jamhuri ya muungano wa tanzania taasisi ya …

56
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA UTAFITI WA RUSHWA YA NGONO KATIKA TAASISI ZA ELIMU YA JUU: UCHUNGUZI KIFANI WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM NA DODOMA JUNI, 2020

Upload: others

Post on 18-Nov-2021

7 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA

UTAFITI WA RUSHWA YA NGONO KATIKA TAASISI ZA ELIMU YA JUU:

UCHUNGUZI KIFANI WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM NA DODOMA

JUNI, 2020

Page 2: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

i

MUHTASARI RASMI (EXECUTIVE SUMMARY)

Usuli

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) ilifanya utafiti kwa lengo la

kuwezesha upatikanaji wa taarifa za kisayansi zitakazosaidia kukabiliana na vitendo vya rushwa

ya ngono katika Taasisi za elimu ya juu nchini. Aidha utafiti huu uliongozwa na malengo

mahususi yafuatayo; Kuwezesha kupata taarifa za kina kuhusu kuwepo kwa tatizo la rushwa ya

ngono; Kuchunguza sababu za kuwepo vitendo vya rushwa ya ngono; Kutathmini uwepo na

ufanisi wa mifumo ya udhibiti wa ndani ya maadili juu ya vitendo vya rushwa ya ngono; na

Kutoa mapendekezo yatakayowezesha Taasisi na Serikali kwa jumla kupambana na kuzuia

rushwa ya ngono kwenye taasisi za elimu ya juu.

Jukumu hili la TAKUKURU linatokana na matakwa ya kifungu cha 7 (a) na (c) cha Sheria ya

Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11/2007. Kwa mujibu wa kifungu hiki, TAKUKURU

inao wajibu wa kuzuia rushwa katika taasisi za umma na binafsi kwa kufanya chambuzi za

mifumo katika taasisi hizo ili kubaini uwepo wa mianya ya rushwa na kisha kutoa ushauri wa

namna bora ya kudhibiti mianya hiyo.

Vilevile, TAKUKURU imefanya utafiti huu kama njia mojawapo ya kutekeleza moja ya

malengo ya Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa na Mpango wa Utekelezaji Awamu ya Tatu

(NACSAP III), “kuimarisha ufanisi, uwazi na uwajibikaji wa utoaji huduma katika sekta ya

umma na binafsi”. Ili kufanikisha utafiti huu, TAKUKURU iliingia ubia na Asasi ya Kiraia ya

WFT (Women Trust Fund) kama sehemu ya utekelezaji wa NACSAP III wa kujenga daraja na

wapiganaji wa vita dhidi ya rushwa. NACSAP III imebainisha majukumu ya wadau mbalimbali

kwenye vita dhidi ya rushwa. Kwa upande wa Asasi za Kiraia, baadhi ya majukumu ni pamoja

na: (i) kufanya utafiti na mafunzo kuhusu rushwa, maadili na utawala bora (ii) kuimarisha

kiwango cha uwazi na uwajibikaji katika shughuli zao, pamoja na (iii) kushiriki katika kampeni

za maadili ya Taifa na Utawala Bora (URT: 2007).

Page 3: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

ii

Pamoja na kwamba Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imechukua hatua kadhaa za

kupambana na rushwa, ikiwemo rushwa ya ngono, bado yapo malalamiko ya rushwa ya ngono

hapa nchini. Zipo sababu nyingi za kuendelea kuwepo kwa malalamiko ya rushwa ya ngono,

ambazo ni pamoja na: matumizi mabaya ya madaraka; mikakati dhaifu ya kutekeleza sheria za

rushwa ya ngono; uelewa hafifu; kutokutambua kina na athari za tatizo la rushwa ya ngono; na

jamii kulionea aibu suala hili. Hali hii inasababisha waathiriwa wa rushwa ya ngono kuendelea

kuumia kimya kimya ambapo wakosaji kuendelea na vitendo hivi bila kuchukuliwa hatua stahiki

za kisheria.

Rushwa ya ngono hugeuza haki ya muombwaji kuwa upendeleo na siyo stahiki yake. Inapohusu

kumpokonya mtu haki yake, husababisha madhara kwenye nyanja mbalimbali kama vile kupata

jeraha lisilotibika kwenye maisha yake na mahala pengine anaweza kugeuzwa mtumwa wa

ngono, na hivyo kushindwa kukuza vipaji vyake vya uhalisia. Hali hii huathiri uchumi wa taifa

Kwanini utafiti wa rushwa ya ngono?

Pamoja na kutambua athari za rushwa ya ngono kwa wahanga, jamii na hata uchumi, hili ni eneo

ambalo halijafanyiwa utafiti wa kina hapa nchini. Tofauti na aina nyingine za rushwa

zinazotumia ubadilishaji wa vitu yakinifu au ridhaa ya mtoa rushwa na mpokea rushwa, hii ni

rushwa inayotokana na tabia ya mdai rushwa kutumia mamlaka yake kushawishi, kushinikiza

ngono badala ya vitu yakinifu.

Licha ya kutumia taarifa na maarifa ya kina yatokanayo na utafiti huu kuhusu suala hili la

rushwa ya ngono linavyoumiza taifa, jamii, taasisi, na watu binafsi wakiwemo waathirika, utafiti

huu ni nyenzo muhimu kwa watunga sera na sheria katika kushughulikia tatizo la rushwa ya

ngono. Dhamira ni kuchangia kwenye juhudi mbalimbali za kupambana na kuzuia vyanzo vikuu

vya uendelezaji wa vitendo vya rushwa ya ngono.

Kwanini Vyuo vya Elimu ya Juu?

Dira ya Taifa inadhamiria ifikapo mwaka 2025, Tanzania itakuwa ni nchi ya Taifa la wasomi na

wenye kupenda kujielimisha. Hivyo basi tatizo au changamoto yoyote inayogusa sekta ya elimu

Page 4: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

iii

itaathiri ufikiwaji wa dira hii. Elimu ya juu ni kiwanda cha kuzalisha nguvu kazi ya taifa hivyo

husaidia kukuza uchumi na kuwezesha nchi kufikia malengo yake ikiwa ni pamoja na kufikia

uchumi wa viwanda.

Hivi karibuni kumekuweko na malalamiko mengi kuhusu uwepo wa matukio ya rushwa za

ngono kwenye taasisi za elimu ya juu, na hivyo utafiti huu utawezesha kubainisha kina cha

tatizo, kwanini hali hii, nini kifanyike na namna ya kulishughulikia suala hili.

Kwa nini Chuo Cha Dar es Salaam na Dodoma?

Hivi ni miongoni mwa vyuo vinavyomilikiwa na umma hapa nchini. Kinadharia, ni vyuo

vinavyohitajika au vinavyotarajiwa kuwa mfano katika utawala bora. Chuo Kikuu cha Dar es

Salaam (UDSM) ndiyo chuo cha kwanza cha umma hapa nchini kilichozalisha viongozi wengi

kuliko vyuo vyote. Aidha, ndicho chuo cha kwanza katika Bara la Afrika kuzalisha fikra za

kimapinduzi, zilizoweza kunoa viongozi wengi walioweza kuchanganua jinsi Bara la Afrika

lilivyoporwa rasilimali zake na linavyoendelea kufukarishwa. Kimantiki, ni chuo ambacho

kinapaswa kuongoza fikra mbadala ikiwa ni pamoja na fikra zinazopinga unyanyasaji wa

kijinsia. Vilevile, ni chuo kikubwa nchini na kinachodahili wanafunzi wengi zaidi. Kwa mwaka

2017/2018 pekee, chuo hiki kilifanya udahili wa wanafunzi 13,626 ambao ni sawa na 21% ya

wanafunzi wote waliodahiliwa kwenye taasisi za elimu ya juu nchini kwa mwaka.

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kipo Makao Makuu ya nchi na kichanga kwa kulinganisha

na UDSM. Kimantiki, chuo hiki hakikuhitaji kuandika sera, au miongozo mipya kwani kilikuwa

na fursa ya kujifunza kutoka chuo cha UDSM kuhusu masuala mengi ikiwa ni pamoja na kanuni

na miongozo inayokataza rushwa ya ngono katika taasisi za elimu ya juu. Vilevile, ni chuo

chenye udahili wa wanafunzi wengi. Kwa mfano, kwa mwaka wa masomo 2017/2018, chuo hiki

kilidahili wanafunzi 9,151 (Tanzania Commission for Universities – TCU, 2018).

Hivyo, vyuo hivi viwili vilihusishwa katika utafiti huu kutokana na historia ya vyuo hivi, umiliki

wake (vyuo vya umma) na wingi wa udahili wa wanafunzi. Hivi ndivyo vyuo vikuu vikubwa

viwili vinavyomilikiwa na Serikali na vinavyoongoza kwa kudahili wanafunzi wengi zaidi

Page 5: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

iv

nchini. Aidha, kutokana na ukubwa wake na idadi kubwa ya wanafunzi nchini, utafiti uliona

kuwa ni sehemu sahihi ya kuweza kuchunguza na kujenga msingi wa kisayansi kuhusu rushwa

ya ngono nchini.

Taarifa na mapendekezo yatokanayo na utafiti huu yanaweza kutumiwa na vyuo na taasisi

nyingine za umma, sekta binafsi na asasi za kiraia kujitathmini katika maeneo yaliobainishwa na

hivyo, kuweza kubuni mikakati ya kukabiliana na tatizo la rushwa ya ngono kwa kuzingatia

uhalisia wa taasisi husika.

Mbinu za ukusanyaji wa taarifa

Taarifa za msingi zilikusanywa kwa kutumia madodoso, usaili, majadiliano ya vikundi na ziara

za watafiti katika vyuo tafitiwa. Taarifa za upili (secondary data) zilipatikana kwa uchambuzi wa

nyaraka zikiwemo sera, sheria, kanuni na miongozo mbalimbali inayosimamia vyuo hivyo.

Aidha, kazi za tafiti zinazohusu rushwa ya ngono zilipitiwa. Taarifa zilizokusanywa

zilichambuliwa kwa kutumia programu tumizi ya kuchambua taarifa za sayansi ya jamii (SPSS)

na taarifa nyingine zilichambuliwa kwa kufanya uchambuzi wa maudhui.

Muhtasari wa mambo makuu yaliyojitokeza kwenye utafiti

Kwa ujumla, utafiti umebaini kwamba tatizo la rushwa ya ngono kwenye vyuo vilivyoshiriki lipo

na kwamba tatizo hili ni kubwa na si la kupuuzwa. Shuhuda za waathiriwa wa rushwa ya ngono

pamoja na shuhuda za uwepo wa watuhumiwa ambao hawajachukuliwa hatua zilitolewa.

Vilevile, utafiti ulibaini kuwepo kwa sera, miongozo na sheria ndogondogo zinazoharamisha

rushwa ya ngono kwenye taasisi zote za umma ikiwa ni pamoja na vyuo vikuu. Kwa mfano,

Kanuni za Utumishi wa umma (2014, kanuni ya 36) zimepiga marufuku kwa mwajiri au

mtumishi wa umma kufanya aina yoyote ya udhalilishaji wa kijinsia kwa kumtaka mwajiriwa

kufanya ngono au kufanya aina yoyote itakayosababisha kufanyika ngono kama kigezo cha ahadi

ya kupendelewa kazini, au kulazimisha ngono ili mwajiriwa kuepuka vitisho ambavyo vitaathiri

ajira yake au kutumia kigezo cha ngono ili mwajiriwa aepuke vitisho dhidi ya maslahi ya sasa au

ya baadae katika ajira yake.

Page 6: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

v

Vyuo vyote viwili vina kanuni za maadili za watumishi; Kanuni za Maadili kwa Watumishi wa

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (2018) na kanuni za maadili Chuo Kikuu Dodoma (2012).

Kanuni hizi zinabatilisha na kutoa katazo la kutumia rushwa ya ngono kutoa ufaulu, kufanya

vitendo vinavyoashiria ngono, au kufanya mawasiliano yanayoashiria uhitaji wa rushwa ya

ngono. Aidha, zinakataza kumsumbua au kumnyanyasa mtu yeyote yule anayetoa taarifa juu ya

unyanyasaji wa kingono (UDSM, 2018).

Pamoja na kuwepo kwa miongozo na kanuni zinazokataza rushwa ya ngono, utafiti ulibaini

mapungufu kwenye uwajibikaji wa udhibiti wa matumizi mabaya ya mamlaka hivyo kutoa

mianya inayosababisha kuwepo kwa vitendo vya rushwa ya ngono. Jambo hili lilielezwa

kusababishwa na kutokuwepo utashi wa dhati kwa wale waliopewa dhamana ya uongozi na

watoa huduma katika kushughulikia tatizo la rushwa ya ngono kikamilifu. Tabia za kuwalinda

wakosaji, zimesababisha kutokuimarisha ufuatiliaji wa sera na miongozo, kutokusimamia

maadili ya watendaji kwenye suala hili na kushindwa kuchukua hatua stahiki za kinidhamu kwa

wale wanaoendeleza vitendo vya rushwa ya ngono kwenye taasisi husika. Mifano ilitolewa ya

wahadhiri wanaodaiwa kujihusisha na rushwa ya ngono wanavyoendelea kupewa nyadhifa

mbalimbali za uongozi na vyeo vya kitaaluma. Shuhuda zilitolewa kuhusu vitisho kwa watoa

taarifa wakiwa waathiriwa au wahadhiri/watumishi wa vyuo husika. Shuhuda zilitolewa kuhusu

wanafunzi waliopendelewa na kupewa aidha ajira au kupewa udhamini wa masomo

(scholarship) bila kustahili pale ambapo wamekubali kutoa rushwa ya ngono. Shuhuda nyingine

zilitolewa kwa kuwepo watuhumiwa waliopewa adhabu kidogo sana kulingana na kosa, kwa

mfano mhadhiri kupewa likizo ya mwaka iliyomwezesha kuendelea na shughuli zake za ushauri

wa kitaalam na hatimaye kurudi chuoni kuendelea na shughuli kama kawaida baada ya muda huo

kupita. Shuhuda zilitolewa kwa uongozi wa vyuo kutokufanyia kazi mapendekezo ya kamati za

maadili hasa kwa masuala yanayohusu rushwa ya ngono. Ukosefu wa utashi na uwajibikaji

unakatisha tamaa waathiriwa wa rushwa ya ngono au watendaji wenye maadili kutoa taarifa

kuhusu vitendo vya rushwa ya ngono.

Utafiti ulibaini mapungufu kwenye mifumo ya utahini inayotoa mwanya kwa wahadhiri kutumia

vibaya mamlaka yao. Shuhuda zilitolewa kuhusu wanafunzi waliofelishwa kutokana na kukataa

rushwa ya ngono au wanafunzi wa kiume kufelishwa kwa vile marafiki wao wa kike wamekataa

Page 7: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

vi

kutoa rushwa ya ngono. Shuhuda zilitolewa kuhusu kubadilishwa kwa alama za mitihani hata

baada ya matokeo kutoka rasmi. Shuhuda zilitolewa kuhusu wanafunzi waliopendelewa kwenye

kupewa alama za juu na hatimaye kuajiriwa chuoni bila kustahili.

Mapungufu yamejitokeza kwenye mifumo ya vyombo vya kusimamia utekelezwaji wa sera na

miongozo hususan kwenye suala la rushwa ya ngono. Kamati za maadili kushindwa kudhibiti

rushwa ya ngono, vitengo vya jinsia kukosa nyezo za kiuchunguzi za kuthibitisha makosa ya

rushwa ya ngono na uwezo wa kuelimisha jamii kuhusu rushwa ya ngono, ofisi za mshauri wa

wanafunzi na vitengo vya jinsia kukosa uwezo wa kutathmini, kufuatilia na kukusanya ushahidi

juu ya malalamiko ya rushwa ya ngono yanayowasilishwa kwao.

Utafiti ulibaini mianya mingine inayosababisha kuendelezwa kwa rushwa ya ngono ikiwa ni

pamoja na ukosefu wa huduma za msingi kwa wanafunzi kama vile nyumba za kulala (hostels),

mikopo, pamoja na mifumo ya ajira za wakufunzi isiyozingatia weledi na maadili ya kazi

kwenye baadhi ya taasisi za elimu (teaching ethics).

Aidha, utafiti umebaini kuwa Sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Na. 11/2007 inatoa

mwanya kwa wasio na mamlaka kuwashawishi kwa makusudi wenye mamlaka kuwapa ngono.

Jambo hili lilifanikiwa kutokana na wahadhiri au watumishi wasio waadilifu wa kutozingatia

kanuni na taratibu zinazowaongoza kwenye utendaji wao.

Mapendekezo

Kutokana na matokeo tajwa, utafiti umebainisha mapendekezo machache yaliyotokana na

mijadala ya washiriki wa utafiti huu. Umuhimu wa kuboresha na kuimarisha mifumo ya

uwajibikaji kwenye kupambana na rushwa ya ngono ulijitokeza kama eneo la kipaumbele

kwenye kupambana na tatizo la rushwa ya ngono ndani ya vyuo vya elimu ya juu na taasisi

nyingine za umma na za sekta binafsi. Mapendekezo yalibainishwa kwa kila mdau:

Serikali

Iuwajibishe uongozi wa vyuo vikuu kwenye kujenga mazingira wezeshi na salama kwa

wanafunzi na wafanyakazi katika ngazi zote ili kuwezesha wanafunzi wa kike na kiume

kupata na kufaidi haki ya elimu katika ngazi hii pamoja na kuwezesha upatikanaji wa

elimu bora;

Page 8: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

vii

Iimarishe mifumo ya ajira ya wafanyakazi wote, hususan wakufunzi na viongozi kwa

kuwapa mafunzo ya ualimu na uongozi wale wote wenye kuajiriwa chuoni ili kuwapa

nyenzo za uwajibikaji wa kuzingatia maadili ya kufundisha na kuongoza katika taasisi za

elimu;

Iongeze fedha za uendeshaji vyuoni na hususan zinazohitajika kwenye kuimarisha

huduma za kuwezesha kuboresha utoaji wa elimu ikiwa ni pamoja na huduma za malazi

kwa wanafunzi ili kupunguza mianya inayotumiwa na wasimamizi na watoa huduma hizi

kwa kuweka sharti la ngono kwa wanafunzi;

Isimamie uwajibikaji wa uongozi wa chuo kuhusu masuala ya jinsia na hususan rushwa

ya ngono kwa kuwawajibisha viongozi waimarishe Kamati za Maadili ndani ya vyuo;

Kuendelea kuijengea uwezo TAKUKURU wa kuweza kuchunguza na kumfikisha

mtuhumiwa mahakamani bila kuhitaji kibali cha Mkurugenzi wa Mashtaka; na

Ifanye mapitio ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11/2007 ili

kuimarisha mapambano dhidi ya rushwa ya ngono.

Uongozi wa Vyuo

Uboreshe mifumo ya udhibiti na uwajibikaji kwenye kuimarisha mifumo ya kusimamia

maadili, mifumo ya utahini, mifumo ya kutoa taarifa na kulinda watoa taarifa pamoja na

kuwajibisha watuhumiwa wa vitendo hivyo;

Uimarishe taasisi na kamati zinazoshughulikia masuala ya maadili ya watumishi wake

ikiwa ni pamoja na kamati za maadili, vitengo vya jinsia, ofisi ya mshauri wa wanafunzi

kwa kuwapatia nyenzo, vitendea kazi na mafunzo ya kuwawezesha kushughulikia

masuala ya rushwa ya ngono pamoja na unyanyasaji wa kijinsia kwenye vyuo; na

Uimarishe mahusiano na TAKUKURU kwenye kutoa elimu, kupeleleza na kuchukua

hatua stahiki kwa wale wote wenye kutuhumiwa kujihusuisha na vitendo vya rushwa ya

ngono.

Page 9: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

viii

Vitengo/Taasisi za Jinsia

Kujijengea uwezo wa uelewa wa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na.

11/2007 kuhusu rushwa ya ngono ili waweze kusimamia utekelezaji wake vyuoni; na

Kuwajengea wanafunzi na jamii yote ya chuo uelewa wa suala la rushwa ya ngono ili

waweze kujitetea na kupambana nalo.

Asasi za kiraia

Kutumia taarifa hii kuimarisha vita dhidi ya rushwa ya ngono;

Kuendeleza na kuimarisha ubia kati yake na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na

Rushwa (TAKUKURU) kwenye vita dhidi ya rushwa ya ngono, hasa kwenye utafiti na

elimu ya umma; na

Kujijengea uelewa wa pamoja wa sheria ya Kuzuia na Kupambana na rushwa hususani

vipengele vinavyoelezea rushwa ya ngono ili kuweza kuendeleza mapambano dhidi ya

rushwa ya ngono.

Wanafunzi wa Vyuo

Waongeze jitihada katika masomo, wazingatie maadili, wasikubali kurubuniwa, wavunje

ukimya na kupaza sauti kunapotokea viashiria vya kuwanyima haki zao, na wachukue

hatua stahiki pale wanapopokonywa hizo haki.

Wadai kuimarishwa kwa mikakati iliyobainishwa katika miongozo na sheria ndogondogo

za kuzuia na kudhibiti rushwa ya ngono;

Wafikishe malalamiko yao TAKUKURU kwa kupitia kamati zao, taasisi za kiraia na hata

wao wenyewe; na

Waungane na kushiriki zaidi kwenye kampeni za kupambana na rushwa ya ngono.

Page 10: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

ix

SHUKRANI

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) inatoa shukrani zake za dhati kwa

wadau wote walioshiriki katika kufanikisha utafiti huu. Kwa kuwa sio rahisi kuwataja wote kwa

majina na vyeo, tunaomba wote wapokee shukrani hizi zinazotambua michango yao kwenye

kufanikisha kazi hii. Hata hivyo, TAKUKURU inawiwa kushukuru uongozi, watumishi na

wanafunzi wa Vyuo Vikuu vya Dodoma (UDOM) na Dar es Salaam (UDSM) kwa ushirikiano

wa karibu kwenye mchakato wote wa kukamilisha zoezi hili. Kipekee tunashukuru Mfuko wa

Udhamini wa Wanawake Tanzania (Women Fund Tanzania Trust - WFT) kwa kuwezesha utafiti

huu, Prof. Ruth Meena na Bi. Anneth Meena kwa kutoa utaalam wao katika utafiti huu, Dkt.

Alfred Wimana Sebahene wa Chuo Kikuu cha St. John na Dkt. Tatu Mkiwa Nyange wa Chuo

Kikuu cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kwa kushiriki katika kufanikisha utafiti huu.

Page 11: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

x

YALIYOMO

MUHTASARI RASMI (EXECUTIVE SUMMARY)................................................................................... i

SHUKRANI ................................................................................................................................................. ix

YALIYOMO ................................................................................................................................................. x

ORODHA YA MAJEDWALI .................................................................................................................... xii

ORODHA YA VIFUPISHO ...................................................................................................................... xiii

SURA YA KWANZA .................................................................................................................................. 1

1.0 UTANGULIZI .............................................................................................................................. 1

1.1 Maelezo ya tatizo .......................................................................................................................... 2

1.2 Lengo kuu ..................................................................................................................................... 2

1.3 Madhumuni mahsusi ..................................................................................................................... 2

1.4 Maswali ya utafiti ......................................................................................................................... 3

1.5 Umuhimu wa utafiti ...................................................................................................................... 3

SURA YA PILI ............................................................................................................................................. 5

2.0 MAPITIO YA MACHAPISHO .................................................................................................... 5

2.1 Nadharia ya utafiti ............................................................................................................................... 5

2.1.1 Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania Na. 11/2007 .......................................... 5

2.1.2 Kanuni za Mienendo na Maadili kwa Watumishi wa Umma ...................................................... 6

2.1.3 Kanuni za Utumishi wa Umma, 2014 .......................................................................................... 7

2.1.4 Kanuni za Maadili kwa Watumishi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Dodoma ................. 8

2.3 Ukubwa wa tatizo ............................................................................................................................... 9

2.4 Kiunzi cha dhana ............................................................................................................................... 11

2.5 Maana tumizi .................................................................................................................................... 11

2.5.1 Rushwa ya ngono ....................................................................................................................... 11

2.5.2 Huduma ...................................................................................................................................... 12

2.5.3 Mamlaka .................................................................................................................................... 12

Page 12: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

xi

SURA YA TATU ....................................................................................................................................... 13

3.0 MBINU ZA UTAFITI ................................................................................................................ 13

3.1 Usanifu wa utafiti ........................................................................................................................ 13

3.2 Eneo na muda wa utafiti .............................................................................................................. 13

3.3 Sampuli ............................................................................................................................................ 14

3.4 Ukubwa wa sampuli ........................................................................................................................ 14

3.5 Mbinu za ukusanyaji wa taarifa ....................................................................................................... 14

3.6 Uchambuzi wa taarifa ................................................................................................................. 16

SURA YA NNE .......................................................................................................................................... 17

4.0 MATOKEO YA UTAFITI ................................................................................................................... 17

4.1 Wasifu wa wahojiwa ......................................................................................................................... 17

4.2 Uwepo wa rushwa ya ngono ............................................................................................................. 18

4.3 Sababu za kuwepo vitendo vya rushwa ya ngono ............................................................................. 20

4.4 Mifumo ya udhibiti ya ndani dhidi ya rushwa ya ngono .................................................................. 24

4.5 Mbinu zinazotumika kushawishi rushwa ya ngono .......................................................................... 30

SURA YA TANO ....................................................................................................................................... 35

5.0 HITIMISHO NA MAPENDEKEZO .................................................................................................... 35

5.1 Hitimisho........................................................................................................................................... 35

5.2 Mapendekezo .................................................................................................................................... 37

Marejeo ....................................................................................................................................................... 40

VIAMBATISHO......................................................................................................................................... 42

Page 13: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

xii

ORODHA YA MAJEDWALI

Jedwali 1: Mgawanyo wa hojaji.................................................................................................................. 15

Jedwali 2: Idadi ya makundi kwenye majadiliano ya vikundi .................................................................... 15

Jedwali 3: Idadi ya wahojiwa lengwa ......................................................................................................... 16

Jedwali 4: Wasifu wahojiwa kwa njia ya hojaji .......................................................................................... 17

Jedwali 5: Mwitiko wa uelewa wa dhana ya na uwepo wa rushwa ya ngono ............................................ 19

Jedwali 6: Mwitiko wa wahojiwa kuhusu sababu za rushwa ya ngono ...................................................... 21

Jedwali 7: Mwitiko wa wahojiwa kuhusu uwepo wa sera, miongozo na taratibu za udhibiti rushwa ya

ngono .......................................................................................................................................................... 25

Jedwali 8: Mwitiko wa wahojiwa kuhusu mbinu zinazotumika kushawishi rushwa ya ngono .................. 31

Page 14: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

xiii

ORODHA YA VIFUPISHO

ARIS - Academic Registration Information System

FGD - Focus Group Discussion

JMT - Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

MUCE - Mkwawa University College of Education

TAKUKURU - Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa

TAMWA - Tanzania Media Women Association

TI - Transparent International

TWJA - Tanzania Women Judges Association

SPSS - Statistical Package for the Social Sciences

UDSM - University of Dar es Salaam

UDOM - University of Dodoma

WFT - Women Fund Tanzania – Trust

Page 15: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

1

SURA YA KWANZA

1.0 UTANGULIZI

Rushwa ya ngono inafasiliwa na wanazuoni kama matumizi mabaya ya madaraka, ili

kujinufaisha kingono visivyo halali au pasipo kuwa na makubaliano ya pande zote mbili

zinazohusika katika ngono (Tanzania Women Judge Association, 2011; Yusuph, 2016). Aina hii

ya rushwa haitumii fedha au vitu kushawishi ila hutumia nguvu ya kisaikolojia kumshawishi

mhanga kutoa mwili wake kingono ili kupata huduma au haki. Mhusika anayedai aina hii ya

rushwa ni lazima awe na madaraka au mamlaka ambayo anaamua kuyatumia vibaya kwa

kujaribu kushawishi au kukubali kupewa ngono kubadilishana na utekelezaji wa mamlaka yale

aliyonayo. Watu wa namna hii hutumia madaraka au mamlaka waliyonayo kwa lengo la

kujinufaisha wao wenyewe na siyo kutumia mamlaka hayo kutekeleza majukumu yao kama

inavyotarajiwa na kwa kuzingatia weledi, uadilifu, sheria na usawa.

Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007 imeharamisha rushwa ya

ngono kwa kukataza mtu yeyote mwenye mamlaka kutumia mamlaka aliyonayo katika

kutekeleza majukumu yake kudai au kulazimisha upendeleo wa kingono au upendeleo mwingine

wowote kama kigezo cha kutoa ajira, kupandisha cheo, kutoa haki au upendeleo wowote

unaotambulika kisheria. Aidha, hivi karibuni, Serikali kupitia Bunge la Jamhuri ya Muungano

wa Tanzania imefanya maboresho ya sheria mbalimbali ikiwemo Sheria ya Uhujumu Uchumi1.

Kupitia maboresho hayo, kosa la rushwa ya ngono limetajwa kuwa moja ya makosa ya uhujumu

uchumi2 na adhabu yake kwa mtu anayekutwa na hatia ni kifungo kisichopungua miaka 20 na

kisichozidi miaka 30 au kifungo pamoja na adhabu nyingine yoyote chini ya sheria hiyo na

iwapo sheria nyingine itatoa adhabu kali zaidi ya adhabu iliyotolewa na Sheria ya Uhujumu

Uchumi kupitia mabadiliko tajwa hapo juu basi Mahakama imeruhusiwa kutoa adhabu hiyo

ambayo ni kubwa.3

1 No.3 Written Laws (Miscellaneous Amendments) Act 2016

2 Section 16(b) of the Written Laws (Miscellaneous Amendments) Act 2016

3 Section 13 (3) Written Laws (Miscellaneous Amendments) Act 2016 "(2) Notwithstanding provision of a different

penalty under any other law and subject to subsection (3), a person convicted of corruption or economic offence

shall be liable to imprisonment for a term of not less than twenty years but not exceeding thirty years, or to both that

Page 16: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

2

Hata hivyo, pamoja na kuwepo kwa sheria, taratibu na kanuni za maadili na mienendo (Codes of

conduct and ethics) ambazo kimsingi zinaharamisha vitendo vyote vya unyanyasaji wa kijinsia

(sexual harassment), rushwa ya ngono bado ni tatizo linaloisumbua jamii. Tatizo hili linachangia

kuzalisha wataalam wasio na weledi kwa kurudisha nyuma ubora wa elimu inayotolewa katika

vyuo vya elimu ya juu nchini. Taasisi za elimu ya juu ni viwanda vya kuandaa wataalam

wanaotarajiwa kuingia kwenye fani mbalimbali za utoaji huduma, uzalishaji, na kuwa walezi wa

familia. Kwa kuzingatia umuhimu wao, wataalam hao wanapaswa kuhitimu wakiwa wameiva

kimaadili na kiweledi. Hivyo, tatizo hili katika Taasisi za elimu ya juu nchini linahitaji

kuangaliwa kwa ukaribu ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea huko baadae kwa

wanafunzi, wahadhiri na jamii kwa ujumla.

1.1 Maelezo ya tatizo

Kumekuwepo na ongezeko la malalamiko kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo watunga

sera, wanazuoni, wahadhiri, wanafunzi na wananchi kuwa wanafunzi wa kike katika Taasisi za

elimu ya juu (vyuo vikuu) nchini wanalazimishwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na baadhi

ya wahadhiri au watumishi waliopo kwenye nafasi za madaraka ili waweze kupata upendeleo au

haki. Malalamiko hayo yamejitokeza kwenye mitandao ya kijamii yakidai kwamba rushwa ya

ngono imekithiri katika vyuo vikuu (Mwai, 2018). Pamoja na kuwepo kwa malalamiko haya,

hakuna taarifa rasmi kutoka vyuo vikuu zilizofikia TAKUKURU kwa ajili ya kuchunguza na

kuchukua hatua stahiki za kukabiliana na tatizo hilo kwenye vyuo vya elimu ya juu.

1.2 Lengo kuu

Lengo la utafiti huu ni kuwezesha upatikanaji wa taarifa za kisayansi zitakazosaidia kukabiliana

na vitendo vya rushwa ya ngono katika Taasisi za elimu ya juu nchini.

1.3 malengo mahususi

Ili kufikia lengo la utafiti huu, malengo mahususi yafuatayo yaliongoza utafiti huu:-

(i) Kuwezesha kupata taarifa za kina kuhusu kuwepo kwa tatizo la rushwa ya ngono;

imprisonment and any other penal measure provided for under this Act; Provided that, where the law imposes penal

measures greater than those provided by this Act, the Court shall impose such sentence.

Page 17: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

3

(ii) Kuchunguza sababu za kuwepo vitendo vya rushwa ya ngono;

(iii) Kutathmini uwepo na ufanisi wa mifumo ya udhibiti wa ndani ya maadili juu ya vitendo

vya rushwa ya ngono; na

(iv) Kutoa mapendekezo yatakayowezesha Taasisi na Serikali kwa jumla kupambana na

kuzuia rushwa ya ngono kwenye taasisi za elimu ya juu.

1.4 Maswali ya utafiti

(i) Je wadau wanauelewa wa dhana hii ya rushwa ya ngono?

(ii) Je hali ya tatizo la rushwa ya ngono katika chuo hiki ikoje?

(iii) Je nini chanzo cha kuwepo vitendo vya rushwa ya ngono?

(iv) Je kuna mifumo ipi ya udhibiti wa vitendo vya rushwa ya ngono katika Taasisi za

elimu ya juu?

(v) Je kuna ufanisi wa mifumo ya udhibiti wa vitendo vya rushwa ya ngono?

(vi) Je ni mbinu gani zinatumiwa kufanya ushawishi wa rushwa ya ngono katika

Taasisi za elimu ya juu?

(vii) Ni nini kifanyike ili kupambana na hatimaye kuzuia rushwa ya ngono

1.5 Umuhimu wa utafiti

Utafiti huu ni muhimu kwa sababu zifuatazo: -

(i) Utaisaidia Serikali kufahamu ukubwa wa tatizo la rushwa ya ngono katika taasisi

za elimu ya juu na namna ya kukabiliana nalo kwani ni dhahiri kuwa kwa sasa

hakuna taarifa sahihi juu ya ukubwa wa tatizo hili;

(ii) Kuweka msingi kwa ajili ya kufanya utafiti wa kina utakaohusisha sampuli kubwa

na wigo mpana kwa siku za usoni. Hii ni kwa sababu taarifa zilizopo kwa sasa ni

finyu na hazitoshelezi kufanyika kwa marekebisho ya kisera na kisheria;

(iii) Utasaidia kuongeza mwamko kwa jamii kuhusu tatizo na madhara ya rushwa ya

ngono nchini;

(iv) Utasaidia kuongeza kasi ya kupambana na tatizo la rushwa katika sekta ya elimu

na hasa wakati huu ambapo Serikali imeonesha dhamira ya kweli ya kutokomeza

rushwa na vitendo vyote vya ufisadi; na

Page 18: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

4

(v) Utasaidia kufahamu iwapo kanuni za mienendo/maadili za vyuo vikuu zimesaidia

kudhibiti rushwa ya ngono au la, na hatua sahihi zinazopaswa kuchukuliwa.

Page 19: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

5

SURA YA PILI

2.0 MAPITIO YA MACHAPISHO

Sura hii inahusisha mapitio ya machapisho mbalimbali; ikijumuisha uchambuzi wa maandiko

mbalimbali, kanuni, Sheria na taratibu zilizoandikwa kuhusu rushwa na rushwa ya ngono.

2.1 Nadharia ya utafiti

2.1.1 Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania Na. 11/2007

Lengo kuu la Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11/2007 ni kukuza utawala bora

na kutokomeza rushwa. Katika kufanikisha hayo sheria inatoa msingi wa kitaasisi na kisheria

kuwezesha kuzuia na kupambana na rushwa kwa njia tofauti zikiwa ni pamoja na kuelimisha,

kuchambua mifumo ya utendaji wa Taasisi za umma na binafsi, na kuchunguza.4 Sheria hii

imeweka kifungu mahususi cha kuzuia rushwa ya ngono ambacho kinabainisha kuwa ni kosa

kwa mtu mwenye mamlaka kudai au kuomba rushwa ya ngono kwa mtu yeyote kama sharti la

kutoa ajira, upendeleo, kumpandisha cheo, kumpatia haki au huduma maalum.5

Sheria ya Kuzuia na Kupambana namba 11 ya mwaka 2007 imetamka kosa hili chini ya kifungu

cha 25, kama kinavyoeleza:

“Any person being in a position of power or authority, who in the exercise of

his authority, demands or imposes sexual favours or any other favour on any

person as a condition for giving employment, a promotion, a right, a privilege

or any preferential treatment, commits an offence….”

Ambapo kwa tafsiri isiyo rasmi kifungu hiki kinasema:

“Mtu yeyote mwenye mamlaka katika kutekeleza majukumu yake anadai,

anaweka sharti la ngono au upendeleo mwingine wowote kama kigezo cha

kutoa ajira, kupandisha cheo, kutoa haki au upendeleo wowote unaotambulika

kisheria atakuwa ametenda kosa.”

4 Kifungu cha 7 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na rushwa

5 Kifungu cha 25 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11/2007

Page 20: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

6

Kifungu kinabainisha mambo muhimu yanayosababisha au uwepo wake yanatengeneza rushwa

ya ngono, ambayo: Kwanza, mtu mwenye mamlaka ambapo kwa mazingira ya Taasisi za Elimu

ya juu ni Wahadhiri na Watawala. Pili, Katika utekelezaji wa majukumu yake kama vile kutoa

alama kwenye mitihani, kupandisha vyeo, uhamisho na malazi. Tatu, Kumwekea sharti la ngono

mtaka huduma kama mwanafunzi au mtumishi wa chuo ili kupata huduma au upendeleo

wowote.

Aidha, hivi karibuni, Serikali kupitia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanya

maboresho ya sheria mbalimbali ikiwemo Sheria ya Uhujumu Uchumi6. Kupitia maboresho

hayo, kosa la rushwa ya ngono limetajwa kuwa moja ya makosa ya uhujumu uchumi7 na adhabu

yake kwa mtu anayekutwa na hatia ni kifungo kisichopungua miaka 20 na kisichozidi miaka 30

au kifungo pamoja na adhabu nyingine yoyote chini ya sheria hiyo na iwapo sheria nyingine

itatoa adhabu kali zaidi ya adhabu iliyotolewa na Sheria ya Uhujumu Uchumi kupitia mabadiliko

tajwa hapo juu basi Mahakama imeruhusiwa kutoa adhabu hiyo ambayo ni kubwa.8

Hata hivyo nadharia hii imeonesha udhaifu kama wa kutoharamisha ukuadi, mhitaji huduma

kutoa rushwa ya ngono kwa mtoa huduma na mazingira ambayo upande wa mtoaji na mpewa

huduma wanapokubaliana kupeana rushwa ya ngono. Kanuni za mienendo na maadili kwa

watumishi wa umma, kanuni za utumishi wa umma, kanuni za maadili kwa watumishi na

wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Dodoma zinaweza kusaidia katika udhibiti wa

rushwa ya ngono.

2.1.2 Kanuni za Mienendo na Maadili kwa Watumishi wa Umma

Kanuni hizi zilizotengenezwa chini ya Sheria ya Utumishi wa Umma zinakataza mtumishi

yeyote wa umma kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtumishi mwenzake au mtu mwingine

katika eneo la kazi na vitendo vyovyote vile vyenye kusababisha usumbufu wa kingono (Sexual

6 No.3 Written Laws (Miscellaneous Amendments) Act 2016

7 Section 16(b) of the Written Laws (Miscellaneous Amendments) Act 2016

8 Section 13 (3) Written Laws (Miscellaneous Amendments) Act 2016 "(2) Notwithstanding provision of a different

penalty under any other law and subject to subsection (3), a person convicted of corruption or economic offence

shall be liable to imprisonment for a term of not less than twenty years but not exceeding thirty years, or to both that

imprisonment and any other penal measure provided for under this Act; Provided that, where the law imposes penal

measures greater than those provided by this Act, the Court shall impose such sentence.

Page 21: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

7

harassment) mahala pa kazi. Aidha, kanuni zimekataza mtumishi yeyote kuweka sharti la ngono

kwa mtumishi mwenzake; kubaka, kutomasa, kumshikashika mtumishi kwa makusudi kwa

namna inayoashiria uhitaji wa ngono, kufanya au kuonesha ishara za vitendo, kelele na utani

wenye kuashiria uhitaji wa ngono na kutoa maoni ya kingono dhidi ya mtumishi mwenzake.9 Hii

inamaanisha kuwa, wahadhiri au watumishi wa vyuo vya elimu ya juu wanakatazwa na kanuni

hizi kujihusisha na masuala ya rushwa ya ngono baina yao na watumishi wengine au wanafunzi

wanaowafundisha na au kuweka masharti ya kingono katika kutoa haki au huduma. Hivyo,

wanawajibika kiweledi kukataa vishawishi vyovyote vya kingono vinavyofanywa na watumishi

wenzao au wanafunzi ikiwa ni kwa lengo la kujipatia manufaa kutoka kwa mhadhiri au mtumishi

mwingine wa chuo.

2.1.3 Kanuni za Utumishi wa Umma, 2014

Kanuni za utumishi wa umma zimeweka makatazo mbalimbali ambayo kimsingi yanalenga

kuzuia rushwa ya ngono katika utumishi wa umma. Kanuni ya 35 imeweka wazi kuwa ni

marufuku kwa mtumishi wa umma akiwa katika kituo chake cha kazi au nje, kujihusisha na

vitendo ambavyo vinakiuka maadili ya jamii yakiwemo ujeuri, matusi, lugha chafu au aina

yoyote ya udhalilishaji wa kijinsia ambao utapelekea ukiukwaji wa Haki za Binadamu. Katazo

hili kimsingi limegusa rushwa ya ngono kwani rushwa ya ngono inadhalilisha jinsi, inakiuka

haki za binadamu na iko kinyume na maadili ya watanzania.

Vilevile, kanuni ya 36 imepiga marufuku kwa mwajiri au mtumishi wa umma kufanya aina

yoyote ya udhalilishaji wa kijinsia kwa kumtaka mwajiriwa kufanya ngono au kufanya aina

yoyote itakayopelekea kufanyika ngono kama kigezo cha ahadi ya kupendelewa kazini, au

kulazimisha ngono ili mwajiriwa kuepuka vitisho ambavyo vitaathiri ajira yake au kutumia

kigezo cha ngono ili mwajiriwa aepuke vitisho dhidi ya maslahi ya sasa au ya baadae katika ajira

yake.

Aidha, mwajiri amekatazwa na kanuni kutumia lugha isiyostahiki inayoashiria kutaka ngono, au

kuonesha tabia ya wazi ya kufanya ngono kama vile kujishika sehemu za siri au kufanya kitendo

chochote kinachoashiria ufanyikaji wa ngono.

9 Kanuni II (6) ya Kanuni za Mienendo na Maadili kwa watumishi wa Umma,

Page 22: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

8

Kwa msingi huo, kanuni zimeweka wazi kuwa mtu yeyote atakayefanya matendo ya ngono kama

yalivyofafanuliwa atachukuliwa hatua za kinidhamu au jinai. Ikiwa kosa hilo ni la jinai mhusika

atafikishwa katika vyombo vya sheria ikiwemo TAKUKURU.

Pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuweka msingi wa kisheria na

kikanuni wa kukataza rushwa ya ngono, bado taasisi za elimu ya juu nchini, kila moja kwa nafasi

yake, zimeweka kanuni mbalimbali za maadili zinazobatilisha mahusiano ya kingono baina ya

wanafunzi na wahadhiri au watumishi wa Taasisi husika.

2.1.4 Kanuni za Maadili kwa Watumishi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Dodoma

Kanuni za maadili kwa watumishi na wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam za mwaka

2018 zinabatilisha na kutoa katazo la kutumia rushwa ya ngono kutoa ufaulu, kufanya vitendo

vinavyoashiria ngono, au kufanya mawasiliano yanayoashiria uhitaji wa rushwa ya ngono.

Aidha, kanuni hizo zinakataza kumsumbua au kumnyanyasa mtu yeyote yule anayetoa taarifa

juu ya unyanyasaji wa kingono (UDSM, 2018).

Kwa upande wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Kanuni ya 3.8 imeweka katazo kwa mtumishi yeyote

wa chuo kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi na mwanafunzi ambaye wana uhusiano wa

moja kwa moja wa kimasomo. Aidha, watumishi wa ngazi ya juu katika chuo wamekatazwa

kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi wanaowasimamia ili kuepuka kushusha

hadhi ya chuo, maadili pamoja na weledi katika utekelezaji wa majukumu ya chuo. Pia, kanuni

hizo zimekataza mtumishi yeyote kushikanashikana na mwanafunzi akiwa na lengo la kuhitaji

ngono kutoka kwa mwanafunzi huyo na kwa mujibu wa Kanuni hizo, ni marufuku mwanafunzi

au mhadhiri kumdhalilisha kijinsia mwanafunzi, mtumishi au mteja kwa kuomba kufanya naye

ngono, na matendo mengine yote yanayoashiria uhitaji wa kufanya ngono.10

Kwa mujibu wa Mkakati wa Kitaifa wa Kupambana na Rushwa na Mpango wa Utekelezaji:

Awamu ya tatu 2017-2022, taasisi zote za umma vikiwemo vyuo vikuu vyote nchini vinatakiwa

10 Rule 3.10 of The University of Dodoma, 2012

Page 23: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

9

kuwa na kamati za kudhibiti uadilifu. Kamati hizi ni muhimu katika kuandaa, kutekeleza na

kutathmini mkakati wa mapambano dhidi ya rushwa.

2.3 Ukubwa wa tatizo

Mara nyingi rushwa ya ngono ni eneo tete ambalo taarifa zake haziwafikii watendaji kwa sababu

ya ukimya wa wahanga. Kwa mfano, kuanzia mwaka 2013 hadi Machi 2020, Taasisi ya Kuzuia

na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imeshughulikia taarifa za malalamiko ya rushwa ya

ngono ambapo majalada 23 yalifunguliwa katika mikoa ifuatayo: Mwanza (4), Kagera (3),

Mtwara (3), Mara (3), Mara (3), Arusha (1), Dodoma (1), Geita (1), Iringa (1), Katavi (1),

Kinondoni (1), Manyara (1), Rukwa (1), Singida (1) na Temeke (1). Jumla ya Kesi 10

zilifunguliwa mahakamani, ambapo Kesi 5 zilishinda (Conviction), na kati ya hizo, nne zilihusu

Taasisi za Elimu. Utafiti uliofanywa na Chama cha Wanahabari Wanawake (TAMWA) nchini

ulieleza kuwa wanawake asilimia 89 walioajiriwa katika sekta ya umma nchini wamewahi

kuombwa rushwa ya ngono wakati wa kuajiriwa, kupandishwa vyeo au wakati wakihitaji

huduma fulani (TAMWA, 2012). Utafiti mwingine uliofanywa nchini Rwanda na shirika

linalojihusisha na tafiti za masuala ya rushwa duniani la Transparent International (TI)

unaonesha kuwa jinsi ya kike ni waathirika wakubwa wa vitendo vya rushwa ya ngono nchini

humo. Utafiti huo unaonesha kuwa asilimia 84.5 ya vitendo vya rushwa ya ngono hufanyika

kwa wanawake ambapo asilimia 15.4 hufanywa kwa wanaume11

. Tafiti hizo zote zinaonesha

kuwa jinsi ya kike imekuwa ikiathiriwa zaidi na vitendo vya rushwa ya ngono kuliko jinsi ya

kiume katika maeneo mbalimbali. Hali kadhalika, katika Taasisi za elimu za juu, wanafunzi wa

jinsi ya kike wamekuwa wakilalamika zaidi kuwa wanatakwa rushwa ya ngono na wahadhiri au

watumishi wengine wa Taasisi hizo.

Aidha, Hoyce Temu (2007), mmoja wa waandishi maarufu wa habari za kijamii katika kitabu

chake kiitwacho “Nayakumbuka yote” ameeleza kuwa, aliwahi kusitisha masomo katika moja ya

Taasisi ya elimu ya juu nchini kutokana na kubughudhiwa na wahadhiri kwa lengo la kutoa

rushwa ya ngono.

11

Transparency International (7 march, 2016) Sextortion: Undermining Gender Equality

https://www.transparency.org/news/feature/sextortion_undermining_gender_equality

Page 24: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

10

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan wakati akifungua Mkutano wa Nane wa Chama cha

Majaji Wanawake Tanzania (TAWJA), alikiri kwamba suala la rushwa ya ngono limeendelea

kuwa tishio nchini hadi kusababisha wanawake wengi kujiengua katika nafasi zao. Mheshimiwa

Samia alisema “Ni jambo la kuvunja moyo, kuona kwamba katika Karne ya 21 suala la rushwa

ya ngono, linaendelea na kusababisha wanawake wengi kujiengua katika nafasi zao. Matumaini,

matarajio na ndoto za wanawake, zimekuwa zikikatishwa na watu wachache ambao ni hatarishi,

hivyo tunahitaji kufanya kazi kuhakikisha kwamba tunawasaidia kwa hali na mali kwa sababu

wahanga hao wanaweza kuwa mama yako, dada, mke na binti yako,‟‟12

Utafiti huu ulilenga kutoa taarifa zaidi kuhusu kuwepo kwa tatizo lenye madhara makubwa kwa

taifa letu ili kuendelea kuchukua hatua stahiki za kupambana nalo. Rushwa ya Ngono ina

madhara kwa jamii kiuchumi, kisiasa, kiustawi wa jamii, kidemokrasia na kiutekelezwaji wa

haki za binadamu. Licha ya athari kwa wahanga wa rushwa ya ngono, rushwa hii huathiri taifa

katika ngazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na ngazi ya taifa, mhanga na jamii.

Katika ngazi ya Taifa, rushwa ya ngono inadhalilisha taifa zima kiujumla: pale ambapo taifa na

vyombo vya dola vinapopuuza hali hii inakinzana na matamko mbalimbali ambayo nchi

imeridhia kimataifa, kikanda na kwa kupita Katiba ya nchi. Kwa hivyo basi, rushwa ya ngono ni

ukiukwaji wa haki za binadamu.

Kiuchumi nchi inashindwa kutumia vipaji vyake kiufanisi pale ambapo wasio na sifa wanapewa

nafasi na kuwanyima wenye sifa. Au pale ambapo nguvu kazi kubwa inatumika kushughulikia

rushwa ya ngono. Vilevile, inadumaza jitihada za kupambana na umaskini, kujenga na

kuimarisha demokrasia shirikishi na utawala bora.

Katika ngazi ya Mhanga, rushwa ya ngono hugeuza haki za wahanga kuwa ni upendeleo na siyo

stahiki yake. Inapohusu kumpokonya mtu haki yake husababisha madhara kwenye nyanja

mbalimbali: inamnyima huyu mhanga stahiki yake hivyo inagusa maisha ya mhusika kwani

anapolazimika kushiriki kwenye rushwa ya ngono, anaweza kupata jeraha lisilotibika kwenye

12

Makamu wa Rais Mh. Samia Suluhu Hassan aliyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa Nane wa chama cha

Majaji Wanawake Tanzania 2017. http://mwaseba5.blogspot.com/2017/01/rushwa-ya-ngono-bado-ni-tishio-

nchini.html

Page 25: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

11

maisha yake, mahala pengine anaweza kugeuzwa mtumwa wa ngono, na hivyo kushindwa

kukuza vipaji vyake vya uhalisia.

Katika ngazi ya Jamii, rushwa ya ngono husababisha jamii kukosa huduma bora kutokana na

watoa huduma waliopatikana kutokana na rushwa ya ngono kutokuwa na weledi na maadili ya

kutosha. Aidha, baadhi ya waathirika waliolazimishwa rushwa ya ngono wanakuwa na msongo

wa mawazo kitu kinachosababisha magonjwa ya afya ya akili.

Kwa muhtasari rushwa ya ngono ina madhara mengi yakiwemo ya kunyima haki za kikatiba

kama kugeuza stahiki kuwa upendeleo, kudhalilisha utu wa waathirika, kusabisha matumizi

mabaya ya rasilimali watu pamoja na kudumaza uchumi na maendeleo ya nchi kwa ujumla.

2.4 Kiunzi cha dhana

Rushwa ya ngono ni matokeo ya mambo makuu matatu: Kwanza, mtu mwenye mamlaka

ambapo kwa mazingira ya Taasisi za Elimu ya juu ni Wahadhiri na Watawala. Pili, katika

utekelezaji wa majukumu yake kama vile kutoa alama kwenye mitihani, kupandisha vyeo,

uhamisho na malazi. Tatu, kumwekea sharti la ngono mtaka huduma kama mwanafunzi au

mtumishi wa chuo ili kupata huduma au upendeleo wowote.

2.5 Maana tumizi

2.5.1 Rushwa ya ngono

Katika utafiti huu, rushwa ya ngono inamaanisha matumizi mabaya ya madaraka ili kujinufaisha

kingono isivyo halali. Aidha rushwa ya ngono hugeuza haki na stahiki kuwa ni upendeleo. Aina

hii ya rushwa haitumii fedha au vitu kushawishi ila hutumia nguvu ya kisaikolojia kumshawishi

mhanga kutoa mwili wake kingono ili kupata huduma au haki. Aidha, mhusika anayedai aina hii

ya rushwa ni lazima awe na madaraka au mamlaka ambayo anaamua kuyatumia vibaya kwa

kudai ngono ili atoe upendeleo kwa asiyestahili, au kumnyima haki anayestahili kwa kitendo cha

kukataa rushwa ya ngono.

Page 26: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

12

2.5.2 Huduma

Huduma katika utafiti huu ni mahitaji ambayo anayahitaji mtumishi wa chuo au mwanafunzi

anapokuwa katika mazingira ya chuo kama vile kudahili, malazi, mikopo, kufundisha, kutunga

mitihani, kusahihisha, kutoa alama, ufadhili wa masomo, kupandisha vyeo, kuhamisha na kuajiri.

2.5.3 Mamlaka

Katika utafiti huu, Mamlaka ni dhamana ya kufanya au kutoa maamuzi kuhusu huduma

zinazotolewa na chuo.

Page 27: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

13

SURA YA TATU

3.0 MBINU ZA UTAFITI

Sura hii inaainisha eneo la utafiti, mbinu za kukusanya taarifa, vyanzo vya taarifa, sampuli na

mbinu za uchambuzi wa matokeo ya utafiti.

3.1 Usanifu wa utafiti

Utafiti huu ulitumia mbinu ya uchunguzi kifani (case study) kukusanya taarifa za utafiti. Kupitia

mbinu hii data za kitaamuli (qualitative data) na data za kitakwimu (quantitative data)

zilikusanywa ili kujibu maswali ya utafiti. Njia hii ilitumika kuchunguza kwa kina vyuo vikuu

viwili vya umma nchini, kulinganisha na kutofautisha namna, aina, na sababu za vitendo vya

rushwa ya ngono katika vyuo hivyo. Matumizi ya mbinu hii yalizingatia manufaa ya kupata

taarifa za kina kuhusu rushwa ya ngono na namna inavyotendeka katika vyuo vikuu na matumizi

ya njia zaidi ya moja ya ukusanyaji wa taarifa – mfano; mahojiano, uchambuzi wa nyaraka,

mijadala ya vikundi ya wazi na ushuhudiaji ili kufikia malengo ya utafiti.

3.2 Eneo na muda wa utafiti

Utafiti huu ulifanyika katika vyuo vikuu vya Dar es Salaam na Dodoma kwa kipindi cha Januari

na Februari 2020. Chuo kikuu cha Dar Es Salaam ndiyo chuo kikuu cha kwanza cha umma hapa

nchini kilichozalisha viongozi wengi kuliko vyuo vyote. Vilevile, ni chuo kikubwa nchini na

kinachodahili wanafunzi wengi zaidi. Kwa mwaka 2017/2018 pekee, chuo hiki kilifanya udahili

wa wanafunzi 13,626 ambao ni sawa na 21% ya wanafunzi wote waliodahiliwa kwenye taasisi

za elimu ya juu nchini kwa mwaka.

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ni chuo cha pili cha umma kilichopo makao makuu ya nchi.

Chuo hiki kina ndaki saba ambazo zinapokea wanafunzi kila mwaka wa masomo. Kwa mwaka

wa masomo 2017/2018, chuo hiki kilidahili wanafunzi 9,151 (Tanzania Commission for

Universities – TCU, 2018).

Hivyo, vyuo hivi viwili vilihusishwa katika utafiti huu kutokana na historia ya vyuo hivi,

umiliki wake (vyuo vya umma) na wingi wa udahili wa wanafunzi. Hivi ndivyo vyuo vikuu

vikubwa viwili vinavyomilikiwa na Serikali na vinavyoongoza kwa kudahili wanafunzi wengi

zaidi nchini. Aidha, kutokana na ukubwa wake na idadi kubwa ya wanafunzi nchini, utafiti

Page 28: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

14

uliona kuwa ni sehemu sahihi ya kuweza kuchunguza na kujenga msingi wa kisayansi kuhusu

rushwa ya ngono nchini.

3.3 Sampuli

Sampuli iliyohusika katika utafiti huu ilipatikana kwa utaratibu wa mpangilio maalum

(Purposive sampling), usampulishaji tajwa (snowball sampling) na usampulishaji nasibu tabaki

(Stratified random sampling). Utaratibu wa mpangilio maalum ulitumika kuwapata wasailiwa

waliopatikana kutokana na vyeo vyao au nafasi zao na uzoefu wao katika Taasisi za elimu ya

juu. Usampulishaji tajwa ulitumika kupata waathiriwa wa vitendo vya rushwa ya ngono. Aidha,

usampulishaji nasibu tabaki ulitumika kupata wanafunzi na watumishi katika maeneo ya utafiti

waliofikiwa na utafiti huu ambapo waligawanywa kwenye tabaki kwa kuzingatia ndaki, vitivo,

shule na idara zao.

3.4 Ukubwa wa sampuli

Utafiti huu uliwahusisha wahojiwa 589: kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam (352) na chuo

kikuu cha Dodoma (237). Utafiti huu umetumia mbinu ya uchunguzi kifani (case study) kwa

lengo la kupata taarifa za kina juu ya namna rushwa ya ngono inavyotendeka katika taasisi za

elimu ya juu zilizofikiwa na utafiti. Waandishi Yin (2012); Crouch and Mckenzie (2006) na

Guest et al., (2006) wanasisitiza kuwa, mbinu hii inataka watafiti kutumia njia mbalimbali

kukusanya data za kina kujibu malengo ya utafiti kuliko kuangalia idadi ya sampuli. Utafiti huu

ulikusanya taarifa za kina na za kutosha kutoka kwa wanafunzi na watumishi 589 wa Vyuo

Vikuu vya Dar es Salaam na Dodoma.

3.5 Mbinu za ukusanyaji wa taarifa

Utafiti huu ulikusanya taarifa za msingi kwa namna tatu: kwanza, kwa kutumia hojaji kwa

watumishi na wanafunzi 589 kama Jedwali 1 linavyoainisha.

Page 29: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

15

Jedwali 1: Mgawanyo wa hojaji

Na Mhusika UDOM UDSM Jumla Jumla

kuu Me Ke Me Ke Me Ke

1 Wahadhiri/watumishi 40 34 40 46 80 80 160

2 Wanafunzi 70 93 132 134 202 227 429

Jumla 110 127 172 180 282 307 589

Me = Wanaume Ke = Wanawake

Pili, kupitia mijadala ya wazi ya vikundi (Focus Group Discussion) tisa (9) ikiwahusisha

watumishi, wahadhiri na wanafunzi (Jedwali 2).

Jedwali 2: Idadi ya makundi kwenye majadiliano ya vikundi

Na. Chuo Idadi ya makundi ya

majadiliano

Idadi ya washiriki

1 UDSM 6 47

2 Dodoma 3 36

Jumla 9 83

Mijadala ya wazi ilifanyika kwa wahadhiri, wanafunzi na watumishi wengine wa vyuo vikuu.

Mijadala hii ilifanyika katika mgawanyo wa kundi la watu kuanzia sita (6) hadi kumi na mbili

(12) kwa kila kundi. Kila kundi la watu lilipatikana kwa kutumia usampulishaji nasibu sahihi

(Simple random sampling) ambapo wanafunzi, wahadhiri na watumishi walichaguliwa kwa

kuzingatia ndaki, vitengo, na idara zao. Mijadala ilifanyika kwa kila kundi kwa kuzingatia jinsi

za washiriki ambapo wahadhiri wa kiume walipatikana kuanzia sita (6), wahadhiri wa kike

kuanzia sita (6), wanafunzi wa kike kuanzia sita (6), wanafunzi wa kiume kuanzia sita (6),

watumishi wasio wahadhiri kuanzia sita (6) wa kiume na wa kike halikadhalika.

Tatu, mahojiano na Wahojiwa Lengwa (key informants) 55 ambao walipatikana kwa njia mbili

za usampulishaji tajwa (snow balling) na kwa utaratibu wa mpangilio maalumu (Purposive

sampling) kama jedwali 3 linavyoonesha.

Page 30: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

16

Jedwali 3: Idadi ya wahojiwa lengwa

Na. Mhusika UDSM UDOM

Idadi Idadi

1 Viongozi wa ngazi ya juu Chuoni

(Makamu Mkuu wa Chuo na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo)

3 3

2 Rasi/Amidi 8 6

3 Kamati ya Maadili, Wakurugenzi wa vitengo mbalimbali na

Mshauri wa Wanafunzi

3 5

4 Viongozi wa Serikali ya Wanafunzi na Klabu ya wapinga

rushwa chuoni

3 8

5 Watalaam wengine wenye uelewa wa kina kuhusu vitendo vya

rushwa ngono Chuoni

9 7

Jumla Kuu 26 29

Taarifa za upili zilikusanywa kwa kupitia nyaraka zinazohusu sheria, kanuni na kumbukumbu

mbalimbali za malalamiko ya vitendo vya rushwa ya ngono. Aidha, takwimu hizo

zilichambuliwa na kutafsiriwa kwa ajili ya kuandaa taarifa ya utafiti.

3.6 Uchambuzi wa taarifa

Utafiti ulitumia programu tumizi ya kuchambua takwimu za kisayansi jamii (SPSS) kuchambua

taarifa zilizokusanywa kwa njia ya madodoso. Aidha, taarifa zilizopatikana kwa njia ya

mahojiano, usaili, na mijadala ya wazi zilichambuliwa kwa kutumia uchanganuzi maudhui

(content analysis).

Page 31: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

17

SURA YA NNE

4.0 MATOKEO YA UTAFITI

4.1 Wasifu wa wahojiwa

Jedwali 4 linaonesha wasifu wa wahojiwa kwa njia ya hojaji kutoka katika vyuo vikuu viwili vya

Umma ambavyo ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Dodoma. Kwa kuzingatia

vigezo vya jinsi, umri, mwaka wa masomo na muda kazini wa wahojiwa hakuna shaka taarifa

zilizopatikana zinajibu malengo ya utafiti huu.

Jedwali 4: Wasifu wahojiwa kwa njia ya hojaji

Kundi Kigeu (variable) Mwitiko

Mdafao

(Frequency)

Chuo

Kikuu

cha Dar

es

Salaam

Mdafao

(Frequency)

Chuo

Kikuu

cha

Dodoma

Wastani

(%)

Wanafunzi Jinsi Wanaume 132 49 70 46 47.5

Wanawake 134 51 93 54 52.5

Umri 18 – 25 237 89 149 91 90.0

26 – 30 22 8 11 7 7.5

31 – 35 7 3 3 2 2.5

Mwaka

wa

masomo

Mwaka wa

kwanza

37 14 50 31 22.5

Mwaka wa

pili

81 31 43 26 28.5

Mwaka wa

tatu

110 41 60 36 38.5

Mwaka wa

nne

38 14 10 7 10.5

Watumishi Jinsi Wanaume 40 46.5 40 53.9 50.2

Wanawake 46 53.5 34 46.1 49.8

Umri 18 – 30 21 24 13 17.5 20.8

31 – 40 31 36 39 52.5 44.3

41 – 50 27 34 16 21.8 27.9

51– 60 5 6 6 8.2 7.1

Muda wa

utumishi

< Mwaka 1 9 11 0 0.0 5.5

Mwaka 1 – 5 21 24 23 25.0 24.5

> Miaka 5 56 65 51 75.0 70.0

Kwa upande wa jinsi, kuna uwiano kati ya wanawake na wanaume kunakosaidia kuaminika kwa

matokeo. Kuhusu umri, wahojiwa wote wapo kwenye rika la watu wazima (majority age) hivyo

taarifa zao ni za kuaminika (Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - JMT, 1977). Aidha, kwa

Page 32: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

18

kuzingatia kigezo cha mwaka wa masomo na muda wa watumishi kazini, wahojiwa wana uzoefu

wa kutosha kuweza kutoa taarifa za kuaminika.

4.2 Uwepo wa rushwa ya ngono

Kifungu cha 25 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11/2007 kinatamka

“Any person being in a position of power or authority, who in the exercise of his authority,

demands or imposes sexual favours or any other favour on any person as a condition for giving

employment, a promotion, a right, a privilege or any preferential treatment, commits an offence”.

Kimsingi kifungu hiki kinaharamisha kitendo chochote cha mtu mwenye mamlaka kumuwekea

kigezo cha ngono mtu yeyote anayetaka huduma yake. Kwa mujibu wa kifungu hiki, rushwa ya

ngono hutokea pale mtu yeyote aliye na mamlaka au madaraka akiyatumia mamlaka hayo kwa

kumlazimisha au kumshawishi mtu mwingine kufanya naye tendo la ngono kwa ahadi ya

kumpatia ajira, promosheni, au upendeleo fulani. Hivyo, mtumishi yeyote wa chuo kikuu

mwenye mamlaka/madaraka anayetumia nafasi yake kumuwekea kigezo cha kupewa ngono

mwanafunzi au mtumishi mwenzake anayetaka huduma anakuwa ametenda kosa kwa mujibu wa

sheria hii. Kwa mantiki hii utafiti ulilenga kujua uwepo wa rushwa ya ngono katika vyuo vikuu

kwa kuangalia iwapo wadau wana uelewa wa dhana hii ya rushwa ya ngono na hali ya tatizo la

rushwa ya ngono.

Matokeo ya utafiti yanaonesha wahojiwa wengi (wanafunzi 81.6% na watumishi 91.4%)

walikuwa na uelewa wa dhana ya rushwa ya ngono (Jedwali 5). Aidha, matokeo yanashabihiana

kwa vyuo vyote viwili vilivyotafitiwa, na yanabainisha kuwa wahojiwa wanaifahamu rushwa ya

ngono kwa mujibu wa kifungu cha 25 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na.

11/2007.

Page 33: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

19

Jedwali 5: Mwitiko wa uelewa wa dhana ya na uwepo wa rushwa ya ngono

Kigeu (variable) Kundi Mwitiko

Mdafao

(Frequency)

*Chuo

Kikuu cha Dar es Salaam

(%)

Mdafao

(Frequency)

*Chuo

Kikuu

cha

Dodoma

(%)

Wastani

Uelewa wa dhana ya rushwa ya

ngono

Wanafunzi 230 86.4 125 76.7 81.6

Watumishi 82 95.3 65 87.6 91.4

Uwepo wa matukio ya rushwa ya

ngono

Wanafunzi 153 57.5 89 54.6 56.1

Watumishi 59 68.6 52 63.1 65.9

Aidha, matokeo yanaonesha zaidi ya 50% ya wahojiwa (wenye uelewa) walieleza uwepo wa

rushwa ya ngono katika vyuo vikuu vilivyofanyiwa utafiti. Matokeo haya yanamaanisha kwamba

rushwa ya ngono ni tatizo katika vyuo vikuu hivi.

Matokeo haya yanathibitishwa na taarifa za kitaamuli (Qualitative data) ambapo wahojiwa

walionesha uelewa na uwepo wa rushwa ya ngono katika vyuo vikuu vilivyofikiwa katika utafiti

huu. Baadhi ya wahojiwa walieleza yafuatayo:

“……rushwa ya ngono ni pale ambapo mtu anahitaji huduma fulani lakini

hapewi na aliye na nafasi ya kumpa huduma hiyo kwa kumtaka kutoa ngono

ndipo apate huduma husika….”

“……rushwa ya ngono kuwa ni kitendo cha mwenye mamlaka kulazimisha

ngono ndipo atoe haki……”

“…rushwa ya ngono ni mtu kutumia nafasi yake ya kimadaraka ili

kujinufaisha kingono….”

“………. rushwa ya ngono ipo na kwa sasa hali ni tete …mtu akijitokeza

kufuatilia rushwa ya ngono anakuwa amejiingiza katika hatari kubwa hata

kutishiwa maisha ……ni sawasawa na kupambana na madawa ya kulevya….”

“……. Mwalimu alimtongoza mwanafunzi wa kigeni katika programu ya

postgraduate, wakati wanafanya majadiliano ya Tasnifu (dessertation) yake,

mwalimu alianza kumshikashika, mwanafunzi alipiga kelele baada ya taarifa

kuenea mwalimu huyo alipelekwa mafichoni kwa muda wa miaka mitatu na

baadaye kurudishwa chuoni hapo.”

Page 34: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

20

Kutokana na taarifa za kitakwimu na kitaamuli, dhana ya rushwa ya ngono katika vyuo vikuu

inaeleweka na kwamba tatizo la rushwa ya ngono lipo katika vyuo vikuu na linatakiwa

kuwekewa mkakati wa kulidhibiti. Matokeo ya utafiti huu yanashabihiana na utafiti uliowahi

kufanywa na Mukama (2017) kuhusu mapambano dhidi ya rushwa ya ngono kwa wanafunzi wa

Taasisi za elimu ya juu nchini Tanzania. Katika utafiti wake alibaini kuwa kuna rushwa ya ngono

katika Taasisi za elimu ya juu na kwamba waathirika wakuu ni wanafunzi wa kike. Aidha,

watafiti walitajiwa majina ya watu wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo vya rushwa ya ngono,

hata hivyo kutokana na maadili ya utafiti majina hayo yamehifadhiwa. Matokeo haya

yanadhihirisha kukiukwa kwa kifungu cha 25 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa

Namba 11/2007 kulikofanywa na baadhi ya watu wenye mamlaka katika vyuo hivi.

Hivyo, ni muhimu kutafuta vyanzo/sababu za kuwepo kwa vitendo vya rushwa ya ngono,

kuchunguza mifumo iliyopo ya udhibiti ili kupima ufanisi wake na kubaini mbinu zinazotumika

kuendeleza vitendo vya rushwa ya ngono katika vyuo hivi. Kwa kufanya hivyo kutasaidia

kuweka mikakati ya kudhibiti na kuondoa athari zitokanazo na rushwa ya ngono. Kuna athari

nyingi zinazotokana na rushwa ya ngono katika taasisi za elimu ya juu zikiwemo: vyuo kuzalisha

watendaji wenye uwezo mdogo kifikra; kuathiri utendaji wa taasisi; kudhalilisha utu wa mtu na

kusababisha mtu kushindwa kujiamini; kuathiri saikolojia ya waathiriwa wa vitendo vya rushwa

ya ngono; magonjwa ya kuambukiza kama UKIMWI; mimba zisizotarajiwa; kushusha morali ya

utendaji kazi kwa watumishi; upendeleo kwa baadhi ya wanafunzi wanaotoa rushwa ya ngono;

kuporomoka kwa maadili ya wanafunzi, wahadhiri na watumishi wasio wahadhiri na kuharibu

taswira ya vyuo ndani na nje ya nchi. Kwa upande mwingine, Mukama (2017) katika utafiti

wake ameeleza kuwa rushwa ya ngono huvunja heshima ya mtu binafsi na Taasisi.

4.3 Sababu za kuwepo vitendo vya rushwa ya ngono

Kwa mujibu wa modeli ya Klitgaard (1998), rushwa hushamiri katika mazingira ya ukiritimba,

uhuru wa kufanya maamuzi usiodhibitiwa na mahali ambapo hakuna uwazi na uwajibikaji. Kwa

kuzingatia modeli hii, utafiti ulitaka kujua sababu zinazochochea rushwa ya ngono katika vyuo

vikuu kwa kuwataka wahojiwa kueleza chanzo cha kuwepo vitendo vya rushwa ya ngono.

Matokeo yanashabihiana kwa vyuo vyote viwili vilivyotafitiwa. Aidha, kwa mujibu wa matokeo

ya kitakwimu matokeo yanaonesha kuwepo kwa sababu tano ambazo ni ukosefu wa maadili,

ushawishi wa mtu mwenye mamlaka, mfumo wa utoaji taarifa kutokuwa rafiki, mifumo dhaifu

Page 35: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

21

ya kushughulikia rushwa ya ngono na mamlaka ya kutoa alama za mitihani kuachwa chini ya

walimu pekee (Jedwali 6).

Jedwali 6: Mwitiko wa wahojiwa kuhusu sababu za rushwa ya ngono

Kundi Sababu Mwitiko

Mdafao

(Frequency)

*Chuo

Kikuu cha Dar es Salaam

(%)

Mdafao

(Frequency)

*Chuo

Kikuu cha

Dodoma

(%)

Wastani

Wanafunzi Ukosefu wa maadili 118 56.7 43 26.4 63.0

Ushawishi wa mtu

mwenye mamlaka

75 36.1 30 19.3 27.7

Mfumo wa utoaji

taarifa kutokuwa rafiki

15 7.2 18 11.3 9.3

Watumishi Ukosefu wa Maadili 44 74.6 25 66.1 76.5

Mifumo dhaifu ya

kushughulikia rushwa

ya ngono

8 13.5 2 6.2 9.8

Mamlaka ya kutoa

alama za mitihani

kuachwa chini ya

walimu pekee

7 11.9 4 15.5 13.7

*Multiple Responses

Matokeo yanaonesha kuwa hududi (range) ya mwitiko ni 9.3% hadi 76.5% kwa maana ya

mfumo wa utoaji taarifa kutokuwa rafiki na ukosefu wa maadili mtawalia. Ukosefu wa maadili

umejitokeza zaidi kwenye utafiti huu kuwa miongoni mwa sababu zinazochochea rushwa ya

ngono kwenye vyuo vikuu, ukifuatiwa na matumizi mabaya ya madaraka/mamlaka na udhaifu

wa mifumo. Sababu hizi zinaweza kudhoofisha misingi ya uwajibikaji na uwazi katika vyuo hivi.

Kwa upande kwa taarifa za kitaamuli (Qualitative data) utafiti ulibaini sababu za kuendelea

kuwepo kwa vitendo vya rushwa ya ngono licha ya kuwepo kwa sera, miongozo, na hata sheria

ndogondogo zenye kuharamisha rushwa ya ngono. Sababu hizo ni: mapungufu kwenye mifumo

ya kuthibiti matumizi mabaya ya mamlaka, kwenye eneo la kutahini, hususani madaraka

makubwa wanayopewa wahadhiri kwenye eneo la kutahini, mapungufu yatokanayo na mifumo

ya kusimamia uwajibikaji katika utoaji wa huduma, ufinyu wa huduma kama vile nyumba za

bweni kwa wanafunzi wa kike, udhaifu wa mifumo ya ajira hasa wakufunzi inayojali zaidi

ufaulu wa darasani bila kujali weledi, uwezo wa kufundisha na maadili ya wanaoajiriwa.

Page 36: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

22

Vilevile, ongezeko la wanafunzi ambalo halikuenda sambamba na ongezeko la waalimu wenye

uwezo wa kumudu mzigo wa kazi kwa ueledi na nidhamu pamoja na mmomonyoko wa maadili

kwa jumla.

Matokeo haya yanashadidishwa na baadhi ya shuhuda ambazo wahojiwa walieleza kuwa ni

visababishi vya rushwa ya ngono katika vyuo vikuu vilivyofikiwa katika utafiti huu. Baadhi ya

wahojiwa walieleza yafuatayo:

“………...kuna vinara wa rushwa ya ngono ambao tunapishana nao kwenye korido

lakini hawastahili kuwepo chuoni maana wanatajwa sana kwenye mitandao na kwenye

taarifa mbalimbali za uchunguzi…….na hakuna pa kukimbilia kwani hata baba

anafanya kwahiyo hakuna wa kulikemea……hii ni sawa na maneno kwenye Biblia

yanayosema kuwa na asiye na dhambi na awe wa kwanza kumrushia mawe mwenye

dhambi…. ninajisikia vibaya kuwa sehemu ya chuo kikuu au kujitambulisha kuwa ni

mhadhiri wa chuo kikuu…...”

“……wahadhiri hawana mafunzo ya maadili ya ufundishaji (teaching ethics) ……. ile

dhana ya mwalimu kuwa mzazi, mlezi na mwenye uadilifu kwa wahadhiri hawa vijana

haipo kwani wamekuwa na tamaa za kingono kwa wanafunzi wao, wanapenda

kubadilisha wanafunzi wa kike kingono kila mwaka wa masomo unapoanza kwa

msemo wa FUSO limetema……”

“……Wahadhiri kuwapata wanafunzi kingono hawatumii fedha au kutongoza bali

wanatumia nafasi zao za uhadhiri…….”

“……….baadhi ya wahadhiri wamekuwa na tabia ya kuwataka kingono watumishi

wanaofanya usafi katika ofisi zao na wanapokataliwa kupewa rushwa ya ngono hutoa

mapendekezo ya kuwatoa katika ofisi walizopangiwa kufanya usafi……wahadhiri

waliokubaliwa ngono walikuwa wakifika ofisini majira ya saa kumi na moja alfajiri

kwa lengo la kupokea rushwa ya ngono…….”

Page 37: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

23

Hata hivyo, wakati wa ufuatiliaji ilibainika kuwepo baadhi ya wahadhiri wanaozingatia maadili

ya kazi zao. Baadhi ya wahojiwa walieleza yafuatayo:

“……..kuna mwanafunzi alimuandikia mhadhiri wa somo barua pepe na kumuomba

amsaidie katika somo lake atamlipa chochote lakini sio pesa…….mhadhiri aliamua

kuwashirikisha wanafunzi wengine na baadhi ya wahadhiri idarani…….aliwaasa

wanafunzi wasome kwa bidii na kuzingatia maadili……”

“…….kuna mwanafunzi mmoja alikiri kosa la kumfanyia „Quiz‟ rafiki

yake……mwanafunzi aliyefanyiwa „Quiz‟ alimshawishi mhadhiri kingono baada ya

kubaini kuwa kosa walilofanya ni la kufukuzwa chuo…….mhadhiri huyo

hakushawishika na kuchukua hatua ya kumkabidhi mwanafunzi kwa mkuu wa

idara…….”

Kwa upande wa mifumo wahojiwa walieleza yafuatayo:

“……mfumo bado siyo mzuri maana wanafunzi wengi walioripoti wamekuwa

wakifukuzwa chuoni……na wanaotolewa taarifa wamekuwa wakikingiwa kifua

na uongozi……lazima uwepo mfumo wa kumlinda mtoa taarifa na mtuhumiwa

asijue mtoa taarifa ni yupi…...”

“……kumekuwa na uingiliaji wa mifumo ya matokeo (Academic Registration

Information System, ARIS) na kubadilisha matokeo pasipo kufuata utaratibu…...”

“……...Kuna mwanafunzi ambaye aliombwa ngono na mhadhiri, lakini alikataa

na kusababisha yule mhadhiri kumfelisha (kumkamata) yeye pamoja na

mwanafunzi mwingine wa kiume aliyekuwa mpenzi wake na hata walipofanya

mtihani wa marudio (supplementary) bado hawakufaulu na hivyo kushindwa

kuendelea na somo hilo mpaka mwaka uliofuata……...”

Page 38: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

24

Kwa ujumla matokeo haya yanabainisha kuwa rushwa ya ngono katika vyuo vikuu vya Dodoma

na Dar es Salaam inasababishwa na matumizi mabaya ya mamlaka yanayotokana na ukosefu wa

maadili kwa wenye mamlaka na udhaifu wa mifumo ya utoaji taarifa za rushwa ya ngono,

ushughulikiaji wa matukio ya rushwa ya ngono na utungaji na usahihishaji wa mitihani. Hali hii

inaashiria kuwepo kwa uwajibikaji mdogo katika vyuo hivi. Kwa mantiki hii, kuna haja ya

kutazama mifumo ya udhibiti wa rushwa ya ngono kwenye vyuo vikuu vya Dodoma na Dar es

Salaam na hasa kwa kuangalia uwezekano wa kuweka udhibiti katika mchakato wa kutoa

maendeleo ya kitaaluma (course work) ambapo kwa sasa yapo mikononi mwa wahadhiri.

4.4 Mifumo ya udhibiti ya ndani dhidi ya rushwa ya ngono

Kupitia mapitio ya nyaraka, utafiti ulibaini kuwepo kwa kanuni, miongozo, sheria na taratibu

mbalimbali zilizowekwa na nchi pamoja na vyuo ili kuharamisha vitendo vya rushwa ya ngono.

Utafiti ulichambua na kupitia: Kanuni za mienendo na maadili ya utumishi wa umma za mwaka

2014; Sheria ndogo ndogo za vyuo kama sheria za chuo kikuu cha Dar es salaam, 2011 na sheria

za chuo kikuu cha Dodoma, 2012; sera ya kusimamia ubora wa Elimu, 2007 (Chuo kikuu cha

Dar es salaam); Kanuni za maadili kwa watumishi wa Chuo kikuu cha Dar es salaam, 2018; na

Kanuni za maadili za chuo kikuu cha Dodoma, 2012. Nyaraka hizi zote zinaharamisha

mahusiano ya kingono kati ya wanafunzi na watumishi wa chuo, zinapinga unyanyasaji wa

kijinsia, zinakata kutumia rushwa ya ngono kutoa ufaulu, kufanya mawasiliano yoyote

yanayoashiria ngono na kufanya vitendo vyovyote vinavyoashiria ngono. Nyaraka hizi zinalenga

kuweka mazingira salama na rafiki ya kutolea taaluma, kufanya utafiti na kutoa huduma kwa

umma wote wa watanzania na wasio watanzania. Lakini kuwepo kwa vitendo vya rushwa ya

ngono kunafifisha juhudi hizi.

Kutokana na kuwepo kwa nyaraka hizi zinazotoa mwelekeo wa namna vyuo hivi

vinavyowajibika kudhibiti rushwa ya ngono; utafiti ulilenga kupima ufanisi wa mifumo hii

katika kuidhibiti rushwa ya ngono katika maeneo yake. Hivyo, utafiti ulipima ufanisi wa mifumo

hii katika kutoa ulinzi kwa mtoa taarifa juu ya rushwa ya ngono; kutoa ulinzi wa mhanga wa

rushwa ya ngono; kupima uelewa wa wadau (wanafunzi na watumishi) kuhusu uwepo wa

mifumo hii; uzingatiaji wa mifumo hii; uwazi na uwajibikaji katika kutekeleza matakwa ya

mifumo hii.

Page 39: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

25

Utafiti ulibaini udhaifu kwenye mifumo ya ndani ya udhibiti wa rushwa ya ngono. Jedwali 7

linaonesha hududi (range) ya 10.7% - 38.2% ya wahojiwa walikubali kuwepo kwa sera,

miongozo na taratibu za udhibiti wa rushwa ya ngono. Hata hivyo, zaidi ya 60% ya wahojiwa

hawakufahamu uwepo wa sera, kanuni, sheria na miongozo ya kudhibiti rushwa ya ngono.

Aidha, matokeo yanashabihiana kwa vyuo vyote viwili vilivyotafitiwa. Hali hii inaweza

kudunisha mifumo ya udhibiti wa rushwa ya ngono katika vyuo hivi. Hii inamaanisha kwamba,

wanajumuiya wa vyuo husika hawawezi kuwawajibisha viongozi wao kwa kutokuchukua hatua

stahiki za kuzuia na kupambana na rushwa ya ngono.

Jedwali 7: Mwitiko wa wahojiwa kuhusu uwepo wa sera, miongozo na taratibu za udhibiti

rushwa ya ngono

Kundi Mfumo Mwitiko

Mdafao

(Frequency)

*Chuo

Kikuu cha Dar es Salaam

(%)

Mdafao

(Frequency)

*Chuo

Kikuu cha

Dodoma

(%)

Wastani

Wanafunzi Sera inayotoa miongozo ya kukataza

udhalilishaji kijinsia

189 32.9 77 31.3 32.1

Uwepo wa elimu kwa wanafunzi wapya

kuhusu sheria, miongozo inayowalinda

wanafunzi wapya dhidi ya vitendo vya

rushwa ya ngono

203 35.3 101 41.1 38.2

Kuwepo kwa huduma za ushauri nasaha

kwa waathirika wa vitendo vya rushwa

ya ngono

120 20.9 42 17.1 19.0

Kuwepo kwa ulinzi kwa watoa

taarifa/wahanga wa rushwa ya ngono

63 10.9 26 10.5 10.7

Watumishi Sera inayotoa miongozo ya kukataza

udhalilishaji wa jinsia

50 24.4 44 23.0 23.6

Maadili ya kazi yanayobainisha vitendo

vya rushwa ya ngono

51 24.9 48 24.9 24.9

Taratibu na miongozo ya utahini

inayoziba mianya ya kutoa rushwa ya

ngono

37 18.0 32 16.6 17.5

Kuwepo kwa kamati za maadili ya

wahadhiri

41 20.0 47 24.3 22.1

Taratibu zilizo wazi za utoaji wa

rasilimali fedha za kufanya utafiti

26 12.7 22 11.2 11.9

*Multiple Response

Page 40: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

26

Taarifa za kitaamuli zinaonesha kuwepo kwa: uadilifu mdogo; ushirika katika kutenda kosa kati

ya watuhumiwa na wenye maamuzi; uvujaji wa taarifa na vitisho kwa watoa taarifa; urasimu wa

mfumo mzima wa utoaji na ushughulikiaji wa malalamiko; ukosefu wa elimu kuhusu sera,

kanuni na taratibu za kudhibiti maadili vyuoni; kutokuwa na takwimu za malalamiko wala hatua

zilizochukuliwa katika madawati ya jinsia/ofisi ya mshauri wa wanafunzi/kamati za maadili;

ukosefu wa mrejesho kuhusu hatua zilizochukuliwa na wenye mamlaka kutokana na

mapendekezo ya kamati za maadili; na imani ndogo kuhusu mfumo wa kushughulikia

malalamiko.

Kwa upande wa uadilifu mdogo, uongozi na kamati za maadili zinatajwa kutokuwa na maadili.

Baadhi ya wahojiwa walieleza:

“……watu wa kamati ya maadili wao wenyewe wanafanya vitu ambavyo

vinawafanya watu wasiwaamini na kuna mhadhiri ana ushawishi mkubwa katika

kutenda vitendo vya rushwa ya ngono……mara nyingi malalamiko yanayopelekwa

hayashughulikiwi…...”

“…...mfumo mzima umeoza…...hakuna pa kukimbilia…...hata wanaopaswa

kushughulikia tatizo hilo nao ni sehemu ya tatizo…...”

“……ebu fikiria mwanafunzi anaenda kwa mshauri wa masomo kuomba ushauri wa

hatua za kuchukua baada ya kutakwa kingono na mhadhiri……lakini „academic

advisor‟ tena mwenye jinsi ya kike anamwambia akubali kwakuwa ni kitendo cha

dakika tano tu kamaliza na anapata „degree‟ yake……ampe tu….”

Mmoja wa wahojiwa alieleza:

“……mfumo hauko wazi……kuna changamoto kubwa ya kumlinda mtoa

taarifa…….muundo wa uongozi unafifisha utoaji wa taarifa…….sanduku la maoni

lipo na husimamiwa na kamati ya maadili...….wanafunzi hawataki kuandika ili tatizo

Page 41: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

27

lake lishughulikiwe ila tunashugulikia kwa mjadala kwa kumfuata mlengwa na

kumuonya……”

Ukosefu wa maadili kwa baadhi ya viongozi na wajumbe wa kamati za maadili kunatajwa

kusababisha kukosekana kwa uwajibikaji, jambo linalosababisha watumishi na wanafunzi

kupoteza imani kwa uongozi na kamati hizo. Pamoja na uwepo wa mifumo ya ndani katika

kusimamia maadili ya kiutumishi na kiuwanafunzi katika vyuo vyote viwili, sera bado zina

mianya inayosababisha vitendo hivi kuendelea kutendeka. Baadhi ya wahojiwa walisema

yafuatayo:

“…...tabia ya kulindana miongoni mwa wahadhiri inatokana na hofu ya kufukuzwa

kazi……kulindana kunasababisha wanafunzi na watumishi kupoteza

imani……kuwepo kwa kamati huru na kuwahamisha vituo vya kazi wahadhiri

wanaotuhumiwa kungesaidia kudhibiti vitendo vya rushwa ya ngono…...tusikae na

watu wasio na maadili vyuoni……”

Kulindana na ukosefu wa uwazi katika mifumo kunaelezwa kuwa chanzo cha uvujaji na vitisho

kwa watoa taarifa dhidi ya wahadhiri au watumishi wenye mamlaka. Kwa baadhi ya waliojitolea

kutoa taarifa hizo walipata vitisho vya kuhatarisha kazi, taaluma na maisha yao. Hii inaonesha

kukosekana kwa utaratibu au mfumo wa kulinda watoa taarifa (whistleblower protection) au

wahanga wa vitendo vya rushwa ya ngono. Haya yanadhihirishwa na maelezo ya baadhi ya

wahojiwa:

“…….kuna mwanafunzi alitoa taarifa kwa Rasi wa Ndaki dhidi ya mhadhiri

aliyemnyanyasa mwanafunzi wa kike kijinsia…….lakini Rasi alimjulisha mhadhiri

husika……mhadhiri huyo alianza kutoa vitisho kwa mwanafunzi aliyetoa tuhuma

hizo……”

“…...hata baadhi ya viongozi hapa chuoni wanaogopa kupeleka matukio kwenye

vikao kwa kuhofia kuundiwa zengwe na hatimaye kufukuzwa au kuondolewa

kwenye nafasi walizonazo……”

Page 42: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

28

Vyuo kama Taasisi ya Elimu ya juu vina sera na miongozo ila bado upatikanaji wake ni

changamoto, na pale zinapopatikana hazipo kwenye lugha nyepesi. Mmoja wa wahojiwa

alieleza:

“…...sera, kanuni, sheria na miongozo ipo lakini haijulikani kwa wanafunzi na

watumishi, lakini inapotokea umefanya kosa ndipo zinaanza kutumika……”

Kwa mfano, ukipitia sheria ndogo ndogo za wanafunzi za mwaka 2011 za Chuo Kikuu cha Dar

es salaam na sheria ndogo ndogo za wanafunzi za Chuo Kikuu cha Dodoma za mwaka 2012,

lugha iliyopo imekaa kisheria na hivyo kuwa ngumu kueleweka kwa urahisi. Imebainika

kwamba taasisi ya jinsia kwa upande wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam inajitahidi kutoa elimu

ingawa kuna changamoto ya uwezeshaji kifedha na ofisi kwa waratibu wa madawati katika

Ndaki na Shule. Kazi hii inaonekana kama ni kazi ya ziada tu kwa waratibu.

Wahadhiri wapya wanatambua kuwepo kwa miongozo na kanuni za maadili, lakini wanadai

kutoziona kutokana na upatikanaji wake kutokuwa rahisi. Aidha, hali hii ilidhihirika wakati wa

utafiti ambapo ilikuwa vigumu kupata nyaraka hizi zinazosimamia sera, mifumo na miongozo.

Wakati wa utafiti ilibainika kwamba nyaraka hizo hupatikana wakati mtumishi/mhadhiri

anapopata matatizo ya kimaadili.

Vile vile, imebainika kwamba Taasisi ya Jinsia ndio yenye jukumu la kuelimisha wanajumuiya

ya chuo juu ya masuala ya jinsia ikiwepo na rushwa ya ngono. Hata hivyo, hakuna kitengo

maalumu chenye jukumu la kuhakikisha kinatoa elimu kuhusu nyaraka (sera, kanuni na

miongozo mbalimbali).

Kutokana na kuvuja kwa taarifa wahanga wengi wamekuwa waoga kutoa taarifa pale

wanapobaini au wanapoombwa rushwa ya ngono. Aidha, uoga unatajwa kusababishwa na

urasimu wa mfumo wa uwasilishaji na ushughulikiaji wa malalamiko, uelewa mdogo wa watoa

taarifa na mrejesho hafifu wa hatua zilizochukuliwa dhidi ya walalamikiwa. Wahojiwa walikuwa

na haya ya kueleza:

Page 43: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

29

“…….mlolongo wa kuwasilisha taarifa ni mrefu ambapo kwa namna moja au

nyingine unasababisha kuvujisha taarifa……mfumo wa utoaji taarifa kwa

“anonymous submission” unaweza kusaidia kukabiliana na uvujaji wa siri……”

“……kuna changamoto kuu mbili katika utendaji kazi wa kamati za maadili ambazo

ni watu kutojitokeza kutoa ushahidi na kutopata mrejesho wa mapendekezo ya

kamati kutoka menejimenti ya chuo…….”

Hata hivyo, wananchi na wanafunzi kwa ujumla bado wana nafasi kisheria kutoa taarifa nje ya

taasisi husika pale wanapoombwa rushwa ya ngono. Kwa mujibu wa kifungu cha 7 cha sheria ya

Mwenendo wa Makosa ya Jinai, sura ya 20 mtu yeyote anayejua au atakayejua kutendeka au

kusudio la mtu yeyote kutenda kosa linaloadhibiwa chini ya Sheria anatakiwa wakati huohuo

kutoa taarifa kwa Afisa wa Polisi au kwa mtu mwenye madaraka katika sehemu hiyo ambaye

atawasilisha taarifa hiyo kwa Afisa wa Polisi msimamizi Msimamizi wa Kituo cha Polisi kilicho

karibu. Hivyo hivyo, chini ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na rushwa Na. 7/2011 kila

mwananchi katika kuzuia na kupambana na rushwa nchini anao wajibu wa kutoa taarifa pale

anapoona rushwa imetendeka, inatendeka au inakaribia kutendeka. Kifungu cha 39 cha sheria hii

kinatamka bayana kwamba kila mtu mwenye taarifa kuhusu kufanyika kwa vitendo vya rushwa

au kuhusiana na mpango wa kufanyika kwa vitendo vya rushwa unaopangwa na mtu au kundi la

watu anawajibika kutoa taarifa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Vifungu hivyo vyote vinalenga kwenye kushirikisha jamii katika kupambana na jinai ikiwemo

rushwa ya ngono. Hii inatokana na ukweli kwamba mapambano dhidi ya rushwa nchini

yanaweza yasifanikiwe kama umma wa Watanzania hautoshirikishwa kikamilifu.

Aidha, Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11/2007, inatoa ulinzi kwa watu

wanaotoa taarifa kuhusu rushwa au mashahidi ili kuhakikisha kwamba wananchi wanashiriki

kikamilifu na bila hofu katika vita dhidi ya rushwa. Kifungu cha 51(1)(a) cha sheria hii kinazuia

kutajwa kwa jina, makazi au anwani ya mtu aliyetoa taarifa kuhusu vitendo vya rushwa kwa

shahidi anayetoa ushahidi mahakamani. Hali kadhalika, kifungu cha 51(1)(b) kinazuia shahidi

kujibu swali ambalo jibu lake laweza kusababisha kujulikana kwa mtu aliyetoa taarifa juu ya

vitendo vya rushwa ambavyo vimesababisha kuwepo kwa mashitaka mahakamani. Kifungu cha

Page 44: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

30

51(3) cha sheria hii kinafafanua kwamba kama mtoa taarifa atatishiwa kuumizwa au kulipiziwa

kisasi na watu aliowataja au maswahiba wao, basi Serikali itafanya mambo au jambo moja kati

ya haya: itampa mtu huyo ulinzi wa kutosha kulingana na vitisho anavyopata; itamlipa fidia

inayolingana na madhara aliyoyapata; itampatia msaada wa aina nyingine unaolingana na

mahitaji halisi. Kifungu cha 52 cha sheria hii kinatoa ulinzi kwa mtu yeyote anayetoa taarifa au

ushahidi kuhusiana na kufanyika kwa vitendo vya rushwa. Ulinzi huo ni kwamba mtoa taarifa

hatawajibika kwa kosa la jinai au madai kama wakati alipotoa taarifa alikuwa na sababu za

msingi za kuamini kuwa taarifa anazotoa ni za kweli.

Kwa ujumla, vitendo vilivyobainishwa na utafiti vinadhihirisha udhaifu wa mifumo ya ndani ya

udhibiti wa mianya ya rushwa ya ngono. Vitendo hivyo vinachavushwa na kuwepo kwa:-

mmomonyoko wa maadili, mamlaka makubwa ya mhadhiri kuhusu ufaulu wa mwanafunzi,

uvujaji wa taarifa, ufahamu hafifu wa haki za msingi na upendeleo katika utoaji huduma. Mambo

haya yanachangia kupunguza uwajibikaji na hatimae kuongezeka vitendo vya rushwa ya ngono

katika vyuo vilivyotafitiwa. Kwa mujibu wa modeli ya Klitgaard (1998), rushwa hushamiri

katika mazingira ya ukiritimba, uhuru wa kufanya maamuzi usiodhibitiwa na mahali ambapo

hakuna uwazi na uwajibikaji.

Aidha, vitendo vya rushwa ya ngono vinakiuka kifungu cha 25 cha Sheria ya Kuzuia na

Kupambana na Rushwa Namba 11/2007 kinachokataza rushwa ya ngono. Sheria hii

inaharamisha kitendo chochote cha mtu mwenye mamlaka kumuwekea kigezo cha ngono mtu

yeyote anayetaka huduma yake. Hivyo, mtumishi yeyote wa chuo kikuu mwenye

mamlaka/madaraka anayetumia nafasi yake kumuwekea kigezo cha kupewa ngono mwanafunzi

au mtumishi mwenzake anayetaka huduma anakuwa ametenda kosa kwa mujibu wa sheria hii.

Kwa mantiki hiyo, kuna umuhimu wa kuimarisha mifumo ya udhibiti katika vyuo hivi ili

kuimarisha maadili na kuongeza uwajibikaji.

4.5 Mbinu zinazotumika kushawishi rushwa ya ngono

Utafiti ulilenga kubaini njia na mbinu zinazotumiwa kufanya ushawishi wa rushwa ya ngono

katika Taasisi za elimu ya juu. Matokeo yanaonesha kuwa mbinu ya utoaji wa alama za chini

kwenye mitihani iliongoza kwa kutajwa na wahojiwa ikifuatiwa na vitisho vya kutofaulu kwa

wanafunzi kama inavyooneshwa kwenye Jedwali 8.

Page 45: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

31

Jedwali 8: Mwitiko wa wahojiwa kuhusu mbinu zinazotumika kushawishi rushwa ya

ngono

Kundi Mbinu Mwitiko

Mdafao

(Frequency)

*Chuo

Kikuu cha Dar es Salaam

(%)

Mdafao

(Frequency)

*Chuo

Kikuu cha

Dodoma

(%)

Wastani

Wanafunzi Kutoa alama za chini kwenye

mitihani.

240 40.5 61 36.6 38.6

Vitisho vya kutofaulu kwa

wanafunzi.

166 28.0 28 34.1 31.1

Ahadi kama kuolewa, cheo,

chumba chuoni, nafasi ya

uongozi, kuongezewa alama

za ufaulu.

157 26.5 16 18.3 22.4

Ushawishi wa makusudi 130 15.7 44 21.7 18.7

Wahadhiri kuwaita wanafunzi

kwenye mazingira yasiyo

rasmi kwa ajili ya kukagua

Utafiti

(Research/Proposal/Assignme

nt).

23 3.9 44 11.0 7.5

Wahadhiri kujiunga whatsapp

group moja na wanafunzi.

7 1.1 0 0.0 0.6

Watumishi Utoaji wa alama za chini

kwenye mitihani.

56 50.5 29 44.4 47.5

Ushawishi wa makusudi 26 16.1 39 43.8 29.9

Kutoa ahadi kama kumpatia

ajira, cheo, ufadhili wa

masomo n.k.

29 26.1 5 18.5 22.3

Vitisho vya mwalimu dhidi ya

mwanafunzi.

18 16.2 10 26.0 21.1

Ushawishi wa makundi rika 24 14.9 2 6.6 10.8

Kuchelewesha huduma. 8 7.2 3 11.1 9.6

*Multiple Response

Kutokana na kumbukumbu za malazi ya wanafunzi zilizopatikana katika Chuo Kikuu cha Dar es

Salaam, inaonekana kuwa mwaka 2018/19 kulikuwa na maombi ya malazi ya wanafunzi 16,206

(kiambatisho I). Hata hivyo, wanafunzi 10,384 tu ndio waliopata malazi ya chuo. Matokeo haya

yanabainisha kuwepo kwa idadi kubwa ya wanafunzi waliokosa vyumba ingawa waliomba.

Katika mwaka huo chuo kilikuwa na uwezo wa kulaza wanafunzi 11,277 (kiambatisho II)

tofauti na idadi ya wanafunzi 33,658 waliodahiliwa. Aidha, nafasi za malazi kwa wanafunzi wa

kike zilikuwa 5,547 kati ya 13,497 waliodahiliwa katika mwaka huo. Uhaba huu unaweza

kutumika kama mwanya wa rushwa ya ngono.

Page 46: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

32

Taarifa za kitaamuli zinaonesha kuwepo kwa vitisho vya baadhi ya wahadhiri vya kutoa alama

za chini kwa wanafunzi kama mbinu ya kuomba rushwa ya ngono. Wahadhiri wanajua kwamba

mwanafunzi anakuja chuoni na lengo kuu la kupata tuzo za kitaaluma. Wahadhiri hutumia

mwanya huo kwa kuwapa alama ndogo za masomo, kubadilisha alama za ufaulu, kuwafelisha au

kuzuia matokeo yao ili kuandaa mazingira ya kuwashawishi kingono. Baadhi ya wahojiwa

walieleza:

“……kuwepo kwa ucheleweshwaji wa fomu za mikopo kwa makusudi au jina la

mwanafunzi kurukwa ili malipo yake yasikamilike kwa wakati. Hii imekuwa moja

ya njia wanayoitumia kushawishi rushwa ya ngono…….”

“……mwanafunzi alitakwa kingono na mhadhiri akamkatalia, baada ya kumkatalia

mwanafunzi alianza kuona madhara yake kwa kuwekewa alama za chini……”

“…....mhadhiri aliomba rushwa ya ngono kwa mwanafunzi aliyekuwa amefaulu

mtihani wa majaribio (test) alikuwa amepata alama 84……lakini mhadhiri

hakumrudishia karatasi yake ya mtihani wa majaribio (test) na kumweleza kuwa

amefeli mtihani na hivyo yuko tayari kumwongezea alama hadi zifike 84 iwapo

atampa rushwa ya ngono……mwanafunzi alipoenda ofisini kwa mhadhiri alimkuta

na mhadhiri mwingine na alipoomba karatasi yake alikataliwa kwa madai kwamba

ana maongezi na mhadhiri mwenzake……..kwa bahati mhadhiri mwenzake bila

kujua kinachoendelea alimshauri mwahadhiri huyo amsikilize mwanafunzi…….

mwanafunzi alipatiwa karatasi yake na kubaini kuwa alikuwa amefaulu kwa kupata

alama 84……...”

“……kumekuwa na tabia kwa baadhi ya wahadhiri kuwatongoza wanafunzi

mapema kabisa wanapofika kuanza masomo chuoni kwa njia mbalimbali zikiwemo

kuwapigia simu na kuwatumia ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu za

kiganjani……wanafunzi wanapokataa wahadhiri hao huwatishia wanafunzi hao

kuwa watahakikisha hawafaulu katika masomo wanayofundisha……...”

“............kuna wanafunzi walilalamika kwa uongozi wa chuo kutokana na kukataa

kutoa rushwa ya ngono kwa mtuhumiwa……uongozi wa chuo ulielekeza

Page 47: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

33

usahihishaji wa somo hilo ufanyike upya na matokeo yalionesha kuwa wanafunzi

hao walikuwa wamefaulu…….uongozi ulichukua hatua za kiutawala dhidi ya

mtuhumiwa…...”

Matokeo haya yanaonesha kuwepo kwa vitendo vya makusudi vya baadhi ya wahadhiri

kulazimisha ngono kwa wanafunzi. Vitendo hivi vinakiuka kifungu cha 25 cha sheria ya Kuzuia

na Kupambana na Rushwa namba 11/2007. Sheria hii inaharamisha kitendo chochote cha mtu

mwenye mamlaka kumuwekea kigezo cha ngono mtu yeyote anayetaka huduma yake. Hivyo,

mtumishi yeyote wa Chuo Kikuu mwenye mamlaka/madaraka anayetumia nafasi yake

kumuwekea kigezo cha kupewa ngono mwanafunzi au mtumishi mwenzake anayetaka huduma

anakuwa ametenda kosa kwa mujibu wa sheria hii.

Matarajio ya mwanafunzi anapofika chuoni ni kukutana na wahadhiri na watumishi wenye

maadili. Matokeo ya utafiti yanabainisha kuwepo kwa mmomonyoko wa maadili unaofanywa na

baadhi ya wahadhiri pamoja na watumishi wengine kwa kukiuka misingi ya sera, kanuni na

miongozo inayoongoza vyuo hivyo.

Hata hivyo, Jedwali 8 linaonesha kuwa watumishi 65 (29.9%) na wanafunzi 174 (18.7%)

walieleza kuwepo kwa ushawishi wa makusudi ili kujipatia huduma kutoka kwa wenye

mamlaka. Aidha, watumishi 26 (10.8%) waliyataja makundi rika kuwa nayo yalishiriki

kuwashawishi kingono wenye mamlaka ili kupata huduma. Taarifa za kitaamuli zinaonesha

kuwepo kwa vitendo mbalimbali vya kushawishi ngono ambavyo wapewa huduma wamekuwa

wakivifanya kwa wenye mamlaka ili kujipatia huduma.

Wanafunzi walikuwa na haya ya kusema:

“…….kuna baadhi ya walimu masomo yao ni magumu hivyo tunaamua kumtuma

mwanafunzi ambaye ni mzuri na ambaye anaonekana kumvutia mwalimu

………..mwalimu akinasa tu, ajue somo lake tunabutua maana huyo mwanafunzi

anakuwa na maelekezo maalumu kuhakikisha anatupatia maswali ……si unajua

hakuna mkate mgumu kwenye chai…………tunachagua pini ya ukweli ambayo

mwalimu hawezi kuchomoka…….”

Page 48: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

34

“…….kuna mwanafunzi mmoja alikiri kosa la kumfanyia „Quiz‟ rafiki

yake……mwanafunzi aliyefanyiwa „Quiz‟ alimshawishi mhadhiri kingono baada

ya kubaini kuwa kosa walilofanya ni la kufukuzwa chuo…..”

Baadhi ya watumishi walitoa shuhuda zifuatazo:

“……..kuna mwanafunzi alimwandikia mwalimu wa somo Email na kumuomba

mhadhiri amsaidie katika somo lake, atamlipa chochote lakini siyo pesa.

Mwalimu aliamua kuwashirikisha wanafunzi wengine na baadhi ya wahadhiri

katika idara husika. Pia aliwaasa wanafunzi wasome kwa bidii na kuzingatia

maadili……..”

“....... kuna mwanafunzi wa kike aliwahi kumtembelea mhadhiri ofisini kwake

akiwa amevaa kanga mbili, alipoingia ofisini kwake alijifunua kanga hizo

kujaribu kumshawishi mhadhiri kutaka ngono alipoona mhadhiri huyo hashtuki

hata baada ya kuona kajionesha mwili wake kwa mtu asiyetaka na hana haraka ya

kumtaka kingono, mwanafunzi husika aliamua kupiga kelele akidai mhadhiri

alitaka kumbaka. Hata hivyo baada ya waliokuwa jirani na ofisi ya mhadhiri huyo

kufika pale walishangazwa na maneno hayo ilihali binti mwenyewe hakuwa hata

na chupi ya kujisitiri…….”

Pamoja na matokeo haya, mbinu hizi za upande wa wasiokuwa na mamlaka

hazijaharamishwa na kifungu cha 25 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na rushwa

Na. 11/2007 kwani kifungu hicho kinamtaja mtu mwenye mamlaka kuwa ndiye

anaweza kutenda kosa hilo pale anapoweka sharti la ngono wakati wa kutoa huduma.

Matendo ya kushawishi ngono kutoka kwa watu wasio na mamlaka kwenye taasisi za

elimu ya juu, hata kama sio rushwa ya ngono kwa sasa, yakiachwa yaendelee yanaweza

kuchangia kushusha kiwango cha elimu na huduma nchini.

Page 49: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

35

SURA YA TANO

5.0 HITIMISHO NA MAPENDEKEZO

5.1 Hitimisho

Kwa ujumla, utafiti umebaini kwamba tatizo la rushwa ya ngono kwenye vyuo vilivyoshiriki lipo

na kwamba tatizo hili ni kubwa na si la kupuuzwa. Shuhuda za waathiriwa wa rushwa ya ngono

pamoja na shuhuda za uwepo wa watuhumiwa ambao hawajachukuliwa hatua zilitolewa.

Vilevile, utafiti ulibaini kuwepo kwa sera, miongozo na sheria ndogondogo zinazoharamisha

rushwa ya ngono kwenye taasisi zote za umma ikiwa ni pamoja na vyuo vikuu. Kwa mfano,

Kanuni za Utumishi wa umma (2014, kanuni ya 36) zimepiga marufuku kwa mwajiri au

mtumishi wa umma kufanya aina yoyote ya udhalilishaji wa kijinsia kwa kumtaka mwajiriwa

kufanya ngono au kufanya aina yoyote itakayopelekea kufanyika ngono kama kigezo cha ahadi

ya kupendelewa kazini, au kulazimisha ngono ili mwajiriwa kuepuka vitisho ambavyo vitaathiri

ajira yake au kutumia kigezo cha ngono ili mwajiriwa aepuke vitisho dhidi ya maslahi ya sasa au

ya baadae katika ajira yake.

Vyuo vyote viwili vina kanuni za maadili za watumishi; Kanuni za Maadili kwa Watumishi wa

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (2018) na kanuni za maadili Chuo Kikuu Dodoma (2012).

Kanuni hizi zinabatilisha na kutoa katazo la kutumia rushwa ya ngono kutoa ufaulu, kufanya

vitendo vinavyoashiria ngono, au kufanya mawasiliano yanayoashiria uhitaji wa rushwa ya

ngono. Aidha, zinakataza kumsumbua au kumnyanyasa mtu yeyote yule anayetoa taarifa juu ya

unyanyasaji wa kingono (UDSM, 2018).

Pamoja na kuwepo kwa miongozo na kanuni zinazokataza rushwa ya ngono, utafiti ulibaini

mapungufu kwenye uwajibikaji wa udhibiti wa matumizi mabaya ya mamlaka hivyo kutoa

mianya inayosababisha kuwepo kwa vitendo vya rushwa ya ngono. Jambo hili linasababishwa na

kutokuwepo utashi wa dhati kwa wale waliopewa dhamana ya uongozi na watoa huduma

kwenye kushughulikia tatizo la rushwa ya ngono kikamilifu. Tabia za kuwalinda wakosaji,

zimesababisha kutokuimarisha ufuatiliaji wa sera na miongozo, kutokusimamia maadili ya

watendaji kwenye suala hili na kushindwa kuchukua hatua stahiki za kinidhamu kwa wale

Page 50: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

36

wanaoendeleza vitendo vya rushwa ya ngono kwenye taasisi husika. Mifano ilitolewa ya

wahadhiri wanaodaiwa kujihusisha na rushwa ya ngono wanavyoendelea kupewa nyadhifa

mbambalimbali za uongozi na vyeo vya kitaaluma. Shuhuda zilitolewa kuhusu vitisho kwa

watoa taarifa wakiwa waathiriwa au wahadhiri. Shuhuda zilitolewa kuhusu wanafunzi

waliopendelewa na kupewa aidha ajira au kupewa udhamini wa masomo (scholarship) bila

kustahili pale ambapo wamekubali kutoa rushwa ya ngono. Shuhuda nyingine zilitolewa kwa

kuwepo watuhumiwa waliopewa adhabu kidogo sana kulingana na kosa, kwa mfano mhadhiri

kupewa likizo ya mwaka iliyomwezesha kuendelea na shughuli zake za ushauri na hatimaye

kurudi chuoni kuendelea na shughuli kama kawaida. Ukosefu wa utashi na uwajibikaji

unakatisha tamaa waathiriwa wa rushwa ya ngono au watendaji wenye maadili kutoa taarifa

kuhusu vitendo vya rushwa ya ngono.

Utafiti ulibaini mapungufu kwenye mifumo ya utahini inayotoa mwanya kwa wahadhri kutumia

vibaya mamlaka yao. Shuhuda zilitolewa kuhusu wanafunzi waliofelishwa kutokana na kukataa

rushwa ya ngono au wanafunzi wa kiume kufelishwa kwa vile marafiki wao wa kike wamekataa

kutoa rushwa ya ngono. Shuhuda zilitolewa kuhusu kubadilishwa kwa alama za mitihani hata

baada ya matokeo kutoka rasmi. Shuhuda zilitolewa kuhusu wanafunzi waliopendelewa kwenye

kupewa alama za juu na hatimaye kuajiriwa chuoni bila kustahili.

Mapungufu yamejitokeza kwenye mifumo ya vyombo vya kusimamia utekelezwaji wa sera na

miongozo hususan kwenye suala la rushwa ya ngono. Kamati za maadili kushindwa kudhibiti

rushwa ya ngono, vitengo vya jinsia kukosa nyezo na uwezo wa kuelimisha jamii kuhusu rushwa

ya ngono, ofisi za mshauri wa wanafunzi kukosa kitengo cha kuwasaidia waathiriwa wa rushwa

ya ngono.

Utafiti ulibaini mianya mingine inayosababisha kuendelezwa kwa rushwa ya ngono ikiwa ni

pamoja na ukosefu wa huduma za msingi kwa wanafunzi kama vile nyumba za kulala, mikopo,

pamoja na mifumo ya ajira za wakufunzi isiyozingatia weledi na maadili ya kazi kwenye taasisi

za elimu (teaching ethics).

Page 51: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

37

Aidha, utafiti umebaini kuwa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11/2007 inatoa

mwanya kwa wasio na mamlaka kuwashawishi wenye mamlaka kuwapa ngono na hivyo

kukwamisha juhudi za Serikali za kupandisha ubora wa elimu na huduma pamoja na kudhibiti

vitendo vya rushwa ya ngono.

5.2 Mapendekezo

Kutokana na matokeo tajwa, utafiti umebainisha mapendekezo machache yaliyotokana na

mijadala ya washiriki wa utafiti huu. Aidha, umuhimu wa kuboresha na kuimarisha mifumo ya

uwajibikaji kwenye kupambana na rushwa ya ngono ulijitokeza kama eneo la kipaumbele

kwenye kupambana na tatizo la rushwa ya ngono ndani ya vyuo vya elimu ya juu na taasisi

nyingine za umma na za sekta binafsi. Mapendekezo yamebainishwa kwa kila mdau:

Serikali

Iuwajibishe uongozi wa vyuo vikuu kwenye kujenga mazingira wezeshi na salama kwa

wanafunzi na wafanyakazi katika ngazi zote ili kuwezesha wanafunzi wa kike na kiume

kupata na kufaidi haki ya elimu katika ngazi hii pamoja na kuwezesha upatikanaji wa

elimu bora;

Iimarishe mifumo ya ajira ya wafanyakazi wote, hususan wakufunzi na viongozi kwa

kuwapa mafunzo ya ualimu na uongozi wale wote wenye kuajiriwa chuoni ili kuwapa

nyenzo za uwajibikaji wa kuzingatia maadili ya kufundisha na kuongoza katika taasisi za

elimu;

Iongeze fedha za uendeshaji vyuoni na hususan zinazohitajika kwenye kuimarisha

huduma za kuwezesha kuboresha utoaji wa elimu ikiwa ni pamoja na huduma za malazi

kwa wanafunzi ili kupunguza mianya inayotumiwa na wasimamizi na watoa huduma hizi

kwa kuweka sharti la ngono kwa wanafunzi;

Isimamie uwajibikaji wa uongozi wa chuo kuhusu masuala ya jinsia na hususan rushwa

ya ngono kwa kuwawajibisha viongozi waimarishe Kamati za Maadili ndani ya vyuo;

Kuendelea kuijengea uwezo TAKUKURU wa kuweza kuchunguza na kumfikisha

mtuhumiwa mahakamani bila kuhitaji kibali cha Mkurugenzi wa Mashtaka; na

Page 52: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

38

Ifanye mapitio ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11/2007 ili

kuimarisha mapambano dhidi ya rushwa ya ngono.

Uongozi wa Vyuo

Uboreshe mifumo ya udhibiti na uwajibikaji kwenye kuimarisha mifumo ya kusimamia

maadili, mifumo ya utahini, mifumo ya kutoa taarifa na kulinda watoa taarifa pamoja na

kuwajibisha watuhumiwa wa vitendo hivyo;

Uimarishe taasisi na kamati zinazoshughulikia masuala ya maadili ya watumishi wake

ikiwa ni pamoja na kamati za maadili, vitengo vya jinsia, ofisi ya mshauri wa wanafunzi

kwa kuwapatia nyenzo, vitendea kazi na mafunzo ya kuwawezesha kushughulikia

masuala ya rushwa ya ngono pamoja na unyanyasaji wa kijinsia kwenye vyuo; na

Uimarishe mahusiano na TAKUKURU kwenye kutoa elimu, kupeleleza na kuchukua

hatua stahiki kwa wale wote wenye kutuhumiwa kujihusuisha na vitendo vya rushwa ya

ngono.

Vitengo/Taasisi za Jinsia

Kujijengea uwezo wa uelewa wa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na.

11/2007 kuhusu rushwa ya ngono ili waweze kusimamia utekelezaji wake vyuoni; na

Kuwajengea wanafunzi na jamii yote ya chuo uelewa wa suala la rushwa ya ngono ili

waweze kujitetea na kupambana nalo.

Asasi za kiraia

Kutumia taarifa hii kuimarisha vita dhidi ya rushwa ya ngono;

Kuendeleza na kuimarisha ubia kati yake na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na

Rushwa (TAKUKURU) kwenye vita dhidi ya rushwa ya ngono, hasa kwenye utafiti na

elimu ya umma; na

Page 53: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

39

Kujijengea uelewa wa pamoja wa sheria ya Kuzuia na Kupambana na rushwa hususani

vipengele vinavyoelezea rushwa ya ngono ili kuweza kuendeleza mapambano dhidi ya

rushwa ya ngono.

Wanafunzi wa Vyuo

Waongeze jitihada katika masomo, wazingatie maadili, wasikubali kurubuniwa, wavunje

ukimya na kupaza sauti kunapotokea viashiria vya kuwanyima haki zao, na wachukue

hatua stahiki pale wanapopokonywa hizo haki;

Wadai kuimarishwa kwa mikakati iliyobainishwa katika miongozo na sheria ndogondogo

za kuzuia na kudhibiti rushwa ya ngono;

Wafikishe malalamiko yao TAKUKURU kwa kupitia kamati zao, taasisi za kiraia na hata

wao wenyewe; na

Waungane na kushiriki zaidi kwenye kampeni za kupambana na rushwa ya ngono.

Page 54: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

40

MAREJEO

Briggs, S. (2009). Criminology for Dummies; Wiley Publishing Inc.

Crouch, M. and McKenzie, H. (2006). The logic of small samples in interview-based qualitative

research. Social Science Information, 45(4), 18. doi: 10.1177/0539018406069584.

Guest, G., Bunce, A. and Johnson, L. (2006). How many interviews are enough? An experiment

with data saturation and variability. Field Methods, 18(1), 24. doi:

10.1177/1525822X05279903.

http://mwaseba5.blogspot.com/2017/01/rushwa-ya-ngono-bado-ni-tishio-nchini.html

http://mwaseba5.blogspot.com/2017/01/rushwa-ya-ngono-bado-ni-tishio-nchini.html

IPP Media (2011). School pregnancies: A call for reflection on teachers morality. Retrieved from

http://www.ippmedia.com/fronted/index.php on 05 November 2019.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (2017). Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa Na Mpango wa

Utekelezaji: Awamu ya tatu 2017-2022

Jamhuri ya Muungano ya Tanzania (1977). Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

Mchapaji Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam.

Klitgaard, R. (1988). Controlling Corruption. Berkeley, CA. University of California Press

Levin, J. and Milgion, P. (2004), Introduction to choice theory. Stanford University.

Mandago, B. (2018). Tanzania: Say No to Sextortion https://genderlinks.org.za/news/tanzania-

say-no-to-sextortion/; ilisomwa tarehe 05 Novemba 2019.

Mwai, P. (2018). Vicensia Shule: mhadhiri aliyezua mjadala wa rushwa ya ngono chuoni UDSM

Tanzania ni nani? Imesomwa kutoka http://www.bbc.com/swahili/habari-46368623

ilisomwa tarehe 05 Novemba 2019.

Sabinus, J. (2019). Rushwa ya ngono vyuoni inaangamiza wengi; imesomwa kutoka

http://www.habarileo.co.tz/2019-09-055d70f90061c4f.aspx ilisomwa tarehe 05

Novemba 2019.

Sheikh, L. (2007). Sexual harassment: The salient crime. Dar es Salaam.

TAMWA (2012). Ripoti ya Utafiti wa Tamwa Kuhusu Unyanyasaji wa kijinsia

http://ateen101.blogspot.com/2012/10/ripoti-ya-utafiti-wa-tamwa-kuhusu.html

TAMWA (2014). The campaign against sextortion 3rd

November. Dar es Salaam.

Page 55: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

41

Tanzania Women Judge Association (TWJA) (2011). Stopping the abuse of power for purposes

of sexual exploitation; a toolkit available at http://iawj/Tanzania_toolkit_final_pdf

ilisomwa tarehe 05 Novemba 2019.

TCU (2018). Higher Education Students admission, enrollment and education statistics

iliyopatikana kutoka http://www.tcu.go.tz/sites/default/files/admission

%20and%20Graduation%statistics.pdf iliyosomwa tarehe 20 Disemba 2019.

Tem, H. (2007). Nayakumbuka yote. Mkuki na Nyota Publishers.

Yin, R. K. (2014). Case Study Research Design and Methods (5th ed.) .Thousand Oaks, CA:

Sage. 282 pages. (ISBN 978-1-4522-4256-9).

Yusuph, K (2016). Sextortion in education sector and response to criminal legal system in

Tanzania-A Review. Asia Pacific Journal of Education, Arts and Sciences, 3(1):56 - 63

Page 56: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA …

42

VIAMBATISHO

Kiambatisho I: Maombi ya vyumba vya malazi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

2016/17 – 2019/20

Malazi 2016/2017 2017/2018 2018/2019 2019/2020

Idadi ya maombi 10,488 19,050 16,206 27,086

Idadi ya waliopata 7,293 10,245 10,259 10,526

Idadi ya waliokosa 3195 8805 5947 16560

Idadi ya maombi

(mahitaji maalum)

94

198 125 138

Idadi ya walioapata

(mahitaji maalum)

94

198 125 138

Kiambatisho II: Idadi ya mabweni na mgawanyo wa wanafunzi katika Chuo Kikuu cha

Dar es Salaam 2018/19

Jina la Bweni Uwezo Nafasi za Wanaume Nafasi za Wanawake

Hall one 512 190 322

Hall two 400 400 0

Judge Julie Manning 494 0 494

Hall four 251 73 178

Hall five 400 400 0

Hall six 310 317 7

Hall seven 304 30 274

Mabibo Hostel 4,298 2,580 1,718

Kunduchi Hostel 50 25 25

Water Resources Houses 16 8 8

CoICT Hostel 240 76 160

Magufuli Hostel 3,840 1,536 2,280

Ubungo Hostel 108 54 54

Mikocheni Hostel 54 27 27

JUMLA 11,277 5716 5547