ewe muislamu, kumbuka mauti - ´allaamah ´abdul-´aziyz aal ash-shaykh

12
Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti! ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aal ash-Shaykh Mfasiri: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush ©

Upload: wanachuoni

Post on 02-Nov-2014

168 views

Category:

Documents


2 download

DESCRIPTION

Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

TRANSCRIPT

Page 1: Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

Ewe Muislamu,

Kumbuka Mauti!

´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aal

ash-Shaykh

Mfasiri:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

©

Page 2: Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

Bismillaahi Rahmaani Rahiym

Mada ya leo ni kuongelea siku ya Aakhirah. Kwanza Allaah (Jalla wa ´Alaa)

Kafanya (nyumba) vituo vitatu; nyumba ya ´amali, nyumba ya malipo na

nyumba baina ya hizo mbili. Dunia yote ni nyumba ya kufanya ´amali bila ya

hesabu.

"Na sema: Tendeni vitendo. Na Allaah, na Mtume wake, na Waumini

wataviona vitendo vyenu." (09:105)

Ni nyumba ya ´amali, hakika Allaah (Ta´ala) Katuumba ili kumuabudu Yeye

mmoja asiyekuwa na mshirika. Na kusimama na ya wajibu ambayo

Kayawajibisha juu yetu; katika kumtakasia dini na kumpwekesha kwa kila

aina ya ´ibaadah na kutekeleza Shari´ah Yake na kusimama kwa hilo.

"Kisha tukakufanyeni nyiye ndio wenye kushika mahala pao baada yao katika

ardhi ili tuone jinsi mtakavyotenda." (10:14)

Na Kaifanya Aakhirah kuwa nyumba ya malipo:

"... ili awalipe walio tenda ubaya kwa waliyoyatenda, na waliotenda mema

awalipe mema." (53:31)

Na kuna nyumba baina ya nyumba hizi mbili, dunia na Aakhirah nayo ni

Barzakh. Nayo ni kaburi anapolazwa mtu baada ya roho kutengana na mwili

wake mpaka Allaah Atapotoa idhini ya kuhesabiwa waja Ewe Muislamu!

Tumeumbwa katika dunia hii ili tupewe mitihani. Kama Asemavyo Allaah:

"Ambaye ameumba mauti na uhai ili kukujaribuni ninani miongoni mwenu

mwenye vitendo vizuri zaidi." (67:02)

Katika uhai kuna mitihani, na katika mauti kuna mitihani. Kaumba Allaah

mauti na uhai ili atujaribu ni nani kati yetu mwenye matendo mazuri zaidi.

Katika mauti kuna balaa na mitihani. Kwa kuwa kuyakumbuka mara kwa

mara daima kunaufanya moyo kuwa sawa na kufanya juhudi ya ´amali njema

na kujitayarisha nayo [mauti] na yaliobaada yake.

Page 3: Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

Uhai ni balaa kwa mja, mja hupewa mitihani katika uhai wake. Je, atakuwa

mja mwenye kushukuru kumtimizia Allaah haki Zake au kinyume chake.

Hakika dunia hii ni upuuzi na mchezo na mapambo tu kama Alivyosema

Allaah:

"Jueni ya kwamba maisha ya dunia ni mchezo, na pumbao, na pambo, na

kujifakhirisha baina yenu na kushindana kwa wingi wa mali na watoto."

(57:20)

Ataejua kuwa uhai wake umekadiriwa kwa zama ambazo Anazijua Mola

wetu, anatakiwa kujiandaa na yalio baada ya mauti. Na ajue kuwa akifanya

mchezo katika dunia hii na kupoteza muda wake, atajuta siku ya Qiyaamah:

"Isije ikasema nafsi: “Ee majuto yangu kwa yale niliyopoteza upande wa

Allaah, na hakika nilikuwa miongoni mwa wanao fanya maskhara!” Au

ikasema: “Ingeli kuwa Allaah Ameniongoa, bila ya shaka ningelikuwa

miongoni mwa wenyekumcha Allaah”. Au ikasema inapo ona adhabu: “Lau

kuwa ningelipata fursa nyengine, ningelikuwa miongoni mwa wafanya

mema”." (39:56-58)

"Na lau ungeliona watavyosimamishwa mbele ya Mola wao, akawaambia: “Je,

si kweli haya?” Na wao watasema: “Kwani? Tunaapa kwa Mola wetu ni

kweli”." (06:30)

Watatamani wakati huo warudishwe duniani ili watengeneze walipoharibu.

Anasema Allaah (Ta´ala) kuhusu wao:

"Na watasema: Lau kuwa tungelisikia, au tungelikuwa na akili, tusingelikuwa

katika watu wa Motoni!." Wakakiri dhambi zao. Basi kuangamia ni kwa watu

wa Motoni!." (67:10-11)

Atatamani kurudishwa duniani huenda akatengeneza alipoharibu na kutimiza

ya wajibu kwake, lakini majito hayo hayatomfaa kitu. Ewe Muislamu! Hakika

Allaah Katuamrisha kujizidishia zawadi duniani kwa ajili ya Aakhirah yetu.

Akasema:

"Na jitengezeeni zawadi. Na hakika bora ya zawadi ni ucha Mungu. Na

nicheni Mimi, enyi wenye akili!." (02:197)

Hakuna atachojizidishia mja zaidi ya kumcha Allaah na ´amali njema, hakika

Allaah (Ta´ala) Hamdhulumu yeyote.

Page 4: Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

"Na anayetenda mema, naye ni Muumini, basi hatakhofu kudhulumiwa wala

kupunjwa." (10:112)

Hatakhofu kudhulumiwa ikawa atabeba makosa ya wengine wala kupunjwa

mema yake. Bali mema yake yamehifadhiwa kwa ajili yake.

"Afanyae wema atalipwa mfano wake mara kumi. na afanyae ubaya hatalipwa

ila sawa nao tu. Na wao hawata dhulumiwa.” (06:60)

Hakika uhai wa muumini ni haki alioamrishwa kumtii Allaah, kufanya khayr

na kujishugulisha kumtii Mola na akatumia siku zake, usiku wake, miezi yake

na miaka yake kujishughulisha na yatayomkurubisha kwa Allaah. Huku

akijua kuwa ´amali zote hizi zitahesabiwa kwake na kusimama kwazo na

huenda akazisahau.

"Siku atapowafufua Allaah, na awaambie yale waliyoyatenda. Allaah

Ameyadhibiti, na wao wameyasahau! Na Allaah ni Mwenye kushuhudia kila

kitu." (58:06)

Ewe Muislamu! Hakika muumini katika uhai (maisha) yake ayaangalie kwa

mtazamo mzuri wa kuyapa umuhimu na kujishughulisha na

yatayomkurubisha kwa Allaah. Na mmoja wetu atapoteza muda wake katika

uhai huu akafanya maasi na maovu huku anaiona nafsi yake kuwa iko katika

usawa.

"Sema: Je, tukutajieni wenye khasara mno katika vitendo vyao? Ni wale

ambao juhudi yao katika maisha ya dunia imepotea bure, nao wanadhani

kwamba wanafanya kazi nzuri." (18:103-104)

Allaah Katueleza kuwa Atatukusanya siku ambayo haina shaka ndani yake na

atatusimamishia ´amali zetu zote tulizofanya.

"Basi itakuwaje tutakapo wakusanya Siku ambayo haina shaka kuja kwake?

Na kila nafsi italipwa kama ilivyochuma, bila ya kudhulumiwa." (03:25)

Ewe Muislamu! Uhai wako umekadiriwa kwa zama ambazo zinajua Allaah,

elimu yake iko kwa Allaah:

"Hakika kuijua Saa (ya Qiyaamah) kuko kwa Allaah. Na Yeye ndiye

anayeiteremsha mvua. Na anavijua viliomo ndani ya matumbo ya uzazi. Na

haijui nafsi yoyote itachuma nini kesho. Wala nafsi yoyote haijui itafia nchi

gani. Hakika Allaah ndiye Mwenye kujua, Mwenye khabari." (31:34)

Page 5: Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

Ewe Muislamu! Hakika Muislamu anatakiwa daima amuombe Allaah

Amthibitishe katika Uislamu na Asiupoteze moyo wake baada ya kuuongoa.

Kwa kuwa anajua kuwa moyo wake uko baina ya vidole viwili katika vidole

vya Allaah; anaupeleka Apendavyo.

"Moyo za waja ziko baina ya vidole viwili katika vidole vya Allaah;

anazipeleka Apendavyo."

Ewe Muislamu! Tumeamrishwa kukumbuka mauti daima na milele. Allaah

Katukumbusha maslahi haya makubwa. Anasema Allaah (Jalla wa ´Alaa):

"Naye ndiye Allaah wa kushinda, aliye juu ya waja wake. Na hukupelekeeni

wa angalizi, mpaka mmoja wenu yakimjia mauti wajumbe wetu humfisha,

nao hawafanyi taksiri. Kisha watarudishwa kwa Allaah, Mola wao wa Haki.

Hakika, hukumu ni yake. Naye ni Mwepesi kuliko wote wanao hisabu."

(06:61-62)

"Sema: Atakufisheni Malaika wa mauti aliyewakilishwa juu yenu; kisha

mtarejeshwa kwa Mola wenu." (32:11)

"Popote mlipo mauti yatakufikieni, na hata mkiwa katika ngome zilizo na

nguvu." (04:78)

Na ni haki kuwa ajali yetu yatusubiri kama jinsi raziki zetu zatusubiri. Muda

wa mja unapoisha katika uhai wake aliomkadiria Allaah na kuupanga,

atafikwa na aliompangia Allaah. Na atajiwa na sakaratul maut na hali zake.

Anasema Allaah (Jalla wa ´Alaa):

"Na uchungu wa kutoka roho utamjia kwa haki. Hayo ndiyo uliyokuwa

ukiyakimbia." (50:19)

Mja wakati anapoachana na dunia hii hukutana na mambo makubwa na hali

mbali mbali za kutisha, Lakini Allaah Huwathibitisha wale walio amini kwa

kauli iliothabiti katika uhai wa dunia na Huwapoteza Allaah madhalimu na

Hufanya Atakacho. Hakika ajali hii ikifikia wakati wake hakuna yeyote

awezae kuizuia.

Anasema Allaah (Ta´ala):

"Sema: Atakufisheni Malaika wa mauti aliyewakilishwa juu yenu; kisha

mtarejeshwa kwa Mola wenu." (32:11)

Page 6: Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

Wakati roho inapotengana na mwili unafikwa na shida na khofu kubwa

zinazojua Allaah. Muislamu anapokuwa katika hali ya kuiaga dunia na

anaelekea Aakhirah huteremkiwa na Malaika wenye nyuso nzuri, nguo nzuri

nyuso zao kama jua. Kisha anajiwa na Malaika wa kutoa roho na kumwambia:

"Ewe ulie na nafsi nzuri, toka uje katika msamaha na radhi za Allaah; hapo

roho hutoka kwa upole na utaratibu.

Malaika wa mauti wanaichukua na kuiweka kwenye kafani waliokuja nayo

kutoka Peponi na harufu nzuri kama miski iliopatikana kwenye uso wa ardhi.

Wanapanda nayo [roho yake] mbinguni wanafunguliwa milango ya

mbinguni. Kila mbingu inasema:

"Hii ni roho ya fulani bin fulani kwa jina lake la duniani."

Anasema Allaah irudisheni katika ardhi:

"Kutokana nayo (ardhi) tumekuumbeni, na humo tunakurudisheni, na kutoka

humo tutakutoeni mara nyengine." (20:55)

Itarudishwa roho kwenye mwili wake kisha ajiwe na Malaika wawili

wamuhoji; Mola wake, dini yake na Mtume wake.

Muumini atasema "Mola wangu ni Allaah, Uislamu ndio dini yangu."

Atapoulizwa "Wamtambuaje mtu huyu [Muhammad]?" Atasema "Alitujia

kwa haki tukamwamini na kumsadikisha." Atanadi Mwenye kunadi kutoka

mbinguni:

"Kasema kweli mja wangu, mfungulieni mlango wa Peponi na ajiwe na

harufu yake na aone mahala pake."

Kisha atajiwa na mtu mwenye nguo na uso mzuri, harufu nzuri. Atamuuliza

"Nani wewe, waonekana umekuja kwa khayr?"

Atasema:

"Mimi ni ´amali zako njema."

Atasema:

"Mola wangu simamisha Qiyaamah."

Page 7: Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

Ama kwa mtu asiekuwa muumini, atajiwa na mtu mwenye uso wakutisha,

nguo mbaya wakiwa na sanda kutoka Motoni. Kisha atajiwa na Malaika wa

kutoa roho na kumwambia:

"Ewe mtu mwenye nafsi chafu, toka uje kwenye ghadhabu na hasira za

Allaah”; roho itatoka kwenye mwili wake, wataivuta kama chuma cha Moto

kitokavyo kwenye pamba ziliolowa. Kisha wanaichukua na kuiweka kwenye

sanda ile, inatoka ikiwa kama kwamba ni harufu mbaya sana iliopatikana

katika uso wa ardhi. Watapanda nayo mbinguni ila hatofunguliwa milango ya

mbinguni, kisha kutasomwa:

"Na anayefedheheshwa na Allaah hana wakumhishimu. Hakika Allaah

Hufanya apendacho." (22:18)

Kisha Atanadi Mwenye kunadi mrudisheni katika ardhi:

"Kutokana nayo (ardhi) tumekuumbeni, na humo tunakurudisheni, na kutoka

humo tutakutoeni mara nyengine." (20:55)

Atarudishiwa roho yake mwilini mwake, ajiwe na Malaika wawili wamuulize

kuhusu Mola wake, dini yake na Mtume wake? Atasema:

"Eeeh sijui! Nilisikia watu wakisema nami nikasema."

Allaah (Ta´ala) Katubainishia hali ya wanaokata roho kwa kusema:

"Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa, basi ni raha, na manukato, na

Bustani zenye neema. Na akiwa katika watu wa upande wa kulia." (56:88-91)

"Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu, basi karamu yake ni maji

yanayochemka, na kutiwa Motoni. Hakika hii ndiyo haki yenye yakini. Basi

litakase jina la Mola wako aliye Mkubwa.” (56:92-96)

Adhabu na neema za kaburini ni jambo limetolewa dalili na Qur-aan na

Sunnah. Anasema Allaah (Ta´ala):

"Allaah Huwatia imara wenye kuamini kwa kauli ya imara katika maisha ya

dunia na katika Aakhirah." (14:27)

Wanasema wanachuoni Aayah hii inathibitisha adhabu na neema za kaburi.

Akasema tena Allaah (Ta´ala):

Page 8: Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

"Wanaonyeshwa Moto asubuhi na jioni. Na itapofika Saa ya Qiyaamah

patasemwa: “Waingizeni watu wa Firauni katika adhabu kali kabisa!" (40:46)

Ni dalili kuwa wanaadhibiwa kwenye makaburi yao. Na Mtume (´alayhis-

Salaam) alipita kwenye kaburi mbili, akasema:

"Hakika hawa wanaadhibiwa na hawaadhibiwi kwa makubwa, Mmoja wao

hakuacha kujikinga na mkojo, ilhali wa pili alikuwa akisambaza uvumi.”

Na akasema:

“Adhabu nyingi za kaburi ni kuacha kujikinga na mkojo."

Na watu katika kaburi wanazidiana daraja. Katika kaburi kuna ajabu

miongoni mwa maajabu ya Allaah, hakuna neema wala adhabu zenye

kudumu. Na kuna wenye adhabu kisha kukaja neema, kadiri na hali za watu

zilivyokuwa duniani.

Adhabu ya kaburi ni haki isiokuwa na shaka, imetolewa dalili na Qur-aan na

Sunnah. Alikuwa Mtume (´alayhis-Salaam) akisema:

"Anapomaliza kusali mmoja wenu, amuombe Allaah kinga kwa mambo

manne kwa kusema: “Ee Allaah, mimi najikinga Kwako na adhabu za moto

na adhabu za kaburi na fitna ya uhai, na ya kufa, na shari ya [fitna] ya

Masiyhid-Dajjaal”."

Watu wa makaburi ndani ya makaburi yao watatamani fursa ya kufanya

´amali njema walipe. Imepokelewa kwa baadhi ya Salaf baada ya kufa kwao

wakiwaambia

"Nyinyi mnafanya ´amali na wala hamjui [yanayowasubiri], na sisi tunajua

na hatufanyia ´amali [hatuna fursa hiyo], hakika rakaa mbili za mmoja

wenu ni bora kuliko dunia na yaliomo ndani yake."

Hii kaburi ni kituo cha kwanza cha Aakhirah, ima itakuwa ni moja katika

Bustani za Peponi au moja ya shimo katika mashimo ya Motoni. Alisimama

´Uthmaan (radhiyallaahu ´anhu) kwenye kaburi moja, akalia mpaka ndevu

zake zikalowa.

Alipoulizwa, akasema: Nilimsikia Mtume (´alayhis-Salaam) akisema:

"Kaburi ndio kituo cha kwanza cha Aakhirah, ima ni moja katika Bustani za

Peponi au moja ya shimo katika mashimo ya Motoni."

Page 9: Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

Allaah (Ta´ala) Anasema:

"Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema." (82:13)

Neema katika dunia, na neema katika kaburi na neema siku ya Qiyaamah.

Watu watabaki kwenye makaburi katika hali zao mpaka Allaah

Ataposimamisha Qiyaamah.Israafiyl atapuliza parapanda.

"Na litapulizwa barugumu, wazimie waliomo mbinguni na waliomo katika

ardhi, isipokuwa aliyemtaka Allaah." (39:68)

Parapanda ambayo itauwa kila kiumbe, kisha kutapulizwa mara tena

wasimamishwe watu kwa Mola wa walimwengu, kisha kutapulizwa mara ya

mwisho watainuka wawe wanangojea. Anasema Allaah (Ta´ala): "Na

litapulizwa barugumu, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola

wao. Watasema: Ole wetu! Nani aliyetufufua kwenye makazi yetu? Haya

ndiyo aliyo yaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume.

Anasema Allaah (Ta´ala):

"Na litapulizwa barugumu, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa

Mola wao. Watasema: Ole wetu! Nani aliye tufufua kwenye makazi yetu?

Haya ndiyo aliyo yaahidi Mwingi wa Rehemana wakasema kweli Mitume.

Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, mara wote watahudhurishwa mbele yetu.

Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa ila yale

mliyokuwa mkiyatenda." (36:51-54)

Anasema Mtume (´alayhis-Salaam):

"Vipi ntaimarika na alie na baragumu kaishika na anasubiri tu lini

ataamrishwa kuipuliza."

Mtu atasimama kwenye mizani yake akitetemeka hajui itakuwa na uzito au

itakuwa khafifu. Wakati wa kupewa vitabu, mtu hujui atapokea kitabu chake

kwa mkono wa kulia au wa kutosho. Na wakati wa kupita juu ya Swiraat, mtu

hajui ataokoka au hapana.

"Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye, na mamaye na babaye, na mkewe na

wanawe; kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha."

(80:34-37)

Page 10: Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

Watasimamishwa watu kisimamo kirefu kizito kinachojua Allaah, kisha

watawaendea Mitume wa Allaah wakiwaomba wawaombee kwa Allaah

kutolewa katika hali waliomo. Watamuendea Aadam, Nuuh, Ibraahim,

Muusa, ´Iysa watakataa na kila Mtume atasema:

"Hakika Allaah leo Kakasirika ghadhabu ambayo Hajawahi kukasirika mfano

wake kabla."

Kila Mtume atasema "Ole wangu nafsi yangu, nendeni kwa mwengine."

Watamuendea imaam, bwana, mbora wa viumbe na Mitume Muhammad bin

´Abdillaah (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Atasema mimi ndio mwenye

kuistahiki, na ndio maqaam al-Mahmuud aliomuahidi Allaah, kama

Alivyosema:

"Na amka usiku kwa ´ibaadah; ni ziada ya sunnah khasa kwako wewe.

Huenda Mola wako Akakunyanyua cheo kinacho sifika." (17:79)

Hakika kila Mtume alitanguliza maombi yake na Mtume kayaacha kwa

Ummah wake siku ya Qiyaamah. Ataenda na kwa unyenyekevu, amsifu na

amsujudie amuombe Allaah. Allaah Atamwambia "Inua kichwa chako, sema

utasikizwa, omba utapewa, ombea utakubaliwa."

Kisha Allaah Awahukumu waja wake:

"Je wanangoja mpaka Allaah Awajie katika vivuli vya mawingu pamoja na

Malaika, na hukumu iwe imekwishatolewa? Na kwa Allaah ndio hurejeshwa

mashauri yote." (02:210)

Allaah Awatahesabu waja katika siku hiyo:

"Hakuna yeyote miongoni mwetu ila atamuongelesha Mola wake, hakuna

baina yake [Allaah] na baina yake mtarjumu; akiangalia kuliani kwake haoni

ila [mema] alioyatanguliza, kushotoni kwake haoni ila [maovu]

alioyatanguliza; akiangalia mbeleni kwake haoni ila Moto. Ogopeni Moto

walau kwa nusu tende."

Atamfanyia hesabu Allaah mja wake muumini na kumkumbusha mabaya

yake yote, kisha Mola wake Atamwambia nilikusitiri duniani na leo pia

nitamsitiri. Atawahesabu waja na kuwakariria na kuwatajia ´amali zao,

Page 11: Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

hawawezi wakayakataa. Wakiyakataa [waliyoyafanya] ni kama Alivyosema

Allaah:

"Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi

miguu yao kwa waliyokuwa wakiyachuma." (36:65)

"Na wao wataziambia ngozi zao: “Kwa nini mmetushuhudilia?” Nazo

zitasema: “Ametutamkisha Allaah Ambaye ametamkisha kila kitu, na Yeye

ndiye Aliyekuumbeni mara ya kwanza, na kwake Yeye tumtarejeshwa”.”

(41:21)

Akikataa mja kukubali makosa yake, ataamrisha Allaah viungo vyake vitoe

ushahidi wa kila ´amali mpaka na ardhi aliokuwemo itashuhudia ima khayr

au shari:

"Siku hiyo itahadithia khabari zake." (99:04)

Kasema Mtume (´alayhis-Salaam):

"Khabari zake" ni kushuhudilia kila aliefanya juu yake [ardhi] ´amali ima za

khary au shari."

Allaah Atawafanyia hesabu waja, baadaye kutakuja kitabu cha kila mmoja

natija ya anaefanyiwa hesabu:

"Na kitawekwa kitabu. Basi utawaona wakosefu wanavyoogopa kwa yale

yaliomo humo. Na watasema: “Ole wetu! Kitabu hichi kina nini! Hakiachi

dogo wala kubwa ila huliandika?” Na watayakuta yote waliyoyatenda

yamehudhuria hapo. Na Mola wako hamdhulumu yeyote." (18:49)

"Na kila mtu tumemfungia ´amali yake shingoni mwake. Na Siku ya

Qiyaamah tutamtolea kitabu atakachokikuta kiwazi kimekunjuliwa.

Ataambiwa: Soma kitabu chako! Nafsi yako inakutosha leo kukuhisabu."

(17:13-14)

Vitabu vitagawiwa, kila mmoja atachukua kitabu chake ima atakichukua kwa

mkono wa kulia akisomea na kusema:

Page 12: Ewe Muislamu, Kumbuka Mauti - ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

"Atasema: Haya someni kitabu changu! Hakika nilijua ya kuwa nitapokea

hisabu yangu. Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza, katika Bustani

ya juu, matunda yake yakaribu. Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha

kwa sababu yamlivyo tanguliza katika siku zilizo pita." (69:20-24)

Kitabu chake atakishika kwa mkono wa kulia kwa enzi na saada. Kitabu cha

mafanikio hana shaka baada ya hapo, na neema haitomuondoka.

Kumeandikwa kwenye kitabu hichi:

"Bismillaahi Rahmaaniy Rahiym. Hichi ni kitabu kutoka kwa Mola wa

walimwengu, muingizeni fulani bin fulani Peponi..."

Hii ni neema na fadhila kubwa na natija nzuri kwa aliemuwafikisha Allaah

kumuimarisha na kujitahidi na akamuomba Allaah thabaat na Tawfiyq.

Asiekuwa muumini atakichukua kwa mkono wake wa kushoto au nyuma ya

mgongo wake huku akisema:

"Basi yeye atasema: “Laiti nisingelipewa kitabu changu! Wala nisingelijua nini

hisabu yangu. Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa. Mali

yangu hayakunifaa kitu. Madaraka yangu yamenipotea”." (69:25.29)

Hakuna yeyote ataingia Motoni ila atajua kuwa Moto unamstahiki kuliko

Pepo kutokana na uadilifu atauona kwa Allaah (Ta´ala).

Tunamuomba Allaah Usalama na afya. Ataezingatia kisimamo kama hichi

kikubwa, hali nzito, ataezingatia ukweli wa kukizingatia itamfanya azidishe

´amali njema; na kusimama na aliomuwajibishia Allaah juu yake, na

kukumbuka hali hizi iwe ni zawadi yake yeye ya kufanya ´amali njema kwa

yale Anayoyapenda Allaah na Kuyaridhia.

Chanzo: http://youtu.be/LuDeh8syfL4