombinu ya reli kwa nchi nzima. Mtandao wa reli ya kati uliopo

ulijengwa miaka mingi iliyopita, takribani miaka 100. Mtandao huu kwa sasa unahitaji

kuboreshwa, ikiwa ni pamoja na utandikaji wa reli nzito zaidi ili kuweza kuhimili na

kukidhi mahitaji ya sasa.

Uchakavu wa Injini, mabehewa na mitambo mbalimbali (Rolling stock).

Ujenzi na Uboreshaji wa miundombinu ya reli unahitaji fedha nyingi (capital intensive).

Serikali inaendelea na mchakato wa kutafuta fedha kwa kutumia njia mbalimbali, ikiwa ni

pamoja na kuishirikisha sekta binafsi kwa utaratibu wa ubia kati ya Sekta ya umma na

Sekta binafsi (Public Private Partnership – PPP).

Kurudisha imani kwa wateja walioamua kusafirisha mizigo yao kwa kutumia barabara

baada ya usafirishaji katika sekta ya reli kuzorota kwa muda mrefu.

Idadi ndogo na kushuka kwa ubora wa injini za treni kwa sababu ya uchakavu.

Kuongezeka kwa gharama za uendeshaji zinazochangiwa na kupanda kwa gharama za

mafuta na vipuri.

Tatizo la uhaba na uchakavu wa mawasiliano na ishara kwa treni.

Mipango ya uboreshaji wa sekta ya Reli katika miaka 50 ijayo

Page 35: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

32

Mipango muhimu ya uboreshaji na uendelezaji wa huduma ya usafiri wa reli inategemewa

kutekelezwa katika kipindi cha miaka hamsini ijayo ni kama ifuatavyo:

viii. Kuboresha kilometa 982 za njia ya reli kutoka Dar es salaam – Isaka ili kufikia

kiwango cha kimataifa (standard gauge) itakayokuwa na kiwango cha upana wa

mm 1435 na uzito wa ratili 120 kwa yadi,

ix. Kujenga kilometa 690 ya njia ya reli mpya kutoka Isaka – Kigali (Rwanda)/Keza-

Gitega-Musongati (Burundi) kwa kiwango cha upana wa mm 1435 na uzito wa ratili

120 kwa yadi kwa kushirikiana na Serikali za Rwanda na Burundi.

x. Kuboresha reli kutoka Isaka – Mwanza, Tabora- Kigoma na matawi ya Kidatu,

Singida na Mpanda kwa kiwango cha kimataifa (standard gauge) itakayokuwa na

upana wa mm 1435 na uzito wa ratili 120 kwa yadi (Jumla ya kilometa 1,105)

xi. Kuboresha na kujenga reli ya kutoka Tanga (Mwambani) – Arusha – Musoma

(kilometa 938) kwa kiwango cha upana wa mm 1435 na uzito wa ratili 120 kwa

yadi. Hii itajumuisha pia kujenga matawi ya njia kwenda sehemu za Minjingu

katika kiwanda cha mbolea na Wosiwosi – Lake Natron panapotarajiwa kujengwa

kiwanda cha kuzalisha magadi.

xii. Kujenga reli ya kutoka Mtwara – Songea mpaka Mbamba Bay na kuunganisha na

maeneo ya Liganga na Mchuchuma kunapotarajiwa kujengwa Migodi ya chuma na

makaa ya mawe.

xiii. Kujenga reli kutoka eneo la Kidomole katika njia ya reli (Ruvu – Mruazi) kwenda

eneo la Bandari mpya ya Mbegani – Bagamoyo.

xiv. Kuboresha na kujenga mtandao mzuri wa reli ndani ya Jiji la Dar es salaam kwa

ajili ya treni za abiria ili kupunguza msongamano.

xv. Kuimarisha Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) kwa kuboresha

miundombinu ya reli.

xvi. Kuimarisha TAZARA ikiwa ni pamoja na ununuzi wa vichwa vya treni, ukarabati

wa vichwa vya treni, ununuzi wa mabehewa ya mizigo, ukarabati wa Kreni za

mizigo, ukarabati wa Kreni za okoa, ununuzi wa malighafi ya utengenezaji wa

mataruma ya reli (Concrete sleepers) na vipuri vya mabehewa 1200 ya mizigo.

10.2 USAFIRI/UCHUKUZI WA MAJINI

10.2.1 Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA)

Bandari ni kiungo muhimu katika uchukuzi kati ya nchi kavu na majini na zaidi ya asilimia 85

ya biashara yote duniani husafirishwa kupitia sekta ya bandari. Tanzania ina ukanda wa bahari

wenye urefu wa kilomita 960 na bandari kuu tatu ambazo ni Dar es Salaam, Tanga na Mtwara.

Pia ina maziwa makuu matatu ambayo yana bandari ambazo ni Mwanza, Bukoba, Musoma na

Kemondo katika ziwa Victoria; Kigoma na Kasanga katika Ziwa Tanganyika; na Itungi na

Mbambabay katika Ziwa Nyasa. Bandari zote ziko chini ya umiliki na usimamizi wa Mamlaka

ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA).

Page 36: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

33

Bandari za Tanzania ni tegemeo katika kuhudumia shehena ya Tanzania na nchi za jirani. Nchi

hizi ni pamoja na Burundi, Rwanda, Congo na Uganda ambazo hutumia reli ya kati (TRL), na

Zambia, DR Congo na Malawi zinazotumia reli ya TAZARA.

Historia Fupi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA)

Historia ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari inaanza mwaka 1893 wakati wa ujenzi wa reli

kutoka Tanga na Bandari ya Dar es Salaam mwaka 1905. Mwaka 1947 hadi 1967 mamlaka

hii ilijulikana kama “East African Railways and Harbours Corporation”. Mwaka 1967 hadi

1977 ilijulikana kama “The East African Harbours Corporation” na mwaka 1977 hadi 2005

kwa jina la “Tanzania Habours Authority - THA”. Mwaka 2004 Bunge la Tanzania lilipitisha

Sheria ya Bandari (Ports Act No. 17) iliyoanzisha Mamlaka mpya inayojulikana kama

“Tanzania Ports Authority - TPA”.

Shirika la Reli na Bandari Afrika Mashariki lililojulikana kama “The East African

Railways and Harbours Corporation (1947-1967)

Mwaka 1947, iliundwa taasisi/mamlaka rasmi iliyojulikana kama „The East African Railways

and Harbours Corporation” ilikuwa na jukumu la kuhudumia mifumo ya njia za reli pamoja

na bandari kwa nchi zilizokuwa makoloni ya Uingereza katika eneo la Afrika Mashariki (yaani

Kenya, Uganda na Tanganyika).

Uongozi wa „The East African Railways and Harbours Corporation‟ uliundwa mwaka 1948

baada ya kuvunjwa kwa uongozi wa mashirika makuu mawili yanayosimamia reli na bandari

eneo la Afrika Mashariki ambayo ni Shirika la Reli na Bandari kwa Kenya na Uganda (KUR)

na Shirika la Reli na Bandari kwa Tanganyika (TR).

Mapema katika miaka ya 1960, nchi tatu za Afrika Mashariki ziliingia mkataba wa ushirikiano

katika kumiliki vyombo vikuu vya usafirishaji kwa njia ya reli, huduma za barabara, huduma

za meli na bandari, huduma za anga, pamoja na karakana kuu zilizokuwa katika miji ya Dar es

Salaam na Nairobi.

Shirika la Bandari Afrika Mashariki lililojulikana kama “The East African Harbours

Corporation” (1967-1977)

Mwaka 1967 nchi tatu za Afrika Mashariki ziliunganisha nguvu na kuunda Jumuiya ya Afrika

Mashariki (EAC). Hivyo, ikalazimu kuunda mamlaka mpya ya usimamizi wa bandari kwa

Jumuiya ya Afrika Mashariki yenye jukumu la kuendesha bandari kuu za Dar es Salaam,

Mombasa na bandari ya Tanga.

Jumuiya ya Afrika Mashariki ilivunjika mwaka 1977. Mwaka 1976 mali na madeni ya Jumuiya

ziligawanywa baina ya nchi hizo tatu na kila nchi ilikuwa huru na yenye mamlaka ya kuhifadhi

Page 37: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

34

mali zake. Tarehe 11 Februari 1977 Mamlaka ya Bandari Tanzania (Tanzania Harbours

Authority) ilianzishwa.

Mamlaka ya Bandari Tanzania (Tanzania Habour Authority - THA) mwaka 1977–2005

Mwaka 1998 THA iliwekwa kwenye orodha ya mashirika ya umma yaliyopangwa

kubinafsishwa (specified) na Serikali kupitia Tume ya Rais ya kurekebisha Mashirika ya

Umma (PSRC). Mwaka 2000, Kitengo cha Kontena kilibinafsishwa kwa TICTS ambayo

mwaka 2001 iliuza hisa kwa Kampuni ya HPH ya Hongkong.

Kati ya mwaka 2003 hadi 2004 Serikali ilifanya utafiti kuhusu kufungua milango ya biashara

(trade liberalization) katika sekta ya usafiri wa majini kwa kutumia kampuni ya „Marine‟

(RMG ya Uholanzi) ambayo ilipendekeza kutungwa Sheria mpya ya Bandari yaani “The Ports

Act No. 17” ambayo ilipitishwa na Bunge Novemba 2004, na kuunda Mamlaka

itakayosimamia bandari zote Tanzania. Mamlaka ilianza kazi zake rasmi Julai 1, 2006.

Mwezi Julai 2006, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania iliondolewa katika orodha ya

Mashirika ya kubinafsishwa yaani (de-specification). Sera ya Serikali ni kukodisha rasilimali

kwa waendeshaji binafsi na Serikali kuendelea kumiliki hisa zote (100%) chini ya mfumo wa

“Landlord Port Authority”.

Ushirikishwaji wa Sekta Binafsi

Jukumu la utoaji wa huduma za bandari unashirikisha pia sekta binafsi na maeneo yafuatayo

yanaendeshwa na kampuni binafsi:

(i) Kitengo cha Kontena katika bandari ya Dar es Salaam ambacho kinaendeshwa na

Kampuni ya TICTS kwa mkataba wa miaka 25 (2000 – 2025);

(ii) Kitengo cha mizigo bandari ya Kigoma katika Ziwa Tanganyika ambacho

kinaendeshwa na Kampuni ya Gravimport ya Burundi chini ya Kampuni tanzu ya

MUAPI kwa mkataba wa miaka 5 (2008 – 2012);

(iii) Bandari ya Kasanga katika Ziwa Tanganyika ambayo inaendeshwa na Kampuni ya

Agro-Trucking ya Sumbawanga kwa mkataba wa mwaka 1 (Novemba 2010 – Oktoba

2011).

Nchi za jirani za Zambia, Jamhuri ya Demokrasia ya Congo, Burundi, Rwanda, Uganda, na

Malawi hupitisha mizigo yake katika bandari za Mamlaka. Makampuni tisa makubwa ya meli

ambayo ni East African Conference Lines, P&O Nedloyd, Maersk, Messina, MSC na Global

Container Line yanahudumiwa katika bandari za Mamlaka.

Matukio muhimu ya historia ya bandari ni kama ifuatavyo:

1901 Ujenzi wa sehemu ya kuundia majahazi Bandari ya Dar es Salaam

ulianza na baadaye ukaendelea mpaka Mwanza.

1912 Ujenzi wa bandari ya Kigoma ulianza

Page 38: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

35

1914 Ujenzi wa bandari ya Tanga ulianza

1927 Chuo cha kusimamia shughuli za reli na huduma za bandari

kilichoitwa Tanzania Railways and Port Services Institution

kilianzishwa.

1954 Bandari ya Mtwara ilianza kujengwa

1950‟s Ujenzi wa bandari za Mwanza, Bukoba, Nansio, Musoma na Itungi

katika Ziwa Victoria na Ziwa Nyasa

1953 Upanuzi wa lango la bandari ya Dar es Salaam

1956 Ujenzi wa gati namba 1 mpaka 3 uliasha na gati hizo zikakabidhiwa na

mtoto wa Malkia wa Uingereza aitwaye Margaret.

1958 Ujenzi wa Kurasini Oli Jet (KOJ).

1967 Ujenzi wa Kituo cha Kuhifadhia Makasha kilichopo Ubungo.

1968 Ujenzi wa gati namba 4, 5 na 6.

1969 Shirika la Bandari la Afrika Mashariki lilianzishwa baada ya

kutenganisha Reli na Bandari.

1973 Kitengo cha mafuta cha Single Bouy Mouring (SBM) kilikabidhiwa

1977 Mamlaka ya Bandari (Tanzania Harbours Authority) ilianzishwa baada

ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki

1978 Kukamilika kwa ujenzi wa gati namba 9, 10 na 11

1984 Kuanzishwa kwa Chuo cha Bandari kilichopo Dar es Salaam

1988 Gati namba 9, 10 na 11 zilibadilishwa na kuwa Kitengo rasmi cha

Makontena.

1989 Kukamilika kwa ujenzi wa Ghala la Nafaka bandari ya Dar es Salaam.

1998 Kina cha Mlango wa Bandari ya Dar es Salaam kiliongezwa kuruhusu

meli kuingia bandarini mchana na usiku.

1998 Mamlaka kuwekwa chini ya usimamizi wa PSRC (specified).

2000 Kitengo cha kontena kilikabidhiwa kwa mwendeshaji binafsi (TICTS).

2004 Sheria iliyounda Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA)

ilipitishwa ba Bunge kwa ajili ya kumiliki na kusimamia shughuli zote

za bandari za mwambao na maziwa.

2006 Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania iliondolewa katika

orodha ya Mashirika ya yaliyoainishwa kubinafsishwa yaani „de-

specification‟.

2008 “Inland Container Depots” binafsi zilianza kutumika kuhudumia

shehena kontena bandari ya DSM.

2009 Mpango Mkakati wa kuendeleza bandari (Ports Master Plan) 2008 –

2028 ulikamilika.

2009 Serikali iliondoa Kipengele cha ukiritimba (Exclusivity) katika

kuhudumia makasha Bandari ya Dar es Salaam.

2010 Ukarabati wa kituo cha mafuta cha SPM (Single Point Mooring)

ulianza ili kukiwezesha kuhudumia mafuta ghafi na yaliyosafishwa.

2010 “Cargo Freight Stataions” (CFS) zilianza kuhudumia shehena ya

magari

Majukumu ya Mamalaka

Page 39: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

36

Mamlaka imerithi majukumu ya iliyokuwa Mamlaka ya Bandari (THA) na kupewa majukumu

zaidi ya kumiliki na kuendeleza bandari zote nchini na zilizo katika Maziwa Makuu ambazo

zilikuwa zikiendeshwa na “Marine Services Company. Majukumu ya Mamlaka ni kama

yafuatayo:

(i) Kuendeleza Bandari (Develop)

(ii) Kuendesha shughuli za Bandari (Operate)

(iii) Kutangaza bandari kimasoko (Promote)

(iv) Kushirikisha na kusimamia sekta binafsi katika uendeshaji wa shughuli za bandari

(Landlord)

Hali ya Shehena

Kumekuwa na ongezeko kubwa la Shehena kupitia bandari za Mamlaka tangu wakati wa

UHURU mwaka 1961 hadi mwaka 2010. Shehena imeongezeka kutoka tani 1.185 milioni

mwaka 1961 hadi kufikia tani 9.624 milioni mwaka 2010.

Hali hii imechangiwa na kukua kwa uchumi katika nchi zinazotumia bandari zetu, uboreshaji

wa njia za usafirishaji kwa barabara na reli na kuongezeka kwa uwezo wa bandari zenyewe.

Shehena iliyopitia katika bandari zetu katika miaka ya 1961 ilikuwa ni ya kawaida iliyobebwa

na meli za kawaida zenye vifaa vya kupakua na kupakia. Hali hii ilibadilika baada ya

kuanzishwa kwa usafirishaji wa kontena katika miaka ya 1975 hadi hivi sasa. Mabadiliko haya

yamechangia shehena ya kontena kuongezeka kutoka kontena 46,507 zilizohudumiwa mwaka

1985 hadi kontena 425,181 mwaka 2010 kama inavyooneshwa katika Jedwali Na. 9.3.

Jedwali Na. 9.3: Shehena iliyohudumiwa na Bandari za Mamlaka 1961-2010

.

Vifaa vya Kuhudumia Shehena

Mamlaka imewekeza zaidi ya dola milioni 500 pamoja na misaada kutoka Benki ya Dunia na

nchi mbalimbali za Ulaya katika kuendeleza miundombinu na manunuzi ya vifaa mbalimbali

kama yalivyoorodheshwa hapa chini:

(a) Magati na maeneo ya kuhifadhi mizigo

(b) Vifaa vya kupakia na kupakua mizigo

(c) Vifaa vya majini

(d) Majengo

MWAKA 1961 1985 1995 2005 2010

Shehena (tani) 1,185,000 1,262,820 4,583,407 6,794,773 9,623,550

Kontena (TEUs) - 46,507 99,708 249,310 425,181

Page 40: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

37

Bandari imeongeza vifaa vya kuhudumia mizigo, sambamba na mabadiliko ya mfumo mzima

wa mabadiliko ya ubebaji mizigo. Usalama wa Bandari, pamoja na vifaa vya doria

umeimarishwa.

Bandari ya Dar es salaam

Bandari ya Dar es salaam ndiyo kubwa kuliko zote ikiwa na urefu wa kilomita 2.6 na upana wa

mita 500 na ina uwezo wa kuhudumia tani milioni 10.1 kwa mwaka. Bandari ina magati 11,

Gati Na. 1 - 7 zinahudumia shehena mchanganyiko na zinaendeshwa na Mamlaka. Gati Na. 8 -

11 zinahudumia shehena ya kontena na zimekodishwa kwa kampuni ya TICTS, Gati hizi zina

uwezo wa kuhudumia kontena 330,000 kwa mwaka. Vitengo vingine ni pamoja na kituo cha

kuhudumia mafuta (KOJ na SPM), kituo cha nafaka na karakana ndogo ya kukarabati meli,

Mashedi 10 ya mizigo, Kitengo cha kuhudumia meli za mwambao na Kitengo cha Nafaka

chenye uwezo wa kuhifadhi tani 30,000.

Lango Kuu la Bandari ya Dar es Salaam

Kabla ya Uhuru 1961, lango lilikuwa na uwezo wa kuingiza meli zenye urefu wa mita 145 –

175 na kina cha maji cha mita 7. Upanuzi wa lango ulifanyika mwaka 1998 ambapo kina

kilichimbwa hadi kufikia mita 10.5 na upana wa mita 140 kwa gharama ya Dola za Kimarekani

240 milioni. Hivi sasa lango linaruhusu meli zenye ukubwa usiozidi mita 234. Kutokana na

utekelezaji wa mradi wa kupanua na uwekaji wa taa katika lango kuu, pamoja na uchimbaji

ndani ya Bandari mwaka 1998, meli zinaweza kuingia usiku na mchana, ukubwa wa meli

umeongezeka hadi kufikia urefu wa mita 234/240 na kina cha maji kimeongezeka hadi kufikia

mita 10.5.

Uzito wa Meli na Vifaa

Uzito wa meli umeongezeka kutoka 18,000 DWT hadi 40,000 DWT. Vifaa vya kuhudumia

meli vimebadilika kutokana na mabadiliko ya meli na mizigo, kama vile ubebaji wa mizigo

kwenye kontena.

Changamoto zinazoikabili Bandari ya Dar es Salaam

Uwezo Mdogo wa Kuhudumia Meli Kubwa

Mabadiliko ya teknolojia yamesababisha meli kuongezeka ukubwa katika dhana ya “economies

of scales” ambapo kampuni nyingi za meli zimeshawishika kuzinunua. Meli hizi kubwa

zimelazimisha bandari nyingi kuongeza kina na upana wa milango ya bandari na kwenye

magati zinapofunga meli. Hivi sasa kuna meli za kizazi cha saba (7th generation) zenye uwezo

wa kuchukua kontena zaidi ya 10,000 kwa mara moja. Meli hizi zinahitaji bandari zenye kina

kinachozidi mita 15 na upana wa zaidi ya mita 240. Aidha, urefu wa gati unatakiwa uwe na

zaidi ya mita 300.

Meli kubwa zinaweza kufunga katika gati namba 7 - 11 tu ambapo gati namba 8 – 11

zinahudumia meli za kontena (kitengo kinachoendeshwa na kampuni ya TICTS). Hata hivyo

Page 41: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

38

gati hizi zina urefu wa mita 180 kila moja na hivyo ni meli nne tu zinazoweza kufunga kwa

wakati mmoja badala ya meli tano.

Miundombinu Hafifu ya Reli na Barabara

Bandari ya Dar es Salaam inaunganishwa na masoko ya bara (hinterland) na nchi jirani kupitia

mtandao wa reli na barabara. Reli ya TRL inayoanzia bandari ya Dar es Salaam na ni tegemeo

kubwa katika usafirishaji wa mizigo ya nchi za DR Congo, Rwanda, na Burundi. Aidha reli ya

TAZARA inatumika kusafirisha mizigo ya Zambia na Malawi. Kutokana na utendaji hafifu wa

reli, mizigo mingi inasafirishwa kwa njia ya barabara. Kiwango cha uondoshaji wa mizigo

bandarini kwa njia ya reli kimeshuka na hivyo kuathiri uwezo wa bandari zetu kushindana

kikamilifu na bandari jirani katika kufikia masoko ya nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya

Congo, Burundi, Rwanda na Uganda. Kwa mfano, shehena yote ya mafuta kuelekea nchi za

Rwanda, Malawi na DR Congo inasafirishwa kwa njia ya barabara.

Njia ya barabara ambayo ndiyo tegemeo kwa kusafirisha karibu asilimia 90 ya shehena

bandarini imeendelea kuathiriwa na gharama kubwa za uchukuzi, safari ndefu za njiani (Transit

times), uwezo mdogo wa kubeba mizigo mizito, na pia vikwazo vya njiani (Non tariff barriers).

Kwa mfano, inakadiriwa kuwa muda wa lori la mzigo kutoka Dar es Salaam kwenda DR

Congo na kurudi ni wastani wa siku 45 kutokana na vikwazo na urasimu mbalimbali njiani.

Hali hii itaendelea kuchangia katika kudumaza mtiririko mzima wa shehena na ufanisi wa

bandari kwa ujumla

Uondoshwaji wa mizigo ya hapa nchini pia unaathiriwa na msongamano wa magari katika

barabara za jiji, ubovu wa barabara zinazoingia na kutoka bandarini na zile zinazounganisha

bandari na vituo vya kuhifadhia kontena. Barabara hizi hazina taa na hivyo zinakwamisha

juhudi za bandari kutoa huduma masaa 24 kama ilivyo bandari nyingine.

Uwezo wa kuhudumia shehena ya Uganda na nchi za Maziwa Makuu umezidi kupungua

kutokana na uchache wa meli za mabehewa katika ziwa Victoria. Hivi sasa kuna meli moja tu

ya Tanzania, MV UMOJA ambayo husafirisha mizigo kutoka Port Bell hadi Mwanza.

Ushindani mkubwa kutoka bandari nyingine

Bandari za Mamlaka hususan bandari ya DSM inakabiliwa na ushindani mkubwa kutoka

bandari nyingine katika eneo hili kama vile bandari ya Mombasa nchini Kenya, Bandari

zilizoko nchini Msumbiji na Afrika Kusini. Shehena inayoshindaniwa ni kutoka nchini

Zambia, Malawi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Uganda, Burundi, Rwanda na

sasa Sudani Kusini.

Kutokana na ushindani huu mkali, hata baadhi ya shehena ya Tanzania inapita bandari ya

Mombasa hasa shehena itokayo Kanda ya Ziwa (yaani Mwanza, Kagera, Shinyanga na Mara)

na mikoa ya Kaskazini mwa Tanzania (Kilimanjaro, Arusha na Manyara).

Pia bandari zilizoko nchini Namibia na Angola zinalenga kuhudumia shehena katika ukanda

huu hasa ile ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Bandari ya Tanga

Page 42: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

39

Bandari ya Tanga ilianza mwaka 1914 ambapo gati la kwanza la matishari lilijengwa na

mwaka 1952 gati lingine liliongezwa. Bandari ina kina kifupi na hivyo meli zinafunga nje ya

bandari (outer anchorage) na hivyo mizigo kupakiwa na kupakuliwa kwa kutumia pantoni.

Bandari ya Tanga ina gati mbili zenye jumla ya urefu wa mita 380 na kina kinafikia mita 2.5.

Mwaka 1970, gati lenye umbo la “L” lilijengwa kwa ajili ya kuhudumia shehena ya mbolea

kavu na ya majimaji. Utumiaji wa gati hili kwa ajili ya shehena ya mbolea ulisitishwa mnamo

mwaka 1990 kufuatia kufungwa kwa kiwanda cha mbolea cha Tanga.

Bandari ina vifaa vinavyotumika kuhudumia shehena ya mafuta yanayoingizwa kutoka nje ya

nchi ikiwa ni pamoja na boya lililounganishwa bomba la mafuta katika kina kifupi na kirefu

cha bandari. Bandari ina uwezo wa kuhudumia tani 500,000 kwa mwaka. Katika mwaka

2009/10, bandari ilihudumia tani 630,000, ikiwa ni zaidi ya uwezo wake kwa asilimia 26.

Changamoto za bandari ya Tanga

(i) Uwezo mdogo wa bandari kuhudumia meli kubwa.

(ii) Ufinyu wa maeneo ya kufanyia kazi (operational area). Bandari ina uhaba wa ardhi kwa

ajili ya upanuzi kwa kuwa maeneo jirani na bandari yanamilikiwa na kampuni na taasisi

nyingine.

(iii) Miundombinu ya barabara zinazoondosha mizigo bandarini ni hafifu.

(iv) Kusuasua kwa usafiri wa reli ambako kumedumaza maendeleo ya bandari. Hapo awali

Bandari ilikuwa inahudumia shehena ya mchanga kutoka migodi ya Kahama; Hivi sasa

shehena hii imepotea kutokana na usafiri wa reli kukoma.

(v) Kupungua sheheha ya viwanda kutokana na viwanda vingi kufungwa.

Bandari ya Mtwara

Bandari ya Mtwara ilianza mwaka 1954 ambapo gati mbili zilijengwa sanjari na reli ya

Nachingwea. Bandari ya Mtwara ilijengwa kwa madhumuni ya kuhudumia zao la korosho.

Hata hivyo reli ya Nachingwea iliondolewa mwaka 1963 kutokana na mradi wa kilimo cha

karanga kusitishwa. Bandari ina uwezo wa kuhudumia tani 400,000 kwa mwaka. Utendaji

wa bandari hivi sasa ni asilimia 25 tu ya uwezo wake.

Changamoto za Bandari ya Mtwara

Matatizo ya Bandari ya Mtwara ni pamoja na gharama kubwa za uendeshaji wa Bandari

ikilinganishwa na mapato. Bandari inategemea aina moja ya shehena ambayo ni Korosho.

Shehena ya korosho inaendelea kupungua kutokana na korosho inayobanguliwa hapa nchini

kufikia takribani asilimia 20 ikilinganishwa na asilimia 10 miaka ya nyuma. Korosho

iliyobanguliwa inasafirishwa kwa njia mbadala. Shehena nyingine iliyopungua ni pamoja na

Saruji kutoka Tanga na mafuta kutokana na uchache wa meli za mwambao.

Changamoto nyingine ya bandari ni pamoja na uwezo mdogo wa uondoshaji mizigo bandarini

kutokana na miundombinu hafifu ya usafirishaji.

Page 43: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

40

Bandari ina fursa nzuri ya kuvutia wawekezaji kutokana na kuwepo eneo kubwa kwa ajili ya

upanuzi wa bandari. Mamlaka inamiliki hekta 2,600 kwa ajili ya upanuzi wa Bandari na

shughuli za EPZ. Matumizi ya bandari yanatarajiwa kuongezeka kutokana na miradi

mbalimbali ikiwa ni pamoja na:

Vifaa vya ujenzi wa kiwanda cha Saruji na kiwanda cha Mbolea vinavyotarajiwa kuanza

kujengwa mwaka 2012;

Vifaa vya utafiti wa mafuta (off-shore exploration) katika bahari ya Hindi unaoendelea;

Shehena ya saruji na vifaa vya ujenzi kwa ajili ya miradi ya ujenzi katika ukanda wa kusini;

na

Kauli mbiu ya Serikali ya ”Kilimo Kwanza” itaongeza uzalishaji wa mazao ya biashara

kwa ajili ya kuuza nje ya nchi.

Bandari za Ziwa Victoria

Ujenzi wa Bandari za Mwanza, Bukoba, Nansio na Musoma ulianza miaka ya 1950. Bandari

hizi zinahudumia maeneo ambayo yana utajiri mkubwa wa kilimo na madini.

Changamoto Zinazokabili Bandari za Ziwa Victoria

Miundombinu ya kizamani, mfano matumizi ya „‟link span” ambayo yanategemea meli za

mabehewa. Shehena kati ya bandari za Mwanza na Port Bell nchini Uganda imepungua

kutokana na uchache wa meli za kubeba mabehewa (wagon ferries). Ukosefu wa

miundombinu ya kuhudumia shehena ya kontena umesababisha maendeleo ya bandari hizi

kudumaa. Aidha,

(a) Utendaji hafifu wa shirika la reli (TRL) pia umeathiri upatikanaji wa shehena;

(b) Wenye meli za abiria kutumia magati binafsi ziwani;

(c) Bandari zinajiendesha kwa hasara.

Bandari za Ziwa Tanganyika

Bandari kuu ni Kigoma ambayo ujenzi wake ulifanyika katika mwaka 1912 sanjari na ujenzi

wa reli ya kati. Gati la bandari ya Kasanga lilijengwa mwaka 1997. Kama zilivyo bandari

nyingine za maziwa, miundombinu yake imechakaa sana na hivyo inahitaji kuboreshwa.

Changamoto Zinazokabili Bandari za Ziwa Tanganyika

Matatizo ya bandari hizi ni pamoja na:

(a) Utendaji hafifu wa reli kati ya Dar es Salaam na Kigoma;

(b) Kutumika kwa gati binafsi ziwani;

(c) Miundombinu hafifu ya kuunganisha bandari na vyanzo vya shehena;

(d) Hali mbaya ya miundombinu ya bandari;

Miundombinu ya Bandari za Ziwa Nyasa

Bandari ya Itungi katika Ziwa Nyasa ilijengwa miaka ya 1950 sanjari na bandari nyingine

upande wa Malawi.

Page 44: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

41

Changamoto zilizojitokeza katika utendaji wa Bandari ya Kyela ni pamoja na:

(a) Hali mbaya ya miundombinu ya bandari;

(b) Upungufu wa shehena ziendazo Malawi ikiwa ni pamoja na mbolea;

(c) Uhaba wa Meli zinazofanya kazi katika ziwa Nyasa.

(d) Gharama kubwa za uendeshaji wa bandari ukilinganisha na mapato.

Chuo Cha Bandari

Chuo cha Bandari kilichopo chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari kilianzishwa mwaka

1984. Madhumni ya kuanzishwa kwa Chuo hiki ilikuwa kutoa wataalamu wa kuendesha

shughuli za bandari. Chuo cha Bandari kama zilivyo idara nyingine za Mamlaka, kimekuwa

kikitekeleza majukumu yake kwa kuzingatia malengo na mipango mkakati ya Mamlaka.

Katika kutekeleza mikakati hiyo, Chuo kinafanya yafuatayo:

(i) Kutoa mafunzo ya kuwaendeleza wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari katika fani zote

za shughuli za Bandari ili kuongeza tija na ufanisi. Katika kutekeleza jukumu hili Chuo

kinafanya kazi kwa karibu na Kurugenzi ya Utumishi na Bandari zote katika kubaini

mahitaji ya mafunzo na hatimaye kuandaa na kufundisha kozi zinazokidhi mahitaji

hayo;

(ii) Kutoa ushauri katika fani za uendeshaji wa bandari (Port Operations) na uendeshaji wa

vifaa vya bandari (Port Equipment Operations) kwa watu binafsi, makampuni,

mawakala wa meli, wadau wa Bandari na wale ambao wanafanya shughuli

zinazohusiana na Bandari;

(iii) Kubuni na kuendesha mafunzo yanayohusiana na biashara ya upakuzi na upakiaji

mizigo katika meli na huduma mbalimbali zinazohitajiwa na jamii;

(iv) Kufuatilia na kutathmini mafanikio ya mafunzo kwa wateja binafsi na wadau wa

biashara ya majini na kufanya mchanganuo wa soko la kozi zinazotolewa;

(v) Kufanya mahusiano na vyuo vya ndani na nje na kufanya ushirikiano wa kimafunzo ili

kuinua viwango vya kozi zinazotolewa;

(vi) Kuendeleza na kuinua viwango vya elimu vya wakufunzi na wafanyakazi wengine;

(vii) Kuhakikisha kuwa mafunzo na vyeti vinavotolewa na Chuo vinatambulika katika

biashara ya majini (maritime industry), na kwa kuzingatia miongozo inayotolewa na

Taasisi za Kitaifa kama vile NACTE (National Council for Technical Education).

Mafanikio ya Chuo

Kuanzishwa kwa masomo ya jioni ili kukidhi mahitaji hasa ya wafanyakazi

wasioweza kuhudhuria vipindi vya asubuhi;

Kujiendesha kibiashara;

Kuwepo kwa ongezeko kubwa la wanafunzi hadi kufikia 887 katika mwaka

2011;

Baadhi ya wakufunzi wamepata mafunzo yanayoendeshwa na UNCTAD na

wangine wanajiendeleza kufikia Shahada ya Uzamili (Masters).

Page 45: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

42

MATARAJIO YA MAMLAKA KWA MIAKA 50 IJAYO

Mpango wa Kuendeleza Bandari ( Ports Master Plan)

Mamlaka imetayarisha Mpango kamambe wa kuendeleza bandari zote katika kipindi cha miaka

20 ijayo.

Jedwali Na. 9.4 “Ports Master Plan” imeainisha miradi kwa kila bandari kama ifuatavyo:

Bandari Mikakati

Bandari mpya (a) Bandari ya Mbegani, Bagamoyo

(b) Bandari ya Mwambani, Tanga.

Dar es Salaam (a) Ujenzi wa gati mbili za kuhudumia kontena yaani gati namba

13 na14.

(b) Kuongeza kina cha lango la bandari kufikia mita 12

(c) Kuongeza kina cha gati namba 1-7 hadi mita 12

(d) Ujenzi wa kituo cha mafuta cha SPM

(e) Kuongeza eneo la Kurasini kwa ajili ya shehena ya kichele,

ujenzi wa silo za mbolea na “conveyor system” kuunganisha

na silo.

(f) Ujenzi wa gati la RoRo kwa ajili meli za magari

(g) Ujenzi wa kituo cha mizigo Kisarawe

(h) Ujenzi wa gati za kontena eneo la vijibweni.

Tanga (a) Kuongeza maeneo kwa ajili ya upanuzi wa bandari

(b) Kuboresha vifaa vya kupakulia na kupakia mizigo

Mtwara (a) Kuboresha miundombinu ya Bandari ya iliyopo

(b) Ujenzi wa miundombinu itakayohudumia shehena

itakayozalishwa na miradi ya Ukanda wa maendeleo ya

Mtwara ( Mtwara Development Corridor)

(c) Kuendeleza bandari kama kituo cha kuhudumia shughuli za

utafiti wa mafuta na gesi (Oil and Gas Supply Base)

(d) Kuifanya bandari kuwa bandari huru (free port)

Bandari za Maziwa (a) Bandari ya Mwanza Kaskazini kuwa tengefu kwa ajili ya

kuhudumia abiria

(b) Bandari ya Mwanza Kusini kuendelezwa kwa ajili ya mizigo

ikiwa ni pamoja na ujenzi wa kitengo cha kontena

(c) Upanuzi wa bandari ya Kigoma

(d) Upanuzi wa Bandari ya Kasanga

Page 46: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

43

(e) Ujenzi wa gati la Kiwira

(f) Kupata ardhi zaidi kwa ajili ya upanuzi wa bandari ya

Kigoma, Kiwira, Mbambabay na Musoma

(g) Ujenzi wa Magati katika ziwa Tanganyika (Kalya, Karema,

Kibirizi, Kirando, Lagosa na Kasanga

(h) Kuendeleza bandari ya Itungi

(i) Kujenga gati bandari ya Ndumbi

(j) Kujenga gati bandari ya Pangani

(k) Kujenga gati bandari ya Mafia

(l) Kujenga gati bandari ya Lindi

10.2.2 Kampuni ya Meli ya SINOTASHIP

Kampuni ya Ushirika wa usafirishaji mizigo kwa meli baina ya Tanzania na China ni ushirika

unaomiliki na kuendesha meli kwa asilimia hamsini kwa hamsini (50 kwa 50) ulio chini ya

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Watu wa China. Wabia

waliopewa mamlaka ya umiliki wa Kampuni ni Wizara ya Uchukuzi Tanzania na Wizara ya

Mawasiliano ya China.

Kampuni hii ilianzishwa mwaka 1967 kutokana na agizo la Waziri Mkuu wa China Zhou Enlai

na Rais wa kwanza Tanzania, Mwalimu Julius K. Nyerere. Kwa kipindi cha miaka 44,

SINOTASHIP imeimarisha urafiki na ushirikiano wa Tanzania na China na meli zake zinabeba

mamilioni ya tani za mizigo kati ya China na Tanzania, na kati ya nchi hizo mbili na nchi

nyingine duniani.

Ukubwa na Umiliki wa Meli na Ugharimiaji

Awali iliamuliwa kwamba SINOTASHIP ingemiliki na kuendesha meli nne za mizigo mikavu

ya kawaida. Kwa hiyo, serikali hizi mbili ziliwekeza paundi za Uingereza milioni 3 katika

kampuni, ambazo zote zililipwa na serikali ya China, nusu ya kiasi hicho kikitolewa kama

mkopo nafuu kwa serikali ya Tanzania. Mkopo huo haukuwa na riba na hivyo kutakiwa

kulipwa kwa awamu sawa za vipindi kumi baada ya kipindi cha nyongeza cha miaka kumi,

tangu malipo kufanyika.

Mipangilio ya Kiuendeshaji

Ofisi kuu ya SINOTASHIP ipo Dar es Salaam, Tanzania, na tawi la ofisi lipo Beijing, China.

Licha ya kumilikiwa na nchi mbili wabia, pia kampuni inasimamiwa na wajumbe kiushirika.

Bodi ya Wakurugenzi inaundwa na wajumbe sita, watatu kutoka kila upande na mjumbe

mmoja kati yao kutoka kila upande, akiwa kama mwenyekiti mwenza. Wakurugenzi Wakuu

wawili, mmoja kutoka kila upande, wakiongoza Utawala wa Ushirika kama Maofisa Watendaji

Wakuu wa kampuni.

Uendeshaji na Utendaji wa Shughuli

Kwa kipindi cha miaka 44 iliyopita, vyombo vya kampuni vimebeba zaidi ya tani milioni 8 za

mizigo hasa bidhaa zinazoingizwa ndani ya nchi na zile zinazouzwa nje ya nchi zikisafirishwa

Page 47: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

44

kwa meli ndani na nje ya China, na Tanzania pia. Kibiashara SINOTASHIP imekuwa ikipata

faida kwa miaka yote, kwa sasa ina utajiri halisi wa takribani DOLA ZA MAREKANI

MILIONI 71. Mapato yaliyokusanywa na kuhifadhiwa yameisaidia kampuni kuboresha mali

zake mara tatu bila kutegemea fedha za ziada kutoka kwa wanahisa.

Kampuni pia imejitahidi kukuza na kutoa huduma za biashara ya kigeni baina ya China na

Tanzania. Aidha, SINOTASHIP iliandaa mafunzo kwa wataalamu wa usimamizi wa meli na

wataalamu wa melini hasa kwa upande wa Tanzania ambapo vijana wake wamenufaika kwa

kiasi kikubwa kwa kupata uwezo na ujuzi mpya.

Viashiria vya Mafanikio

Kuna viashiria vingi vilivyofanya SINOTASHIP iweze kudumu na kufanikiwa katika kipindi

cha miongo minne iliyopita. Viashiria hivyo ni pamoja na;

i. Tabia ya kujali na jitihada zinazofanywa na serikali zote mbili katika kampuni.

ii. Msaada mkubwa unaotolewa na kikundi cha COSCO kampuni ya usafirishaji mizigo

kwa meli inayomilikiwa na Serikali iliyopewa mamlaka na Wizara ya Mawasiliano ya

China kushughulikia usimamizi wa SINOTATHIP kwa upande wa China.

iii. Ubora wa hali ya juu wa usimamizi wa kitaalamu na wataalamu wa ufundi

waliowekwa kwenye ushirika na pande zote mbili umekuwa na uhakikisho wa kampuni

kusimamiwa vyema wakati wote.

iv. Ushirikiano mzuri na bidii kati ya wafanyakazi wa pande zote mbili za Tanzania na

China.

Changamoto zilizopo sasa

i. Utekaji nyara wa meli hasa katika bahari ya Hindi ambako kumefanya gharama za

uendeshaji kupanda kwa ajili ya kugharamia ulinzi baharini.

ii. Upungufu wa mizigo inayosafirishwa kwa meli duniani.

Uamuzi wa Kununua Meli kubwa mpya

Kutokana na kushindwa kupata meli nzuri za mtumba sokoni kwa kipindi cha miaka ya nyuma,

kampuni iliamua kwa mara ya kwanza katika historia yake, kutengeneza meli mbili mpya. Meli

ambazo zilikwishaagizwa kutoka karakana ya kutengeneza meli ya China, ni meli kubwa zenye

uwezo wa kubeba uzito mkubwa wa tani 57,000 na tani 34,000.

Kuletwa kwa meli hizi kutasaidia kuongeza uwezo wa safari za kampuni kwa sababu uwezo

wake wa kubeba utakuwa ni mara sita ya uwezo wa meli zilizokuwepo.

Ugharimiaji

Page 48: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

45

Jumla ya uwekezaji katika meli mbili ni DOLA ZA MAREKANI MILIONI 73.1 ambapo 40%

inatoka kwenye fedha za kampuni. Salio la 60% ni mkopo kutoka Benki ya Exim ya China

baada ya kufikiria njia nyingine zote kama vile;

1. Kuita wanahisa kuchangia kiasi hicho kwa utaratibu wa asilimia hamsini kwa hamsini

(50 kwa 50). Njia hii ilikuwa si halisi kwa sababu ya matatizo ya sera na fedha kwa

upande wa Tanzania.

2. Kuomba upande wa China pekee kuchanga mchango wote wa hisa. Njia hii

haikushauriwa kwa sababu ingebadili kabisa muundo wa umiliki kwa kupunguza nguvu

ya uwekezaji wa Tanzania kwa zaidi ya asilimia 50.

Meli moja yenye uwezo wa tani 57,000 ililetwa mwezi Septemba 2009 na sasa inafanya kazi.

Meli ya pili yenye uwezo wa tani 34,000 inatarajiwa kuletwa mwezi Desemba 2011.

Mdororo wa Uchumi Duniani

Matokeo ya mdororo wa uchumi katika viwanda vya usafirishaji mizigo kwa Meli na vya

utengenezaji meli duniani yamekuwa mabaya zaidi baada ya soko la usafirishaji kwa meli

kuanguka kama ilivyooneshwa kwenye Baltic Dry Index (BDI) ambayo ilishuka kutoka 11,793

mwezi Mei 2008 mpaka kufikia 800 mwezi Novemba 2008. Hii ni hali tete kwa kampuni za

usafirishaji kwa meli ndogondogo na za kati kama SINOTASHIP.

Hata hivyo, wataalam wanatabiri kuwa tasnia ya usafiri wa meli utahimili masharti ya soko hili

dhaifu kwa kipindi cha mwaka 2009 na 2010.

Malengo ya Baadaye

Malengo ya kampuni yetu kwa kipindi cha miaka 50 ijayo ni kuongeza usafirishaji kufikia

takribani vyombo 20, makontena na vichukuzi vikubwa ikijumuisha matangi ya kubeba gesi

yenye uwezo wa kubeba tani 10,000 kila moja, ikizingatiwa kwamba kwa wakati huo

uchimbaji wa gesi katika mwambao wa kusini mwa Tanzania utakua kwa kiasi kikubwa.

Pia tunatarajia kuwa takribani asilimia 50 ya vyombo vya kampuni vitakuwa vikipeperusha

bendera ya Tanzania, kwa maana hiyo tunatengeneza nafasi za kazi zaidi kwa Maofisa na

wafanyakazi wengine kuajiriwa Melini.

Page 49: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

46

MV Chang Shun Ii Bulk Carrier

Meli mpya yenye uwezo wa kubeba shehena ya tani 57,000

10.2.3 Kampuni ya Huduma za Meli – MSCL

Kampuni ya Huduma za Meli (Marine Services Company Limited – MSCL) ilianzishwa chini

ya Sheria ya Makampuni sura 212 mnamo tarehe 08/12/1997 kutokana na kilichokuwa kitengo

cha usafirishaji wa majini cha Shirika la Reli (TRC).

Page 50: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

47

Baada ya kuanzishwa kwa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL), mali zote zilizokuwa chini

ya kitengo cha usafiri majini cha TRC zilihamishiwa katika Kampuni hii mpya mnamo tarehe

21/06/1999 kupitia Gazeti la Serikali No. 125A. Kampuni ilianza kazi tarehe 01/08/1999 ikiwa

na mtaji wa meli 15 bila fedha yoyote.

Kampuni iliendelea kufanya kazi huku ikimiliki meli, bandari zote na miundombinu yake yote

katika maziwa makuu hadi tarehe 30/06/2006. Mnamo mwaka 2004, serikali ilianzisha

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari kupitia sheria No. 17 ya 2004. Sheria iliyoanzisha

Mamlaka ya Bandari ilianza kutumika tarehe 01/07/2006.

Kutokana na mabadiliko haya baadhi ya mali za Kampuni ya Huduma za Meli ikiwemo

miundombinu yote ya kibandari, meli moja, majengo ya ofisi, karakana na vyelezo katika

maziwa yote makuu vilihamishiwa Mamlaka ya Bandari Tanzania.

Aidha wafanyakazi 77 ikiwemo Menejimenti nzima ya Kampuni, nao walihamishiwa Mamlaka

ya Bandari. Mali za Kampuni ya Huduma za Meli zilihamishiwa TPA kwa GN No. 303 ya

tarehe 14/10/2005. Mabadiliko haya yalipunguza ukubwa na mali za Kampuni pamoja na

baadhi ya vyanzo vyake vya mapato.

Kampuni hii kwa sasa inaendesha jumla ya meli 14 za abiria na mizigo, ambapo meli 9 ziko

ziwa Victoria, 3 ziko ziwa Tanganyika na 2 ziwa Nyasa. Idadi hii ni baada ya meli moja

kuhamishiwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari. Jedwali Na. 9.3 inaonesha meli hizo kwa

kila ziwa.

Kampuni hii inaundwa na Matawi matatu yaani Tawi la Mwanza katika Ziwa Victoria; Tawi la

Kigoma katika Ziwa Tanganyika na Tawi la Kyela Katika Ziwa Nyasa. Makao Makuu ya

Kampuni yako Mwanza.

Shughuli kubwa za Kampuni hii ni kusafirisha abiria na mizigo katika maziwa yote matatu,

ikitoa huduma kwa wananchi wanaoishi katika maeneo ya mwambao wa maziwa haya na

katika visiwa, ndani ya nchi na nje ya nchi.

Vile vile Kampuni hii ni daraja katika shughuli za kibiashara na kijamii kati ya Tanzania na

nchi jirani. Nchi za Uganda na Kenya katika Ziwa Victoria, Burundi, Mashariki ya Jamhuri ya

Kidemokrasia ya Kongo na Zambia katika Ziwa Tanganyika, na Malawi katika Ziwa Nyasa.

Kutoa huduma bora, inayotegemewa, inayoaminika, inayotabirika, angalifu na yenye kujali

usalama kwa wateja wake katika maziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa.

Kuwa kampuni ya usafirishaji katika maziwa iliyo na ushindani, yenye kutegemewa,

salama na itendayo kwa kuwalenga wateja wake siku zote.

Kufanya matengenezo ya mara kwa mara (preventive/routine maintenance) ya meli

zake kufuatana na miongozo iliyopo katika “Merchant Shipping Act”. Kuboresha

Page 51: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

48

usalama wa abiria kwa kuhakikisha uwepo wa vifaa vya kuokolea maisha melini

vinatosheleza mahitaji kulingana na idadi na wafanyakazi walioko melini.

Kampuni hii inaendelea kutekeleza makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania, Jamhuri

ya Kidemokrasia ya Kongo na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Wakimbizi

(UNHCR) kwa kuwarudisha nyumbani Wakimbizi wa DRC toka Kigoma, Tanzania na

Mpulungu, Zambia kwenda Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Zoezi hili bado ni

endelevu.

Jedwali Na. 9.5 Uwezo wa Kila Meli na Mwaka wa Ujenzi kabla na Baada ya Uhuru

Jina la Meli Uwezo wa Ubebaji Mwaka Meli

Ilipojengwa Abiria Mzigo (Tani)

ZIWA VICTORIA

M.V. Victoria 1200 200 1960

M.V. Butiama 200 100 1980

M.V. Serengeti 593 350 1983

M.V. Clarias 293 10 1961

M.T. Nyangumi - (Mafuta) 350 1964

M.T. Ukerewe - 480 1983

M.L. Maindi - 120 1938

M.L. Wimbi - 120 1938

M.V. Umoja - 1200 1964

ZIWA TANGANYIKA

M.V. Liemba 600 200 1913

M.V. Mwongozo 800 80 1979

M.T. Sangara - (Mafuta) 350 1981

ZIWA NYASA

M.V. Iringa 139 5 1974

M.V. Songea 212 50 1973

Hali ya Uongozi na Utawala Kuanzia 1961

1976: Idara ya Usafirishaji Majini ilikuwa chini ya Mkurugenzi wa Usafirishaji Reli

ambayo makao makuu yake yalikuwa Nairobi – Kenya na hapa Tanzania

upande wa usafirishaji majini kitengo kilikuwa chini ya Mrakibu

Usafirishaji (District Traffic Superintendent – Mwanza) kitengo cha “Marine

Transport Officer – Mwanza” (Mwanza na Kigoma).

1977: Baada ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuvunjika kitengo cha Usafirishaji

majini kilibaki kikiendeshwa na Ofisi iliyokuwa ya Meneja Usafirishaji (CTM)

chini ya Warakibu wa Usafirishaji (Mwanza na Tabora) chini ya Marine

Transport Officer (MTO) Mwanza.

Page 52: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

49

1977: Meli zilizokuwa za Jumuiya ya Afrika Mashariki (East Africa Railways) Ziwa

Victoria nyingi zilikamatwa zikabaki nchini Kenya – Kisumu nazo ni M.V.

Victoria, M.V. Umoja, M.T. Nyangumi, M.S. Usoga, M.V. Uhuru na

nyinginezo nyingi.

Meli tulizobaki nazo upande wa Tanzania Ziwa Victoria ni M.V. Clarias, M.S.

Buvuma na M.V. Ng‟ombe na S.S. Buganda. Kwa Ziwa Tanganyika tulibaki na

meli ya M.S. Liemba ikiwa kwenye matengenezo makubwa ya kubadilishwa

kutoka injini za mvuke (steam engine) kuwekewa injini za mafuta (Diesel

Engine). Kazi ilikamilika mwaka 1978 na kuanza kazi ya kuhudumia wananchi

wa mwambao wa Ziwa Tangnyika kwa upande wa Tanzania na baadaye

wananchi wa nchi za jirani za Burundi, Zaire na Zambia.

1978: Kurudishwa kwa meli 3 kutoka Kenya ambazo ni M.V. Victoria, M.T.

Nyangumi na M.V. Umoja.

1979: Ndiyo ujenzi wa meli zilizotoka Ubelgiji ulipoanza. Meli hizo ni: M.V. Bukoba

ilijengwa mwaka 1979, M.V. Butiama na M.T. Sangara zilijengwa mwaka 1980,

M.V. Mwongozo mwaka 1982 na M.T. Ukerewe mwaka 1983.

Kitengo cha uendeshaji meli, kwenye maziwa haya matatu (3); Ziwa Nyasa,

Tanganyika na Victoria ziliwekwa chini ya Meneja Usafirishaji. Reli (CTM)

kwa kuunda matawi matatu. Tawi la Mwanza chini ya cheo kipya

kilichojulikana kama Engineer Incharge – Lake Victoria, hivyo hivyo ilikuwa

kwa vituo vya Kyela na Kigoma.

1982: Shirika la Reli lilipata udhamini wa uendeshaji wa meli katika maziwa kutoka

Denmark kupitia DANIDA.

Uundwaji wa kitengo cha usafirishaji majini kiliondolewa kwa Meneja

Usafirishaji (CTM) Reli na kuanzishwa Idara iliyojulikana kama TRC MARINE

DIVISION chini ya Chief of Marine Operations (CMO), ambaye aliwajibika

kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli.

1983: Zilizokuwa meli za TACOSHILI Ziwa Nyasa zilikabidhiwa Shirika la Reli kwa

kuziendesha na miundombinu yake yote. Meli hizo ni M.V. Iringa na M.V.

Songea.

1988: Pamoja na hayo yote kufanyika chini ya msaada wa DANIDA, yaliundwa

matawi matatu ambayo ni Mwanza, Kigoma na Kyela chini ya uongozi wa

District Marine Manager na vitengo kama vile Karakana, Ugavi na mengineyo.

Makao makuu yakiwa Dar-es-salaam. Katika kipindi hicho meli za M.V.

Serengeti na M.T. Linda zilijengwa kwa msaada wa DANIDA. Pia, katika

kipindi hicho meli za M.V. Victoria na M.V. Liemba zilifanyiwa matengenezo

makubwa ikiwa ni pamoja na kuwekewa mitambo mipya.

1996: Kampuni ya Huduma za Meli (Marine Services Company Limited – MSCL)

ilianzishwa chini ya Sheria ya Makampuni sura 212 mnamo tarehe 08/12/1997

kutokana na kilichokuwa kitengo cha usafirishaji wa majini cha Shirika la Reli

(TRC). Kutenganisha Shirika la Reli na kitengo cha usafirishaji wa majini na

Page 53: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

50

kuanzishwa Kampuni mpya ya Huduma za Meli ilikuwa ni mwanzo wa

utekelezaji wa mkakati wa ubinafishwaji wa taasisi hizo mbili.

Ajali ya meli ya M.V. Bukoba

Tarehe 21 Mei, 1996 meli ya M.V. Bukoba ilipata ajali umbali wa kilometa 8 kutoka Bandari

ya Mwanza Kaskazini ikiwa njiani kutoka Bukoba. Athari za ajali ni pamoja maisha ya watu

kupotea, kuzama kwa chombo cha usafiri na hivyo kufanya baadhi ya njia kukosa chombo cha

kuhudumia, Wananchi walipoteza imani kwa Serikali na Shirika la Reli (TRC). Pia, ajali ya

M.V. Bukoba ilisababisha kuanzishwa Mamlaka ya Uthibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi

Kavu (SUMATRA) na kuboreshwa kwa usalama wa usafiri wa majini. Kuna mpango wa

uokozi majini unaoandaliwa chini ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Meli ya M.V. Bukoba ikiwa inazama

Mara tu baada ya uhuru wa Tanzania, sera ilikuwa ni Serikali kuendesha na kusimamia usafiri

wa majini katika maziwa makuu. Sera hiyo iliendelea hadi mwaka 1995 ambapo Serikali

ilijitoa kabisa katika shughuli za biashara na hivyo kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji

binafsi kuwekeza katika shughuli mbalimbali za kibiashara zikiwemo usafiri wa majini.

Serikali imeweka mazingira mazuri na inakaribisha wawekezaji toka nje ya nchi na ndani ya

nchi kuwekeza katika eneo hili, yaani kununua meli nzuri zaidi ambazo zitakidhi vyema

mahitaji ya wasafiri katika Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa.

Shughuli kuu ya MSCL ni kutoa huduma ya usafirishaji majini kwa abiria na mizigo katika

Maziwa ya Victoria, Tanganyika na Nyasa. Vile vile hujishughulisha na utengenezaji na

utunzaji wa vyombo vyake. Katika kutekeleza shughuli zake za kudhibiti na kiutawala, MSCL

imekuwa ikiweka maanani yafuatayo:

i. Malengo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

ii. Kipengele cha wajibu wa huduma kwa umma (Public Service Obligation) kwa watu

waishio kuzunguka maziwa hayo matatu ambao hawana njia mbadala za usafiri,

hususan, kuzunguka Maziwa ya Tanganyika na Nyasa, ambako huduma za usafiri ni

chache.

Page 54: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

51

iii. Usalama, afya na ustawi wa jumla wa umma kwa kufanya shughuli zake katika njia

ambazo zinalinda mazingira kwa taratibu zilizofungamana na endelevu.

Tanzania imepitia mifumo miwili ya kisiasa tangu mwaka 1961. Mara tu baada ya uhuru

tulikuwa na mfumo wa ujamaa. Katika kipindi hicho meli zilitoa huduma kwa hasara na

serikali ilifidia hasara hiyo.

Katika ulinzi, meli zimetoa michango mbalimbali katika ulinzi wa nchi. Kwa mfano, meli ya

M.V. Victoria ilisafirisha zaidi ya wanajeshi 2,000 wa Tanzania kutoka Mwanza kwenda

Uganda katika Ziwa Victoria ili kufanikisha vita ya kumuondoa madarakani nduli Idd Amin.

Meli hii pia ilitumika kuwarudisha wanajeshi Tanzania.

Meli ya M.V. Umoja ilisafirisha vifaa vya kijeshi kama vile vifaru na wanajeshi kwenda

Uganda wakati vya vita hivyo. Pia meli ya M.T. Nyangumi ilisafirisha mafuta ya kuendeshea

vifaa mbalimbali wakati wa vita hivyo.

Katika kipindi hiki cha soko huria, Kampuni imekuwa ikijiendesha kibiashara kwa kutumia

mapato yanayotokana na usafirishaji wa abiria na mizigo.

Mafanikio Yaliyopatikana Hadi Sasa

i) Kampuni imeendelea kuzifanyia matengenezo makubwa na yale ya kawaida meli

ambazo ni chakavu.

ii) Kampuni imeendelea kufanya ukarabati mkubwa (Rehabilitation) na kuboresha hali

ya meli zake ili kuziongezea maisha na uhakika wa kufanya safari zake salama.

iii) Kuongeza na kuimarisha hali ya usalama wa meli zake kwa kuboresha vifaa vya

usalama, kusisitiza uangalifu wa utendaji kazini, kuepusha ulevi na kuelimisha

wananchi (wasafiri) matumizi sahihi ya vifaa vya usalama ndani ya meli zetu.

iv) Kuzifanyia ukaguzi kila mwaka kupitia Mkaguzi wa Serikali na kufuata miongozo ya

Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (SUMATRA) kwa uendeshaji salama.

v) Kampuni imekuwa ikiziwekea bima meli zote dhidi ya matukio yoyote yasiyotarajiwa

ikiwa ni pamoja na abiria na mizigo pamoja na wafanyakazi melini.

vi) Kupanua soko la meli za Kampuni kupitia matangazo redioni na katika majarida

mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.

vii) Kukuza na kuboresha huduma kwa wateja (Customer Care) ambao ndiyo msingi wa

kuboresha soko.

viii) Uongozi wa Kampuni kwa kutambua kuwa uwezo wa serikali kugharamia miradi

yote una ukomo, tuliandaa andiko la mradi wa ukarabati wa meli za Kampuni na

Page 55: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

52

ujenzi wa meli mpya na kulisambaza kwa washirika wa maendeleo (development

partners).

Serikali ya Denmark, kupitia Shirika lake la maendeleo “DANIDA” ilionesha utayari kutoa

fedha za kugharamia mradi na tayari upembuzi yakinifu umefanyika na ripoti yake iko kwenye

hatua za mwisho. Aidha, serikali ya Ujerumani imeonesha utayari wa kugharamia matengenezo

makubwa ya kuboresha meli ya M.V. Liemba.

Changamoto

Kampuni ya Huduma za Meli inakabiliwa na changamoto mbalimbali kama ifuatavyo:

i) Meli nyingi kuwa za zamani sana na kuwa chakavu na hivyo kuchukua sehemu

kubwa ya mapato yapatikanayo katika kufanya matengenezo ya mara kwa mara na

pia kusababisha ongezeko la matumizi ya mafuta.

ii) Kupanda kwa bei za vipuri vinavyohitajika kuzifanyia matengenezo meli zetu

ambavyo vinapatikana nje ya nchi.

iii) Ushindani wa kibiashara na vyombo binafsi katika usafirishaji katika barabara

zinazozunguka maziwa yetu.

iv) Gharama na kodi zilizowekwa na Serikali kama ushuru wa mafuta, gharama za

matumizi ya maji ya Ziwa, ushuru wa Serikali za mitaa, na gharama za Mamlaka ya

Uthibiti wa Vyombo vya Majini na Nchi Kavu (SUMATRA).

v) Maslahi madogo kwa watumishi ikiwa ni mishahara na posho mbalimbali ambazo

zinafanya baadhi ya watumishi kukimbilia kwa washindani wetu kwa visingizio vya

kufuata maslahi bora zaidi.

vi) Kuzorota kwa utendaji wa reli katika kusafirisha abiria na mizigo wakati wa kipindi

cha mpito kuelekea ubinafsishaji kuliathiri sana utendaji wa meli zetu.

vii) Kupungua kwa kina cha maji katika maziwa yetu kuliathiri uwezo wa upakiaji wa

mzigo katika kiwango kinachohitajika na vile vile kuathiri usalama wa meli zetu.

viii) Kuchakaa kwa miundombinu ya kibandari katika maziwa yetu na sehemu nyingine

kutokuwepo kabisa, kumeathiri utendaji wa meli zetu katika kubeba abiria na mizigo.

ix) Kutokuimarika kwa hali ya kisiasa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya

Kongo ambako kumeendelea kukwaza shughuli za kibiashara na usafirishaji wa

abiria.

x) Majukumu ya kuendelea kutoa huduma katika maeneo ambayo Kampuni inafanya

uendeshaji kwa hasara (Public Obligation) bila kupata ruzuku yoyote kutoka

Serikalini.

Page 56: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

53

Matarajio ya Kampuni

i. Kujiendesha kwa uwezo wote tulio nao ifikapo mwaka 2013.

ii. Kutoa huduma zenye ongezeko la thamani.

iii. Kuajiri na kubakiza watumishi stadi katika soko la sasa.

iv. Kuongeza mapato ya shughuli kwa zaidi ya 50% ifikapo mwisho wa mwaka

2013.

v. Kutoa huduma ya usafiri wa abiria na mizigo kwa usalama, uhakika na kwa bei

nafuu.

vi. Kuwekeza kwenye miradi ambayo inalenga kupunguza gharama za uendeshaji

na kuboresha huduma.

10.2.4 Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA)

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) ilianzishwa kwa Sheria ya

Bunge Na.9 ya mwaka 2001. Mamlaka ilianza kazi mwaka 2004 na kupewa jukumu la

kudhibiti usafiri wa Nchi Kavu na Majini. Mamlaka hii iliundwa kufuatia kufutwa kwa Shirika

la kudhibiti shehena (TCFB), na kuunganishwa na Mamlaka ya Leseni za Usafirishaji (CTLA),

hivyo kuundwa kwa chombo kijulikanacho kama SUMATRA. Utekelezaji wa majukumu ya

Mamlaka ulianza mwezi Novemba, 2004 baada ya Serikali kukamilisha uundwaji wa Bodi na

uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu.

Mamlaka inaongozwa na Bodi ya Wakurugenzi na shughuli za kila siku za Mamlaka

zinasimamiwa na Mkurugenzi Mkuu. Mamlaka ina ofisi katika mikoa kumi na tano ya

Tanzania Bara ikiwemo Dar es Salaam, Kilimanjaro, Mbeya, Mwanza, Dodoma, Kagera,

Rukwa, Kigoma, Mtwara, Tanga, Mwanza, Tabora, Mara, Arusha na Iringa. Aidha, ili

kusogeza huduma karibu na wananchi, Mamlaka ina Waratibu Wateule kutoka ofisi za

Makatibu Tawala katika mikoa ambayo Mamlaka haijafungua ofisi zake. Lengo ni kuwa na

ofisi katika mikoa yote ya Tanzania Bara ifikapo mwaka 2013.

Majukumu ya Mamlaka kwa mujibu wa sheria iliyounda SUMATRA na kwa mujibu wa Sheria

za Sekta ni:

Kuhimiza na kukuza ushindani na ufanisi katika soko la usafirishaji wa nchi kavu na

majini, kulinda maslahi ya watumiaji wa huduma,

Kulinda na kujenga mazingira ya kuvutia kwa watoa huduma,

Kuendeleza na kuhakikisha kuwa huduma za usafirishaji zinakidhi mahitaji ya

watumiaji ikiwa ni pamoja na wenye kipato cha chini na wasiojiweza,

Kuwaelimisha watumiaji wa huduma za usafiri na Wananchi kwa ujumla kuhusu

huduma zinazotolewa na sekta na kuhakikisha kwamba watoa huduma na watumiaji

wanalinda na kutunza mazingira.

Page 57: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

54

Majukumu ya Mamlaka kwa Mujibu wa Sheria za Sekta

(a) Usafiri kwa Njia ya barabara - kutoa leseni za usafirishaji kwa magari ya abiria

kuanzia saba na kuendelea na magari ya mizigo.

(b) Bandari na Usafiri Majini - kuweka na kusimamia viwango na masharti ya

huduma ili kuleta ufanisi katika utendaji, ushindani na huduma bora;

(c) Ulinzi na Usalama wa usafiri Majini - kusimamia ulinzi na usalama wa vyombo

vya usafiri majini na pia kulinda mazingira.

(d) Reli: kudhibiti usalama wa reli.

Mamlaka inafanya kazi kwa misingi na maadili ya udhibiti, uwazi, ushirikishwaji, wepesi wa

kutambua mabadiliko (flexibility), uwajibikaji (accountability) na kutokuwa ubaguzi (non-

discrimination).

Mafanikio ya SUMATRA

Tangu kuanzishwa kwake Mamlaka kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imepata mafanikio

mengi ikiwa ni pamoja na:

Kukabiliana na ajali za barabarani,

i. Mamlaka ilifanya Utafiti wa kina kuhusu ajali za barabarani kwa kutumia

mshauri mwelekezi (Consultant) na kuonekana kuwa asilimia 76% ya ajali zote

za barabarani Tanzania Bara zinasababishwa na madereva. Kwa kutumia

mapendekezo ya utafiti huo utaratibu wa mabasi ya abiria kuanza kutumia “log

book” umeanzishwa ili kuratibu mwendo kasi wa mabasi hayo.

ii. Mamlaka imekuwa ikihakikisha kwamba wenye mabasi wanakuwa na nyaraka

muhimu ikiwa ni pamoja na hati za ukaguzi wa gari/magari (Vehicle Inspection

Report) kutoka Jeshi la Polisi na hati ya bima (insurance cover) kabla ya

kupewa leseni.

iii. Mamlaka imekuwa ikipanga ratiba ya safari za mabasi ya abiria zinazozingatia

mwendo salama barabarani na kusimamia masharti ya ratiba na leseni ikiwa ni

pamoja na madereva kufuata muda uliopangwa kwenye ratiba na kutembeza

basi kwenye njia zilizoidhinishwa na Mamlaka.

iv. Mamlaka imekuwa ikiweka utaratibu wa kuwa na madereva wawili kwa mabasi

yanayosafiri kwa muda unaozidi saa 12 na kutoa elimu kwa umma kupitia

vipindi vya redio na matangazo ya mara kwa mara katika vyombo vya habari

ikisisitiza umuhimu wa matumizi salama ya barabara.

Juhudi za kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Dar-es-Salaam

i. Kuondoa mabasi madogo (vipanya) na kuingiza mabasi makubwa;

Mamlaka ilikwishaanza juhudi za kupunguza matumizi ya mabasi madogo

Page 58: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

55

(vipanya) kwa kutotoa leseni mpya kwa mabasi hayo kutoa huduma katikati ya

Jiji tangu Julai, 2006. Mabasi madogo kwa hivi sasa yanatoa huduma

pembezoni mwa Jiji na hivyo kuboresha upatikanaji wa usafiri katika maeneo

hayo. Aidha, kuondolewa kwa mabasi madogo kutoa huduma katikati ya Jiji

kumehamasisha uingizaji wa mabasi makubwa ya kutoa huduma ya usafiri wa

umma Jijini na kuongeza ubora wa huduma hii. Idadi ya mabasi makubwa

ikilinganishwa na mabasi madogo katika kipindi cha mwaka 2006 hadi mwaka

2010 imeainishwa katika jedwali hapa chini.

Jedwali Na: 9.6 Idadi ya mabasi makubwa na madogo ilivyokuwa Dar es

Salaam kwa kipindi cha Julai 2006 hadi Julai 2010

Mwaka Mabasi madogo Mabasi makubwa

Julai 2006 3,382 1,273

Julai 2008 2,978 2,002

Julai 2009 2,212 2,779

Julai 2010 1,747 4,182

Chanzo: SUMATRA

Changamoto Zinazoikabili Mamlaka

i. Ajali za barabarani: Pamoja na jitihada mbalimbali zinazochukuliwa serikali

kwa kushirikiana Mamlaka na wadau wengine, ajali za barabarani zimeendelea

kuongezeka. Hali ya ajali barabarani ni kama ilivyoonyeshwa katika jedwali

namba 2 na kielelezo namba 1 hapa chini.

Jedwali Na.9.7: Ajali za Barabarani: Mwaka 2005 - 2010

Mwaka 2005 2006 2007 2008 2009 2010

Ajali 16,388 17,039 17,753 20,615 22,739 24,665

Ongezeko

%

4 4 16 10 8.5

Chanzo: Polisi Usalama Barabarani

Page 59: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

56

Chati Na: 9.1 .Idadi ya Ajali za Barabarani

ii. Uharamia katika baharí ya Hindi: pamoja na kuwa na kituo cha kisasa cha

mawasiliano cha uokoaji na utafutaji katika bandari ya DSM, uwezo mdogo wa

kuitikia na kutoa msaada haraka pindi taarifa za majanga zitolewapo bado ni

changamoto.

iii. Usalama wa vyombo vidogo vya usafiri majini: kumekuwa na ugumu wa

wamiliki wa vyombo vidogo vya majini kuitikia wito ili vyombo vyao

vikaguliwe.

iv. Miundombinu duni ya barabara: maeneo yenye miundombinu duni ya

barabara katika miji hukumbwa na tatizo la ubora na uhaba wa huduma za

usafiri. Imekuwa ni jambo la kawaida kwa maeneo yenye miundombinu hafifu

kuhudumiwa na vyombo vya usafiri ambavyo ni duni ama /chakavu huku

watumiaji wakilazimika kulipia huduma kwa bei ya juu.

v. Uchakavu wa miundombinu ya reli na wizi wa vifaa vya reli: uchakavu wa

miundombinu ya reli na wizi wa vifaa vya reli kwa kiwango kikubwa unaathiri

hali ya usalama na ulinzi wa reli.

Page 60: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

57

Matarajio Kwa Miaka 50 Ijayo

Matarajio ya Mamlaka kwa kipindi cha miaka 50 ijayo ni kutatua changamoto

zinazoikabili sasa ili kuboresha utoaji wa huduma kufikia viwango bora kama ilivyo

katika mataifa yaliyoendelea. Ili kufikia matarajio hayo ni jitihada za makusudi

zinahitajika ili kuendeleza na kuboresha matandao wa miundombinu nchini

ikijumuisha; reli, bandari na usafiri majini na barabara.

Kwa kuwa Mamlaka ni mdhibiti wa usafiri wa nchi kavu na majini inatarajia kufanya

yafuatayo;

i. Kushirikiana na vyombo ya usalama hapa nchini na nje katika kukabiliana na

majanga mbalimbali yanayogusa usafiri wa majini na nchi kavu. Hii itajumuisha

kuwa na vifaa vya kisasa vya mawasiliano (ambapo huduma ya udhibiti inaweza

kufanywa mikoani ikisimamiwa na mtu akiwa DSM

ii. Kuimarisha ofisi kwa ajili ya kutoa huduma katika ngazi ya chini (Wilaya au

Kata) na kujenga uwezo wa kitaaluma kwa watumishi ili kusimamia udhibiti

kwa ufanisi zaidi.

10.3 USAFIRI WA ANGA

10.3.1 Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA)

Kabla ya Uhuru, kuanzia mwaka 1948 nchi za Kenya, Tanganyika, Uganda na visiwa vya

Zanzibar zilikuwa chini ya utawala wa Uingereza, ambazo baadhi ya shughuli za kiuchumi

zilikuwa zikifanywa kwa pamoja chini ya East African High Commission. Moja ya shughuli

hizo ni masuala ya Usafiri wa Anga.

Tangu wakati huo, shughuli nyingi za usafiri wa anga zilikuwa zikifanywa kwa pamoja kwa

sababu mtawala wa eneo hilo lote alikuwa ni Muingereza. Kwa hali halisi, ushirikiano wa nchi

hizi ulianza kabla ya mwaka 1948.

Hatua ya kwanza kabisa zilianza mwaka 1943 wakati wa Mkutano mkuu wa magavana wa

Afrika Mashariki ulioteua kamati kuandaa mpango wa maendeleo ya mawasiliano baada ya

vita kuu ya kwanza ya dunia.

Lakini kimsingi, shughuli za usafiri wa anga, hasa za kibiashara zilianza tangu mwaka 1929

wakati huo kukiwa na shirika la ndege la Wilson ambalo lilianzishwa na Florence Wilson.

Shirika hilo lilivunjika mwaka 1939 vita kuu ya pili ya dunia ilipoanza na kutumika kama

Kikosi cha Jeshi la Anga la Mfalme wa Uingereza.

Page 61: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

58

Baada ya Tanganyika kupata uhuru wake mwaka 1961, East African High Commission

ilivunjwa na kuanzishwa East African Common Services Organisation. Moja ya idara yake

katika organizesheni hii ilikuwa ni Kurugenzi ya Usafiri wa Anga ya Afrika Mashariki (East

African Directorate of Civil Aviation).

Majukumu ya Kurugenzi hii yalikuwa ni kutoa huduma za uongozaji ndege, huduma za

mawasiliano, utoaji leseni, usajili wa ndege, utafutaji na uokoaji ndege zinapopotea na kupata

ajali, utoaji leseni kwa mashirika ya ndege, uchunguzi wa ajali za ndege na utoaji wa taarifa za

anga.

Makao Makuu ya kurugenzi hii yalikuwa Nairobi, Kenya ambako Mkurugenzi Mkuu alikuwa

na ofisi zake na nchi zilikuwa na ofisi ambazo zilikuwa zikimsaidia Mkurugenzi Mkuu. Kituo

Kikuu cha kuongozea ndege nacho kilikuwa Nairobi.

Usimamizi wa viwanja vya ndege ulikuwa chini ya Serikali zenyewe, hazikuwa chini ya

Kurugenzi za Usafiri wa Anga. Shughuli na majukumu ya Kurugenzi hii yaliendelea hadi

mwaka 1967 wakati mataifa haya yalipoamua kuanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Wakati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

Baada ya kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1967, shughuli za usafiri wa

anga ziliendelea kuwa chini ya Kurugenzi ya Usafiri wa Anga ya Afrika Mashariki. Ingawa

Kurugenzi hii ilikuwa ikifanya shughuli za kiufundi katika masuala ya usafiri wa anga, utoaji

wa huduma za matengenezo na uangalizi wa viwanja, zimamoto zilibaki kuwa ni jukumu la

serikali za nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kulingana na sheria ya Usafiri wa Anga ya Afrika Mashariki, Kurugenzi hii ilikuwa chini ya

bodi ambayo ilikuwa na mwenyekiti aliyekuwa akiteuliwa na Jumuiya, Mkurugenzi Mkuu na

Wakurugenzi kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Makao Makuu

yalikuwa Nairobi, Kenya. Chini yake kulikuwa na Wakurugenzi watatu kutoka nchi tatu

wanachama wa jumuiya wakiwakirisha nchi zao na ambao pia ofisi zilikuwa katika nchi zake,

Dar es Salaam- Tanzania, Nairobi- Kenya na Entebbe- Uganda. Mtanzania wa kwanza kuwa

Mkurugenzi wa Usafiri wa Anga Tanzania alikuwa Lot Mollel.

Ofisi ya Nairobi ilikuwa inawajibika kusimamia shughuli zote zinazohusu masuala ya usafiri

wa anga kama uongozaji wa ndege, ikisimamia pia shughuli za ajira na mafunzo.

Katika kipindi hiki, Watanzania mbalimbali walifunzwa na kupata ujuzi katika masuala ya

urubani, uhandisi wa ndege, uongozaji ndege na nyinginezo zinazohusiana na shughuli za anga.

Mitambo mbalimbali pia iliwekwa katika vituo mbalimbali kwa ajili ya kusaidia mawasiliano

kati ya marubani na waongoza ndege na pia utoaji wa taarifa mbalimbali, ingawa kimsingi

kituo kikubwa zaidi cha kuongozea ndege kilikuwa Nairobi.

Page 62: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

59

Baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki

Baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977 nchi zote zililazimika

kubadilisha muundo wa Kurugenzi hiyo ambayo kwa upande wa Tanzania ilikuwa sasa

Kurugenzi ya Usafiri wa Anga Tanzania ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu, Lot Mollel.

Majukumu yote ambayo Kurugenzi ya Afrika Mashariki ilikuwa ikiyafanya sasa yalihamia

Tanzania na hivyo kuwa na mamlaka ya kufanya shughuli zao wenyewe chini ya Wizara ya

Mawasiliano na Uchukuzi. Hata hivyo kutokana na unyeti wa masuala ya usafiri wa anga, anga

la Tanzania liliendelea kusimamiwa chini ya kituo cha kuongozea ndege cha Nairobi kwa

miezi kadhaa hadi Serikali ilipojiweka sawa.

Hii ilitokana na ukweli kwamba kituo kikuu cha kuongozea ndege kilikuwa Nairobi, hivyo

serikali ilipaswa kwanza kuweka kituo chake. Kituo kiliwekwa Dar es Salaam na kilifungwa

vifaa vyote muhimu vilivyokifanya kuwa na uwezo wa kufanya mawasiliano na vituo vingine

vyote nchini na vituo vingine vikuu nje ya mipaka ya Tanzania.

Kurugenzi hii ilianzishwa kwa sheria ya Bunge ya mwaka 1977 mbayo ilikuwa chini ya Bodi

iliyokuwa na wajibu wa kumshauri Waziri anayehusika na masuala mbalimbali yahusuyo

usafiri wa anga nchini. Mkurugenzi Mkuu ni mmoja wa wajumbe katika bodi hiyo ambaye

alikuwa akiingia kwa wadhifa wake wakati wajumbe wengine walikuwa wakiteuliwa na

Waziri. Chini ya sheria hii, Kurugenzi ilipewa mamlaka ya kusimamia shughuli zote za usafiri

wa anga kama ilivyokuwa wakati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kutokana na mageuzi ya kiuchumi na kimifumo, Kurugenzi hii ilibadilika na kuwa Wakala wa

serikali mwaka 1997, lengo likiwa kuipa madaraka ya kufanya maamuzi na kazi zake kwa

haraka na ufasaha. Kuanzia wakati huo ikabadilishwa jina na kuitwa Mamlaka ya Usafiri wa

Anga. Kazi zake ziliendelea kuwa zile zile na Mkurugenzi Mkuu wa kwanza chini ya Mamlaka

hii alikuwa Mhandisi Bibi Margaret Munyagi.

Mageuzi haya yalileta mabadiliko zaidi kwani mwaka 2003, Mamlaka ilipewa uhuru zaidi

chini ya Sheria ya kuanzishwa Mamlaka ya mwaka 2003, Wizara ikijiondoa katika shughuli za

utendaji ikibaki kuisimamia sera zaidi. Mkurugenzi Mkuu wake aliendelea kuwa Mhandisi Bibi

Margaret Munyagi hadi mwaka 2010 alipostaafu kwa mujibu wa sheria.

Tangu uhuru mwaka 1961, kumekuwa na maendeleo ya kutosha wa upande wa Mamlaka

katika kusimamia na kujishughulisha na majukumu yake kama ilivyoanishwa katika sheria na

pia kama ilivyoanishwa katika Mkataba wa Chicago chini ya Shirika la Kimataifa la Usafiri wa

Anga Duniani (ICAO).

Tangu wakati huo, kumekuwa na maendeleo mengi, kuanzia katika mafunzo kwa Watanzania

ambao walikuwa wachache wakati ule hadi hivi sasa ambapo wataalam wote waliopo kwa sasa

ni matunda ya serikali kuwasomesha na kuwapata madaraka kufanya kazi walizotakiwa

kufanya.

Udhitibi wa Usalama wa Anga

Kiwango cha udhibiti wa usalama wa anga ni kikubwa hadi sasa, na Tanzania ni moja ya anga

ambalo inajulikana kuwa ni salama kuliko anga nyingine nyingi za Afrika. Ni ajali chache

zimetokea katika eneo hilo ikilinganishwa na maeneo mengine mbalimbali ya Afrika, hasa

Page 63: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

60

ikizingatiwa kwamba kutokana na takwimu za ICAO, Afrika ni bara linaoongoza kwa kuwa na

ajali nyingi za ndege.

Haya yote yamewezekana kutokana na utaratibu wa Mamlaka kuendelea kufanya ukaguzi na

utoaji vyeti kwa ndege, makampuni ya ndege, viwanja vya ndege na kutoa mitihani kwa

marubani na wahandisi.

Hivi sasa Mamlaka imekamilisha kuandaa Kanuni za Mfuko wa Mafunzo kwa ajili ya

marubani na wahandisi wa ndege uliowekwa kwa sheria namba 10 ya TCAA ya 2003 kwa ajili

ya kukabiliana na uhaba wa wataalamu katika sekta baada ya serikali kwa kipindi kirefu

kusitisha mafunzo kwa wataalam wake kutokana na hali mbaya ya kiuchumi iliyolikabili taifa.

Mafanikio mengine ni kukamilishwa kwa uanishaji wa kanuni za usafiri wa anga kwenye

Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kuboresha usalama, siyo tu katika anga la Tanzania, bali pia

katika anga la jirani zetu katika eneo la Afrika Mashariki.

Uanzishwaji wa Wakala wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wa Kusimamia Usalama wa Usafiri

wa Anga ni moja ya mafanikio ambayo katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru serikali

imefanikiwa kuianzisha. Lengo la wakala hii ni kuendeleza rekodi safi ya nchi katika suala la

kuwa na anga salama kwa sababu chini ya wakala hii, nchi za Afrika Mashariki zitaunganisha

utaalam wa usalama wa anga na hivyo kuwa na nguvu zaidi katika kusimamia usalama na

kuepusha ajali. Mkurugenzi wake wa kwanza ambaye bado anaendelea na wadhifa huo ni

Mtanzania, Bw. Mtesigwa Maugo.

Udhibiti wa Biashara na Uchumi

Idadi ya watoa huduma ya usafiri wa anga wenye leseni imeongezeka kiasi kikubwa hivi sasa

wamefikia 34. Zamani tulikuwa na shirika moja tu la ndege, ATC, lakini hivi sasa baada ya

kufungua masoko, tumekuwa na mashirika mengi zaidi ya ndege ambayo yanatoa huduma za

usafirishaji abiria ndani na nje ya nchi.

Mashirika na Makampuni ya ndege kutoka nje nayo yanazidi kuongeza huduma za usafiri wa

anga nchini. Hivi sasa mashirika ya Kimataifa yanayotoa huduma nchini yapo zaidi ya 22.

Idadi ya marubani wazalendo imeongezeka tangu kupata uhuru na hivyo kufanya kazi katika

mashirika mbalimbali ya ndege, si ndani tu ya Tanzania, bali wapo pia marubani watanzania

ambao wanafanya kazi nje ya nchi katika mashirika mbalimbali ya ndege.

Idadi ya abiria wanaotumia usafiri wa anga kuja na kuondoka katika viwanja inaendelea

kuongezeka. Hadi hivi sasa, kwa mwaka zaidi ya abiria milioni 4 wanatumia usafiri huu.

Uongozaji Ndege

Kuanzishwa kwa Chuo cha Waongoza ndege Tanzania (Civil Aviation Training College -

CATC) ambacho hadi sasa kimetoa karibu waongoza ndege wote wanaofanya kazi katika vituo

mbalimbali vya kuongozea ndege ndani na nje ya nchi. Chuo hiki pia kinatoa mafunzo kwa

waongoza ndege wengine kutoka nje ya Tanzania hata kwenda nje ya nchi kutoa mafunzo kwa

maombi mbalimbali kutoka katika nchi hizo. Chuo hiki kimekuwa msaada mkubwa kwa

serikali kwa sababu kimesaidia kupunguza matumizi ya fedha nyingi za kigeni ambazo serikali

ingetoa kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wataalam wapya wanaoingia katika fani hii muhimu.

Page 64: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

61

Mamlaka ya Usafiri wa Anga imeendelea na mpango wake wa uwekaji wa mitambo ya kisasa

katika vituo mbalimbali na ubadilishaji wa mitambo chakavu ya kuongozea ndege katika

maeneo mengi ya nchi kama Songea, Arusha, Kigoma na Tanga. Moja ya maeneo ambayo

teknolojia inakwenda kasi na kuathiri utendaji ni katika usafiri wa anga, lakini pamoja na hali

hiyo, serikali imeweza kwenda na wakati kwa kuweza kubadilisha mifumo mbalimbali ya

mawasiliano na mitambo kiasi cha kuweza kuendana na matakwa na kanuni za ICAO.

Ubadilishaji wa mitambo ya mawasiliano ya VSAT wa SADC umekamilika na sasa mitambo

ya kisasa zaidi imeshasimikwa na inafanya kazi. VSAT pia imeunganishwa na mtandao wa

mawasiliano wa nchi za Kaskazini mwa Afrika (NAFISAT VSAT).

Mamlaka pia imeweza kuweka mitambo ya kisasa ya kungozea ndege (VOR/DME) na wa

mwisho umewekwa katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Zanzibar na katika Kiwanja

cha Mwanza.

Rada ya kuongozea ndege ambayo ilifungwa katika Kiwanja cha Kimataifa cha Julius Nyerere

(JNIA) ni moja ya mitambo muhimu ambayo kwa kiasi kikubwa inasaidia kuingiza mapato na

pia kuhakikisha kwamba usalama katika anga letu unaimarika.

Kujengwa jengo la Makao Makuu ya Mamlaka lililokamilika hivi karibuni ambalo

limewezesha wafanyakazi wote wa Makao Makuu kufanyakazi pamoja na pia kuwarahisishia

wateja kupata huduma zote sehemu mmoja kwa wakati mmoja.

Malengo ya Mamlaka katika kipindi cha miaka 50 ijayo

Malengo ya Mamlaka yapo kwenye makundi makubwa yafuatayo:-

(a) Usalama (Safety and Security)

Pamoja na kuhakikisha usalama (safety and security), kwa kufanya juhudi za makusudi

kuzuia matatizo, Mamlaka kwa kushirikiana na taasisi nyingine kama yetu zitaweka

utaratibu wa kutumia wataalam kwa pamoja. Hatua hii itaenda sambamba na kuongeza

idadi ya wataalam katika fani za uhandisi na urubani. Aidha, ili kutunza mazingira na

kupunguza usumbufu, mifumo mizima ya utoaji moshi (engine emissions) na kelele

(noise pollution) itaboreshwa.

(b) Uongozaji Ndege

Mitambo yote itabadilishwa ili itumie teknolojia ya “digital” kwa njia ya satelaiti.

Mitambo ya Automatic Dependent Survaillance – Broadcast (ADS-B), yenye uwezo wa

kusambaa nchi nzima. Aidha, mawasiliano ya uongozaji ndege yataendelea kuboreshwa

kwa kutumia mfumo wa kisasa wenye ufanisi (Performance Based Navigation). Pia

matumizi ya anga yataboreshwa kwa kushirikiana na nchi za EAC, SADC na hatimaye

Afrika nzima.

(c) Chuo cha Mafunzo ya Usalama wa Anga

Chuo cha Usalama wa Anga kitaendelea kuimarishwa kwa kuwa na majengo yake

yenyewe na kuweza kujitegemea. Mafunzo ya wakufunzi yataimarishwa ili kukidhi

kiwango cha elimu ya juu cha kitaifa na kimataifa. Chuo kinategemewa kupanua wigo

Page 65: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

62

wake kwa kutoa mafunzo ya Urubani, uhandisi wa ndege na huduma za uendeshaji

ndege (Flight Operations). Mitambo ya mafunzo (simulators) itaendelea kuwekwa

kulingana na teknolojia ya kisasa.

(d) Ukuaji wa Sekta

Ukuaji wa idadi ya abiria na huduma za ndege unategemea zaidi ukuaji wa uchumi.

Inakadiriwa kuwa, abiria wataongezeka kutoka abiria 3,027,512 mwaka 2010 hadi

abiria 55,767,238 mwaka 2050 hili likiwa ongezeko la 1,742%. Aidha, safari za ndege

zinategemewa kuongezeka kutoka safari 181,240 hadi safari 3,334,816, likiwa ni

ongezeko la 1,740%, katika kipindi hicho.

10.3.2 Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA)

Mara baada ya Tanganyika kupata uhuru wake tarehe 9 Desemba, 1961, serikali ya

Tanganyika ilirithi miundo ya uendeshaji wa viwanja vya ndege kutoka kwa serikali ya

kikoloni ya Mwingereza. Viwanja vya ndege vilikuwa chini ya „Public Works

Department (PWD)”, muundo ambao uliendelea hadi miaka ya 1970. Muundo huu

ulibadilika mwaka 1970 wakati serikali ilipounda Wizara ya Mawasiliano na Kazi

(Ministry of Communication and Works) na viwanja vya ndege vikaendelea kuwa chini

ya Wizara hii.

Mkurugenzi wa kwanza wa Viwanja vya Ndege aliteuliwa rasmi tarehe 01/07/1974

akiwa chini ya Wizara ya Mawasiliano, Usafirishaji, Nishati na Kazi. Viwanja vya

Ndege viliendelea kuwa ni kitengo tu cha Idara ya Barabara na Viwanja vya Ndege

(Department of Roads and Aerodromes).

Historia ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) inaanzia mwaka 1974

ilipoundwa kama Kitengo chini ya Idara ya Barabara na Viwanja vya Ndege katika

Wizara ya Ujenzi. Mwaka 1980, ikawa Idara kamili chini ya Wizara ya Ujenzi,

Mawasiliano na Uchukuzi. Kati ya mwaka 1980 hadi 1999, Idara hii ilipita katika

miundo kadhaa sambamba na mabadiliko mbalimbali yaliyokuwa yanafanyika katika

Wizara ya Mawasiliano na Wizara ya Ujenzi.

TAA ilianzishwa tarehe 29 Novemba, 1999 na kuzinduliwa rasmi mnamo tarehe 03

Desemba, 1999 chini ya Sheria ya Wakala wa Serikali.

Viwanja vya ndege vilivyorithiwa kutoka kwa utawala wa Mwingereza vilikuwa ni

sabini (70) ikiwa ni pamoja na Kiwanja cha Kimataifa cha Dar es Salaam amabacho

kwa sasa kinajulikana kama Kiwanja Cha Kimataifa cha Julius Nyerere. Baada ya

Uhuru, Serikali ilijenga kiwanja cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA) ambacho

kilifunguliwa mwaka 1971. Hivi sasa, Serikali inakamalisha ujenzi wa Kiwanja cha pili

cha Kimataifa cha Songwe mkoani Mbeya.

Page 66: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

63

Hali ya Viwanja kwa Wakati Huo

Viwanja vya lami vilikuwa kumi na mbili (12) ambavyo ni; Kiwanja cha Ndege cha

Kimataifa cha Dar Es Salaam, Mwanza, Arusha, Mtwara , Tanga, Kigoma, Tabora,

Moshi, Iringa na Musoma. Viwanja vingine vilikuwa vya changarawe na nyasi.

Maelezo ya kila kiwanja ni kama ifuatavyo:

Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Dar Es Salaam (DIA).

Kwa mujibu wa mapokezi ambayo si rahisi kupata maandiko yanayoweza kuthibitisha

usahihi na tarehe zake, Kiwanja cha ndege cha kwanza katika Jiji la Dar es Salaam,

kilikuwa ni cha maji “sea port”. Kiwanja hiki kilikuwa kwenye sehemu ya bahari

iliyopo kati ya Ferry na pwani ya karibu na Kanisa Kuu la Mt. Joseph. Jengo lake la

abiria (Terminal) lilikuwa jirani na Ardhi House. Kiwanja hicho kilianza wakati wa

mkoloni, na kilihamishiwa barabara ya Kilwa karibu na Uwanja wa Taifa kikiitwa

Kiwanja cha Ndege cha Mkeja. .

Kiwanja cha kisasa cha Kimataifa cha Dar es Salaam kilijengwa eneo la Ukonga

mwaka 1954. Jiwe la msingi la kiwanja la Jengo la abiria (Terminal I) liliwekwa na

Right Hon. A.T. Lennox Boyd P.C. MP ambaye alikuwa ni „Secretary of State for

colonies” tarehe 16 Oktoba, 1954. Kiwanja cha ndege cha Mkeja (Kilwa Road)

kilifungwa mwaka 1954, Wakati huo Gavana wa Tanganyika alikuwa ni Sir Edward

Twining.

Kiwanja cha Kimataifa cha Dar es Salaam kiliendeshwa na “East African Airways”

ambalo lilikuwa ni shirika la ndege la Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, na hata

Menejimenti yake ilikuwa chini ya “Station Manager” wa East African Airways.

Wafanyakazi wake, Marshallers, Security, Porters na Cleaners walikuwa chini ya

Station Manager wa East African Airways.

Shughuli za usanifu na ujenzi wa jengo jipya la abiria (Terminal II) la Kiwanja Cha

Ndege cha kimataifa cha Dar es Salaam zilihusisha ujenzi wa majengo ya mnara wa

kuongozea ndege (Control Tower), radar, huduma za hali ya hewa (meteorlogical

services); barabara za kuruka na kutua ndege (runways), njia za viunganishi (taxiways)

na mitambo ya kuongoza ndege (Air Navigational Aids). Jiwe la msingi la kiwanja

hicho liliwekwa na Baba wa Taifa Mwl Julius K. Nyerere tarehe 16 Oktoba, 1982.

Shughuli za usanifu na maandalizi ya ujenzi wa Terminal II ulianza tangu mwaka 1979

na kukamilishwa Oktoba, 1984. Fedha za uwekezaji katika mradi huu zilipatikana

kutoka serikali ya Ufaransa wakati wakandarasi walikuwa ni kampuni ya kifaransa ya

Bouygues na wahandisi washauri walitoka “Airport de Paris”.

Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA)

Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro kilijengwa na Mkandarasi wa

Kiitaliano tangu mwaka 1969 mpaka 1971 chini ya usimamizi wa Idara ya Barabara na

Viwanja vya Ndege. Katika ujenzi huo, mwaka 1969 kazi iliyofanywa ni ya uchoraji na

Page 67: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

64

usanifu wa michoro ya kiwanja. Aidha ujenzi halisi ulianza mwanzoni mwa mwaka

1970.

Mwaka 1998, Serikali iliingia mkataba wa kubinafsisha Kiwanja cha Ndege cha KIA

kwa kampuni ya “Kilimanjaro Airports Development Limited” (KADCO) chini ya

ubinasishaji huo, Serikali ilimiliki asilimia 24 ya hisa katika kampuni hiyo. Wabia

wengine waliokuwa na hisa katika kampuni hiyo ni Mott McDonald asilimia 41.4,

SAIF asilimia 30 na Interconsult asilimia 4.6.

Kutokana na sababu mbalimbali, mwaka 2010 Serikali iliamua kukirudisha Kiwanja

kwa kuvunja Mkataba uliokuwepo na kampuni za Mott McDonald na SAIF.

Kiwanja cha Ndege cha Mwanza

Kiwanja cha Ndege cha Mwanza kilijengwa mwaka 1946 kikiwa kwenye kitongoji cha

Butuja kwa sasa kinajulikana kama Sabasaba kilometa saba (7) kutoka mjini kwenye

barabara ya Makongoro au Airport. Kiwanja hiki kilikuwa kinamilikiwa na kampuni ya

machimbo ya madini ya Mwadui Diamond Mines. Mmiliki wa kiwanja hiki yaani Sir

Williamson alikitumia kiwanja hiki kwa ajili ya kusafirisha almasi kwenda Uingereza

kupitia Nairobi Kenya.

Mwaka 1954 Serikali ya mkoloni ikishirikiana na Sir Williamson waliamua

kukihamisha kiwanja hiki na kujengwa sehemu ijulikanayo kama Kisaka mahali kilipo

sasa.

Serikali ya Tanganyika ilikabidhiwa Kiwanja cha Ndege cha Mwanza mwaka 1961.

Huduma za matengenezo ya kiwanja zilikuwa zikifanywa na Idara ya Ujenzi wakati

huo ikiitwa PWD (Public Works Department). Usafi wa Runway ulifanyika kwa

kutumia ng‟ombe maksai waliokuwa wakikokota fagio la kufagilia runway mara moja

kwa wiki.

Mwaka 1972 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilikipanua kiwanja hiki na

kampuni ya “Mouldad & Rose” ilipewa kandarasi ya kukipanua tena na kukiongezea

urefu kutoka mita 2,000 hadi mita 3,000 ikiwa ni pamoja na kujenga “service road”.

Mradi huu ulisimama mwaka 1978 kutokana na vita kati ya Tanzania na Uganda

(Kagera).

Mwaka 1990 Kiwanja kiliendelea kuboreshwa ambapo majengo kadhaa yalijengwa

kama kituo cha kisasa cha Zimamoto na Uokoaji, msingi wa mnara wa kuongozea

ndege (Control Tower), Ofisi za Hali ya Hewa (MET), upanuzi wa maegesho ya ndege

na ujenzi wa majengo mbalimbali ya ofisi. Miongoni mwa wahandisi waliosimamia

miradi hii ikiwa chini ya Wizara ya Ujenzi ni pamoja na Inj. Prosper F. H. Tesha

Page 68: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

65

ambaye alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa kwanza wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege

baada ya kuundwa mwaka 1999.

Kiwanja cha Ndege cha Mwanza ni miongoni mwa viwanja vikubwa vya ndani (Major

Domestic Airports), ambacho kinahudumia ndege nyingi za ndani na nje ya Tanzania.

Safari nyingi za ndege za abiria ni kati ya Mwanza na Dar es Salaam, Arusha, Bukoba

Kigoma, Geita, Shinyanga Zanzibar, Kilimanjaro na Mpanda. Wakati safari za nje ya

nchi ni Nairobi, Entebbe, Bujumbura, Mombasa, Kisumu na Kigali. Kiwanja hiki kina

barabara ya kurukia ndege ya lami yenye urefu wa kilomita 3.3 na upana wa mita 45,

maegesho ya ndege manne (4) ambayo ni „Terminal apron, Cargo apron, Military apron

na Isolation area‟.

Kiwanja cha Ndege cha Arusha

Kiwanja cha Ndege cha Arusha kilianzishwa mwaka 1954 kama mali ya mtu binafsi

chini ya mzungu aliyekuwa anajulikana kwa jina la Colonel Aggrey, ambaye alikuwa

akimiliki mashamba ya mazao mbalimbali ikiwemo kahawa na ngano. Wakati huo

“runway” ya Kiwanja hiki ilikuwa inatoka Kaskazini kuelekea Kusini, tofauti runway

na iliyopo sasa ambapo „runway‟ inatoka Mashariki kuelekea Magharibi. Kiwanja kipo

kilomita saba (7) Magharibi kutoka katikati ya mji wa Arusha, kikiwa na eneo la hekari

129.96 zenye hati miliki.

Miaka ya 1960 Bwana Aggrey aliamua kumilikisha mali zake zote kwa Serikali, ikiwa

ni pamoja na Kiwanja cha Ndege cha Arusha, ambapo kilikabidhiwa kwa Wizara ya

Kilimo, Idara ya Kilimo Anga, ambapo Serikali ilinunua Ndege ndogo za umwagiliaji

zikawa zinatumika kumwagilia dawa kwenye mashamba ya NAFCO huko Mbulu.

Katikati ya miaka ya 70 alitokea mfanyabiashara aliyekuwa anajulikana kwa jina la

Gerry Hunt, ambaye alinunua ndege chakavu za serikali akazikarabati, na kuzileta

Arusha, akaanza kuziendesha kibiashara kwa kubeba abiria na kuwapeleka sehemu

mbalimbali na hasa kwenye mbuga za wanyama. Miaka ya 1990 mahitaji ya safari za

ndege yaliongezeka na hivyo kuanzisha safari za Dar es Salaam na Zanzibar ambapo

makampuni kadhaa ya ndege za kukodi yakazaliwa na hatimaye kukawa na ndege za

ratiba maalum ikiwa ni pamoja na ndege za ATCL.

Kiwanja cha Ndege cha Mtwara

Kiwanja cha ndege cha Mtwara kilijengwa mwaka 1952/53. Kiwanja hiki ni cha tabaka

la lami na kina barabara mbili za kutua na kuruka ndege (2 runways), moja ni ya nyasi

na nyingine ni ya lami (R/way 01/19 na 08/26). Kiwanja cha ndege cha Mtwara kina

urefu wa mita 2258 na upana wa mita 30 (lami) na “runway” ya nyasi ina urefu wa mita

1158 na upana wa mita 30.

Page 69: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

66

Kiwanja cha ndege cha Mtwara ni miongoni mwa viwanja vikubwa vinavyomilikiwa na

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA). Kiwanja cha ndege kina uwezo wa

kuhudumia ndege zenye uzito wa kilogram 56470 na kinapata ndege 50 kwa mwezi.

Kiwanja cha ndege cha Mtwara kilipata umaarufu sana wakati wa kusafirisha shaba

kutoka Lusaka (Zambia) kuja bandari ya Mtwara ili isafirishwe kuja Dar es Salaam.

Wakati Shirika la Ndege la Afrika Mashariki linafanya kazi, kiwanja cha ndege

kilikuwa kiungo kikubwa kati ya Maputo, visiwa vya Shelisheli na Dar es salaam. Kwa

upande wa Msumbiji (Maputo), kiwanja hiki kilitumika sana wakati wa vita ya harakati

za kupata uhuru wa nchi hiyo.

Kiwanja cha Ndege cha Lake Manyara

Kiwanja cha ndege cha Lake Manyara kilijengwa mwaka 1960 kikiwa mali ya mzungu

aliyejenga hoteli ya kitalii iliyojulikana kwa jina la Lake Manyara. Mzungu huyo

alikuwa anaitwa Dougras na alipewa eneo hilo na wananchi wenyeji.

Barabara ya kiwanja cha ndege cha Lake Manyara ni ya changarawe yenye urefu wa

mita 1221 na upana wa mita 23. Kiwanja hiki kinatumiwa sana na ndege za kitalii

zinazotoka Arusha, Dar es salaam, Zanzibar na Kilimanjaro. Wakati wa Shirika la

Ndege la Afrika Mashariki, Kiwanja hiki kilitumika kwa ajili ya kupokea ndege moja

kwa moja toka nje ya nchi (entry point).

Kiwanja cha Ndege cha Songea

Kiwanja cha ndege cha Songea kilianzishwa na raia wa Uingereza aliyeitwa Robert kwa

matumizi binafsi mwaka 1952. Mwaka 1960 kiwanja kilikabidhiwa kwa serikali

kikiwa cha vumbi. Kati ya mwaka 1974 na 1980 kiwanja hiki kilibadilishwa na kuwa

cha lami, kazi iliyofanywa na Wizara ya Ujenzi chini ya usimamizi wa Mhandisi

Kambona. Kiwanja hiki kina uwezo wa kuhudumia ndege aina ya Fokker 50.

Kiwanja cha Ndege cha Tanga

Kiwanja cha ndege cha Tanga kilijengwa mwaka 1930 na serikali ya kikoloni kwa ajili

ya kurahisisha usafiri wa kwenda kukagua mashamba yao ya mkonge yaliyoko Lugoba,

Amboni, Kogome na Sakura. Kabla ya kujengwa kwa kiwanja hiki, wamiliki hao

walikuwa wanatumia “Air strip” iliyojulikana kama Mnyanjani nje kidogo ya mji wa

Tanga. Kiwanja cha Ndege cha Tanga kilifunguliwa rasmi mwaka 1942 baada ya

kuwekwa tabaka la lami.

Page 70: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

67

Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia Kiwanja cha Ndege cha Tanga, kilitumiwa na

ndege za majeshi ya Waingereza yaliyokuwa yakipigana na majeshi ya Wajerumani.

Hivyo, huduma ya safari za kiraia hazikuwepo kabisa.

Baada ya uhuru wa Tanganyika mwaka 1961, Kiwanja cha Ndege cha Tanga kilipata

umaarufu mkubwa kwani kilikuwa kiungo kati ya Tanzania (Tanganyika), Kenya na

Uganda.Wakati huo kulikuwa na Shirika la Ndege la Afrika Mashariki (EAA)

lililokuwa linafanya safari zake kati ya Nairobi, Mombasa, Dar es Salaam na Zanzibar.

Wakati huo kiwanja cha ndege cha Tanga kilikuwa kinapata ndege hata nyakati za

usiku.

Kiwanja cha Ndege cha Kigoma

Kiwanja cha ndege cha Kigoma kilijengwa na mkoloni (Mwingereza) mwaka 1954.

Baada ya uhuru wa Tanganyika mwaka 1961, kiwanja hiki kiliendeshwa na Idara ya

Kazi (Public Works Department – PWD).

Madhumuni ya kuanzishwa kwa kiwanja hicho wakati wa ukololoni yalikuwa ni

kurahisisha usafiri wa anga kati ya Kigoma na miji mingine ya Tanganyika na

Usafirishaji wa barua, mizigo ya posta na vifurushi.

Mwaka 1982 njia ya kutua/kuruka ndege (runway) pamoja na majengo mawili ya abiria

yalikamilika na hivyo kukifanya kiwanja cha ndege cha Kigoma kutumika kikamilifu.

Barabara ya kuruka na kutua ndege ya Kigoma ina urefu wa mita 1767 na upana wa

mita 30. Aidha kiwanja kina uwezo wa kuhudumia ndege yenye uzito wa tani 21.

Kiwanja cha Ndege cha Dodoma

Kiwanja cha ndege cha Dodoma ni miongoni mwa viwanja vya Mamlaka ya Viwanja

vya Ndege Tanzania ambacho uhudumia zaidi Viongozi wa Kitaifa baada ya Makao

Makuu ya nchi kuhamishiwa Dodoma. Kiwanja hiki kilijengwa mwaka 1948 kikiwa na

urefu wa chini ya mita 100 ulioiwezesha ndege aina ya C. 206 (Cesna 206) kutua na

kuruka na lengo kuu likiwa ni kutoa huduma kwa vile Mkoa wa Dodoma upo katikati

ya Afrika Kusini na Misri.

Mahali panapoegeshwa magari ya Zimamoto (kwa sasa) ndipo kilipokuwa kituo cha

kuongozea ndege (control tower). Waanzilishi wa kiwanja hiki ni kanisa la Angalikana

kwa ajili ya kutoa misaada baada ya vita kuu ya pili ya dunia. Ujenzi wa barabara ya

kiwanja hiki haukujengwa kwa mara moja ulikuwa ukiongezwa kidogo kidogo.

Kiwanja hiki kilipata umaarufu sana mwaka 1974 Serikali ilipoamua kuwa Makao

Makuu ya Chama na Serikali yawe Dodoma. Hivyo kiwanja kiliboreshwa na kuwa na

uwezo wa kupokea ndege yenye uzito wa tani 36 na kina Runway ya lami yenye

Page 71: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

68

urefu wa mita 2042 na upana mita 30. Aidha mwaka 1973-1974, Kiwanja hiki

kiliwekwa tabaka la lami chini ya usimamizi wa Mhandisi Mtetemela akisaidiwa na

Mazengo.

Kiwanja cha Ndege cha Tabora

Kiwanja cha kwanza kujengwa nchini Tanzania (wakati ule Tanganyika) kilikuwa ni

kiwanja cha ndege cha Tabora ambacho kilijengwa mwaka 1939. Kilijengwa wakati

huo kwa ajili ya kuunganisha makoloni ya uingereza kutoka kusini Rhodesia na Kenya

hadi Uingereza. Kiwanja hiki kilitumika sana wakati wa vita kuu ya pili ya dunia (1939

-1945) kwa ajili ya ndege za kivita kutoka Afrika Kusini kwenda Ethiopia kupigana na

Wataliano.

Kiwanja cha Ndege cha Musoma

Kiwanja cha ndege cha Musoma kina barabara ya kutua na kuruka ndege yenye urefu

wa mita 1600 na upana wa mita 33. Kiwanja cha ndege cha Musoma kina hudumia

wastani wa ndege 40 kwa mwezi. Kiwanja hiki kilifunguliwa tarehe 01/01/1950 na

kilitumika zaidi kwa ndege ndogo kwa kuwa wakati huo wa ufunguzi kilikuwa ni

“airstrip”.

Kiwanja cha Ndege cha Lindi

Kiwanja cha ndege cha Lindi kilibuniwa na utawala wa kikoloni wa kiingereza mwaka

1924. Kiwanja hiki kina barabara za kutua/kuruka ndege mbili (2) nazo ni 16/34 yenye

urefu wa mita 1847 na upana wa mita 46.

Mwaka 1933 kiwanja hiki kilianzishwa rasmi kwa ajili ya matumizi ya kijeshi.

Kutokana na kubadilika kwa muelekeo wa upepo mara kwa mara kulisababisha

kujengwa kwa “runway” mbili (2) za kutua/kuruka ndege hivyo kuwa na “runway” sita

(6) za Changarawe. Aidha eneo la maegesho ya ndege (apron) lina uwezo wa kuegesha

ndege tano (5) kwa wakati mmoja zenye uzito wa tani 20.

Kukosekana kwa matengenezo ya mara kwa mara (preventive maintenance) kwa

kipindi kirefu, runway zote zimekuwa za nyasi isipokuwa mita 300 za “Threshold and

Touchdown” ya barabara 04/22 na eneo la maegesho. Kiwanja cha ndege cha Lndi

kilitumika wakati wa vita kuu ya pili ya dunia kikiwa ni kiwanja pekee chenye barabara

nyingi za kutua/kuruka ndege.

Page 72: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

69

Majukumu

Kama ilivyoelezwa katika Tangazo la Gazeti la Serikali la kuunda Mamlaka ya Viwanja

vya Ndege Taanzania (G.N Number 404 la mwaka 1999), chini ya Kifungu cha 3.2 cha

tangazo hilo la Serikali, majukumu ya TAA yameainishwa kama ifuatavyo:-

Kuendesha, kusimamia, kutunza na kuendeleza viwanja vya ndege

vinavyomilikiwa na Serikali.

Kutoa huduma bora na salama katika kuwahudumia abiria, ndege na mizigo pale

usafiri wa anga unapotumika ili kujenga taswira nzuri ya nchi kwa mataifa

mengine duniani.

Kutoa ushauri wa kiufundi kwa Serikali katika masuala yanayohusu uendelezaji

wa viwanja vya ndege.

Kuhakikisha kwamba sera za Serikali, kanuni na taratibu zinazohusiana na

masuala ya viwanja vya ndege yanatekelezwa kwa viwango vya kimataifa.

Kuishauri Serikali katika masuala ya kitaifa na kimataifa yanayohusu

usimamiaji wa viwanja vya ndege pamoja na kanuni, ada na tozo zinazoendana

na utoaji wa huduma hiyo.

Kuunga mkono maendeleo ya kitaifa na kiuchumi kwa kuhakikisha

kunakuwepo miundombinu na huduma muhimu.

Malengo

Sambamba na Kifungu 2.1, malengo mkakati ya TAA ni kama yalivyoainishwa katika

kifungu cha 3.3 cha tangazo hilo la Serikali kama ifuatavyo:

Kupata ziada ya mapato dhidi ya matumizi katika kutekeleza Sera ya Taifa

ya Usafirishaji pamoja na kutekeleza malengo mkakati mengine ya

Mamlaka.

Kuboresha utoaji wa huduma katika viwanja vya ndege kupitia mipango

madhubuti ya kuendeleza na kutunza miundombinu.

Kujenga nguvukazi madhubuti na yenye uwezo kitaaluma kupitia sera na

kanuni husika za utumishi.

Kutekeleza matakwa ya kufuata viwango vya kimataifa vinayohusiana na

masuala ya usalama na mfumo wa habari.

Kuongeza mbinu za upatikanaji wa mapato kwa kuvutia vitega uchumi vya

ziada katika viwanja vya ndege.

Katika utekelezaji wa majukumu yake, TAA kama Wakala wa Serikali inasimamiwa na

Bodi ya Ushauri ya Wizara (Ministerial Advisory Board) ambayo kwa mujibu wa

kifungu cha 3.4 cha Tangazo hilo la Serikali, Bodi hiyo hutakiwa kila mara kufuatilia

na kupima utendaji wa TAA katika masuala ya kuboresha viwango vya huduma

zitolewazo pamoja na masuala mengine ya usimamizi wa kifedha na uendeshaji.

Page 73: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

70

Mafanikio Yaliyopatikana Hadi Sasa

(a) Tangu tulipopata uhuru, Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Dar es Salaam

kiliendelea kukua mwaka hadi mwaka na kuweza kuhudumia abiria laki tano

kwa mwaka (500,000) hadi ilipofika mwaka 1982.

(b) Kutokana na ukuaji huo wa abiria, ililazimu kujengwa kwa Jengo Jipya la

Abiria (Terminal II) lenye uwezo wa kuhudumia hadi abiria wapatao 1,500,000

kwa mwaka. Jengo hilo Jipya lilianza kujengwa mwaka 1979 na kuanza

kutumika mwaka 1984.

(c) Ujenzi wa kiwanja cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA) ulianza mwaka 1969

na kukamilika 1971 kikiwa na uwezo wa kuhudumia hadi abiria 500,000 kwa

mwaka. Kiwanja hiki kilijengwa kwa madhumuni ya kukuza utalii katika Kanda

ya Kaskazini.

(d) Viwanja vingi vilifanyiwa matengenezo ya lami kwenye njia ya kuruka na kutua

ndege (runway & apron) kama vile Mwanza, Kilimanjaro, Dodoma, Iringa,

Songea na Arusha.

(e) Kushirikisha wadau katika umiliki na uendeshaji wa viwanja kwa mfano;

KIA kinaendeshwa na kampuni ya KADCO,

Seronera kinaendeshwa na TANAPA,

Liwale kinaendeshwa na Idara ya Wanyama Pori, Wizara ya Maliasili na

Utalii,

Mbalizi kilikabidhiwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ),

Geita kilikabidhiwa kampuni ya AshantiAnglogold - Mgodi wa Geita,

Morogoro kinaendeshwa na kampuni ya tumbaku ya TTLC,

Sao Hill kinaendeshwa na kampuni ya Mufindi Paper Mills na,

Mkwaja kinaendeshwa na TANAPA.

Changamoto Zilizojitokeza

i. Kuvunjika kwa “East African Airways” ambako kulipelekea viwanja vingi

kukosa ndege baada ya ndege zilizokuwa zinatumika aina ya “Dakota” (DC 3)

kubakia Kenya.

ii. Ndege zilizotumika na ATC aina ya Fokker Friendship (F27) zilikuwa ni chache

na zilihitaji runway ndefu zaidi ya kutua/kuruka, wakati viwanja vingi vya

Page 74: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

71

mikoani na wilayani vilijengwa kwa ajili ya ndege ya Dakota ambayo ilihitaji

runway fupi. Hivyo viwanja vingi vilikosa huduma za ndege.

iii. Kukosekana kwa Kampuni kubwa ya ndege (Strong National Carrier)

kumechangia kiwanja cha JNIA kutokuwa kitovu (hub) cha kuunganishia ndege

kama ilivyokuwa enzi za “East African Airways”.

iv. Uhaba wa mameneja na wahandisi wa viwanja vya ndege ulipelekea usimamizi

wa viwanja kuwa chini ya Regional /District Engineers.

v. Uangalizi mdogo na ukosefu wa hatimiliki, ulipelekea baadhi ya viwanja

kuvamiwa na makazi ya watu (Encroachment). Baadhi ya viwanja vilifungwa

kwa kukosa usalama (mfano Newala na Oldean) kwa vile kulijengwa majengo

kwenye maeneo ya „approach‟ na “runway strips”.

vi. Makampuni ya ndege yalikosa fedha za kigeni kutoka Benki Kuu ya Tanzania

(BOT) kwa mauzo ya tiketi zilizonunuliwa kwa shilingi hapa Tanzania. Hivyo,

Mashirika mengi yalifunga ofisi na safari zao hapa nchini k.m. TRANS

WORLD AIRLINE, SABENA, PAKISTANI, LUFTHANSA, SCANDINAVIA

na mengine mengi.

vii. Mwamko na maandalizi ya kukabiliana na matukio ya kiusalama yalikuwa

madogo sana. Matukio ya utekaji nyara uliofanywa na magaidi wa hapa nchini

yalifanyika mara mbili na kuharibu sifa ya usalama wa viwanja vyetu.

Kukosekana kwa vifaa vya kufanyia kazi hasa upande wa ukaguzi wa abiria na

mizigo, kama mwongozo wa International Civil Aviation Organization (ICAO).

Kazi hii ilifanywa kwa mikono (hand search).

viii. Matukio ya kigaidi ya Septemba 11 nchini Marekani (New York), yalisababisha

kubadilisha mifumo ya usalama kuanzia vifaa vipya, kuajiriwa kwa maafisa

usalama wengi zaidi, mafunzo na taratibu mpya za kukabiliana na matishio

mbalimbali ya ugaidi. Hivyo gharama za uendeshaji ziliongezeka sana na nafasi

za kumbi za abiria zilipunguzwa kwa kufungwa mitambo ya ukaguzi.

ix. Ujenzi wa makazi kwenye maeneo ya viwanja vya ndege ambao unasababisha

ugumu katika juhudi za maendeleo ya upanuzi wa miundombinu mbalimbali

inayohitajika kwa ajili ya uendeshaji wa viwanja,

x. Upungufu wa makandarasi, wahandisi wazalendo kwenye fani ya viwanja vya

ndege.

xi. Kukua na mabadiliko ya kasi katika matumizi ya teknolojia ya usafiri wa anga

duniani ambayo yanahitaji uwezo mkubwa wa uwekezaji katika miundombinu

na huduma za viwanja vya ndege.

Page 75: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

72

Matarajio ya TAA katika Miaka 50 ijayo

Mpango Mkakati wa Uendelezaji wa Viwanja vya ndege katika miaka 50 ijayo na uendeshaji

wa viwanja vya ndege itazingatia yafuatayo:

(a) Viwanja vyote katika majiji na vilivyopakana na nchi jirani, vipanuliwe na

kuboreshwa ili kuwezesha kutua na kuruka ndege aina ya B737 au inayolingana na

hiyo na vitoe huduma masaa 24.

(b) Viwanja vilivyopo mikoani viboreshwe na kupanulia ili viweze kuhudumia Ndege

yenye uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 50 na viweze kutoa huduma masaa 24.

(c) Ushirikishwaji wa Sekta Binafsi /Umma (PPP) katika kuendesha, kuendeleza na

kuboresha miundombinu ya viwanja vya ndege.

(d) Mkakati wa kuufanya Wakala wetu kuwa Mamlaka kamili (Full Authority) tofauti

na ilivyo sasa.

Katika mpango wa Serikali wa “Transport Sector Investment Programme”, (TSIP), viwanja

vya ndege 16 vimepata kipaumbele katika mpango huo wa kitaifa viwanja hivyo ni JNIA,

Arusha, Mwanza, Lake Manyara, Mafia, Mtwara, Tabora, Bukoba, Dodoma, Kigoma, Moshi,

Shinyanga, Musoma, Tanga, Singida, na Songwe. TSIP inatekelezwa kupitia “Medium Term

Expenditure Framework (MTEF).

Katika jitihada za kutekeleza dira, dhima na malengo ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege

Tanzania inatekeleza majukumu yake hayo kwa kutumia Mpango Mkakati wa Kati (wa miaka

3) na Mpango Kazi (wa mwaka 1). Aidha katika utekelezaji wa Mpango kazi, utajumuisha pia

mipango taraji ya kibiashara pamoja na Bajeti ya mwaka husika.

Nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) chini ya mpango huu zimeshaandaa

mpango mkakati na upembuzi yakinifu kwa ajili ya viwanja vya ndege ambayo vinakuza

shughuli za kitalii. Mchakato huo unaendelea kushughulikiwa

10.3.3 Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL)

Shirika la Ndege Tanzania (ATC) lilianzishwa Machi 10, 1977 chini ya sheria ya Mashirika ya

Umma ya mwaka 1969 baada ya kuvunjwa lililokuwa Shirika la Ndege la Afrika Mashariki

ambalo lilikuwa ni ushirikiano wa nchi tatu ambazo ni Tanzania, Kenya na Uganda.

Uendeshaji ulianza rasmi mwezi Juni 1,1977.

Shirika lilianza kutoa huduma kwa kutumia ndege tatu, moja aina za DC-9 na mbili aina ya

Foker Friendships F27.

Serikali ilinunua ndege nyingine aina ya Boeing B737-200 Combi (mbili), Foker Friendships

(mbili) na Twin Otters (nne).

Page 76: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

73

Hadi kufikia mwaka 2002 ATC ilikuwa na ndege moja aina ya B737-200 na nyingine ya

kukodi ya B737-300.

Aidha ATC iliwekeza katika shughuli nyingine za kutoa huduma viwanjani kwa kununua hisa

asilimia 45 za kampuni ya DAHACO -ambayo kwa sasa inaitwa SWISSPORT, asilimia 50 za

kampuni ya Tanzania Airport Catering Company Ltd na asilimia 15 za kampuni ya African

Join Air Services Company.

Kwa sasa shirika la ndege la Tanzania linamilikiwa na Serikali kwa asilimia mia moja. Aidha,

shirika limebaki na ndege mbili aina ya Q-400 dash 8. Ndege moja inafanya kazi na nyingine

ipo kwenye matengenezo.

Makao Makuu ya Shirika la Ndege yako makutano ya barabara ya Ohio na „Garden Avenue‟

Dar es Salaam. Shirika lina „Hangar‟ moja ambayo iko katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa

wa Julius Nyerere.

Ubinafsishwaji wa Shirika la Ndege la Tanzania

Katika kutekeleza Sera ya Serikali ya ubinafsishwaji na ushirikishwaji wa sekta binafsi katika

uendeshaji wa mashirika ya umma ya mwaka 2002, Serikali ilikuwa na asilimia 49 ya hisa zake

kwa Shirika la Ndege la Afika ya Kusini (SAA) na uendeshaji wa shirika hili ulipewa shirika la

Ndege la Afrika ya Kusini. Zoezi la ubinafsishwaji lilipekelekea kuundwa upya kwa Kampuni

ya Ndege ya Tanzania (ATCL).

Baada ya ubinafsishwaji kampuni ilikuwa na haki (rights) za kufanya safari za nje katika miji

ya Entebbe, Nairobi, Kigali, Bujumbura, Kinshasa, Addis Ababa, Harare, Lusaka, Luanda,

Mauritius, Gaborone , London, Mumbai, Rome na mingineyo. Kutokana na uchache wa ndege,

kampuni ilitoa huduma kwenye miji ya Afrika ya Kusini, Entebbe, Nairobi na Visiwa vya

Komoro katika mji ya Hahaya na Afrika ya Kusini katika mji wa Johannesburg, kama

inavyoonyeshwa kwenye jedwali Na.9.7 hapo chini.

Kwa safari za ndani, kampuni ilikuwa na haki ya kutoa huduma katika miji ifuatayo; Kilwa,

Mafia, Pemba, Sumbawanga, Musoma, Shinyanga, Kigoma, Tabora na mingneyo. Kutokana na

uchache wa ndege, kwa Tanzania Kampuni iliweza kuhudumia miji ifuatayo; Mwanza,

Kilimanjaro, Mtwara na Zanzibar.

Kampuni ilitoa huduma kwa kutumia ndege mbili ambazo ni Boeing B737-200 ambayo

ilikuwa mali ya shirika na Boieng B737-300 ambayo ilikodishwa.

Page 77: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

74

Jedwali Na 9.7: Safari za Ndege mbili Boeing 737 kwa mwaka 2002

Na Njia Kupitia Miruko kwa Wiki

1 DAR/JRO/DAR DCT 7

2 DAR/MWZ/DAR DCT 7

3 DAR/MYW/DAR DCT 3

4 DAR/JNB/DAR DCT 3

5 DAR/NBO/DAR DCT 3

6 DAR/EBB/DAR JRO 3

7 DAR/ZNZ/DAR DCT 7

Ili kuhakikisha kampuni mpya ya ATCL inafanikiwa katika uendeshaji wake, Serikali ya

Tanzania ilichukua madeni yote yaliyokuwa ya ATC. Kampuni mpya ya ATCL ilianza bila

madeni kwenye mizania yake. Serikali ilianzisha shirika jingine lililosimamia madeni na mali

ambazo zilikuwa hazihusiki mojamoja kwa uendeshaji wa shirika jipya.

Nia ya Serikali ilikuwa ni kuifanya kampuni ya ndege kuwa imara na kutoa huduma bora za

ndani na nje ya nchi. Hata hivyo, baada ubinafsishaji na uundwaji mpya, kampuni ilishindwa

kukua na kuanza kujiendesha kwa hasara. Hali hii ileta mzigo wa madeni kwa ATCL na

Serikali iliamua kuvunja ubia kati ATCL na SAA mwaka 2006 kwa kununua hisa asilimia 49

zilizokuwa zinamilikiwa na SAA.

Baada ya kuvunjika kwa ubia, Serikali iliendelea na mikakati ya kuifufua kampuni hiyo.

Mikakati hiyo iliwezesha kampuni kuanza kutoa huduma zake mwanzoni mwa mwezi

Novemba, 2011.

10.3.4 Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA)

Historia ya Wakala wa Ndege za Serikali

Kabla ya Uhuru wa Tanganyika, kulikuwa na Kitengo cha Ndege za Serikali chenye Historia

ndefu. Kitengo hiki kilianzishwa mwaka 1930 kama kitengo maalum cha Jeshi la Anga la

Kifalme (R.A.F) kikiwa na jukumu la kupima ramani na kuwasafirisha viongozi wa kikoloni

waliopewa dhamana ya kutawala na kuendesha Tanganyika. Baada ya vita vya pili vya dunia,

Serikali ya kikoloni iliunda Kitengo cha Kiraia na kukipangia majukumu hayo hayo. Kitengo

hicho kipya kiliendelea kutumia marubani na mafundi wa jeshi walioachishwa kazi

kukiendesha.

Mwishoni mwa miaka 1960 shughuli za upimaji ramani kwa ndege ulisitishwa hivyo kufanya

Kitengo kuwa cha Usafiri wa ndege wa Serikali (TGFU) chini ya Wizara ya Mawasiliano na

Uchukuzi. Kitengo hicho kilipewa Marubani na mafundi wazalendo kutoka Jeshi la Wananchi

ambao waliongezeka kadiri walivyoendelea kupatikana.

Mwaka 1974, Serikali ilinunua ndege moja kubwa aina ya HS 748 na mbili ndogo za kisasa

aina ya Beechcraft King Air 100 na kuongeza ufanisi wa huduma kwa Serikali na chama.

Aidha, 1978 Serikali iliongeza ndege moja kubwa aina ya Jet, Fokker 28 iliyokiwezesha

kitengo hiki kuendelea kutoa huduma kwenda popote barani Afrika na Ulaya. Ndege hii ndio

Page 78: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

75

iliyowahudumia Marais wote wastaafu yaani Rais wa kwanza wa Tanzania Hayati Baba wa

Taifa, Mwl. Julius K. Nyerere, Mhe. Ali Hassani Mwinyi Rais wa awamu ya pili wa Tanzania

na Mhe. Benjamin William Mkapa, Rais wa awamu ya Tatu wa Tanzania. Ndege hii pia

inamhudumia Rais wa awamu ya nne wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete. Ndege

mbili(2) aina ya Beechcraft King Air 100 ziliuzwa mwaka 1984 na kununuliwa ndege

nyingine mbili (2) aina ya Aero Turbo Commander 690 ambazo hazikukaa sana kwani zote

mbili ziliuzwa. Mwaka 1992 Serikali ilinunua ndege nyingine aina ya Fokker 50 kuwa mbadala

wa HS 748. Ndege hii ina uwezo wa kubeba abiria 50 na kutua viwanja hata vya udongo. Ni

chombo kinachosaidia sana kutoa huduma ya ndege kwa Rais pamoja na viongozi wakuu wa

Serikali. Kwa miaka mingi tegemeo la Serikali la Usafiri wa Anga limekuwa ni vyombo hivi

viwili tu Fokker 28 na Fokker 50.

Mwaka 2004 Serikali ilinunua ndege mpya ya kisasa aina ya Gulfstream G550. Ndege hii ina

uwezo wa kuruka dunia nzima, inasaidia kusafirisha viongozi wakuu wa kitaifa masafa marefu

popote ulimwenguni kwa usalama wa hali ya juu na kwa gharama nafuu zaidi. Aidha pia kuna

ndege ndogo ya watu 7 aina ya PA 31, Navajo tuliyoirithi kutoka TCAA.

Kuanzishwa kwa Wakala wa Ndege za Serikali

Wakala wa Ndege za Serikali ni Wakala chini ya Sheria ya Wakala namba 30 ya mwaka 1997,

ulianzishwa tarehe 17 Mei, 2002 ili kusafirisha Viongozi Wakuu wa nchi pamoja na Viongozi

wengine wa Serikali.

Wakala una wajibu wa:

i. Kutoa huduma ya Usafiri wa Anga kwa Viongozi Wakuu wa Kitaifa na wageni wa

Kitaifa.

ii. Kutunza, kuongeza na kuendesha vyombo kwa kiwango cha Kimataifa

iii. Kuboresha Menejimenti ya Wakala.

Katika kutekeleza wajibu wake, Wakala una majukumu ya:

i. Kumhudumia Mhe Rais, Viongozi Wakuu wa Kitaifa na wageni mashuhuri wa Taifa

letu.

ii. Kuhakikisha kuwa vyombo hivyo (ndege na karakana) vinatunzwa pamoja na

kutengenezwa kwa kiwango cha juu cha Kimataifa.

iii. Kuendesha vyombo hivi kwa kuzingatia Sheria na viwango vinavyokubalika Kimataifa.

iv. Kuendelea na uboreshaji wa Menejimenti ya Wakala wa nia ya kuongeza ufanisi katika

kutoa huduma.

v. Kushauri Serikali juu ya vyombo hivi kila mara inapohitajika.

Mafanikio

Page 79: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

76

i. Wakala umeweza kuendelea kutoa huduma kwa Viongozi Wakuu wa Kitaifa na

Serikali.

ii. Kuhakikisha uzima wa ndege zote nne (4).

iii. Kuweza kusimamia matengenezo ya ndege zote nne (4), matengenezo makubwa na ya

kawaida.

iv. Wakala umeweza kuwapeleka watumishi kwenye mafunzo kulingana na taaluma zao ili

kuboresha utendaji wa kazi.

Matarajio ya Wakala

i. Kununua ndege kubwa moja na helikopta kwa ajili ya Viongozi Wakuu wa

Kitaifa.

ii. Kudumisha na kuboresha usalama na ubora wa huduma zetu kwa kufuata

taratibu zilizopo kwenye mkataba wa huduma kwa mteja.

iii. Kuendelea kuboresha mazingira ya kufanyia kazi yakiwemo maslahi ya

watumishi kulingana na uwezo wa Mamlaka.

iv. Matumizi mazuri ya rasilimali zilizopo, watu, teknolojia ya kisasa, mbinu za

kisasa na fursa mbalimbali ili kujiletea maendeleo ya haraka.

v. Kufanya ukarabati mkubwa wa karakana ya Ndege za Serikali pamoja na ofisi

ili ndege zote ziwe zinaegeshwa humo kwa usalama zaidi.

vi. Kuendelea kuelimisha umma wa Tanzania kuhusu wajibu na majukumu ya

Wakala ili wananchi wapate kufahamu Wakala wa Ndege za Serikali.

vii. Ununuzi wa vyombo vya ukarabati wa majengo na vifaa na uboreshaji wa

nyenzo za kufanyia kazi.

viii. Kuendelea kuwapa watumishi mafunzo mbalimbali kwa lengo la kuboresha

utoaji wa huduma ili kwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia duniani.

ix. Kuendelea kulinda mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka tisa na

kukamilisha malengo ambayo Mamlaka imejipangia.

x. Kuboresha ukusanyaji wa mapato, pamoja na kuimarisha nidhamu ya matumizi

ya fedha.

xi. Kuendeleza mapambano na maambukizi ya ukimwi kwa watumishi wa Wakala.

10.4 VYUO VYA MAFUNZO CHINI YA WIZARA

10.4.1 Chuo Cha Bahari Dar Es Salaam (DMI)

Chuo cha Bahari (DMI) kina wajibu wa kutoa elimu na mafunzo ya mambo

yanayohusiana na shughuli za bahari (Maritime Sector). Chuo hiki kilianzishwa kwa

Page 80: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

77

sheria ya Bunge Na.22 ya mwaka 1991 (Act No 22 of 1991). Hata hivyo historia ya

DMI inakwenda nyuma zaidi hadi tarehe 3 July 1978 ilipokuwa ni kitengo kidogo

kilichojulikana kama DMTU kilichoanzishwa kwa lengo la kukidhi mahitaji ya

mabaharia kulingana na mahitaji ya Kampuni ya Meli Mwambao Tanzania

(TACOSHILI) wakati huo.

DMI ina ithibati (Accreditation) ya ‟National Council for Technical Education

(NACTE), „Association of Business Managers and Administrators‟ (ABMA-UK) na

„Chartered Institute of Logistics and Transport‟ (CILT-UK).

Chuo kinatambuliwa na Mamlaka na Taasisi mbalimbali kama SUMATRA, Wizara ya

Uchukuzi, Kampuni ya Ukaguzi ya Det Norske Veritas (DNV) ya Norway. Vilevile

DMI ina uhusiano wa kitaalam katika masuala ya usalama baharini na Kampuni ya

„Viking-Liferafts AS‟ ya Dernmark na Kampuni ya Jotron AS ya Norway. Pia chuo

kina uhusiano wa kitaaluma na:

i. Chuo Kikuu cha Aaresund-Norway - AUC

ii. Chuo Kikuu cha Dalian cha China - DMU

iii. Chuo Kikuu cha Bahari Shanghai cha China - SMU

iv. Chuo Kikuu Kishiriki cha Hangesund cha Norway -HUC

v. Taasisi ya Bahari na Uvuvi ya Namibia - NAMFI

Kufuatia kiwango cha ubora wa elimu inayotolewa na Chuo hiki kutambuliwa

kimataifa, udahili wa wanafunzi kutoka ndani na nje ya nchi kama Comoro, Namibia,

Uganda na Kenya(taja) umeongezeka sana baada ya Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania kuingia kwenye orodha ya ubora (White list) ya Shirika la Kimataifa

linalosimamia shughuli za Bahari duniani (IMO ) mwaka 2003.

Tanzania inatekeleza kikamilifu mkataba wa kimataifa wa mafunzo ya Mabaharia wa

mwaka 1978 kama ulivyorejewa mwaka 1995 (STCW 78 as amended in 1995).

Utekelezaji huo unawapa nafasi wahitimu wa DMI kufanya kazi nje na ndani ya nchi na

hivyo kuongeza uwezo wa Serikali katika mikakati yake ya kuongeza ajira.

Vilevile Chuo kimeweza kuanzisha mfumo wa viwango vya ubora (Quality Standards

System) na kukaguliwa na Shirika la Kimataifa katika ukaguzi wa ubora katika mambo

ya bahari na kutunukiwa hati ya ubora ya ISO- 9001/2000 na Shirika la Kimataifa la

Det Norske Veritas (DNV).

Majukumu ya Chuo cha Bahari Dar es Salaam

Majukumu ya Chuo cha Bahari Dar es Salaam ni kutayarisha wataalamu katika Nyanja

mbalimbali ili kusimamia na kuendesha sekta ya bahari. Chuo kinatoa Wataalamu kwa

gharama nafuu na kwa idadi kubwa ikilinganishwa na gharama ya kusomesha

wataalamu hao nje ya nchi. Kozi zinazotolewa na chuo hiki ni:

Page 81: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

78

Ukarabati wa meli ( Ship Repair)

Kuendesha meli

Kuendesha shughuli za bandari na container terminal

Mafunzo kwa Watendaji wa Hifadhi za wanyama pori

Mafunzo kwa Watendaji wa Uvunaji maliasili baharini

Mafunzo kwa Waratibu usafirishaji shehena na huduma za meli (Freight

Forwarders, Shipping agents na ships handlers)

Chuo pia kinatoa mafunzo Maalumu kwa taasisi za Jeshi la Wananchi, Polisi na

Uvuvi.

Uongozi na Utawala wa Chuo

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 1978, Chuo cha Bahari Dar es Salaam kimepitia utawala wa

wakuu mbalimbali. Kama inavyoelezea historia ya chuo, chuo kilianzishwa kwa msaada wa

Serikali ya Norway, na mkuu wa Chuo wa kwanza alikuwa ni raia kutoka nchi ya Norway

(Ona Jedwali Na. 9.8).

Baada ya kuanzishwa mwaka 1991 na kutambuliwa rasmi kama chuo cha Bahari (DMI),

uongozi wa chuo ulisimamiwa na bodi ya kwanza iliyoundwa mwaka 1992, chini ya

Mwenyekiti Mr.Peter Mtandu. Kikianzishwa kama sehemu ya iliyokuwa Kampuni ya Meli ya

Mwambao (TACOSHILI), na chuo kilikuwa na Idara mbili:

i. Idara ya Usafirishaji wa Majini

ii. Idara ya Uhandisi na Teknolojia.

Mbali ya kuwa kila moja ya Idara hizi ilikuwa inaongozwa na kiongozi wake (Course Leader),

pia Idara hizi zilikuwa katika maeneo tofauti ambapo idara ya Usafirishaji wa Majini ilikuwa

ipo Ubungo katika majengo ya Chuo Cha Usafirishaji (NIT) na Idara ya Uhandisi na

Teknolojia ikiwa katika eneo la TACOSHILI.

Mwaka 1989 Idara ya Usafirishaji ilihamishwa kutoka Ubungo na kuja katika jengo la

TACOSHILI na kuziweka Idara zote katika jengo moja. Mwaka 1991, Chuo kilihamia katika

jengo lililokuwa linatumiwa na kitengo cha Ugavi (Supplies Department) cha Mamlaka ya

Usimamizi wa Bandari ya Tanzania.

Jedwali Na 9.8: Wakuu waliokiongoza chuo kuanzia mwaka 1988.

Jina la Mkuu wa Chuo Kuanzia

Mwaka

Mpaka

Mwaka

Uraia wa Mkuu wa

Chuo

1. Capt. Peder Solem 1988 1992 Mnorway

2. Capt Tim Harris 1992 1994 Mwingereza

3. Mr. Nil Nes 1994 1995 Mnorway

Page 82: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

79

4. Mr. Fabian Ninalwo 1995 2000 Mtanzania

5. Mhandisi Thomas J.Mayagilo 2000 2009 Mtanzania

6. Capt S.A. Mkali 2010 Hadi sasa Mtanzania

Udahili wa wanafunzi

Kozi ndefu, kozi za ujuzi na za jioni

Idadi ya wanafunzi waliodahiliwa katika Chuo cha Bahari chuoni imekuwa ikiongezeka kila

mwaka. Udahili wa wanafunzi wa kozi ndefu umekuwa ukiongezeka hasa baada ya wanafunzi

wa Stashahada ya Juu kupata udhamini wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa elimu ya juu. Pia

udahili wa wanafunzi wa kozi za jioni umekuwa ukiongezeka kila mwaka kama

unavyooneshwa katika Chati ifuatayo.

Page 83: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

80

DMI ilidahili wanafunzi wa kozi ndefu wapatao 428 mwaka 2009/2010 na wanafunzi 480

mwaka 2010/2011. Udahili huu unaonesha kuwa wanafunzi wamekuwa wakiongezeka kila

mwaka, hali inayoashiria hitaji la kuwa na vyumba vya madarasa, vifaa vya kufundishia na

rasilimali watu ili kuendana na ongezeko hilo.

Kozi fupi

Ili kuzuia kutokea kwa ajali za meli zinazoweza kusababisha hasara kubwa, Chuo kinaendesha

kozi fupi ili kuwawezesha wafanyakazi melini na katika bandari kujikinga na kuchukua hatua

za tahadhari pindi ajali zinapotokea.

Chati 2: Udahili wa wanafunzi wa kozi mbalimbli

Page 84: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

81

Kumekuwa na ongezeko la wanafunzi waliodahiliwa takribani kila mwaka ukiacha mbali

upungufu uliojiotokeza mwaka 2009/2010

Wahitimu

Katika kipindi cha mwaka 2006 hadi 2010 Chuo kimedahili wanafunzi 1,540 wa kozi ndefu na

wanafunzi 25,051 wa kozi fupi. Jumla ya wanafunzi waliodahiriwa ni 26,591.

Jedwali Na: 9.9 Kuonyesha Idadi ya Wahitimu wa Kozi ndefu kuanzia mwaka 1986 – 2006

Nchi Idadi ya Wahitimu

Watanzania 379

Wamalawi 8

Waganda 12

Wacomoro 1

Jumla 400

Jedwali Na. 9.10: Kuonyesha Idadi ya Wahitimu wa Kozi ndefu kuanzia mwaka 2006 –

2010

Nchi Idadi ya Wahitimu

Watanzania 1485

Wakenya 71

Waganda 22

Chati 3: Udahili wa wanafunzi wa kozi fupi

Page 85: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

82

Wacomoro 40

Wanamibia 2

Jumla 1620

Huduma na Ushauri wa kitaalamu

Katika kipindi cha mwaka 2006 hadi 2010 meli 54 zimefanyiwa ukaguzi, Meli 1

imetathiminiwa ili kujua thamani yake, na uchunguzi wa matukio ya ajali kwa vyombo vya

majini ulifanyika katika meli 2. Kupitia kituo cha Liferaft (servicing of life-saving appliances)

kinachoshughulika na vifaa vya kujiokolea, jumla ya vifaa vya kujiokolea 589 vimefanyiwa

ukarabati mdogo na mkubwa, vilevile vifaa vya zima moto vipatavyo 1,049 vimehudumiwa.

Changamoto

i. Kuboresha miundombinu

ii. Kusomesha Wakufunzi kwa ngazi ya Shahada ya uzamili na Shahada ya udaktari

iii. Kufanya tafiti katika sekta ya bahari

iv. Kuandaa na kupitia upya mitaala ya kozi mbalimbali kulingana na mahitaji ya soko.

Kuanzisha kozi za Shahada ya Kwanza

Uchumi endelevu wa taifa lolote lile hutegemea elimu na ujuzi walionao watu wake pamoja na

nyenzo za kufanyia kazi. Kwa kuzingatia umuhimu huo wa rasilimali watu, Chuo kupitia

uhusiano wetu kitaaluma na Chuo Kikuu cha Dalian – China tumekubaliana tuanze na kozi

moja ngazi ya shahada ya kwanza ili kupata kada ya wahitimu ambao wataweza kuchangia

katika kuendeleza Sekta. Kozi hiyo ni Port and Logistics Management.

Chuo pia kimeandaa mitaala ambayo imeshapita NACTE (National Council for Technical

Education) kwa kuhakikiwa na kupata ithibati. Mitaala hiyo ni katika ngazi ya Shahada ya

kwanza ( Degree):

i. Marine Engineering Technology

ii. Nautical Science (Maritime Transport Management)

Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi

Chuo cha bahari Dar es Salaam (DMI) kinayo fursa kubwa katika kutoa kozi mbalimbali

zinazopatikana katika ukanda wa bahari kama utafutaji na uchumbaji wa mafuta na gesi.

Page 86: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

83

Taaluma hii mpaka sasa haitolewi hapa nchini japokuwa Tanzania ina rasilimali hiyo ya mafuta

na gesi. DMI kwa kushirikiana na International Marine Institute of Memorial University (MI)

cha Canada inaweza kuendesha kozi fupi na ndefu zinazohusiana na utafutaji na uchimbaji wa

mafuta (Petroleum Technology) hapa nchini baada ya kusaini makubaliano (MoU). Mafunzo

hayo yatatoa mwanya wa kuwa na wataalam katika maeneo yafuatayo:-

i. Dynamic positioning

ii. Anchor handling

iii. Off-shore safety

Taaluma hii itapunguza utegemezi wa wataalam kutoka nje ya nchi na pia kuepuka kusomesha

wataalamu nje ya nchi kwa gharama kubwa. Kwa taarifa, sehemu ya mazungumzo ya suala hili

ilifanyika hapa nchini wakati ndugu Glenn Blackwood ambaye ni Mkurugenzi na Mkuu wa

Chuo Kikuu cha MI (Executive Director and CEO) na ndugu Bill Chislett ambaye ni

Mkurugenzi wakati walipotembelea DMI na kupendekeza DMI itembelee Canada ili kuona na

kukamilisha ushirikiano huo wa kitaaluma.

Kuanzisha Mafunzo ya Cadetship

Kozi hii inaanzishwa mwaka huu (2011/2012) ili kuweza kupata wanafunzi watakaoingia

katika kozi za shahada ya kwanza. Wanafunzi hawa watakapohitimu watakuwa na sifa

zinazohitajika katika soko la ajira katika sekta ya bahari. Sekta hii ya bahari, kwa taarifa ya

IMO litakuwa na uhaba wa mabaharia wapatao 83,900 ifikapo 2012. Hivyo DMI inayo nia ya

dhati na mipango madhubuti katika kuhakikisha kwamba wahitimu wake wanafaidika na fursa

hii kwa kujaza nafasi hizo za ajira, kitaifa na kimataifa.

Matarajio ya Miaka 50 Ijayo

Kwa sababu ya kukua kwa Sayansi na Teknolojia, Chuo kimejipanga kutoa programu ambazo

zinakidhi mahitaji ya nchi na yale ya kimataifa. Chuo pia kinatarajia kufundisha Shahada

(Degree) katika maeneo yafuatayo:-

i. Maritime Economics and Management,

ii. Port and Shipping Administration,

iii. Naval Architecture and Shipbuilding,

iv. Marine Electronics and Electro-technology,

v. Maritime Law.

vi. Computer Science

Matarajio ya Chuo kwa miaka 50 ijayo yamegawanyika katika maeneo mbalimbali. Katika

orodha ya matarajio ya chuo katika kipindi cha miaka 50 kuanzia sasa, chuo kinakusudia

Page 87: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

84

kuongeza idadi ya wanafunzi kuweza kufikia wanafunzi 10,000 kwa mwaka. Sambamba na

hilo, chuo kinakusudia kupanua miundombinu itakayofanikisha azma hiyo.

Chuo kinakusudia katika kipindi hicho kuzitumia eka 500 za ardhi ambazo zimepatikana

katika maeneo ya Mkuranga kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya kisasa ikiwa ni pamoja

na mabweni, maabara, uwanja wa michezo wa kisasa utakaoweza kuingizia chuo mapato.

Ongezeko la idadi ya wanafunzi litaambatana na kuongeza Kitivo na idara ili kukidhi

mahitaji ya idadi hiyo kubwa ya wanafunzi.

Chuo kinakusudia kukuza ushirikiano uliopo na makampuni na taasisi mbalimbali na pia

kupanua wigo wa ushirikiano na makampuni zaidi. Matarajio zaidi yanalenga kufanikisha

Chuo kuwa na hadhi ya Chuo kikuu kamili.

10.4.2 Chuo Cha Usafirishaji (NIT)

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kilianzishwa rasmi mwaka 1975 kama Idara ya Serikali

chini ya Shirika la Taifa la Uchukuzi kwa madhumuni ya kutoa mafunzo katika Sekta ya

Usafirishaji na Uchukuzi. Mwaka 1982, Chuo kilipanda hadhi na kuwa Chuo cha Elimu ya

Juu chini ya sheria ya Bunge Na.24 ya mwaka 1982 (The National Institute of Transport

Act No.24 ya 1982). Kwa sheria hiyo, Chuo kilipewa uwezo kamili wa kisheria na

madaraka ya kuendesha shughuli zake ikiwa ni pamoja na kutoa elimu na mafunzo,

kufanya tafiti na elekezi katika fani mbalimbali za Usafirishaji, Uchukuzi na Mawasiliano

chini ya Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi.

Mafanikio Yaliyopatikana

Katika kipindi cha Miaka 50 ya Uhuru, Chuo katika kutekeleza mipango na mikakati yake

kimeweza kupata mafanikio yafuatayo:

Ithibati na “Chartered Institute of Logistics and Transport ( CILT International –

UK)”

Mwaka 2006/2007, Chuo kilipata ithibati “Chartered Institute of Logistics and Transport”

ya Uingereza na kuweza kufundisha na kudahili kozi za kimataifa za uchukuzi na

usafirishaji kuanzia ngazi ya Astashahada hadi Stashahada ya Juu. Hii imekiwezesha chuo

kuweza kutambulika kimataifa.

Ithibati na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE)

Katika mwaka 2008/2009, Chuo kimepata ithibati (accreditation) kamili kutoka Baraza la

Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) katika ngazi ya Nane (NTA level 8) - ya Muundo wa

Tuzo (Awards) hilo. Hii imekiwezesha Chuo kuanza kutoa taaluma katika ngazi ya

Page 88: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

85

Shahada ya kwanza (Degree) na kufuta rasmi utoaji wa taaluma katika ngazi ya Stashahada

ya Juu ikilinganishwa na kutoa taaluma katika ngazi ya Stashahada ya Juu mara tu

kilipoanzishwa.

Kutoa Mafunzo Katika Mfumo wa Ufanisi Competence Based Education and

Training (CBET)

Chuo kimeweza kutoa mafunzo ya ufanisi „Competence Based Education and Training

(CBET)‟ hadi shahada ya kwanza (NTA level 8). Hii imekiwezesha Chuo kutoa wahitimu

ambao watakidhi soko la ajira.

Ongezeko la Programu na wadahili wa Kozi ndefu

Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) kimeweza kuongeza programu zake kutoka kozi

ndefu mbili (2) ambazo zilikuwa Stashahada ya Juu Uongozi katika Usafirishaji na

Stashahada ya Kawaida ya Uhandisi Magari mwaka 1975/76 hadi kufikia programu tisa (9)

kwa mwaka 2010/11 ambazo ni; Shahada ya Lojistiki na Menejimenti ya Usafirishaji,

Shahada ya Upokeaji na upelekaji Shehena, Shahada ya Uhandisi Magari, Stashahada ya

Kawaida ya Upokeaji na Upelekaji Shehena, Stashahada ya kawaida ya Uhandisi Magari,

Stashahada ya Kawaida ya Lojistiki na Menejimenti ya Usafirishaji, Stashahada ya

Kimataifa ya Lojistiki na Ushafirishaji, Stashahada ya Teknolojia ya Habari na

Mawasiliano na Astashahada ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.

Kutokana na kuongezeka kwa programu, idadi ya wanafunzi waliodahili kozi ndefu

iliongezeka kutoka wanafunzi 32 mwaka 1975/76 hadi kufikia wanafunzi 288 katika

mwaka 2010/11 ambapo ni ongezeko la wanafunzi 256. Aidha, chuo kimeweza kuongeza

idadi ya wanafunzi wa kozi mbali mbali kutoka wanafunzi 32 mwaka 1975/76 hadi kufikia

wanafunzi 585 katika mwaka 2010/11. Hili ni ongezeko la wanafunzi 553.

Ongezeko la Programu za Kozi Fupi za Udereva na Ukaguzi Magari.

Chuo kimeendelea kuendesha kozi fupi za kuanzia siku moja hadi miezi sita. Mwaka

1975/76, Chuo kilikuwa na kozi fupi tatu ambapo zimeongezeka hadi kufikia kozi fupi 14

mwaka 2010/11 ambazo ni ; Udereva Mahiri Daraja la Kwanza, Udereva Mahiri Daraja la

Pili, Udereva wa Magari ya Viongozi, Udereva wa Magari ya Abiria, Udereva wa

Kujihami, Udereva wa Magari ya Mizigo, Udereva Mwandamizi, Maafisa Usafirishaji,

Ualimu wa Madereva, Udereva wa Pikipiki, Semina kwa Askari wa Usalama Barabarani

Tanzania Bara na Visiwani, Mfumo wa Udhibiti wa Menejimenti ya Usafirishaji,

Utengenezaji wa Injini za Dizeli na Ukaguzi wa Magari na Utahini wa Madereva.

Katika kipindi hicho zaidi ya washiriki 23,333 walishiriki katika kozi mbali mbali za

udereva na ukaguzi wa magari.

Ongezeko la Miundombinu

Wakati kilipoanzishwa chuo kilikuwa na jengo moja la Utawala ambalo lina madarasa nane

(8), ofisi za watumishi kumi na moja (11) pamoja maktaba yenye uwezo wa kuchukua

wanafunzi 56 kwa wakati mmoja. Vile vile chuo kilikuwa na mabweni mawili (2) yenye

Page 89: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

86

uwezo wa kuchukua wanafunzi 300 tu . Katika kipindi hiki, Chuo kimeweza kuongeza

madarasa saba (7) na ofisi za watumishi ishirini na moja (21). Katika hatua nyingine ya

kuongeza miundombinu ya chuo, mwaka wa 2007/2008, Chuo kilianza rasmi

ujenzi wa kituo cha rasilimali mafunzo na jengo la ghorofa sita(6) lenye uwezo wa

kuchukua wanafunzi mia tano (500) kwa wakati. Jengo hilo litakuwa na maktaba ya kisasa,

maabara za kompyuta, kumbi za mihadhara na mikutano, madarasa, ofisi za watumishi,

maabara za modeli za kufundishia, kitengo cha maandiko, machapisho na kurudufu.

Ushirikiano na Vyuo Vingine

Chuo kimeendelea kuimarisha ushirikiano na vyuo vingine kama vile Chuo Kikuu cha

“Leeds Metropolitan” cha Uingereza (Ushirikiano ulianza mwaka 2004). Vyuo vingine ni

pamoja na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Vyuo

vingine vya Elimu ya Juu vilivyopo hapa nchini. Vyuo na mashirika mengine ya nje ni

pamoja na kuingia makubaliano na ''Berlin University of Technology '' ya Ujerumani,

''International Supply Chain Management Consultant'' ''TRANSAID” vya Uingereza na

''Nigeria Institute of Transport Technology''.

Ongezeko la Vifaa vya Kufundishia

Chuo kimeweza kuongeza vifaa vya kufundishia kama vitabu rejea katika maktaba kufikia

10,000, magari ya kufundishia - “Bus” aina ya Marcopolo – Scania lenye uwezo wa kubeba

abiria 59 kwa ajili ya mafunzo ya madereva wa magari ya abiria, Basi aina ya TATA, vifaa

vya Karakana na kompyuta 71 pamoja na ''Digital Projector'' saba (7).

Kufanya Tafiti na kutoa Ushauri Elekezi

Chuo kimeendelea kufanya tafiti na elekezi mbali mbali katika sekta ya usafirishaji,

uchukuzi na nyinginezo. Jumla ya tafiti 20 na elekezi 18 zimefanyika ambazo zimetoa

ufumbuzi na ushauri katika Serikali, Mashirika na jamii kwa ujumla.

Ongezeko la Utumiaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano

Chuo kimeongeza utumiaji wa teknolojia ya habari na mawasiliano katika kufundishia na

utendaji kazi. Kwa sasa Chuo kina maabara tatu (3) za kompyuta na kupata “Software” kwa

ajili ya utunzaji wa taarifa za wanafunzi inayoitwa “Students Academic Records

Information System” (SARIS).

Changamoto

Pamoja na mafanikio makubwa ambayo Chuo kimeyapata tangu kupatikana kwa uhuru,

Chuo kimepata changamoto nyingi ambazo zimeathiri utekelezaji wa majukumu ya msingi

kwa ufanisi. Changamoto hizo ni pamoja na:-

a. Vifaa Vya Kufundishia

Page 90: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

87

Chuo kinakabiliwa na upungufu wa vifaa vya kufundishia ikizingatiwa kuwa

chuo kinatoa mafunzo ya ufanisi '' Competence Based Education'' ambayo

yanaenda sanjari na vitendo. Vifaa hivi ni pamoja na vitabu vya rejea kwa ajili

ya maktaba, magari ya kufundishia, vifaa vya karakana, 'Simulators', 'training

models', barabara za mafunzo n.k.

b. Miundombinu

Kwa ujumla hali ya miundombinu ya madarasa, ofisi za wahadhili, watumishi,

mabweni, uzio wa kuzungukia chuo na barabara za ndani si ya kuridhisha na

hivyo kuleta changamoto katika ufundishaji.

c. Tatizo la Umeme

Chuo kinakabiliwa na tatizo la umeme ambao husababishwa na umeme mdogo

(Low Voltage). Tatizo hili linatokana na kupanuka kwa chuo na ongezeko la

matumizi ya umeme.

d. Tatizo la Maji

Chuo kinakabiliwa na tatizo kubwa la maji ambalo husababisha upungufu wa

maji katika matumizi ya chuo. Hii inatokana na upungufu wa maji kutoka

DAWASCO na kisima kilichokuwepo kuchakaa.

Matarajio ya Chuo kwa Miaka 50 Ijayo

Kuendelea na utoaji wa mafunzo bora ya taaluma za lojistiki, upokeaji na

uondoshaji mizigo, usafirishaji, ufundi na mawasiliano kwa ukanda wa Afrika

Mashariki, Kati na dunia nzima kwa jumla.

Kuanzisha utoaji wa mafunzo kwa kiwango cha Uzamili na Uzamivu katika

taaluma za lojistiki, upokeaji na uondoshaji mizigo, usafirishaji, ufundi,

mawasiliano utawala wa rasilimali watu na nyinginezo.

Kuwa na sura ya Kimataifa kwa ubora wa taaluma itolewayo itakayowavutia

washiriki wengi zaidi kutoka ndani na nje ya nchi kwa kuboresha mitaala ya

kufundishia ili kuongeza kiwango cha ubora wa wahitimu sanjari na mabadiliko

ya sayansi na teknolojia.

Kuanzisha vituo vya mafunzo katika kanda zote za Tanzania Bara na Visiwani.

Kuongeza idadi ya wahadhiri, watumishi na vitendea kazi.

Kuongeza vifaa vya kufundishia kwa lengo la kutoa mafuzo bora ya vitendo.

Kuwa kitovu cha kufanya utafiti na kukusanya takwimu zitakazosaidia kutoa

suluhu ya matatizo ya Menejimenti ya usafiri nchini, hususan katika miji yetu na

nchi za jirani.

Kuwa Taasisi inayoaminika na kushauri jamii na Serikali kwa ujumla kuhusiana

na masuala ya kitaalam ya Sekta na hivyo kufanywa kitovu cha taarifa muhimu

zinazohusu na Sekta ya Uchukuzi.

10.5 HUDUMA ZA HALI YA HEWA NCHINI

Huduma za hali ya hewa nchini zilianza kutolewa mwaka 1929 chini ya Taasisi ya Hali ya

Hewa ya Uingereza iliyojulikana kama British East Africa Meteorological Services (BEAMS).

Katika kipindi husika vituo viwili vya hali ya hewa vilijengwa Kazeh Hill huko Tabora na

Chukwani Zanzibar ambapo makao makuu ya taasisi hii yalikuwa Tabora. Taasisi hiyo ilikuwa

Page 91: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

88

na majukumu ya kutoa huduma za hali ya hewa kwa nchi za Kenya, Tanganyika, Zanzibar na

Rhodesia ya Kaskazini (sasa Zambia). Baadaye Taasisi hiyo iliitwa British East African

Meteorological Department (BEAMD) chini ya British East African High Commission kwa

nchi za Kenya, Tanganyika, Uganda na Zanzibar.

Baada ya kuanzishwa kwa Shirika la Hali ya Hewa Ulimwenguni (WMO) mnamo mwaka

1951, huduma za hali ya hewa duniani ziliimarika ambapo mwaka 1963 British East African

High Commision ilibadilishwa muundo na kuwa East African Common Services Organisation

(EACSO) ambapo BEAMD ilibadilika na kuwa East African Meteorological Department

(EAMD) iliyokuwa na jukumu la kuhudumia nchi tatu za Afrika Mashariki yaani; Kenya,

Uganda na Tanzania. Makao makuu ya BEAMD na EAMD yalikuwa Kabete, Kenya na

baadaye yakahamishiwa Nairobi, Kenya. Mwaka 1967 EACSO ilibadilika na kuwa East

African Community (EAC). Taasisi ya Hali ya Hewa nayo ilipata muundo mpya lakini

iliendelea kuitwa EAMD na makao yake makuu kuwa huko Nairobi, Kenya.

Mwaka 1977, baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, huduma za hali ya

hewa nchini zilikuwa chini ya Wizara ya Mawasiliano na Ujenzi kama Idara ya Serikali. Idara

Kuu ya Hali ya Hewa (Directorate of Meteorology (DoM)) ilianzishwa rasmi 1978 kwa Sheria

namba 6 ya mwaka huo.

Idara Kuu ya Hali ya Hewa ilibadilishwa na kuwa Wakala wa Serikali mnamo mwaka 1999

kwa Sheria namba 30 ya Executive Agencies (Act) na ikaitwa Mamlaka ya Hali ya Hewa

Tanzania. Mabadiliko hayo yalilenga kuongeza ufanisi katika kutoa huduma kwa vile wakala

uliongezewa uwezo wa kufanya baadhi ya maamuzi ya kiutendaji.

Historia ya Ofisi Kuu za Hali ya Hewa Tanzania

Tanzania kulikuwa na ofisi ndogo na ya kiutawala zaidi kwa vile shughuli za hali ya hewa

hazikuwa nyingi na makao makuu yalikuwa Nairobi, Kenya. Shughuli zilianza kupanuka baada

ya Uhuru na ofisi za hali ya hewa zilikuwa katika jengo la Avalon Building, Sokoine Drive.

Mnamo mwaka 1966, Jumuiya ya Africa Mashariki (EAC) ilijenga makao makuu yake

Sokoine Drive kwenye jengo la EAC Building ambalo sasa linaitwa Mapato House. EAMD

Tanzania na baadaye DoM walikuwa ghorofa ya 6 katika jengo hilo. Kutokana na kupanuka

kwa shughuli zake, EAC ilijenga ofisi nyingine kwa ajili ya EAMD na Directorate of Civil

Aviation (DCA) kanda ya Tanzania katika eneo la Sokoine Drive karibu na Posta ya zamani.

Kwa bahati mbaya wakati EAC ilipovunjika mwaka 1977 jengo hilo halikuwa limekamilika na

1978 lilichukuliwa na Wizara ya Maji na Nishati.

Shughuli za DoM zilizidi kupanuka na majukumu yaliyokuwa yakifanyika makao makuu

Nairobi yalianza kufanyika hapa nchini kwa hiyo kukawa na uhitaji mkubwa wa ofisi. Shughuli

nyingi za makao makuu ya DoM zilitawanyika katika majengo ya EAC Building (Mapato

House), Tancot House Building, Dar es Salaaam Airport na Revenue (TRA) Samora Avenue.

Katika kutatua tatizo hili, Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) ilihamia katika jengo la Ubungo

Plaza mwaka 2004.

Historia ya Utabiri wa hali ya hewa Tanzania

Page 92: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

89

Utabiri wa hali ya hewa ulianzishwa na mwana sayansi wa Uingereza, Lewis Richardson

mwaka 1926 ambapo aligundua kuwa mifumo ya hali ya hewa inafuata kanuni za hesabu na

fizikia. Kabla ya 1961, utabiri wa hali ya hewa nchini ulikuwa unafanyika katika viwanja vya

ndege.

Baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ilianzishwa National Meteorological

Centre iliyokuwa na jukumu la kutoa utabiri wa hali ya hewa nchini. Katika kipindi hicho,

utabiri uliokuwa unatolewa ulikuwa wa muda mfupi wa saa sita kutokana na uwezo mdogo wa

teknolojia iliyokuwa inatumika wakati huo.

Mnamo miaka ya 1990, utabiri wa hali ya hewa kwa kutumia mifumo ya modeli za hesabu

(Numerial Weather Prediction) na picha za satellite ilianza kutumika nchini. Mifumo hii

imeimarisha huduma za utabiri wa saa sita na kuwa wa saa 24, siku kumi na msimu. Aidha,

mifumo hiyo imerahisisha kazi ya kuandaa utabiri nchini.

Historia ya mfumo wa ubadilishanaji wa taarifa za hali ya hewa Tanzania

Ili kuweza kutabiri hali ya hewa nchini na pia kubadilishana na nchi nyingine kwa ajili ya

usalama wa binadamu na mali zao lazima nchi zote zibadilishane taarifa na takwimu za hali ya

hewa. Kabla ya uhuru, mfumo wa mawasiliano ulitumia mikanda na mapigo maalum ya sauti

(Torn tape’ na „morse code) katika ubadilishanaji wa taarifa za hali ya hewa.

Mamlaka ya Hali ya Hewa inatumia njia mbili za kukusanya na kubadilishana taarifa na

takwimu za hali ya hewa. Mfumo wa kwanza ni ule wa WMO wa Global Telecommunications

System (GTS) na mwingine ni ule mahsusi kwa ajili ya Usalama wa Usafiri wa Anga uitwao

Aeronautical Fixed Telecommunications Network (AFTN) wa ICAO.

Katika kipindi cha 1971 – 1981, mfumo wa mawasiliano ulitegemea „land-line Teletype (LLT)‟

kwa kiasi kikubwa na simu za mezani ambapo Shirika la Posta na Simu ndio lililokuwa

likisimamia kwa uhakika wa mawasiliano. Aidha, mifumo ya mawasiliano ya „Facsmile’

ilitumika ambapo taarifa zilikuwa zinabadilishwa kupitia „Line Teletype (LTT), Telexes, Radio

Teletype (RTT)‟ pamoja na kutumia radio za „High Frequency (HF)‟.

Kuanzia miaka ya 1990, mifumo ya mawasiliano iliboreshwa na kuanza kutumia Premicel,

tovuti, Transmet, Radio Telephone (SSB), VSAT, SADIS, Retim Synergie na Microwave link.

Aidha, maendeleo ya kisayansi duniani yamekuwa yakiendelea kuboresha mifumo ya

mawasiliano ya hali ya hewa.

Ramani iliyopo hapa chini inaonesha mifumo ya mawasiliano inayotumika kubadilishana data

za hali ya hewa toka vituo mbalimbali nchini kwenda kituo kikuu cha utabiri kilichopo Dar es

Salaam. Aidha, data hizo hupelekwa kituo cha kanda – Nairobi.

Page 93: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

90

Historia ya usambazaji wa taarifa za hali ya hewa Tanzania

Tangu mwaka 1961, mfumo wa utoaji wa taarifa za hali ya hewa, ulikuwa unalenga kuboresha

huduma za usafiri wa anga maeneo maalum na majini, kilimo cha mazao ya biashara pamoja na

tahadhari. Njia kuu ya utoaji habari kipindi hicho ilikuwa ni vyombo vya habari ikiwa ni

pamoja na magazeti na radio. Magazeti haya yalikuwa hayawafikii walengwa kwa kiasi

kikubwa hasa vijijini na radio zilizokuwepo wakati huo zilikuwa hazisikiki nchi nzima na pia

sio walengwa wote waliweza kumiliki Radio. Kwa hivi sasa, Mamlaka imefanikiwa kuboresha

ufikishaji wa taarifa za hali ya hewa kwa walengwa kwa kuongeza idadi ya vyombo vya habari

ikiwemo radio, tovuti, magazeti na televisheni.

Madhumuni ya kutoa huduma za hali ya hewa

Kabla ya uhuru huduma za hali ya hewa zilikuwa zinatolewa kwa ajili ya kukidhi matakwa ya

Wakoloni ikiwemo kufanikisha safari za ndege za Ulaya na Afrika ya Kusini. Aidha, huduma

za hali ya hewa zililenga katika kutoa huduma kwa sekta ya kilimo cha mazao ya biashara

(Groundnut scheme-Nachingwea na Kongwa).

Baada ya uhuru, majukumu ya utoaji wa huduma za hali ya hewa nchini yaliongezeka na

huduma ziliboreshwa ili kukidhi mahitaji ya jamii na kuchangia katika ukuaji wa sekta za

kiuchumi na kijamii kwa ajili ya maendeleo ya Tanzania hasa sekta ya usafiri wa anga.

Page 94: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

91

Mwaka 1999, Serikali ilifanya mabadiliko kwa iliyokuwa Idara Kuu ya Hali ya Hewa kuwa

Wakala wa Hali ya Hewa yenye majukumu yafuatayo:-

Kuanzisha na kuendesha vituo vya hali ya hewa ili kupata takwimu na taarifa za hali ya

hewa kwa ajili ya kutoa huduma za hali ya hewa katika sekta mbalimbali za kiuchumi

na kijamii.

Kutoa utabiri wa hali ya hewa wa kila siku, muda wa kati (siku 10) na wa msimu na

kutoa tahadhari ya hali mbaya ya hewa na kuhakikisha taarifa hizi zinawafikia

walengwa katika muda muafaka.

Kutoa huduma za hali ya hewa kwa sekta za kilimo, usafiri na uchukuzi, miundombinu,

maji, nishati, mazingira, utalii, nk

Kufuatilia na kufanya utafiti wa kisayansi kuhusu masuala ya mabadiliko ya tabia nchi

(Climate change) nchini.

Kushirikiana na taasisi za kimataifa na nchi nyingine katika kubadilishana takwimu na

taarifa za hali ya hewa, hususani majanga ya asili kama ukame na vimbunga kwa ajili

ya kutoa tahadhari.

Sekta ya hali ya hewa ina jukumu la kuendeleza na kutunza mtandao wa vituo vya

kupima na kuangaza hali ya hewa ili kukidhi makubaliano ya kimataifa ya

kubadilishana taarifa hizo na nchi nyingine. Masuala ya mabadiliko ya tabia nchi

(climate change) yanahitaji ushirikiano wa kimataifa. Mamlaka ina jukumu la kufuatilia

na kupima kisayansi mabadiliko ya hali ya hewa nchini.

Kufanya utafiti na kutoa mafunzo ya fani ya hali ya hewa kwa kushirikiana na vyuo vya

ndani na nje ya nchi.

Kushirikiana na taasisi za kanda na za kimataifa zinazojihusisha na shughuli za hali ya

hewa kama vile Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC);

Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO).

Mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru

Upanuzi wa mtandao wa Vituo vya kupima hali ya hewa nchini.

Wakati tunapata uhuru mwaka 1961 kulikuwa na Kituo Kikuu kimoja tu cha Dar es salaam

kilichokuwa kinafanya kazi kwa saa ishirini na nne (24). Kwa sasa Tanzania ina vituo vikuu 28

vya kupima hali ya hewa vinavyopima kwa saa 24.

Vituo vya kupima mvua

Upimaji mvua ulianza 1892 wakati Tanganyika ikiwa chini ya utawala wa Kijerumani. Wakati

huo upimaji mvua ulikuwa ni wa kujitolea na haukuwa na malipo.

Serikali ya Kikoloni ilijenga vituo 1074 vya kupima mvua na lengo kuu lilikuwa ni kukuza

kilimo cha mazao ya biashara. Baada ya uhuru, Serikali iliendeleza na kuongeza mtandao wa

vituo hivi na kufikia 2043. Katika miaka ya 1960 hadi 1980, vituo vilipungua hadi kufikia 1200

kutokana na kupungua kwa bajeti ya kuhudumia shughuli za hali ya hewa nchini. Kwa

kutambua umuhimu wa taarifa na takwimu za mvua, Mamlaka kuanzia miaka ya 1990

Page 95: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

92

ilianzisha mpango wa kuwalipa posho wapimaji mvua wachache wanaofanya vizuri na mpango

ukazaa matunda ambapo mpaka sasa vituo vimeongezeka na kufikia 1600.

Vituo vya hali ya hewa Mahsusi kwa Kilimo (Agromet stations)

Wakati wa ukoloni kulikuwa na vituo sita (6) tu vya hali ya hewa mahsusi kwa kilimo

(agrometeolojia). Baada ya uhuru, Serikali kwa kutambua mchango wa Sekta ya Kilimo

ambayo ndiyo mhimili mkuu wa uchumi wa Tanzania ilifanya jitihada za kujenga vituo zaidi 7

na kuongeza idadi ya vituo hivyo kufikia 13.

Vituo vya Rada za hali ya hewa

Wakati tunapata uhuru, tulikuwa tunamiliki vituo viwili vya rada za hali ya hewa zilizokuwa

Dar es Salaam na KIA, lakini kutokana na mabadiliko ya Teknolojia, Rada hizi zilipitwa na

wakati hivyo, hazitumiki tena. Kwa sasa Mamlaka imekamilisha ujenzi wa kituo cha Rada ya

Hali ya Hewa kilichopo Dar es salaam na taratibu za ununuzi wa rada ya pili itakayofungwa

Mwanza zinaendelea.

Vituo vya kupima hali ya hewa ya anga za juu (Radiosonde Stations)

Baada ya uhuru tulianzisha vituo vya Radiosondes Dar es Salaam na Tabora na baadaye

tuliongeza vituo vingine huko Kigoma na Mtwara kupitia mradi wa FINNIDA (1988–1992).

Hata hivyo, kutokana na kubadilika kwa teknolojia, mitambo ya vituo hivi ilipitwa na wakati

ikawa haitumiki tena. Kwa sasa Mamlaka imefufua kituo cha Dar es Salaam kwa kufunga

mtambo mwingine wa kisasa.

Wafanyakazi na Mafunzo

Wafanyakazi

Wakati tunapata uhuru mwaka 1961, Taasisi ya Hali ya Hewa kwa nchi zote za Afrika ya

Mashariki ilikuwa na wafanyakazi 330 kati yao wanasayansi walikuwa 14 na hakukuwa na

watabiri (forecasters) wazalendo. Kwa sasa huduma za hali ya hewa zinatolewa na TMA iliyo

chini ya Wizara ya Uchukuzi yenye wafanyakazi 570 kati yao wanasayansi ni 407 wanawake

wakiwa ni asilimia 20 ya wanasayansi waliopo. Aidha, kwa hivi sasa wako watabiri 82

miongoni mwa hao wanawake ni 26.

Mafunzo

Tangu enzi za ukoloni, mafunzo ya taaluma ya hali ya hewa katika ngazi zote yamekuwa

yakipatikana nje ya nchi. Mnamo mwaka 1977 baada ya kuvunjika kwa iliyokuwa Jumuiya ya

Afrika Mashariki, Serikali ilianzisha Chuo cha Hali ya Hewa Dar es Salaam na baadaye mwaka

1981 kuhamishiwa Kigoma ili kupunguza gharama ya kuwapeleka wanafunzi katika elimu ya

awali nje ya nchi. Mnamo mwaka 1999, Chuo kilianza kutoa mafunzo ya kati ya watabiri

(Class III) na mwaka 2002 kilianzisha mafunzo ya stashahada ya utabiri (Forecasting) hapa Dar

es Salaam na baadae kuhamishiwa Kigoma.

Page 96: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

93

Mpaka sasa, Mamlaka ina wafanyakazi wenye shahada wapatao 92 wanawake wakiwa ni 22.

Wafanyakazi wenye shahada ya kwanza wakiwa 62 wanawake 14, shahada ya pili wakiwa 24

wanawake 7 na shahada ya tatu wakiwa 6 mwanamke mmoja.

Mifumo ya Utabiri

Baada ya mwaka 1961, Mamlaka haikuwa na mfumo wa utabiri kwa kutumia Numerical

Weather Prediction Models, NWP hadi ilipofika miaka ya 1990 ambapo utabiri wa aina hii

ulianza kutumika toka vituo vikuu vya utabiri kupitia tovuti. Mpaka kufikia mwaka 1994,

Mamlaka ilianzisha mfumo wa utabiri wa NWP na imeendelea kuuboresha mfumo huo mpaka

sasa.

Hadi kufikia mwaka 2011, Mamlaka imekuwa na mafanikio makubwa katika upatikanaji wa

taarifa mbalimbali za hali ya hewa katika satelaiti ambazo zimewekwa angani na kuangalia

eneo moja la dunia (geostationary satellites).

Kutokana na kuongezeka kwa mtandao wa vituo nchini, Mamlaka imekuwa ikitoa utabiri wa

kila siku, siku kumi, mwezi na msimu kwa usahihi na kuaminika katika kiwango cha

kuridhisha ukilinganisha na miaka 50 iliyopita.

Mifumo ya usambazaji wa taarifa za hali ya hewa

Mamlaka imeweza kuanzisha studio ya hali ya hewa inayotumika kuandaa utabiri wa hali ya

hewa kwa ajili ya kuutangaza kwenye luninga. Pia imefungua tovuti yake (www.meteo.go.tz)

kwa ajili ya kurahisisha utoaji wa huduma zake. Hapo awali, utabiri wa hali ya hewa ulikuwa

unatolewa kupitia redio na magazeti. Mabadiliko ya utoaji wa taarifa yaliambatana moja kwa

moja na mabadiliko makubwa ya kisayansi na kiteknolojia katika vifaa vya mawasiliano

ambapo serikali ilichangia kwa kiasi kikubwa ikiwemo uundwaji wa sera mbalimbali za

vyombo vya mawasiliano nchini. Vyombo vya habari vimekuwa vikiongezeka ambapo

Mamlaka ilianza kutoa taarifa zake kupitia Televisheni moja mwaka 1995 na hadi kufikia sasa

kuna magazeti 5, radio 11, Televisheni 6.

Mfumo wa kuhifadhi taarifa za hali ya hewa

Wakati wa uhuru 1961, takwimu zote za hali ya hewa zilikuwa zikihifadhiwa Nairobi ambapo

mnamo mwaka 1972, kiasi kikubwa cha takwimu hizo zililetwa nchini. Idara Kuu ya Hali ya

Hewa nchini ilikuwa ikizihifadhi taarifa na takwimu za hali ya hewa katika mifumo ya

makabrasha, magnetic tapes na punch-cards. Mnamo mwaka 1990, Idara Kuu ya Hali ya Hewa

ilifanya mabadiliko katika kuhifadhi na kuchambua taarifa na takwimu za hali ya hewa kwa

kuanza kutumia teknolojia ya kompyuta. Teknolojia hiyo ya kuchambua na kuhifadhi takwimu

kupitia kompyuta inayoitwa CLICOM ilianza kutumika 1990. Shughuli ya ubadilishaji na

uhifadhi wa taarifa na takwimu za hali ya hewa ni kubwa kutokana na wingi wa takwimu za

hali ya hewa zilizopo kuanzia mwaka 1892 na inaendelea hadi sasa.

Page 97: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

94

Changamoto katika utoaji wa huduma za hali ya hewa Tanzania

Kutokuwepo kwa Sera na Sheria ya Hali ya Hewa

Upungufu wa vituo na vifaa vya kupimia hali ya hewa

Gharama kubwa za kununua na kuendesha mitambo ya hali ya hewa.

Mabadiliko ya hali ya hewa duniani (Climate Change) yanayosababisha changamoto

katika kutoa utabiri.

Upungufu wa wataalam wa hali ya hewa.

Ufinyu wa bajeti.

Kutokuwa na jengo la Kituo Kikuu cha Utabiri.

Uchakavu wa Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma

Matarajio katika miaka 50 ijayo

Mamlaka ina mikakati ya muda mrefu ya kuboresha huduma zake ili kukidhi mahitaji ya

huduma za hali ya hewa nchini ambayo yameongezeka kutokana na kukua kwa sekta

mbalimbali za kiuchumi na kijamii. Mikakati hiyo ni pamoja na:-

Kuongeza idadi ya vituo vinavyopima taarifa zote za hali ya hewa kutoka 27 hadi

kufikia 70. Pia kununua mitambo 100 ya kupima taarifa za hali ya hewa inayojiendesha

yenyewe.

Page 98: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI€¦ · Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Dira ya Wizara ni kuwa na Miundombinu ya uchukuzi na Huduma za Uchukuzi na Hali ya Hewa

95

Kuwa na vituo saba Dar es Salaam, Kigoma, Mwanza, Dodoma, Kilimanjaro, Mbeya,

Mtwara vya rada nchi nzima. Katika utekelezaji wa mradi huo tayari ufungaji wa rada

moja umekamilika na taratibu za ununuzi wa rada ya pili zinaendelea. Kukamilika kwa

mradi huo kutaimarisha shughuli za utabiri wa hali ya hewa pamoja na tahadhari dhidi

ya matukio ya hali mbaya ya hewa.

Kuongeza idadi ya vituo vya hali ya hewa mahsusi kwa kilimo kutoka 13 vilivyopo sasa

na kufikia ishirini (20) ili kukidhi mahitaji ya sekta ya kilimo.

Kuongeza vituo 900 vya kupima mvua na kuviimarisha vilivyopo ili kufikia vituo

2,500. Aidha Mamlaka ina mpango wa kununua vifaa 2,500 vyenye uwezo wa kupima

mvua vyenyewe (Automatic raingauges) ili kufikia malengo ya kuwa na vituo 5,000

nchi nzima.

Kuboresha Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma na kuanzisha mafunzo ya shahada, uzamili

na uzamivu ya Hali ya hewa hapa nchini.

Kuboresha mfumo wa mawasiliano ili kwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia

ya ubadilishaji wa taarifa za Hali ya Hewa duniani.