kampuni ya reli tanzania.docx

2
KAMPUNI YA RELI TANZANIA TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI YA KUAHIRISHA SAFARI YA TRENI KWENDA BARA LEO IJUMAA SEPTEMBA 11, 2015, HADI KESHO JUMAMOSI SEPTEMBA 12, 2015 SAA 11 JIONI! Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL unasikitika kuwataarifu abiria wote na wananchi kwa jumla kuwa kutokana na ajali ya treni ya mizigo iliyotokea kati ya Ngerengere na Kinonko jana mkoa wa Morogoro , safari ya treni ya abiria kwenda Bara iliopangwa kuondoka leo saa 11 jioni imeahirishwa hadi kesho Jumamosi Septemba 12, 2015 saa 11 jioni. Mafundi wa TRL wako katika eneo la ajali tokea jana wakifanya kazi kwa lengo la kuhakikisha njia inafunguliwa kwa wakati ili huduma ya treni za kampuni zirejeea kama kawaida mapema hapo kesho. Uongozi wa TRL unawaomba radhi wale wote watakaopatwa na usumbufu wowote utakaojitokeza. Atakaye soma taarifa hii amwarifu na mwenziwe! Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Mhandisi Elias Mshana TRL Makao Makuu, Dar es Salaam. Septemba 11, 2015

Upload: katuma-masamba

Post on 12-Dec-2015

248 views

Category:

Documents


4 download

TRANSCRIPT

Page 1: KAMPUNI YA RELI TANZANIA.docx

KAMPUNI YA RELI TANZANIATAARIFA  KWA VYOMBO VYA HABARI YA  KUAHIRISHA SAFARI YA

TRENI KWENDA  BARA  LEO IJUMAA SEPTEMBA 11, 2015, HADI KESHO JUMAMOSI SEPTEMBA 12, 2015  SAA  11 JIONI!

  Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL unasikitika kuwataarifu

abiria wote na wananchi kwa jumla  kuwa kutokana na ajali ya treni

ya mizigo iliyotokea kati ya Ngerengere na Kinonko jana mkoa wa

Morogoro , safari ya  treni ya abiria kwenda Bara  iliopangwa

kuondoka  leo saa 11 jioni imeahirishwa hadi kesho Jumamosi

Septemba 12, 2015  saa 11 jioni.

Mafundi wa TRL wako katika eneo  la ajali tokea jana wakifanya kazi

kwa lengo la  kuhakikisha njia inafunguliwa kwa wakati ili huduma

ya  treni za kampuni zirejeea kama kawaida mapema hapo kesho.

Uongozi wa TRL unawaomba radhi wale wote watakaopatwa na

usumbufu wowote utakaojitokeza.

Atakaye soma taarifa  hii amwarifu na mwenziwe!

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi

Mtendaji Mhandisi Elias Mshana

TRL Makao Makuu,

Dar es Salaam.

Septemba 11, 2015