al-barjas
DESCRIPTION
salafyTRANSCRIPT
![Page 1: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/1.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
1
www.firqatunnajia.com
امعتقد الصحيح الواجب على كل مسلم اعتقاد
al-Mu´taqad as-Swahiyh
[I´tiqaad sahihi wajibu kwa kila Muislamu kuiamini]
Mwandishi:
Shaykh ´Abdus-Salaam bin Barjas Aal ´Abdil-Kariym
Tarjama:
Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush
![Page 2: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/2.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
2
www.firqatunnajia.com
00. Dibaji ya kitabu al-Mu´taqad as-Swahiyh .................................................................................. 3
01. ´Aqiydah sahihi juu ya Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah ................................................................... 8
02. ´Aqiydah sahihi juu ya Tawhiyd al-Asmaa´ was-Swifaat ...................................................... 13
03. ´Aqiydah sahihi juu ya Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah .................................................................... 16
04. ´Aqiydah sahihi juu ya nguzo za imani sita ............................................................................. 24
05. ´Aqiydah sahihi juu ya imani ..................................................................................................... 51
06. Msimamo wa Ahl-us-Sunnah juu ya Takfiyr ........................................................................... 55
7. ´Aqiydah sahihi juu ya muislamu mtenda dhambi ................................................................... 57
08. ´Aqiydah sahihi juu ya Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa
sallam) .................................................................................................................................................. 61
09. ´Aqiydah sahihi juu ya watu wa nyumba ya kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa
sallam) .................................................................................................................................................. 66
10. ´Aqiydah sahihi juu ya karama za mawalii .............................................................................. 69
11. ´Aqiydah sahihi juu ya watawala wa waislamu ...................................................................... 71
12. Msimamo sahihi juu ya mijadala katika dini ........................................................................... 74
13. Matahadharisho ya kukaa na Ahl-ul-Ahwaa´ .......................................................................... 77
14. Hitimisho ya kitabu ..................................................................................................................... 79
![Page 3: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/3.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
3
www.firqatunnajia.com
00. Dibaji ya kitabu al-Mu´taqad as-Swahiyh
Himdi zote anastahiki Allaah. Swalah na salaam ziwe juu ya Mtume wa
Allaah, kizazi chake na Maswahabah zake.
Amma ba´d:
Hakika ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ndio dini ya haki ambayo
ni wajibu kwa kila muislamu aiitakidi, kwani ndio ´Aqiydah ya Mtume wa
Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na Maswahabah zake watukufu
(Radhiya Allaahu ´anhum). Atakayechagua ´Aqiydah nyingine, basi
ameipelekea nafsi yake katika adhabu, khasira na ghadhabu za Allaah kali.
Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kuhusu
mapote ambayo yatazuka katika Ummah wake na akataja mapote sabini na
tatu:
"Yote yatakuwa Motoni isipokuwa moja tu ambalo ni al-Jamaa´ah."1
Hakika Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesifu mkusanyiko huu
ambao umesalimika kutokamana na matishio ya Moto pale aliposema:
"Ni wale wataokuwemo katika mfano wa yale niliyomo mimi hii leo na
Maswahabah."2
Hiki ndio kidhibiti cha Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah. Hakika wao ni wenye
kushikamana na Sunnah za Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa
1 Ahmad na Abu Daawuud kutoka kwa Mu´aawiyah na ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Haakim, adh-Dhahabiy, ash-
Shaatwibiy na wengineo. Ahmad, Ibn Maajah na Ibn Abiy ´Aaswim kutoka kwa Anas.
2 Ameipokea al-Aajurriy katika "ash-Shariy´ah" kutoka ´Abdullaah bin ´Amr na at-Twabaraaniy katika "as-
Swaghiyrah" na katika "al-Awsatw" kutoka kwa Anas bin Maalik.
![Page 4: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/4.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
4
www.firqatunnajia.com
sallam) na Sunnah za makhaliyfah wake waongofu. Ni wenye kuziuma kwa
magego. Kwa ajili hio ndio maana wakawa ni pote lililookoka (Firqat-un-
Naajiyah). Ni wenye kuokoka na Moto siku ya Qiyaamah. Ni wenye
kusalimika na Bid´ah hapa duniani. Vilevile wao ni kundi lililonusuriwa
(Firqat-ul-Mansuurah). Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
"Hakutoacha kuwepo kipote katika Ummah wangu kuwepo katika haki
wazi wazi mpaka itapowajia amri ya Allaah ilihali wako wazi wazi."
"Hakutoacha kuwepo kipote kwenye Ummah wangu katika ushindi mpaka
itapowajia amri ya Allaah ilihali ni washindi."3
Maana ya kuwa wazi hapa ni nusura (Ta´ala):
فأيدنا الذين آموا على عدوهم فأصبحوا ظاهرين
"Tukawatia nguvu wale walioamini dhidi ya maadui zao, wakapambaukiwa wakiwa washindi." (61:149)
م الغالبون دنا وإن ج
"Na hakika jeshi Letu ndilo litakaloshinda." (37:173)
Wao ni wenye kushinda kwa panga na mikuki au kwa hoja na dalili. Inahusu
kundi moja na sio mengi. Kwa ajili hiyo ndio maana wameitwa ´mkusanyiko`.
Amesema (Ta´ala):
ل ق إ الض فماذا ب عد ا
"Na kuna nini baada ya haki ila upotofu." (10:32)
Hawatambuliki kwa jina lingine zaidi ya Uislamu na Sunnah na majina
mengine yenye dalili. Imaam Maalik (Rahimahu Allaah) amesema:
3 Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim kutoka kwa al-Mughiyrah bin Shu´bah.
![Page 5: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/5.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
5
www.firqatunnajia.com
"Ahl-us-Sunnah hawana jina lingine wanalotambulika kwalo, si Jahmiyyah,
Qadariyyah wala Raafidhwah."
Aliulizwa vilevile kuhusu as-Sunnah ambapo akajibu kwa kusema:
"Hawana jina lingine zaidi ya as-Sunnah."
Bi maana Ahl-us-Sunnah hawana jina wanalojinasibisha nalo zaidi yalo.
Kumetiliwa umuhimu mkubwa juu ya kuipa nguvu ´Aqiydah ya wema
waliotangulia (Salaf-us-Swaalih) na kubainishwa dalili zake. Imewekwa wazi
na maimamu wengi wakubwa katika vitabu vingi, vya kibinafsi na vya kwa
pamoja. Miongoni mwa vitabu hivyo kuna vinavyoitwa "as-Sunnah", bi
maana "´Aqiydah". Ni zaidi ya vitabu mia mbili na khamsini. Baadhi yavyo ni:
1 – ”as-Sunnah” ya Ibn Abiy ´Aaswim
2 – ”as-Sunnah” ya ´Abdullaah bin Imaam Ahmad
3 – ”as-Sunnah” ya al-Khallaal
4 – ”as-Sunnah” ya Ahmad bin al-Furaat Abiy Mas´uud ar-Raaziy
5 – ”as-Sunnah” ya Ismaa´iyl bin Usayd al-Madiyniy
6 – ”as-Sunnah” ya Ibn-ul-Qaasim – mwanafunzi wa Maalik
7 – ”as-Sunnah” ya Muhammad bin Salaam al-Baykandiy
8 – ”as-Swifaat wa ar-Radd ´alaa al-Jahmiyyah” ya Nu´aym bin Hammaad
9 – ”as-Sunnah” ya al-Athram
10 – ”as-Sunnah” ya Harb bin Ismaa´iyl al-Karmaaniy
11 – ”as-Sunnah” ya Ibn Abiy Haatim
12 – ”as-Sunnah” ya Ibn Jariyr at-Twabariy
13 – ”at-Tabasswur fiy ´Alam-id-Diyn” vilevile ni ya Ibn Jariyr
![Page 6: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/6.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
6
www.firqatunnajia.com
14 – ”as-Sunnah” ya at-Twabaraaniy
15 – ”as-Sunnah” ya Abush-Shaykh al-Aswbahaaniy
16 – ”as-Sunnah” ya Abul-Qaasim al-Laalakaa’iy
17 – ”as-Sunnah” ya Muhammad bin Naswr al-Marwaziy
18 – ”´Aqiydat-us-Salaf wa Asw-haab-il-Hadiyth” ya as-Swaabuuniy
19 – ”al-Ibaanah” ya Ibn Battwah
20 – ”at–Tawhiyd” ya Ibn Khuzaymah
21 – ”at-Tawhiyd” ya Ibn Manda
22 – ”al-Iymaan” ya Ibn Abiy Shaybah
23 – ”al-Iymaan” ya Abu ´Ubayd al-Qaasim bin Salaam
24 – ”Sharh-us-Sunnah” ya al-Muzaniy – mwanafunzi wa ash-Shaafi´iy
25 – ”Sharh-us-Sunnah” ya al-Baghawiy
26 – ”Sharh Madhaahib Ahl-is-Sunnah” ya Ibn Shaahiyn
27 – ”al-Hujjah fiy Bayaan-il-Mahajjah wa Sharh ´Aqiydah Ahl-is-Sunnah” ya
Abul-Qaasim al-Aswbahaaniy
28 – ”Usuul-us-Sunnah” ya Abu Abdullaah Ibn Abiy Zamaniyn
29 – ”ash-Shariy´ah” ya al-Aajurriy
30 – ”I´tiqaad Ahl-is-Sunnah” ya Abu Bakr al-Ismaa´iyliy
31 – ”as-Sunnah” ya al-Barbahaariy
32 – ”al-Iymaan” ya Ibn Manda
33 – ”al-Iymaan” ya al-´Adaniy
34 – ”al-´Arsh” ya Ibn Abiy Shaybah
![Page 7: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/7.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
7
www.firqatunnajia.com
35 – ”al-Qadar” ya Ibn Wahb
36 – ”al-Qadar” ya Abu Daawuud
37 – ”ar-Ru’yah” ya ad-Daaraqutwniy
38 – ”as-Swifaat” ya ad-Daaraqutwniy
39 – ”an-Nuzuul” ya ad-Daaraqutwniy
40 – ”Jawaab Ahl Dimashq fiys-Swifaat” ya al-Khatwiyb al-Baghdaadiy… na vitabu vinginevyo vingi.
Vivyo hivyo inahusiana na vitabu vilivyoandikwa baada ya waandishi hawa.
Miongoni mwao ni Ibn ´Abdil-Barr, Ibn Qudaamah al-Maqdisiy, Ibn
Taymiyyah, Ibn-ul-Qayyim, adh-Dhahabiy, Ibn Kathiyr, Muhammad bin
´Abdil-Wahhaab na wengineo. Humo mmebainishwa ´Aqiydah sahihi.
Vinasimamisha hoja na kufichua utata wa Ahl-ul-Ahwaa´.
Tutataja sehemu katika ´Aqiydah ya watu hawa vigogo.
Sipati kuwezeshwa haya isipokuwa na Allaah. Kwake Yeye ninategemea na
kwake Yeye naelekea.
![Page 8: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/8.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
8
www.firqatunnajia.com
01. ´Aqiydah sahihi juu ya Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah
Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wanaamini kuwa Allaah (Ta´ala) amepwekeka
juu ya kuumba, uola na uendeshaji wa mambo. Allaah (Ta´ala) amesema:
است وى على العرش ي غشي الل إن رض ستة أيام وم ربكم الل ه الذي خلق السماوات وا والقمر والج ياا والشم لبه ار ي يل المر مسخرات بأمر لق وا ت بارك الل ه ربج العالمي أ له ا
"Hakika Mola wenu ni Allaah Ambaye Ameumba mbingu na ardhi katika siku sita kisha akalingana juu ya ´Arshi. Anafunika usiku kwa mchana, unaufuatia upesi upesi na [ameumba] jua na mwezi na nyota vyote vimetiishwa kwa amri Yake. Tanabahi! Ni Vyake Pekee uumbaji na amri. Amebarikika Allaah, Mola wa walimwengu." (07:54)
رض لق ما يشاء لل ه ملك السماوات وا
"Ni wa Allaah Pekee ufalme wa mbingu na ardhi. Anaumba Atakavyo." (42:49)
رض له ملك يت السماوات وا وهو على كل شيء قدير يي و
"Ni Wake Pekee ufalme wa mbingu na ardhi, Anahuisha na Anafisha, Naye juu ya kila kitu ni Muweza." (57:02)
Tawhiyd hii inaitwa Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah na imekita katika nafsi ya kila
mwanaadamu. Hakuna mwanaadamu yeyote anayepingana nayo, sawa awe
muislamu au kafiri. Allaah (Ta´ala) amesema kuhusu makafiri:
رض لي قولن الل ه م من خلق السماوات وا ولئن سألت
"Na ukiwauliza: “Ni nani aliyeumba mbingu na ardhi?” bila shaka watasema: “Allaah." (31:25)
وما ي ؤمن أك رهم بالل ه إ وهم مجشركون
![Page 9: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/9.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
9
www.firqatunnajia.com
"Na wengi kati yao hawamwamini Allaah isipokuwa wao ni wenye kufanya shirki." (12:106)
Mujaahid amesema:
"Wanaamini kuwa Allaah ndio Muumbaji na Mruzukaji wao anayewafisha.
Hii ndio imani yao pamoja na kuwa wanamshirikisha na wengine."
Washirikina walikuwa hawaitakidi kuwa waungu wao wana sehemu katika
uumbaji wa Allaah. Walikuwa wakiamini kuwa Allaah ndiye mwenye
kuendesha hayo peke yake. Pamoja na hivyo walikuwa wakidai kuwa
wanawatumia waungu wao kwa kujikurubisha kwa Allaah na wawashufaie
Kwake. Amesema (Ta´ala):
الص الل ه زلفى أ لل ه الدين ا ذوا من دونه أولياء ما ن عبدهم إ لي قربونا إ والذين ا
"Tanabahi! Ni ya Allaah Pekee dini iliyotakasika. Na wale waliojichukulia badala Yake walinzi [husema]: “Hatuwaabudu isipokuwa ili watukurubishe kwa Allaah ukaribio."" (39:03)
م ش رض أم م على قل أرأي تم شركاءكم الذين تدعون من دون الل ه أرو ماذا خلقوا من ا اهم كتاباا ف ب ي ت رك السماوات أم آت ي م ب عضاا إ غروراا مه بل إن يعد الظالمون ب عض
"Sema: “Je, mnawaona washirika wenu ambao mnawaomba badala ya Allaah? Nionyesheni ni nini walichoumba katika ardhi au wana ushirika wowote mbinguni au Tumewapa kitabu chochote kile, kisha wao kwa hicho wakawa na hoja bayana?” Hapana! Bali hawaahidiani madhalimu wao kwa wao isipokuwa uongo." (35:40)
تا ون وي قولون أئا لتاركو آ م إل ه إ الل ه يستك م كانوا إذا قيل ون ل إن شاعر
"Hakika wao walipokuwa wakiambiwa: "hakuna mungu wa haki isipokuwa Allaah" wanatakabari na wanasema: “Je, sisi kweli tuache miungu yetu kwa ajili ya mshairi mwendawazimu?"" (37:35-36)
ا دا ا وا ا ة إل اب إن ه ذ أجعل ا ا لشيء ع
![Page 10: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/10.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
10
www.firqatunnajia.com
"Amewafanya miungu wote kuwa ni mungu mmoja? Hakika hili ni jambo la ajabu mno!" (38:05)
Allaah (Ta´ala) aliasisi Tawhiyd hii ili ihakikishwe, ithibitike na kumwelekeza mtu katika uwajibu wa Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah, kwa sababu Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah ni yenye kulazimisha mtu asimuabudu yeyote isipokuwa Allaah (Ta´ala). Allaah (Ta´ala) amesema:
ا الاس اعبدوا ربكم الذي خلقكم والذين من ق بلكم لعلكم ت ت قون يا أي ج
"Enyi watu! Mwabuduni Mola wenu Ambae Amekuumbeni na wale wa kabla yenu mpate kuwa na taqwa." (02:21)
لكم الل ه ربجكم له الملك تصرفون إل ه إ هو ذ فأ
"Huyo Ndiye Mola wenu Pekee Ana ufalme, hakuna mungu wa haki mwingine asiokuwa Yeye, basi vipi mnageuzwa?" (39:06)
م من خوف م من جوع وآم ف لي عبدوا رب ه ذا الب يت الذي أطعم
"Basi wamuabudu Mola wa nyumba hii. Ambaye Anawalisha kutokana na njaa na Akawapa amani kutokana na khofu." (106:03-04)
Allaah (Ta´ala) amesema kwamba Yeye peke yake ndiye Mwenye kuwaumba
na Mwenye kuwaruzuku, jambo ambalo hawana shaka nalo. Amefanya hilo
kuwa ni hoja dhidi yao ili iwe ni wajibu kumuabudu yeye peke yake, hali ya
kuwa hana mshirika. Allaah (Ta´ala):
مد لل ه وس الذين اصفى قل ا رض وأنزل لكم من السماء ماءا فأنبت م على عباد ر أما يشركون أمن خلق السماوات وا ا به آلل ه خي رها بتوا ش ة ما كان لكم أن ت دائق ذات ب اراا وجعل ع الل ه أإل ه م ا أن رض ق راراا وجعل خ بل هم ق وم ي عدلون أمن جعل ا
اجزاا ا رواسي وجعل ب ي البحرين يب الم أإل ه مع الل ه ويكشف السجوء وعلكم خلفاء بل أك رهم ي علمون أمن ر إذا دعا ضرض ديكم ظلمات الب ر والبحر ومن ي رسل الرياح بشراا ب ي يد أإل ه مع الل ه ا ا ما تذكرون أمن ي ته قلي ه مع أإل ي ر
الل ه الل ه عما يشركون ت عا
"Sema: "Sifa zote kamilifu na tukufu anastahiki Allaah na amani kwa waja Wake ambao Amewachagua. Je, Allaah ni bora au wale wanaowashirikisha? Au nani Aliyeumba mbingu na ardhi na Akakuteremshieni kutoka
![Page 11: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/11.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
11
www.firqatunnajia.com
mbinguni maji, kisha Tukaotesha kwayo mabustani anisi za kupendeza kabisa, nyinyi hamna uwezo wa kuotesha miti yake. Je, yuko mungu mwengine pamoja na Allaah? Bali wao ni watu wanaosawazisha. Au nani Aliyeijaalia ardhi kuwa mahali pa matulio na Akajaalia baina yake mito na Akaiwekea milima na Akajaalia baina ya bahari mbili kizuizi. Je, yuko mungu mwengine pamoja na Allaah? Bali wengi wao hawajui. Au nani Anayemuitika aliyedhikika anapomwomba, na Akamuondoshea dhiki, na Akakufanyeni makhalifa wa ardhi? Je, yuko mungu mwengine pamoja na Allaah? Ni machache mno mnayokumbuka. Au nani Anayekuongozeni katika viza vya nchi kavu na bahari na nani anayetuma pepo za bishara kabla ya Rahmah Yake. Je, yuko mungu mwengine pamoja na Allaah? Ametukuka Allaah kutokana na yale wanayomshirikisha."" (27:59:63)
Katika Aayah zote hizi Allaah (Ta´ala) anawakemea washirikina wanaokiri kuwa Allaah (Ta´ala) peke yake ndiye muumbaji wa mbingu na ardhi na mwenye kunufaisha na kudhuru. Pamoja na hivyo kukiri kwao huku hakukuwanufaisha kitu, kwa sababu walimshirikisha Allaah pamoja na waungu wengine ambao walikuwa wakiwaabudu kama wanavyomuabudu Allaah. Hakika nadharia hii inaenda kinyume na Shari´ah na akili. Ambaye amepwekeka katika mambo yote haya - kama kuumba, kuruzuku, kuhuisha na kufisha - ndiye mwenye haki ya kutekelezewa utiifu aina yote. Ndio maana Allaah (Ta´ala) amewakemea pale aliposema:
أإل ه مع الل ه
"Je, yuko mungu mwengine pamoja na Allaah?"
Hata hivyo hakusema:
"Je, kuna muumbaji mwengine pamoja na Allaah," kwa sababu walikuwa ni
wenye kuthibitisha hili.
Allaah (Ta´ala) amebainisha ni ubatilifu uliyoje kuwa na mshirika katika uola.
Lau angelikuwepo mwengine aliye na sehemu katika hilo, basi mbingu na
ardhi vingeharibika. Hili ni lenye kufahamika pia kwa akili ya kimaumbile.
Allaah (Ta´ala):
ذ الل ه من ولد وما كان معه من إل ه م على ب عض إذاا لذهب ك ما ا ب عض ا خلق ولع سبحان الل ه عما يصفون لج إل ه
![Page 12: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/12.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
12
www.firqatunnajia.com
"Allaah Hakujifanyia mwana yeyote na wala hakukuwa pamoja Naye mungu yeyote - hapo bila shaka kila mungu angelichukua vile alivyoviumba na bila shaka baadhi yao wangeliwashinda wengineo. Utakasifu ni wa Allaah kutokana na yale wanayoyaelezea." (23:91)
ة إ الل ه لفسدتا ما آ لو كان في
"Lau wangelikuweko humo miungu mingi asiyekuwa Allaah, bila shaka zingelifisidika." (21:22)
![Page 13: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/13.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
13
www.firqatunnajia.com
02. ´Aqiydah sahihi juu ya Tawhiyd al-Asmaa´ was-Swifaat
Miongoni mwa ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni pamoja na
kwamba wanathibitisha majina mazuri na sifa tukufu ambazo Allaah (Ta´ala)
amejithibitishia katika nafsi yake na ambazo Mtume Wake (Swalla Allaahu
´alayhi wa sallam) amemthibitishia. Hawavuki Qur-aan na zile Hadiyth
zilizothibiti kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Wanathibitisha hayo kimatamshi na wanatambua maana yake katika lugha ya
kiarabu ambayo Qur-aan imeteremshwa kwayo. Hata hivyo namna yake
wanamwachia Allaah (Ta´ala), kwa kuwa ni maalum kwa Allaah (Ta´ala) na
hakuna mwengine yeyote mwenye ujuzi kwazo.
Katika mlango huu wa khatari wanapita kutokamana na misingi ya Kishari´ah
iliyothibiti; yule mwenye kushikamana nayo basi amesalimika na upindaji.
Wa kwanza: Kuthibitisha yale ambayo Allaah (Ta´ala) amejithibitishia nayo
katika nafsi yake na yale ambayo Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa
sallam) amemthibitishia. Haya yanatakiwa kufanyika pasi na kuongeza wala
kupunguza, kwa kuwa hakuna yeyote ambaye ni mjuzi wa kumtambua
Allaah (Ta´ala) kuliko Allaah Mwenyewe:
قل أأنتم أعلم أم الل ه
“Je nyinyi mnajua zaidi au Allaah?" (02:140)
Hakuna mwanaadamu yeyote ambaye ni mjuzi wa kumtambua Allaah kuliko
Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Allaah (Ta´ala)
amesema:
ى ي يو وى إن هو إ و ق عن ا وما ي
"Na wala hatamki kwa matamanio yake. Hayo ayasemayo si chochote isipokuwa ni Wahy unaofunuliwa kwake." (53:03-04)
![Page 14: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/14.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
14
www.firqatunnajia.com
Wa pili: Mtu amtakase Allaah (Ta´ala) na kushabihiana na sifa za viumbe. Allaah (Ta´ala):
كمله شيء وهو السميع البصي لي
"Hakuna chochote kinachofanana Naye - Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona." (42:11)
د يكن له كفواا أ و
“Na wala haiwi Awe na yeyote anayefanana na kulingana Naye." (112:04)
Wa tatu: Mtu asijaribu kufikiria sifa Zake. Allaah (Ta´ala):
ا يون به علما و
"Na wala wao hawawezi kuzunguka elimu Yake." (20:110)
يا هل ت علم له
"Je, unamjua mwengine mwenye Jina kama Lake?" (19:65)
Miongoni mwa sifa hizi ni pamoja na maneno Yake (Ta´ala):
ن على العرش است وى الر
"Mwingi wa Rahmah amelingana juu ya ´Arshi." (20:05)
Haya yametajwa sehemu nyingi katika Qur-aan. Hapa mtu anatakiwa
kuelewa ya kwamba kulingana kwa Allaah juu ya ´Arshi ni kulingana
kihakika. Tunaelewa maana yake na hatujui namna yake. Maana yake ni kuwa
juu na kungatika. Haya ndio yenye kufahamishwa na lugha ya kiarabu. Ahl-
us-Sunnah wal-Jamaa´ah wamekubaliana juu ya maana hii. Kuhusiana na
namna ya kulingana huku, hakuna yeyote anayeijua isipokuwa Allaah peke
yake - hali ya kuwa hana mshirika.
Hali kadhalika Allaah (Ta´ala) anasema:
![Page 15: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/15.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
15
www.firqatunnajia.com
كموا با كمتم ب ي الاس أن ا وإذا أهل مانات إ يعاا إن الل ه نعما يعظكم به لعدل إن الل ه يأمركم أن ت ؤدجوا ا إن الل ه كان بصياا
"Hakika Allaah Anakuamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe na mtakapohukumu baina ya watu mhukumu kwa uadilifu. Hakika uzuri ulioje wa mawaidha Anayokuwaidhini nayo Allaah! Hakika Allaah daima ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona." (04:58)
Hapa kunathibitishwa usikizi wa Allaah. Kwa mujibu wa lugha ya kiarabu
usikizi maana yake ni "kufikia sauti".
Tunamthibitishia Allaah (Ta´ala) usikizi ambao anafikia kwao sauti. Usikizi
huu haufanani na usikizi wa viumbe vya Allaah. Kuhusu namna yake,
tunamwachia Allaah (Ta´ala). Hivyo hatusemi: "Anasikia vipi?" Hatujiingizi
katika hilo, kwa kuwa Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) hakutufanya tujue hilo.
Bali ni katika mambo ambayo Allaah (Jalla wa ´Alaa) peke yake ndiye
mwenye ujuzi kwayo.
Vivyo hivyo inahusu uoni; kufikia vyenye kuonwa. Imethibiti katika "as-
Swahiyh" ya Muslim kutoka kwa Abu Muusa al-Ash´ariy ya kwamba Mtume
(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
"Hakika Allaah halali na wala haimstahikii Yeye kulala. Huteremsha
uadilifu na huupandisha. Kwake kunanyanyuliwa matendo ya usiku kabla
ya matendo ya mchana na matendo ya mchana kabla ya matendo ya usiku.
Pazia Yake ni nuru; lau ataiondosha basi nuru ya uso na enzi Yake
ingeliunguza kila kiumbe Chake ambapo unafikia uoni Wake."
Tunamthibitishia Allaah uoni wa kihakika ambao kwao anafikia vyenye
kuonwa. Pamoja na kwamba hatuna ujuzi wowote kuhusu namna ya uoni
huu.
Hii ni baadhi ya mifano ya namna ambavyo Ahl-us-Sunnah wanaamini majina
na sifa za Allaah.
![Page 16: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/16.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
16
www.firqatunnajia.com
03. ´Aqiydah sahihi juu ya Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah
Miongoni mwa ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni pamoja na mtu
kumpwekesha Allaah (Ta´ala) katika ´ibaadah. Hawaabudu mwengine
pamoja na Allaah. Badala yake wanamtekelezea aina zote za ´ibaadah za
wajibu na za mapendekezo Allaah, hali ya kuwa hana mshirika.
Hawamsujudii yeyote isipokuwa Allaah. Hawamfanyii Twawaaf yeyote
isipokuwa Allaah. Hawachinji kwa ajili ya yeyote isipokuwa Allaah.
Hawamuwekei nadhiri isipokuwa Allaah. Hawaapi kwa yeyote isipokuwa
kwa Allaah. Hawategemei isipokuwa kwa Allaah. Hawamuombi yeyote
isipokuwa Allaah. Hii ndio Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah:
واعبدوا الل ه و تشركوا به شيئاا
"Na mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote." (04:36)
وقضى ربجك أ ت عبدوا إ إيا
"Na Mola wako Amehukumu kwamba: “Msiabudu yeyote isipokuwa Yeye."" (17:23)
او دا ا وا ا ما أمروا إ لي عبدوا إل
"Hawakuamrishwa isipokuwa kumwabudu mungu wa haki Mmoja." (09:31)
لصي له الدين وما أمروا إ لي عبدوا الل ه
"Na hawakuamrishwa isipokuwa wamwabudu Allaah hali ya kuwa ni wenye kumtakasia Yeye dini." (98:05)
إ لي عبدون ن ن وا وما خلقت ا
"Na Sikuumba majini na wanadamu isipokuwa waniabudu." (51:56)
Waniabudu maana yake ni "wanipwekeshe mimi tu".
![Page 17: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/17.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
17
www.firqatunnajia.com
Kinyume chake ni shirki - Allaah atukinge nayo. Shirki ndio dhambi kubwa
ambayo Allaah ameasiwa kwayo. Amesema (Ta´ala):
لك لمن يشاء ومن يشرك بالل ه ف قد اف ت رى إاا عظيماا إن الل ه ي غفر أن يشرك به وي غفر ما دون ذ
"Hakika Allaah hasamehi kushirikishwa, lakini anasamehe yaliyo chini ya hayo kwa Amtakae. Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amebuni dhambi kuu." (04:48)
لك لمن يشاء ا ومن يشرك بالل ه ف قد ضل إن الل ه ي غفر أن يشرك به وي غفر ما دون ذ ا بعيدا ض
"Hakika Allaah hasamehi kushirikishwa, lakini anasamehe yaliyo chini ya hayo kwa Amtakae. Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amepotoka upotofu wa mbali." (04:116)
ر مشركي به فاء لل ه غي وي به الريح مكان سحيق ومن يش ر أو ت ا خر من السماء ف تخفه الي رك بالل ه فكأ
"Muelemee haki kwa Allaah bila ya kumshirikisha. Na yeyote anayemshirikisha Allaah basi kama kwamba ameporomoka kutoka mbinguni, wakamnyakua ndege au upepo ukamtupa mahali mbali mno." (22:31)
تشرك بالل ه به وهو يعظه يا ب إن الشرك لظلم عظيم وإذ قال لقمان
"Na Luqmaan alipomwambia mwanawe huku akimuwaidhi: “Ee mwanangu! Usimshirikishe Allaah, hakika shirki ni dhulma kuu!"" (31:13)
Amebainisha (Ta´ala) ya kwamba shirki inabatilisha matendo yote na inamtoa
mtu katika Uislamu. Amesema (Ta´ala):
م ما كانوا ي عملون بط ع ولو أشركوا
"Na kama wangemshirikisha bila shaka yangebatilika yale waliyokuwa wakitenda." (06:88)
اس ن عملك ولتكونن من ا الذين من ق بلك لئن أشركت ليحب ي إليك وإ رين ولقد أو
![Page 18: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/18.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
18
www.firqatunnajia.com
"Kwa yakini umefunuliwa Wahy na kwa wale walio kabla yako: “Ukifanya shirki bila shaka zitabatilika ‘amali zako na bila shaka utakuwa miongoni mwa waliokhasirika."" (39:65)
Katika "as-Swahiyh" ya Muslim kutoka kwa Jaabir bin ´Abdillaah (Radhiya
Allaahu ´anh) ameeleza ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi
wa sallam) amesema:
"Mwenye kukutana na Allaah pasi na kumshirikisha Yeye na chochote,
ataingia Peponi, na mwenye kukutana Naye ilihali anamshirikisha Yeye na
chochote, ataingia Motoni."
Katika "as-Swahiyh" ya al-Bukhaariy kutoka kwa Ibn Mas´uud (Radhiya
Allaahu ´anh) ameeleza ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi
wa sallam) amesema:
"Mwenye kufa ilihali ni mwenye kuomba mwenza asiyekuwa Allaah,
ataingia Motoni."
Yule mwenye kufanya aina yoyote ile ya ´ibaadah akamfanyia asiyekuwa
Allaah, basi huyo ni mshirikina kafiri.
Kwa mfano du´aa ni moja miongoni mwa ´ibaadah ambazo Allaah
ameamrisha. Hivyo basi, yule mwenye kumuomba Allaah peke yake, huyo ni
mpwekeshaji. Upande mwingine, yule mwenye kumuomba asiyekuwa
Allaah, ameshirikisha. Amesema (Ta´ala):
فعك و يضرجك فإن ف علت فإنك إذاا من الظالمي و تدع من دون الل ه ما ي
“Wala usiombe badala ya Allaah asiyekufaa na wala asiyekudhuru. Endapo utafanya hivo, basi hakika utakuwa miongoni mwa madhalimu." (10:106)
د ربه سابه ع ا ا آخر ب رهان له به فإ ا إنه ي فلح الكافرون ومن يدع مع الل ه إل
"Na yeyote yule anayeomba pamoja na Allaah mungu mwengine hana ushahidi wa wazi wa hilo, basi hakika hesabu yake iko kwa Mola wake - hakika hawafaulu makafiri." (23:117)
![Page 19: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/19.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
19
www.firqatunnajia.com
ا وأنه لما قام عبد الل ه يدعو كادوا ي دا تدعوا مع الل ه أ ا أدعو ر و أشرك به وأن المساجد لل ه ف ا قل إ دا كونون عليه لبدا أ
"Na kwamba mahala pote pa kuswalia ni kwa ajili ya Allaah Pekee, basi msiombe yeyote pamoja na Allaah. Na kwamba mja wa Allaah aliposimama kumwomba, walikaribia kumzonga. Sema: “Hakika mimi namuomba Mola wangu Pekee na wala simshirikishi na yeyote."" (72:18-20)
ق لغ فا له دعوة ا الماء ليب م بشيء إ كباسط كفيه إ يبون وما دعاء الكافرين وما هو ببالغه والذين يدعون من دونه يستل إ ض
"Kwake ndiko kuna maombi yote ya haki. Na wale wenye kuomba badala Yake hawawaitikii kwa chochote isipokuwa kama anayenyosha viganja vyake viwili vya mikono kwenye maji ili yafikie kinywani mwake, wala hayafikii - na du’aa za makafiri hazipo ila katika upotofu." (13:14)
ياء و ر أ لقون أموات غي لقون شيئاا وهم عون الذين يدعون من دون الل ه وما يشعرون أيان ي ب
"Na wale wanaowaomba badala ya Allaah hawaumbi kitu chochote, bali wao wanaumbwa. Ni maiti si wahai na hawatambui lini watafufuliwa." (16:20-21)
ا آخر ف تكون من المعذبي ا تدع مع الل ه إل ف
"Basi usiombe pamoja na Allaah mungu mwengine ukaja kuwa miongoni mwa watakaoadhibiwa." (26:213)
ار ويولج ال جل مجسمىيولج الليل ال ري والقمر كل ار الليل وسخر الشم لكم الل ه ربجكم له الملك والذين تدعون ذمي لكون من ق ع من دونه ما ابوا لكم إن تدعوهم يسمعوا دعاءكم ولو و ي بئك وي وم القيامة يكفرون بشرككم وا ما است
مل خبي
"Anauingiza usiku katika mchana na Anauingiza mchana katika usiku na Anaitisha jua na mwezi - kila kimoja kinakwenda mpaka muda maalumu uliokadiriwa. Huyo Ndiye Allaah Mola wenu, ufalme ni Wake Pekee. Na wale mnaowaomba badala Yake hawamiliki hata kijiwavu cha kokwa ya tende. Mkiwaomba, hawasikii maombi yenu na hata wakisikia, hawatakuitikieni. Na Siku ya Qiyaamah watakanusha ushirikina wenu na wala hakuna atakayekujulisha kama Mjuzi." (35:13-14)
![Page 20: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/20.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
20
www.firqatunnajia.com
رض لي قولن الل ه م من خلق السماوات وا الل ه بضر هل هن كاشفات ضر أو ولئن سألت قل أف رأي تم ما تدعون من دون الل ه إن أراد سكات ر ة هل هن الل ه ته أراد بر س عليه ي ت وكل المت وكلون قل
"Na ukiwauliza: “Ni nani aliyeumba mbingu na ardhi?” Bila shaka watasema: “Allaah." Sema: “Je, mnaonaje wale mnaowaomba badala ya Allaah ikiwa Allaah Atanikusudia dhara, je, wao wataweza kuondosha dhara Yake? Au Akinikusudia Rahmah, je, wao wataweza kuizuia Rahmah Yake?” Sema: “Ananitosheleza Allaah”, Kwake wategemee wenye kutegemea."" (39:38)
رض أم م شرك السماوات قل أرأي تم ما تدعون من دون الل ه أرو ماذا خلقوا من ا ائ تو بكتاب من ق بل ه ذا أو أثارة من علم إن ي وم القيامة وه يب له إ تم صادقي ومن أضلج ن يدعو من دون الل ه من يست م غافل ك م م عن دعائ شر الاس كانوا ون وإذا
م كافرين أعداءا وكانوا بعباد
"Sema: “Je, mnaonaje wale mnaowaomba badala ya Allaah! Nionyesheni nini wameumba katika ardhi au wana ushirika katika mbingu? Nileteeni Kitabu kabla ya hiki au alama yeyote iliobakia ya elimu mkiwa wakweli". Na nani aliyepotoka zaidi kuliko ambaye anayeomba asiyekuwa Allaah ambaye hamuitikii mpaka Siku ya Qiyaamah nao kuhusu du’aa zao ni wenye kughafilika. Na [siku ya Qiyaamah] watakapokusanywa watu [miungu ya uongo] watakuwa maadui wao na watakuwa kwa ‘ibaadah zao ni wenye kuzikanusha." (46:04-06)
Imethibiti katika "as-Sunan" kutoka kwa an-Nu´maan bin Bashiyr (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza kwamba amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:
"Du´aa ndio ´ibaadah."
Tawhiyd hii - Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah - ndio ambayo kulitokea magomvi kati
ya Mitume na watu wao. Tawhiyd hii ndio sababu ya Allaah kuwatuma
Mitume kwa ajili ya kuibainisha na kulingania kwayo. Hali kadhalika
Akateremsha Vitabu kwa ajili ya kuihakikisha, kuiweka wazi na kutumia hoja
kwayo. Amesema (Ta´ala):
ولقد ب ع ا كل أمة رسوا أن اعبدوا الل ه واجتبوا الاغوت
![Page 21: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/21.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
21
www.firqatunnajia.com
"Na kwa yakini Tulituma katika kila ummah Mtume [awaamrishe watu wake] kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na miungu ya uongo." (16:36)
ي إليه أنه إل ه إ أنا فاعبدون وما أرسلا م ن ق بلك من رسول إ نو
"Na Hatukutuma kabla yako Mtume yeyote isipokuwa Tulimfunulia Wahy ya kwamba: “Hakika hapana mungu wa haki ila Mimi, basi Niabuduni."" (21:25)
زل الم أن أنذروا أنه إل ه إ أنا فات قون ي ئكة بالرجوح من أمر على من يشاء من عباد
"Anateremsha Malaika na Roho kwa amri Yake juu ya Amtakaye miongoni mwa waja Wake, kwamba: “Onyeni: Hakika hapana mungu wa haki ila Mimi basi Nicheni."" (16:02)
Hii ndio ambayo Mitume kwanza walikuwa wakianza kuwaamrisha watu
wao pindi walipokuwa wakiwalingania katika dini ya Allaah. Kila Mtume
alikuwa akiwaamrisha watu wake:
ر يا ق وم اعبدوا الل ه ما لكم من إل ه غ ي
“Enyi watu wangu! Mwabuduni Allaah, hakika hamna mungu mwingine wa haki asiokuwa Yeye." (07:59,65,73,85)
Nuuh alisema hivyo na hali kadhalika Huud, Swaalih, Shu´ayb na Mitume wengine wote - swalah na salaam ziwashukie wote.
Allaah (Ta´ala) amesema:
ا ت عبدون من دون الل ه أوثاناا ولقون إفكاا وإب راهيم إذ قال لقومه اعبدوا الل ه وات قو تم ت علمون إ ر لكم إن ك لكم خي إن الذين ذلكون د الل ه الرزق واعبدو واشكروا له ت عبدون من دون الل ه إليه ت رجعون لكم رزقاا فاب ت غوا ع
"Ibraahiym alipowaambia watu wake: “Mwabuduni Allaah na mcheni. Hivyo ni kheri kwenu mkiwa mnajua. Hakika mnaabudu badala ya Allaah masanamu na mnazua uzushi. Hakika wale mnaowaabudu badala ya Allaah hawakumilikiini riziki, basi tafuteni riziki kwa Allaah na mwabuduni Yeye na mshukuruni, Kwake mtarejeshwa." (29:16-17)
![Page 22: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/22.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
22
www.firqatunnajia.com
Vilevile amesema (Ta´ala) kuhusu Mtume Wake Yuusuf (´alayhis-Salaam):
ا اءا يا صا ار ما ت عبدون من دونه إ أ د الق ر أم الل ه الوا ن أأرباب مجت فرقون خي ا من لس يتموها أنتم وآباؤكم ما أنزل الل ه كم إ لل ه سلان لك الدين القيم ول كن أك ر الاس ي علمون بدوا إ إيا أمر أ ت ع إن ا ذ
“Enyi masahibu wangu wawili wa jela! Je, waungu wengi wanaofarakana ni bora au Allaah ambaye ni Mmoja Pekee, Mwenye nguvu? Hamuabudu badala Yake isipokuwa majina [ya masanamu] mmeyaita nyinyi na baba zenu - hakuyateremshia Allaah kwayo ushahidi wowote. Hakuna hukumu isipokuwa ya Allaah. Ameamrisha kwamba msimwabudu yeyote isipokuwa Yeye Pekee - hiyo ndio dini iliyonyooka, lakini watu wengi hawajui." (12:39-40)
Washirikina hawana mashiko yoyote kwa ushirikina wao. Hawawezi kupata
mashiko yoyote kutoka katika akili sahihi wala andiko kutoka kwa Mitume.
Amesema (Ta´ala):
ةا ي عبدون ن آ واسأل من أرسلا من ق بلك من رجسلا أجعلا من دون الر
“Na waulize wale Tuliowatuma kabla yako miongoni mwa Mitume Wetu, je, Tulifanya badala ya Mwingi wa Rahmah miungu mingine iabudiwe?" (43:45)
Maana yake ni kwamba hakuna Mtume yeyote ambaye alimwita mtu
kuabudu chochote pamoja na Allaah. Bali wote, kuanzia wa kwanza wao hadi
wa mwisho wao, walikuwa ni wenye kuita katika kumuabudu Allaah Mmoja
wa Pekee, hali ya kuwa hana mshirina. Amesema (Ta´ala):
م شرك السماوات ق رض أم ائ تو بكتاب من ق بل ه ذا أو أثارة من علم إن ل أرأي تم ما تدعون من دون الل ه أرو ماذا خلقوا من اتم صادقي ك
"Sema: “Je, mnaonaje wale mnaowaomba badala ya Allaah! Nionyesheni nini wameumba katika ardhi au wana ushirika katika mbingu? Nileteeni Kitabu kabla ya hiki au alama yeyote iliobakia ya elimu mkiwa wakweli." (46:04)
![Page 23: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/23.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
23
www.firqatunnajia.com
Kutokana na yaliyotangulia, inapata kufahamika kuwa Tawhiyd hii ndio wajibu wa kwanza, jambo la kwanza la wajibu na ndio dini pekee ambayo Allaah anaikubali.
![Page 24: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/24.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
24
www.firqatunnajia.com
04. ´Aqiydah sahihi juu ya nguzo za imani sita
Miongoni mwa ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni kumuamini
Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Mitume Wake, kufufuliwa baada ya
kufa na kuamini Qadar.
Imani ya kumuamini Allaah ni kuthibitisha Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah,
Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah na Tawhiyd al-Asmaa´ was-Swifaat, jambo ambalo
tumeshatangulia kulitaja.
Imani ya kuamini Malaika ni kuthibitisha na kuamini uwepo wao, majina yao
yaliyotajwa na matendo yao yaliyotajwa. Amesema (Ta´ala):
ا أنزل إليه من ربه والمؤمون د من رجسله آمن الرسول ئكته وكتبه ورسله ن فرق ب ي أ كل آمن بالل ه وم
"Mtume ameamini yaliyoteremshwa kwake kutoka kwa Mola wake na waumini. Wote wamemwamini Allaah, na Malaika Wake, na Vitabu Vyake, na Mitume Wake. [Nao husema:] Hatutafautishi baina ya yeyote kati ya Mitume Wake."" (02:285)
من آمن بال أن ت ولجوا وجوهكم قبل المشرق والمغرب ول كن ال ال ئكة والكتاب والبيي لي خر والم ل ه والي وم ا
"Wema haina maana ya kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa mashariki na magharibi, lakini wema khasa ni mwenye kuamini Allaah na Siku ya Mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii." (02:177)
Katika "as-Swahiyh" ya Muslim ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu
´anh) amepokea katika Hadiyth yake ndefu kuhusu swali la Jibriyl
alipomuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) juu ya imani. Akajibu
ifuatavyo:
"Imani ni kumuamini Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake, siku ya
Mwisho na kuamini Qadar; kheri na shari yake."
Allaah (Ta´ala) amewasifu katika Kitabu Chake ifuatavyo:
رض ار ي فت رون وله من السماوات وا ون عن عبادته و يستحسرون يسبحون الليل وال يستك د ومن ع
![Page 25: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/25.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
25
www.firqatunnajia.com
"Na ni Vyake Pekee vyote vilivyomo katika mbingu na ardhi na wale walio Kwake hawatakabari na ‘ibaadah Yake na wala hawachoki. Wanasabihi usiku na mchana wala hawazembei." (21:19-20)
ا ن ولدا ذ الر بل عباد مجكرمون يسبقونه بالقول وهم بأمر ي عملون سبحانه وقالوا ا
"Na wakasema: “Mwingi wa Rahmah Amejichukulia mwana. Utakasifu ni Wake! Bali [hao Malaika] ni waja waliokirimiwa. Hawamtangulii kwa kauli nao kwa amri Yake wanafanya." (21:26-27)
ون عن عبادته ويسبحونه وله يس د ربك يستك دون إن الذين ع
"Hakika wale walioko kwa Mola wako hawatakabari kufanya ‘ibaadah Yake na wanamsabihi na Kwake Pekee wanasujudu." (07:206)
Wao ni waja na viumbe miongoni mwa viumbe vya Allaah (Ta´ala) wakubwa. Malaika hawastahiki chochote katika ´ibaadah. Amesema (Ta´ala):
ء إياكم كانوا ي عبدون قالوا سبحانك ئكة أه ؤ ي قول للم يعاا شرهم ن أنت ولي جا من دوم وي وم أك رهم بل كانوا ي عبدون ا م مجؤمون
"Na Siku Atakayowakusanya wote kisha Atawaambia Malaika: “Je, hawa ndio waliokuwa wakikuabuduni?” Watasema: "Utakasifu ni Wako! Wewe ni mlinzi wetu sio hao. Bali walikuwa wakiabudu majini, wengi wao wakiwaamini."" (34:40-41)
ئكة و أيأمركم بالكفر ب عد إذ أنتم مجسلمون البيي أربابااو يأمركم أن ت تخذوا الم
"Na wala hakuamuruni kuwachukua Malaika na Manabii kuwafanya miungu. Je, anakuamrisheni ukafiri baada ya nyinyi kuwa waislamu?" (03:80)
Katika "as-Swahiyh" ya Muslim ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amepokea
ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
"Malaika wameumbwa kutokamana na nuru, majini wameumbwa
kutokamana na moto na Aadam ameumbwa kutokamana na kile
kilichosifiwa kwenu."
![Page 26: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/26.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
26
www.firqatunnajia.com
Miongoni mwa sifa zao ni kwamba wana mbawa. Katika wao kuna ambao
wana mbawa mbili, wengine wana mbawa tatu, wengine wana mbawa nne na
kadhalika. Amesema (Ta´ala):
ث ور وث ا أو أجحة م ئكة رس رض جاعل الم مد لل ه فاطر السماوات وا لق ما يشاء باع ا إن الل ه على كل يزيد ا شيء قدير
"Himidi zote Anastahiki Allaah muanzilishi wa mbingu na ardhi, Mwenye kuwafanya Malaika kuwa wajumbe wenye mbawa mbilimbili, tatutatu na nnenne. Huzidisha katika uumbaji Atakavyo. Hakika Allaah juu ya kila kitu ni Muweza." (35:01)
Katika "as-Swahiyh" ya al-Bukhaariy kumepokelewa kutoka kwa Ibn Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anh) kwamba:
"Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimuona Jibriyl akiwa na
mbawa mia sita."
Allaah (Ta´ala) amewapa uwezo wa kuweza kujigeuza katika maumbile
mazuri. Kama ambavyo Jibriyl (´alayhis-Salaam) alivyojigeuza kwa Maryam
katika umbile la mtu wa sawa. Vivyo hivyo kama walivyojidhihirisha kama
wageni wawili watukufu pindi walipomtembelea Ibraahiym (´alayhis-
Swalaatu was-Salaam) na hali kadhalika wakafanya pindi walipomjia Luutw
(´alayhis-Salaam) ili kuwaadhibu watu wake na mfano wa hivo.
Allaah amewakemea washirikina ambao wamedai kuwa Malaika ni mabanati
wa Allaah - Allaah ametakasika na yale ambayo madhalimu wanasema.
Amesema (Ta´ala):
ا ن ولدا ذ الر م وما خ سبحانه وقالوا ا م و يشفعون بل عباد مجكرمون يسبقونه بالقول وهم بأمر ي عملون ي علم ما ب ي أيدي لف مشفقون إ لمن ارتضى وهم من خشيته
"Na wakasema: “Mwingi wa Rahmah Amejifanyia mwana. Utakasifu ni Wake! Bali [hao Malaika] ni waja waliokirimiwa. Hawamtangulii kwa kauli nao kwa amri Yake wanafanya. Anajua yale yaliyoko mbele yao, na yale yaliyoko nyuma yao na wala hawamuombei uombezi yeyote yule
![Page 27: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/27.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
27
www.firqatunnajia.com
isipokuwa kwa yule ambaye Amemridhia. Nao kutokana na kumkhofu, ni wenye kutahadhari." (21:26-28)
Baada ya hapo amesema (Ta´ala) kuhusu Malaika:
ئكة إ م الب ون أم خلقا الم م ألربك الب ات و م لكاذبون أصفى فاست فت م لي قولون ولد الل ه وإن م من إفك ناثاا وهم شاهدون أ إن تذكرون أم لكم سلان مجبي فأتوا بكت كمون أف تم صادقي ابكم إ الب ات على البي ما لكم كيف ن ك
"Waulize: “Je, Mola wako ndio ana mabanati na wao ndio wana watoto wa kiume au Tumewaumba Malaika kuwa wanawake nao wameshuhudia? Tanabahi! Hakika wao kwa uzushi wanasema: “Allaah Amezaa." Na hakika wao bila shaka ni waongo kweli kweli. Je, Amechagua mabanati kuliko wana wa kiume? Mna nini! Vipi mnahukumu? Je, hamkumbuki? Je, mna hoja bayana? Basi leteni kitabu chenu mkiwa ni wakweli." (37:149-157)
حن المسبحون وما ما إ له مقام معلوم وإنا لحن الصافجون وإنا ل
"Na hakuna miongoni mwetu isipokuwa ana mahali maalumu. Na hakika sisi bila shaka tutajipanga safu. Na hakika sisi bila shaka ni wenye kumsabihi." (37:164-166)
Miongoni mwao ni Jibriyl (´alayhis-Salaam). Kazi yake ni kupeleka Wahy. Amesema (Ta´ala):
يل فإنه ن زله على ق لبك بإذن الل ه قل من كان عدوا
"Sema: “Yeyote aliyekuwa adui wa Jibriyl, basi hakika yeye ameiteremsha Qur-aan katika moyo wako kwa idhini ya Allaah."" (02:97)
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimuona juu na mbawa zake mia
sita na umbile lake kubwa limefunika upeo wa juu. Kisha baada ya hapo
akamuona mbinguni usiku wa safari ya mbinguni. Amesema (Ta´ala):
دها ى ع ت د سدرة الم ن زلةا أخرى ع جة المأوى ولقد رآ
"Na kwa yakini amemuona katika uteremko mwingine. Kwenye mkunazi wa mpaka wa mwisho kabisa. Karibu yake ndio ipo bustani inayokaliwa." (53:13-15)
![Page 28: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/28.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
28
www.firqatunnajia.com
Hakumuona katika umbile lake isipokuwa mara hizi mbili tu. Kuhusiana na mara nyinginezo, alijionyesha katika muonekano wa mtu na mara nyingine katika muonekano wa Dihyah al-Kalbiy. Allaah (Ta´ala) amesema kuhusu Jibriyl:
ون بكم أمي وما صا د ذي العرش مكي ماع فق المبي إنه لقول رسول كرم ذي ق وة ع با ولقد رآ
"Hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu, Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye ´Arshi, Anayetiiwa, tena muaminifu. Na wala huyu mwenzenu hana wazimu. Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho uliosafi." (81:19-23)
Malaika mwingine ni Mikaaiyl. Kazi yake ni mazao na namna
itakavyogawiwa. Yote hayo yanatokamana na maamrisho ya Allaah (´Azza
wa Jall). Imaam Ahmad amepokea kutoka kwa Anas ya kwamba Mtume
(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema kumwambia Jibriyl:
"Ni kwa nini sijapatapo kumuona Mikaaiyl akicheka?" Akasema: "Mikaaiyl
hajapatapo kucheka tangu uumbwe Moto."
Allaah (Ta´ala) amesema kuhusu Mikaaiyl:
يل وميكال فإن الل ه عدو للكافرين ئكته ورسله وج من كان عدوا لل ه وم
"Yeyote aliyekuwa adui wa Allaah na Malaika Wake, na Mitume Wake, na Jibriyl, na Miykaal, basi hakika Allaah ni adui kwa makafiri." (02:98)
Miongoni mwao kuna mwingine ambaye ni Israafiyl. Kazi yake ni kupuliza
baragumu ambalo atalipuliza mara tatu baada ya kuamrishwa na Mola Wake
(´Azza wa Jall); mara ya kwanza itakuwa ya mfazaiko, ya pili ya kufa na ya
tatu kwa ajili ya kusimama kwa ajili ya Mola wa walimwengu. Malaika
watatu hawa ndio wale waliotajwa na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa
sallam) katika du´aa yake ya swalah ya usiku:
"Ee Allaah, Mola wa Jibraaiyl, Mikaaiyl na Israafiyl. Muumba wa mbingu
na ardhi. Mjuzi wa yenye kujificha na yenye kuonekana. Hakika Wewe
utahukumu baina ya waja Wako katika yale yote waliyotofautiana.
![Page 29: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/29.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
29
www.firqatunnajia.com
Niongoze katika yale yaliyotofautiana kwayo kwa idhini Yako. Hakika
Wewe unamuongoza Umtakaye katika njia iliyonyooka."
Imepokelewa na Muslim.
Katika "Sunan" ya an-Nasaa´iy imepokelewa kutoka kwa ´Aaishah (Radhiya
Allaahu ´anhaa) ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa
sallam) amesema:
"Ee Allaah, Mola wa Jibraaiyl, Mikaaiyl na Israafiyl. Ninajilinda Kwako
kutokamana na vuke la Moto na adhabu ya kaburi."
Kadhalika kuna Malaika wa mauti. Kazi yake ni kutoa roho. Amesema
(Ta´ala):
ربكم ت رجعون إ قل ي ت وفاكم ملك الموت الذي وكل بكم
"Sema: “Atakufisheni Malaika wa mauti ambaye amewakilishwa kwenu kisha kwa Mola wenu mtarejeshwa."" (32:11)
Vilevile kuna Malaika ambao kazi yao wamewekwa ili kumhifadhi mwanaadamu katika hali zake zote; asipokuwa safarini, anapokuwa safarini, anapokuwa amelala na anapokuwa macho. Amesema (Ta´la):
كم من أسر القول ار له معقبات من ب ي يديه ومن خل سواء م ر به ومن هو مستخف بالليل وسارب بال فظونه من أمر ومن ج فه م الل ه ي غي روا ما بأنفس مرد له وإذ إن الل ه ي غي ر ما بقوم م من دونه من وال ا أراد الل ه بقوم سوءاا ف وما
"Ni sawasawa kwenu anayefanya siri kauli yake au anayeisema kwa juu na anayenyemelea usiku na anayetembea huru mchana. Ana [Malaika] wanaofuatana mfululizo mbele yake na nyuma yake wanamhifadhi kwa amri ya Allaah. Hakika Allaah Habadilishi yale yaliyoko kwa watu mpaka wao wenyewe wabadilishe yale yaliyomo katika nafsi zao. Na Allaah Akiwatakia watu uovu basi hakuna wa kuurudisha. Na wala hawana mlinzi yeyote badala Yake " (13:10-11)
Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amefasiri Kauli Yake (Ta´ala) "Ana
wanaofuatana mfululizo" ifuatavyo:
![Page 30: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/30.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
30
www.firqatunnajia.com
"Ni Malaika wenye kumlinda mbele yake na nyuma yake. Pindi wakati
wake wa kueshi unapofika, wanamwacha."
Malaika wengine ni waandishi Watukufu. Ni wale wenye kuandika matendo
mema na maovu ya waja. Amesema (Ta´ala):
افظي كراماا كاتبي ي علمون ما ت فعلون وإن عليكم
"Na hakika juu yenu bila shaka mmewekewa wenye kulinda. Watukufu wanaoandika. Wanajua yale myafanyayo." (82:10-12)
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
"Nyumba yenye kuamiriwa mbinguni wanaingia - na katika upokezi
mwingine "wanaswali" - kila siku Malaika elfu sabini na baada ya hapo
hawarejei tena."
Yule mwenye kupinga kuwepo kwa Malaika ni kafiri kwa mujibu wa
maafikiano ya waislamu. Amesema (Ta´ala):
ا ا بعيدا خر ف قد ضل ض ئكته وكتبه ورسله والي وم ا ومن يكفر بالل ه وم
"Na atakayemkufuru Allaah na Malaika Wake na Vitabu Vyake na Mitume Wake na Siku ya Mwisho, basi kwa yakini amepotoka upotofu wa mbali." (04:136)
Kuhusu kuamini vitabu vilivyoteremshwa, Allaah (Ta´ala) amemteremshia
kitabu kila Mtume. Amesema (Ta´ala):
م الكتاب والميزان لي قوم الاس بالقسط لقد أرسلا رسلا بالب ي ات وأنزلا مع
"Kwa yakini Tuliwapeleka Mitume Wetu kwa hoja bayana na Tukateremsha pamoja nao Kitabu na shariy‘ah ili watu wasimamie kwa uadilifu." (57:25)
م الكتاب با ذرين وأنزل مع دةا ف ب عث الل ه البيي مبشرين وم وما اخت لف فيه يحكم ب ي الاس فيما اخت لفوا فيه ق ل كان الاس أمةا وام م الب ي ات ب غياا ب ي ق بإذنه إ الذين أوتو من ب عد ما جاءت دى الل ه الذين آموا لما اخت لفوا فيه من ا دي من يشاء والل ه ف ي
صراط مجستقيم إ
![Page 31: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/31.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
31
www.firqatunnajia.com
"Watu walikuwa Ummah mmoja kisha Allaah Akatuma Manabii wabashiriaji na waonyaji na Akateremsha pamoja nao Kitabu kwa haki ili kihukumu baina ya watu katika waliyokhitilafiana kwayo. Na hawakukhitilafiana katika hayo isipokuwa wale waliopewa hicho baada ya kuwajia hoja bayana kwa uhusuda baina yao. Allaah Akawaongoza wale walioamini kuendea haki katika yale waliyokhitilafiana, kwa idhini Yake. Na Allaah Humwongoza Amtakaye kuelekea njia iliyonyooka." (02:213)
Tunaviamini vitabu hivi, tunatambua kuwa ni vyenye kutoka kwa Allaah na
kujisalimisha kwa maneno Yake (Ta´ala):
اعيل وإسحاق وي عقوب و إب راهيم وإ ا وما أنزل إ م قولوا آما بالل ه وما أنزل إلي البيجون من ر موسى وعيسى وما أو سباط وما أو ام ون د م ن له مسلمون ن فرق ب ي أ
"Semeni: “Tumemwamini Allaah na yaliyoteremshwa kwetu na yaliyoteremshwa kwa Ibraahiym na Ismaa’iyl na Is-haaq na Ya’quub na al-Asbaatw na aliyopewa Muusa na ‘Iysaa na waliyopewa Manabii kutoka kwa Mola wao, hatutofautishi baina ya mmoja yeyote miongoni mwao nasi Kwake tunajisalimisha."" (02:136)
ا الذين آموا آموا بالل ه ورسوله والكتاب الذي ن زل على رسوله والكتاب ال ئكته ذي أنزل من ق بل يا أي ج وكتبه ورسله ومن يكفر بالل ه وما ا بعيدا خر ف قد ضل ض والي وم ا
"Enyi mlioamini! Mwaminini Allaah na Mtume Wake na Kitabu Alichokiteremsha kwa Mtume Wake na Kitabu Alichokiteremsha kabla. Na atakayemkufuru Allaah na Malaika Wake, na Vitabu Vyake na Mitume Wake na Siku ya Mwisho, basi kwa yakini amepotoka upotofu wa mbali." (04:136)
ا أنزل الل ه من كتاب ت وقل آم
"Na sema: “Nimeamini yale Aliyoyateremsha Allaah katika Kitabu." (42:15)
لك الكتاب ريب فقون والذين ي ؤ هدا فيه ا ذ ا رزق اهم ي ة و ا أنزل إليك وما ى للمتقي الذين ي ؤمون بالغيب ويقيمون الص مون خرة هم يوقون أنزل من ق بلك وبا
![Page 32: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/32.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
32
www.firqatunnajia.com
"Alif Laam Miym. Hiki ni Kitabu kisicho na shaka ndani yake, ni Mwongozo kwa wenye taqwa. Ambao huamini ya ghayb na husimamisha swalah na katika vile Tulivyowaruzuku hutoa. Na ambao huamini yaliyoteremshwa kwako na yale yaliyoteremshwa kabla yako na ni wenye yakini na Aakhirah." (02:01-04)
Tunaamini kuwa vitabu hivi ni maneno ya Allaah (´Azza wa Jall) na si ya
mwingine. Allaah (Ta´ala) amezungumza kwavyo kihakika kama
Alivyopenda na Kutaka. Katika maneno haya kuna yenye kusikika kutoka
Kwake nyuma ya pazia pasi na mkati kati. Kama Allaah alivyozungumza na
Muusa kihakika pasi na mkati kati. Amesema (Ta´ala):
ولما جاء موسى لميقاتا وكلمه ربجه
"Na alipokuja Muusa katika miadi Yetu na Mola wake Akamsemesha." (07:143)
اصفيتك على الاس برسا ميقال يا موسى إ وبك
"Akasema: “Ee Muusa hakika Mimi Nimekuteua juu ya watu kwa ujumbe Wangu na maneno Yangu." (07:144)
Maneno mengine ni yale ambayo Allaah (Ta´ala) anamsikilizisha mjumbe
Malaika na anamuamrisha amfikishie mjumbe mwanaadamu. Amesema
(Ta´ala):
ي بإذ اب أو ي رسل رسوا ف يو ياا أو من وراء كيم نه ما يشاء وما كان لبشر أن يكلمه الل ه إ و إنه علي
"Na wala haikuwa kwa mtu yeyote kwamba Allaah Amsemeze isipokuwa kwa njia ya Wahy au kutoka nyuma ya kizuizi au Hutuma Mjumbe, kisha Anamfunulia Wahy kwa idhini Yake Ayatakayo. Hakika Yuko juu, Mwenye hikmah." (42:51)
Imani ya kuamini vitabu kunajumuisha kuamini zile Shari´ah zilizomo katika vitabu vyote na kwamba ilikuwa ni wajibu kwa nyumati walioteremshiwa navyo kujisalimisha navyo na kuhukumu kwa yale yaliyomo ndani. Vitabu hivi vinasadikishana na havikadhibishani. Vitabu vyote kimoja kufutwa na
![Page 33: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/33.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
33
www.firqatunnajia.com
chenye kuteremshwa baada yake ni jambo la haki. Kwa mfano baadhi ya Shari´ah katika Tawrat zilifutwa na Injiyl. Amesema (Ta´ala) kuhusu ´Iysaa (´alayhis-Swalaatu was-Salaam):
رم عليكم ل لكم ب عض الذي ومصدقاا لما ب ي يدي من الت وراة و
"Na mwenye kusadikisha yaliyo kabla yangu katika Tawraat na ili nikuhalalishieni baadhi ya yale yaliyoharamishwa kwenu." (03:50)
Vivyo hivyo Qur-aan ilifuta vitabu vya kimbingu vilivyotangulia. Amesema
(Ta´ala):
يماا عليه مصدقاا لما ب ي يديه من الكتاب وم
"Kinachosadikisha yale yaliyokuja katika Vitabu vilivyokuwa kabla yake na ikivilinda." (05:48)
وما هو إ ذكر للعالمي
"Na haikuwa isipokuwa ni ukumbusho kwa walimwengu." (68:52)
Imani ya kuamini vitabu ni jambo linalotakiwa kuwa la kijumla kwa yale
yaliyotajwa kwa jumla na kwa ufafanuzi kwa yale yaliyotajwa kwa ufafanuzi.
Kuna baadhi ya majina ya vitabu ambavyo Allaah (Ta´ala) amevitaja kwa
ufafanuzi. Kitabu ambacho Allaah amemteremshia Muusa kinaitwa "Tawrat",
kitabu alichoteremshiwa ´Iysaa kinaitwa "Injiyl", kitabu alichoteremshiwa
Daawuud kinaitwa "Zabuur" na kitabu alichoteremshiwa Muhammad
kinaitwa "Qur-aan". Hali kadhalika ametaja (Ta´ala) suhuf ya Ibraahiym na
Muusa - Swalah na salaam ziwaendee. Tunaamini vitabu hivi kwa mujibu wa
ufafanuzi uliyoelezwa.
Allaah ametaja vitabu vingi kwa njia ya ujumla bila ya kutaja kitu juu yake.
Vivyo hivyo tunaviamini kwa ujumla huu. Amesema (Ta´ala):
ا أنزل الل ه من كتاب ت وقل آم
![Page 34: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/34.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
34
www.firqatunnajia.com
"Na sema: “Nimeamini yale Aliyoyateremsha Allaah katika Kitabu."" (42:15)
Qur-aan Tukufu ambayo Allaah amemteremshia Mtume wetu Muhammad
(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndio kitabu cha mwisho cha mbinguni na
hakuna kitabu kingine baada yake. Kimefuta vitabu vyote vilivyotangulia na
ni chenye kutumika kwa wanaadamu na majini. Amesema (Ta´ala):
وما هو إ ذكر للعالمي
"Na haikuwa isipokuwa ni ukumbusho kwa walimwengu." (68:52)
Ni chenye kuyazunguka mambo yote ambayo watu wanayahitajia katika dini
na dunia yao. Amesema (Ta´ala):
مت ع م ديااالي وم أكملت لكم ديكم وأ س ليكم نعم ورضيت لكم ا انف ر مت مصة غي ر فإن الل ه غفور فمن اضيم ر
"Leo Nimekukamilishieni dini yenu na Nimekutimizieni neema Yangu na Nimekuridhieni kwenu Uislamu uwe ndio dini yenu. Basi atakayefikwa na dharura na kushurutishwa kutokana na njaa kali pasipo kuelekea dhambi; basi hakika Allaah ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu." (05:03)
Qur-aan ni miujiza na hakuna yeyote ambaye anaweza kuja na mfano wake.
Amesema (Ta´ala):
نج على أن يأتوا ل ه ذا القرآن يأتون له ولو ك وا ن يااقل لئن اجتمعت ا م لب عض ظ ان ب عض
"Sema: “Ikiwa watajumuika wanadamu na majini ili walete mfano wa hii Qur-aan hawatoweza kuleta mfano wake, japokuwa watasaidiana wao kwa wao." (17:88)
Kadhalika amesema (Ta´ala):
يد يأتيه الباطل من ب ي يديه و من خلفه كيم زيل من ت
"Haitokifikia ubatili mbele yake na wala nyuma yake - ni uteremsho kutoka kwa Mwenye hikmah, Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote." (41:42)
![Page 35: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/35.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
35
www.firqatunnajia.com
Kimehifadhiwa na kuzidishwa na kupunguzwa. Amesema (Ta´ala):
افظون إنا نن ن زلا الذكر وإنا له
"Hakika Sisi Tumeteremsha Ukumbusho na hakika Sisi bila shaka ndio Tutakaouhifadhi." (15:09)
Kuhusu imani ya kuwaamini Mitume, inatakiwa iwe kwa usadikishaji wa
kukata kabisa ya kwamba Allaah ameutumia kila Ummah Mtume ambaye
aliwalingania katika kumuabudu Allaah Pekee na kukufuru vile vyote
vinavyoabudiwa badala Yake.
Katika hili kunaingia pia ya kwamba wote ni wakweli, wenye kusadikishwa,
wema, wasafi, wachaji Allaah, waaminifu na waongofu na wenye kuongozwa.
Wote wamefikisha ujumbe wa Allaah.
Allaah alimfanya Ibraahiym kuwa kipenzi wa hali ya juu na kadhalika
akamfanya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuwa kipenzi wa
hali ya juu. Allaah alimzungumzisha Muusa kihakika na akamnyanyua Idriys
nafasi ya juu. ´Iysaa ni mja na Mtume wa Allaah, ni neno Lake tu
alilompelekea Maryam na ni roho iliyotoka Kwake.
Allaah amewafadhilisha baadhi juu ya wengine na akawanyanyua daraja
baadhi juu ya wengine.
Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndio bwana wa wanaadamu
siku ya Qiyaamah na ni jambo litapitika pasi na ufakhari.
Ulinganizi wa Mitume wote ulikuwa ni wenye kuafikiana katika msingi wa
dini, nako ni kumpwekesha Allaah (Ta´ala) katika uungu Wake, uola Wake na
majina na sifa Zake. Amesema (Ta´ala):
م س د الل ه ا إن الدين ع
"Hakika dini mbele ya Allaah ni Uislamu." (03:19)
ر ا اسرين ومن ي بتغ غي خرة من ا م دياا ف لن ي قبل مه وهو ا س
![Page 36: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/36.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
36
www.firqatunnajia.com
"Na yeyote anayetaka dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitokubaliwa kwake naye Aakhirah atakuwa miongoni mwa waliokhasirika." (03:19)
Amesema (Ta´ala) kuhusu Nuuh:
أكون من المسلمي وأمرت أن
"Sitaki ujira isipokuwa kwa Allaah na nimeamrishwa niwe miongoni mwa Waislamu." (10:72)
Kadhalika amesema (Ta´ala) kuhusu Muusa:
تم تم بالل ه ف عليه ت وكلوا إن ك تم آم مي مجسل وقال موسى يا ق وم إن ك
“Enyi watu wangu! Ikiwa mmemwamini Allaah; basi Kwake mtegemee, mkiwa ni Waislamu." (10:84)
Vivyo hivyo amesema (Ta´ala) kuhusu Sulaymaan pindi Balqiys aliposema:
ظلمت ن فسي وأسلمت مع سليمان لل ه رب العالم ي رب إ
"Mola wangu! Hakika mimi nimejidhulumu nafsi yangu na sasa nimesilimu pamoja na Sulaymaan kwa Allaah Mola wa walimwengu." (27:44)
Amesema (Ta´ala):
ا به ا إليك وما وصي ي ا والذي أو ا كب ر أن أقيموا الدين و ت ت فرقوا فيه إب راهيم وموسى وعيسى شرع لكم من الدين ما وصى به نودي إليه من ييب على المشركي ما تدعوهم إليه ت إليه من يشاء وي الل ه
“Amekuamuruni katika dini yale Aliyomuusia kwayo Nuuh, na ambayo Tumekufunulia Wahy na Tuliyomuusia kwayo Ibraahiym, na Muusa na ‘Iysaa kwamba: “Simamisheni dini na wala msifarikiane humo." Yamekuwa makubwa kwa washirikina yale unayowalingania. Allaah Anamteua Kwake Amtakaye na Anamuongoza Kwake anayerudia rudia kutubia." (42:13)
![Page 37: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/37.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
37
www.firqatunnajia.com
Mitume walikuwa 315 na Manabii 124.000. Haya yamethibiti katika Hadiyth
kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kutoka
katika Hadiyth ya Abu Umaamah na ya Abu Dharr4.
Tofauti kati ya Mtume na Nabii, ni kwamba Nabii ni yule ambaye anapokea
Wahy kutoka kwa Allaah. Akitumwa vilevile kwa wale wenye kwenda
kinyume na maamrisho ya Allaah ili afikishe ujumbe wa Allaah, anahesabika
kuwa Mtume. Ama yule ambaye anatendea kazi Shari´ah ya kabla yake na
asitumwe kwa yeyote ili kufikisha ujumbe kutoka kwa Allaah, anahesabika
kuwa Nabii na sio Mtume5. Mujaahid (Rahimahu Allaah) amesema:
"Mtume ni yule anayezungumzishwa na kupokea Wahy kutoka kwa Allaah
na wala hatumwi [kwa watu]."
Kujengea juu ya haya ni kwamba kila Mtume ni Nabii na sio kila Nabii
anakuwa Mtume.
Allaah (Ta´ala) ametaja wengi katika wao. Kwa mfano Aadam, Nuuh, Idriys,
Huud, Swaalih, Ibraahiym, Ismaa´iyl, Ish-aaq, Ya´quub, Yuusuf, Luutw,
Shu´ayb, Yuunus, Muusa, Haaruun, Ilyaas, Zakariyyah, Yahyaa, al-Yasaa´,
Dhul-Kifl, Daawuud, Sulaymaan, Ayyuub, asbaatw (makabila), ´Iysaa na
Muhammad - Swalah na salaam ziwaendee wote. Allaah ametueleza khabari
zao ambazo ndani yake mna mafunzo na mazingatio na mawaidha:
م عليك ن قصص ا ا قد قصصاهم عليك من ق بل ورس ا ورس وكلم الل ه موسى تكليما
"Na Mitume Tuliokwishakusimulia habari zao kabla na Mitume [wengine ambao] Hatukukusimulia habari zao - na bila shaka Allaah Alimsemesha Muusa maneno ya kikweli." (04:164)
Kwa hivyo tunawaamini kwa ufafanuzi pale wanapotajwa kwa ufafanuzi na kwa jumla pale wanapotajwa kwa jumla.
4 Tazama ”Silsilah al-Ahaadiyth as-Sahiyhah” (6/358/2668) ya Imam Muhammad Naaswir-ud-Dîn al-Albaaniy.
5 ”an-Nubuwwaat” ya Shaykh-ul-Islaam, uk. 255.
![Page 38: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/38.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
38
www.firqatunnajia.com
Tunaamini kuwa Mitume na Manabii wote ni wanaadamu walioumbwa na
hawana sifa yoyote ile ya kiungu. Amesema (Ta´ala):
د كم إل ه وا ا إل أ ى إ ا أنا بشر م لكم يو ا قل إ دا اا و يشرك بعبادة ربه أ ا صا فمن كان ي رجو لقاء ربه ف لي عمل عم
"Sema: “Hakika mimi ni mtu kama nyinyi Isipokuwa tu nafunuliwa Wahy kwamba: "Hakika mungu wenu wa haki ni mungu Mmoja Pekee". Hivyo anayetaraji kukutana na Mola wake na atende ‘amali njema na wala asishirikishe katika ‘ibaadah za Mola wake yeyote." (18:110)
م إن نن إ بش م رسل نج على من يشاء من عباد قالت وعلى وما كان لا أن نأتيكم بسلان إ بإذن الل ه ر م لكم ول كن الل ه الل ه ف ليت وكل المؤمون
"Mitume wao wakawaambia: “Sisi si chochote isipokuwa ni watu kama nyinyi, lakini Allaah Anamfadhilisha Amtakaye miongoni mwa waja Wake. Na haikutupasa sisi kukujieni kwa hoja mnazotaka isipokuwa kwa idhini ya Allaah. Na kwa Allaah Pekee wanategemea waumini." (14:11)
لك من المرسل سواق وما أرسلا ق ب م ليأكلون العام وشون ا ون ي إ إن ةا أتص وكان ربجك بصياا وجعلا ب عضكم لب عض فت
"Na Hatukupeleka kabla yako Mitume wowote isipokuwa bila shaka walikuwa wanakula chakula na wanatembea masokoni. Na Tumejaalia baadhi yenu nyinyi kwa nyinyi kuwa ni majaribio je mtavumilia? Na Mola wako daima ni Mwenye kuona." (25:20)
ملك دي خزائن الل ه و أعلم الغيب و أقول لكم إ إن قل أقول لكم ع ى إ عمى أتبع إ ما يو قل هل يستوي ا ت ت فكرون والبصي أف
"Sema: “Sikuambieni kuwa mimi nina hazina ya Allaah na wala kwamba najua ya ghayb na wala sikuambieni kuwa mimi ni Malaika. Sifuati ila yale nilofunuliwa Wahy". Sema: “Je, analingana sawasawa kipofu na mwenye kuona - basi hamtafakari?"" (06:50)
فسي ن فعاا و ضرا إ ما شاء الل ه ال قل أملك ل ي وما مس ستك رت من ا ت أعلم الغيب وء ولو ك إن أنا إ نذير وبشي سج لقوم ي ؤمون
![Page 39: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/39.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
39
www.firqatunnajia.com
"Sema: “Siimilikii nafsi yangu manufaa yoyote wala dhara yoyote isipokuwa Apendavyo Allaah na lau ningekuwa najua ya ghayb, bila shaka ningelijikithirishia ya kheri na wala lisingelinigusa ovu. Mimi si chochote isipokuwa ni mwonyaji na mbashiriaji kwa watu wanaoamini."" (07:188)
Tunaamini kuwa ni waja miongoni mwa waja wa Allaah ambao Allaah amewaheshimisha kwa Ujumbe. Amewasifu kuwa ni waja pindi zinapotajwa nafasi zao kuu na pindi Anapowasifu.
Tunaamini kuwa Allaah (Ta´ala) amekhitimisha Ujumbe kwa Ujumbe wa
Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kwamba Alimtuma kwa
walimwengu wote majina na wanaadamu:
يعاا رسول الل ه إليكم ا الاس إ قل يا أي ج
"Sema: “Hakika mimi ni Mtume wa Allaah kwenu nyinyi nyote."" (07:158)
ةا للعالمي وما أرسلاك إ ر
"Na Hatukukutuma isipokuwa uwe ni Rahmah kwa walimwengu." (21:107)
وما أرسلاك إ كافةا للاس بشياا ونذيراا ول كن أك ر الاس ي علمون
"Na Hatukukutuma isipokuwa kwa watu wote uwe mbashiriaji na muonyaji, lakini watu wengi hawajui." (34:28)
Ameeleza (Ta´ala) kuwa amechukua ahadi kwa Mitume endapo wataishi zama za Mtume wetu Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) basi wamfuate. Hapa kuna dalili ya wazi kabisa ya kwamba Ujumbe wake ndio wa mwisho na kuwa unafuta nyujumbe zingine zote zilizotangulia. Amesema (Ta´ala):
جاءكم رسول مجصدق لما وإ كمة صرنه ذ أخذ الل ه مياق البيي لما آت يتكم من كتاب و معكم لت ؤمن به ولت قال أأق رر وأخذلكم إصري لك فأول ئك هم الفاسقون ق قالوا أق ررنا على ذ ب عد ذ دوا وأنا معكم من الشاهدين فمن ت و ال فاش
"Na pale Allaah Alipochukua ahadi kwa Manabii: Nikisha kupeni Kitabu na hikmah, kisha akakujieni Mtume mwenye kusadikisha mliyo nayo, ni juu yenu mumuamini na mumsaidie. Akasema: "Je, mmekiri nammekubali
![Page 40: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/40.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
40
www.firqatunnajia.com
kushika agizo langu juu ya hayo?" Wakasema: "Tumekubali." Akasema: "Basi shuhudieni na Mimi nipamoja nanyi katika kushuhudia. Watakaogeuka baada ya haya basi hao ndio mafusaki." (03:81-82)
Mitume walikuja na bishara njema juu ya Ujumbe wa Muhammad (Swalla
Allaahu ´alayhi wa sallam) - swalah na salaam ziwe juu yao wote. Amesema
(Ta´ala):
رسول الل ه إليكم مجصدقاا لما ب ي يدي إسرائيل إ ه وإذ قال عيسى ابن مرم يا ب من الت وراة ومبشراا برسول يأ من ب عدي اد سحر مجبي ف لما جاءهم بالب ي ات قالوا ه ذا أ
"Na pale ´Iysaa mwana wa Maryam aliposema: “Enyi wana wa Israaiyl! Hakika mimi ni Mtume wa Allaah kwenu mwenye kusadikisha yaliyo kabla yangu katika Tawraat na mwenye kubashiria kuja kwa Mtume baada yangu jina lake "Ahmad." Basi alipowajia kwa hoja bayana, walisema: “Huu ni uchawi wa wazi." (61:06)
خرة إنا هدنا إليك سةا و ا ن يا الدج وسعت كل شيء قال عذا أصيب به من أشاء واكتب لا ه ذ ا ور فسأكتب م للذين ا يل ي ت قون وي ؤتون الزكاة والذين هم بآياتا ي ؤمون الذين ي تبعون الرسول ال دهم الت وراة وا دونه مكتوباا ع ي الذي
“Na Tuandikie katika dunia hii mazuri na katika Aakhirah. Hakika sisi tumerudi kutubu Kwako. Akasema: “Adhabu Yangu Nitamsibu nayo Nimtakaye na Rahmah Yangu imeenea kila kitu. Basi Nitawahukumia wale wenye taqwa na wanaotoa zakaah na ambao wao wanaziamini Aayaat Zetu. Wale wanomfuata Mtume, Nabii asiyejua kuandika na kusoma, wanamkuta ameandikwa kwao katika Tawraat na Injiyl." (07:156-157)
Katika "as-Swahiyh" ya Muslim imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
"Ninaapa kwa yule ambaye nafsi ya Muhammad iko mkononi Mwake.
Hatosikia kuhusu mimi sawa awe myahudi au mnaswara kisha asiamini
yale niliyotumwa kwayo isipokuwa atakuwa katika watu wa Motoni."
![Page 41: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/41.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
41
www.firqatunnajia.com
Yule mwenye kukanusha Ujumbe wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa
sallam) kwa walimwengu wote, amewakanusha Mitume wote hata yule
Mtume ambaye anadai kuwa anamuamini na kumfuata. Amesema (Ta´ala):
كذبت ق وم نوح المرسلي
"Watu wa Nuuh walikadhibisha Mitume." (26:105)
Amefanya kuwa waliwakadhibisha Mitume wote pamoja na kuwa Nuuh ndiye alikuwa Mtume wa kwanza.
Tunaamini kuwa hakuna Nabii yoyote baada ya Muhammad (Swalla Allaahu
´alayhi wa sallam). Yule mwenye kudai kuwa kuna Nabii mwingine baada
yake, amekufuru. Allaah (Ta´ala) amesema:
د من رجالكم ول كن رسول الل ه وخا البيي مد أبا أ ما كان
"Hakuwa Muhammad baba wa yeyote miongoni mwa wanaume wenu, lakini ni Mtume wa Allaah na ni mwisho wa Manabii." (33:40)
Katika "as-Swahiyh" ya Muslim imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
"Nimefadhilishwa juu ya Mitume wengine kwa mambo sita: nimepewa
maneno ambayo ni machache lakini yenye maana pana, nimenusuriwa kwa
woga [unaotiwa kwenye nyoyo za maadui], nimehalalishiwa mateka,
nimefanyiziwa ardhi yote kuwa safi na mahali pa kuswalia, nimetumwa
kwa viumbe wote na mimi ndiye Nabii wa mwisho."
Mwenye kukanusha Ujumbe wa Nabii au Mtume yoyote, amekufuru kwa
maafikiano ya waislamu. Amesema (Ta´ala):
ا ن بب إن الذين يكفرون بالل ه ورسله ويريدون أن ي فرقوا ب ي الل ه ورسله وي قولون ن ؤم لك سبي عض ونكفر بب عض ويريدون أن ي تخذوا ب ي ذقا د م أول ئك هم الكافرون ي فرقوا ب ي أ ياا والذين آموا بالل ه ورسله و م أول وأعتدنا للكافرين عذاباا مج م ئك سوف ي ؤتي
ا أجورهم يما وكان الل ه غفوراا ر
![Page 42: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/42.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
42
www.firqatunnajia.com
"Hakika wale waliomkufuru Allaah na Mitume Wake na wanataka kufarikisha baina ya Allaah na Mitume Wake na wanasema: “Tunaamini baadhi [ya Mitume] na tunawakanusha wengine”, na wanataka kuchukua njia iliyo baina ya hayo - hakika hao ndio makafiri wa kweli na Tumewaandalia makafiri adhabu ya kudhalilisha. Na wale waliomwamini Allaah na Mitume Wake na hawakumfarikisha yeyote baina yao, hao Atawapa ujira wao na Allaah daima ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu." (04:150-152)
Kuhusu kuamini siku ya Mwisho, ni siku ya Qiyaamah na yale mambo na hali
zitazopitika ndani yake.
Ahl-us-Sunnah wanaamini hilo kwa yakini. Amesema (Ta´ala):
خرة هم يوقون ا أنزل إليك وما أنزل من ق بلك وبا والذين ي ؤمون
"Na ambao huamini yaliyoteremshwa kwako na yale yaliyoteremshwa kabla yako na ni wenye yakini na Aakhirah." (02:04)
ي وم القيامة ريب فيه الل ه إل ه إ هو معكم إ دياا لي ومن أصدق من الل ه
"Allaah, hakuna mungu wa haki ila Yeye. Bila ya shaka Atakukusanyeni Siku ya Qiyaamah haina shaka ndani yake. Na nani mkweli zaidi katika maneno kuliko Allaah?" (04:87)
تية وإن الساعة
"Hakika Saa bila shaka itafika." (15:85)
Katika hilo kunaingia vilevile kuamini Ufufuliwaji, nayo ni ile Siku maiti
watahuishwa. Allaah (Ta´ala) amesema:
رض إ من شاء الل ه ونفخ الصجور فصعق من السماوات وم ظرون ن ا نفخ فيه أخرى فإذا هم قيام ي
"Na itapulizwa katika baragumu watazimia wale walioko mbinguni na ardhini isipokua Amtakaye Allaah. Kisha litapulizwa humo jengine tahamaki hao wanasimama wakitazama." (39:68)
![Page 43: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/43.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
43
www.firqatunnajia.com
ا كما بدأنا أول خلق نجعيد ا علي إنا كا فاعلي وعدا
"Kama Tulivyoanza uumbaji umbo la awali Tutalirudisha. Hiyo ni ahadi juu Yetu - hakika Sisi ni Wafanyao." (21:104)
Katika haya kunaingia pia kuamini madaftari ya matendo ambayo
yatagawiwa kwa mkono wa kulia au wa kushoto nyuma ya mgongo. Allaah
(Ta´ala) amesema:
سابيه ق م ت أ ظ كتابه بيميه ف ي قول هاؤم اق رءوا كتابيه إ و فأما من أو ا دانية كلوا ف وف عيشة راضية جة عالية ق كتابه بشماله ف ي قول ي الية وأما من أو يام ا ا أسلفتم ا ساب واشربوا هيئاا أدر ما أوت كتابيه و ا كانت القاضية ا ليت يه يا ليت
ماليه ع عون ذراعاا ف ما أغ ا سب سلسلة ذرع حيم صلجو ا سلانيه خذو ف غلجو اسلكو إنه كان ي ؤمن بالل ه هلك عيم و طعام إ من غسلي ي العظيم له الي وم هاها ضج على طعام المسكي ف لي اطئون و أكله إ ا
"Ama yule atakayepewa kitabu chake kuliani mwake, atasema: “Hebu chukueni someni kitabu changu! Hakika mimi niliyakinisha kuwa hakiki mimi ni mwenye kukutana na hesabu yangu". Basi yeye atakuwa katika maisha ya kuridhisha. Kwenye Pepo ya juu. Matunda yake ya kuchumwa ni karibu. [Wataambiwa]: “Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyoyatanguliza katika siku nyingi zilopita." Na ama yule atakayepewa kitabu chake kushotoni mwake, atasema: “Ee, laiti nisingelipewa kitabu changu na wala nisingelijua hesabu yangu! Ee, laiti yangelikuwa mauti ndio kumalizika kwangu. Haikunifaa mali yangu. Ufalme wangu umeangamia." [Itasemwa]: “Mchukueni na mfungeni pingu kisha kwenye [Moto wa] al-Jahiym muingizeni aungue. Halafu katika minyororo yenye urefu wa dhiraa sabini mtieni pingu. Hakika yeye alikuwa hamuamini Allaah Mkuu na wala hahamasishi kulisha masikini. Basi leo hapa hatokuwa na rafiki wa dhati, na wala [hawatopata] chakula isipokuwa maji ya vidonda vilooshwa [vya walio Motoni]. Hawakili [chakula] hicho isipokuwa wenye hatia. (69:19-37)
Vilevile kuamini Mizani itayowekwa siku ya Qiyaamah na hivyo hakuna yoyote atayedhulumiwa. Amesema (Ta´ala):
م خالدون فمن ث قلت موازيه فأول ئك هم المفلحون م ج ومن خفت موازيه فأول ئك الذين خسروا أنفس
![Page 44: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/44.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
44
www.firqatunnajia.com
"Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, hao ndio wenye kufaulu. Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, basi hao ni wale ambao wamekhasirika nafsi zao watakuwa katika [Moto wa] Jahannam ni wenye kudumu." (23:102-103)
Kadhalika kunaingia kuamini uombezi katika kisimamo hicho. Kuna aina nne za uombezi:
Uombezi mkubwa [ash-Shafaa´ah al-´Udhwma]: Hii ni kwa Muhammad
(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) peke yake na itapitika pindi watu
wanasubiri wahukumiwe.
Uombezi ili milango ya Peponi ifunguliwe: Aina hii pia ni kwa Mtume
(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) peke yake.
Uombezi wa kukhafifishiwa adhabu yule mwenye kuiistahiki: Kadhalika
aina hii ni kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) peke yake pindi
atapomuombea ami yake Abu Twaalib akhafifishiwe adhabu ya Moto. Haya
ni malipo kwa kuwa alikuwa akimlinda na kumchunga.
Uombezi ili baadhi ya watu zinyanyuliwe daraja zao Peponi: Aina hii
imesemekana kuwa ni kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) peke
yake na imesemekana pia kuwa si yeye pekee.
Uombezi kwa wenye madhambi makubwa: Hawa ni wale wapwekeshaji
watenda madhambi. Wametumbukia Motoni kwa sababu ya madhambi yao
na wataombewa ili watoke humo. Uombezi huu Mtume wa Allaah (Swalla
Allaahu ´alayhi wa sallam), Mitume na Malaika na waja wema wana haki juu
yake.
Kadhalika Qur-aan na swawm vitawaombea watu wake siku ya Qiyaamah.
Vilevile watoto wa waumini watawaombea wazazi wao.
Vilevile inahusiana na kuamini hodhi ya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi
wa sallam). Maji yake ni maeupe kushinda maziwa, matamu kushinda asali na
yenye harufu nzuri kushinda ya miski. Atayekunywa humo mara moja, basi
hatohisi kiu tena kamwe.
![Page 45: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/45.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
45
www.firqatunnajia.com
Ni lazima pia kuamini Njia itayowekwa juu ya Moto. Watu watapita juu yake
kwa mujibu wa matendo yao. Mtu wa kwanza atapita kama umeme, halafu
kama upepo na halafu mwingine kama ndege. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi
wa sallam) amesimama kwenye Njia akisema:
"Ee Mola! Salimisha, salimisha!"
Baada ya hapo matendo ya waja yatapungua mpaka atapokuja mtu ambaye
atatambaa kwa sababu hawezi kutembea. Kwenye ncha ya Njia
kumetundikwa ndoano zilizoamrishwa kumchukua wenye wastahiki. Hivyo
mwenye furaha ataokoka na mla khasara atatumbukia Motoni.
Tunaamini yale yote yaliyokuja katika Qur-aan na Sunnah juu ya siku hiyo na
hali zake - Allaah atulinde nazo.
Kuhusu kuamini Qadar kheri na shari yake, inahusiana na kuthibitisha kwa
kukata kabisa ya kwamba Allaah alikadiria makadirio ya viumbe na kwamba
yale yote yaliyopitika, Allaah aliyataka, na yale yote ambayo hayakupitika,
Allaah hakuyataka. Allaah (Ta´ala) amesema:
بقدر eإنا كل شيء خلقا
"Hakika sisi Tumekiumba kila kitu kwa makadirio." (54:49)
وكان أمر الل ه قدراا مقدوراا
"Na amri ya Allaah daima ni majaaliwa yaliyohukumiwa." (33:38)
Qadar ina daraja nne:
Ya kwanza: Tunaamini kuwa Allaah (Ta´ala) anakijua kila kitu. Anakijua kila
kilichokuwepo, kilichopo na vipi kitakuwa kwa elimu Yake ya milele. Hajiwi
na elimu mpya baada ya kutokujua na wala hasahau baada ya kujua.
Ya pili: Tunaamini kuwa Allaah aliandika katika Ubao uliohifadhiwa kila
kitachokuwepo mpaka Qiyaamah kisimame. Amesema (Ta´ala):
![Page 46: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/46.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
46
www.firqatunnajia.com
رض ت علم أن الل ه ي علم ما السماء وا لك كتاب أ لك على الل ه يسي إن ذ إن ذ
"Je, hujui kwamba Allaah Anajua yale yote yaliyomo katika mbingu na ardhi? Hakika hayo yamo katika Kitabu. Hakika hayo kwa Allaah ni mepesi." (22:70)
د ر كتاب ا ع قال علم و سى قال فما بال القرون ا يضلج ر و ي
"Akasema: "Basi nini hali ya karne za awali?" Akasema: "Ujuzi wake uko kwa Mola wangu katika Kitabu. Hapotezi Mola wangu na wala Hasahau."" (20:51-52)
إمام مجبي ا صي وكل شيء أ
"Kila kitu Tumekirekodi barabara katika daftari bayana." (36:12)
Katika nukta hii kunaingia vilevile makadirio ya milele kabla ya kuumba
mbingu na ardhi. Amesema (Ta´ala):
نا قل لن يصيب ا إ ما كتب الل ه لا هو مو
"Sema: “Halitusibu lolote isipokuwa lile Alilotukidhia Allaah - Yeye ni mlinzi Wetu."" (09:51)
Kadhalika inahusiana na Siku makubaliano yalipoandikwa:
ألست بربكم
“Je, Mimi siye Mola wenu?” (07:172)
Amesema (Ta´ala):
م ألست بربكم دهم على أنفس م وأش ورهم ذري ت آدم من ظ قالوا ب لى وإذ أخذ ربجك من ب
"Na pindi Mola wako Alipochukua katika wana wa Aadam kutoka migongoni mwao kizazi chao na Akawashuhudisha juu ya nafsi zao: “Je, Mimi siye Mola wenu?” Wakasema: “Ndiye." (07:172)
![Page 47: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/47.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
47
www.firqatunnajia.com
Kuhusu makadirio ya maisha, yanapitika pale tone la mbegu linapotumbukia
kwenye kifuko cha uzazi. Ndipo hutumwa Malaika anayepulizia kipande cha
nyama roho na anaamrishwa mambo mane; riziki yake, muda atakaoeshi,
matendo yake na kama atakuwa mwenye furaha au mla khasara.
Ama kuhusu makadirio ya hali, yanapitika katika usiku wenye Cheo.
Amesema (Ta´ala):
كيم ا ي فرق كلج أمر في
"Humo hupambanuliwa kila jambo la hikmah." (44:04)
Ibn ´Abbaas amesema:
"Katika usiku wenye Cheo kunaandikwa kwenye mama wa Kitabu
yatayokuwepo katika mwaka mauti, uhai, riziki, mvua na mahujaji.
Kunasemwa: "Atahiji fulani, atahiji fulani.""
Kuhusu makadirio ya kila siku, amesema (Ta´ala):
كل ي وم هو شأن
"Kila siku Yeye Yumo katika kuleta jambo." (55:29)
Makadirio ya kila siku ni upambanuzi wa makadirio ya hali, makadirio ya hali
ni upambanuzi wa makadirio ya maisha pindi kinapoumbwa kipomoko,
makadirio ya maisha ni upambanuzi wa makadirio ya maisha ya kwanza
pindi ilipopitika Siku ya makubaliano ambapo pia ni upambanuzi wa
makadirio ya milele ambayo Kalamu iliandika kwenye Kitabu
kinachobainisha. Kitabu hichi chenye kubainisha ni katika elimu ya Allaah
(´Azza wa Jall). Kadhalika kikomo cha makadirio kinaishia katika elimu ya
Allaah (´Azza wa Jall).
ى ت ربك الم وأن إ
"Na kwamba kwa Mola wako ndio kikomo." (53:42)
![Page 48: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/48.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
48
www.firqatunnajia.com
Ya tatu: Utashi. Tunaamini kuwa Allaah (Ta´ala) ametaka kila kilichomo
mbinguni na ardhini. Hakukuwi kitu isipokuwa kwa kutaka Kwake.
Anachokitaka, huwa, na asichokitaka, hakiwi. Amesema (Ta´ala):
ا أمر إذا أراد شيئاا أن ي قول له كن ف يك ون إ
"Hakika amri Yake Anapotaka chochote hukiambia: “Kuwa!" nacho huwa." (36:82)
تت لوا ول كن الل ه ي فعل ما يريد ولو شاء الل ه ما اق
"Na lau Angelitaka Allaah wasingelipigana lakini Allaah Anafanya Ayatakayo." (02:253)
دى ولو م على ا مع شاء الل ه
"Na kama Angetaka Allaah Angeliwakusanya katika uongofu." (06:35)
دةا عل الاس أمةا وا ولو شاء ربجك
"Na kama Angetaka Mola wako, basi Angejaalia watu wote kuwa ni ummah mmoja." (11:118)
ول ق القول م هداها ول كن ا كل ن ف ت ي ا و شئ
"Na Tungelitaka, Tungeliipa kila nafsi mwongozo wake, lakini imethibiti kauli kutoka Kwangu." (32:13)
ز من شيء السماوات و ا رض وما كان الل ه لي ع
"Na hakuna lolote limshindalo Allaah mbinguni na wala ardhini." (35:44)
Ya nne: Uumbaji. Hakika Yeye (Ta´ala) ndiye ameumba kila mtendaji na matendo yake, kila mwenye kufanya harakati na harakati zake na kila mwenye kutulia na utulivu wake. Amesema (Ta´ala):
والل ه خلقكم وما ت عملون
![Page 49: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/49.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
49
www.firqatunnajia.com
"Allaah Amekuumbeni na yale mnayoyatenda." (37:96)
وهو على كل شيء وكيل الل ه خالق كل شيء
"Allaah ni Muumbaji wa kila kitu, Naye juu ya kila kitu ni mdhamini Anayetegemewa kwa yote." (39:62)
Pamoja na hivyo tunaamini kuwa waja wana uwezo, utashi na matakwa juu
ya matendo yao. Allaah (Ta´ala) ndiye amewaumba wao na matakwa yao,
uwezo wao, maneno yao na matendo yao. Maneno na vitendo vinavyotoka
kwao, vinanasibishwa kwao kihakika na kwavyo ndivyo ima watalipwa
thawabu au adhabu. Hata hivyo wao hawawezi isipokuwa yale ambayo
Allaah (Ta´ala) amewawezesha na wala hawatotaka isipokuwa Allaah akitaka
kwanza. Amesema (Ta´ala):
تذكرة رب إن ه ذ ذ إ ا فمن شاء ا كيماا وما تشاءون إ أن يشاء الل ه ه سبي ا إن الل ه كان عليما
"Hakika huu ni ukumbusho, basi anayetaka achukue njia ya Mola wake. Na hamtoweza kutaka chochote isipokuwa Atake Allaah - hakika Allaah daima ni Mjuzi wa yote, Mwenye hikmah." (76:29-30)
كم أن يستقيم وما تشاؤون إ أن يشاء الله ربج ا لعالمي إن هو إ ذكر للعالمي لمن شاء م
"Haikuwa huu ila ni Ukumbusho kwa walimwengu wote - kwa yule miongoni mwenu anayetaka anyooke. Wala nyinyi hamtataka isipokuwa atake Allaah, Mola wa walimwengu." (81:27-29)
ا ا إ وسع ا ما اكتسبت يكلف الل ه ن فسا ا ما كسبت وعلي
"Allaah Hakalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya uwezo wake. Itapata [thawabu] iliyoyachuma na ni dhidi yake [kwa dhambi] iliyojichumia." (02:286)
تم ت عملون ا ك أورث تموها ة ال وتلك ا
"Na hiyo ni Pepo ambayo mmerithishwa kwa yale mliyokuwa mkitenda." (43:72)
![Page 50: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/50.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
50
www.firqatunnajia.com
ا ك لد تم ت عملون وذوقوا عذاب ا
"Onjeni adhabu yenye kudumu kwa yale mliyokuwa mkiyatenda." (32:14)
راا ي ر ومن ي عمل م قال ذرة شرا ي ر فمن ي عمل م قال ذرة خي
"Basi yule atakayetenda kheri sawa na uzito wa chembe ya atomu, ataiona, na yule atakayetenda shari sawa na uzito wa chembe ya atomu, ataiona." (99:07-08)
Tunaamini kuwa makadirio hayamzuii mtu na kutenda kama ambavyo
vilevile hayamfanyi mtu akayategemea. Pindi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi
wa sallam) alipowaeleza Maswahabah zake juu ya Qadar, na kwamba
yameanza kufanya kazi na kwamba kalamu imekauka, wakamwambia:
"Tusitegemee yaliyopangwa kwetu na tukaacha kutenda?"
Akasema:
"Hapana. Tendeni, kila kitu kimewepesishwa."
Halafu akasoma:
ى وات قى وصدق ب فأما من أع س يسر للعسرى ا فس س وكذب با ل واست غ يسر لليسرى وأما من فس
"Basi yule anayetoa na akamcha Allaah na akasadikisha lililo jema, basi Tutamuwepesishia kwa yaliyo mepesi. Ama yule afanyaye ubakhili na akajiona amejitosheleza na akakadhibisha lililo jema, basi Tutamuwepesishia kwa yaliyo magumu." (92:05-10)
Makadirio yana sababu zinazomfanya mtu akayafikia. Kama ambavyo kuoa ni
sababu inayopelekea kupata kizazi na kilimo ni sababu inayopelekea katika
mavuno, kadhalika matendo mema ni sababu inayopelekea kuingia Peponi na
matendo mabaya ni sababu inayopelekea katika Moto.
![Page 51: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/51.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
51
www.firqatunnajia.com
05. ´Aqiydah sahihi juu ya imani
Katika ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni pamona na kuonelea
kuwa imani ni kutamka shahaadah ya upwekeshaji ya kwamba hakuna
mungu wa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wa
Allaah, kuyaamini yakini maneno haya na matendo ya viungo vya mwili.
Imaam ash-Shaafi´iy amesema:
"Maswahabah, Taabi´uun na wale tuliokutana nao walikuwa ni wenye
kuafikiana kwa kusema kwamba imani ni maneno, matendo na nia. Mtu
halipwi kwa kuacha moja katika hivyo vitatu."
Imepokelewa na al-Laalakaa´iy katika "as-Sunnah".
Imani inazidi kwa utiifu na inapungua kwa maasi. Allaah (Ta´ala) amesema:
انااالذي عوا لكم فاخشوهم ف زادهم إ م الاس إن الاس قد ن قال
"Wale walioambiwa na watu: “Hakika watu wamejumuika dhidi yenu, basi waogopeni" yakawazidishia imani." (03:173)
م م آياته زادت م ي ت وكلون وإذا تليت علي اناا وعلى ر إ
"Wanaposomewa Aayaat Zake huwazidishia imani na kwa Mola wao wanategemea." (08:02)
اناا إ م من ي قول أيجكم زادته ه ذ اناا وهم يستبشرون فأما الذين آموا ف زا وإذا ما أنزلت سورة فم م إ دت
"Na inapoteremshwa Suurah, basi miongoni mwao wako wanaosema: “Nani kati yenu [Suurah] hii imemzidishia imani? Ama wale walioamini huwazidishia imani nao wanafurahia." (09:124)
ا زاب قالوا ه ذا ما وعدنا الل ه ورسوله وصدق الل ه ورسوله ولما رأى المؤمون ا اناا وتسليما وما زادهم إ إ
"Basi waumini walipoona yale makundi, walisema: “Haya ndio yale Aliyotuahidi Allaah na Mtume Wake na Amesema kweli Allaah na Mtume Wake - na haikuwazidishia isipokuwa imani na kujisalimisha." (33:22)
![Page 52: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/52.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
52
www.firqatunnajia.com
م ا اناا مع إ هو الذي أنزل السكية ق لوب المؤمي لي زدادوا إ
"Yeye Ndiye Aliyeteremsha utulivu katika nyoyo za waumini ili Awazidishie imani pamoja na imani zao." (48:04)
اناا وي زداد الذين آموا إ
"Na iwazidishie imani wale walioamini." (74:31)
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kutoka kwa Ibn ´Umar ya kwamba
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwatolea mawaidha wanawake
na akawaambia:
"Sijaona walio na akili punguani na dini pungufu wanaomghalibu mtu
mwenye busara kama nyinyi [wanawake]."
Hii ni dalili juu ya kupungua kwa imani. Vilevile amesema (Swalla Allaahu
´alayhi wa sallam):
"Muumini aliye na imani kamilifu zaidi ni yule aliye na tabia njema zaidi."
Ameipokea Ahmad na wengineo kutoka kwa Abu Hurayrah.
Ikiwa ambaye yuko imani kamilifu zaidi ana tabia njema zaidi, basi aliye na
tabia mbaya ana imani pungufu zaidi.
Imani sio maneno na matendo peke yake pasi na kuamini, kwa kuwa hii ni
imani ya wanafiki. Amesema (Ta´ala):
ؤمي خر وما هم ومن الاس من ي قول آما بالل ه وبالي وم ا
"Na miongoni mwa watu wako wasemao: ”Tumemuamini Allaah na Siku ya Mwisho" hali ya kuwa si wenye kuamini."" (02:08)
Wala imani sio kule kuwa na utambuzi peke yake, kwa kuwa hii ni imani ya
makafiri na wakanamungu. Amesema (Ta´ala):
ا وعلوا م ظلما ا أنفس قت ا واست ي وجحدوا
![Page 53: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/53.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
53
www.firqatunnajia.com
"Wakazikanusha na hali kuwa nafsi zao zimeziyakinisha kwa dhulma na majivuno." (27:14)
حدون م يكذبونك ول كن الظالمي بآيات الل ه فإن
"Hakika wao hawakukadhibishi wewe lakini madhalimu wanakanusha Aayaat za Allaah." (06:33)
اهم الكتاب ي عرفونه كما ي عرفون أب اءهم الذين آت ي
"Wale Tuliowapa Kitabu wanatambua kama wanavyotambua watoto wao." (02:146)
م وكانوا من ق بل يست فتحون على الذين د الل ه مصدق لما مع ف لعة الل ه ما عرفوا كفروا به كفروا ف لما جاءهم ولما جاءهم كتاب من ع على الكافرين
"Na kilipowajia Kitabu kutoka kwa Allaah kisadikishacho yale yaliyo pamoja nao na japokuwa hapo kabla walikuwa wakiomba ushindi dhidi ya wale waliokufuru, basi yalipowajia yale waliyokuwa wakiyatambua waliyakanusha, basi laana ya Allaah iwe juu ya makafiri." (02:89)
م ود وقد ت ب ي لكم من مساك م فصدهم عن السبيل وكانوا مستبصرين وعاداا و م الشيان أعما وزين
"Na [Tuliwaangamiza pia kina] ‘Aad na Thamuud na yamekwishakubainikieni masikani yao; na shaytwaan aliwapambia ‘amali zao akawazuia na njia, na walikuwa ni wenye kumaizi." (29:38)
Kadhalika imani sio maneno na kuamini pasi na matendo. Allaah ameyaita
matendo kuwa ni imani. Amesema (Ta´ala):
انكم وما كان الل ه ليضيع إ
"Na Allaah Hakuwa Mwenye kupoteza imani zenu." (02:143)
Bi maana swalah zenu kuelekea Yerusalemu. al-Bukhaariy na Muslim
wamepokea kutoka kwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ya
![Page 54: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/54.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
54
www.firqatunnajia.com
kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema kuuambia
msafara wa ´Abdul-Qays:
"Ninakuamrisheni mambo mane; kumuamini Allaah na hivi mnajua ni nini
kumuamini Allaah? Ni kushuhudia ya kwamba hapana mungu wa haki
isipokuwa Allaah, kusimamisha swalah, kutoa zakaah, kufunga
Ramadhaan na kutoa khumusi ya mateka yenu."
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea vilevile kutoka kwa Abu Hurayrah
(Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa
sallam) amesema:
"Imani ni tanzu sabini na kitu - au ni tanzu sitini na kitu. Bora yake ni
kushuhudia ya kwamba hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah na ya
chini yake ni kuondosha chenye kudhuru njiani na hayaa pia ni tanzu
katika imani."
![Page 55: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/55.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
55
www.firqatunnajia.com
06. Msimamo wa Ahl-us-Sunnah juu ya Takfiyr
Hakuna kitendo chochote kukiacha kwake ni kufuru isipokuwa swalah peke
yake. Yule mwenye kuiacha pasi na kifungamanishi basi amekufuru.
Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)
wameafikiana juu ya hilo. ´Abdullaah bin Shaqiyq amesema:
"Hakuna kitu Maswahabah wa Mtume wa Allaah ambacho walikuwa
wakionelea kukiacha kwake ni kufuru isipokuwa swalah."
Ameipokea at-Tirmidhiy.
Takfiyr ni haki ya Allaah. Asiwepo atayemkufurisha yeyote isipokuwa tu yule
ambaye amekufurishwa na Allaah na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi
wa sallam) au mtu ambaye waislamu wameafikiana juu ya kumkufurisha.
Ambaye atamkufurisha mtu kwa kitu kisichokuwa ukafiri ambacho
kimesimama juu ya hoja zilizo wazi kutoka katika Qur-aan tukufu, Sunnah
Swahiyh au maafikiano, basi mtu huyo anastahiki adhabu kali na kuaziriwa.
Kwa sababu al-Bukhaariy amepokea kupitia kwa Thaabit bin adh-Dhwahhaak
(Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu
´alayhi wa sallam) amesema:
"Mwenye kumtuhumu muumini ukafiri basi ni kama kumuua."
Kufuru inaweza kupatikana kwa kutamka neno, kufanya kitendo na kuitakidi
imani fulani ya kufuru ambayo hakuna tofauti yoyote inayozingatiwa.
Miongoni mwa mambo vilevile yanayoshurutisha ukafiri ni mtu kuhalalisha
[kitu au jambo la haramu].
Tofauti kati ya kukufurisha kwa jumla na kumkufurisha mtu maalum:
kukufurisha kwa jumla ni kama makemeo ya jumla. Mtu anatakiwa kusema
vile ilivyo kama ambavyo haikufungamana na kwa ujumla wake. Mfano wa
hilo ni kama walivyosema maimamu:
"Mwenye kusema Qur-aan imeumbwa ni kafiri."
![Page 56: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/56.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
56
www.firqatunnajia.com
Ibn Khuzaymah (Rahimahu Allaah) amesema:
"Ambaye hathibitishi kuwa Allaah amelingana juu ya ´Arshi na yuko juu ya
mbingu saba ni kafiri ambaye damu yake ni halali. Mali yake inakuwa fai."
Kuhusu kumkufurisha mtu maalum ni lazima masharti yatimie na kusiwepo
vikwazo. Kukufurisha kwa jumla ambako hakufungamana hakupelekei
kumkufurisha mtu maalum mpaka yatimie masharti ya kukufurisha na
vikwazo viondoke.
![Page 57: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/57.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
57
www.firqatunnajia.com
7. ´Aqiydah sahihi juu ya muislamu mtenda dhambi
Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wanaonelea kuwa hakuna dhambi, mbali na
shirki, inayomtoa muislamu katika Uislamu isipokuwa pale atapoihalalisha.
Ni mamoja akawa ni mwenye kuifanya na huku anaona kuwa ni halali au
akawa anaamini kuwa ni halali pasi na kuifanya. Kwa sababu hii ina maana
ya kwamba atakuwa ni mwenye kuikadhibisha Qur-aan na Mtume (Swalla
Allaahu ´alayhi wa sallam), jambo ambalo ni kufuru kwa mujibu wa Kitabu,
Sunnah na maafikiano.
Hakuna dhambi inayomfanya mwenye nayo kudumu Motoni milele
isipokuwa tu shirki. Allaah (Ta´ala) amesema:
لك لمن يشاء إن الل ه ي غفر أن يشرك به وي غفر ما دون ذ
"Hakika Allaah hasamehi kushirikishwa, lakini anasamehe yaliyo chini ya hayo kwa Amtakae." (04:48)
Aayah imefahamisha kuwa mtenda dhambi yuko chini ya matakwa ya Allaah;
Akitaka (Ta´ala) kumsamehe atamsamehe kwa fadhila na ukarimu Wake, na
Akitaka atamuingiza Motoni kwa kiasi cha dhambi yake ili umsafishe na
madhambi halafu baada ya hapo atamtoa kutokana na Tawhiyd yake kisha
amwingize Peponi.
Allaah ametaja baadhi ya madhambi makubwa katika Kitabu Chake. Baadhi
yake ni kuua na manyanyaso. Hata hivyo Amethibitisha imani kwa wenye
nayo. Mtu kama huyo ni muumini kwa imani yake, mtenda dhambi kwa
dhambi zake. Amesema (Ta´ala):
ا الذين آموا كتب عليكم القصاص ا لىيا أي ج نى لقت نى با ر والعبد بالعبد وا رج با فمن عفي له من أخيه شيء فات باع اسان بالمعروف وأداء إليه بإ
"Enyi mlioamini! Mmeandikiwa shariy’ah kisasi waliouawa. Muungwana kwa muungwana na mtumwa kwa mtumwa na mwanamke kwa
![Page 58: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/58.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
58
www.firqatunnajia.com
mwanamke, na anayesamehewa na nduguye kwa lolote basi kufuatilizwa kwake kuwe kwa wema na kumlipa kwake iwe kwa wema." (02:178)
Amemthibitishia (Ta´ala) imani yule muuaji na muuliwaji kama ambavyo amethibitisha kuwa ni wandugu katika imani. Hakuna mgongano wa kutumia neno "dhambi" katika kitendo au yule mtendaji, kumwita yule mtendaji muislamu na kumpitishia zile hukumu za Kiislamu juu yake. Kitu kinachoweka hilo wazi, ni kile kisa cha ´Abdullaah bin Himaar ambaye alikuwa anakunywa pombe. Pindi alipoletwa kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), Swahabah mmoja akasema:
"Allaah akulaani. Ni wingi uliyoje unaletwa!"
Ndipo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema:
"Usimlaani; hakika anampenda Allaah na Mtume Wake."
Dhambi hii haikumtoa katika Uislamu. Bali uhakika wa mambo ni kuwa
alimthibitishia imani, pamoja na kutumbukia katika dhambi hii kubwa. Kitu
kinachobainisha hilo, ni kuwa kufuru, shirki, dhuluma, dhambi na unafiki
vimegawanyika aina mbili katika Shari´ah:
Aina kubwa: Aina hii ni ile inayomtoa mtu katika Uislamu.
Aina ndogo: Aina hii inapingana na ukamilifu wa imani wa yule mwenye
nayo pasi na kumtoa katika Uislamu.
Mgawanyiko huu umebainishwa na Salaf (Radhiya Allaahu ´anhum). Mmoja
katika wabingwa wa Ummah na mfasiri wa Qur-aan, Ibn ´Abbaas (Radhiya
Allaahu ´anhumaa), amesema kuwa kuna kufuru ndogo, dhuluma ndogo,
dhambi ndogo na unafiki mdogo. Allaah amemwita yule mwenye kuomba
badala Yake kwamba ni "kafiri", "mshirikina" na "dhalimu". Allaah (Ta´ala)
amesema:
د ربه سابه ع ا ا آخر ب رهان له به فإ ا إنه ي فلح الكافرون ومن يدع مع الل ه إل
![Page 59: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/59.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
59
www.firqatunnajia.com
"Na yeyote yule anayeomba pamoja na Allaah mungu mwengine hana ushahidi wa wazi wa hilo, basi hakika hesabu yake iko kwa Mola wake - hakika hawafaulu makafiri." (23:117)
ا دا ا أدعو ر و أشرك به أ قل إ
"Sema: “Hakika mimi namuomba Mola wangu Pekee na wala simshirikishi na yeyote."" (72:20)
فإن ف علت فإنك إذاا من الظالمي فعك و يضرجك و تدع من دون الل ه ما ي
“Wala usiombe badala ya Allaah asiyekufaa na wala asiyekudhuru. Endapo utafanya hivo, basi hakika utakuwa miongoni mwa madhalimu." (10:106)
ن ف كان من ا فسق عن أمر ربه إ إبلي
"Isipokuwa Ibliys alikuwa miongoni mwa majini akaasi amri ya Mola wake." (18:50)
Haya yote yanahusiana na kufuru kubwa, shirki kubwa, dhuluma kubwa na dhambi kubwa ambavyo haviwezi kukusanyika na imani. Allaah (Ta´ala) amesema:
ا أنزل الل ه فأول ئك هم الكافرون و كم من
"Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio makafiri." (05:44)
ا أنزل الل ه فأول ئك هم الظالمون كم ومن
"Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio
madhalimu." (05:45)
ا أنزل الل ه فأول ئك هم الفاسقون كم ومن
"Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio mafasiki." (05:47)
![Page 60: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/60.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
60
www.firqatunnajia.com
وم نارااإن الذين ي ا يأكلون ب وسيصلون سعياا أكلون أموال اليتامى ظلماا إ
"Hakika wale wanaokula mali ya mayatima kwa dhulma hapana shaka kwamba wanakula katika matumbo yao moto na watauingia [Moto wa] Sa’iyraa." (04:10)
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
"Kumtukana muislamu ni dhambi na kumpiga vita ni kufuru."
Vilevile amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
"Mwenye kuapa kwa mwengine asiyekuwa Allaah amekufuru au
ameshirikisha."
Haya yanahusiana na kufuru ndogo, shirki ndogo, dhuluma ndogo na dhambi
ndogo ambavyo vinaweza kukusanyika na imani, kama ilivyokuja katika Qur-
aan, Sunnah na maafikiano ya Salaf. Mambo haya yanafanya imani kupungua
na kupingana na ukamilifu wake.
![Page 61: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/61.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
61
www.firqatunnajia.com
08. ´Aqiydah sahihi juu ya Maswahabah wa Mtume wa Allaah
(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)
Miongoni mwa ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni kuwapenda
Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam),
kujenga urafiki nao, kuwatakia radhi na kuwaombea msamaha na kuwasifia.
Allaah (Ta´ala) amesema:
سان رضي الل ه ع نصار والذين ات ب عوهم بإ اجرين وا ولون من الم ار والسابقون ا ن ا ا ت ري م جات م ورضوا عه وأعد ا أب اخالدين في لك الفوز العظيم دا ذ
"Na wale waliotangulia awali miongoni mwa Muhaajiruun na Answaar na wale waliowafuata kwa wema Allaah Ameridhika nao, nao wameridhika Naye. Na Amewaandalia mabustani yapitayo chini yake mito - ni wenye kudumu humo milele. Huko ndiko kufuzu kukubwa." (09:100)
Allaah (Ta´ala) amewaridhia waliotangulia awali pasi na kushurutisha wema.
Kuhusu wale waliokuja nyuma, hayuko radhi na wao endapo hawatowafuata
kwa wema. Amesema (Ta´ala):
رة لقد رضي الل ه عن المؤمي إ ت الش ذ ي بايعونك
"Kwa yakini Allaah Amewawia radhi waumini walipofungamana nawe ahadi ya utiifu chini ya mti." (48:18)
Yule ambaye Allaah ameridhika naye basi hatomkasirikia maishani. Imethibiti
katika Hadiyth Swahiyh ya kwamba (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)
amesema:
"Hakuna yeyote aliyetoa kiapo cha usikivu na utiifu chini ya mti atayeingia
Motoni."
Allaah amewaelezea Muhaajiruun na kuwasifu ya kwamba ni wakweli.
Amesema (Ta´ala):
اجرين الذين أخرجوا صرون الل ه ورسوله للفقراء الم ا من الل ه ورضواناا وي م ي بت غون فض أول ئك هم الصادقون من ديارهم وأموا
![Page 62: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/62.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
62
www.firqatunnajia.com
"Kwa ajili ya mafuqara Muhaajiruun ambao wametolewa kutoka majumbani mwao na [zikataifishwa] mali zao wanatafuta fadhila na Radhi kutoka kwa Allaah na wanamnusuru Allaah na Mtume Wake - hao ndio wakweli." (59:08)
Halafu Akawataja Answaar na kusema:
دون م و بجون من هاجر إلي م ان من ق بل م ولو كان م والذين ت ب وءوا الدار وا ا أوتوا وي ؤثرون على أنفس اجةا صدورهم ومن يوق شح ن فسه فأول ئك هم المفلحون خصاصة
"Na wale waliokuwa na makazi na wakawa na imani kabla yao wanawapenda wale waliohajiri kwao na wala hawapati kuhisi choyo yoyote vifuani mwao kwa yale waliyopewa, na wanawapendelea kuliko nafsi zao japokuwa wao wenyewe wameshikwa na ufukara. Na yeyote anayeepushwa na ubakhili na tamaa ya uchu wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufaulu." (59:09)
Kisha Akataja (Ta´ala) hali za waumini baada yao wenye kuwafuata
Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa
wema na kusema:
خوانا الذين سب قونا ب يم والذين جاءوا من ب عدهم ي قولون رب ا اغفر لا و عل ق لوبا غ للذين آموا رب ا إنك رءوف ر ان و ا
"Na wale waliokuja baada yao wanasema: “Mola wetu! Tusamehe na ndugu zetu ambao wametutangulia kwa imani na wala Usijaalie katika nyoyo zetu mafundo ya chuki kwa wale walioamini. Mola wetu! Hakika Wewe ni Mwenye huruma mno, Mwenye kurehemu." (59:10)
م جمد رسول الل ه اء ب ي ا من ا والذين معه أشداء على الكفار ر ا ي بت غون فض دا سيماهم لل ه ورضواناات راهم ركعاا سود م من أثر السج م الت وراة وجوه لك م ل ب ذ فآزر فاست غلظ فاست وى على سوقه ي ع أ يل كزرع أخرج ش م ا وم ل
م مغفرةا وأجراا عظيماا الكفار الزجراع ليغيظ م ات م وعد الل ه الذين آموا وعملوا الصا
"Muhammad ni Mtume wa Allaah. Na wale walio pamoja naye ni wakali zaidi dhidi ya makafiri wanahurumiana baina yao. Utawaona wakirukuu na wakisujudu wakitafuta fadhila na Radhi kutoka kwa Allaah. Alama zao dhahiri zi katika nyuso zao kutokana na athari za sujudu. Huo ni mfano wao katika Tawraat na mfano wao katika Injiyl kama mmea umetoa chipukizi lake, likautia nguvu kisha likawa nene, kisha likasimama
![Page 63: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/63.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
63
www.firqatunnajia.com
sawasawa juu ya shina lake liwapendezeshe wakulima ili kuwakasirisha makafiri. Allaah Amewaahidi wale walioamini na wakatenda mema miongoni mwao msamaha na ujira mkubwa." (48:29)
Imaam Maalik (Rahimahu Allaah) amesema:
"Yule ambaye moyoni mwake mna chuki dhidi ya mmoja katika Maswahabah
wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), basi anaingia ndani
ya Aayah:
ق والذين آموا وهاجروا وجاهدوا سبيل الل ه والذين آووا ونصروا أول ئك هم المؤمون م مغفرة ورزق كرم ا
"Na wale walioamini na wakahajiri na wakafanya jihaad katika njia ya Allaah na wale waliotoa makazi na wakanusuru - hao ndio waumini wa kweli. Watapata msamaha na riziki tukufu." (08:74)
Amesema (Ta´ala) juu ya Maswahabah akibainisha fadhila za wale
waliojitolea na kupigana kabla ya Ushindi - mkataba wa Hudaybiyah - juu ya
wale waliojitolea na kupigana baada ya Ushindi - lakini makundi yote mawili
yameahidiwa Pepo na Allaah:
كم من أنفق من ق أول ئك أعظم درجةا من الذين أنفقوا من ب عد وقات لوا بل الفتح وقاتل يستوي م س ا وك وعد الل ه ا والل ه ت عملون خبي
"Na mna nini hata hamtoi katika njia ya Allaah na hali urithi wa mbingu na ardhi ni wa Allaah Pekee. Hawi sawa miongoni mwenu aliyetoa kabla ya Ushindi na akapigana. Hao watapata daraja kuu kabisa kuliko wale waliotoa baada [ya ushindi] na wakapigana - na wote Allaah Amewaahidi Pepo. Na Allaah kwa yote myatendayo ni Mjuzi." (57:10)
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kupitia kwa Abu Sa´iyd al-Khudriy
(Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi
wa sallam) amesema:
"Msiwatukane Maswahabah zangu."
Katika matamshi ya Muslim imekuja:
![Page 64: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/64.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
64
www.firqatunnajia.com
"Msimtukane yeyote katika Maswahabah zangu. Lau atakuwepo mtu
atayetoa dhahabu mfano wa [mlima wa] Uhud, basi hautofikia Mudd wala
nusu ya mmoja wao."
Mudd ni robo ya Swaa´ [chini ya gramu mia sita] na nusu yake ni nusu ya
Mudd.
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kutoka kwa ´Imraan bin Huswayn
(Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa
sallam) amesema:
"Watu bora ni karne yangu, kisha wataofuatia, kisha wataofuatia." ´Imraan
amesema: "Sijui alisema karne mbili au tatu baada ya karne yake." Halafu
baada ya hapo watakuja watu wataotoa ushuhuda pasi na kuombwa
kushuhudia, watafanya khiyana pasi na kuaminiwa, wataweka nadhiri pasi
na kutimiza na kutadhahiri kwao kuipenda dunia."
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kutoka kwa Anas (Radhiya Allaahu
´anh) ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema juu ya
Answaar:
"Alama ya imani ni kuwapenda Answaar. Alama ya unafiki ni kuwachukia
Answaar."
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kutoka kwa al-Baraa´ bin ´Aazib
(Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa
sallam) amesema kuhusu Answaar:
"Hakuna anayewapenda isipokuwa muumini tu na hakuna anayewachukia
isipokuwa mnafiki tu. Allaah anampenda yule mwenye kuwapenda na
Allaah anamchukia yule mwenye kuwachukia."
Muslim amepokea kutoka kwa Abu Hurayrah na Abu Sa´iyd al-Khudriy
(Radhiya Allaahu ´anhumaa) ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa
sallam) amesema:
"Hakuna mtu anayemwamini Allaah na siku ya Mwisho anayewachukia
Answaar."
![Page 65: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/65.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
65
www.firqatunnajia.com
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kutoka kwa ´Aliy bin Abiy Twaalib
(Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa
sallam) amesema kuhusu kisa cha Haatwib bin Abiy Balt´ah:
"Ameshuhudia [vita vya] Badr. Allaah aliwatazama watu wa Badr na
kusema: "Fanyeni mtakalo, hakika Nimekusameheni.""
Muslim amepokea kutoka kwa Jaabir bin ´Abdillaah (Radhiya Allaahu ´anh)
ambaye amesema kuwa Umm Mubashshir alimsimulia ya kwamba alimsikia
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema kwa Hafswah:
"Hakuna yeyote katika wale waliokula kiapo cha usikivu na utiifu
atayeingia Motoni - Allaah akitaka."
Walikuwa watu zaidi ya 1400 na miongoni mwao alikuwa Abu Bakr, ´Umar,
´Uthmaan na ´Aliy.
Ahl-us-Sunnah wanaitakidi kuwa mbora wa Ummah huu baada ya Manabii
wake ni Abu Bakr as-Swiddiyq. Kisha ´Umar al-Faaruq. Haya ni kwa
maafikiano ya Maswahabah na Taabi´uun. Hakuna yeyote katika wao
aliyepingana na hili.
Kumepokelewa mapokezi tele kutoka kwa kiongozi wa Waumini ´Aliy bin
Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba amesema:
"Wabora wa Ummah huu baada ya Manabii wake ni Abu Bakr na ´Umar."
Ahl-us-Sunnah wanaonelea kuwa watatu ni ´Uthmaan na wanne ni ´Aliy bin
Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anhumaa).
![Page 66: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/66.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
66
www.firqatunnajia.com
09. ´Aqiydah sahihi juu ya watu wa nyumba ya kwa Mtume
(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)
Katika ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni pamoja na kuwapenda
watu wa familia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kutambua
fadhila na utukufu wao. Katika hali hii mtu anatakiwa kutendea kazi wasia
wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) siku ya Ghaadiyr Khumm.
Alimhimidi Allaah na akamsifu, akawaidhisha na kukumbusha. Kisha
akasema:
"Amma ba´d: Enyi watu! Hakika mimi si mwingine isipokuwa ni
mwanaadamu tu. Anakaribia mjumbe kutoka kwa Mola wangu kunijia
[kunichukua] na hapo itabidi niitikie. Nimekuachieni vitu viwili. Cha kwanza
ni Kitabu cha Allaah ambacho ndani yake mna uongofu na nuru. Hivyo basi
kichukueni Kitabu cha Allaah na shikamaneni nacho."
Akasisitiza juu ya Kitabu cha Allaah halafu akasema:
"Na familia yangu. Ninakukumbusheni juu ya Allaah kwa familia yangu.
Ninakukumbusheni juu ya Allaah kwa familia yangu. Ninakukumbusheni juu
ya Allaah kwa familia yangu."
Ibn Kathiyr amesema katika Tafsiyr yake:
"Hatuukatai wasia wa watu wa nyumba ya kwa Mtume na kuwatendea
wema, kuwaheshimu na kuwatukuza. Hakika wanatokamana na kizazi kisafi
na familia tukufu kabisa iliyopo katika uso wa ardhi kifakhari, kiukoo na
kinasabu. Hili khasa pale ambapo watakuwa ni wenye kufuata Sunnah ya
kinabii, sahihi na ilio wazi. Hali kama hii ndio waliokuwa nayo wahenga wao
kama al-´Abbaas na watoto wake na ´Aliy na familia yake na dhuriya yake -
Allaah awawie radhi wote."
Miongoni mwa watu wa familia yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni
wakeze. Amesema (Ta´ala) kuhusu wao:
![Page 67: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/67.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
67
www.firqatunnajia.com
اهلي و وق رن ب يوتكن و ت ب رجن ت ب رجج ا ة وآتي الزكاة وأطعن الل ه ورسوله ة ا وأقمن الص كم الرج ا يريد الل ه ليذهب ع إلى ب يوتكن من آيات الل ه ياا واذكرن ما ي ت ركم ت كمة أهل الب يت وي يفاا خبياا وا إن الل ه كان ل
"Na bakieni majumbani mwenu na wala msionyeshe mapambo uonyeshaji mapambo wa zama za ujahili. Na simamisheni swalah, na toeni zakaah na mtiini Allaah na Mtume Wake. Hakika Allaah Anataka Akuondosheeni uchafu enyi watu wa nyumba na Akutakaseni mtakaso barabara. Na dhukuruni yale yanayosomwa majumbani mwenu katika Ayaat za Allaah na Hikmah, hakika Allaah daima ni Mjuzi, Mwenye khabari." (33:33-34)
Ibn Kathiyr (Rahimahu Allaah) amesema katika Tafsiyr yake:
"Aayah hii ni dalili juu ya kwamba wakeze Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa
sallam) wanaingia katika familia yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kwa
sababu wao ndio sababu ya kuteremka kwa Aayah. Sababu ya kuteremka kwa
Aayah na kwamba inaingia ndani yake ni jambo lisilokuwa na tofauti juu
yake. Ima inaingia na kutumika hiyo tu, jambo ambalo ni maoni moja, au hiyo
na nyenginezo, jambo ambalo ndio maoni sahihi zaidi."
al-Bukhaariy amepokea kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh)
kuhusu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumuoa kwake Zaynab bint Jahsh
na humo kumetajwa ya kwamba (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliingia
ndani kwenye chumba cha ´Aaishah na kusema:
"Ah-ul-Bayt [watu wa nyumba yangu]! Swalah na salaam iwe juu yao!"
Ndipo akasema: "Swalah na salaam iwe juu yako!"
Yaliyotajwa vilevile kuhusiana na fadhila zao, ni maneno ya Allaah (Ta´ala):
م بالمؤمي من أنفس ج أو م ال ات وأزواجه أم
"Nabii ana haki zaidi kwa waumini kuliko nafsi zao na wake zake ni mama zao." (33:06)
Inahusiana na uzito, heshima, maadhimisho, utukufu na wema wa mama wa waumini. Hata hivyo haijuzu kuwa pamoja nao faragha. Ni jambo lenye
![Page 68: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/68.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
68
www.firqatunnajia.com
maafikiano juu ya kwamba nafasi hii haihusiani na wasichana wao na dada zao.
![Page 69: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/69.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
69
www.firqatunnajia.com
10. ´Aqiydah sahihi juu ya karama za mawalii
Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wanaamini karama za mawalii ambazo Allaah
(Ta´ala) ametaka wafanye, jambo ambalo limetajwa katika Maandiko mengi.
Kwa mujibu wao walii ni yule mwenye kutekeleza maamrisho ya Kishari´ah
na akajiepusha na yale ambayo yamekatazwa kwa mujibu wa Shari´ah.
Amesema (Ta´ala) kuhusu mawalii:
م زنون الذين آموا وكانوا ي ت قون أ إن أولياء الل ه خوف علي و هم
"Tanabahi! Hakika vipenzi wa Allaah hawana khofu juu yao na wala hawatohuzunika. Ambao wameamini na wakawa wanamcha Allaah." (10:62-63)
Ili mtu awe sampuli hii ya mtu kunahitajika imani na uchaji Allaah.
Karama ni kitu chenye kwenda kinyume na mazowea ambacho Allaah
(Ta´ala) huwafanya wachaji Allaah na waja waumini wakifanye. Mambo hayo
yanawasaidia kufanya mambo ya kidini au ya kidunia. Lakini hata hivyo
karama za mawalii hazifikii ile daraja ya miujiza ya Manabii na Mitume.
Miongoni mwa karama za mawalii wa Allaah ni kile kisa cha watu wa
Pangoni, kisa cha Maryam (Radhiya Allaahu ´anhaa) pindi uchungu
ulipompeleka katika shina la mtende ambapo akaamrishwa na Allaah kutikisa
mashina yake na matunda yakawa yameanguka pembezoni mwake, kule
Allaah kumruzuku kwa njia ya kwamba alikuwa akipata matunda ya majira
ya baridi wakati wa joto na matunda ya majira ya joto wakati wa baridi, kisa
cha ´Aaswif, ambaye alikuwa ni mwandishi wa Sulaymaan, kisa cha mtu
ambaye Allaah alimfisha miaka mia moja halafu baada ya hapo akamuhuisha,
kisa cha Jurayj, kisa ch watu watatu katika wana wa Israaiyl ambao
walichukua hifadhi kwenye pango na jiwe likawa limeziba maingilio yao na
mfano wa visa kama hivyo ambavyo ni vyenye kujulikana kwa wanachuoni
na vimethibiti katika Qur-aan, Sunnah iliyothibiti au yaliypokelewa kutoka
kwa Salaf au waliokuja baada yao.
![Page 70: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/70.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
70
www.firqatunnajia.com
Karama itaendelea kuwepo katika Ummah huu hadi Qiyaamah kisimame,
kwa kuwa sababu yake ni imani na uchaji Allaah na hivyo vitu viwili
vitaendelea kuwepo mpaka siku ya Qiyaamah.
Lakini ikiwa jambo lenye kwenda kinyume na mazowea linatoka kwa mtu,
hiyo haina maana kuwa ni dalili yenye kuonesha wema, imani na uchaji
Allaah wake. Katika hali hii ni lazima matendo yake kwanza yalinganishwe
na Qur-aan na Sunnah ili kuangalia kama yanaafikiana navyo na kama
anavifuata kidhahiri na kindani.
![Page 71: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/71.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
71
www.firqatunnajia.com
11. ´Aqiydah sahihi juu ya watawala wa waislamu
Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wanaitakidi kuwa Allaah (Ta´ala)
amewawajibishia waumini kuwatii watawala wao katika yote yasiyokuwa
maasi.
Wanaamini maana ya maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)
iliyotajwa katika Hadiyth ya ´Ubaadah bin as-Swaamit (Radhiya Allaahu
´anh):
"Sikiliza na utii katika kipindi chako kizito na chepesi, katika
unayoyapenda na unayoyachukia hata kama watatawalia juu yako mambo
ya kidunia pasi na kukupatia haki yako, hata kama watachukua mali yako
na kupiga mgongo wako, midhali haihusiani na maasi."
Wanaonelea kuwa ni haramu kuwafanyia uasi watawala, hata kama
watakuwa wakandamizaji na wenye kudhulumu, midhali hawajaona kufuru
ya wazi ambayo kwayo wana dalili kutoka kwa Allaah. Hayo ni kutokana na
yale aliyosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
"Wabora wa viongozi wenu ni wale mnaowapenda na wao wanakupendeni
na wale mnaowaombea du´aa na wao wanakuombeeni du´aa. Waovu wa
viongozi wenu ni wale mnaowachukia na wao wanakuchukieni na
mnawalaani na wao wanakulaanini." Kukasemwa: "Ee Mtume wa Allaah!
Je, tusipambane nao kwa panga?" Akasema: "Hapana, maadamu
wanasimamisha swalah. Mtapoona kitu kutoka kwa watawala wenu
mnachokichukia, basi chukieni kitendo chake na wala msinyanyue mkono
kutoka katika utiifu."
Katika matamshi mengine imekuja:
"Yule aliye na mtawala juu yake na akaona anafanya kitu katika kumuasi
Allaah, basi na achukie kitendo kinachomuasi Allaah na wala asinyanyue
mkono kutoka katika utiifu." Ameipokea Muslim kutoka kwa ´Awf bin
Maalik (Radhiya Allaahu ´anh).
![Page 72: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/72.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
72
www.firqatunnajia.com
Yule mwenye kutoka katika Mkusanyiko, basi Shari´ah itamuadhibu adhabu
kali duniani na Aakhirah kutegemea na ukubwa wa dhambi yake. Mwenye
kufa baada ya kutoka katika utiifu na akafarikiana na Mkusanyiko, basi
amekufa kifo cha kipindi cha kikafiri. Mtu asiulizie juu ya mtu mwenye
kufarikiana na Mkusanyiko kutokana na ukubwa wa dhambi yake. Mwenye
kufarikiana na Mkusanyiko basi hana hoja yoyote mbele ya Allaah (Ta´ala)
siku ya Qiyaamah. Yule mwenye kufarikiana na Mkusanyiko shaytwaan yuko
pamoja naye bega kwa bega. Mwenye kufarikiana na Mkusanyiko basi damu
yake ni halali.
Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wanaonelea kuwa ni jambo zuri na lenye
kusifika kumuombea mtawala kwa Allaah juu ya mafanikio na usalama. Nayo
ni alama yenye kuonesha kuwa mtu ni katika Ahl-us-Sunnah, kama
alivyosema Imaam al-Barbahaariy katika kitabu "Sharh-us-Sunnah":
"Ukimuona mtu anaomba dhidi ya mtawala, basi tambue kuwa ni katika watu
wenye kufuata matamanio. Na ukimuona mtu anamuombea du´aa mtawala
juu ya mafanikio, basi tambua kuwa ni katika watu wa Sunnah - Allaah
akitaka."
Fudhwayl bin ´Iyaadhw amesema:
"Lau mimi ningelikuwa na du´aa [yenye kuitikiwa] basi nisingelimuombea
mwengine asiyekuwa mfalme. Tumeamrishwa kuwaombea utengemavu na
hatukuamrishwa kuomba dhidi yao hata kama watakuwa ni wakandamizaji
na wenye kudhulumu. Ule ukandamizaji na dhuluma zao ni jambo
linawapata wao wenyewe na waislamu pia na kutengemaa kwao ni jambo
linawapata wao wenyewe na waislamu pia."
Imaam as-Swaabuuniy amesema katika "´Aqiydat-us-Salaf wa Aswhaab-il-
Hadiyth":
"Wanaonelea kuwaombea utengemavu, mafanikio na uongofu."
![Page 73: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/73.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
73
www.firqatunnajia.com
Wanaona wale wakubwa wa Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla
Allaahu ´alayhi wa sallam) walikuwa ni wenye kuafikiana juu ya kwamba ni
haramu kuwatukana. Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
"Wakubwa wetu wa Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu
´alayhi wa sallam) wametukataza [kwa kusema]: "Msiwatukane watawala
wenu, msiwafanyie ghushi na wala msiwachukie. Mcheni Allaah na kuweni
na subira, hakika mambo yako karibu."" Ameipokea Ibn Abiy ´Aaswim katika
"as-Sunnah" na wengineo.
![Page 74: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/74.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
74
www.firqatunnajia.com
12. Msimamo sahihi juu ya mijadala katika dini
Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ahh wanakataza mijadala na mizozo katika dini,
kwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza hilo.
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu
´alayhi wa sallam) ambaye amesema:
"Isomeni Qur-aan maadamu nyoyo zenu zimezunguka kwayo.
Mtapotofautiana, basi simameni kutoka kwayo."
Katika "al-Musnad" na "as-Sunan" ya Ibn Maajah - asli matamshi yake
yanapatikana katika "as-Swahiyh" ya Muslim kutoka kwa ´Abdullaah bin
´Amr - kumesimuliwa:
"Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alitoka na wao wakijadiliana
juu ya Qadar. Uso wake ukageuka mwekundu kabisa kama mkomamanga.
Akasema: "Haya ndio mliyoamrishwa au mliumbwa kwa ajili ya haya?
Mnaigonganisha sehemu ya Qur-aan na nyingine. Haya ndio yaliwafanya
kuangamia nyumati zilizokuwa kabla yetu.""
Imepokelewa vilevile kuwa mijadala ni njia moja wapo ya adhabu ya Allaah
kwa Ummah. Katika "as-Sunan" ya at-Tirmidhiy na Ibn Maajah
kumepokelewa kutoka kwa Abu Umaamah (Radhiya Allaahu ´anh) ya
kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
"Hakuna watu waliopotea baada ya uongofu waliokuwemo isipokuwa
baada ya kuanza kujadili." Kisha akasoma:
ما ضربو لك إ جدا
"Hawakukupigia mfano huo isipokuwa tu kutaka kubisha." (43:58)
Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) amesema:
"Misingi ya Sunnah kwetu ni kushikamana yale waliyokuwemo Maswahabah
wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kuwaiga, kuacha Bid´ah na
![Page 75: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/75.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
75
www.firqatunnajia.com
kila Bid´ah ni upotevu, kuacha magomvi na kukaa na Ahl-ul-Ahwaa´ pamoja
na kuacha mizozo, mijadala na magomvi katika dini."
Yote haya yanazingatiwa kuwa ni mijadala ya batili, mijadala ya haki baada
ya kuwa haki imeshabainika, mijadala ambayo hoja zake hazitambuliki na
yule anayejadiliwa, mijadala juu ya zile Aayah zisizokuwa wazi au mijadala
pasi na kuwa na nia nzuri na mfano wa hayo.
Hata hivyo endapo mijadala itakuwa ni yenye kuhusiana na kuidhihirisha na
kuibainisha haki na ikawa ni yenye kubainishwa na mwanachuoni aliye na nia
nzuri na amelazimiana na adabu, basi inazingatiwa kuwa ni yenye kusifiwa.
Allaah (Ta´ala) amesema:
كمة والموعظة ا سبيل ربك با سن سة ادع إ هي أ م بال ن ضل عن سبيله وجاد وهو أعلم إن ربك هو أعلم تدين بالم
"Waite watu katika njia ya Mola wako kwa hikmah na mawaidha mazuri na jadiliana nao kwa njia bora zaidi. Hakika Mola wako Yeye Anamjua zaidi aliyepotea njia Yake Naye Anawajua zaidi walioongoka." (16:125)
سن هي أ ادلوا أهل الكتاب إ بال و
"Na wala msibishane na Ahl-ul-Kitaab isipokuwa kwa yale ambayo ni bora zaidi." (29:46)
ت من قالوا يا نوح ا تعدنا إن ك الصادقي قد جادلت ا فأك رت جدالا فأتا
"Wakasema: “Ee Nuuh! Kwa yakini umejadiliana nasi na umekithirisha majadiliano nasi, basi tuletee adhabu unayotutishia nayo ukiwa ni miongoni mwa wakweli."" (11:32)
Kadhalika Amesimulia (Ta´ala) juu ya mjadala wa Ibraahiym (´alayhis-
Swalaatu was-Salaam) na watu wake na Muusa (´alayhis-Swalaatu was-
Salaam) na Fir´awn. Katika Sunnah kumetajwa mjadala wa Muusa na Aadam
(´alayhimaas-Swalaatu was-Salaam) kama ambavyo vilevile kumetajwa
mijadala mingi kutoka kwa Salaf. Yote hii ni mijadala yenye kusifiwa midhali
![Page 76: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/76.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
76
www.firqatunnajia.com
ndani yake ina elimu, nia nzuri, yenye kuafikiana na Shari´ah na adabu katika
kujadiliana.
![Page 77: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/77.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
77
www.firqatunnajia.com
13. Matahadharisho ya kukaa na Ahl-ul-Ahwaa´
Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wanatahadharisha vikali kabisa kukaa na Ahl-
ul-Ahwaa´ wal-Bid´ah, kwa sababu kukaa nao ni kwenda kinyume na
maamrisho ya Allaah. Isitoshe ni alama ya kuwapenda. Vilevile kunachelea
kwa yule mwenye kukaa nao akajisalimisha na upotevu wao na akawafuata
katika batili yao. Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah)
amesema:
"Bid´ah ambayo mtu anazingatiwa kwayo ni katika Ahl-ul-Ahwaa´ ni zile
zenye kujulikana kwa Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah zinazoenda kinyume na
Qur-aan na Sunnah. Mfano wa Bid´ah hizo ni kama Bid´ah ya Khawaarij,
Raafidhwah, Qadariyyah na Murjia-ah."
Allaah (Ta´ala) amesema:
ديث غي وضوا م وضون آياتا فأعرض ع ت قع وإذا رأيت الذين سي ك الشيان ف د ب عد الذكرى مع القوم وإما ي الظالمي
"Na unapowaona wale wanaoziingilia Aayaat Zetu, basi jitenge nao mpaka waingie katika mazungumzo mengineyo. Na kama shaytwaan akikusahaulisha, basi baada ya kukumbuka, usikae pamoja na watu madhalimu." (06:68)
Ibn ´Abbaas amesema:
"Kila mwenye kuzua katika dini ameingia katika Aayah hii na kila mzushi
mpaka siku ya Qiyaamah."
Haya yamenukuliwa kutoka kwa al-Baghawiy katika Tafsiyr yake. Ibn Jariyr
at-Twabariy amesema:
"Katika Aayah hii kuna dalili ya wazi kabisa juu ya makatazo ya kukaa na
watu wa batili kwa sampuli zote za wazushi na watenda madhambi pindi
wanapoingilia batili yao."
Ibn ´Abbaas amesema:
![Page 78: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/78.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
78
www.firqatunnajia.com
"Usiikae na Ahl-ul-Ahwaa´, kwa kuwa kukaa nao kunazigonjwesha nyoyo."
![Page 79: al-Barjas](https://reader034.vdocuments.site/reader034/viewer/2022050704/577c808b1a28abe054a927c2/html5/thumbnails/79.jpg)
al-Mu´taqad as-Swahiyh
Shaykh ´Abdus-Salaam Barjas
79
www.firqatunnajia.com
14. Hitimisho ya kitabu
Mpaka hapa kwa himdi na mafanikio ya Allaah ndio mwisho wa kitabu "al-
Mu´taqad as-Swahiyh al-Waajib ´alaa kulli Muslim I´tiqaaduh". Ninamuomba
Allaah (Ta´ala) akijaalie kiwe kimefanywa kwa ajili ya Uso Wake Mtukufu,
chenye kuafikiana na Sunnah ya Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi
wa sallam) na awanufaishe nacho waislamu wote kwa jumla.
Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad, watu wa nyumbani
kwake watwaharifu, Maswahabah zake bora na wale watakaowafuata kwa
wema hadi siku ya Malipo.